Simulizi: Wanawake ni wauaji

Simulizi: Wanawake ni wauaji

WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 48
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
"Dada, mzima huyu?"
"Aaagh! Fanu maswali gani hayo? we kamata huko tum bebe tumpeleke.... unauliza mzima!! sasa toka lini mtu aliyekufa akawa anatoa ukoromo?"
maneno ya kijana wa mwanzo yalinichoma sana japo sikuweza kujibu chochote lakini niliumia sana kuona dadaangu kipenzi akifananishwa na maiti angali yu hai kwa kigezo cha ile harufu..!?
Aaaaah!! ama kweli wanaadamu tunakufuru kubwa.
Afadhali kauli ya yule mwenzake aliyemjibu kidogo ilinifurahisha japo sikuipenda pia kwani dadaangu alikuwa hakoromi bali alikuwa anaugulia maumivu makali aliyokuwa anayapata lakini kile kidonda ndicho kilichokuwa kinaifanya sauti yake kusikika kama mkoromo kutokana na kutokota kwake kadri alivyokuwa anachezesha koromeo.
Nilimnyanyua na kum beba Asha ambae bado alikuwa kashikilia bakuli lake akilia na kutoka nae nikiwa nyuma ya wale vijana waliom beba dadaangu Mariam na sikukumbuka hata kufunga mlango zaidi nilikuwa makini na kumshika Asha ubavuni nilipom beba kutokana na kulia kwake na nilipandwa na hasira zaidi mara baada ya kupita hatua chache kwa majirani wale ambao walininyima msaada awali na kuwakuta wameeka vigenge vya umbea kwenye baraza zao huku macho yao yakiwa kwetu na tolipofika karibu walinyamaza na kuishia kutututazama na tulipopita ndipo waliangua kicheko kikubwa kwa pamoja.
'''HEEHEEEEEE KAPIMEEEEEEEE'''
Nilitamani nirudi nikachambane nao lakini nilishindwa na kubaki nimefura hasira iliyochanganyika na maumivu mpaka tulipofika pale stendi ambapo kila aliyetuona hakuacha kutushangaa wakati dada alipokuwa aningizwa kwenye ile Taxi nami nikamnunulia soda na Keki mbili Asha mara baada ya kumalizana na wale vijana,
na hapo kidogo kelele za kilio cha mwanangu Asha zilipungua pindi tulipoingia kwenye ile Taxi na kumueka mbele huku mimi nikikaa nyuma na kumpakatia dada ambae sauti aliyokuwa anaitoa iliyo mithili ya ukoromo ilizidi kuongezeka na kuniumiza zaidi kwa kugundua kuwa maumivu yanazidi mwilini mwa dadaangu kipenzi.

Nilimuamuru dereva kutuwahisha mwananyamala hospitali na kumpigia simu mama muda uleule gari ilipoanza kutoka na kumuelekeza hali ya dada huku nikimficha juu ya kidonda cha ajabu kilichokuwa shingoni kwa dada kwa kujua kuwa mamaangu anakuwaga na uoga unaoambatana na presha ya kushuka hasa anapomuona mwanae anaumwa sana ama kazidiwa hivyo hata ile kauli yangu kuwa nampeleka hospitali ilitosha kumstua kule aliko na mara baada ya taxi yetu kufika hospitali mwananyamala niliwakuta tayari mama na baadhi ya rafiki zake waliokuwa kwenye shughuli wakiwa na nyuso za huzuni getini huku mamaangu akiwa peku kabisa licha ya kuwa alitoka nyumbani akiwa amependeza na zaidi alivaa viatu ambavyo alinunuliwa na dada Mariam.
Ilibidi nishushe kioo na kuwapungia kuwaelekeza kuwa Taxi wanayoitazama inayoingia sasa ndiyo niliyomo na kweli walianza kuifatilia hadi iliposimama ndani ya ile hospitali na ndipo mama alipoingia kumchungulia dada pindi nilipomuacha na kwenda kuwaita manesi ambao walikuja haraka na kitanda cha matairi kwa nia ya kuja kum beba dada.
Moyo uliniuma sana nilipotoka na kumkuta mama akiwa analia huku ameshikwa na wale shoga zake na manesi wa mwananyamala sitoweza kuwasahauuu..... aaaaaagh nakumbuka jinsi walivyokuwa wanampakia dada kwenye kitanda kile mithili ya mzigo mbali na kelele za ukoromo wa maumivu na kusababisha kile kitenge nilichomtanda kwa kuziba eneo lile la jeraha kufunuka na kudondoka na hapo kila mtu aliyekuwa jirani alistaajabu kushuhudia ule uchafu ambao hata mimi nilishangaa kuona umezidi mara dufu huku lile tundu likiwa si dogo kama nilivyoona awali bali liliongezeka na ilitaka moyo sana kulitazama.
''"Aaaaaaaaaaaaaaaaaaagh, Mariaaaaamu Mwananguuuuuuuuu"''
Sintoisahau kauli hii ya mama angu.. mamaetu kipenzi aaagh,
Sikujua kabisa kama ile siku niliyomuambia 'mama umependeza sana leo umekuwa kijana kabisa' asubuhi yake pindi aliponiaga anakwenda kwenye shughuli ya harusi ya rafiki ake wa miaka mingi Mwananyamala kama itakuwa ndio siku yetu ya mwisho kucheka pamoja....!
Aaaaah sikuwaza wala kuhisi kama ipo siku mamaangu atanitoka ghafra namna ile tena mbele ya macho yangu na watu wengi kiasi kilee aaaah, masikini Zena mimiii nitalia na nani na tulizaliwa wawili tu na dadaangu ambae ndio nae alitoa ukoromo wa sauti ya juu uliotokea kwenye lile tundu na kurusha uchafu mwingi sambamba na damu mithili ya bomba mara baada ya kitenge kilichokuwa kinaburuza na kukanyagwa na nesi kudondoka na mama kupiga ule ukelele uliopelekea kuanguka chini.
aaaaaaaaaah kwanini hamkunambia ndugu zangu kama mmepanga kuondoka pamoja kwenye ulimwengu wa mauti na kunifanyia suprize iliyoutesa moyo wanguuu na kuniachia upweke wa milele!!??...... aaaaaaaaaaah
Nilijikuta nami nawasindikiza mama na dada kwa kupoteza fahamu pindi nilipokuwa nashuhududia vifo vyao ambapo mama alitapatapa na kukata roho pale chini muda mfupi baada ya kudondoka huku dada Mariam nae alimalizikia muda mfupi baada ya kutoa ule mkoromo mkubwa mithili ya firimbi uliorusha mafunda ya uchafu na damu.

Sintosahau maneno ya yule daktari alipokuwa ananipa maelezo ya uthibitisho wa vifo vya ndugu zangu siku moja baadae pindi nilipopata fahamu na kuruhusiwa wodini.
Alinambia kuwa kifo cha mamaangu kilisababishwa na presha iliyoshuka ghafra kupita kiwango vilevile dadaangu Mariam kifo chake kilisababishwa na kansa hatari ya koo.
Sintosahau kabisa hata mara baada ya ndugu na majirani kuungana nami hospitali na kuchukua maiti kurudisha misiba ile ya kihistoria moyoni mwangu mpaka nyumbani na baada ya taratibu za mazishi kukamilika hatimae mama na dada wote walizikwa siku moja na makaburi yao yalifatana. aaaah! Mungu awaeke mahali pema.

Siku moja kupita baada ya mazishi ilibidi nitoke na vijana wa kiume wachache sambamba na mzee wetu wa mtaa tuliokuwa tunaishi tuliyezoea kumwita babu japo hakuwa na undugu wa damu na sisi lakini alikuwa jirani mwema na alisifika kuwa mzee mwenye busara sana.
Safari yetu ilikuwa ni kule alipokuwa anaishi dada Mariam kwa niaba ya kukusanya vitu vyote lakini hatukuamini baada yakufika na kukutana na habari za uvamizi na wizi uliotokea siku moja iliyopita ambapo vitu vyote muhimu vya dada viliibiwa na chumba kubaki cheupe mithili ya mtu aliyehama.
Japo ilituuma lakini tulipiga moyo konde na kushukuru tu, kwani iwapo tumempoteza mtu kabisa sembuse hivo vitu?
tuliwaaga wale wenyeji tuliowakuta kwenye vile vyumba viwili ambavyo siku ile nilipokuja kumchukua dada vilikuwa na makufuri tu.
Yule mzee alinisaidia kuongea na wale majirani visilani mara baada ya kumuhadithia mkasa ulipoanzia ambapo kwa busara zake aliweza kuambua sababu kuwa kumbe dada Mariam alikuwa ni mtu wa kujiona ona sana kipindi anaishi pale na mashoga zake watatu waliopanga pamoja huku mmoja wao akiwa si mwanamke bali ni shoga kabisa tena mbaya zaidi waliitumia ile nyumba kama dangulo la kuingiza wanaume hali iliyokuwa inawakera sana majirani kwa vile kujiona kwao, kutoshiriki kwenye misiba ya wenzao na matatizo mengine huku wakiwa ni watu wenye nyodo nyingi na ndio sababu kuu za kuwachukia wote na kuwatenga. Hapo kidogo nilielewa lakini bado sikulidhika na yale waliyonionesha lakini niliamua yote kuyapuuza na kurudi nyumbani sambamba na yule mzee na wale vijana.

ulipita mwezi mmoja baada ya kumaliza matanga ndugu wote walitawanyika na kuniacha nikiwa na mwanangu Asha mtoto wa marehemu dada bila msaada wowote wa kimalezi zaidi ya kuniachia maneno ya pole na maisha mema na huo ndio ukawa mwanzo wa maisha mapya ya misukosuko na mazoea baina yangu na Asha.

Lakini kabla hazijaanza tabu na misukosuko ambayo sikutaraji kama yatatukuta mimi na mwanangu yule niliumizwa na kulizwa na kitu kimoja ambacho nilikikumbuka mwenyewe baada ya kusahau kwa muda mrefu..... Kitu chenyewe ni barua, barua ambayo ilionesha wazi kwa nje ilinihusu mimi, barua ambayo sikujua imebeba nini hasa ndani yake, barua ya mwisho ambayo muandishi wake nilijua kama hatoniandikia tena barua nyengine milele, ila kwa barua ile niliweza kuihisi sauti yake akiongea pindi nilipokuwa nasoma hati ya maandishi yake, barua toka kwa marehemu dada Mariam ambayo licha ya kupotea kwake kutokana na janga kubwa la mafuriko ya mwaka lililokuja kutokea wiki chache baada ya kuisoma lakini maneno yake yaliendelea kuishi akilini mwangu kila nilipomkumbuka yeye ama nilipomuangalia Asha.
Barua yenyewe ilikuwa hivi................

^..................................................................................^
Mdogo angu Zena, naandika barua hii nikiwa na maumivu makali sana sehemu za shingo na kifua hususani kooni na hivi sasa uvimbe ambao awali ulikuwa kwa ndani lakini sasa umezidi kutokeza nje ya shingo, najua muda wowote unaweza kupasuka na kuimaliza safari yangu ya hapa duniani kuianza safari mpya kwenye ulimwengu wa ahadi kwa kila mja aliyeumbwa.
Uvimbe huu si wa jipu la kawaida bali ni ugonjwa ambao nimeuficha kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na aibu na kutopenda niwatie majonzi mapema lakini kwa kuwa sasa naona ule wakati wa kuumbuka umefika nimeamua kukuweka wazi ukae ukijua kinachoniua ni nini..
Hiki kinachonitafuna Zena ni Kansa.
ITAENDELEA...
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 49
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
Kansa ambayo imesababishwa na wadudu wabaya waliotoka kwenye mbegu za mwanaume nisiyemjua ambae kumbe alikuwa na ugonjwa m baya sehemu zake za kutungia mbegu nami bila kujua nilijikuta nazipokea mdomoni kwa kumnyonya uume wake mpaka anafika kilele kinywani mwangu nikijua nampagawisha ili nimchune vizuri kumbe nilikuwa naeka lehani maisha yangu mara baada ya bakteria hatari ambao sijawahi kuota kama wapo walipoingia na kueka makazi pembeni ya koo langu kutokana na ukweli huwezi kutema chote kile kichofika kwenye ulimi na hiyo ndio ikawa mwanzo wa tatizo ambalo nilikuja kugundulika tayari nimechelewa.

Ni aibu lakini nimeamua kutubu kwa kukuandika ukweli huu mdogo angu Zena nakusihi kama nawe una tabia ya kunyonya tupu za wanaume kwa kuamini ndio unamkoleza nakusisitiza acha haraka tabia hiyo na hili uje kumfunza hadi mtoto ninayemkabidhi kwako baada ya kifo changu.
Narudia Zena kumbuka kinachoniua dadaako na simjui ni mwanaume yupi aliyeniachia hawa bakteria walioshindika kutokana na kuwafanyia mchezo huu karibu kila mwanaume niliekutana nae kimwili kasoro mwanaume wangu wa kwanza na yule wa pili ambae ndie baba halali wa mtoto huyu nae ni shemeji ako niliyemuacha kimakosa mimi mwenyewe baada ya kumsaliti sana ambae ni Hussein.

Zena nakukumbusha pia hata utapoolewa ukiwa na mumeo usikubali kumuacha awe anakunyonya tupu yako mpaka unafika kishindo kwani kuna hatari kubwa ya magonjwa ya ajabu kupitia sehemu za siri si kwa mwanaume wala mwanamke ambayo mengi hayajaibuka ila leo hii mimi nimekuwa mfano wa mavuno ya tabia hizi chafu ambazo asilimia kubwa ya vijana si wa kike si wa kiume wanafanya haya kila siku ilihali sehemu husika zipo. Basi waambie wataokusikia habari za kifo changu labda utasaidia kuwaokoa baadhi yao japo najua wengi watakupuuza na hata wataokaidi basi waache waendelee ila wajue yanaweza kuwakuta kama yaliyonikuta mimi kwani hizi ni zama za mwisho wasiige mafunzo ya kishetani yanayosambazwa kwenye mikanda ya ngono.
Kifo kinauma sana hasa kifo cha dhihaka kama hiki... Dawa pekee ya haraka niliyoambiwa na daktari ni kukata sehemu inayoshambuliwa lakini sasa mimi nashambuliwa koo maana yake hata nikikatwa haitakuwa tiba.

Huo ndio ukweli Zena najua mwanangu hatolelewa na babaake wala hajawahi walau kushikwa mkono na babaake ambae wote tunajua maisha yake anayamalizia gerezani.
Basi nakuomba pindi utapokuwa unamlea Asha mlee katika maadili tofauti sana Zena mdogo wangu na uwe unampeleka walau mara moja kwa mwaka gerezani akamuone babaake kwani taarifa za uwepo wake naamini anazo.
Kumbuka Zena kumbuka mpeleke Asha madrasa akajifunze elimu ya dini.
Naamini kifua chake kitapojaa imani na jina la mungu litapokaa kinywani naamini atafauru majaribu mengi ya kishetani na kamwe hatokuwa mwanamke muuaji kama walivyo wanawake wengi wa leo nikiwemo mimi na wewe kwa kitendo chako cha kutoa mimba zaidi ya mara mbili tulipokuwa shule.
Nakusihi nawe utubu mdogo wangu na uzingatie usije kumpa mtu mwengine amlee Asha naogopa asije kuharibika na kuwa mwanamke muuaji akaja umiza wanaume kama mimi nilivyomuumiza babaake.

Kwa heli Mdogo angu,
mimi natangulia....
Mungu akipenda tutaonana kwenye ulimwengu wa mauti pindi nawe utapokuja mwaka wowote.

^................................................................^

Barua ya dada ilifufua msiba upya moyoni mwangu huku nikilia kwa uchungu sana kwani hata mimi nilikuwa na tabia hiyo ya kunyonya tupu za wanaume lakini daaaah! kumbe harufu na uchafu ule ambao ulikuwa unatokota shingoni mwa dada ni kansa ya koo?!!
Tena chanzo chake ni mchezo ambao hata mimi nilikuwa ni mmoja wa wachezaji wake...!! aaagh nilipogundua na kukumbuka mateso ya dada hadi pale alipotoa mkoromo mkubwa tena sauti ikitokea kwenye tundu lililokuwa linarusha uchafu wa usaha na damu hadi kufa kwake.... Nami kuanzia muda huo niliapa kamwe sitoruhusu mwanaume aninyonye utupu wala mimi kumnyonya utupu na kuahidi kuutumia mdomo wangu kwa kula, kunywa na kuramba vile vilivyohalalishwa tu.

Lakini mwezi mmoja baadae lilitokea janga la mvua iliyosababisha mto uliopita jilani na pale tunapoishi kufurika na maji kupasua kwenye makazi ya watu ikiwemo nyumba yetu majira ya usiku ambapo nilichobahatika ni kujiokoa mimi na mwanangu Asha niliyeachiwa na dada na hapo ndipo tulipogeuka wahanga wa mafuriko tulioishi katika kambi maalum uwanja wa taifa baada ya kupoteza makazi kwa zaidi ya miezi miaka miwili.
Serekali yetu imejaa hila na rushwa kwakweli japo machoni na midomoni haiko hivyo kwani baada ya kupewa ile kambi kipindi cha janga lile na kutusaidia miezi michache ya awali, ndipo walipotutelekeza kabisa na hapo nami nikakata shauli baada ya kumpata bwana ambae alitukaribisha kwake kabla ya kumuhama baada ya manyanyaso na kumuonesha chuki za wazi mwanangu Asha ndipo nilipopanga maeneo ya uwanja wa fisi na kujiajili kwa kuutumia mwili wangu. aaaag Moyo unaniuma sana kwa nilichofanya kwani nilimpeleka Asha kwenye shule ya watoto walio kwenye mazingira magumu sana na yatima na kumuacha kwa muda huko mwanangu Asha si kwa lengo kuwa simpendi bali kwa kumueka mbali na mazingira yale ambayo nilijua yatamuharibu kisaikolojia pindi atapokuwa anaona mamaake kila siku nalala na wanaume tofauti tofauti.
Siku zilikwenda huku kipato changu kikiongezeka na kuwa namtembelea mara kwa mara mwanangu Asha ambae alikuwa anazidi kunipenda siku hadi siku na pia nilizidisha mapenzi kwake hasa baada ya kipaji chake cha elimu kuonekana kwa wafadhili wa kihindi miaka minne tu tokea aishi pale na alipata bahati ya kupendwa na wale watu ambapo zilifanyika taratibu za kuondoka nae kwenda kumsomesha huko japo awali nilitaka kukataa lakini kwa ushauri wa watu na walimu wake sambamba na kalatasi za serikalini na kuhakikishiwa kuwa mwanangu hawezi kupotea na hii ni kwa faida yetu wote pindi atapofanikiwa huko kwani hata mimi nilishindwa kumlea hadi nikampeleka pale ndipo akiwa na miaka kumi tu niliweza kuvunja vunja zaidi yoote niliyoagizwa na dada Mariam juu ya Asha na hiyo ndio safari ya mafanikio yaliyokuja kuibuka na kufaidi matunda ya mwanangu Asha na kwa bahati mbaya dawa nilizokuwa natumia nisipate mimba ziliniletea madhala pale nilipohitaji mtoto nilishindwa kabisa kubeba mimba na nilipochunguzwa nilihakikishiwa haitawezekana kubeba mimba na ndio sababu hadi leo sina mtoto yeyote zaidi ya mwanangu Asha ambae siku zote aliamini mimi ndie mamaake mzazi.

<<<===>>>
.............................
* * *

Kipindi Zena akimalizia simulizi yake iliyowafanya Hussein bubu na dk Asha kubaki wanadosha machozi kwa uchungu mkubwa huku wakiwa wameshabadilisha kila aina ya mikao wakimtazama Zena bila kujua kumbe mlango ulikuwa unagongwa muda mrefu sana na walichostushwa ni baada ya kufunguliwa na kusikia viatu vya mtu akiingia pale sebureni na walipogeuka wote walimshuhudia Kamishna Shebby akiwa amesimama baada ya kuingia tena akiwa amestaajabu kupita kiasi kwa kile alichokuwa anakiona watu wamekaa chini wameyaacha makochi na zaidi wote walikuwa wanalia.

"Vipi Asha?! samahani mama kwa kuingia pasi na ruhusa.. vipi mzee wangu mbona sielewi kwema??"
aliongea kwa taharuki Kamishna Shebby na kusogea pale walipokaa kina Hussein baada ya mama mdogo wa Asha kumruhusu kwa ishara nae akae tu sofani huku nao wakijizoazoa kuketi vizuri kwenye masofa wakiwa bado na nyuso za huzuni.
"Vipi mzee wangu, umenitisha sana baada ya kuchelewa Asha.. Mama nini kimetokea hapa?"
aliuliza Shebby huku akiwatazama machoni ndipo Hussein alipoanza kumsimulia kisa kizima na kumfanya Kamishna Shebby abaki ameduwaa.
"Kha!! Ina maana Asha ni mwanao!!! yaani kumbe wewe niliyekutuma ni baba Mkwe!? Eee Mungu mbona siamini.."
"Amini hivyo baba, mimi ni mama mdogo tu wa Asha na huyu ndie babaake kweli kabisa wala sio utani hata mimi siamini kama leo hii tumekutana"
aliongea Zena kwa majonzi
"BABA"
Kwa mara ya kwanza Hussein masikioni mwake aliisikia sauti ya mtoto wa kike akimwita baba tena mtoto ambae hakuwahi kuilea hata mimba yake, walijikuta wananyanyuka kwa pamoja Asha na Hussein na kukumbatiana kwa nguvu huku wote wakilia lakini kilio cha sasa kilikuwa ni cha furaha.

ITAENDELEA...
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 50
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
"sikuwahi kufikiria hiki kitu jamani babaangu pole sana kwa yaliyokukutaa"
"Aaaah! mwanangu usinipe pole mamaaa nisamehe sana mimi nilichelewa kujua uwepo wako aaa"
Ilikuwa ni furaha ya baba na mwana kujuana huku Zena na Shebby wakiwa wamekaa wakiwaangalia na kumshukuru Mungu kabla nao hawajasimama na kuungana nao pamoja kuwafariji.

Baada ya kuliwazana na kila mtu kurejea katika hali ya kawaida huku furaha ya aina yake ikiwa kwenye moyo wa kila mmoja ndipo Asha aliposimama na kumshukuru sana Kamishna Shebby kwa ukalimu aliomuonesha babaake huku akimuomba babaake (Hussein) kuanzia siku hiyo afanye makazi yake pale kwenye ile nyumba wakti pia akimtafutia makazi mengine mazuri ya kuishi lakini ajabu Hussein alikataa na kumwambia Asha maneno ambayo hakuyatarajia.
"Asha mwanangu nakupenda sana na nimefurahi mno kukujua, lakini wewe ni mwanamke na sasa upo mbioni kuolewa na mwanangu wa hiyari ambae nataraji atakuwa mkwe wangu mwema siku zote, kwa sasa furahia kuwepo pale mpaka mtapooana ndipo kwa amri ya Mkwe wangu ndipo nitatoka na kukaa sehemu nyengine mtayojadili kwa pamoja nikae lakini si kwa amri wala matakwa yako binafsi."
Maneno mazito ya Hussein yalitosha kuutafsiri moyo wa Asha kiasi gani babaake alikuwa na mapenzi mazito na mchumbaake hivyo alikubaliana na mawazo ya babaake ila alimuomba Kamishna Shebby amruhusu basi alipie yeye gharama za pale hoteli na kwa mapenzi ili mradi mpenzi wake alidhike Shebby alikubali.

Baada ya hayo kumalidhika ndipo Hussein alipomuomba Asha alete kalamu na karatasi kwa niaba ya kuijibu ile barua tena mbele ya Shebby mwenyewe ambae awali alitaka awapishe nje ili wajadiliane vizuri lakini Hussein alimzuia na Zena alikuwa radhi Hussein amalize kila kitu.
"Nimekuja kama mshenga na sasa naichana bahasha na kuijibu barua kama baba, Asha mwanangu taja mahali yako ya Ndoa."
"Mh! baba si utaje wewe tu"
"Hapana wewe ndie unayeolewa"
"sawa basi mi.... mi Elfu kumi tu inatosha"
"Safi sana mwanangu"
alijibu Hussein na kuendelea kuandika na alipomaliza alimkabidhi Shebby palepale.
"Mwanangu tuachane na mambo yote barua hii ifike nyumbani ukitaka kuoa hata kesho njoo nitatoa mimi hiyo elfu kumi ya Asha japo ni katika pesa zako ulizonipa, hakuna gharama nyengine zaidi ya hiyo elfu kumi huku kwetu"
alisisitiza Hussein na kumshangaza mno Shebby lakini ukweli ndio ukawa hivyo na lilikuwa jambo geni kabisa kwa mila na desturi za kibantu barua kujibiwa mbele ya muhusika wa kiume na kumkabidhi yeye moja kwa moja.

Baada ya hapo ndipo Hussein na Shebby walipoondoka huku wakiwaacha Zena na Asha wakiwa nusu wameamini nusu hawajaamini kwa kilichotokea siku hiyo.

* * * * * *
MKESHA WA MAWAZO

^^^^^^^^
HUSSEIN BUBU
______________
Usiku wa siku hiyo ulikuwa mgumu kwa Hussein kupata usingizi kwani muda wote mawazo yalimpeleka mbali sana huku akiwa haamini kama leo yuko huru na kumbe yule daktari bingwa Asha aliyesaidia kumtibu mtu aliyemsaidia yeye kwa moyo ni mwanae na kwa uwezo wa Mungu alifanya kazi ya kumsaidia jeraha baya alilopata Shebby mpaka amepona kabisa na kujikuta wanakuwa wachumba?
Alijikuta anageuza msikiti chumba cha ile hotel mala baada ya kujiazinia mwenyewe na kuanza kusali usiku kucha ambapo kila alipopumzika aliomba dua na kumshukuru Mungu na kuendelea kusali.
("Aaaaaah! kweli Mungu wewe ni Mkubwa sana na mwenye sifa za kipekee, Nakuomba kama ulivyonitendea muujiza wa kutoka jela na ukafanya kunikutanisha na mwanangu ambae nilijua habari zake nikiwa jela na kukata tamaa ya kumuona tena, basi baba nakuomba kama ulivyofanya hayo yote basi iwe hivyo na kwa Mr X niweze kumjua na kulipa kisasi kwa mikono yangu")
Na hiyo ndio ilikuwa dua kubwa ya Hussein bubu katika nafsi yake kila alipopumzika na kumshukuru Mungu na alisali huku mawazo yake hayo ambayo alikuwa nayo toka jela yakijirudiarudia akilini mwake

^^^^^^^^^^^
KAMISHNA SHAABAN
___________
Si Hussein tu, mambo yalikuwa hivyo pia kwa Kamishna Shebby ambae nae alikosa lepe la usingizi kwa kufikiria mengi sana huku akivuta picha siku ya kwanza anakutana na Hussein bubu.
("Daaah! Mungu kweli wa ajabu na ameeka siri nzito sana katika maisha ya kila kiumbe yalivyo mbele kutokana na mzunguko anaomuonesha kabla daa.... Yaani kumbe muda wote natoa msaada kwa mtu ambae imeandikwa ndie baba mkwe wangu!!! ")
aliendelea kuwaza Shebby
("Nina sababu zote za kumtafuta mshenzi mr.X na kulipa kisasi bado niko sahihi kwa hili")
aligeuka Shebby pale kitandani na kuchukua simu iliyokuwa pembeni ya mto na kumtumia txt Cj4 akimjuza kila kitu kilichotokea kule walipopeleka posa ambacho awali hajamjuza.
)('So huyo mkeo mtarajiwa Hussein kumbe ni babaake?')(
iliingia sms ya Cj4
na Shebby kumjibu ndipo sms ya Cj4 ilipoingia nyengine
)('Kuwa makini sana na mchumbaako hupaswi nae kumwambia habari zozote za mipango yetu')(
))('Sawa lakini kwanini unasema hivyo')((
)('Kumbuka upo kwenye mchezo na mr X sasa usikubali uchezeshe na mr X kwenye huu mchezo ila wewe ndie umchezeshe mr X ktk huu mchezo na hapo tutamshinda.. Kumbuka kama Hussein bubu tumemumtoa kama chambo harafu mwanae kumbe ni mchumbaako nina shaka hili mr.X analijua na isije kuwa na huyo mchumbaako akawa anachezeshwa na mr X kwenye huu mchezo pasi na yeye kujijua')(
SmS ya Cj4 ilimfanya Shebby ashushe pumzi na kuirudia mara mbilimbili huku moyoni akikili kuwa kuna upana mkubwa sana wa kimbinu na fikra baina yake na Cj4

ITAENDELEA.....
 
WANAWAKE NI WAUAJI
Mtunzi/mwandishi HUSSEIN BAKARI
MTOTO WA BECKER
mtotowabecker@gmail.com
0713 46 26 29
_________________
EPS 01
========

********

“Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa pumzi na afya njema hadi leo hii niko hai japo niko tofauti sana na nilivyokuwa awali hata wasionijua wakiniona hii leo watadhani nilizaliwa hivi. La hasha! Ila leo nitawaambia ukweli wa yote yaliyonisibu na yanayowasibu wanaume wengi katika dunia hii ya leo. Nakumbuka zamani babu aliwahi kuniambia niwe makini sana na wanawake pindi nitapokuwa mkubwa. Na alinisihi ya kwamba niwaelewe wanawake ni watu wa aina gani na jinsi ya kuishi nao. Lakini sikuwahi kuamini maneno yake hadi yalipokuja kunisibu na ndipo nilipokumbuka na kuelewa kwanini babu alinisihi vile. Aaaaagh! Wanawake ni mama zetu na ni pambo la dunia na ndio maana Mungu aliwaumba ili watufariji na watulee, lakini ukweli bado unabaki kuwa wanawake ni watu hatari sana kwetu wanaume. Hebu tukumbuke hata kwenye hadithi za watu wa kale kwenye vitabu vya dini tukianzia mwanzo kabisa wa dunia enzi za Adam na Hawa/Eva. Adam alitii kila kitu katika mamlaka aliyopewa na Mungu lakini mwishowe alikuja kumkosea Mungu kwa kutenda dhambi aliyoponzwa na mkewe (Hawa/Eve) mara baada ya kushawishiwa na Shetani, Eeeh, amini usiamini shetani ni vigumu sana kumuingia mwanaume hivyo anamtumia mwanamke kama alivyomtumia Hawa/Eve kwenda kumlubuni mwanaume kama alivyolubuniwa Adam na kujikuta mwanaume anaumia kwaajili ya upendo na kumuamini sana mwanamke pasi na kuelewa kiundani udhaifu mkubwa wa mwanake mwenyewe. Tuachane na Adam, tukumbuke Samson mtu mwenye nguvu aliyewapa tabu sana Wafiristi enzi hizo lakini mwishoe anakuja kukamatwa na kupata mateso makali baada ya kulubuniwa na Delila aliyetumiwa na Wafirist kubaini siri za nguvu za Samsoni. Eee, Samsoni nae aliponzwa kwa ajili ya mwanamke, na si yeye wala Adam tu tukumbuke hata mtu wa kwanza kufa alikuwa ni mwanaume na sababu ya kifo chake kilitokana na mwanamke!! Eeeh ni wanaume wengi mno wameponzeka kwaajili ya wanawake na mmoja wao ni mimi na ndio maana leo hii nasema wanawake ni wauaji. Najua wengi mtanielewa vibaya hususani wanawake, lakini naomba msizime tv zenu ama radio ili mnielewe vizuri kwanini hasa nimekazania kusema Wanawake ni Wauaji? Hii ni asili iliyoanza toka kwa mwanamke wa kwanza kabisa kuumbwa na bado ipo na itakuwepo na itawaumiza wanaume wengi sana wasiokuwa makini na ndio maana hata Mungu hakuwahi kushusha nabii wa kike. Wanawake ni wadhaifu wasiokubali udhaifu wao na ndio maana nawaita Wauaji. Achilia mbali vitabu vya dini tukija kwenye maisha yetu ya kila siku lini ulishawahi kusikia mwanaume katupa katoto kachanga? Naamini kama mimba wangekuwa wanabeba wanaume usingesikia neno kutoa mimba. Hivi ushawahi kujiuliza mwanamke ana moyo wa namna gani hadi anadiliki kukiua kiumbe alichokibeba tumboni miezi tisa na kujifungua kwa uchungu?!! au unadanganywa na maumbile yake na sauti laini unajisahau na unaacha kuwa makini nae? hivi hujui kwamba simba dume ana muungurumo mkubwa sana lakini jike ndiye jasiri wa kuua. Huo ni mfano tu lakini nataka unielewe na uwe makini kwanini nasema WANAWAKE NI WAUAJI..”
Ilikuwa ni sauti ya bwana mmoja mlemavu wa macho na miguu akiongea luningani katika kipindi cha YA WALIMWENGU LIVE kilichokuwa kinarushwa kupitia kituo cha BECKER TV kila siku za jumapili asubuhi na marudio yake ilikuwa jumamosi jioni.
Nilikaa kwenye sofa kwa hamasiko. Macho na masikio niliyatupa luningani huku mkono mmoja nikiwa na kikombe chenye chai na mwengine ukiwa na rimoti nikiongeza sauti ya luninga. Mada ya yule bwana ilinistua na kunigusa sana hali iliyochochea niwe na shauku kubwa ya kumsikiliza ili nimuelewe vizuri kwanini anasema wanawake ni wauaji.
Nilitulia na kujikuta nashindwa hata kupiga funda moja la chai na kubaki nimekishikilia kikombe kwa kumakinika na yule bwana alipokuwa anazungumza ambapo aliendelea kwa kusema......
“Nakumbuka miaka kumi iliyopita nilikuwa na maisha mazuri kabisa ya furaha, mimi na mke wangu kipenzi baada ya kufunga ndoa. Kiukweli nilimpenda sana mke wangu nae alinionesha mapenzi hasa na kunisahaulisha maumivu niliyopata kutoka kwa mke wangu wa kwanza tuliyeachana muda mfupi tu baada ya kukaa kwenye ndoa kwa miaka mitatu na kuanza visa vilivyosababisha nimuache aishi maisha aliyotaka yeye na ndipo baada ya miezi kadhaa nilipompata huyu mwanamke wangu mwengine aliyeonesha kuwa na vigezo vyote nilivyohitaji na mwaka mmoja tu katika mahusiano yetu tuliamua kufunga ndoa kabisa.
Kiukweli mke wangu nilijivunia uzuri aliokuwa nao upole wake na tabia ya kupenda ibada. Na mara nyingi alinibadilisha kwa maneno matamu na kunisihi niache kunywa pombe, na kweli ilifika kipindi niliacha pombe na taratiibu nilipunguza kabisa kuvuta sigara kutoka pakiti moja kwa siku hadi ikafika mahali siku nzima nikavuta sigara mbili tu, hali iliyofanya hadi walionijua kunishangaa na kumsifu sana mke wangu na ndipo nami nilizidisha moyo wa kumpenda na kumpa uhuru wa kila kitu kwani nilimuamini mno…!” Alinyamaza kisha aliendelea…….
“Kila nilichofanya nilihakikisha lazima mke wangu ajue na nilisikiliza sana na kufata ushauri wake kuliko mtu mwengine. Akisema nisifanye kitu fulani nami nilitii, akisema nifanye nami nilitii, hiyo yote nilifanya nikiamini namjenga na kumuonesha kiasi gani namthimini bila kujua kua kuna ugonjwa m baya nilikuwa naufuga.
Awali sikuona tofauti yoyote wala kuhisi kama kuna kitu nakosea zaidi nilianza kusikia minong’ono kutoka kwa majilani na baadhi ya ndugu zangu kuwa napelekeshwa na nimetawaliwa na mke wangu. Kiukweli nilichukizwa na habari zile na kugombana na baadhi ya ndugu zangu waliomsema vibaya mke wangu nikiamini fika wanataka watugombanishe na wananionea wivu kwa kupata mke wa namna ile kwani maisha yetu yalizidi kunyooka siku hadi siku.
Aaaaaagh.. kuna muda huwa nahisi kama ndoto vilee kwani sikujua kabisa kumbe kuna bomu nalitengeneza mwenyewe ambapo baadae litapolipuka litaniletea madhara makubwa na kama si kuniua basi litanipa ulemavu wa kudumu kama ilivyotokea baadae…. Aaaagh, mke wangu!!!...”
Alivyozidi kuongea ndivyo nami nilivyozidi kutulia kumsikiliza kwa umakini huku nikibofya bofya rimoti kuongeza sauti mara kwa mara utafikiri nilikuwa na ubovu wa masikio. Nilimuangalia kwa jicho la shauku ya kujua yaliyomsibu. Uso wake wa jitimai ulitia huruma ukichochewa na ulemavu uliobeba tafsiri ya mazito yaliyomsibu. Kiu ya kujua ilikuwaje ilizidi kuniparua milango yangu ya fahamu. Lakini kabla sijafaidi vizuri hadithi ya yule bwana mara umeme ulikatika na kila kitu kuzimika.
“Aaaagh, Tanesco bwana kama maboya!!!”
Nilinyanyuka kwa hasira kuzima kitufe cha luninga na kuwasha kile cha taa ili umeme utaporudi tu, taa inijulishe mapema.
Wakati huo ile chai kikombeni ilikuwa ya baridi kabisa na sikuambulia kunywa hata chembe. Nilienda imwaga na kurudisha kikombe kabatini na ndipo nilipoikumbuka simu yangu niliyoiacha chumbani kwenye chaji. Haraka niliiendea na kukuta ikiwa na ‘missed calls’ tisa ‘sms’ nne. Nilipofungua zote zilitoka kwa mtu mmoja. Mtu ambae alikuwa zaidi ya uwaridi moyoni mwangu. Mwanamke wa ndoto zangu ambaye tulikuwa na miadi ya kukutana wikiendi hiyo ili tufurahi pamoja. Huyo alikuwa MARIAM ama MAMU kama nilivyopenda kumwita.
Nilizisoma zile ‘sms’ ambapo mojawapo iliandikwa hivi…
MBONA HUPOKEI SIMU WALA HUJIBU MSG ZANGU? KAMA UPO NA MALAYA WAKO SI UNAMBIE TU NISIJE..!!
“hahaa Mamu bwana..”
Nilijisemea moyoni na kuingia sehemu ya ujumbe kujibu lakini kabla sijabonyeza kitufe cha kutuma ujumbe, mara mlango wa sebuleni uligongwa kwa rabsha. Nilipouendea kabla sijaufikia, ulifunguliwa na mgongaji aliyeingia akiwa kashiba ununo. Alikuwa ni Mamu kipenzi changu. Nilifurahi nilipomuona nilimkumbatia na kum-busu lakini aliitoa mikono yangu kiunoni mwake na kunisukuma pembeni huku akiingia na kunipita bila kusema chochote na kwenda kukaa sebuleni. Nilibaini kuwa amekasilishwa kutokana na kutopokea simu yake na nilijua sasa nina wajibu wa kum-bembeleza ili nimuweke sawa. Nilimjua kipenzi changu ni chakudeka, nami kwa huba nilimdekeza.
“Unakunywa nini bebi” nilimuuliza kwa sauti ya mahaba.
“Sitaki kunywa chochote niache.” Alijibu kwa hasira huku akipandisha miguu sofani na kubetua midomo huku uso wake akiuelekezea pembeni.
Hali ile ilizidi kunihakikishia kuwa nina shughuli pevu ya kubembeleza mtu mzima sasa. Lakini kabla sijafanya hivyo mara taa ya sebuleni iliwaka na ndipo nilipokumbuka kuwasha luninga kwanza niendelee na kile kipindi huku moyoni nikiwa na shauku Mamu nae amsikie yule bwana juu ya hadithi yake iliyowatuhumu kuwa wanawake ni wauaji.
Lakini lol! Mada ya yule bwana hasa kauli yake ya kuwa wanawake ni wauaji ilimchukiza zaidi Mamu na kuamua kuzima luninga kwa hasira.
“Aaag! Wee vipi?” nilitahayuri.
“Vipi nini!!?” Alinijibu kwa kuniswalika.
“Si uache tuangalie sasa unazimia nini?!”
“Hivi Hussein kwa akili zako timamu unaona hiki kitu anachokizungumza huyu mpuuzi ni sahihi!!”
“Kitu gani..?”
“Kusema wanawake ni wauaji.!!”
“Mh! hapo kumjaji moja kwa moja itakuwa ngumu, sasa nitamjaji vipi wakati hata hadithi yenyewe sijaisikia!! anaweza kuwa sahihi au si sahihi inategemea na point zake mwenyewe.”
”Hee! hivi nyinyi wanaume mpoje!!!” Aliwaka Mamu kwa sauti ya juu na kusimama huku akinitazama kwa hasira. Alihema juu juu na kuzidisha povu akinguruma kama moto wa kifuu.
“Hivi mnatuchukuliaje sisi wanawake eeh!!?”
“Kivipi baby.. mbona tunawakiana sasa.”
“Sio Nawakaa.. ila nakwambia ukweli acha kuwa na mitazamo ya kijinga au ndio kashakulisha ujinga huyo mpuuzi mwenzio…! Kwa hiyo na mimi muuaji si ndio, au unanionaje!!”
“Hapana baby sijamaanisha hivyo..”
“kumbe unanionaje..!”
“Unaweza kuwa muuaji au si muuaji inategemea tuu.”
“Aahaa.. kwa hiyo hadi mamaako aliyekuzaa muuaji, dada zako wauaji, shangazi zakoo si ndio..!”
“Sasa Mamu hayo matusi..”
“Matusi nini.. si wanawake ni wauaji! We vipi..?! Hebu nipishe huko nisije nikakuua buree..”
Alichukua mkoba wake kishari pale sofani kwa hasira Mamu alielekea mlango wa kutokea ulipo na kutoka huku akiubamiza kwa nguvu.
“Aaagh!! Sasa huo mlango umekukosea nini..!”
Nilibaki nimebumbazika pale kwenye kiti huku nikiwa nimechanganyikiwa kwa jinsi Mamu alivyonibadilikia siku hiyo kuliko siku zote. Hakuwa cha kudedee tena bali alikuwa mbogo. Nilijilaumu kidogo kwa kubishana nae punde alipozima luninga na kumsababishia mpenzi wangu kuwa na hasira mara tatu zaidi alivyoingia. Niliuendea mlango na kuokota funguo zilizodondoka pindi ulipobamizwa kisha nilirudi na kujitupa kwenye sofa huku akili yangu ikiwa imecheza makida. Niliiwasha tena luninga safari hii nikiwa sina shauku kabisa wa kuangalia kile kipindi ambacho ndio kilikuwa kinaishia lakini kuna maneno ya mwishoni ya yule bwana yalipenya vizuri masikioni mwangu na kukistua kichwa changu kidogo pindi aliposema.
“Najua wanawake wengi wataobahatika kunisikiliza na kunitazama watanichukia na kuona nimewadhalilisha na kuwatusi. Nami sitoshangaa wala kuogopa hilo kwa sababu najua kuwa wanawake tayari wana ulemavu wa asili ambao Mungu aliwaumba nao kwa dhumuni la kuwa wasaidizi na wafariji kwa wanaume tu. Mwanaume hajaumbwa kwaajili ya mwanamke ila mwanamke aliumbwa kwaajili ya mwanaume na ndio maana tunaambiwa kuwa mwanamke ametoka ubavuni kwa mwanaume. Lakini udhaifu wao ndio unafanya tuone mpaka leo hii wanawake wakitaka kushindana na wanaume wakisahau kuwa mwanaume ni wa kwanza tu kiasili. Na hii inatokana na kuwa mwanamke ni rafiki mkubwa wa shetani anayetumiwa katika kuiharibu dunia na hata baadhi ya wasomi wa dini kiimani wanatwambia wanawake wengi sana wataingia motoni.
Mungu ameweka mifano mingi sana ya wazi kuwakumbusha wanawake kuwa mwanaume ni kiongozi na anapaswa kunyenyekewa na mwanamke japo kwa akili mbovu za wanawake wengi wanaona kufanya hivyo ni ujinga kwani hata wao wanaweza kufanya wanayofanya wanaume. Ha ha haa yaani hata mifano ya wanyama hawaioni!! Wazee waliosema Wanawake mwalimu wao kipofu walikuwa na maana kubwa sana ambayo sasa imepuuzwa.
Cha mwisho nakukumbusha wewe mwanaume unayenitazama hususani wewe uliegombana na mkeo au mpenzi wako hivi punde chanzo kikiwa hiki kipindi na hii mada yangu. Nataka ujue kwamba uko katika wakati mgumu sana na huyo mwanamke tena nakusihi uwe makini nae sana. Ukipuuza siku moja yanaweza kukukuta kama yaliyonikuta mimi hata kama hautakuwa na ulemavu wa viungo kama mimi. Kuweni makini sana na wanawake wanaume wenzangu kwani hata mwenyezi Mungu ametwambia tuishi nao kwa akili.”
Nilistuka kwa maneno yale na kuhisi kama naambiwa mimi moja kwa moja. Muda mfupi baada ya kile kipindi kuisha nikiwa nimemezwa mawazoni nikijiuliza mwenyewe nishike yapi niache yapi haswa nikiambatanisha na kauli za Mchumbaangu kipenzi.
Mara ujumbe uliingia kwenye simu yangu na nilipoichukua kuufungua alikuwa ni Mariam.
Ujumbe ulisomeka hivi…
“Hussein nashukuru sana kwa matusi yako ya kuwa eti mimi ni muuaji haina shida ila kama ulikuwa hunitaki na ulikuwa unatafutia sababu ungenambia mapema tuu kuliko kunipoteza muda wangu.. Nashukuru sana, usinitafute nakutakia maisha Mema..”
Sio siri ujumbe wa Mamu ulinishangaza. Sikutaraji kabisa kama kile kipindi kinaweza kusababisha yote yale. Niliisoma mara mbili mbili ile 'sms' na kuamua kumpigia Mamu lakini simu yake iliita bila kupokelewa.
Sikuchoka niliendelea kupiga lakini bado haikupokelewa na mara nyengine ilikatwa na mwishoe nikawa nasikia sauti ya huduma kwa wateja wakinambia kuwa namba ninayopiga inatumika.
Niliachana na simu na kuingia bafuni kuoga niliporejea chumbani nikatupia pamba kama kawaida yangu.
Eeeh.. kupendeza ilikuwa kawaida kwangu kutokana na jinsi nilivyojua kupangilia mavazi hadi watu wengi kitaani wakawa wananita bitozi, si unajua tena uswahilini kila 'chocho' unayokata ukiwa 'umejitupia' sana watu macho kodooo.
Nilirejea sebuleni baada ya kujiridhisha kwa nguo nilizovaa siku hiyo na kabla sijatoka nilipiga tena simu ya Mamu lakini jibu lilikuwa lile lile kwamba namba ninayopiga ipo bize.
Sikuwa na jinsi ilibidi nitoke na kuchukua bodaboda kuelekea kwa kina Mariam nikiwa na nia na madhumuni ya kwenda kuomba msamaha ili mapenzi yetu yaendelee kwani nilimpenda sana na nilijua kama nisingeenda muda huo basi ingebidi nisubiri hadi wiki ijayo kwani nisingepata nafasi kutokana na kuwa kazini muda mwingi. Baada ya mwendo wa dakika kumi tulifika maeneo ya kina Mam na kumlipa ujira wake yule dogo aliyenileta nami moja kwa moja nikaanza kuongoza njia ya kwa kina Mamu huku nikiwazia jinsi ya kuanza.

_________________ITAENDELEA..
Hongera sana kwa kazi nzuri,kama unayoyote kwenye PDF naomba unitumie kwa email,wilsongamba825@yahoo.com
 
EPS 22
========

"Mh! mkuu hapaaaa daah!! okeeee.. auuu au alimaanisha kwenye picha?!!"
"Swadakta Kimaro, alichokuwa ananielekeza marehemu Mnyungunyungu nimepata siri ya maana ya hayo maneno kuwa mr.X aliwahi kupiga nae picha na dalili kuu ya kumtambua mr.X ana kovu usoni mwake kwa hiyo itatubidi tuibe siku mapema wiki hii twende mkuyuni tuombe picha zote alizowahi kupiga mzee Mnyungunyungu miaka ya nyuma."
"sawa mkuu sasa tutajuaje jina halisi la mr.X kama tutamgundua kwenye picha kwa ushahidi wa hilo kovu? kumbuka atakuwa kabadilika mno kwa sasa ila jina ndio la msingi zaidi, sasa tutajuaje hapo...?"
"Naam, swali lako ni zuri lakini usiwe na wasi kwani kabla hajafa mzee Mnyungunyungu aliwahi mwambia yule mwanae mganga kuwa mr.X anamfahamu vizuri tu. kwa hiyo tutapoiona picha ya mtu mwenye kovu ktk ulbamu ya mnyungunyungu ndipo tutapomuuliza mwanae yule atutajie majina ya mtu huyo, na alikuwa nani enzi hizo na hapo itaanza kazi moja tu ya kumtafuta."
"hapo mkuu sina swali kabisa, naona mipango imekaa vizuri sana Mr.X lazima afichuke safari hii."
Aliunga mkono st;sajent Kimaro mara baada ya kusikia mazungumzo ya Kamishna wake bwana Shaaban Mwinchande.

* * * * * *

Siku ya siku ilifika ambapo kwa mara nyengine alioneka Kamishna Shaaban na St;sajent Kimaro wakiwa moto chini ndani ya Land cruzer New Model ya kijivu wakipangusa (wakiyapita) magari na kukanyaga barabara ipasavyo kuelekea kijiji cha Mkuyuni mkoa wa Morogoro.
Muda mwingi kila mmoja alikuwa bussy na yake kichwani huku wakipeana story za hapa na pale na walipoianza barabara ya vumbi iliyokuwa inaelekea morogoro vijijini ndipo st;sajent Kimaro alivunja ukimya uliotawala muda mwingi na kuyapamba mazungumzo wakati huo akiendeesha gari.
"Sasa mkuu endapo tukishindwa kuiona hiyo picha ya mtu mwenye kovu usoni unafikiria nini cha kufanya ambacho kitatusaidia zaidi"
"Mh! sidhaani kwa haraka harakaaaa... lakini we umefikiriaje kwani"
"ahkah! mi nakusikiliza wewe bosi wangu niko tayari kutii mipango yako na kufata vile usemavyo."
"Sikia Kimaro, mapigo ya moyo wangu yanadunda kwa furaha furani ambayo naiona dhahili ni ishara ya ushindi na akili zangu zinaniaminisha kabisa kwamba safari hii tutamjua Mr.X tu."
"sawa mkuu lakini inabidi twende tukiwa na mbinu mbadala pia."
"Hebu nishauli mbinu mbadala uliyonayo."
"sawa mkuu, mi nadhani itatubidi tutumie mbinu za kijeshi zaidi kum bana yule mganga mtoto wa mzee Mnyungunyungu"
"Mbinu za kijeshi? kivipi Kimaro."
Aliuliza kamishna Shebby kwa mshangao kidogo huku akimtazama st;sajent Kimaro kwanini amefikiria hilo ilhali walishapanga awali kwamba ktk mission ile hawatatakiwa kujionesha ama kugundulika wao ni kina nani hasa.
"Mkuu kuna kitu nilikifikiria sana toka uliponipa habari ya maneno uliyoyaunganisha aliyotamka marehemu Mnyungunyungu na kunijengea wazo ambalo nahisi kabisa lipo jirani na ukweli ama ndio ukweli wenyewe."
"Wazo lipi hilo tena!! hebu nambie."
"wazo kuwa ni nani anaweza kuwa mr.X"
"Mh! Kimaro acha utani hebu nifafanulie unahisi nini?"
"Akili zangu zinanambia kuwa huenda yule mganga aliyetupokea akawa ndie mr.X mwenyewe"
"Mh! unamaanisha mtoto wa mzee Mnyungunyungu?"
"Haswaa ndie huyo."
"Kivipi sasa hadi umehisi hivyo?"
"kutokana na maneno uliyoyaunganisha aliyosema mzee Mnyungunyungu na ukijumlisha hadithi ya Hussein ukigawanya tukio la barua, namba ya simu hadi kushambuliwa kule kibamba miaka hiyo.. Pia umli wake vile nilivyomuona bado akili yangu inasema kuwa mzunguko woooote uko palepale yule mganga ndie mr.X"
"Daaah! Kimaro leo kweli umeamua kuchemsha kupe walio kwenye ndonga (kichwa) langu, Mh!! lete prove ya kile usemacho."
"Sawa mkuu ninazo sababu, Kwanza kumbuka mara ya kwanza mke wa Hussein ambae ni Zai alipoonwa na baba mkubwa wa Hussein ambae ndie mzee Mnyungunyungu alionesha hali ya mshangao sana hadi kupelekea kumpa maneno ya mafumbo Hussein juu ya yule mwanamke. Hii inanijengea picha kuwa mzee Mnyungunyungu alimtambua Zai mapema kabla ya pale, inawezekana mtoto wake ambae ndie yule mganga nae walishakuwa na mahusiano... kuthibitisha hili rejea kauli za Zai kuwa hajawahi kumkatalia mwanaume aliyemtongoza ila wote akawapa mitihani ktk kumtafuta aliyempenda kweli na walishindwa wote kasoro Hussein aliweza na kumpata Zai so mmoja wa washindwaji anaweza kuwa mtoto wa Mnyungunyungu.
Pili, barua ya Hussein huenda alipewa na yuleyule mganga kwenye daladala na kwa kuwa alizijua dawa nyingi kuna uwezekano barua ile ilibeba nguvu za giza ndani yake na pindi iliposomwa na mke wa Hussein ilianza kumlevya taratibu na kujikuta anaanza kufanya mawasiliano ya siri na yule mganga pasi na kujitambua na hata siku walipokuwa wanaenda kwa ba mkubwa inawezekana waliwasiliana tena kwa msg na yeye ndie aliyemny'ang'anya mtoto Hussein na kumshambulia akishilikiana na wenzake aliowajua yeye vilevile hata Mzee Mnyungunyungu alitoa ushahidi ule kwa kumkingia mwanae kifua na kuificha ile siri na ndio sababu ya kuhama kwao ili kupoteza kabisa habari zile zisije kuzuka tetesi pale kijijini.
Tatu, Kipindi unamuuliza swali marehemu Mnyungunyungu juu ya mr.X kuna uwezekano mlaika mtoa roho alikuwa mbele yake na akashindwa kusema uongo hivyo alitaka kumfichua mwanae na ndio maana ya maneno ANA KOVU USONI.
Na hii ni dhahili kama siku ile hujamuangalia vizuri yule mganga mimi nilimuona vizuri zaidi kuwa ana kovu kubwa tu usoni.
Kwa sababu hizi kuu tatu nina mashaka ya kuthubutu kusema kuwa mtoto wa Mzee Mnyungunyungu ndie Mr.X.."

"Uuuuuuppphhhhhh!!!!"
Alishusha pumzi kwa nguvu Kamishna Shebby huku akimtazama mara mbili mbili stafsajent Kimaro pasi na kumwambia chochote na ukimya ulifuata tena baina yao kipindi Shebby alipotulia na kuanza kuyachekecha maneno na prove alizotoa Kimaro sambamba na hadithi ya Hussein.
Kiupande furani yalimuingia yale maneno na kuzishawishi akili zake kuwa akubaliane na Kimaro lakini bado upande wa pili moyo wake Ulimkatalia kabisa kuwa yule mganga mtoto wa Mzee Mnyungunyungu kuwa ndie Mr.X

** ** ** **

Ilitimu majira ya saa saba mchana ambapo waliwasili kijiji cha Mkuyuni na kupaki gari yao eneo lile lile walipopaki pindi walipokuja awali na pembeni yake kulionekana imepaki difenda ya polisi na gari ya wagonjwa, na baada ya kushuka walivuka barabara na kuelekea moja kwa moja ile njia ya bondeni ambayo walipitishwa siku ile na yule kijana aliyeitwa Chibu.

Lakini cha ajabu siku hiyo hakukuonekana watu wengi eneo lile la stendi huku frem nyingi pia zilifungwa japo ilikuwa mchana na wakati wakishusha kile kibarabara waliwaona watu kwa mbali wengi wengi mbele yao huku wengine wakija nyuma yao na kuwapita wakionesha walikuwa na haraka ya kuwahi kule walipokuwa wanaelekea wenzao.
Hali hii iliwafanya hata wao kuzidisha mwendo ili wawakaribie wale watu wajue kulikoni.
"Wakuu .. wakuu wakuuuu salamualeikuuu waheshimiwaa.."
Ilisikika sauti kutokea nyuma yao ndipo walipogeuka kumuona aliyekuwa anawasalimia ndipo Kamishna Shebby na Kimaro walipotabasam baada ya kugundua alikuwa ni yule mpiga debe wa stend Chibu.
"aaah Chibu. waleikumsalaam vipi kwema."
"Aaah!! ndo hivyo bwana bado tunahema tuko pamoja na nilipowaona mnapita pale chini nikaona si mbaya niikatae tenda ya leo nikajumuike nanyi ndugu zangu ktk harakati za kwenda kumpumzisha mwenzetu."
"Harakati za kumpumzisha mwenzetu? mbona hatukuelewi Chibu?"
Aliuliza St;sajent Kimaro huku Kamishna Shebby akiwa nae kataharuki akijiuliza au ina maana mzee Mnyungunyungu hakuzikwa toka kipindi kile? wakati ilishapita wiki naa.
"Aaaah!! wakubwaa nyie si mmekuja tena kwenye huu msiba au hamuelekei kwa Mnyungunyungu?"
"Tunaelekea huko huko Chibu, sasa huo msiba wa nani tena?"
"Daah!! Mnanishangaza sasa, mi nimejua taarifa ya tukio lililotokea juzi ndio limewaleta huku kumbe sio..?"
"He!! unatuchanganya sasa Chibu kwani kumetokea tukio gani tena.!!?"
"Mnyungunyungu mtoto (jr) mzee wa nyanga na tunguli kakata kamba, yaani amekufa."
"Amekufa? mtoto yupi kwani"
"Mtoto wa Mnyungunyungu wakubwa aliyeachiwa mikoba."
"HAA!! Unamaanisha yule MGANGA?!!"
walistuka kwa pamoja baada ya Chibu kutikisa kichwa kukubaliana na swali waliloliuliza juu ya huyo aliyefariki.
ITAENDELEA..

Dah!

Wale wote wanaowahisi wanaweza kua na ukweli wana kufa tu...

Kaanza Mnyungunyungu, sasa kafuatia mtoto wake... ambae wanahisi ndiyo anaweza kua huyo Mr.X...


Cc: mahondaw
 
Asante Madame. Sometimes Nam suspect Asha.ila tuone mwisho wake
 
Haibooo hadithii hii nimelewa mbayaaa yaan
uki ikosa kdogo tuu unakuta wenzio wako Mbeya we uko Moro kasi yake imetisha
 
SEHEMU YA 51
_________________________

SmS ya Cj4 ilimfanya Shebby ashushe pumzi na kuirudia mara mbilimbili huku moyoni akikili kuwa kuna upana mkubwa sana wa kimbinu na fikra baina yake na Cj4

* * * *

"Twambie nani Mr X na wapi alipo?"
lilikuwa ni swali toka kwa Kamishna Shebby akimuuliza mateka wao yule ambae ni Tyga.
"Sijui unazungumzia nini"
alijibu Tyga kwa kujiamini mbali na kuwa uso wote ulikuwa umechakaa hata hakuweza kuona vizuri kutokana na uvimbe na damu zilizokuwa bado zinamvuja.
"Narudia twambie wapi Mr X alipo na ni NANI??"
"Nimeshasema sijui unamaanisha nini wala sijawahi sikia hiko kitu"
bado aliendelea kutia ngumu Tyga wakati huo Cj4 alikuwa anasikia kile alichokuwa anajibu Tyga lakini alimuacha Shebby aendele kumuhoji huku upande wake binafsi alikuwa na mtu mmoja akimuhabarisha kinachoendelea nae si mwengine ni mkuu wa majeshi tu.
"Nani Mr X??????"
"SI-JU-I"
Mabishano yaliendelea ambapo safari hii Cj4 aliamua kutoka kule nje alipokuwa na kurudi speed hadi kwa Tyga bila kumuuliza kitu chochote alichomoa kisu chake cha kikomandoo na alipomfikia Tyga tu alikamata sikio na kulikata lote palepale mbele ya Kamishna Shebby aliyekuwa anatumia maneno mengi kumuhoji Tyga.
"Aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaghhhhhhhhhhh"
Alipiga yowe la maumivu Tyga mara baada ya Cj4 kumpangusa sikio na kulieka mbele yake pasi na huruma.
"Sasa Muulize tena kama atakuwa hasikii vizuri au haelewi nakuja baada ya dakika kumi kumalizia la upande wapili"
Aliongea Cj4 na kunyanyuka tena kwenye sehemu ile waliyoiandaa mapema kipindi wanasuka mchezo wao wa kumnasa Mr X hivyo ndani ya lile gofu haikumaanisha tu waliingia kwa dharula ama walibahatisha. bali walikuwa walipaandaa mapema kwa kujua lazima Mr X atatuma mtu wake wa kummaliza Hussein bubu.

Kitendo cha Cj4 kumkata kwanza sikio Tyga bila kutumia muda wa kubembeleza kumsemesha wala kumuuliza kidogo kilimstaajabisha Shebby ambae yeye hasira zake muda wote zilikuwa kwa Ninja wa kike ambae Cj4 alimuacha aende.
Maumivu yalikuwa makali sana kwa Tyga lakini bado msimamo wa kumficha Mr X ulikuwa palepale hali iliyomtia hasira zaidi na Shebby aliyeamua kumzibua sehemu za sikio zilezile zilizokuwa zinarusha damu na kupelekea Tyga kupoteza fahamu.
"Huyu atasema kweli?"
aliuliza Shebby kwa kuhisi kuwa yule mateka wao anaonesha yuko tayari kabisa kufa kuliko kusema ukweli kuhusu mr X
"Kwa kuwa ana mdomo atasema tu kile anachokijua kweli, ukimshindwa utanambia nije nimsemeshe"
alijibu kwa kujiamini Cj4 na kuingia tena mmule ndani alipozimia Tyga.
Lakini alipokuwa anamsogelea kumkaribia pale chini alisikia mlio wa kitu mithili ya alarm ya saa ya kimulimuli ikibeep kwenye mavazi ya Tyga ambapo alimpekua harakaharaka ndipo alipostuka baada ya kugundua kumbe kwenye lebo ya nyuma ndani ya kola ya gwanda ile ya kininja aliyovaa Tyga kulikuwa na maneno madogo ambayo kumbe yalishonewa na wire wenye signal maalum za bomu la kuendeeshwa na rimoti... Yaani lile vazi zima la Kininja lilitengenezwa kwa nyuzi maalum za baruti nyeusi ikiwa na maana combat aliyovaa Tyga lilikuwa ni bomu.
Hii ilimstua na kumshangaza Cj4 kwa kuhisi kuwa hata yule Ninja mwenyewe hakuwa anajua kama amevaa bomu muda wote na sasa namba zake zimeingizwa kwenye systim na rimoti imewashwa na ishaanza kuhesabu japo pale haikuwaonesha itahesabu kwa dakika ngapi.
"Tokaaaa Shebby Rukia nje harakaa Tokaaaaa"
alikimbia Speed kutoka nje Cj4 na kumkamata Kamishna Shebby kuruka nae kwa nje ya ile nyumba pindi alipokuwa anashangaa Cj4 alipokuwa anampigia kelele za kutaka arukie nje wakimbie eneo la kile kibanda.

Waliangukia mita kumi na lile gofu huku Shebby akiwa bado haelewi, Cj4 alimshika tena mkono na kuanza kukimbia nae pamoja kuelekea mbali zaidi na lile gofu.
"CJ....Vi....."
alitaka kuongea kitu Shebby lakini kabla hajamalizia alistushwa na kishindo cha mlipuko kutokea nyuma yao na alipogeuka hakuamini kuona gofu lile alilokuwemo mateka wao likisambaratika kwa moto.

"Shiit Cj4 ina maana umeamua kumlipua!!?"
aliuliza kwa mshangao Kamishna Shebby pindi alipokuwa anashuhudia ule mlipuko uliowasha moto ghafra kule kwenye gofu walilomfunga mateka wao Tyga.
"Huu sio muda wa kuuliza Kamishna bado tupo kwenye mchezo wa Mr X japo na sisi tumeanzisha mchezo wetu ndani yake tuondoke hapa haraka."
aliongea Cj4 na kukimbilia kule ilipo gari yao sambamba na Shebby na kujitoma ndani yake ambapo safari hii dereva alikuwa Cj4 mwenyewe.
"Lakini kwa nini umemlipua?"
"Mimi sie niliyemlipua ila ni Mr X mwenyewe"
"Mr X?? Kamlipua lipuaje sasa"
"Kwa kutumia akili za siku nyingi kabla hajatafuta wachezaji nyota wa kuucheza mchezo wake"
majibu ya Cj4 si kwamba yalikuwa yanamsaidia Shebby kutatua maswali aliyokuwa nayo, bali ndio kwanza yalikuwa yanampa maswali mapya ambayo yalikuwa yanamuonesha mwanga jinsi ya kutafuta majibu pasi na kuuliza tena.
"So what is Next..?"
aliuliza Shebby japo alihisi wanaenda kwa Hussein bubu ila alitaka kujua kama itawalazimu wamuhamishe ama waendelee kumtega palepale lakini jibu la Cj4 lilizidi kuonesha tofauti baina ya KOMANDOO wa JESHI na KAMISHNA wa POLISI.
"Next mimi nitadili na Hussein wewe pitiliza alfajiri hii hii kwa mchumbaako na umuhamishe pale anapoishi haraka kwa usalama zaidi"
"Mchumbaangu? Ina maana dokta Asha?"
"Ndio hivyo, all the best Kamishna"
Alijibu maneno haya Cj4 wakati huo tayari gari ilifika pale Mbagara karibu na ile hoteli kulipoonekana kun mkusanyiko wa watu na maaskali polisi hususani sehemu ile ya nyuma kwenye bustani.
Alishuka Cj4 na kumuachia usukani Shebby ambae alikuwa bado anayatafutia ufumbuzi majibu ya maswali ya Cj4 huku akipiga gia kuelekea kwa mchumbaake kwa kufata kauli ya mtu aliyeamini kwa moyo mmoja kuwa amemzidi mbinu na akili ya vita.

Lakini ukweli ni kua Cj4 alibaini mchezo uliotegwa na Mr X kwa wale Maninja wake hasa alipowaona wanapambana usiku wake sare zao zilishabihiana karibu kila kitu na kubaini kuwa matereo ndio yaleyale na system ndio ile ile hivyo kuna uwezekano mkubwa na yule Ninja mwengine akalipuliwa na mavazi yake ambayo aliamini wazi kuwa hajui kama ni bomu.
Na kwa kuwa alihisi kwa asilimia kubwa kuwa yule Ninja ni mchumbaake Shebby aliyevaa kivuli cha Dokta Asha na yote hayo aliyabaini kupitia maongezi yao wenyewe pindi walipokuwa wanapambana bustanini.
Hivyo aliamini kama asipoenda mtu kumtoa kule basi maisha yake nayo yatakuwa hatarini.
Aliamka asubuhi ile Asha na kujichoma tena sindano ya kuua maumivu kabla hajatoka kuelekea chini akiwa na maana ya kufanya mazoezi ya kutembea kwa kupandisha ngazi na kutroti kidogo ili kukipa shurba kidonda chake kibichi kisijivute na kumfanya astukiwe na watu kama alikuwa na jeraha mwilini mwake.
Alivaa full tracksuit na kwa jinsi alivyokuwa anatembea kwenye ngazi mara baada ya kutoka chumbani kwake ilikuwa ni vigumu mno kumtambua kama ana jeraha la mshono mwilini mwake.
Mazoezi ya kupanda na kushuka ngazi yaliendelea wakati huo bado mamaake alikuwa hajaamka na kutoka chumbani kwake.

Akiwa anafanya yale mazoezi mepesi ya kupanda na kushuka vingazi mulemule ndani bado mawazo yalikuwa mengi sana kichwani mwake Asha hususani kuhusu kifo cha Mr X.
Hakuwahi kumuona alivyo wala kujua wapi alipo hata historia yake alikuwa haijui zaidi alichojua kipindi cha nyuma kuwa mr X ni mtu mwenye kutetea haki za watu na kuwasaidia na kuwafichua wabaya na ndio sababu ya kuwa na maadui waliokuwa wanataka afe ili akosekane mtu wa kuwafichua na kusaidia wengine.
Awali aliamini hayo lakini sasa ameujua ukweli kuwa wote waliokuwa wanamtafuta mr X kwaajili ya kumuua walikuwa sahihi kabisa.
Lakini ugumu unakuja ni kugundua picha halisi ya mr X na jina lake halisi ama hata wadhfa aliowahi kuwa nao kwani ingesaidia kumgundua na kumpata kiurahisi.
"Mwisho wako unakuja... Mwisho wako ndio huu, Mwisho wako unakuja , Mwisho wako ndio huu"
aliongea haya maneno Asha kwa hisia huku akiwa kama anaimba pale alipokuwa anapandisha ngazi na kushuka.

Lakini mara akiwa bado anapandisha na kushuka pale kwenye ngazi ndipo aliposikia mlio wa kitu cha alarm ukitokea chumbani kwake kama vile alivyokuwa anasikia Cj4 na kumfanya Asha asijue Alarm ile ni ya nini kwa kuwa yeye hajawahi kuset alarm yenye mlio kama ule.
Alianza kupandisha taratibu kurejea chumbani kwake kuangalia hiyo alarm ilikuwa ya nini, lakini akiwa anapandisha kabla hajaufikia mlango wa chumbani mwake alijikuta moyo unamuenda mbio na kusita kuingia kwanza na kusimama mlangoni kusikilizia akiwa anajishauli inapotokea hiyo alarm na kupata hisia ni pale kitandni alipozivua nguo zake za Kininja usiku aliporudi na hapo kidogo alijipa moyo kuwa hakuna kitu kibaya na ndipo alipotaka kufungua mlango lakini Hamaaaaaadiiiii.......!!! Alirushwa yeye na Mlango baada ya mlipuko wa ajabu kutokea ghafra mule chumbani na kumstua hadi mamaake aliekuwa analala chumba cha chini.
''Aaaaaaaaaaaaaaaaaghhhhhh''
ITAENDELEA..
 
SEHEMU YA 52
_________________

"Ashaaaa!!! Ashaaaa Ashaaa Mwananguuuu Jamaaaaniii msaadaaa...
Motoooo Moootoooo"
alipagawa Zena huku akimbuluza Asha kwa nje kumtoa pale alipodondokea na kwa bahati nzuri alidondokea kwenye Sofa huku ule mlango uliofatuka kwa mlipuko na kurushwa sambamba nae ukiwa umedondokea sakafuni na hapo ndipo moto ulianza kukamata zuria pale chini taratibu.
"Jamani msaaadaaaaaa aaaaaah"
alipiga yowe Zena lakini kumbe mlinzi pale getini alishatimua mbio muda mrefu mara baada ya kishindo kizito kilichosikika upande ule wa juu ya nyumba chumbani kwa Asha sambamba na fungu la moto lililofumuka angani mithili ya wingu na kushuhudia hadi vigae vilivyokuwa upande ule vikifumuka kwa mlipuko ambao uliwatisha hadi majirani na wapita njia waliokuwa karibu na eneo lile.

Akiwa anahangaika mwenyewe Zena kumvuta Asha huku akiogopa hali ya usalama mule ndani mara baada ya moshi kuanza kutanda hususani na ule moto ulioshika zuria kuzidisha kasi yake ya uwakaji, alizidi kuchanganyikiwa Zena na kulia kama mtoto mdogo hasa kila alivyomtazama Asha alikuwa kalegea mwili mzima hasemi wala hatazami.
"Ashaaaa mwaanaaanguuuu Ashaaaaa amkaa mamaaaa"
hakuweza kum beba kutokana na umli na nguvu chache alizokuwa nazo Zena lakini hakuweza kumuacha pia alijitahidi kumnyanyua sehemu za juu na kumbuluza vivyo hivyo kuelekea mlango wa kutokea nje mara baada ya kuona msaada umeenda kombo.
Lakini mara ghafra mlango ulifunguliwa kwa nguvu na mwanaume aliingia huku akiwa kachanganyikiwa mno haamini kile alichokuwa anakiona.
"Ashaaaaaa ASHA Wanguuu"
alitoa ukelele wa maumivu na mshangao Kamishna Shebby mara baada ya kuingia na kumkuta Zena akimkokota Asha aliyekuwa katika hali mbaya huku sehemu zake za chini ya tumbo kukionekana damu kumvuja kwa wingi.
"Mama Tangulia haraka nje kabisa Usishike hilo geti la mlangoni niachie mimi"
alinena Shebby na kutoa tahadhari ile huku akimnyanyua Asha mara baada ya kuona cheche zikizidi kwenye socket za umeme mule ndani na ule moto wa kwenye zuria ulianza kudaka masofa na mapazia makubwa yaliyokuwa Dirishani pale Sebuleni.

Alinyanyuka huku akiwa kam beba Asha Kamishana Shebby na kutoka nae haraka haraka na kuelekea alipopaki gari kule nje na kumkuta Zena akiwa kasimama huku ameeka mikono kichwani.
"Mama ingia kwenye gari twende mamaaa"
aliongea Shebby kwa sauti ya kazi zaidi kutokana na uchungu aliokuwa nao na kumfanya Zena afungue mlango wa nyuma na kutangulia kukaa pindi Shebby alipomuingiza Asha na kumlaza huku mapajani mwa Zena, ndipo baada ya kuufunga mlango Shebby alizunguka upande wake haraka na kuingia ndani ya gari kuondoka eneo lile ambalo tayari moto ulianza kuwa mkubwa kule kwenye ile nyumba na watu walianza kuzongea huku wengine wakipiga simu sehemu za usalama wa zimamoto kitu ambacho Zena na Shebby hawakukikumbuka wala kujali zaid walichanganyikiwa na hali aliyokuwa nayo Dokta Asha.
("Mr X MR X lazima nikuue lazima nikuue na Ninja wako malaya wako unayemtumia lazima nae Nimuueee Lazimaaa damu ya mchumbaangu ilipwe hata kama atabaki hai..")
aliwaza moyoni Shebby huku akiendeesha gari speed kuwahi hospitali kuokoa maisha ya mchumbaake kipenzi, mkewe mtarajiwa, thamani ya moyo wake hasa alipokuwa anakumbuka alivyotibiwa mguu wake, mwanamke aliyeamini ndie mke bora wa kumuoa kutokana na sura yake ya bashasha, upole na upendo wa dhati aliomuonesha kipindi anamtibu.
Nae si mwengine ni Dokta Asha ambae mpaka muda huo Shebby hakujua kuwa yule ndie Ninja wa kike aliyekuwa anatumiwa na Mr X.

* * * *

Kelele za watu pamoja na ving'ora vya polisi vilivyokuwa vinasikika upande wa chini ya jengo la Hoteli ile ndio zilizomsababisha Hussein bubu aamke alfajiri ile na kuelekea usawa wa dirisha la chumba chake kile alichopangiwa na Shebby kwenye ile hoteli.
Alishangaa sana mara baada ya kuona umati wa watu wengi sambamba na polisi wakiwa eneo la bustani kubwa iliyokuwa nyuma ya ile hoteli usawa wa vyumba vile vya upande aliokuwepo.
(He!! Nini tena kimetokea?")
alijiuliza mwenyewe kimoyo moyo baada ya kuona kuna ambulance iliyokuwa inapakia miili ya watu wawili iliyokutwa imeuawa mahala pale pa bustani alfajiri ile hali iliyomstua zaidi Hussein na kuamua kuvaa nguo zake harakaharaka ili apate kwenda kule chini akajionee mwenyewe kilichokuwa kinaendelea.

"Nini kimetokea hapa?"
alimuuliza swali bwana mmoja baada ya kushuka chini na kupenya penya kwenye jopo la watu mpaka alipofika nyuma ya yule bwana aliyekuwa amesimama sehemu za mbelembele kulipozungushiwa warning tape za police kutoruhusu mtu yeyote kusogea eneo lile la tukio zaidi ya wana usalama waliokuwa wanafanya kazi yao ya upelelezi na utafiti wa kina kujua kilichowasibu wale maiti waliokutwa pale.
"Kuna walinzi wameuawa hapa"
alijibu yule bwana
"Walinzi...!!"
alitaharuki Hussein
"Eee, bwana walinzi wamevamiwa na watu wasiojulikana na kuchomwa na vitu vya ncha kali shingoni kila mmoja"
"Kwani walikuwa wangapi?"
"wawili"
"na walinzi wengine je?"
"Wengine walikuwa upande wa mbele kule naona hawajasikia wenzao wlipokuwa wanauawa"
"Duh! kwa hiyo hao majambazi wamefanikiwa na kuiba?"
"Dah! ndugu yangu hata mimi mwenyewe mpita njia tu sio msemaji wa hoteli wala polisi we sikiliza tu fatilia utajua kila kitu"
Alijibu yule bwana mara baada ya kuona maswali ya Hussein yanazidi kuwa mengi.

Aliangalia huku na huko Hussein huku akiwa na maswali ya wale watu waliovamiwa upande ule wa nyuma ambao ulinzi ulikuwa mchache kutokana na kutoonekana kuna thamani kubwa ya kuchukua zaidi eneo lile lilikuwa kama la kupumzika wageni tu, tofauti na eneo la mbele ambapo pia kulikuwa na parking kubwa ya magari na ndio kulikuwa na mashine za ATM na milango ya kuingilia mule hotelini.
("sasa hawa majambazi gani wamevamia na kuua watu upande huu huku kukionekana hakuna madhara menggine yoyote upande wa mbele? Mh! itakuwa visasi tu hivi sio bure")
aliwaza Hussein huku anaangaza macho huku na huko na mara alipogeuka kwaajili ya kuondoka pale kuna mtu alimuona upande wa pili aliyemstusha kidogo macho yake.
("Haa!..!>>!)
alipigwa bumbuwazi huku akiwa haamini kama mtu anayemtazama pale ndie au sie na kuanza kusogea haraka ili avuke barabara eneo lile la upande wa pili kumuwahi kabla hajaondo kwani ni mtu ambae alikuwa anamkumbuka vizuri sana na alipomuona moyo wake ulistuka na kubadilisha mapigo kwani hakuwahi kufikiria kama atamuona tena mtu yule ambae sasa alikuwa mita chache tu mbele ya macho yake.
ITAENDELEA..
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (53)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_____________________
______________

Alikuwa ni Cj4 nae alishamuona Hussein muda mwingi tu japo alijifanya kutomuona na katika hali ya kumzuga na kumpoteza maboya alisubiria roli moja ambalo lilikuwa linapita pale barabarani pindi lilipowaziba tu baina yao alizunguka haraka na kuingia kwenye ile nyumba ya wageni ambayo ndio alikuwa amefikia na kupandisha juu chumbani kwake mpaka dirishani na kuanza kumuangalia Husein ambae sasa alionekana kutamtafuta.

("Mh!! kaendea wapi sasa yule kijana!!?")
alijiuliza Hussein kipindi akitafuta na kutomuona Cj4 ambae alichokuwa anakumbuka yeye ni kwamba alikuwa mfungwa mwenzake kule gerezani ambae nae alikuwa na mkasa kama wake na hata alipoingia gerezani kwa mara ya kwanza alikuwa na maneno kama yale yale aliyoyaamini yeye kuwa Wanawake ni Wauaji lakini kilichokuja kumshangaza baada ya kuzoena nae alikuja kutoweka kwa kutoroka jera na jitihada zilifanywa za kumtafuta lakini hadi anatoka gerezani alikuwa hajapatikana wala hata dariri za kuonekana kwake.
("Mh! mbona maajabu haya, au mzimu!!)
alijisemea moyoni Hussein mara baada ya kuona hakuna hata dariri ya uelekeo wa yule mtu aliyekuwa amekusudia kumfata pale na kuamua kugeuza kurudi tena kule hotelini.

Lakini wakati wote huo Cj4 alikuwa anamtazama Hussein na kumfanya atabasam kw vile Hussein alivyoonekana kuhaha kwa kumtafuta yeye bila kujua ameelekea wapi wala kutambua kama yuko nae pale kila siku.

* * * *

Kwa speed ya hatari yenye umakini wa ajabu Kamishna Shebby aliweza kuiingiza gari mpaka hospitali kuu ya Jeshi la polisi Kilwa road na pindi gari iliposimama walikuja watu wa machera haraka haraka kutokana pia na kuitambua gari ile ilikuwa ya nani na aliposhuka tu ndio kabisa huduma za kumtoa Asha garini zilifanywa haraka sana na kwa umakini mkubwa.

Alionekana kudata Kamishna Shebby huku akiwa anazunguka zunguka wodini pindi Asha alipoingizwa chumba cha upasuaji bada ya kutolewa taarifa kuwa alirushwa na mlipuko hivyo madaktari walihisi huenda pia kuna vyuma au vibati vimeingia mwilini mwake hususani sehemu ya tumbo kulipooneaka kuvuja damu kwa wingi.
("Ama zako ama zangu.. ama zako Ama zangu..")
alirudia rudia Shebby maneno haya huku akiimaliza korido na kurudi mwanzo akifika mwisho anarudi tena mwanzo huku kichwa kakiinamisha wakati huo Zena alikaa kwenye viti vya kusubiri wagonjwa akilia kwa uchungu.
Baada ya nusu saa alitoka Dokta mmoja kwenye chumba cha upasuaji.
"Vipi Dokta?!"
aliuliza Shebby kwa mshtuko huku akiwa na shauku ya kujua kilichoendelea kwenye kile chumba cha upasuaji.
"Usijali mkuu, maendeleo ni mazuri tu inaonesha zaidi alipata mshtuko wa moyo uliosababisha presha kuwa chini sana lakini hana majeraha makubwa wala mwilini mwake hakuna kipande chochote cha chuma au chenye ncha kali, kwa sasa wanarekebisha mshono aliokuwa nao ambao ndio ulifumka na kumsababishia damu nyingi kuvuja"
majibu ya yule Dokta yalishusha presha aliyokuwa nayo awali Shebby kwa kiasi kikubwa na ndipo alipomfata na mama (Zena) kumuelezea lile na kumtoa wasiwasi kisha alimuachia kiasi cha ths laki moja kwa niaba ya dharula yoyote itayojitokeza pale nae aliahidi kurudi baada ya muda mfupi ujao.
Alitoka na kuingia kwenye gari huku mawazo yake kichwani yakiwa kwenda kukutana na Cj4 ambae alizidi kumuona mchawi wa mbinu kwa kugundua vitu ambavyo yeye hakuvifikiria.

Lakini akiwa njiani alikumbuka vizuri maelezo ya yule daktari pindi alipotoka chumba cha upasuaji na alipoyafikiria vizuri maneno yake kuna kitu kimoja kilianza kumchanganya na kutoelewa.
("Mshonooo, mshonooo. Mh!! mbona sikumbuki kama Asha aliwahi kuwa na mshono. mshonooo!!.. mshono gani tena huo?!!")
aliwaza Shebby na kujiuliza mwenyewe pindi alipokuwa njiani baada ya kukumbuka vizuri maelezo ya yule daktari.

* * * *

"Huwezi amini Cj yaani kabla hata sijafika kwenye ile nyumba kwa macho yangu nilishuhudia mlipuko upande wa juu na nilipoingia sikuamini hali niliyomkuta nae Asha .. Daaah!! Mr X naamini nitapomuua nitapata thawabu Dah!"
aliongea Shebby mara walipokutana kwa siri na Cj4.
"Kwa hiyo mchumbaako vipi?"
"Mungu amesaidia nimemuacha hospitali kwa matibabu zaidi ila kuna kitu sijakielewa"
"Kipi hiko?"
"Nimeambiwa jeraha lililokuwa linavuja damu tumboni kwa Asha ni la mshono.."
aliongea Shebby kauli ambayo Cj4 aliichekecha harakaharaka na kupata uhakika sasa kua mtoto wa Hussein ambae ni mke wa Kamishna Shebby ndie yule Ninja aliyemsaidia usiku baada ya kuchomwa na kisu cha kininja tumboni hivyo alijua mshono unaozungumziwa pale laima atakuwa amejishona mwenyewe usiku uliopita na kutokana n msukosuko wa bomu umefumka.
"Sasa neno Mshono limekuchanganya nini? mbona mi naona kawaida."
alijibu Cj4 kwa kumzunguka Shebby kwani hakutaka kabisa agundue mapema mchumbaake ni nani.
"Sikia Cj, sijawahi kumuona na mshono Asha wala hajawahi kunambia hiko kitu."
"hahahaha, tatizo Shebby unapanik mapema, nataka ukumbuke kuwa mshono unamaanisha sehemu ambayo iliwahi kufumka ikazibwa upya. sasa unajuaje kama kipindi cha nyuma mchumbaako aliwahi kufumka sehemu hizo?"
"Mh! sasa ndio uachie na kuvuja damu?"
"Inawezekana kishindo kilikuwa kikubwa.. Ila mi nataka nikushauri kuwa fanya jitihada mapema tu umuoe Asha"
"Mh! Cj mi naona kwanza tumalize hili la mr X"
"Hapana, unajua mr X anatumia akili na mambo yake mengi aliyaeka kwenye mipango kabla hayajatokea. sasa ili akuchanganye anataka kudili kwanza na watu uwapendao. Ndio maana nakwambia muoe kwanza Asha mueke jilani harafu hapo sasa hata mr X mwenyewe utakuwa umeshamzunguka"
Ushauli wa Cj4 hakuutarajia kabisa Kamishna Shebby lakini hakutaka kuupinga kwani moyo wake tayari ulikuwa unamuamini sana Cj4 na kumkubali hivyo aliongea na wazazi wake ambao walikubali lifanyike hilo jambo haraka hususani mzee Mwinchande limpongeza mno mwanae kwa maamuzi aliyofikia lakini kwa kile kilichotokea kwa Asha Shebby alizificha taarifa zile nyumbani kwao kwa kuogopa kuwatisha pia kwa kuzingatia ushauri wa awali aliopewa na Cj4 na hata Hussein babu bubu hakuambiwa kilichompata mwanae zaidi ya kuja kusikia habari za nyumba kuwaka moto huku akidanganywa ni kwa shoti ya umeme kipindi ambacho wakazi wote (Zena na Asha)
hawakuwepo pale nyumbani.

* * * * *

Siku ileile masaa machache baada ya Shebby kuondoka Asha alirejewa na fahamu wakati huo tayari madaktari walikuwa wamemaliza kumshona vizuri sehemu ile ya chini ya tumbo kulipoachia.
Kutokana na kupungukiwa damu ililazimika kuongezewa chupa nne za damu na usiku huo alilala pale wodini huku upande wa Shebby alihaha na kufanikiwa kuwakodia nyumba nyengine nzuri maeneo ya jilani na ile hoteli aliyopngiwa Hussein kwa kujua kuwa pale amewaeka kwenye usalama kwa uwepo wa rada za Cj4.

Baada ya kila kitu kuwa sawa upande wa Cj4 siku hiyo asubuhi na mapema alitoka kinyemela pale alipokuwa anaishi pasi na kumuarifu Shebby na alielekea kule hospitali akiwa amevaa sare zake za kipolisi zilizomtambulisha kama Inspecta na kufanikiwa kuingia wodini kumuona mgonjwa ambae siku hiyo ndio ilikuwa siku yake ya kuruhusiwa.
Hakukuwa na vizuizi wala maswali mengi pindi alipotaka kukutana na yule mgonjwa, ila kukaibuka mstuko na taharuki kubwa kutoka kwa yule mgonjwa ambae ni Asha pindi alipokutanisha macho na Cj4 ambae nae alistuka kidogo baada ya yale macho kuyakumbuka vizuri siku ile ya ajali ya kule chalinze ambayo ilipelekea kupoteza kwa maisha mtu muhimu aliyetakiwa kuhojiwa juu ya upelelezi wa kum baini Mr X.

ITAENDELEA...
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (54)
BY - MTOTO WA BECKER (TheSpecial Thinker)
______________________
____________

Asha alijitahidi kuificha hali ile ya mstuko wake machoni lakini Cj4 alimgundua vizuri sana na kwake yeye hakuonesha mstuko wowote machoni zaidi ya kumsogelea na kumpa pole kabla hajaanza kumuuliza maswali ambayo Asha alibaki kama bubu asijue aanzie wapi kuyajibu.
"Hebu nambie unajua nini zaidi kuhusu mr X, wala usinifiche ila nataka unijuze mr X alikupa neno gani la mwisho pindi ulipoasi?"
Aliuliza Cj4 kwa sauti ya chini sana lakini iliyosikika vizuri masikioni mwa Asha na kubaki anababaika aanzie wapi na hapo ndipo Cj4 alipomuachia kikaratasi cha namba za mawasiliano kisha akatoka taratibu na kumuacha Asha ametumbua macho kwa taharuki.
("Khaa! huyu si ndio yule Afande wa Chalinze? kajuaje kama niko hapa? kajuaje mambo yangu na Mr X?")
alijiuliza maswali haya Asha ambayo alijua fika kuwa hakuna mtu wa kumfata moja kwa moja akampa majibu yale bila yeye mwenyewe kuyatafutia ufumbuzi kupitia yule yule mtu.

Baada ya masaa mawili Kamishna Shebby nae alifika pale hospitali na kufanya utaratibu wa kuwatoa na kuwapeleka kwenye makazi mapya aliyowatafutia.
"Mama kwa sasa mtakuwa hapa kipindi tunafanya taratibu za kumaliza hili suala la ndoa, nataka Mungu akitujaalia tulifanye hata wiki ijayo"
"Wiki ijayo?"
"Eeh mama"
"Atakuwa kashapona vizuri kweli!?"
aliuliza kwa mshangao yule mama kutokana na kuona mambo yamekaa jilani sana tofauti na alivyodhani baada ya Asha kupatwa matatizo
"Kwa hilo usijali mama, kama yeye alivyoniuguza na tukakaa wote hadi kuwa wachumba basi nami nitamuuguza tukiwa wote kama mtu na mkewe, naamini Mungu ndie anayetupangia tukutane aktika vipindi vigumu vya mataaizo kama hivi"
aliongea Shebby maneno ambayo Zena aliyaelewa na kukubali
"Lakini naomba mjitahidi baba asijue kama ana mshono mwanae mtamchanganya"
aliwakumbushia nao walikubali jambo lile na Hussein bubu hakuambua kujua ukweli juu ya kilichompata Asha zaidi ya kujua makazi mapya na kuingojea hiyo siku ya kumuoza mwanae kwa udi na uvumba.

Kwa upande wa Asha ilikuwa ngumu sana kwa kumtazama tu ukagundua kuwa ana jeraha mwilini mwake kwa jins vile alivyokuwa anajichangamsha na kujiweka lakini kuna kitu kimoja kilimuumiza akili zake na kuufanya usiku ule wa kwanza kwenye yale makazi mapya kuwa mgumu sana upande wake na si kwa sababu ya kufikiria juu ya ndoa bali ni kwa sababu ya ule ujio wa askali ambae anakumbuka alionana nae siku ile aliposababisha ajali iliyopelekea kifo cha mzee Cypilian.
Alishangaa kila alipomuangalia Shebby hakuonesha dariri zozote za kumstukia zaidi alipowahi kumuuliza juu ya mshono kule hospitali nae alijibu aliwahi kweli kufanyiwa upasuaji mdogo wa kidole tumbo (appendex) wiki za karibuni na alifanya siri ili asimtie hofu mamaake na uongo huo Shebby aliuamini kabisa.
Usiku huo Asha hakuwa na jinsi ilibidi amtafute hewani yule askali na kweli alipopiga tu zile namba Cj4 alipokea na baada ya kujua anayeongea nae alimuuliza swali lile lile na Asha hakuwa na jinsi ilibidi aongee yote anayoyajua na kumpa lile neno la mwisho aliloambiwa na mr X ambalo lilikuwa sawa kabisa kama alilowahi kuambiwa amwambie Shebby.

* * * *

Mipango ya ndoa ya Kamishna Shebby na Dokta Asha ilizidi kushika kasi kwenye vichwa vya wanafamilia ambapo kwa upande wa mzee Mwinchande na mkewe ilikuwa ni zaidi ya furaha na walifanya utaratibu na kuongea na sheikh mkuu wa jiji la Dar ndie aje kuwa mfungishaji Ndoa hiyo ambayo Mwinchande alipania kuifanya iwe ya kipekee sana japo mipango yake ilikuwa ni ya muda mfupi.

Na hatimae baada ya maandalizi yote kukaa katika mstari (kuwa sawa) Kamishna Shebby alikutana tena kwa siri na Cj4 siku moja kabla ya ndoa kwa maongezi maalum.
"Sikia Shebby, kesho ni siku kubwa sana na muhimu katika kujua muelekeo wa Mr X"
aliongea Cj4
"Kivipi kiongozi"
"Kumbuka neno la mwisho la mr X uliloambiwa na yule Ninja."
"Yap nakumbuka lile fumbo"
"sasa kwa kuwa kesho kutakuwa na wageni wengi kwenu wanaokutambua nina wasiwasi kutakuwa na ugeni wa Mr X pia kwa kuwa anakutambua. Na hii ndio inanifanya na mimi kuja kwenye hiyo sherehe lakini hakuna atayejua kama nimekuja zaidi yako lakini pia nawe hutoniona kama nimekuja lakini nitakuja."
alichanganya maneno Cj4 na kumfanya Shebby akubali lakini asijue maana halisi ya maneno yale zaidi alipata picha kuwa kuna uwezekano kweli mr X akahudhulia hiyo sherehe au akatuma mtu wake kwaajili ya kuwamaliza katika hiyo sherehe ya harusi iliyotarajiwa kufanyika kesho yake.

"Kitu chengine Shebby umepangaje kuhusu Hussein akitoka hapo hotelini?"
aliuliza Cj4
"Nimepanga nikamnunulie nyumba sehemu salama."
alijibu Kamishna Shebby kauli iliyopingwa na Cj4
"Hapana Shebby, hakuna nyumba iliyo salama kwa Hussein kabla ya kifo cha Mr X"
"sasa Unanishauri vipi kiongozi"
"Inabidi ukae na wazazi wako uwaombe waishi na Hussein pale kwenu kidogo hiyo itakuwa salama kwake"
"Kwa hiyo unananambia Hussein akaishi nyumbani ndo itakuwa salama?"
"Ndio hivyo nionavyo"
"Sio kama nitasogeza maadui wanaomuinda nyumbani?"
"Hapana Shebby, hiyo ndio njia ya msingi"
"sawa kiongozi"
Kamishna Shebby alikubali tena swala la pili lililotolewa na Cj4 na kuagana huku wakitakiana kila la kheri hiyo kesho yake ambapo Cj4 atakuja kwa ngazi maalum ya kuwachunguza wageni wataofika ili apate kumtambua Mr X.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 55
______________________

WANAWAKE NI WAUAJI..!? (55)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_______________________
_______________

* * * * *

Wageni na viongozi mbalimbali waliendelea kumiminika katika ukumbi maalum uliokodiwa kwa niaba ya sherehe za kuwapongeza bwana Shaaban Mwinchande na bibi Asha Hussein kwa muungano wao wa kimwili na kuwa kitu kimoja kama ilivyo katika maandiko yaani mke na mume.

Ilikuwa ni majira ya saa kumi jioni mara baada ya ndoa iliyofungwa majira ya saa nne asubuhi katika Msikiti mkubwa kabisa jijini chini ya Sheikh mkuu.
Ilikuwa ni furaha sana kwa kila mtu hususani Hussein yeye muda wote alikuwa na leso akifuta machozi kwa kutoamini kama leo amefanikiwa kumuoza mwanae kwa mtu ambae alitokea kuwa chachu ya yeye kutolewa jera.
Ilikuwa ni furaha kwenye sherehe ambayo kweli ilikuwa ya kipekee na wageni walikuwa wengi sana kuanzia viongozi wastaafu waliokuwa na urafiki mkubwa na mzee Mwinchande miaka hiyo pamoja na viongozi wa usalama hususani jeshi la polisi na magereza.
Bila kusahau wageni wengine tu waalikwa ambao wao hawakuwa na wadhifa wowote nchini.

Akiwa amekaa upande maalum kulipotegwa kwa wazazi wa kiumeni na wale wa kikeni Hussein muda mwingi alikuwa na furaha lakini kila anapogonganisha macho na mamaake Kamishna Shaaban alijikuta anapata mshtuko muda mwengine ambao hakujua unatokea wapi lakini alikuwa anaupotezea.
Kuna wakati hasa ule wa kula keki na kupiga picha ndio kabisa Hussein alizidi kuushangaa moyo wake kuongeza mapigo kila anapoangaliana na yule mama hasa wakati walipokaa pamoja na mzee Mwinchande, Zena na yule mama Shaaban alijikuta kama anatamani kumuuliza kitu lakini hakujua ni kitu gani na kuishia kujichekesha tu.

kulikuwa na wapiga picha waalikwa tofauti tofauti kwenye ule ukumbi na mmoja wapo kati ya wale wapiga picha alikuwapo Cj4 ambae ilikuwa ni vigumu sana kutambulika kwa mtu yeyote aliyekuwa anamjua hapo kabla kwa ule muonekano alioingia nao pale.
Hata Shebby alipokaa na mkewe jukwaa kuu kusikiliza nasaha za hapa na pale kutoka kwa wazazi na watu wengine, macho yake muda mwingi yalikuwa yanaangaza huku na huko ndani ya ukumbi kwa lengo la kumuona Cj4 lakini hakufanikiwa kumgundua japo alikuwa jilani nae muda wote kwani wapiga picha walikaa mbelembele ya eneo la tukio ili kuweza kuchukua na kupiga picha vizuri.

Muonekano wa Cj4 siku hiyo alikuwa na Mustachi mkubwa tu sambamba na miwani ambayo kwa nje ni kama ya macho lakini haikuwa hivyo na hata mustach aliokuwanao ulikuwa wa bandia.
Alichokuwa anafanya kwa kutumia ile kamera Cj4 ni kurekodi video huku akiwachukua karibu wageni waalikwa hususani wale wastaafu wote nia na madhumuni pindi atapoondoka akirudie kuikagua kwa umakini ile video apate kumjua mr X kwani aliamini kivyovyote mr X lazima angekuja mwenyewe sehemu ile ya ukumbi na iwapo atakuja basi amani itatawala lakini iwapo mr X asipokuja aliamini kuna tukio lolote lingeweza kutokea hivyo muda wote alikuwa makini kwa hayo yote mawili Cj4.

Kwa jinsi mambo yalivyoenda vizuri pale ukumbini hakukuwa na aliyegundua wala kuhisi kama yule bibi harusi ana jeraha la mshono tumboni na hiyo ilibaki siri ya watu wachache tu japo wengi walisikia tukio la kuungua kwa nyumba ya Dokta Asha.

* * * * *

Sherehe ziliisha majira ya usiku sana na kutokana na sababu maalum fungate la Shebby na Asha lilipangwa kufanyika palepale kwenye Jumba kubwa la kifahari la mzee Mwinchande.
Nyumba ile nyengine aliyokodi Shebby ililipiwa na kukabidhiwa Zena kuwa nyumba yake huku kwa upande wa Hussein bubu alijumuika pamoja na wazazi wa Kamishna Shebby kwaajili ya makazi ya muda pale kwenye jumba la Mwinchande kipindi ambacho Kamishna Shebby atapokuwa anamtafutia makazi rasmi ya kudumu.

Alfajiri na mapema ndani ya jengo la mzee Mwinchande kwa mara ya kwanza Hussein bubu alijiona kweli yuko huru mara baada ya kulala katika chumba kikubwa chenye mandhali ambayo hajawahi hata siku moja kulala tokea kuzaliwa kwake mpaka pale alipofikia.
Usiku huo alimshukuru sana Mungu kwa yote yaliyoendelea na aliendelea kumuomba kama ilivyokuwa kawaida yake kuwa amsaidie aweze kumtendea muujiza alipe kisasi kwa kumuua Mr X kwa mikono yake.
Japo kwa akili ya kawaida ilikuwa ni kazi ngumu na ni kitu kama cha kufikirika tu kutokana na wengi waliokuwa mashupavu na uwezo wa vita kushindwa walau kumjua mr X sembuse Hussein ambae kashaanza kujiishia umri umemtupa mkono harafu aweze kumuua?
Lakini kwa Mungu Hussein aliamini hakuna linaloshindikana aliamini kabisa imani thabiti na kumuomba kila siku japo alijua kuua ni dhambi lakini kwa dhambi ya kumuua Mr X aliiomba na kuikubali kwa moyo mmoja kuliko kumuacha hai.

"Aslaam alaykum"
alisalimia mzee Hussein asubuhi ile pindi alipotoka na kumkuta Mzee Mwinchande upande wa sebuleni ambapo alikaa kwenye mswala akisoma qur'aan baada ya kusali sala ya alfajiri.
"Waaleikum salaam warahma tullah wabarakatul"
alijibu kiurefu kabisa Mzee Mwinchande kwa rafudhi maridhawa ya kiarabu kuonesha jinsi gani dini imelala kwenye ubongo wa Mzee Mwinchande.
Moyoni Hussein alijisikia faraja sana kukutana na familia ya wacha Mungu kama ile na akiwa maeketi kwenye moja ya sofa akimtazama babaake Kamishna Shebby akisoma qur aan kwa utulivu kabisa na kumliwaza Hussein japo alikuwa hajui tafsiri yake na alipata imani ya kumuelewa vizuri Kamishna Shebby kwanini kawa mtu tofauti mwenye roho nzuri, kumbe kwa sababu amelelewa na watu wenye imani na kuishika dini.
Akiwa ametabasamu pale sebuleni mara alimuona kwa mara nyengine mamaake Shebby ambae rich ya kwamba nae umli kidogo ulisogea lakini pindi anapokutanisha nae macho moyo wake unastuka sana na hadi muda mwingi alipuuzia na hakujua kwanini lakini safari hii asubuhi mara tu aliposikia sauti ikimsalimia na kuinua kichwa chake kuitikia huku akimtazama akili yake ilimletea picha iliyomfanya apigwe na bumbuwazi hadi yule mama alishangaa.

ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom