Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Special thread: Vikaragosi vya Masoud Kipanya

Mnakumbushwa jaribuni kuandamana mkione na unyonge wenu, wewe na anayekuhamasisha uingie kwenye maandamano
 
Tafsiri yangu ni 1. kisu ni nyenzo ya kutolea uhai kwa hao ndege walionyonyolewa
2. Cage ni ishara ya gereza au kunyimwa uhuru wa kutoa mawazo au maoni
3. Ndege walionyonyolewa ni ishara ya kudhalilishwa kwa njia mbali mbali kama vile kiuchumi, kijamii na mengineyo.
Asante mzee umefafanua vzr
 
Hicho kibanda ni bunge ambalo linajifanya lipo huru kwa wabunge wake lakini hapo nje kuna kisu ambacho ni serikali, na hao ndege ni wabunge, mmoja aliye ndani ni wa upinzani na aliye nje ni wa chama tawala, ingawa aliyopo nje anajiona yuko huru kutembea anapotaka lkn nae hana mabawa kama aliye ndani kwani wote hawawezi kuruka.
 
Akiwa ndani anafungiwa, akiwa nje anachimjwa, yaani kuna walio jela na kuna wanaokatwa mapanga
 
Hicho kibanda ni bunge ambalo linajifanya lipo huru kwa wabunge wake lakini hapo nje kuna kisu ambacho ni serikali, na hao ndege ni wabunge, mmoja aliye ndani ni wa upinzani na aliye nje ni wa chama tawala, ingawa aliyopo nje anajiona yuko huru kutembea anapotaka lkn nae hana mabawa kama aliye ndani kwani wote hawawezi kuruka.
Wewe kwa mtazamo wangu umewakilisha vyema mawazo ya mchoraji...

Uko vizuri..
 
Alichokitaka kipanya ndo hiki mnachokifanya! Kuwafikirisha zaidi!
Wale ndege hawana uhuru tena wa kuruka kama kawaida! Alichokifanya mtu alowafungulia ni kuwapa uhuru hewa baada ya kuwanyonyoa manyoya! Hawawezi kwenda mbali kwa kutembea na akiwahitaji anawapata na kuwachinja apendavyo!

Labda anajaribu kuongelea ule uhuru wa mahakama! Au wa bunge! Au wa naniii nawaza tu
 
Tafsiri yangu ni 1. kisu ni nyenzo ya kutolea uhai kwa hao ndege walionyonyolewa
2. Cage ni ishara ya gereza au kunyimwa uhuru wa kutoa mawazo au maoni
3. Ndege walionyonyolewa ni ishara ya kudhalilishwa kwa njia mbali mbali kama vile kiuchumi, kijamii na mengineyo.
Hapo unahitimisha kwamba hakuna penye unafuu! Aidha ufungwe kwenye cage au uwe nje uuawe kwa mapanga, ndo tulipofikia
 
Kwa maono yangu, yaani hao kuku wote walikuwa ndani, wakiwa ndani wakanyolewa tens wakiwa hai. Baadaye mlango ukafunguliwa ili yule kuku aliyeko ndani tayari kashonyolewa akiona huko ndani matezo yamemzidi basi atoke nje aungane na maisha ya mnyoaji. Huyo aliyeko nje yeye kashatoka na anamgeukia yule aliyebaki ndani na kumtazama kwa majonzi huku akimshangaa kwanini aendelee kuteseka huko ndani wakati anaweza kutoka. Cha ajabu ni kwamba kuku aliyeko ndani haoni kisu kilichoko hapo juu iliyoandaliwa tayari kumchinja endapo ataendelea kukaigi kutoka nje lakini kuku wa nje yeye hicho kisu anakiona na hiki ndicho kinamfanya azidi kumuonea huruma huku mwenzake aliyebaki ndani kimoyo moyo. Huu mchoro kama hujaishi maeneo ya NORTH KIVU, SOMALIA, DARFUR, huwezi kulielewa vzr. Hii kawachorea wanaishi kwenye maeneo hayo ambayo nadhani ndiyo mambo ya kutesa watu wenye mawazo tofauti na wenye nguvu, kuwaiba hao wenye mawazo tofuti kwa njia mbali mbali kama vitisho, pesa au vyeo na baadaye kuwachinja wale wanaokaidi yanafanyika. Huu mchoro kwa hapa kwetu ni uchochezi na ni kama uhaini, sasa kwavile analeta chokochoko na anawashwawashwa asije akatulilia tena hahahahahaa
 
Ndege wote wanaonekana walikua ndani wakiwa wamenyonyolewa tafsiri yake ni kwamba wote walikua katika dhiki kuu, matatizo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa


Ijapokua wamewekwa ndani aliyewaweka ndani inaonekana kaacha mlango wazi, jaijulikani kaacha bahati mbaya au kajisahau hana akili...

Pamoja na uminywaji huo wa ndege lakini wana nafasi ya kutoka nje kukimbia kutafuta uhuru,

Ukiangalia vizuri ndege mmoja kichwani hajanyolewa nywele zote hvyo bado ana akili kidogo za kuchanganua

Ndege wawili inamaanishabwatu wa aina mbili tofauti wanaojitambua(mwenye kinywele kichwani alieko nje) na alieko ndani anawakilisha wasiojitambua

Conclusion, wengi wa watanzania hali zao ni mbaya kisiasa kiuchumi na kijamii lakini nafasi wanayo mlango umeachwa wazi....akili kumkichwa, ila wengine ndo hvyo akili hamna hyo nafasi waliyonayo hawaioni mazwazwa, matatizo hawayaoni pia wameridhika....wapo gerezani ambalo bado mlango upo wazi

Ndege aliopo nje ana nafasi ya kumbadilisha wa ndani akimbie lakini wa ndani kanyolewa nywele zote haelewi kitu

Karibuni, asanteniii
 
Hapo ishue ni kwamba uchague moja tu ,KUFA au KUFUNGWA.
Aliyepo nje maana yake ni kuwa "mapanga yanamhusu kama Diwani wa Morogoro pale" na aliye ndani maana yake kakubali bora afungwe na sio "MAPANGA".
Chagua moja kusuka au kunyoa, ila cha ajabu option zote ni ngumu.
Tz politics defined by this sketch.
Ova
 
Hapo ishue ni kwamba uchague moja tu ,KUFA au KUFUNGWA.
Aliyepo nje maana yake ni kuwa "mapanga yanamhusu kama Diwani wa Morogoro pale" na aliye ndani maana yake kakubali bora afungwe na sio "MAPANGA".
Chagua moja kusuka au kunyoa, ila cha ajabu option zote ni ngumu.
Tz politics defined by this sketch.
Ova
Apa ndo nmeelewa!
 
Back
Top Bottom