Siri inayofichwa kwenye "Yoni Detox" na miungu ya Kike

Siri inayofichwa kwenye "Yoni Detox" na miungu ya Kike

OgaBoy

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2022
Posts
3,167
Reaction score
4,481
CC: Mshana Jr

TUFUNDISHE ZAIDI

Wimbi la mafunzo yanayoitwa ya "asili" yakilenga wanawake, Kwa kutumia maneno kama Yoni Healing, Womb Health, au Kundalini. Ingawa yanaonekana kama ni mazoezi ya kawaida au afya, ndani yake kuna mambo mazito unayopaswa kuyajua kabla hujaingia.

1. Mtego wa Kiroho (Nguvu za Giza)​

Mafundisho HAYA mara nyingi hutumia neno "Goddess" (Mungu mke). Hili si neno kama sifa; ni mlango unaomfanya mwanamke aanze kujiabudu mwenyewe au kuabudu miungu mingine.

  • Kundalini: Wanaposema "activation," kimsingi wanazungumzia kuamsha nguvu ya kiroho inayofananishwa na nyoka (serpent power). Kwa mtu anayemwamini Mungu wa kweli, haya ni matambiko ya kualika roho ngeni mwilini mwako kupitia "meditation."

2. Udanganyifu wa "Yoni Detox"​

Kibaolojia, uke (yoni) hauhitaji "detox" ya nje, mvuke (steaming), wala dawa za kuingiza ndani ili kusafisha.

  • Sayansi inasemaje? Uke una mfumo wake wa asili wa kujisafisha. Kuingiza vitu vya "asili" au kufanya matambiko ya "sisterhood" kwenye viungo hivyo kunaweza kusababisha maambukizi (infections) na kuharibu mfumo wako wa uzazi.

3. Siri ya Lugha ya "Asili"​

Watu wasiomwamini Mungu wa kweli hupenda kupamba mambo yao kwa neno "Asili" (Nature). Wanakuambia ni nguvu za asili ili usishtuke kuwa ni ushirikina. Ni rahisi mtu kukubali kitu akiamini ni "asili" kuliko akiambiwa ni "nguvu za giza."

Usidanganyike na picha nzuri za Yoga au maneno matamu. Afya ya mwanamke inatunzwa kwa ushauri wa kitaalamu wa madaktari na amani ya kweli inatoka kwa Mungu pekee, si kwa kufanya matambiko ya siri.

Kuwa mwangalifu na unachokikaribisha kwenye mwill WAKO.

Checki huyu dada aiizungumza mafundisho hayo.





View: https://www.instagram.com/reel/DUTo2oED_PM/?igsh=eHlvM2xxanRjemhy
 
Nlimekuelewa shahidi WA Yehova WA zamani now a so called non believer😄
Humo kanisani mnajazanaga ujinga bila hata uelewa wa jambo , yoga ni mazoezi ya kawaida tu , ila kunawatu wanayafanya wanaongezea na imani zao ,jambo ambalo ni haki yao tu.

Hizo mambo za kwako za Mungu wa kweli ni ego zenu za kiimani tu.
 
Humo kanisani mnajazanaga ujinga bila hata uelewa wa jambo , yoga ni mazoezi ya kawaida tu , ila kunawatu wanayafanya wanaongezea na imani zao ,jambo ambalo ni haki yao tu.

Hizo mambo za kwako za Mungu wa kweli ni ego zenu za kiimani tu.
I expected this🤣
 
Back
Top Bottom