Spika Makinda achezea Kibano - Bungeni Live!

Spika Makinda achezea Kibano - Bungeni Live!

basi wananchi kwenye jimbo lake ndio wamemtuma na hao ndio wakumhadhibu!
 
Kilichotokea leo bungeni kwa Mh. Wenje kulazimishwa kufuta usemi wake kimemtia aibu sana mbunge huyu, kwani ameonekana ni mtu asiye na msimamo na ni muoga pale anapo kemewa, na hasa pale alipoambiwa kuwa atatolewa nje ya bunge, kama si hekima na busara za Zitto za kumuomba Mh. Spika amvumilie hakujua asemalo kwa kuita kikao cha kamati ya uongozi kilichokaa ni ‘black market' . Hii imemshushia sana hadhi yake !

What Does Black Market Mean?
A type of economic activity that takes place outside of government-sanctioned channels.
 
Sasa kama hoja ya Wenje ilikuwa ya kujishushia hadhi mbona imekuwa lazima kutoa hoja kwanza bungeni ya kusitisha kanuni? Na huyo Zitto angetoa ushauri gani kwa Spika kufuta kwanza kanuni kama si Wenje kuibua hoja kuwa hata kama ilivyofanywa katika kamati, kamati haina uwezo wa kubadilisha kanuni za bunge!!!! Hii ndiyo point hapo. Chombo halali kama kamati kina mipaka yake ya uwezo. Uhalali wake hautoi haki ya kuingilia chombo kingine. kanuni alizosimamia Wenje si za kamati ni za uchaguzi wa wenyeviti ndani ya bunge na hapo lazima wawe 6. Wenje nakupongeza maana unaona yaliyojificha.
 
Nimesikia mabishano makal kati ya spika na mbunge wa Nyamagana Wenje. Kuna nini walio mjengoni tupeni kwa undani kinachoendelea. Radio TBC 1-kipindi baada ya taarifa ya habari saa 7
 
cHILDISH!
Jivue Gamba wewe!
Naona tokea jana uko kwenye kazi maalum...Payroll inakaribia kutema nini?

snake_4n.jpg
 
Hoja ya Mh. Wenje ilikuwa sawa, alipotezwa ni Viongozi wake Zitto na Mbowe waliohudhuria kikao cha 'black market' kisha wakakaa kimya bila kuwaarifu wenzao.
 


Teeeeh teeeeeh! Bunge letu nadhani linaelekea kwenye hatua hiii. Si unacheki hapo hakuna cha suti, sketi wala gauni ni kichapo tu!!:love::love:
 
unamatatizo wewe......genius wa wajinga!pambanua mambo na shuhulisha kichwa chako c unatuma mada za kitaarabu
 
Inaonekana miswada inayopelekwa haitoi fursa kwa wabunge kuelewa kwa sababu huandaliwa kwa kiingereza.Nadhani hiki ni kikwazo mojawapo kwa wabunge,wabunge wetu hawasomi vitabu.kwa kuwa lugha ni tatizo.Leo hii mtu anataka akatuwakilishe lakini haelewi Lugha.Si lazima atumie misamiati migumu kwa sababu hata waingereza walo wengi hawaongei kiingereza kilichonyooka sana.

Hata Mkuu wetu wa nchi nilishamsikiliza sana ,lugha ni Tatizo.Mkapa kwa kweli anongea kiingereza vizuri na ndiyo maana kwenye majukwaa ya kimataifa alikuwa anatuwakilisha vizuri.Waige mfano wa akina Dr.Salim Ahmed Salim na Balozi Juma Mwapachu
 
Kama kufuta kauli bungeni ni kujishushia heshima basi wengi sana walishajishushia heshima wakiwemo dr slaa, zitto na marehemu wangwe maana wote hao walishawahi kufuta kauli zao kwa nyakati tofauti. Sidhani kama wenje kafanya makosa kufuta kauli kama ametumia kauli isiyo sahihi. Pale unapoona umekosea lazima ujirekebisha sio kila mara kuwa mbishi tu. Waliojishushia heshima ni wabunge wa ccm walioanza kuropoka na kumwambia wenje akanywe kikombe cha babu.
 
Back
Top Bottom