Mpaka kesho Adolf Hitler anasemwa vibaya mno licha ya kwamba alikufa zaidi ya miaka 70 iliyopita. Magufuli ni nani watu wasimseme?
Kama ambavyo Hitler aliwaumiza watu enzi za utawala wake, vivyo hivyo na Magufuli amewaacha baadhi ya Watanzania wakiwa na majeraha mazito mioyoni mwao.
Wapo wanaoamini ndugu zao waliuawa au kupotea kwa amri au maelekezo yake. Wapo waliodhulumiwa mali na kufungwa jela bila hatia. Hawa wote bado wanamchungu mengi sana na marehemu. Na sasa ndiyo nafasi yao ya kutoa nyongo. Tuwaache watoe yao ya moyoni.
Pia wapo ambao Magufuli aliwatendea mema. Pia wanahaki ya kuwa upande wake.