Spika Ndugai anaendesha Bunge kwa matakwa yake binafsi na si kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,160
Nimestushwa sana na kauli ya Spika wa Bunge la Tanzania, aliyoitoa jana kuhusiana na wabunge wa Chadema, waliofukuzwa uanachama katika kikao cha Kamati Kuu ya Chadema.

Spika Ndugai amenukuliwa akiwaambia wabunge hao kuwa hatambui kufukuzwa kwao uanachama na chama chao cha Chadema na hivyo waendelee na vikao hivyo vya Bunge, kwa kuwa yeye ndiye aliyewaapisha kuingia Bungeni humo na hivyo hakuna mtu yeyote mwenye mamlaka ya kuwavua ubunge wao!

Katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ibara ya 71(1)(e) inatamka hivi "Mbunge atakoma kuwa mbunge ikiwa Mbunge ataacha kuwa mwanachama wa chama alichokuwamo wakati alipochaguliwa au kuteuliwa kuwa Mbunge" mwisho wa kunukuu

Huyu Spika Ndugai anasahau kuwa hata yeye kabla hajakabidhiwa mamlaka aliyo nayo aliapa kuitii na kuiheshimu Katiba hiyo ya nchi

Sasa nimuulize Spika Ndugai, hicho kiburi cha kuwaambia wabunge hao waliovuliwa uanachama wa chama chao, waendelee na ubunge wao anakipata wapi?

Katiba ya nchi ipo wazi kabisa kuwa mtu anaendelea kuwa Mbunge pale tu anapoendelea kuwa mwanachama wa chama cha siasa.

Hivi hawa akina Silinde, hivi sasa wameshafukuzwa uanachama wa chama cha Chadema, kilichowapa ubunge huo, sasa yeye Spika Ndugai anapowaambia waendelee na ubunge wao, wanakuwa wabunge wa chama kipi cha siasa?

Kwa kuwa kwa kufukuzwa uanachama wa Chadema, kwa mujibu wa Katiba ya nchi "automatically" wamepoteza pia ubunge wao.

Kama Spika Ndugai anawaambia hao wabunge waendelee na ubunge wao, wanakuwa ni wabunge wa Spika Ndugai na wala siyo wabunge kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, ambayo yeye Spika Ndugai aliapa kuitii na kuiheshimu kabla hajakabidhiwa madaraka hayo aliyo nayo hivi sasa.
 
Ndugai ni spika wa ajabu haijawahi kutokea. Utawala wa Jiwe hauachi kuwavua nguo watetezi wake kila siku uchwao. Wacha kina mzee mwanakijiji wakae kimya jukwaani😂😂😂😂
Huyu Spika Ndugai nilimshangaa pia alipotamka kuwa Mbunge Mbowe hatarudi kwenye ubunge wake, hapo mwisho wa mwaka baada ya uchaguzi mkuu.

Hivi yeye kama Spika anawezaje kutoa matamshi kama hayo wakati yeye siyo mmoja wa wapiga kura wa jimbo la Hai, analotoka Mheshimiwa Mbowe?
 
Hiki Ni kipindi ambacho viongozi Na wananchi waipendao nchi yao kwa dhati kusimama Na kuhesabiwa kupinga uvunjaji huu Wa wazi Wa katiba. Uzalendo Wa kwanza Ni kulinda katiba.wapi wastaafu wetu? Ndugai alipaswa kudhibitiwa Na chama chake kilichomdhamini bungeni
 
Huyu Spika Ndugai nilimshangaa pia alipotamka kuwa Mbunge Mbowe hatarudi kwenye ubunge wake, hapo mwisho wa mwaka baada ya uchaguzi mkuu.

Hivi yeye kama Spika anawezaje kutoa matamshi kama hayo wakati yeye siyo mmoja wa wapiga kura wa jimbo la Hai, analotoka Mheshimiwa Mbowe?
Our bodies are temporarily, Our legacies are not. Ndugai kama ilivyo kwa jiwe wamepoteza kabisa hata zile sifa za kuwa watawala maana sifa za uongozi hawana kabisa. Hivi makada waandamizi wa Ccm wapo wapi?

Najua kina bashiru hawana ubavu wa kuwanyooshe kidole watu hawa, ipo wapi role ya wazee wa chama kama kina mkapa? Huu si ndio wakati wao? Au bado ile kauli ya wastaafu wanawashwa washwa ipo akilini mwao. Kwa Tulipofikia tunahitaji mapinduzi ya kijeshi kabisa
 
Our bodies are temporarily, Our legacies are not. Ndugai kama ilivyo kwa jiwe wamepoteza kabisa hata zile sifa za kuwa watawala maana sifa za uongozi hawana kabisa. Hivi makada waandamizi wa Ccm wapo wapi? Najua kina bashiru hawana ubavu wa kuwanyooshe kidole watu hawa, ipo wapi role ya wazee wa chama kama kina mkapa? Huu si ndio wakati wao? Au bado ile kauli ya wastaafu wanawashwa washwa ipo akilini mwao. Kwa Tulipofikia tunahitaji mapinduzi ya kijeshi kabisa
Jeshi lenyewe la akina mabeyo hawa wanaotembea na kadi za ccm mfukoni
 
Our bodies are temporarily, Our legacies are not. Ndugai kama ilivyo kwa jiwe wamepoteza kabisa hata zile sifa za kuwa watawala maana sifa za uongozi hawana kabisa. Hivi makada waandamizi wa Ccm wapo wapi? Najua kina bashiru hawana ubavu wa kuwanyooshe kidole watu hawa, ipo wapi role ya wazee wa chama kama kina mkapa? Huu si ndio wakati wao? Au bado ile kauli ya wastaafu wanawashwa washwa ipo akilini mwao. Kwa Tulipofikia tunahitaji mapinduzi ya kijeshi kabisa
Hebu Mkuu Dembe Jr jaribu kuimagine huyo Spika Ndugai anapata wapi kiburi cha kumuita aliyekuwa Mbunge wa Chadema, Ceci Mwambe, wakati kila mwananchi anajua kuwa huyo bwana mwanzoni mwaka mwaka huu alishajitoa kwenye chama hicho na kujiunga na chama cha CCM?

Kama anatambua ubunge wake Mwambe, atueleze akiwa mwanachama wa CCM, alichaguliwa kwenye jimbo lipi?
 
Kosa alianza kulifanya mbowe
Chama cha siasa kinaendeshwa na katiba na kanuni
Haujakaa kikao na mtu yeyote yule unakuja na maazimio makubwa hakuna kuingia bungeni twendeni tukajikarantini
Ni kama vile mwalimu mkuu anawapa amri wanafunzi wake,
Wabunge ni watu wazima wanaamini vikao vya chama, kamati kuu nk
Sio amri ya mtu mmoja kana kwamba chama ni chake,

Ukimlaumu ndugai anaendesha bunge bila kufuata katiba

Vile vile rudi na kwa mbowe anaendesha chama cha siasa kama kampuni yake binafsi
Ili tupate kujenga nchi tuache double Standard kama ni kusema tuwaseme wote..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
chadema wanahubiri demokrasia ambayo HAWAIFUATI..
Ndugai ana matatizo na viongozi wa chadema nao wana matatizo.
TUSIANGALIE UPANDE MMOJA.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hao Chadema unawatuhumu kuwa hawana demokrasia kwa vipi?

Huo uamuzi ulikuwa wa kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na wala siyo maamuzi binafsi ya Mbowe, iweje sasa yeye Ndugai akatae maamuzi halali ya kikao cha Kamati Kuu ya Chadema?
 
Kosa lilifanyika tokea mwanzo mbowe amewazuia wabunge wasiingie bungeni alikaa kikao na nani?
Silinde ndio katibu wa bunge Chadema alafu yeye katibu wa bunge Silinde hajui chochote hiyo ni siasa ya wapi?
Hao Chadema unawatuhumu kuwa hawana demokrasia kwa vipi?

Huo uamuzi ulikuwa wa kikao cha Kamati Kuu ya Chadema na wala siyo maamuzi binafsi ya Mbowe, iweje sasa yeye Ndugai akatae maamuzi halali ya kikao cha Kamati Kuu ya Chadema?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kosa alianza kulifanya mbowe
Chama cha siasa kinaendeshwa na katiba na kanuni
Haujakaa kikao na mtu yeyote yule unakuja na maazimio makubwa hakuna kuingia bungeni twendeni tukajikarantini
Ni kama vile mwalimu mkuu anawapa amri wanafunzi wake,
Wabunge ni watu wazima wanaamini vikao vya chama, kamati kuu nk
Sio amri ya mtu mmoja kana kwamba chama ni chake,

Ukimlaumu ndugai anaendesha bunge bila kufuata katiba

Vile vile rudi na kwa mbowe anaendesha chama cha siasa kama kampuni yake binafsi
Ili tupate kujenga nchi tuache double Standard kama ni kusema tuwaseme wote..

Sent using Jamii Forums mobile app
CAG hajawahi kusema chadema ni kampuni binafsi au saccos, kwa sababu kila mwaka anawakagua achana na propaganda
 
Back
Top Bottom