Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Sibishani na mtu asiyejua maana ya heading. Heading ndiyo inamaliza yale yoote yanayofuata baada yake. Na heading ya hii thread imeshasema kwamba huo ni uwongo. Wewe unataka kulazimisha nini sasa.

Safi sana mkuu!
 
Hongera naibu katibu mkuu na mjumbe wa kamati kuu,umenena vema ila chukuwa tahadhari kwani hawa jamaa(ccm)wanaweza kutumia maneno hayo wanayoyanadi kila sku na vibaraka wao,wakatengeneza wangwe sityle wakidhani kuwa ndyo turufu yao kisiasa 2015,naamini kul-nafsi-idhaa-ikatrumaut lakini sio kila kifo anapanga yeye kuna vingine anapanga mwanadamu.
 
Huwa siku zote nakukubali jembe. Mungu akubariki uwe na maisha marefu sana
 
asante kamanda kwa kututoa njia panda maana watu wanapika propanganda usiku na mchana
 
tatizo lililopo ni kwamba,waandishi wanalazimisha swala hili lionekane ni lakweli,tangu awali Mh Zitto alishalisemea hili kuwa hajawahi onana na saanane na hata wakipishana barabarani watapishana,kwanini tunalazimisha mtu kumfahamu fukani?
watanzania tuache kuunganisha dots,tuache kulazimisha mambo,Zitto sio mjinga,anachokisema anamaanisha na tusilazimishe
Kauli kama hii ilishawahi kusemwa na JK "...simfahamu na wala sijawahi kumuona mmiliki wa DOWANS" wakati DOWANS ndo kaiangusha serikali yake nzma na cha ajabu aliye mahakamani kuishtaki serikali yake juu ya mkataba wa DOWANS ni yulyule aliyemuweka madarakani kwa hela za KAGODA - Rostam".
Hata kama ni kweli Rais alitaka kutuaminisha kuwa hajui kama DOWANS ni mali ya Rostam lakini kitendo cha kuiangusha serikali yake kilitosha kumpa interest ya kumtafuta na kumjua.
Leo Zitto anatuambia hanjui Ben Saanane. Hata kama kweli alikuwa hamjui mwanzoni, lakini kitendo cha Ben kuangusha serikali yake ya masalia ingempa interest ya kuonana na Ben na kumfahamu. Ikumbukwe kuwa Zitto hawezi kuwakimbia masalia akina Shonza na Stella Mwampamba. Zitto hajawahi kuwakana kiuwazi masalia wenzake wote. amekuwa akisema kwa kumeza maneno tu. angalia thread yake ya kuomba radhi mwishoni mwa mwaka jana hayupo specific, anaomba radhi kiujumlajumla tu. Leo pia anasema WALIOHAMA sio WALIOFUKUZWA kama akina Shonza na Mtella. Kwa nini anaongea kiujanjaujanja, Ataje majina ya anaotaka waache kuizungumzia CDM, mbona wao wako wazi sana? wanamtaja mbaya wao Dr Slaa waziwazi, wanamtaja Mbowe waziwazi. (HAWAJAWAHI KUMTAJA ZITTO KWA UBAYA - Hili linathibitisha alichokisema Ben kuwa Zitto ndo alikuwa prezo wao). Zitto come out! ongea kwa kufungua kinywa vizuri na sio kumung'unyamung'unya maneno.
 
Duh! nyinyi watu kwa spinning!

btw naona baada ya zoezi la kumchonganisha Zitto na viongozi wengine kushindwa mnataka kuanzisha Lissu na viongozi wake lakini hili ndio hamtafanikiwa kabisaaaa!!

Mkuu MTAZAMO Spinning zinaanziswa na hao viongozi wa CHADEMA kwa sababu hawako straight kwenye majibu yao kila mara.

Ukiangalia hii statement ya Mh. Zitto, inatoa jibu kwa upande mmoja halafu inaleta tena mjadala kwa upande wa mwingine ukiangalia matukio ya nyuma.

Mpaka hapo viongozi wa CHADEMA watakapo acha siasa zao za ndani za kunyemelea kati ya kiongozi na kiongozi basi hata spin nazo zitaisha.
 
Last edited by a moderator:
Mtanzania hiyo habari wameitoa humu kwenye JF Mbona jf bado Maarufu?
hilo ni tatizo la mods kuruhusu upuuzi kukaa humu jamvini. Habari kama ile ilikuwa inaonekana wazi kuwa ni ya kipuuzi na kichonganishi na wanaoweka wanajulikana kwa majina na IDs lakini mambo yanaachwa tu yaende.

JF isipoangalia, inaweza kuwa moja ya sababu ya misuguano katika jamii yetu.
 
Hello ndugu yangu Zitto, nakupongeza sana kwa majibu haya ambayo hayana kujiumauma ndani yake lakini yanayooneysha ujasiri wa kile unachokiamini kuelekea maono yako na ya CHADEMA kwa ujumla.

CHADEMA na wana CHADEMA wataendelea kupata vita ya maneno na propaganda nyingi toka upande wa walioko CCM na vyama vingine. Na ukweli ni kuwa CHADEMA sasa ni THREAT/TISHIO kwa watawala na CCM yake na hasa tunapoelekea/kukaribia mwaka 2015.

Ushauri wangu kwa wana CCM kama wangepunguza propaganda za uongo, wakajitahidi kuwaletea maendeleo ya kweli wananchi wala wasingekuwa na kazi ya kuwashawishi wapiga kura mwaka 2015. Lakini kwa kuwa wameamua vinginevyo/hawataki kufanya hili ndiyo maana wananchi walio wengi sasa wanaona bora kuchagua chama kingine anagalau tutaona kitu tofauti na kile kinachoendelea ndani ya Serkali sasa na CCM yake.

Kwa mara nyingine nakupongeka ndugu yangu Zitto na maombi yangu ni kuwa maono yako ya kuona nchi hii ikikombolewa kwa mara nyingine kutoka mikono ya wachache iweze kufikiwa.
 
Ukiketi kwenye jamvi kinachoendele ni UMBEA TU. Shonza ona sasa ulivyojiumbua pua juu pye pye pye pye!!!! Aibu tupu huko Lunch Time ulikuwa na nani vile?? Umesahahu???

Hao uliowatuhumu wanakushitaki mahakani!!!
 
Bravo Zitto. Well said Mkuu. Hao magamba waambie wakome kutumia jina lako kwa manufaa yao ya kisiasa!
 
Nilisema hapa huu ni uzushi sasa Mwandishi wa habari ile anasemaje? ndio maana baadhi ya wanandishi wanaitwa Makanjanja hawa watu njaa njaa sana...
 
Wale WAPUMBUVU mnaoota KIFO cha CHADEMA mtakufa kwa kukosa usingizi.kwani hamuvioni CUF,TLP,UDP,NCCR-M na vyama vingine
 
Zito ni mvumilivu sana

Ujumbe umefika lakini nina uhakika iko siku tutasikia kitu hapa.

Mie binafsi siamini kuwa kuna njama za kumuua Zito .

Mambo mengi huanzia hapa JF, hivyo nina uhakika iko siku tutasikia jingine.
Ni vigumu sana kondoo kuishi kwenye nyumba yenye simba wenye njaa, iko siku watamtafuna tu.
Kuna uwezekano mkubwa watu wanaokuchukia wakatumia jina la Dr Slaa kukutishia maisha na hii ni ndani na nje ya chadema.
Mie binafsi sijawhi kukutana nawe ila tumeongea mara nyingi kwenye simu na ningekupa ushauri tu
Kila unalolisikia litilie maanani, kwa sababu tayari mtu kapakwa tope basi mwingine anaweza kuja kukumaliza halafu wakasema si mnakumbuka ilivyoandikwa before? Yale yalee ya afande mshutiii!

NA UKIONA SIMBA ANAKUKENULIA MENO USIDHANI ANAKUCHEKEA.
 
Back
Top Bottom