Ndata
JF-Expert Member
- Mar 2, 2017
- 226
- 321
ZITTO ANAPOMFUNDA MBOWE KWA VITENDO.
Aliyekuwa kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na mpigania demokrasia ndani ya vyama na serikali kwa ujumla Zitto kabwe aachia ngazi baada ya miaka kumi ya utumishi ndani ya chama cha ACT.
Hii ni habari chungu sana kwa Mbowe, kiongozi aliyekiongoza chama tangu mwaka 2005 mpaka leo na bado anaamini ndani ya chama chake hakuna mrithi bora wa kukikalia kiti alichokikalia kwa miaka kumi na tisa (19).
Yaani Lissu mnayetaka tumpe nchi chama tuu chenye watu million moja hakimuamini ila mnataka tumpe nchi yenye watu milioni 60.
Kwa Mbowe chama ni cha muhimu zaidi ya nchi. Anyway hayo ni mawazo yake na ya heshimiwe.
Uenyekiti wa Chadema umesababisha maafa, kufukuzana na kukibomoa chama. Yaani Kaborou hakufaa, Wangwe hakufaa na Zitto hakufaa baada ya hapo hakuna nwanachadema hata mmoja anayetamani kukitaka kiti. Maana usipokufa ponapona yako ni kufukuzwa.
ACT iliyoanzishwa rasmi mwaka 2014 na Zitto kuwa KC wa kwanza mwaka 2015 leo kinashuhudia mabadiliko makubwa kipindi ambacho chama kinaanza kukuwa, kupokea ruzuku na kuenea kila kona ya nchi. Ila Mbowe aliyekula ruzuku za chama tangu uanzishwaji wake anaona dhambi kuachia akili mpya.
Sawa tukubaliane na hoja ya Chadema kwamba Zitto kaachia usukani huku mlango wa nyuma akiendelea kuwa Kc, vipi Mbowe anashindwaje kufanya hivyo kwa kuwaachia vijana wake anaowaamini kina Lema?
Zitto aliondoka Chadema baada ya figisu za uenyekiti, hakuamini katika udikteta wa Mbowe kung'ang'ania kiti, alitamani kumfundisha kwa vitendo na leo kamfundisha kwelikweli. Sidhani kama Mbowe bado ni mkosa aibu kuendelea kushikilia usukani wa Chadema.
Zitto ameachia uongozi mkuu wa chama akiwa bado kijana shupavu, mjenga hoja na mwenye ushawishi tofauti na Mbowe anayeng'ang'ania ilihali hana tena ushawishi, ujenzi wa hoja sifuri na ule ushupavu wake ulishajiishia.
Watanzania wameshindwa kuuamini upinzani kwa miaka mingi sababu ya viongozi aina ya Mbowe wanaotuhubiria demokrasia huku wao wakitenda udikteta, wanaohubiri ubadhirifu ndani ya serikali huku wao wakijilia ruzuku ambayo nayo ni kodi anayotozwa mtanzania.
Zitto ndani ya miaka kumi ya uongozi wake kajenga ofisi kubwa, nzuri na iliyo organised wakati Mbowe ndani ya miaka 19 ya uongozi wake hata choo cha Chadema hakipo.
Zitto ndani ya miaka kumi ya uongozi wake kafanikiwa kuiteka Zanzibar wakati Mbowe kwa miaka 19 hata diwani Zanzibar hana achilia mbali mbunge.
Tujiulize kwa pamoja, 2015 Mbowe angekubali kumuachia Zitto uenyekiti Chadema ingekuwa wapi?
2015 Mbowe angeamua kumuachia Zitto uenyekiti upinzani kwa ujumla ungekuaje?
Asante sana Zitto kwa kuubadilisha upinzani kwa vitendo, Asante sana Zitto kwa kumfunda Mbowe kwa vitendo. Mpira tunamiachia Mbowe aonyeshe kaelewa somo au ataendeleza uhuni wake wa kulinda Mali ya ukoo.
Aliyekuwa kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na mpigania demokrasia ndani ya vyama na serikali kwa ujumla Zitto kabwe aachia ngazi baada ya miaka kumi ya utumishi ndani ya chama cha ACT.
Hii ni habari chungu sana kwa Mbowe, kiongozi aliyekiongoza chama tangu mwaka 2005 mpaka leo na bado anaamini ndani ya chama chake hakuna mrithi bora wa kukikalia kiti alichokikalia kwa miaka kumi na tisa (19).
Yaani Lissu mnayetaka tumpe nchi chama tuu chenye watu million moja hakimuamini ila mnataka tumpe nchi yenye watu milioni 60.
Kwa Mbowe chama ni cha muhimu zaidi ya nchi. Anyway hayo ni mawazo yake na ya heshimiwe.
Uenyekiti wa Chadema umesababisha maafa, kufukuzana na kukibomoa chama. Yaani Kaborou hakufaa, Wangwe hakufaa na Zitto hakufaa baada ya hapo hakuna nwanachadema hata mmoja anayetamani kukitaka kiti. Maana usipokufa ponapona yako ni kufukuzwa.
ACT iliyoanzishwa rasmi mwaka 2014 na Zitto kuwa KC wa kwanza mwaka 2015 leo kinashuhudia mabadiliko makubwa kipindi ambacho chama kinaanza kukuwa, kupokea ruzuku na kuenea kila kona ya nchi. Ila Mbowe aliyekula ruzuku za chama tangu uanzishwaji wake anaona dhambi kuachia akili mpya.
Sawa tukubaliane na hoja ya Chadema kwamba Zitto kaachia usukani huku mlango wa nyuma akiendelea kuwa Kc, vipi Mbowe anashindwaje kufanya hivyo kwa kuwaachia vijana wake anaowaamini kina Lema?
Zitto aliondoka Chadema baada ya figisu za uenyekiti, hakuamini katika udikteta wa Mbowe kung'ang'ania kiti, alitamani kumfundisha kwa vitendo na leo kamfundisha kwelikweli. Sidhani kama Mbowe bado ni mkosa aibu kuendelea kushikilia usukani wa Chadema.
Zitto ameachia uongozi mkuu wa chama akiwa bado kijana shupavu, mjenga hoja na mwenye ushawishi tofauti na Mbowe anayeng'ang'ania ilihali hana tena ushawishi, ujenzi wa hoja sifuri na ule ushupavu wake ulishajiishia.
Watanzania wameshindwa kuuamini upinzani kwa miaka mingi sababu ya viongozi aina ya Mbowe wanaotuhubiria demokrasia huku wao wakitenda udikteta, wanaohubiri ubadhirifu ndani ya serikali huku wao wakijilia ruzuku ambayo nayo ni kodi anayotozwa mtanzania.
Zitto ndani ya miaka kumi ya uongozi wake kajenga ofisi kubwa, nzuri na iliyo organised wakati Mbowe ndani ya miaka 19 ya uongozi wake hata choo cha Chadema hakipo.
Zitto ndani ya miaka kumi ya uongozi wake kafanikiwa kuiteka Zanzibar wakati Mbowe kwa miaka 19 hata diwani Zanzibar hana achilia mbali mbunge.
Tujiulize kwa pamoja, 2015 Mbowe angekubali kumuachia Zitto uenyekiti Chadema ingekuwa wapi?
2015 Mbowe angeamua kumuachia Zitto uenyekiti upinzani kwa ujumla ungekuaje?
Asante sana Zitto kwa kuubadilisha upinzani kwa vitendo, Asante sana Zitto kwa kumfunda Mbowe kwa vitendo. Mpira tunamiachia Mbowe aonyeshe kaelewa somo au ataendeleza uhuni wake wa kulinda Mali ya ukoo.