Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Iko hv. Magufuli anahangaika kujenga au kusafisha saiti (ku-clear site) lakini kuna mitoto au watu wanacheza juu ya kifusi na wengine wamepanda na wanacheza kwenye kijiko sasa badala ya yeye kuendelea na kazi anabaki kukimbizaa nao.

Kwa ufupi ni kwamba hawaelewi ni nini anachofanya wanadhani ni mchezo tu.

My Note. HILI NI KWELI na Masoud ni jinias kweli.
Mkuu yaani umeeleza kama wewe ndo umechora hicho kibonzo ,,,, nimeielewa sanaa,,, na ni kweli maana miongoni mwa wanaocheza juu ya kifusi nahisi nami nipo simuelewi ngosha chochote anachokifanya wallah
 
Nimekuelewa mkuu, tafsiri mrua kabisaa au wewe ndo kipanya mwenyewe vipi!!!?
Halafu wakati anahangaika na hao wanacheza kwa kifusi wengine wanakuja nyuma ya tinga na vikapu wanarundika tena michanga alikorekebisha Hahahahaha hatari sana
Teh teh. Wabongo shida sana ndo maana anakuwa mkali
 
Kiufupi kabisa nimegundua:
Operator amepewa chombo ambacho hana weledi wa kukitumia (badala ya kutumia honi kainuka kwenye kiti na kuanza kufukuza watu kwa fimbo....ishara ya ujuha)
Pili ni mtu anayeonekana kulemewa na kazi sababu ya mazingira
Tatu: Eneo analofanyia kazi watu waishaona hawezi na hivyo kuamua kuendelea na ya kwao. ...wengine wakicheza wengine wakiangalia mali zao na kuziamisha wakiamini huenda akaja operator mwingine mweledi na kumalizia kazi au kuanza kazi hiyo upya.

Hii picha ina mengi sana
 
Kadri muda unavyozidi kwenda walimu wengi wa lugha wanaibuka
FB_IMG_1523475066272.jpg
 
HAHAHA naona bigger mind mmejua what the hell mimi bado natafakuri...!!
 
Back
Top Bottom