Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Hapo nyuma naona kama wasaidizi wake in Black uniform japo wanaona huku mali inapotea (aliyejitwika ndoo kichwani) lakini hawachukui hatua yoyote coz top manyota anajikuta ndyo kila kitu .........!
 
The Bulldozer hawamsikilizi tena. Hawamwogopi, anapiga nduru wampishe ndo kwanza wanapiga sarakasi.

Wengine wamepanda kabisa tingatinga, ila wachache wanachota mafuta.

Sijui mwisho wake.
Mkuu umenisaidia kuelewa kwa hakika kabla sikuwa nimeng'amua chochote.

Ahsante Sana!
 
Huyo aliyekaa kwenye Hilo bulldozer huku akiwa amenyanyua mikono anashangilia lazima atakuwa ni Bashite tuu!
 
Wananchi wamekua jeuri..tingatinga anawapa maelekezo wenyewe ndio kwanza wanabiduka wengine wanacheza
 
Iko hv. Magufuli anahangaika kujenga au kusafisha saiti (ku-clear site) lakini kuna mitoto au watu wanacheza juu ya kifusi na wengine wamepanda na wanacheza kwenye kijiko sasa badala ya yeye kuendelea na kazi anabaki kukimbizaa nao.

Kwa ufupi ni kwamba hawaelewi ni nini anachofanya wanadhani ni mchezo tu.

My Note. HILI NI KWELI na Masoud ni jinias kweli.
Ok!, kumbe, jamani mimi nilikuwa kapa kabisa.
 
Mi nimeona Kifusi na Tingatinga!View attachment 735969

Hapo naona dereva kashuka akiwaonya watu watawanyike asawazishe kifusi lakini hawaelewi ndio kwanza wanaonyesha umahiri wa sarakasi, wasaidizi wake nao wamekaa bila msaada na huyo mama sehemu alipo imekwisha kusawazishwa na maisha yake yanaendelea kama kawaida.
 
Back
Top Bottom