Siri ya Kuuwawa Zitto - UWONGO

Ukweli Zitto mm nakufagilia ile mbaya mdogo wangu. Niliisoma thread yako ya mkasa wa issue ya dini na kampeni zako kule vijijini jimboni kwako uliyoielekeza kwa speaker nikagundua kichwa yako iko vizuri. So man you call me at any time that we hav much to share anytime from now! Hope we need to talk! 0715314066
 
 
Chanzo cha habari hiyo kwenye gazeti la Mtanzania ni Juliana Shonza, ambaye amekuwa kipenzi cha wana CCM kwa maneno anayozungumza kuhusu chadema

Juliana Shonza: hatutakuamini tena uyasemayo.
Kama uliwahi kumuamini pole sana, sitalajii mtu makini kama wewe mpaka leo hii ulikuwa unasikiliza porojo za kitchen party za Juliana Shonza na huyu Mwampamba.

Ila kwa sababu Chadema inaonesha hakuna wagongaji wazuri sasa CCM ndio amefika siku si nyingi kitumbo mtakiona kimeshajibu maana mpaka sasa nadhani Mtela atakuwa ameshanyanganywa huo Mrupo na vijana machachari wa UVCCM.
 
Aibu yao clouds FM. Kina Kibonde wanavyoshabikia huo umbeya mpaka unaamua kuzima redio. kesho sijui watasemaje?
 
Msalimie Mzee bwana sijui na mimi utanitukana manake ni salamu tu nimekuomba unifikishie
 
Heshima ya Upande mmoja! Hapa Zitto utapongezwa kwakuwa tu 'umem-save' 'nabii' SLAA. Hawa hawa ndio wanaokuporomoshea matusi kila siku! Lengo lao wakutumie tu kama 'kile kifaa' kisha waku-dump! Sijui kama hulijui hili!

Wewe akili yako bado sana gamba limekuelemea. Fahamu kuwa cdm haiwezi kum-dump zito kwa kuwa ni mbunge halali aliyepigiwa kura na hao unaodhani watam-dump. Kama nyie magamba si wanafiki na mnampenda mbona mliweka mgombea wenu kwenye uchaguzi? Si mngemwacha zito "mnayempenda" apite bila kupingwa?
 

wenye akili zetu tumekusoma. naona mmeanza kujihami hata akitiwa hatiani muwe mmesepa.
cc kwa Mtela mwampamba, kilio cha usaliti.
 
Hili gazeti ningekuwa hata mtendaji wa kata tu ningekomaa lifungiwe.

Kwanza hawa mabindi na hawa wavulana ( maana inaonyesha hawajakuwa), wanastahili wafikishwe mahakamani kwa kula njama ya kuona maisha ya ZITO yanahatarishwa kwa sumu na kisha wakakaa kimya-Ujinga huu nyie mabinti na wavulana mliofukuzwa CDM mkome.
 
heko sana mkuu,umefanya jambo la busara sana kutokea na kusema ukweli.
Sasa naanza kuiona CDM mpya,yenye nguvu,mshikamano na umoja ikianza kujengwa kwa kasi kubwa sana, na kwa mtindo huu uliofanywa nawe kamanda, naomba wale wote wenye chuki binafsi dhidi ya mtu au kiongozi ndani ya CDM waweke pembeni chuki zao na tukijenge chama kwa ajili ya ukombozi wa kweli wa mtanzania. Ningependa kuona huu kuwa mwisho wa malumbano baina ya mtu na mtu ndani ya CDM. Mungu akubariki sana kamanda ZZK,Mungu ibariki CDM, Mungu wabariki watanzania waondokane na utawala dhalimu wa magamba.
 
Mara nyingi wanasiasa huwa hawaishii kukanusha tu,bali huiwasisitizia gazeti husika wakanushe la sivyo watawashitaki mahakamani.

Kukanusha ni hatua nzuri tu,however kuna mengine alishawahi kusema humu kuhusiana na issue ya "kutaka kuuwawa".

Kwa namna flani siasa za bongo ni kama mambo ya "abra kadabra","now you see it,now you dont"
 
Chadema imetoa msaada wa wanasheria ili kuhakikisha kuwa anatendewa haki.

Tusubiri kwanza ithibitike kuwa video ile ni authentic ndiyo tuwaulize kuhusu hatua za kuchukua.

Only if kama una nia nzuri na mageuzi nchini.
 
I bet the movie has just began bro,you have given it out clearly to him....yetu macho na masikio.
 
Josephine Mushumbusi ID yake ni Josephine. Huyu Josephine03 ni mtu mwingine.
Are you sure of this,Kama zote ni zake je?mimi sioni Kama ni issue this is a free forum for great thinkers she is so free to use any Id na kuchangia atakavyo mahusiano yake hayawezi kumkataza kuchangia kma watu wengine wanavyodai.
 

na wasiwasi sana na wewe,ni swala la muda tu,ngoja tusubiri.
wanaowatumia leo,hawatawatumia kesho
kwanini msifanye kazi halali,kuliko kutumika,hii si kazi halali.
 
Msalimie Mzee bwana sijui na mimi utanitukana manake ni salamu tu nimekuomba unifikishie

Ukikimbizana na kichaa aliyeiba nguo zako ukiwa unaoga.......................Utaumia sana lakini ndo imekuwa tena
 
Zitto: CHADEMA si pango la wauaji

• ASEMA HAAMINI KAMA DK. SLAA ANAWEZA KUMUUA

na Waandishi wetu




SIKU moja baada ya gazeti la Mtanzania kuandika habari likidai kuwa siri ya kumuua Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA) imefichuka, kiongozi huyo amejitokeza akisema ni uzushi.

Habari hiyo ilidai kuwa ilipangwa Zitto anyweshwe sumu hotelini na kumtaja Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa kuwa ndiye alimtuma kijana Ben Saanane kutimiza mkakati huo.

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa kisiasa walisema habari hiyo inayodai tukio hilo lilitokea Mei mwaka jana jijini Dar es Salaam, ilikuwa ni propaganda ya kuhamisha mjadala wa sakata la kuteswa na kuumizwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Absalom Kibanda.

Kibanda alitendewa unyama huo Machi 6 mwaka huu, lakini hadi leo vyombo vya dola vimeshindwa kuwakamata wahusika na badala yake yamekuwa yakiibuliwa matukio mbalimbali ili kupoteza ajenda hiyo inayoonesha udhaifu wa kiutendaji wa vyombo hivyo.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Zitto alisema habari hiyo imemletea usumbufu mkubwa kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wake wamejawa na wasiwasi kwamba anaweza kuuawa.

“Moja, sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi,” alisema.

Alifafanua kuwa haijawahi kutokea yeye kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika.

“Pili, siamini kamwe kuwa Katibu Mkuu wa chama changu (Dk. Slaa) anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo. Napenda kurudia kusema kwamba mimi ninaamini kuwa kila nafsi itaonja mauti.

“Kila mtu atakufa. Kama nitakufa kwa kuuawa na mtu mwingine ndiyo itakuwa nimeandikiwa hivyo na Mungu. Ndiyo maana hata siku moja silalamiki kuhusu vitisho vya kuuawa. Kama kuna mtu anafikiria kuwa kumuua Zitto ndiyo furaha ya maisha yake atakuwa anajidanganya tu maana Zitto anaweza kufa kimwili, lakini mawazo, fikra na maono yake yataishi tu,” alisema.

Aliongeza kuwa haogopi kufa maana maisha aliyoyachagua ndiyo haya ambayo yamejaa vitisho, kwamba muhimu kwake ni kufanya kazi zake kwa bidii, uhodari na uaminifu.

“Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena.

“Kama mtu kaamua kuhama CHADEMA anapoteza haki ya kujadili masuala ya CHADEMA, maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa,” alionya Zitto.

Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA (Bara), alisema chama hicho si pango la watesaji wala wauaji, kwamba kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya CHADEMA anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki.

“Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi. Nne, Nawashauri viongozi wa CHADEMA na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama,” alisema.

Saanane ang’aka

Naye Saanane aliyedaiwa na gezeti hilo kuwa ndiye alikuwa ametumwa kumdhuru Zitto, alisema amesikitishwa jinsi lilivyoshiriki katika dhamira nzima ya kumchafua.

Akizungumza katika ofisi za Tanzania Daima jana, Saanane ambaye ni mjumbe wa Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) alisema kutokana na habari hiyo ameamua kukutana na wanasheria wake kuangalia hatua za kuchukua ili ukweli ubainike.

“Nasisitiza sijawahi kupanga kumuua mtu yeyote, sijawahi kutumwa kumuua Zitto Kabwe. Nimesikitishwa kuona chombo cha habari kikitumika kwa maslahi binafsi ya kuchafua watu kisiasa,” alisema.

Aliongeza kuwa mara zote alizokutana na Zitto, hawajawahi kufika katika Hoteli ya Lunch Time wakiwa pamoja kama ilivyoelezwa katika gazeti hilo.

Hayo ndo majibu ya Mhe Zitto na Saanane kwa hiyo tafadhalini chambueni matatizo yenu badala ya kupoteza lengo la kumpata aliempiga Kibanda
 
heshima ya upande mmoja! Hapa zitto utapongezwa kwakuwa tu 'umem-save' 'nabii' slaa. Hawa hawa ndio wanaokuporomoshea matusi kila siku! Lengo lao wakutumie tu kama 'kile kifaa' kisha waku-dump! Sijui kama hulijui hili!

omba assignment nyingine, kwa leo zzk amewatibulia...
 

Vipi unataka ahamie CCM nini?,kila siku mnaambiwa CDM sio mtu lakini vichwa vyenu vimejaa maji hamuelewi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…