mi naona tuwaache watu wafanye wanayoona ni sawa maana kitu kisipokuwa sawa kwa wote hakiachi kuwa sawa.
Basi na wewe niache na mie nitoe maoni yangu, ni wapi nimemlazimisha afanye asichotaka? Nimeweka arguments zangu mezani, ziponde kama zilivyo.
hizi habari za haki haki wakati mwingine hazina maana.
Sijui unaposema hizi haki hazima maana unakuwa unamaanisha nini? Kwa nini mtu akiua mwanae anafungwa? Au akitelekeza kichanga ama kutoa mimba? Si mwanae bana, what do you care, labda hana uwezo wa kumtuza.
watu wengi hapa wameonyesha walijaribu kutekeleza huo wajibu wa kuwataarifu wazazi wenzao juu ya watoto lakini walichoambulia ni maumivu tu. baba hataki kumtambua mtoto lakini mama bado anang'ang'ana kumtambulisha japo kwa ndugu wa baba. haki ya mtoto kufahamu mzazi. nilishawahi kutoa mfano wa ukweli hapa juu ya binti aliyeamua kumtafuta babaye ukubwani baada ya kufichwa na mamake. yaliyomkuta yule binti hatakaa asahau. aliponea kubakwa na babake siku ya kwanza tu waliyoonana. Inawezekana kabisa mama alijua amezaa na kichaa wa ngono - si ajabu naye alibakwa. Hatujui yanayoendelea kwenye vichwa vya watu, ikiwezekana tuwaache tu.
Kwa hiyo, huyu mtoto anyimwe haki yake kwa kuhofia yaliyotokea kwa wengine? Yaani sababu mtoto mmoja alitaka kubakwa na baba yake, basi kila mwanamke akizaa aogope kumjulisha baba mtoto kwa kuhofia atambaka? Does not make any sense to me.
Kumtaarifu baba mtoto ni A, mama kuumizwa na majibu ya baba mtoto ni B, havina uhusiano.
Halafu unavyodai ni haki ya mtoto kufahamu wazazi wake mbona kule juu ulimponda mama anayedai haki ya matunzo ya mtoto mpaka mahakamani kwa kusema malezi si material tu??? Kwa hiyo mzazi wa kiume ana haki ya kumjua mwanae ila ana uchaguzi wa kulea au kuacha?
Kumjulisha baba existance ya mtoto ni A, baba mtoto kukataa kulea ni B, havihusiani.
Nilimponda kwa sababu alitaka kujua haki zake kisheria, wakati huo huo hakuwa ameweka wazi madai anayotaka kusaidiwa ni yapi na hakuwa ameweka wazi kama yeye ni mke halali ama lah. Sasa hapo asaidiweje?
Lakini pia nilikuwa najaribu kumuonesha vita anayotaka kuipigana ina tija? Uhangaike na kesi RITA weee, afu unapewa 50K kwa mwezi? Si bora huo muda utumie kuchoma vitumbua.