Spika Makinda achezea Kibano - Bungeni Live!

Spika Makinda achezea Kibano - Bungeni Live!

Mbona hoja yako haina mashiko, masuala ya kufa kila mtu atakufa. Na tatizo lenu mnapenda vitu vya bure mlivyoahidiwa na CDM, ndio maana maisha yanakuwa magumu, fanyeni kazi kwa bidii na maarifa maisha yatawanyookea tu
CDM wanafanya biashara gani???
 
Hiyo mbona cha Mtoto kuna libunge limoja limeropoka"Tufunge milango Milango tupigane"Et huyu nae Mbunge!! Tunayemtegemea atutungie sheria.Afu mie nahisi ni lile huni la Mtera coz aliwahi kutoa kauli kama hii.Wabunge lazima Mjitathimini hamtutendei Haki kabisa yaani hayo Mamilioni mnayolipwa thru kodi zetu na huo upuuzi na Upumbavu mnaoufanya mnatushangaza sana hamna faida yoyote kwa wananchi pa1 na Nchi kwa ujumla.CCM Mp's muwe serious plz.
Hatuna bunge aisee!!
 
Nchi hii ina hadhi sana , ww kama huijui tuna walakini na uraia wako
Hadhi ipi mkuu! hii yakuombamisaada na kutegemea wafadhili! au ya kuvua gamba? Ipi mkuu zaidi ya aibu kubwa au ndo science na technoligia au michezo, au uchumi, hahahha sasa hadhi ipi au hii mnayosema ya amani na utulivu! mmmh sijui unasema ipi mkuu!?
 
There are currently 190 users browsing this thread. (71 members and 119 guests)

Yaan huku bunge linaendelea Zitto yuko JF, Je kweli tuna wabunge?

wewe kihio, sie wenye blackberry tupo JF 24/7...unahitaji tuition kwenye hili kama wabunge wako wa ccm??
 
Mama Makinda kila mara alikuwa anasema..." .... now it is your time to explain yourselves and you will be asked..." Sijui kwa nini anatumia wingi wakati akiwa anaongea na mgombea mmoja mmoja. Mimi nilifikiri hawa waliosoma enzi zake Kizungu chao ni kizuri kuliko hawa wa shule za kata!



Inategemea, inawezekana hata shule alikua hahudhurii sana; anaishia chipukizi ili aweze kupanda ngazi za uongozi kwenye chama haraka. Matokeo ndio haya tunayaona. Bila kingereza kwenye ulimwengu wa sasa Tanzania hatufurukuti kitu. Ingewezekana tu kama tusingekua tegemezi kwa nchi nyingine.
 
Imeandikwa na Basil Msongo, Dodoma; Tarehe: 13th April 2011

SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, leo amepata wakati mgumu kuongoza kikao cha uchaguzi wa wajumbe kwenye taasisi mbalimbali za kibunge kwa kuwa wabunge walikuwa wanajibishana na kusababisha vurugu bungeni.

“Msitumie wingi wenu kutuburuza, mmezoea kutuburuza, tufunge mlango tupigane” walisema wabunge na kusababisha vurugu bungeni kwa takribani dakika kumi.

Mabishano hayo yalisababisha Spika akasirike na kuwaeleza wabunge kuwa walikuwa wanafanya mambo ya kijinga.

Vurugu hizo zilianza baada ya Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje (Chadema), kusema bungeni kuwa, mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi hizo ulifanywa kwenye dark market.

Wabunge wanaoaminika kuwa ni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walishinikiza Mbunge huyo afute kauli yake, Makinda akamtaka Wenje afute kauli yake.

Wenje alisimama lakini hakufuta kauli yake, baadhi ya wabunge wakawa wanapiga kelele kushinikiza afukuzwe wakitumia maneno ‘out out out, atoke nje .

Wabunge hao walimtaka Mbunge huyo atoke, akanywe kikombe cha Babu, Loliondo.

Mara kwa mara Spika alilazimika kuwatuliza wabunge kwa kuwataka wamsikilize Mbunge aliyekuwa anazungumza.

Makinda aliwaeleza wabunge kuwa wanapaswa kutambua kuwa wananchi wamewachagua, na walikuwa wanawaangalia.

“Kwa nini mnafanya fujo isiyokuwa na akili… waheshimiwa wabunge tunafanya mambo ya kijinga” alisema Makinda lakini wabunge waliendelea kurushiana maneno.

Kwa mara nyingine Spika alimtaka Wenje afute kauli yake kwa kumweleza kuwa alikuwa amemtukana yeye Makinda na wajumbe wote wa Kamati ya Uongozi ya Bunge.

Alimweleza Wenje kuwa wao wote ni watu wazima na ni jambo la kawaida kwa Mbunge kufuta kauli bungeni.

Alimuuliza Wenje kwamba ingemgharimu shilingi ngapi kufuta kauli yake, na akamuuliza Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kama Mbunge huyo angefanya hivyo, ingemgharimu kiasi gani.

Baadhi ya wabunge waliendelea kushinikiza Wenje afukuzwe, na kelele hizo zilizidi baada ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, kumweleza Spika kuwa ulikuwa wakati mwafaka kwake kumuamuru Wenje atoke nje ya Bunge.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, alisema ni kweli Kamati ya Uongozi ya Bunge ilikutana kuzungumzia suala hilo, lakini hazikutolewa fomu ili wagombea wajaze.

Zitto alisema, kamati hiyo si dark market lakini haikuwa sahihi kuitafsiri visivyo kauli ya Wenje, wao (wabunge) wote ni wanasiasa, wawe na ngozi ngumu.

Baadhi ya wabunge waliendelea kusisitiza kuwa Wenje atoke, Zitto akawajibu kuwa hatoki, na wabunge wengine wakasema “hatoki mtu, tutatoka wote”

Makinda alimpa Wenje fursa nyingine ya kufuta kauli yake, Mbunge huyo akasema, hakusema Kamati ya Uongozi ni dark market, ila alimaanisha mchakato uliotumika, ma mwishoni akasema, anafuta maneno dark market, anaweka white market.
 
Wengine dunia hii wameibeba Africa peke yao na wakisikia neno BLACK wanakuwa wakali kama Pilipili

Huku kujishuku kunawatokea sana watu wenye Complex fulani hivi.

Kwa mfano binti kama ana makalio makubwa na akasikia vijana wakisema "PUNDA" basi atajishuku kuwa ni yeye.

Ujumbe hata hivyo umefika.
 
Mh!! haya tutaona na kusikia mengi.. Ila hongera kwa Zitto Kabwe..:yield::yield::yield:
 
Inaonekana Spika wa Bunge hana nguvu za kuongoza vikao hivyo vya bunge; Tatizo ni kuwa hakugombea aliteuliwa
 
Back
Top Bottom