Spika Ndugai na Katibu wa Bunge wapelekwe Mahakamani kwa kutoiheshimu Katiba waliyoapa kuitetea

Anzeni kwanza chadema kukataa ruzuku inayotoka kwenye serikali ambayo imeingia kwa uonevu Then ndio mje na ishu ya ndugai
Ruzuku haitoki kwenye serikali haramu Bali inatoka kwenye kodi inayokusanywa toka kwa Watanzania.
 
Kama Chadema walivyojiwekea sheria ndani ya Katiba yao kulinda udhalimu wao eti Mwanachama akienda Mahakamani kukishitaki chama basi moja kwa moja uanachama wake unakuwa umekoma
Ukiwa hutaki kipengele hicho cha katiba basi hujiungi na hicho chama, unaenda TLP au CCM.
Hata FIFA wana kanuni kuwa mambo yao yana taratibu zao kuyatatua, ukienda mahakamani unakuwa umejitoa FIFA
 
Kwa nionavyo..katiba itaendelea kukanyagwa kwa kiwango cha kutisha baada ya kukamilisha 'lile' la kuondoa ukomo wa muda kwa Rais Magufuli.

Ni suala la muda tu kujongea.!
 
Job Ndugai alishasema waziwazi kwamba hakuna mahakama Tanzania inauwezo wa kumsimamisha na kumhoji juu ya jambo lolote lile - Yeye ndiye mwenye uwezo wa kumwita Jaji yoyote yule Bungeni na akachukuliwa hatua za kinidhamu lakini si yeye kwenda the other side
Namkumbuka Saddam Hussein, akiwa kizimbani alimuuliza Jaji nani kakupa mamlaka ya kunihoji mie?
Mwisho aliishia kula kitanzi kwa maamuzi ya huyo aliyehoji mamlaka kayatoa wapi!
 
Ujinga mwingine ni pale mtu anapotoka madarakani anatunga kitabu na kuandika maovu na mazuri ya awamu yake, utadhani hakuwepo wakati huo.

Hii ni mbaya sana, pembeni kuna raia wanashangilia na kusema safi, 😖😷!
 
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
Sasa imekuwa Jambo la kawaida kwa viongozi wa ngazi za juu kuvunja katiba bila ya kuchukuliwa hatua yoyote. Labda swali la kujiuliza ni nani mwenye wajibu wa kuchukua hatua pale viongozi wanapofanya mambo hayo kwa kiburi kilichopindukia. Mtu anasema hadharani kwamba atawalinda wahalifu na hakuna mtu wa kumchukulia hatua. Mbaya zaidi sasa wamejitungia sheria ya kuwalinda na kutoshitakiwa kwa makosa yao bila kujali ukubwa wa kosa. Kwe bunge lilopita ni Ndugai huyuhuyu aliyeruhusu kama siyo kulazimisha Cecil Mwambe sender kuhudhuria vikao vya bunge hata baada ya kutangaza hadharani kuwa amejivua uwanachama wa chama kilichomdhamini. Ubunge wa Zito Kabwe ulikoma na yeye kuacha kuhudhuria kuacha vikao mara baada ya kutangaza kujitoa CHADEMA. Hii ilikuwa enzi ya Makinda. Ndugai ameambiwa na spika mstaafu na aliyeheshimika Msekwa kuhusu ukomo wa ubunge pale mbunge anapokosa udhamini wa chama lakini kwa kiburi ameamua kupuuza tufanyeje?
 
Ivi ndugai, jajo mkuu na magufuli si kwa sasa hawawez kushitakiwa??
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
 
Chadema ilitoa fursa ya waliofukuzwa kukata rufaa na kwa mantiki hiyo hukumu ya kamati kuu haikupelekwa kwa spika mpaka Baraza kuu litakapokaa na kuisikiliza rufaa ya wanachama 19.

Mpaka hapo mpira uko miguuni mwa Chadema,Baraza kuu litabariki maamuzi ya kamati kuu na kumuandikia spika au baraza kuu litawasamehe na kuwarudishia uanachama wao,NI suala la muda.

Mpaka sasa Ndugai yupo huru kufanya lolote na hao wabunge 19!

Ni kwa uelewa wangu!!
Fuatilia mambo vizuri. Uamuzi wa kamati ulitolewa taarifa kwa spika na kwa kawaida uamuzi uapotolewa utekelezaji wake unaanza mara moja hadi maamuzi ya ngazi za juu yatakapotolewa. Rejea kesi za Lijualikali na Sugu.
 
Fuatilia mambo vizuri. Uamuzi wa kamati ulitolewa taarifa kwa spika na kwa kawaida uamuzi uapotolewa utekelezaji wake unaanza mara moja hadi maamuzi ya ngazi za juu yatakapotolewa. Rejea kesi za Lijualikali na Sugu.
Kwa mara nyingine nakushukuru sana ingawa tangu mwanzo nilisema "kwa uelewa wangu".Asante muungwana.
 
Kutoheshimu katiba ya nchi unayo apa kuifuata na kuilinda ni kosa kubwa la pili baada ya uhaini na mauaji.

Spika wa Bunge Job Ndugai na Katibu wa Bunge wanapaswa kupelekwa mahakamani kama sio leo basi baada ya utawala huu unaowalinda kuondoka madarakani.

Sakata la Wanachama wa CHADEMA waliofukuzwa uanachama na kuendelea kuwa wabunge kinyume na maelekezo ya katiba ni kuidharau hiyo katiba na kwa maana hiyo ni kosa kubwa la jinai linalofanywa kwa makusudi.

Kama Spika wa Bunge hawezi kuheshimu katiba kuna sababu gani raia wengine kuiheshimu?
Hatuendi na katiba, mbona Mwambe alijitoa Chadema akajiunga CCM na akarudishiwa ubunge wake wa Chadema kupitia CCM.
Waliweka sheria inayokataza kushitakiwa hata aistaafu.
 
Tuna shida kubwa sana kwamba tuna rais asiyejua kwamba kila mtu ktk nchi anapaswa kufuata sheria bila shuruti.

Tatizo Magufuli amejenga tabia ya kiburi na kuamini kua yeye yuko juu ya sheria na kwamba kwa kauli yake anaweza kutengua sheria yoyote iliyomo kwenye katiba ya nchi.

Ndugai yupo kutii chochote kile anachoagizwa na Magufuli kukifanya, atafanya tu na wala kamwe hawezi kuhoji na ndio maana Magufuli alipanga akawapa kinga bandia ya kutokushitakiwa.
Nimependa nebula "kinga bandia"
 
We kweli mwehu! Kwani kalia au kaeleza?
Halafu sidhani kama Chadema wanashida na wanalipwa nini! Walisha weka wazi kuwa Ndugai awatambue tuu wabunge wake lakini wasiseme wabunge wa Chadema bali awaite apendavyo maana hawana agenda ya chama wanayo iwakilisha pale.
Akae nao na kuwalipa apendavyo, ila bado atakuwa kavunja katiba maana mbunge lazima awe na chama.
Umenielewa brother!
Chadema wenyewe wamekaa kimya ww uko kisiju huko unakuwa kimbelembele
 
Nilijua wamepelekwa mahakamani kumbe unatoa pendekezo.
Endelea kutoa mapendekezo
 
Hakuna Jambo rahisi Kama kuwaongoza wafuasi wa chadema,Wana uwezo mdogo sana wa kufikiri,hawana nguvu ya kuhoji,hawajui wanataka nini
Chadema ilitangaza kutoyatambua matokeo yote ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020,Cha kushangaa!!
Madiwani wote wameapa mabarazani
Mbunge wa Nkasi,ameapa bungeni
Chama kinapokea ruzuku inayotokana na matokeo yaliosuswa
 
Back
Top Bottom