Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Ganzi aka Stela Mwampamba! U suck it pal! Kiko wapi sasa? Hadi presidaa kawakana? Wap my hero Ben wa Saanane?
 
Nimependa saana hii... Maana hapa karibuni ilikuwa kila anaye weza anasema ajualo na aaminilo bila kujalisha ni kitu gani na kimetoka wapi. That is to say Zitto alikuwa na wasemaji hadi baaas! Bora umekuja na umeonyesha wazi msimamo wako!

Chadema ilipo sasa inahitaji kujipangua palipo jipanga ovyo kwa kujipanga vilivyo maeneo panguliwa. Na hiyo inawezekana tu pale Viongozi wa juu wapo karibu kwa mshikamano na niya thabiti ya kujenga chama na kuacha ubinafsi pembeni.

Kwa hili nakupongeza sana Mkuu Zitto, habari za Dr. Slaa kutaka kukupa sumu via Ben zipo too low na kutamka kwako inaonyesha wazi kuwa kuna watu ambao furaha yao ni kutokuwepo na maelewano mazuri kati yako na Viongozi wenzako hasa wa juu.

Nimependa pia suala la kuonyesha msimamo wako juu ya wale ambao wametoka Chadema! Inawezekana wanakukubali genuinely but it is high time washikamane na vyama vyao na waache kabisa masuala ya Chadema na viongozi wake kwani haviwahusu tena.

Hongera sana.

Aunty naomba niongeze kidogo. Hapo unasema inawezekana wanamkubali genuinely nadhani sio kweli.

Wangekua wanamkubali wangemtakia mema. Na wangemtakia mema wasinge thubutu kutunga uongo huu kua walikua hotel ambapo Zitto hajawahi fika, with someone Zitto hajawahi ona.

Hii inaonesha kua wanataka kutumia beef yao ya kijinga na ben saanane kwa kujitafutia umaarufu kupitia jina la Zitto. After all they were once in the same team, they use the same methods.

Mtu wowote mwenye akili timam, mwenye uchungu na chadema hawezi ku-entertain uongo kwa kufikia malengo yake. In this particular case the ends don't justify the means.
 
Kauli kama hii ilishawahi kusemwa na JK "...simfahamu na wala sijawahi kumuona mmiliki wa DOWANS" wakati DOWANS ndo kaiangusha serikali yake nzma na cha ajabu aliye mahakamani kuishtaki serikali yake juu ya mkataba wa DOWANS ni yulyule aliyemuweka madarakani kwa hela za KAGODA - Rostam".
Hata kama ni kweli Rais alitaka kutuaminisha kuwa hajui kama DOWANS ni mali ya Rostam lakini kitendo cha kuiangusha serikali yake kilitosha kumpa interest ya kumtafuta na kumjua.
Leo Zitto anatuambia hanjui Ben Saanane. Hata kama kweli alikuwa hamjui mwanzoni, lakini kitendo cha Ben kuangusha serikali yake ya masalia ingempa interest ya kuonana na Ben na kumfahamu. Ikumbukwe kuwa Zitto hawezi kuwakimbia masalia akina Shonza na Stella Mwampamba. Zitto hajawahi kuwakana kiuwazi masalia wenzake wote. amekuwa akisema kwa kumeza maneno tu. angalia thread yake ya kuomba radhi mwishoni mwa mwaka jana hayupo specific, anaomba radhi kiujumlajumla tu. Leo pia anasema WALIOHAMA sio WALIOFUKUZWA kama akina Shonza na Mtella. Kwa nini anaongea kiujanjaujanja, Ataje majina ya anaotaka waache kuizungumzia CDM, mbona wao wako wazi sana? wanamtaja mbaya wao Dr Slaa waziwazi, wanamtaja Mbowe waziwazi. (HAWAJAWAHI KUMTAJA ZITTO KWA UBAYA - Hili linathibitisha alichokisema Ben kuwa Zitto ndo alikuwa prezo wao). Zitto come out! ongea kwa kufungua kinywa vizuri na sio kumung'unyamung'unya maneno.

Mkuu kuna kitu unaDIG aiseee!!!!! tengua kauli, nasema tengua kauli, ohooooo ngoja nikuonyeshe sasa kama mimi ndo tajri wa kigoma braza K, eeeeeeeehhh unacheza na mimi wewe.
 
gazeti yawezekana limemnukuu ndivyosivyo.kumbuka story za mwanzo za hawa mnawaita masalia ilikua ni kwamba zito akimkwepa ben na hawakuwahi kutana.

Na kwamba siku mwapamba anakamata kipakiti kile cha ungaunga HAWAKUWA NA ZITO.walikua ni kina mwapamba na ben.
Kwanza according to mtanzania,anaandika wakati ben akitoa pesa kulipa bili yote ndo kipakiti kikadondoka.hapa kama zito alikuwepo haingii akilini ben ndo awe wa kuclear bill.

Sasa na wewe unashindwa kufahamu jasusi mjuzi hadi aaminiwe na katibu mkuu kufanya mauaji kwa kiongozi mmkubwa nnchini anaweza kufanya ujinga wa kulewa chakari kwenye mision kama ile halafu akamatwe na sumu na vijana wasiopitia mafunzo ya usalama,halafu wamuhoji bila hata ya kumnyofoa hata kucha moja,naye akiri kuwa anakwenda kumpa sumu ZZK.Mnasema Ben ni muuaji na jasusi,wale Shonza na Mtela hawana hata robo ujanja wa kupambana na mikono ya Ben.Nashawishika kwamba hiki unachoandika hukiamini hata kwa asilimia sifuri ila kwa kuwa upo kazini ndio maana unashindana na ukweli
 
HIlo ndo jembe bana mtazusha kila aina ya maneno lkn mtaambulia patupu
 
Nimezisikia hizi habari zikishabikiwa na kiredio fulani kama sikosei ni clouds fm wameishabikia hii mada utadhani siyo professionals, as if ni wamama fulani wamekaa kibarazani wanajadiri umbea. Clouds FM inajipotezea sana status yake kushupalia uzushi tena kwa upendeleo, uzushi unaokichafua CCM wanakuwa kimya ila uzushi wa kuichafua CHADEMA utamsikia Geladi Hando, Kibonde na watu wa level hiyo jinsi wanavyo ishupalia kimbea,

Namshukuru Mungu kwa kuniepusha na aibu ya kutumika na wanasiasa.
Hilo liredio hua linabugi kila kukichwa, sijui la nani? Mapamba na Mavyonza kwisha kazi yao.
 
...ahsante Mungu kwa kutubainishia maadui zetu mapema..."kila ubaya waufanyao gizani,ukuja roho na nyuso za wanafiki"...
 
Anamtaja mtu aliyetumwa kumuua Zitto kuwa ni Ben Saanane, ambaye aliangusha karatasi ya nailoni iliyokuwa na ungaunga unaosadikiwa kuwa sumu na kuonekana kwa watu waliokuwa eneo hilo, akiwemo Zitto mwenyewe pamoja na aliyekuwa Naibu Mwenyekiti wa Bavicha, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba.
Mimi binafsi nikikutana na Ben Saanane leo naweza kupishana naye maana sijawi kumwona, wala kukutana naye
Haya hapa angalieni uongo wa walau mmoja wa wahusika wa stori. Gazeti la Mtanzania linasema Ben Saanane aliangusha sumu na ikaonekana na watu waliokuwepo eneo hilo, akiwemo Zitto mwenyewe. Zitto anasema hajawahi kukutana na Ben Saanane na hata wakikutana hatamjua. Sasa nani mkweli na nani muongo, Gazeti Mtanzania/Shonza au Zitto au wote hawa?
Kuna mahali niliandika hayo kuonyesha kuwa at least one of them must be a liar
 
Nakuheshimu sana ZZK, wewe ni kiongozi unayejua unachofanya. Naunga mkono maono yako na namna unavyoyasimamia masuala ya msingi kwa chama na Taifa.

Kuwa makini sana na watu wanaotaka kutumia jina lako kuchafua chama. Naamini Dr. Slaa ni tishio kwa kila mpinzani wa CDM, ni wajibu wa kila mmoja akiwemo Dr. Slaa mwenyewe kuitunza heshima hiyo. Ninawaamini sana kuelekea 2015 tutafanikiwa.
 
Zito ni mvumilivu sana

Ujumbe umefika lakini nina uhakika iko siku tutasikia kitu hapa.

Mie binafsi siamini kuwa kuna njama za kumuua Zito .

Mambo mengi huanzia hapa JF, hivyo nina uhakika iko siku tutasikia jingine.
Ni vigumu sana kondoo kuishi kwenye nyumba yenye simba wenye njaa, iko siku watamtafuna tu.
Kuna uwezekano mkubwa watu wanaokuchukia wakatumia jina la Dr Slaa kukutishia maisha na hii ni ndani na nje ya chadema.
Mie binafsi sijawhi kukutana nawe ila tumeongea mara nyingi kwenye simu na ningekupa ushauri tu
Kila unalolisikia litilie maanani, kwa sababu tayari mtu kapakwa tope basi mwingine anaweza kuja kukumaliza halafu wakasema si mnakumbuka ilivyoandikwa before? Yale yalee ya afande mshutiii!

NA UKIONA SIMBA ANAKUKENULIA MENO USIDHANI ANAKUCHEKEA.
Wakati unaandika hapo juu ulikuwa unakunya.. Naona umetandaza hapo kinyesi!
 
Heshima ya Upande mmoja! Hapa Zitto utapongezwa kwakuwa tu 'umem-save' 'nabii' SLAA. Hawa hawa ndio wanaokuporomoshea matusi kila siku! Lengo lao wakutumie tu kama 'kile kifaa' kisha waku-dump! Sijui kama hulijui hili!
Wewe unawashwa na nini? Nenda JKT, kwa kujitolea.
 
Katika gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno ‘SIRI YA KUUWAWA ZITTO YAFICHUKA' na vichwa vidogo ‘yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini' dk. Slaa atajwa kumtuma Saanane kummaliza'.
Napenda kusema yafuatayo:

Pili, Siamini kamwe kuwa Katibu Mkuu wa chama changu anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo.
Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena. Kama mtu kaamua kuhama CHADEMA anapoteza haki ya kujadili masuala ya CHADEMA maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. CHADEMA sio pango la watesaji wala wauaji. Kama kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya CHADEMA anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki. Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi.

Kamanda Zitto,hongera sana kwa kauli ambayo inaendelea kuwaonyesha watanzania kuwa ni CDM ni moja.Watanzania bado tunakumbuka moto wa kambi rasmi ya upinzani bungeni.

ukiongozwa na Mh. Mbowe, Mnyika, Sugu, Mdee, Wenje,Lissu na wewe mwenyewe Mh. Zitto kwenye masuala mbali mbali yahusuyo Taifa letu. Tunawakumbusha wale wote wanaosubiri Dr. Slaa na Zitto wagombane watasubiri sana! M4C inasonga mbele,
 
Hata kama Zitto asingekana habari hiyo bado ningeamini ni uongo na uzushi. CDM imechafuliwa sana na jina la Zitto linarudiwa kutajwa lakini amekuwa kimya. Leo hii ndio umeona haya?
 
Muheshimiwa Zitto hapa ulikuwa unamaanisha nini! kama leo unadai huko CDM hakuna threat ya kukutoa uhai
quote_icon.png
By Zitto


..........Angalieni, wanaozungumzia sana usaliti waweza kuta ndio wasaliti wakubwa. wanazungumzia usaliti kama 'defensive mechanism'.
Tuacheni ujinga huu. Tufanye kazi. Kazi tu ndio kipimo cha ukamanda na sio kurambaramba visigino vya watu.

Mwisho, nasikia sikia sana habari za kuchinjana. Kuuana nk. Nasikia habari hizi kwa watu wale wale wa kikundi kile kile. Moja, natoka Kigoma. Nimeaga kwetu. Nitakufa kwa amri ya Mungu. Siogopi kufa. Iwapo kifo changu kitatokana na mkono wa mtu, sidhani kama kwa mtu huyo kama hata panya atabaki nyumbani kwao. Underline this.

 
Last edited by a moderator:
Unafanania na vigezo vya rais ninayemuota kila siku za maisha yangu!kama jana ingekua kesho,leo hii Zzk angekua rais wa tanzania kuptia chadema!
 
Back
Top Bottom