Sitaki Ualimu, nimechoka naombeni ushauri

Sitaki Ualimu, nimechoka naombeni ushauri

Kuna wanadamu walioumbwa kutokutulia hata apate kazi ya namna gani , yeye atatamani tu mahangaiko. Yaani wao kukaa sehemu moja hawaridhiki.

Hizi biashara unazotaka kufanya nje ya ajira unaweza kuzifanya ukiwa bado upo ndani ya ajira yako- shida watumishi tukikopa tunakimbiliaga kujenga na kununua magari badala ya kuanzisha miradi ya uzalishaji na maendeleo. Sasa makato yanapopamba moto hlf take home mwisho wa mwezi inabakia kidunchu unakosa hamu ya kazi kabisa

Biashara nyingi zilizofunguliwa ukiwa kazini zimefeli kwasababu ya usisamizi.
Kabla hujafungua biashara ANGALIA SANAA MSIMAMIZI.

#YNWA
 
Tulia Sasa mkuu vuta pumzi, hapo cha kufanya kopa benki, baada ya hapo nenda Bayport kopa mpaka moja ya Tatu hakikisha kadi yako mshahara unaingia buku tano tu, baada ya hapo usiache kazi mwenyewe fanya kudoji kazini mwezi mzima bila taarifa utakuta barua ya kufukuzwa kazi juu ya Meza ya mkuu wa shule ndipo lengo lako litakuwa limetimia maana mkopo una Bima kwahiyo watajijua na mwajiri wako na Bayport itakuwa imekula kwao

Fanya biashara ya huduma za kifedha na ufugaji wa kuku kienyeji hutajuta baada ya miaka mitatu pesa yako ya mwezi utakuwa mshahara wa walimu watano wenye TGTS Wasio kuwa na madeni yoyote
Haya mawazo ya kizamani sana au huna information za Sasa kuhusu ma bank! Ma Bank yote siku hizi yana wasiliana kwenye system linapokuja swala la Mikopo!!
 
Nawashauri walimu mpende kusoma kanuni za utumishi wa umma (public standing order)
Tatizo kubwa ni kutojua kanuni na akitokea mtu wa kuwatetea hamuungi mkono.

Hofu ya kuhamishwa vituo vya kazi kama adhabu, kushushwa cheo kwa wakuu, inatawala sana. Baadhi ya walimu wanaendeshwa kama magari yasiyo na injini
 
habarini wanajamvi?

Nimekuwa nwalimu wa miaka 5 sasa katika mkoa X na shule nayofundisha kwakweli si mbaya sana ina mazingira mazuri kiasi.Lengo la kuja hapa JF ni kuomba ushauri juu ya hatma ya maisha yangu.

Najua kila mtu hajawahi kutosheka juu ya mishahara yao lakini kwa sisi walimu naona hali inazidi kuwa mbaya, Serikali inatukandamiza kwa makato ya siyo ya lazima kama kuchangia mwenge na tunalazimishwa eti mwenge ukija mkoani kwetu lazima walimu tuwepo kuupokea.

kwanini kila kitu mpka sisi walimu tushiriki aiseee, nimechoka kuona kada yangu pendwa imekuwa inadharaulika na serekali kwa kutupiwa kila kitu cha kisiasa matokea yake walimu tumekuwa watu wa mkakati kwa wanasiasa ili kufanikisha azma yao.

Natamani kuacha ualimu ila naogopa wapi ntapata chanzo kingine cha mapato,na sitaki mikopo kabisaa

Naonmbeni ushauri wa wa biashara gani ya kufanya ili niondoke kwenye ualimu

(Sitaki kufungua kijiwe cha tuisheni, walimu tumekuwa tukiona tuisheni kama ni njia pekee ya kujiajiri SITAKIII)

msaada jamani
Nimekuwa nwalimu wa miaka 5 sasa katika mkoa X
Sorry si kwamba nakushushua lakini uko Moro.. Usiniulize nimejuaje..
 
Biashara nyingi zilizofunguliwa ukiwa kazini zimefeli kwasababu ya usisamizi.
Kabla hujafungua biashara ANGALIA SANAA MSIMAMIZI.

#YNWA
Rwehumbizadarlin ebu mtafute huyu mtani wangu Liverpool VPN aliyenipiga 7-0 hata inbox Ili akupe madini yaliyo na hands-on life experience Ili huepuke kufanya makosa utakayojutia baafae
 
Kazini kwetu wapo wawili.
Wa kwanza.
1. Alikopa mkopo wa Hazina mil 38
2. Akakopa mikopo umiza Mil. 5
Akasepa, sasa yupo dar ana bonge la biashara.

Wa pili.
Alikopa benki ya posta mil 25
Yupo Iringa analima parachichi na ufugaji.

Hivyo, INAWEZEKANA.

#YNWA
Usijali kuna siku watakamatwa tu Jinai haifi Mzee Baba!!
 
Rwehumbizadarlin ebu mtafute huyu mtani wangu Liverpool VPN aliyenipiga 7-0 hata inbox Ili akupe madini yaliyo na hands-on life experience Ili huepuke kufanya makosa utakayojutia baafae

Wengine tulikuja ajirani kutafuta mtaji, tukifikia lengo LAZIMA TUONDOKE.

Tuendelee kupambana, kila mtu ashinde mechi zake.

#YNWA
 
Unapowaza cha kazi gani, kuna wanaowaza watakipata lini.

Yachunguze mawazo yako kwa kina isije ikawa ni umeikinai kazi, hauna tu hamu na kazi jambo ambalo humkuta kila binadamu katika kila kazi..

Na kama ni hivyo, ku-deal na changamoto kama hiyo sio kuicha hiyo kazi
 
Hii njia niliitumia mwaka 2012 baada ya kuchoka ualimu.so nilikopa NMB,CRDB na Posta Bank..20M in total..nikaenda chuo kikuu X nikasoma Banking and finance nilipomaliza 2015 nikaajiliwa kwenye private company X hadi 2021...nikaacha now Nina migodi yangu ya dhahabu mkoa X...Maisha mazuri sana km ukithubutu...NB nimefanya story iwe fupi japo nimepitia changamoto nyingi mzito

mkuu una migodi ya dhahabu??

kama hutojali tubadilishane uzoefu mimi pia niko kwenye sekta hyo
 
Unapowaza cha kazi gani, kuna wanaowaza watakipata lini.

Yachunguze mawazo yako kwa kina isije ikawa ni umeikinai kazi, hauna tu hamu na kazi jambo ambalo humkuta kila binadamu katika kila kazi..

Na kama ni hivyo, ku-deal na changamoto kama hiyo sio kuicha hiyo kazi
Miye napiga ualimu,ni mwanasiasa,ni mfugaji,mkulima na mfnyabiashara

Mshahara haukupi utajiri ila unakupa koneksheni na watu
 
Back
Top Bottom