SMS hizi! Ungefanyaje?

SMS hizi! Ungefanyaje?

Ama kweli UALIMU kazi ya wito

MWANAFUNZI mmoja hajui kujumlisha wala kutoa. Mwalimu katumia njia zote kumuelimisha lakini wapi ikabidi ajaribu njia hii.
Mwalimu: Kwenu mnafuga nini?
Mwanafunzi: Kuku na mbuzi
Mwalimu: Mbuzi mnao wangapi?
Mwanafunzi: 25
Mwalimu: Mbuzi 25 toa mbuzi 5 watabaki wangapi?
Mwanafunzi: Unawajua mbuzi wetu au unawasikia? Ukimtoa mmoja tu nje wote wanatoka!
Mwalimu: Mmh! Naacha kazi mimi kama mambo yenyewe ni hivi, basi tena.

teh teh teh
 
AMA KWELI

  1. Maji ya nazi nayo ni maji, lakini huwezi kuchemsha chai.
  2. Kaa ukijua dagaa haanikwi kwenye kamba.
  3. Hata uwe mkurugenzi wa bandari huwezi kwenda na meli nyumbani.
  4. Pilipili hata iwashe vipi haiwezi kuwasha TV.
  5. Hata uongee neno zuri kwenye msiba hupigiwi makofi.
  6. Hata uwe mpishi vipi huwezi kusonga ugali kwenye frying pen.
  7. Hata uwe na haraka vipi huwezi kuomba lift kwenye gari la taka.
  8. Kumbuka kuku wa kuchorwa hadonoi.
  9. Ujinga ni kufuta namba ya mpenzi wako kwa hasira wakati ipo kichwani.

HIYO NI MISEMO YA WIKI NZIMA USINISUMBUE MPAKA WIKI IJAYO, SAWA?
 
Mume: Kiwango gani unanipenda baby?
Mke: Zaidi ya unavyofikiria.
Mume: Hebu nieleze basi.
Mke: Mimi ni simu na wewe ni line. Bila ya line simu haiwezi fanya kazi yoyote hivyo bila ya wewe sina kazi.
Mume: Oh honey I love you!
Mke: (Kimoyomoyo) "Asante Mungu, hili kweli jinga. Halijui kama simu za kichina zinaingia hadi line 3
 
Wasukuma watatu walienda mjini kwa ndugu yao. Walipofika wakapewa soda wakanywa. Mmoja akachukua kisoda akaweka mfukoni, akamnong'oneza mwenzake "NASOLA MBIYU (nimechukua mbegu) TUKAHAMBE NUBHISE UKUKAYA TUNONINO UTWENUTU (tukapande na sie nyumbani utu tumaji tutamu)".

Chezea Wasukuma wewe!
 
VIKOJOZI WATARUDI KIJIJINI

Baba anawaambia watoto atakayekojoa kitandani usiku dawa yake ni kurudi kijijini. Basi siku hiyo usiku baba na mama wakiwa katika mambo yetu yaleeee! Mama aliponogewa akaanza kupiga kelele nak**oa! Mara mtoto akadakia Mama usik**oe utarudishwa kijijini!
 
*************************************

Mrembo alipokea simu ngeni na mambo yalikuwa kama hivi:
Simu: Hellow una boy friend?
Mrembo: Ndio nine. Kwani we nani?
Simu: Mimi baba yako. Kumbe una boy friend ukirudi utanitambua. Simu ikakatika akiwa na mawazo nini afanye. Simu ikaita tena kwa namba ngeni.
Simu: Hello una boy friend?
Mrembo: Hapana sina!
Simu: Vipi mpenzi ina maana unanisaliti?
Mrembo: Hapana BABY nilijua baba!
Simu: Ni mimi baba yako nilitaka kuhakikisha tu kama kweli una boy friend. UTANIKOMA LEO!

*********************************

Fikiria ingemuwa baba yako ni Remmy Ongala, na mama yako Anne Makinda. Mjomba wako ni Mizengo Pinda na shangazi yako ni Anna Mkapa. Babu yako ni Stephen Wasira na bibi yako ni Bi. Kidude. Je sura yako ingekuwaje?

***********************************

Mwanasheria alimuuliza Lulu, Mbona wewe malaya sana? Lulu akajibu, Rose Muhando ndio malaya kwani Ameonja hadi Utamu wa Yesu. Mwanasheria akaguna!!

************************************

Ingekuwa kama ya mama yako hahahahha
 
Jamaa alikuwa anasumbuliwa na panya akaamua kuwategea sumu kwenye nyama ya nguruwe. Kesho yake akakuta karatasi imeandikwa 'TUWEKEE KWENYE SAMAKI SISI WENGINE NI WAISLAM'

hahaha!
Mbavu zangu mie!
 
MFUMO wa MAPENZI kwa vipindi tofauti


MIAKA YA: 1975 -1980
"NIMEKUBALI lakini namwogopa Baba na Mama watajua!"

MIAKA YA: 1980 - 1985
"NIMEKUBALI lakini sitaki kufanya mapenzi mpaka unioe!"

MIAKA YA: 1987 - 1993
"NATAKA lakini tutumie kondomu!"

MIAKA YA: 1994 -2000
"NI PESA yako tu maneno sitaki!"

SASA balaa tupu ipo hapa 2006 - 2013
"NIMEKUBALI lakini haupo peke yako!"
 
PROFESA WA SAYANSI YA KOMPYUTA ANAMTONGOZA BINTI


"Penzi langu lina "GB" kubwa sana kwako mpenzi. Nataka ni "INSTAL" moyo wangu kwenye "CPU" ya nafsi yako. Naomba uni "double click" kwenye maisha yako ili niwe "software" moyoni mwako"
 
MWALIMU WA KEMIA NAYE SASA KATOA KALI

Dada kiukweli uzuri wako ume-increase The Rate of Chemical Reaction moyoni mwangu. Zaidi pozi lako la kuongea limeweka catalyst na kunifanya ni-react vigorously. Pia nahisi unaweza kutoa heat zaidi ya luminous flame. Hivyo tukiwa pamoja organic compounds za moyo wangu zitabond na zako ili kuconfirm kuwa mimi ni cation na wewe ni anion pale penzi letu litakapotoa Brick Red Flame. Nadhani tupo kwenye equillibrium!!
 
Kwa kuwa mwanamuziki akifa husindikizwa kwa nyimbo, jeshi na polisi mizinga/ bunduki hupigwa. Je akifa mwalimu kuna ubaya gani akisindikizwa kwa bakora? au wewe unaonaje?
 
Ichunge misingi 6 ya mafanikio

  1. Usimchukie yeyote hata kama atakukosea vipi.
  2. Ishi maisha ya kawaida hata kama upo juu kwa kiasi kikubwa.
  3. Tarajia kheri hata kama mitihani ya maisha inakusakama.
  4. Toa kwa wingi hata kama wewe umenyimwa.
  5. Onesha tabasamu hata kama wamekuvunja moyo.
  6. Usiache haya ili yawe kinga yako nyuma upole, mbele hekima, kushoto uvumilivu, kulia subira
 
Cheki kimombo cha polisi wa bongo baada ya kumkamata mzungu:

Yesterday I saw you at the maize shop (jana nilikuona dukani kwa muhindi). When you saw me you started to six six (uliponiona ukaanza kusitasita). When I follow you run and plant a car (nilipokufuata ukakimbia na kwenda kupanda gari). Now your down of security (sasa upo chini ya ulinzi). Sleep and snake well before I cut you a millet (lala nyooka vizuri kabla sijakukata mtama)
 
Maisha ya DAR tunayajua wenyewe jamani! Hongera walio SHAMBA ambako wanachinja kuku na kuliwa nyumba hiyo hiyo. Hapa DAR KUKU anachinjwa KISUTU. Shingo inaliwa KINONDONI. Kibawa kinaliwa MANZESE, kidari TABATA, paja OYSTERBAY, firigisi MASAKI, miguu MBAGALA, mbavu MIKOCHENI, utumbo TANDIKA, kichwa TANDALE, mgongo MWENGE, ngozi KEKO.

Chezea DAR wewe, msoso wetu kama mgao wa UMEME kila mtu lazima apate
 
Dogo mmoja alikuwa amekaa na baba yake, ghafla demu wake akaja
Dogo: Karibu sana. Vipi umefata kile kitabu chako cha SPEAK ENGLISH MY FATHER CANNOT UNDERSTAND?
Demu: Ndio, nipe na kile cha WHERE CAN WE MEET?
Dogo: Hicho sina, labda nikupe cha WE CAN MEET UNDER MANGO TREE
Demu: Basi nipe kile cha I GIVE YOU 5 MINUTES.
Demu: Haya mi naenda ila usisahau kile cha I LOVE YOU
Baba: Mbona huyu mtoto anataka vitabu vingi sana, vyote atavisoma avimalize kweli?
Dogo: Huyu ana akili sana, ndo huwa anaongoza darasani.
Baba:Basi mpe na kile cha I HAVE UNDERSTOOD ALL THE STUPIDITY YOU WERE TALKING...
 
Back
Top Bottom