kix
JF-Expert Member
- Mar 21, 2009
- 319
- 86
too low!!!!Zitto wewe sio mtu makini hata siku moja ,kwa uzi huu umekurupuka .Kila siku nasema Watanzania watakufahamu vyema kuwa wewe ni mtu wa aina gani . Sio kila tuhuma zinazokuhusu unatakiwa kuzijibu ,kukaa kimya pia ni busara . Usililolijua ni kama usiku wa giza ,bila kujua umeshajiingiza kwenye mtego wa malumbano na vijana walioaminika kuwa walikuwa wanashirikiana na wewe kwa mabaya ama mazuri pindi wakiwa CDM kabla hawajafukuzwa na kwenda CCM .
"Brother you're falling ",amini usiamini .Kuna uzi umeanzishwa humu muda si mrefu na Mwampamba (kama vile mods wameuondoa ) ila unazunguka kwa kasi twitter na Facebook .Hawa vijana wameanza kukuvua nguo jemedari ,chukua hatua stahiki . Kama ni kweli unayotuhumiwa ya kuihujumu CDM ni kweli rudi kwa Watanzania waombe radhi bado wanaimani kubwa sana na wewe . Ukiona wanakukingia kifua kwa kila baya unalorushiwa jua hawaamini wanaona kama vile ni chuki binafsi .Ila kama unajua na kuamini huna makosa endelea kupambana na kutunishiana misuli na hawa vijana .
Umeandika humfahamu Ben Saanane ,ila wameshaanza kukusuta kuhusu hilo .Huo ni mwanzo tutasikia mengi sana ,hao vijana kwa uzi huu wanaona kama vile unaanza kuwasaliti kwani wanajua wazi kuwa wameanguka ,hawatakubali waanguke peke yao .Utakuwa salama kama ni kweli hukushirikiana nao kwa jambo lolote lililopelekea kwa wao kufukuzwa CDM .Wanavidonda visivyotibika ,walichokiandika leo kupitia Mwampamba imenishangaza sana nanukuu "Ni maneno yanayoudhi na kutoka katika misingi ya kulindana" ,leo maneno yako yanawaudhi kwamba ugomvi wao sasa wanaugeuzia kwako na sio Dr.Slaa na Ben Saanane.Mbaya zaidi wanasema walikula kiapo kutokukuhusha na tuhuma zao iweje wewe unaanza kuwachokonoa ! Wanajitapa wanayo last card inayoweza kukupoteza "Blackmail "
Kila jambo lina mwanzo na mwisho ,baadhi ya mambo huishia pabaya .