we mzalendokweli, siku hizi inaruhusiwa hapa jf kuibiana avatar!??Before I was like; if Zitto is as bright as many think he is,he shld say something about what Mtanzania wrotte....there you go.
Respect.
Heshima ya Upande mmoja! Hapa Zitto utapongezwa kwakuwa tu 'umem-save' 'nabii' SLAA. Hawa hawa ndio wanaokuporomoshea matusi kila siku! Lengo lao wakutumie tu kama 'kile kifaa' kisha waku-dump! Sijui kama hulijui hili!
Katika gazeti la Mtanzania toleo na. 7269 la Jumatano Machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno SIRI YA KUUWAWA ZITTO YAFICHUKA na vichwa vidogo yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini dk. Slaa atajwa kumtuma Saanane kummaliza. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa.
Napenda kusema yafuatayo:
Moja, sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa Ben Saanane na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa Hoteli ya Lunch Time ambayo sio tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi kufanya kikao cha pamoja na Ben Saanane, Juliana Shonza na Mtela Mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.
Pili, Siamini kamwe kuwa Katibu Mkuu wa chama changu anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo. Napenda kurudia kusema kwamba mimi ninaamini kuwa kila nafsi itaonja mauti. Kila mtu atakufa. Kama nitakufa kwa kuuwawa na mtu mwingine ndio itakuwa nimeandikiwa hivyo na Mungu. Ndio maana hata siku moja silalamiki kuhusu vitisho vya kuuwawa nk. Kama kuna mtu anafikiria kuwa kumuua Zitto ndio furaha ya maisha yake atakuwa anajidanganya tu maana Zitto anaweza kufa kimwili lakini mawazo, fikra na maono ya Zitto yataishi tu. Siogopi kufa maana maisha niliyoyachagua ndio haya ambayo yamejaa vitisho. Muhimu kwangu ni kufanya kazi zangu kwa bidii, uhodari na uaminifu. Siku zote nitasimamia ukweli bila kujali uchungu wa ukweli huo.
Tatu, nawashauri watu ambao wamehama CHADEMA na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena. Kama mtu kaamua kuhama CHADEMA anapoteza haki ya kujadili masuala ya CHADEMA maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. CHADEMA sio pango la watesaji wala wauaji. Kama kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya CHADEMA anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki. Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi.
Nne, Nawashauri viongozi wenzangu wa CHADEMA na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama. Chama chetu lazima kiwe mfano bora wa kuheshimu demokrasia na haki za binaadamu. Wananchi hawawezi kutoa dola kwa chama chenye mifarakano. Tusiruhusu kugawanywa kwa matakwa ya watu wachache. Tusimamie misingi ya kuanzishwa chama chetu.
mjomba life is not a rehersal is a performance nimefurahishwa sana na hii paragraph ya nne!!!!!!!umemaliza kila kitu ccm mijinga mijinga tu.katika gazeti la mtanzania toleo na. 7269 la jumatano machi 27, 2013 kuna habari yenye kichwa chenye maneno siri ya kuuwawa zitto yafichuka na vichwa vidogo yadaiwa ilipangwa anyweshwe sumu hotelini dk. Slaa atajwa kumtuma saanane kummaliza. Habari hii imeniletea usumbufu mkubwa kwani ndugu, jamaa, marafiki na wapiga kura wangu, wamejazwa na wasiwasi mkubwa sana kwamba ninaweza kuuwawa.
Napenda kusema yafuatayo:
Moja, sijawahi katika maisha yangu yote kukutana na mtu anayeitwa ben saanane na hivyo hicho kikao ambacho inasemekana nilikuwa naye na akajaribu kunipa sumu hakijawahi kutokea. Imetajwa hoteli ya lunch time ambayo sio tu sijawahi kufika, pia hata siijui ipo wapi. Haijawahi kutokea mimi kufanya kikao cha pamoja na ben saanane, juliana shonza na mtela mwampamba. Hivyo habari iliyoandikwa ni ya kufikirika na hivyo naomba mwandishi ahakikishe kuwa vyanzo vyake vya habari vimempa habari sahihi.
Pili, siamini kamwe kuwa katibu mkuu wa chama changu anaweza kupanga kuniua maana hana sababu ya kufanya hivyo. Napenda kurudia kusema kwamba mimi ninaamini kuwa kila nafsi itaonja mauti. Kila mtu atakufa. Kama nitakufa kwa kuuwawa na mtu mwingine ndio itakuwa nimeandikiwa hivyo na mungu. Ndio maana hata siku moja silalamiki kuhusu vitisho vya kuuwawa nk. Kama kuna mtu anafikiria kuwa kumuua zitto ndio furaha ya maisha yake atakuwa anajidanganya tu maana zitto anaweza kufa kimwili lakini mawazo, fikra na maono ya zitto yataishi tu. Siogopi kufa maana maisha niliyoyachagua ndio haya ambayo yamejaa vitisho. Muhimu kwangu ni kufanya kazi zangu kwa bidii, uhodari na uaminifu. Siku zote nitasimamia ukweli bila kujali uchungu wa ukweli huo.
Tatu, nawashauri watu ambao wamehama chadema na kuhamia vyama vingine watumie muda wao kujenga vyama vyao badala ya kila siku kuzungumzia masuala ya chama ambacho wao sio wanachama tena. Kama mtu kaamua kuhama chadema anapoteza haki ya kujadili masuala ya chadema maana kama angekuwa anapenda kuyajadili asingehama. Naonya mtu yeyote ambaye anatumia jina langu ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. Chadema sio pango la watesaji wala wauaji. Kama kuna mwanachama wa chama kingine cha siasa anayedhani kuna mtu ndani ya chadema anapanga mipango ovu aende kwenye vyombo vya sheria kumshtaki. Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi.
nne, nawashauri viongozi wenzangu wa chadema na hasa wanachama tutumie muda wetu kujenga mshikamano ndani ya chama. Fitna, majungu, uongo, uzandiki nk kamwe havijengi chama. Chama chetu lazima kiwe mfano bora wa kuheshimu demokrasia na haki za binaadamu. Wananchi hawawezi kutoa dola kwa chama chenye mifarakano. Tusiruhusu kugawanywa kwa matakwa ya watu wachache. Tusimamie misingi ya kuanzishwa chama chetu.
Hakuna mwana chadema anayependa zitto afe ila wanataka mikono ya ccm inayomuelekea zitto ikatiliwe mbali ..Well said,
Msimamo wa Mheshimiwa huyu toka enzi hizo pale Rev square umebaki vilevile. sijaona mabadiliko. He believes in himself. Kama ni kufa basi DUA NYINGI za wana CDM zingeshamuua. Tuseme Ukweli na wala sio kuwa ni wa CCM tu wanaomchukia. Nadhani katika ratio CDM 7 CCM 3 ambao wangependa Zito afe. Kweli au si kweli???
Lakini kwa taarifa yenu Zitto hatokufa mpaka amri ya Mungu itakapofika.
Big up MZALENDO ZITTO. Dua zangu kwako. Mungu akuepushe na mahasidi na wafitini. Nyota yako ing'are Duniani hata Mbinguni. Alilolipanga Mungu kwako liwe kama ndoto zako zilivyo.
mtu yeyote anayechukia ccm huyo ni rafiki yangu....Hivi ni nani yule aliimba: kumbe CCM waongo, au nilikuwa naota? Nayachukia haya maCCM.
Kuna kauli moja ya kifalsafa inasema hivi; ''wapo wale wawazao mema kuanzia nafsini mwao hadi kwenye jamii yao, hawa huitwa wenye hekima ila kuna wale wawazao njama, visa,chuki, machafuko na hata vita,hawa tunawaita washenzi''. Mh. ZZK umeonesha nia ya dhati kuanzia nafsini mwako kwamba we si mtu wa kuyumbishwa na political assassination propaganda tunakuombea uendelee na moto huo ili maadui tuwaone kama rafiki japo tunaijua tahadhari ya unafki wao. Big up.
Juliana na kundi lako umesikia wosia wa Zitto kabwe? maana nyie kutwa nzima mpo JK kuchafua hali ya hewa hivi mnapata muda hata wa kupitia ilani yenu ya CCM na kuielewa? hivi hiyo mlivyofundishwa kwamba kwenye siasa mchafue mwenzako? tumewachoka.
Yaani ni sawa Unampa taraka mkeo au mumeo lakini kutwa kucha unaongelea ubaya wake, mwenye akili timamu lazima atagundua kuwa wewe u zuzu.
Asante Zitto kutuweka sawa kwa hili, ila umeniacha njia panda kwenye sentensi hii "Matendo ya mtu mmoja yasifanyiwe propaganda kama ni malengo ya taasisi." nitaomba ufafanuzi wako kama una muda.
Otherwise nakubaliana na wewe kwamba CDM kipo imara na kitavuka hiki kikwazo cha mwisho kuelekea ukombozi wa kweli wa taifa hili.
Ben saanane is typing.............
Mkuu ni kweli hakuna mtu asiyeshauriwa lakini ushauri unatolewa pale mtu anapotaka ushauri, halafu pia kuna taratibu zake. sidhani kama Invisible ametaka huo ushauri.Hajamsfundisha bali amemshauri. Hakuna mtu asiyeshauriwa, huenda wewe utakuwa wa kwanza. Hata rais ana rundo la washauri.