Spika Makinda achezea Kibano - Bungeni Live!

Spika Makinda achezea Kibano - Bungeni Live!

Wenje ajishushie hadhi kwani TZ tuna hadhi bado? Kama nchi yenyewe haina hadhi tunaigawa kwa masultani wenje ashushe hadi gani tena?

Nchi hii ina hadhi sana , ww kama huijui tuna walakini na uraia wako
 
Mama Makinda kila mara alikuwa anasema..." .... now it is your time to explain yourselves and you will be asked..." Sijui kwa nini anatumia wingi wakati akiwa anaongea na mgombea mmoja mmoja. Mimi nilifikiri hawa waliosoma enzi zake Kizungu chao ni kizuri kuliko hawa wa shule za kata!
 
Kama kufuta kauli bungeni ni kujishushia heshima basi wengi sana walishajishushia heshima wakiwemo dr slaa, zitto na marehemu wangwe maana wote hao walishawahi kufuta kauli zao kwa nyakati tofauti. Sidhani kama wenje kafanya makosa kufuta kauli kama ametumia kauli isiyo sahihi. Pale unapoona umekosea lazima ujirekebisha sio kila mara kuwa mbishi tu. Waliojishushia heshima ni wabunge wa ccm walioanza kuropoka na kumwambia wenje akanywe kikombe cha babu.

Tell me you are joking!!! Hii kauli imetoka kwa wabunge kweli, tena bungeni???
 
Kama Mtanzania naona aibu wabunge kukubaliana kutumia Kiingereza bugeni badala ya Kiswahili. Uamuzi huu ni hatua 10 nyuma kukifanya Kiswahili kuwa lugha ya Taifa kweli.

Faida ya kutumia kiswahili ni kwamba hata sisi akina yahe tunafuatilia kwa nje tutaweza kufuatilia bila ya kuingia gharama za kutafuta wakalimani
 
Zat iz wai I'm stending ini fronti here

Duh ! ha ha ha haaaaaa !!!!!! Sasa ni kitu gani kinachompeleka nje ya Tanzania,si abaki tu na ubunge wake hapa nyumbani?Hayo majaribio ni ya hatari.

Huko nje wabunge wa aina hii watakuwa na kazi ya ziada,kutafsiri kiingereza kwenda kiswahili,kutoka kiswahili hadi kwenye lugha yao kisha waanze kuelewa na kuanza kufikiria kiuchambuzi.Loh,we are doomed!
 
Ni upumbavu kuwafunga watu midomo eti kwa sababu tu hawajui lugha fulani. Ni watu wajinga tu ndo wanaoweza kupitisha sheria inayosema lugha ya mawasiliano iwe lugha wasiyoijua. Kwa hili sishabikii. Narudia tena kusema, ili Tanzania iendelee tunahitajia Kiswahili na lugha nyingine za makabila tu! Ni upuuzi kulazimisha tuongee Kiingereza wakati watu waliopo kilomita 20 kutoka Dodoma mjini hawaelewi Kiswahili chenyewe. Ni matumizi mabaya ya rasilimali za nchi kuwawakilisha watu kwa kuongea lugha wasiyoijua. Sioni mantiki yoyote. Mamikataba yote mabavu yametokana na vilaza wetu kutojua lugha ya Kiingereza.
Tujifunze kwa waarabu, mikataba kwa Kiarabu, mabunge yao wanaendesha kwa Kiarabu. Sisi Kiingereza, Kifaransa, Kireno, Kihispania. Ni aibu. Hatuna siri, hatuna utamaduni. Tunahaha tu. Narudia tena kuandika miswada, kuongea Kingereza bungeni, kuongea kiingereza kwenye mikutano ya kimataifa ni ukosefu wa akili!

Waarabu wepi unaowasemea, au wa Narung'ombe Kkoo???
Ulizia vyuo vikuu UK na USA zilivyojaa waarabu na wachina wanaosoma English, acha kujifariji.
 
Mkuu kusikia jambo ukalitoa ulingoni ili walio karibu na tukio habari watupe linalojiri nafikiri ni sahihi. All the same thread nyingi zimefuata tunapata habari zikiwa moto
 
Sasa kama hoja ya Wenje ilikuwa ya kujishushia hadhi mbona imekuwa lazima kutoa hoja kwanza bungeni ya kusitisha kanuni? Na huyo Zitto angetoa ushauri gani kwa Spika kufuta kwanza kanuni kama si Wenje kuibua hoja kuwa hata kama ilivyofanywa katika kamati, kamati haina uwezo wa kubadilisha kanuni za bunge!!!! Hii ndiyo point hapo. Chombo halali kama kamati kina mipaka yake ya uwezo. Uhalali wake hautoi haki ya kuingilia chombo kingine. kanuni alizosimamia Wenje si za kamati ni za uchaguzi wa wenyeviti ndani ya bunge na hapo lazima wawe 6. Wenje nakupongeza maana unaona yaliyojificha.

Amefundishwa na kuelimishwa nguvu ya bunge kuwa sio sehemu ya kutumia maneno ya kihuni na kujitafutia umaarufu wa kisiasa !
 
Ukiisha futa ina maana huna msimamo tofauti na watu wanavyo mjua !
GeniusBrain, jina kubwa nikadhani wewe ni genius kumbe huna lolote!, Wenje aliufuta ule usemi, au kugeuza black kuuita white kwako ndio kafuta. Zitto alimuunga mkono kuwa wabunge wengi sio waelewa, kumbe hata wewe sio muelewa.

Mhe. Wenje ana bahati, spika sio muelewa sana, kuufuta usemi kwa kuugeuza jina, bado sio kuufuta. Kwa maoni yangu, Wenje amethibitisha yeye ni kidume!.
 
ZItto hatakuwa hayuko serious na kazi yake

Haiwezekani sa 4.22.10 bunge linaendelea huku yeye yuko busy na simu

Mbona wewe upo kazini lakini unatembelea JF. Na wewe haupo serious na kazi yako?. Hii ni kama sehemu ya kupati taarifa mahali popote iwe nyumbani, kazini au kwenye daladala. Ili mradi usiharibu kazi.
 
Mama Makinda kila mara alikuwa anasema..." .... now it is your time to explain yourselves and you will be asked..." Sijui kwa nini anatumia wingi wakati akiwa anaongea na mgombea mmoja mmoja. Mimi nilifikiri hawa waliosoma enzi zake Kizungu chao ni kizuri kuliko hawa wa shule za kata!
Kuifahamu lugha kunataka mazoezi ndugu yangu. Uiseme, uiandike, uisikilize na uisome mara kwa mara.
 
Kama nilivyoelewa ni kuwa Kamati ya Uongozi ilichemsha katika katika suala la uchaguzi wa wajumbe kuwa watu 3 wa kupigiwa kura knyume na kanuni ambayo ilitaka watu 6 wapigiwe kura. Wenje alikosea katika kutumia lugha mbovu lakini si katika hoja.

Wenje amekubali kufuta maneno "black market". Si vibaya kufanya hivyo, lakini kama kamati ya uongozi ilikosea naye amefanya vizuri kuikosoa.
 
GeniusBrain, jina kubwa nikadhani wewe ni genius kumbe huna lolote!, Wenje aliufuta ule usemi, au kugeuza black kuuita white kwako ndio kafuta. Zitto alimuunga mkono kuwa wabunge wengi sio waelewa, kumbe hata wewe sio muelewa.

Mhe. Wenje ana bahati, spika sio muelewa sana, kuufuta usemi kwa kuugeuza jina, bado sio kuufuta. Kwa maoni yangu, Wenje amethibitisha yeye ni kidume!.

Mh. Ziito amemuombea msamaha mpaka povu limemtoka mdomoni, Mh. Spika amemuheshimu zitto tu la sivyo angemtoa bungeni, bunge ni sehemu takatifu sio ya vijiweni kama alivyo zoea wenje, safi sana bunge !
 
Ni watu wajinga tu ndo wanaoweza kupitisha sheria inayosema lugha ya mawasiliano iwe lugha wasiyoijua.

Ni upuuzi kulazimisha tuongee Kiingereza wakati watu waliopo kilomita 20 kutoka Dodoma mjini hawaelewi Kiswahili chenyewe.

Kumbe hata kiswahili hakieleweki? Sasa ni ipi inaeleweka?
 
Back
Top Bottom