Zitto anapendwa sana na watu, akiwa mgombea wa kiti cha urais kwa kupitia CHADEMA, CCM tutakuwa na wakati mgumu sana.
kwa wanafalsafa na wataalamu wa fasihi, watabaini kuwa uzi wa zitto umejaa falsafa ya hali ya juu. anaonekana kukanusha lkn kwa undani anasema kuwa kama ni kweli basi itakua imeandikwa na Mungu.
kwa kusoma juujuu, zitto amemuokoa slaa na tope la ugaidi ambalo lilikua limeanza kumchafua. kisiasa ana sababu zake anazozijua zilizomfanya amuokoe mzee.
TAHADHARI KWA ZITTO
kamanda zitto ni kwa mara ya kwanza naona zaidi ya 90% ya wachangiaji wakikuunga mkono! wamekuunga mkono kwa asilimia kubwa KWA SABABU UMEMUOKOA SLAA. habari ya leo ya gazeti la mtanzania ni kubwa sana! weka maanani kuwa una maadui wengi chamani
Mh.zitto haya magazeti yetu na vyombo mbalimbali vya serekali vinaendeshwa na skendo/mawazo ya watu humu jamii forums
1)TCRA ilivifungia vyombo kadhaa vya habari baada ya thread kuanzishwa humu
2)gazeti hilo la mtanzania na magazeti mengine yanaendeshwa na habari wanazoziona huku
3)hata kukamatwa kwa lwakatare walipata hiyo clip hukuhuku jamii forums
Kwaiyo nadhani wasikupe shida sana na pili washauri wabadilike kama nchi inaendeshwa na mawazo ya watu hapa jf inasikitisha
Kikubwa mheshimiwa zitto nakushauri hama chadema na utengeneze chama chenye malengo ya kumkomboa mtanzania
Chadema imeshaoza sana .........Take this from me
nadhani mnachokitafuta kitakuja tu,ila msiwe wa kwanza kuja JF na kuanza kupiga kelee,maana watanzania tumewazoeaNinachofahamu ni kuwa serikali ya masalia iliyokuwa inaongozwa na ZZK ilipinduliwa na Ben Saanane kama ambavyo Serikali ya JK ilivyopinduliwa na RICHMOND/DOWANS ya Rostam. Kama ambavyo haiingii akilini JK anaposema hamfahamu Rostam ndivyo hivyohivyo haiingii akilini ZZK anaposema hamfahamu aliyepindua kikundi chake cha Masalia.
kumuita dogo....nk.... sidhani kama kichwani kwako pamekaa vizuri
Zitto wewe sio mtu makini hata siku moja ,kwa uzi huu umekurupuka .Kila siku nasema Watanzania watakufahamu vyema kuwa wewe ni mtu wa aina gani . Sio kila tuhuma zinazokuhusu unatakiwa kuzijibu ,kukaa kimya pia ni busara . Usililolijua ni kama usiku wa giza ,bila kujua umeshajiingiza kwenye mtego wa malumbano na vijana walioaminika kuwa walikuwa wanashirikiana na wewe kwa mabaya ama mazuri pindi wakiwa CDM kabla hawajafukuzwa na kwenda CCM .
"Brother you're falling ",amini usiamini .Kuna uzi umeanzishwa humu muda si mrefu na Mwampamba (kama vile mods wameuondoa ) ila unazunguka kwa kasi twitter na Facebook .Hawa vijana wameanza kukuvua nguo jemedari ,chukua hatua stahiki . Kama ni kweli unayotuhumiwa ya kuihujumu CDM ni kweli rudi kwa Watanzania waombe radhi bado wanaimani kubwa sana na wewe . Ukiona wanakukingia kifua kwa kila baya unalorushiwa jua hawaamini wanaona kama vile ni chuki binafsi .Ila kama unajua na kuamini huna makosa endelea kupambana na kutunishiana misuli na hawa vijana .
Umeandika humfahamu Ben Saanane ,ila wameshaanza kukusuta kuhusu hilo .Huo ni mwanzo tutasikia mengi sana ,hao vijana kwa uzi huu wanaona kama vile unaanza kuwasaliti kwani wanajua wazi kuwa wameanguka ,hawatakubali waanguke peke yao .Utakuwa salama kama ni kweli hukushirikiana nao kwa jambo lolote lililopelekea kwa wao kufukuzwa CDM .Wanavidonda visivyotibika ,walichokiandika leo kupitia Mwampamba imenishangaza sana nanukuu "Ni maneno yanayoudhi na kutoka katika misingi ya kulindana" ,leo maneno yako yanawaudhi kwamba ugomvi wao sasa wanaugeuzia kwako na sio Dr.Slaa na Ben Saanane.
Kila jambo lina mwanzo na mwisho ,baadhi ya mambo huishia pabaya .