Simulizi za polisi kuua gaidi Arusha

Simulizi za polisi kuua gaidi Arusha

Juni 15 mwaka 2013 saa 11:50 jioni
katika viwanja vya Soweto, kata ya
Kaloleni, jijini Arusha na wenzake,
wanadaiwa kurusha bomu na kuua watu
wanne, kujeruhi 60.
Polisi hivi hamna Mungu yaani hata tukio mlilofanya nyie mnamsingizia walimu wa judo wa waislam mgesema tu mmemuua kwa kosa la kufundisha judo na kareti jamii pengine ingewaelewa soweto tulishambuliwa kwa mabomu, smg na bastola leo mnataka kuwadanganya watu...pumbavu zenu siku video ikiwekwa wazi mjiandae kuficha sura zenu uvunguni kwa matendo haya naanza kuamini pengine hata kanisani polisi ndiyo walirusha lile bomu...
 
Sinaipenda wala kuiamini hii taarifa. Bora angesema "kwa sasa hatuwezi kuongelelea swala hili" kwanini apigwe risasi mtu mwenye pingu?
Kwa nini asafirishwe kwa staili hio?
Kwa nini hajazungumzia hata kidogo nia au makusudi hayo mashambulio?
Kwa nini mtu mmoja anaweza kuwa kichwa cha mashambulio ambayo hayaonekani kuwa na uhusiano? Mfano kushambulia makanisa na maeneo ya starehe kwa ujumla na kiongozi mmojammoja wa kiislamu. Bado sidhani kama ni mtu au kundi moja lenye nia moja.
 
Nimeamini watanzania ni Watu rahisi sana kuwaendesha hata kwa uongo mdogo tu. Kwa kuwa ni roho ya mtu mmoja basi tutadharau . Ila hapa naona kabisa UONGO na Watu wataupokea na kusahau kesho wengine wauwawe. Napenda kusema uislamu umejeruhiwa hapa. Kwa kuwa hakuna atakayefuatilia Nawaomba waislamu wavalie njuga Suala hili kwani litaendelea kuwaandama na wengine watauwawa kama hivi. Tutaambiwa hiki objectively tuache ushabiki. Mimi Si mwislamu LAKINI naona na kuelewa kinachoendelea.
 

Liberatus-Sabas--Agust8-2014%281%29%281%29.jpg

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas

Mkazi wa Mianzini, jijini Arusha, Yahaya Sendei (31), anayedaiwa kuwa kiongozi wa watuhumiwa ulipuaji mabomu nchini na umwagiaji tindikali watu, ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi wakati akidaiwa kujaribu kuruka kwenye gari lao kwa lengo la kutoroka.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas (pichani), jana alisema kuwa mtuhumiwa huyo aliuawa juzi saa 5:30 usiku katika barabara ya Arusha- Babati eneo la Kisongo, wilayani Monduli, wakati wakimpeleka kijijini alikozaliwa Chemchem, wilaya ya Kondoa, mkoa Dodoma, kuwaonyesha askari bomu jingine aliloficha.

Alidai kuwa, mtuhumiwa huyo ambaye inadaiwa wakati wa uhai wake alikuwa mwalimu wa karate na judo ni mwasisi na kinara wa matukio ya ugaidi yaliyotokea jijini Arusha, Zanzibar, Mwanza na Dar es Salaam.

“Huyu tulimpata kutokana na intelejensia imara ya polisi ya kisasa na ya hali ya juu na tulimkamata mkoani Morogoro Oktoba 6, mwaka huu na kusafirishwa Oktoba 11 mwaka huu kuletwa Arusha na alipohojiwa alikiri kuhusika na kuratibu matukio ya ugaidi na alikuwa akijificha kwenye nyumba tofauti na porini, ” alisema kamanda huyo.

Alidai mtuhumiwa huyo alipigwa risasi kwenye mguu wa kulia na kalio la kulia alipojaribu kutumia uzoefu wake wa kuruka judo na kupiga karate kutaka kuwazidi polisi ili atoroke na kwamba alifia njiani wakati akipelekwa Hospitali ya Mkoa wa Arusha ya Mount Meru kwa matibabu.

Hata hivyo, hakueleza sababu za kumpiga risasi mtuhumiwa huyo ambaye hakuwa na silaha yoyote na kama alijeruhi askari yeyote zaidi ya kudai kuwa maiti yake imehifadhiwa hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi na kusubiri ndugu kuichukua kwa maziko.
Vile vile Kamanda Sabas hakueleza kama hatua ya kuuawa kwa mtuhumiwa huyo muhimu itawakosesha polisi taarifa muhimu katika mchakato wa upelelezi wao.

Awali Kamanda huyo alitaja baadhi ya matukio ambayo mtuhumiwa huyo inadaiwa alikiri kuhusika nayo kuwa ni la Oktoba 25 mwaka 2012 lililotokea saa 5:30 usiku katika mtaa wa Kanisani Paloti, kata ya Sokoini One, jijini Arusha.

Katika tukio hilo, yeye na wenzake inadaiwa walitega bomu kwenye chumba cha Sheikh Abdulkarim Idd Jonjo (52) nyumbani kwake na kumjeruhi baada ya kulipuka.
Inadaiwa tukio la pili na wenzake ambao wamefikishwa mahakamani, lilitokea Mei 5 mwaka jana saa 10:30 maeneo ya Kanisa la Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi lililopo Olasiti jijini Arusha.

Katika tukio hilo inadaiwa kuwa aliratibu kurushwa kwa bomu na kusababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi 56.

Juni 15 mwaka 2013 saa 11:50 jioni katika viwanja vya Soweto, kata ya Kaloleni, jijini Arusha na wenzake, wanadaiwa kurusha bomu na kuua watu wanne, kujeruhi 60.
Julai 11 mwaka 2013 saa 5:00 eneo la Kwa Mrombo, jijini Arusha na wenzake wanadaiwa walimwagia tindikali usoni Sheikh Said Juma Makamba.

Februari 12 mwaka 2014 saa 3:45 katika eneo la Tindigani, Unga Ltd, jijini humo, kwenye msikiti wa Sawiyatu Qadiria, wanadaiwa kumwagia tindikali usoni Sheikh Hassan Bashir.
Februari 28 mwaka 2014 saa 5:15 alfajiri katika msikiti wa Bondeni, wanadaiwa kumwagia tindikali Mistapha Mohamed Kiago na kumjeruhi usoni na shingoni.

Aprili 13 mwaka 2014 saa 1:30 usiku, eneo la Mianzini kwenye nyumba ya wageni na Baa ya Niht Park, wanadaiwa walirusha bomu na kujeruhi watu 11 na kusababisha kifo cha mmoja.
Aprili 13 mwaka 2014 la saa 5:00 katika eneo la Majengo, jijini Arusha, anadaiwa alirusha bomu kwa kushirikiana na wenzake na kuwajeruhi watu wawili Sudi Ali Sudi (37) ambaye ni Mkurugenzi wa Answar Muslim Kanda ya Kaskazini na mwenzake Muhaji Hussein Kifea (38), mkazi wa Dar es Salaam. Julai 7 mwaka huu, saa 4:15 usiku eneo la
Uzunguni, mgahawa wa Vama Traditional Indian, uliopo jirani na Viwanja vya Gymkhana, wanadaiwa walirusha bomu na kujeruhi watu wanane.

Kamanda huyo polisi alisema wanaendelea kuwasaka watuhumiwa wengine wanaojihusisha na kikundi hicho ambacho mtuhumiwa huyo alikiri kuendesha mafunzo ya karate na judo kwenye baadhi ya misikiti jijini Arusha.

Hata hivyo, alisema vikundi hivyo vimesambaratishwa na polisi.
Alitoa wito kwa wananchi kutoa taarifa polisi ili kuendelea kudumisha amani jijini Arusha na maeneo mengine ya nchini.

“Hawa watu hawakuwa wanafadhiliwa nje ya nchi ila walikuwa wanajifadhili wenyewe na kwa faida zao wenyewe” alisema Kamanda Sabas.

CHANZO: NIPASHE


Bila shaka wale waliotubisha sana kwamba baadhi ya misikiti hapa Dar es Salaam kuna mafunzo ya karate yenye kuashiria mafunzo kigaidi kutokana na mafunzo hayo kuambatana na matumizi ya majambia na morali wanayopewa kufanya mauaji dhidi ya wakristo. Haya yote ni utekelezaji wa maelekezo ya Sheikh Ilunga alipowaasa vijana wa kiislam kuwaua Wakristo hususani Maaskofu na Mapadre kama tulivyoona matukio kule Zanzibar, Arusha na Dar ni matokeo ya mahubiri ya chuki ya dini yanayotolewa na baadhi ya waislam. Tunaitaka serikali isiwe inapuuzia taarifa zinazotolewa raia wema kuhusu mafunzo ya kigaidi ndani ya misikiti kwa mfano msikiti mmoja Vingunguti, chuo kimoja ndani ya kisiwa cha Ukerewe ambako tulielezwa kuwa wahusika hata walifikia hata kupiga marufuku dala dala kupiga nyimbo za Kikristo. Sisi Wakristo tunathamini sana michango mbalimbali inayotolewa na waislam wenye mapenzi mema.
 
Sasa kama walikuwa hawafadhiliwi na waliku wanajifadhili! Ilikuwaje wamiliki mabomu ya kijeshi?

Na Je! ni kwanini wafanye mashambulizi katika mazingira tofauti yasiyo na uhusiano kabisa kama:
  • Kushambulia makanisa?
  • Kushambulia mikutano ya siasa?
  • Kuwashambulia mashehe?
  • kushambulia kumbi za starehe?
Huyu Liberatus Sabas atueleze kuwa huyo marehemu na kikundi chake kilikuwa kuina entrance gani katika uhalifu wao.?

Kama ndiyo waliohusika katika mkutano wa Chadema kutupa bomu basi CDM ishitakiwe. Hapa nadhani Jeshi la Polisi linatumika kisiasa tu.
 
Swali ni je alichokisema kamanda Sabas ni kweli au ameudangaya umma?amesema huyu jamaa alikua anakimbia ,lakini ukiangalia amepigwa risasi na mtu aliyekua mbele yake
Alisema amepigwa kiunoni ni kweli hapo ni kiunoni?

dada...
huo ni upande risasi ilikotokea na sio ilikoingilia. hujui jeraha la risasi lilivyo so will you please shut up your fuc.... mouth!!!!!
 
CHADEMA itakapoingia madarakani kazi ya kwanza ni kulivunja jeshi la police na kuliunda upya
 
Bila shaka wale waliotubisha sana kwamba baadhi ya misikiti hapa Dar es Salaam kuna mafunzo ya karate yenye kuashiria mafunzo kigaidi kutokana na mafunzo hayo kuambatana na matumizi ya majambia na morali wanayopewa kufanya mauaji dhidi ya wakristo. Haya yote ni utekelezaji wa maelekezo ya Sheikh Ilunga alipowaasa vijana wa kiislam kuwaua Wakristo hususani Maaskofu na Mapadre kama tulivyoona matukio kule Zanzibar, Arusha na Dar ni matokeo ya mahubiri ya chuki ya dini yanayotolewa na baadhi ya waislam. Tunaitaka serikali isiwe inapuuzia taarifa zinazotolewa raia wema kuhusu mafunzo ya kigaidi ndani ya misikiti kwa mfano msikiti mmoja Vingunguti, chuo kimoja ndani ya kisiwa cha Ukerewe ambako tulielezwa kuwa wahusika hata walifikia hata kupiga marufuku dala dala kupiga nyimbo za Kikristo. Sisi Wakristo tunathamini sana michango mbalimbali inayotolewa na waislam wenye mapenzi mema.

Na Masheikh waliyomwagiwa tindikali hujazungumzia vp nao?usikurupuke
 
Habari za polisi ni ngumu sana kuaminika. Tangu walipotoka kwenye job description yao ya kikatiba na kufata ya kimatamko matatizo ndo haya.
 
Is Tanzania Police Force licensed to kill?!

“Huyu tulimpata kutokana na intelejensia imara ya polisi ya kisasa na ya hali ya juu Beside, hii kauli inapingana kabisa na mlolongo wa matukio yaliyoorodheshwa kufanywa na mtuhumiwa, kwa kuwa kama kauli hii ingekuwa kweli basi yasingekuwa mengi kiasi hicho.
 
Magazeti yetu huwa na wahariri kweli?
Mengi naona kama siasa tu!
 
Ila kiukweli polisi wanapiga kazi hasa inapotokea hali inayotishia amani kwa raia. Wote mmekwenda shule na mnafahamu nini utafiti. Na binafsi naamini wote waliosalia watakamatwa ila tu wasijaribu kutoroka. Au wajisalimishe na mabomu yao haramu
 
kama kuna mtu atkaye amin maelezo ya kamanda sabas, basi mtu huyo ataamini kila kitu hapa duniani, including hata kamanda sabas akimwambia mtu huyo kwamba mimi ndiyo masiah yesu kiristu niamini mtu wa aina hiyo ataamini na kumfuata.

Kweli jeshi la polisi limejaa akina kova wengi! (ref kesi ya mulundi/gwajima/dr. Ulimboka)

nashindwa kuelewa jukumu la polisi ni nini, pamoja na kuua, kuwa mahakama? Tanzania iko kwenye hari ya hatari kiasi mtu akiuwawa mahakama haziusiki?
 
Yaani waananchi wangeni bhana hawana shukrani kweli ni matukio mangapi ya Uhalifu na watu kumwagiwa tindikali yametokea huku arusha Leo jeshi LA polisi linakamata mhalifu watu wanamtetea inashangaza sana polisi wasipo kamata watu wanalalamika eti kwamba jeshi LA polisi halifanyi kazi wakikamata watu wanatetea wahalifu hivi nyie binadamu gani? Jeshi LA polisi linapaswa kupongezwa kwa kazi walioifanya hongera sana pt endeleeeni hivyo hivyo sisi humu katika mitandao tunawasaidia tunawaungamkono msichoke kwani humu wengine ni kama hao mliowakamata yaani wahalifu wanatumia mitandao ya kijamii kuwarudisha nyuma nasema tens hongereni polisi kwa kazi nzuri. Watu wamesahau matendo ya ugaidi Leo Hi wanawaunga mkono kweli ubinadamu kaxi.
 
Yaani watu mnatetea magaidi kweli? Licha ya matukio ya Uhalifu, watu kumwagiwa tindikali yaliyotokea mnatetea mhalifu aliyekamatwa na polisi? Mi nadhani nanyi mtakuwa wahalifu tu sio watu WA kawaida . polisi wanapaswa kupongezwa na kutiwa moyo kwa kazi nzuri hongera sana polisi Mimi nakupongeza kwa kuwa Mimi si mhalifu hongera polisi hongereni vijana WA mangu.
 
binafsi ni mwananchi wa hali ya chini na miongoni mwa waoga wa kung'olewa kucha. Na sina utaalamu sana wa seikolojia lakini nilivyomwona yule kamanda wa polisi kwenye tv akitoa ile taarifa uso wake ulionyesha wazi kuwa anachokiongea kina tofauti na anachokijua!
Najaribu kufuatilia kwenye pod-casts za BBC kuna moja kwenye 'heart and soul' yenye tittle "why do people lie". Nikiisikiliza labda nitapata undani wa ni kwa nini alipata ujasiri wa kusimama mbele ya waandishi.

Kikubwa hapa ni kuwa na subira maana kama kweli cdm hawana ile video clip ya kilichojili Soweto basi ukweli utatokea kwingine kusikojulikana na wengi lakini lililo wazi ni kuwa hautapotea!
 
Hizi porojo za "poa lisi" hazimezeki hata kwa kilevi. Yaani "kaa manda" mkuu kama huyo kuja na story kama za paukwa pakawa ni aibu na fedheha kwa "siri kali" yetu hii inayodai "kue ndeshwa" kwa misingi ya haki na usawa. Maswali ni mengi kuliko majibu.
 
Yaani waananchi wangeni bhana hawana shukrani kweli ni matukio mangapi ya Uhalifu na watu kumwagiwa tindikali yametokea huku arusha Leo jeshi LA polisi linakamata mhalifu watu wanamtetea inashangaza sana polisi wasipo kamata watu wanalalamika eti kwamba jeshi LA polisi halifanyi kazi wakikamata watu wanatetea wahalifu hivi nyie binadamu gani? Jeshi LA polisi linapaswa kupongezwa kwa kazi walioifanya hongera sana pt endeleeeni hivyo hivyo sisi humu katika mitandao tunawasaidia tunawaungamkono msichoke kwani humu wengine ni kama hao mliowakamata yaani wahalifu wanatumia mitandao ya kijamii kuwarudisha nyuma nasema tens hongereni polisi kwa kazi nzuri. Watu wamesahau matendo ya ugaidi Leo Hi wanawaunga mkono kweli ubinadamu kaxi.

Mbona unakuwa kama juha ,umeielewa taarifa ya police au umeidaka kama kasuku!!?
 
Hakuna kisochoeleweka nyie ndo wahalifu wenyewe mnataka huruma ya wananchi
 
kama polisi katika intelijensia yao wanaamini kwamba Mwangosi aliuwawa na chadema kwa kutupiwa kitu kutoka kwa mashabiki wa chadema,unafikiria hapo tutaambiwa hadidhi gani zaidi ya kudaganywa? ili kuepukana na haya mabo ni lazima wananchi wakubali kuitoa serikali ya ccm madarakani,tatizo ni baadhi ya waislamu pamoja na kufanyiwa haya yote bado wanaikumbatia ccm kwa kuambiwa tu eti chadema ni chama cha wakiristo
ni kweli kabisa hata kule kalenga waislam ni 99%. ndo maana ccm walishinda kiurahisi. ama kweli wewe ni taahira.
 
Back
Top Bottom