Asante Mkuu.
Naomba kama unaamini uliyoyasema humu usiishie hapo.Kuna haja ya kulitaka Gazeti la Mtanzania kukanusha habari hizi kwenye Ukurasa ule ule waliotumia kuandika.Uzushi wa namna hii kwenye jamii iliyojaa matatizo, watu wasiofikiri sawa tayari wamehitimisha na kuamini kilichoandikwa ndiyo ukweli wenyewe.Lakini haitoshi hata wale wanaozusha uongo huu kwa sasa wanatumia Gazeti hilo kama ndiyo ukweli wenyewe.
Naomba sana kwa faida ya ukweli na kuitendea Chama chako haki chukua hatua.
Watu wa mwanzo kabisa kushughulika nao ni hawa hapa: Charles Mulinda ambaye ni mhariri wa Mtanzania Jumatano. Haeleweki. Wa pili ni Ester Mbusi aliyeandika habari hiyo, kama hakupewa by line na Mulinda, na wa tatu ni William Shao ambaye ni mwandishi na mtunzaji wa website ya Mtanzania aliyeposti habari hiyo mtandaoni. Anzeni na hao watatu.