Hili kundi lililoua watu wakisali sidhani hata kama wanaujua uislamu vizuri, kwahiyo wao walitaka wenzao wasisali ili waenda tu kushinda Polisi mpaka wenzao watolewe?
Kwa uislamu salaa inaweza kuachwa na mtoto mdogo,Mwenye matatizo ya akili,mwanamke anapokua kwenye siku zake (coz mwili unakua sio msafi) huwezi kuacha kusali kisa wenzenu wamefungwa!!
Unapofika wakati wa salaa ni lazima kusali, hata kama utakua unazama baharini ila unapofika muda wa salaa utasali japo kifikra bila vitendo kama vile kusujudu n.k na Mungu anakukubalia tu salaa yako,huwezi kuua wenzako eti kisa wanasali,
Wanajuaje hapo kwenye sala zao pengine hao waliowaua pia walikua wanamuomba Mungu awasaidie wenzao ili watoke jela kwa amani? Tusihukumu uislamu wote kwa vitendo vya vikundi fulani tuu,
Amani ni kitu cha thamani sana na ikipotea ni ngumu sana kuirudisha,tudumishe amani na tuungane wote kulaani hicho kitendo cha watu walio uawa bila hatia,
Mungu azilaze mahala pema peponi roho za marehemu wote...Amin