Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #101
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 48
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
"Dada, mzima huyu?"
"Aaagh! Fanu maswali gani hayo? we kamata huko tum bebe tumpeleke.... unauliza mzima!! sasa toka lini mtu aliyekufa akawa anatoa ukoromo?"
maneno ya kijana wa mwanzo yalinichoma sana japo sikuweza kujibu chochote lakini niliumia sana kuona dadaangu kipenzi akifananishwa na maiti angali yu hai kwa kigezo cha ile harufu..!?
Aaaaah!! ama kweli wanaadamu tunakufuru kubwa.
Afadhali kauli ya yule mwenzake aliyemjibu kidogo ilinifurahisha japo sikuipenda pia kwani dadaangu alikuwa hakoromi bali alikuwa anaugulia maumivu makali aliyokuwa anayapata lakini kile kidonda ndicho kilichokuwa kinaifanya sauti yake kusikika kama mkoromo kutokana na kutokota kwake kadri alivyokuwa anachezesha koromeo.
Nilimnyanyua na kum beba Asha ambae bado alikuwa kashikilia bakuli lake akilia na kutoka nae nikiwa nyuma ya wale vijana waliom beba dadaangu Mariam na sikukumbuka hata kufunga mlango zaidi nilikuwa makini na kumshika Asha ubavuni nilipom beba kutokana na kulia kwake na nilipandwa na hasira zaidi mara baada ya kupita hatua chache kwa majirani wale ambao walininyima msaada awali na kuwakuta wameeka vigenge vya umbea kwenye baraza zao huku macho yao yakiwa kwetu na tolipofika karibu walinyamaza na kuishia kutututazama na tulipopita ndipo waliangua kicheko kikubwa kwa pamoja.
'''HEEHEEEEEE KAPIMEEEEEEEE'''
Nilitamani nirudi nikachambane nao lakini nilishindwa na kubaki nimefura hasira iliyochanganyika na maumivu mpaka tulipofika pale stendi ambapo kila aliyetuona hakuacha kutushangaa wakati dada alipokuwa aningizwa kwenye ile Taxi nami nikamnunulia soda na Keki mbili Asha mara baada ya kumalizana na wale vijana,
na hapo kidogo kelele za kilio cha mwanangu Asha zilipungua pindi tulipoingia kwenye ile Taxi na kumueka mbele huku mimi nikikaa nyuma na kumpakatia dada ambae sauti aliyokuwa anaitoa iliyo mithili ya ukoromo ilizidi kuongezeka na kuniumiza zaidi kwa kugundua kuwa maumivu yanazidi mwilini mwa dadaangu kipenzi.
Nilimuamuru dereva kutuwahisha mwananyamala hospitali na kumpigia simu mama muda uleule gari ilipoanza kutoka na kumuelekeza hali ya dada huku nikimficha juu ya kidonda cha ajabu kilichokuwa shingoni kwa dada kwa kujua kuwa mamaangu anakuwaga na uoga unaoambatana na presha ya kushuka hasa anapomuona mwanae anaumwa sana ama kazidiwa hivyo hata ile kauli yangu kuwa nampeleka hospitali ilitosha kumstua kule aliko na mara baada ya taxi yetu kufika hospitali mwananyamala niliwakuta tayari mama na baadhi ya rafiki zake waliokuwa kwenye shughuli wakiwa na nyuso za huzuni getini huku mamaangu akiwa peku kabisa licha ya kuwa alitoka nyumbani akiwa amependeza na zaidi alivaa viatu ambavyo alinunuliwa na dada Mariam.
Ilibidi nishushe kioo na kuwapungia kuwaelekeza kuwa Taxi wanayoitazama inayoingia sasa ndiyo niliyomo na kweli walianza kuifatilia hadi iliposimama ndani ya ile hospitali na ndipo mama alipoingia kumchungulia dada pindi nilipomuacha na kwenda kuwaita manesi ambao walikuja haraka na kitanda cha matairi kwa nia ya kuja kum beba dada.
Moyo uliniuma sana nilipotoka na kumkuta mama akiwa analia huku ameshikwa na wale shoga zake na manesi wa mwananyamala sitoweza kuwasahauuu..... aaaaaagh nakumbuka jinsi walivyokuwa wanampakia dada kwenye kitanda kile mithili ya mzigo mbali na kelele za ukoromo wa maumivu na kusababisha kile kitenge nilichomtanda kwa kuziba eneo lile la jeraha kufunuka na kudondoka na hapo kila mtu aliyekuwa jirani alistaajabu kushuhudia ule uchafu ambao hata mimi nilishangaa kuona umezidi mara dufu huku lile tundu likiwa si dogo kama nilivyoona awali bali liliongezeka na ilitaka moyo sana kulitazama.
''"Aaaaaaaaaaaaaaaaaaagh, Mariaaaaamu Mwananguuuuuuuuu"''
Sintoisahau kauli hii ya mama angu.. mamaetu kipenzi aaagh,
Sikujua kabisa kama ile siku niliyomuambia 'mama umependeza sana leo umekuwa kijana kabisa' asubuhi yake pindi aliponiaga anakwenda kwenye shughuli ya harusi ya rafiki ake wa miaka mingi Mwananyamala kama itakuwa ndio siku yetu ya mwisho kucheka pamoja....!
Aaaaah sikuwaza wala kuhisi kama ipo siku mamaangu atanitoka ghafra namna ile tena mbele ya macho yangu na watu wengi kiasi kilee aaaah, masikini Zena mimiii nitalia na nani na tulizaliwa wawili tu na dadaangu ambae ndio nae alitoa ukoromo wa sauti ya juu uliotokea kwenye lile tundu na kurusha uchafu mwingi sambamba na damu mithili ya bomba mara baada ya kitenge kilichokuwa kinaburuza na kukanyagwa na nesi kudondoka na mama kupiga ule ukelele uliopelekea kuanguka chini.
aaaaaaaaaah kwanini hamkunambia ndugu zangu kama mmepanga kuondoka pamoja kwenye ulimwengu wa mauti na kunifanyia suprize iliyoutesa moyo wanguuu na kuniachia upweke wa milele!!??...... aaaaaaaaaaah
Nilijikuta nami nawasindikiza mama na dada kwa kupoteza fahamu pindi nilipokuwa nashuhududia vifo vyao ambapo mama alitapatapa na kukata roho pale chini muda mfupi baada ya kudondoka huku dada Mariam nae alimalizikia muda mfupi baada ya kutoa ule mkoromo mkubwa mithili ya firimbi uliorusha mafunda ya uchafu na damu.
Sintosahau maneno ya yule daktari alipokuwa ananipa maelezo ya uthibitisho wa vifo vya ndugu zangu siku moja baadae pindi nilipopata fahamu na kuruhusiwa wodini.
Alinambia kuwa kifo cha mamaangu kilisababishwa na presha iliyoshuka ghafra kupita kiwango vilevile dadaangu Mariam kifo chake kilisababishwa na kansa hatari ya koo.
Sintosahau kabisa hata mara baada ya ndugu na majirani kuungana nami hospitali na kuchukua maiti kurudisha misiba ile ya kihistoria moyoni mwangu mpaka nyumbani na baada ya taratibu za mazishi kukamilika hatimae mama na dada wote walizikwa siku moja na makaburi yao yalifatana. aaaah! Mungu awaeke mahali pema.
Siku moja kupita baada ya mazishi ilibidi nitoke na vijana wa kiume wachache sambamba na mzee wetu wa mtaa tuliokuwa tunaishi tuliyezoea kumwita babu japo hakuwa na undugu wa damu na sisi lakini alikuwa jirani mwema na alisifika kuwa mzee mwenye busara sana.
Safari yetu ilikuwa ni kule alipokuwa anaishi dada Mariam kwa niaba ya kukusanya vitu vyote lakini hatukuamini baada yakufika na kukutana na habari za uvamizi na wizi uliotokea siku moja iliyopita ambapo vitu vyote muhimu vya dada viliibiwa na chumba kubaki cheupe mithili ya mtu aliyehama.
Japo ilituuma lakini tulipiga moyo konde na kushukuru tu, kwani iwapo tumempoteza mtu kabisa sembuse hivo vitu?
tuliwaaga wale wenyeji tuliowakuta kwenye vile vyumba viwili ambavyo siku ile nilipokuja kumchukua dada vilikuwa na makufuri tu.
Yule mzee alinisaidia kuongea na wale majirani visilani mara baada ya kumuhadithia mkasa ulipoanzia ambapo kwa busara zake aliweza kuambua sababu kuwa kumbe dada Mariam alikuwa ni mtu wa kujiona ona sana kipindi anaishi pale na mashoga zake watatu waliopanga pamoja huku mmoja wao akiwa si mwanamke bali ni shoga kabisa tena mbaya zaidi waliitumia ile nyumba kama dangulo la kuingiza wanaume hali iliyokuwa inawakera sana majirani kwa vile kujiona kwao, kutoshiriki kwenye misiba ya wenzao na matatizo mengine huku wakiwa ni watu wenye nyodo nyingi na ndio sababu kuu za kuwachukia wote na kuwatenga. Hapo kidogo nilielewa lakini bado sikulidhika na yale waliyonionesha lakini niliamua yote kuyapuuza na kurudi nyumbani sambamba na yule mzee na wale vijana.
ulipita mwezi mmoja baada ya kumaliza matanga ndugu wote walitawanyika na kuniacha nikiwa na mwanangu Asha mtoto wa marehemu dada bila msaada wowote wa kimalezi zaidi ya kuniachia maneno ya pole na maisha mema na huo ndio ukawa mwanzo wa maisha mapya ya misukosuko na mazoea baina yangu na Asha.
Lakini kabla hazijaanza tabu na misukosuko ambayo sikutaraji kama yatatukuta mimi na mwanangu yule niliumizwa na kulizwa na kitu kimoja ambacho nilikikumbuka mwenyewe baada ya kusahau kwa muda mrefu..... Kitu chenyewe ni barua, barua ambayo ilionesha wazi kwa nje ilinihusu mimi, barua ambayo sikujua imebeba nini hasa ndani yake, barua ya mwisho ambayo muandishi wake nilijua kama hatoniandikia tena barua nyengine milele, ila kwa barua ile niliweza kuihisi sauti yake akiongea pindi nilipokuwa nasoma hati ya maandishi yake, barua toka kwa marehemu dada Mariam ambayo licha ya kupotea kwake kutokana na janga kubwa la mafuriko ya mwaka lililokuja kutokea wiki chache baada ya kuisoma lakini maneno yake yaliendelea kuishi akilini mwangu kila nilipomkumbuka yeye ama nilipomuangalia Asha.
Barua yenyewe ilikuwa hivi................
^..................................................................................^
Mdogo angu Zena, naandika barua hii nikiwa na maumivu makali sana sehemu za shingo na kifua hususani kooni na hivi sasa uvimbe ambao awali ulikuwa kwa ndani lakini sasa umezidi kutokeza nje ya shingo, najua muda wowote unaweza kupasuka na kuimaliza safari yangu ya hapa duniani kuianza safari mpya kwenye ulimwengu wa ahadi kwa kila mja aliyeumbwa.
Uvimbe huu si wa jipu la kawaida bali ni ugonjwa ambao nimeuficha kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na aibu na kutopenda niwatie majonzi mapema lakini kwa kuwa sasa naona ule wakati wa kuumbuka umefika nimeamua kukuweka wazi ukae ukijua kinachoniua ni nini..
Hiki kinachonitafuna Zena ni Kansa.
ITAENDELEA...
EPS 48
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
"Dada, mzima huyu?"
"Aaagh! Fanu maswali gani hayo? we kamata huko tum bebe tumpeleke.... unauliza mzima!! sasa toka lini mtu aliyekufa akawa anatoa ukoromo?"
maneno ya kijana wa mwanzo yalinichoma sana japo sikuweza kujibu chochote lakini niliumia sana kuona dadaangu kipenzi akifananishwa na maiti angali yu hai kwa kigezo cha ile harufu..!?
Aaaaah!! ama kweli wanaadamu tunakufuru kubwa.
Afadhali kauli ya yule mwenzake aliyemjibu kidogo ilinifurahisha japo sikuipenda pia kwani dadaangu alikuwa hakoromi bali alikuwa anaugulia maumivu makali aliyokuwa anayapata lakini kile kidonda ndicho kilichokuwa kinaifanya sauti yake kusikika kama mkoromo kutokana na kutokota kwake kadri alivyokuwa anachezesha koromeo.
Nilimnyanyua na kum beba Asha ambae bado alikuwa kashikilia bakuli lake akilia na kutoka nae nikiwa nyuma ya wale vijana waliom beba dadaangu Mariam na sikukumbuka hata kufunga mlango zaidi nilikuwa makini na kumshika Asha ubavuni nilipom beba kutokana na kulia kwake na nilipandwa na hasira zaidi mara baada ya kupita hatua chache kwa majirani wale ambao walininyima msaada awali na kuwakuta wameeka vigenge vya umbea kwenye baraza zao huku macho yao yakiwa kwetu na tolipofika karibu walinyamaza na kuishia kutututazama na tulipopita ndipo waliangua kicheko kikubwa kwa pamoja.
'''HEEHEEEEEE KAPIMEEEEEEEE'''
Nilitamani nirudi nikachambane nao lakini nilishindwa na kubaki nimefura hasira iliyochanganyika na maumivu mpaka tulipofika pale stendi ambapo kila aliyetuona hakuacha kutushangaa wakati dada alipokuwa aningizwa kwenye ile Taxi nami nikamnunulia soda na Keki mbili Asha mara baada ya kumalizana na wale vijana,
na hapo kidogo kelele za kilio cha mwanangu Asha zilipungua pindi tulipoingia kwenye ile Taxi na kumueka mbele huku mimi nikikaa nyuma na kumpakatia dada ambae sauti aliyokuwa anaitoa iliyo mithili ya ukoromo ilizidi kuongezeka na kuniumiza zaidi kwa kugundua kuwa maumivu yanazidi mwilini mwa dadaangu kipenzi.
Nilimuamuru dereva kutuwahisha mwananyamala hospitali na kumpigia simu mama muda uleule gari ilipoanza kutoka na kumuelekeza hali ya dada huku nikimficha juu ya kidonda cha ajabu kilichokuwa shingoni kwa dada kwa kujua kuwa mamaangu anakuwaga na uoga unaoambatana na presha ya kushuka hasa anapomuona mwanae anaumwa sana ama kazidiwa hivyo hata ile kauli yangu kuwa nampeleka hospitali ilitosha kumstua kule aliko na mara baada ya taxi yetu kufika hospitali mwananyamala niliwakuta tayari mama na baadhi ya rafiki zake waliokuwa kwenye shughuli wakiwa na nyuso za huzuni getini huku mamaangu akiwa peku kabisa licha ya kuwa alitoka nyumbani akiwa amependeza na zaidi alivaa viatu ambavyo alinunuliwa na dada Mariam.
Ilibidi nishushe kioo na kuwapungia kuwaelekeza kuwa Taxi wanayoitazama inayoingia sasa ndiyo niliyomo na kweli walianza kuifatilia hadi iliposimama ndani ya ile hospitali na ndipo mama alipoingia kumchungulia dada pindi nilipomuacha na kwenda kuwaita manesi ambao walikuja haraka na kitanda cha matairi kwa nia ya kuja kum beba dada.
Moyo uliniuma sana nilipotoka na kumkuta mama akiwa analia huku ameshikwa na wale shoga zake na manesi wa mwananyamala sitoweza kuwasahauuu..... aaaaaagh nakumbuka jinsi walivyokuwa wanampakia dada kwenye kitanda kile mithili ya mzigo mbali na kelele za ukoromo wa maumivu na kusababisha kile kitenge nilichomtanda kwa kuziba eneo lile la jeraha kufunuka na kudondoka na hapo kila mtu aliyekuwa jirani alistaajabu kushuhudia ule uchafu ambao hata mimi nilishangaa kuona umezidi mara dufu huku lile tundu likiwa si dogo kama nilivyoona awali bali liliongezeka na ilitaka moyo sana kulitazama.
''"Aaaaaaaaaaaaaaaaaaagh, Mariaaaaamu Mwananguuuuuuuuu"''
Sintoisahau kauli hii ya mama angu.. mamaetu kipenzi aaagh,
Sikujua kabisa kama ile siku niliyomuambia 'mama umependeza sana leo umekuwa kijana kabisa' asubuhi yake pindi aliponiaga anakwenda kwenye shughuli ya harusi ya rafiki ake wa miaka mingi Mwananyamala kama itakuwa ndio siku yetu ya mwisho kucheka pamoja....!
Aaaaah sikuwaza wala kuhisi kama ipo siku mamaangu atanitoka ghafra namna ile tena mbele ya macho yangu na watu wengi kiasi kilee aaaah, masikini Zena mimiii nitalia na nani na tulizaliwa wawili tu na dadaangu ambae ndio nae alitoa ukoromo wa sauti ya juu uliotokea kwenye lile tundu na kurusha uchafu mwingi sambamba na damu mithili ya bomba mara baada ya kitenge kilichokuwa kinaburuza na kukanyagwa na nesi kudondoka na mama kupiga ule ukelele uliopelekea kuanguka chini.
aaaaaaaaaah kwanini hamkunambia ndugu zangu kama mmepanga kuondoka pamoja kwenye ulimwengu wa mauti na kunifanyia suprize iliyoutesa moyo wanguuu na kuniachia upweke wa milele!!??...... aaaaaaaaaaah
Nilijikuta nami nawasindikiza mama na dada kwa kupoteza fahamu pindi nilipokuwa nashuhududia vifo vyao ambapo mama alitapatapa na kukata roho pale chini muda mfupi baada ya kudondoka huku dada Mariam nae alimalizikia muda mfupi baada ya kutoa ule mkoromo mkubwa mithili ya firimbi uliorusha mafunda ya uchafu na damu.
Sintosahau maneno ya yule daktari alipokuwa ananipa maelezo ya uthibitisho wa vifo vya ndugu zangu siku moja baadae pindi nilipopata fahamu na kuruhusiwa wodini.
Alinambia kuwa kifo cha mamaangu kilisababishwa na presha iliyoshuka ghafra kupita kiwango vilevile dadaangu Mariam kifo chake kilisababishwa na kansa hatari ya koo.
Sintosahau kabisa hata mara baada ya ndugu na majirani kuungana nami hospitali na kuchukua maiti kurudisha misiba ile ya kihistoria moyoni mwangu mpaka nyumbani na baada ya taratibu za mazishi kukamilika hatimae mama na dada wote walizikwa siku moja na makaburi yao yalifatana. aaaah! Mungu awaeke mahali pema.
Siku moja kupita baada ya mazishi ilibidi nitoke na vijana wa kiume wachache sambamba na mzee wetu wa mtaa tuliokuwa tunaishi tuliyezoea kumwita babu japo hakuwa na undugu wa damu na sisi lakini alikuwa jirani mwema na alisifika kuwa mzee mwenye busara sana.
Safari yetu ilikuwa ni kule alipokuwa anaishi dada Mariam kwa niaba ya kukusanya vitu vyote lakini hatukuamini baada yakufika na kukutana na habari za uvamizi na wizi uliotokea siku moja iliyopita ambapo vitu vyote muhimu vya dada viliibiwa na chumba kubaki cheupe mithili ya mtu aliyehama.
Japo ilituuma lakini tulipiga moyo konde na kushukuru tu, kwani iwapo tumempoteza mtu kabisa sembuse hivo vitu?
tuliwaaga wale wenyeji tuliowakuta kwenye vile vyumba viwili ambavyo siku ile nilipokuja kumchukua dada vilikuwa na makufuri tu.
Yule mzee alinisaidia kuongea na wale majirani visilani mara baada ya kumuhadithia mkasa ulipoanzia ambapo kwa busara zake aliweza kuambua sababu kuwa kumbe dada Mariam alikuwa ni mtu wa kujiona ona sana kipindi anaishi pale na mashoga zake watatu waliopanga pamoja huku mmoja wao akiwa si mwanamke bali ni shoga kabisa tena mbaya zaidi waliitumia ile nyumba kama dangulo la kuingiza wanaume hali iliyokuwa inawakera sana majirani kwa vile kujiona kwao, kutoshiriki kwenye misiba ya wenzao na matatizo mengine huku wakiwa ni watu wenye nyodo nyingi na ndio sababu kuu za kuwachukia wote na kuwatenga. Hapo kidogo nilielewa lakini bado sikulidhika na yale waliyonionesha lakini niliamua yote kuyapuuza na kurudi nyumbani sambamba na yule mzee na wale vijana.
ulipita mwezi mmoja baada ya kumaliza matanga ndugu wote walitawanyika na kuniacha nikiwa na mwanangu Asha mtoto wa marehemu dada bila msaada wowote wa kimalezi zaidi ya kuniachia maneno ya pole na maisha mema na huo ndio ukawa mwanzo wa maisha mapya ya misukosuko na mazoea baina yangu na Asha.
Lakini kabla hazijaanza tabu na misukosuko ambayo sikutaraji kama yatatukuta mimi na mwanangu yule niliumizwa na kulizwa na kitu kimoja ambacho nilikikumbuka mwenyewe baada ya kusahau kwa muda mrefu..... Kitu chenyewe ni barua, barua ambayo ilionesha wazi kwa nje ilinihusu mimi, barua ambayo sikujua imebeba nini hasa ndani yake, barua ya mwisho ambayo muandishi wake nilijua kama hatoniandikia tena barua nyengine milele, ila kwa barua ile niliweza kuihisi sauti yake akiongea pindi nilipokuwa nasoma hati ya maandishi yake, barua toka kwa marehemu dada Mariam ambayo licha ya kupotea kwake kutokana na janga kubwa la mafuriko ya mwaka lililokuja kutokea wiki chache baada ya kuisoma lakini maneno yake yaliendelea kuishi akilini mwangu kila nilipomkumbuka yeye ama nilipomuangalia Asha.
Barua yenyewe ilikuwa hivi................
^..................................................................................^
Mdogo angu Zena, naandika barua hii nikiwa na maumivu makali sana sehemu za shingo na kifua hususani kooni na hivi sasa uvimbe ambao awali ulikuwa kwa ndani lakini sasa umezidi kutokeza nje ya shingo, najua muda wowote unaweza kupasuka na kuimaliza safari yangu ya hapa duniani kuianza safari mpya kwenye ulimwengu wa ahadi kwa kila mja aliyeumbwa.
Uvimbe huu si wa jipu la kawaida bali ni ugonjwa ambao nimeuficha kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na aibu na kutopenda niwatie majonzi mapema lakini kwa kuwa sasa naona ule wakati wa kuumbuka umefika nimeamua kukuweka wazi ukae ukijua kinachoniua ni nini..
Hiki kinachonitafuna Zena ni Kansa.
ITAENDELEA...