Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #141
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (69)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
___________________________
_________________
Alisafiri salama usalimini toka Arusha hadi katika jiji la Raha na Karaha na alipofika ubungo alipokelewa na Shangazi yake Mwinchande na kufika nae Kinondoni ambapo ndipo walipokuwa wanaishi.
Wiki moja baadae Zai alifanya mawasiliano na kukutana na Hussein maeneo ya stendi Mkwajuni baada ya kumuacha shangazi yake akiwa amelala mchana ule lakini alipofika kuongea na Hussein nia na madhumuni kujua alimjuaje juaje alishangazwa na majibu ya Hussein eti kuwa alimuota ndotoni.
Akilini mwake Zai alihisi hawa ndio wale wanaume aliowasikia wapenda ngono na kumtaka kila msichana mzuri na hivyo alimkataa kabisa palepale na kumsisitizia kuwa yeye kilichomleta Dar ni masomo na si vinginevyo, jambo ambalo moyoni mwake alijua si kweli lakini hakuona umuhimu kumwambia vile kutokana na jinsi yeye mwenyewe alivyo.
Aliporudi ndipo kwa mara ya kwanza alianza kuigundua roho mbaya aliyokuwa nayo Shangazi ake Mwinchande mara baada ya kumkuta ameamka.
"Hee! yaani wewe huna hata mwezi tayari ushavijua hadi vichochoro vya kukuniwa?... Wewe ni bint wa aina gani unafanywa hadi mchana huu tena ugenini..? haya utanambia ulipokuwa wapi na umalaya wako usije kuniulia mwanangu.."
alibwata shangazi na kuanza kumpiga Zai na ufagio uliokuwa pale ukumbini kama mtoto mdogo.
Maisha yalienda kwa mtindo huo pale nyumbani na kipindi hiko chote hakuwahi kupata nafasi ya kuzungumza na mumewe ambae ni Mwinchande aliyekuwa huko Israel ktk mafunzo maalum na hadi unakatika mwezi tayari Zai maisha ya pale kwa Shangazi yalimkifu mno na hadi kufikia kukubali moyoni mwake kuachana na Mwinchande ili apate mwanaume mwengine ambae kidogo kwao kunaweza kuwa na amani kuliko maisha ya pale kwa shangazi vile anavyofanyiwa mara kwa mara na kupewa maneno ya kashfa na kejeli asijue wapi zinapotokea huku akiambiwa kuwa asije akamuua Mwinchande kutokana na tabia yake ya umalaya ambao hakuujua kabisa na ukweli hakuwahi kukutana kimwili na mwanaume yeyote tokea kuzaliwa kwake.
Hali ile ilimfanya siku moja amkumbuke Hussein na kutamani kumfahamu zaidi.
Lakini aliwaogopa sana wanaume Zai hali hiyo ilimfanya kabla hajampigia Hussein simu alipiga kijijini kwao Arusha kwa Ustaadh mmoja aliyekuwa na utaalam mkubwa wa kusaidia watu kupitia Marohani (Majini) na ndie huyo aliyemfundisha yeye Qur'an.
Mara alipompigia simu simu na kuongea nae kwa kujiiba siku moja majira ya usiku ndipo alipomuelezea juu ya kijana aliyekutana nae toka Arusha na kwa mara ya pili Dar ambae alimwambia kuwa eti jina lake aliliota, hivyo alikuwa anataka Ustaadh kupitia marohani yake wajaribu kumtazama huyo kijana kama ni mwanaume mzuri au ni wale wahuni wenye tamaa na ndipo hapo Ustadh yule alipofanya mambo yake baada ya kutaka jina la huyo kijana na vile alivyo ndipo baada ya dakika kadhaa Ustadh alianza kuzungumza lakini safari hii kwa sauti tofauti na ya awali na Zainab aligundua kuwa sasa anayezungumza nae ni Jini.
[["Zainab, huyo Kijana ni mwanaume mzuri sana kwako kuliko huyo unayeamini mumeo kwa sasa. Japo nae anakupenda...! lakini si mume bora kwako kama huyo Hussein.
Pia labda tukwambie kitu huyo Hussein ndie mumeo ambae Allah amekuandikia uwe nae na kupata familia na ukumbuke mwenye kumiliki Ndoto nini Mwenyezi Mungu pekee... Amemuonesha Hussein wewe ni nani sasa baada ya kutojua kuwa ulibadilishwa jina.. Yaani ina maana kama hujui yule Hussein ndie yule yule rafiki ako wa utotoni uliyemjua kwa jina la Zungu. Na inaonesha wazi Mungu ndie anayewakutanisha nyinyi ili muungane muwe kitu kimoja na amini kabisa kulingana na nyota zenu zilizong'aa pamoja tangia wadogo kuwa matatimiza ndoto zenu kama mkiwa pamoja. Hussein ana ndoto ya kujenga nyumba na kama akikuoa hautopita muda mrefu atajenga kweli na wewe una ndoto ya maisha ya furaha na watoto wawili wa kwanza awe wa kiume na wa pili wa kike, na kama utaolewa na Hussein kwa mapenzi yake Mungu utapata ila kama haitakuwa hivyo basi niyi nyote hamtotimiza ndoto zenu pia utengano wenu wowote ule unaweza kuleta madhara ama dholuba kubwa, tena Dholuba kubwa sana litaloponza hata nafsi za watu wasio na hatia..... Kumbuka haya Zainabu jua kama hutokuwa muwazi na kumwambia Hussein kuwa uliwahi kuolewa kimira basi jua utakuwa bado unatengeneza dhoruba kubwa zaidi kwa jinsi nyota za huyu mumeo zinavyoonyesha. Muombe sana Mungu Zai usiufiche ukweli ingali bado mapema.
waaadhaa Salaaam.."]]
Ndivyo alivyomaliza yule Jini aliyeongea na Zainab kupitia Ustadh na maneno yake yalimfanya Zainab apigwe bumbuwazi baada ya kusikia kuwa kumbe yule kijana ndie yule Zungu wake wa utoto.
Alijikuta anatabasam na kumshukuru Mungu kumkutanisha tena na Zungu japo alijua kuwa Zungu hamkumbuki na hakutaka amkumbushe kwani alijua angesababisha maswali kuwa mengi mwisho wa siku akayajua mabo ambayo hakutaka ayajue.
Na hapo ndipo alipompigia simu Hussein na kumuomba amuelekeze anapoishi ili aweze kwenda mwenyewe wakaongee kirefu zaidi juu ya kile alichokizungumza awali.
* * * * *
("Wanaume ni watu waongo kweli, yani Mwinchande kumuamini kote leo hii ameondoka ameniacha nimekuja kukaa na shangazi na hata muda wa kuongea na mimi hana?! sasa hat huyu lazima nimpe masharti kabambe nisiamini moja kwa moja kwa sababu eti nimeambiwa na kiumbe mwenye uwezo wa kuona zaidi yangu.. Lazima nimpe mtihani")
Yalikuwa ni mawazo akilini mwa Zai siku aliyokuwa anaenda kukutana na Hussein na kweli baada ya mazungumzo yao alimpa masharti magumu sana matatu ambayo yote Hussein alikubaliana nayo na kumshangaza sana Zai aliyejikuta furaha inamzidi na kumkumbatia Hussein huku akijisahau na kumwita jina la Zungu ambalo lilistua masikio ya Hussein lakini mwishoe alipuuzia tu japo kuna muda alitamani kumuuliza amelijuaje lile jina lakini kutokana na kuwehuka ghafra kwa vile alivyokubaliwa huku akiwa kaekwa kwenye mabano ya mtihani ambao kwa upande wake aliamini lazima ataufauru kwani aliweza kukaa mwaka mzima kabla hajaonana na Zai baada ya kuachana na mchumbaake wa awali Mariam ambae kumbe alikuwa na mimba changa siku wanaachana na hakulijua hilo hadi kipindi hiko anakubaliana kuwa wapenzi na Zai tayari upande wa pili Mariam alishajifungua katoto ka kike.
Lakini baada ya miezi kadhaa Mwinchande alirejea Tanzania kwa dharula maalum mara baada ya wenzao wawili kufariki katika mazoezi maalum ambayo hayakuekwa wazi huku yeye Mwinchande akibaki na alama ya kuchomwa na kitu cha ncha kali maeneo ya shavu ambayo alama ile iliyojichora herufi ya X haikuekwa wazi nini hasa kilichopelekea zaidi ya yeye mwenyewe kukiri kuwa aliumia kwenye hayo mafunzo na wenzake wawili wote walikufa kwa bahati mbaya kwenye hayohayo mafunzo.
Na mara baada ya Mwinchande kurudi na kumkuta mkewe wa mila alifurahi mno japo hakupata muda wa kukaa nae na kuzungumza mipango kutokana na kupewa wiki moja tu na Taifa ili watapomaliza kuistili miili ya wenzao basi na wao warejee wakamalizie hiyo kozi ambayo ilijumuisha askali kutoka nchi mbalimbali.
Lakini kuna jambo ambalo Mwinchande aliliona la muhimu sana lililomfanya siku mbili kabla ya safari ya kurudi Israel aliomba ruhusa ya uongo ya masaa sita ambayo aliyatumia kurudi nyumbani na kumchukua mkewe hadi kwa rafiki ake yule mganga aliyeitwa Mnyungunyungu nia na madhumuni ikiwa ni kumuonesha live huyo mkewe aliyewahi kumuongelea japo Zai hakuelewa kitu na nia ya pili ilikuwa ni yeye mwenyewe kufanyiwa dawa itayomuwezesha kufuzu vizuri kwenye hayo mafunzo na hapo ndipo Manyungunyungu alipomfanyia kitu maalum na kuipitisha dawa aliyoiita 'Kauzibe' kuwa itamfanya awe mtu asiyeonekana iwe kwenye vita au matatizo yatayomfanya atafutwe na kadhalika na alimwambia pia ile dawa ua 'kauzibe ' itaweza kudumu mwilini mwake kwa miaka thelathini, jambo ambalo Mwinchande alilifurahia mno. na kumpa zawadi kubwa ya fedha taslimu Manyungunyungu kabla ya kuondoka na mkewe na kumrudisha nyumbani nae kurudi kambini kureport na baada ya siku mbili walirudi tena Israel
ITAENDELEA
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
___________________________
_________________
Alisafiri salama usalimini toka Arusha hadi katika jiji la Raha na Karaha na alipofika ubungo alipokelewa na Shangazi yake Mwinchande na kufika nae Kinondoni ambapo ndipo walipokuwa wanaishi.
Wiki moja baadae Zai alifanya mawasiliano na kukutana na Hussein maeneo ya stendi Mkwajuni baada ya kumuacha shangazi yake akiwa amelala mchana ule lakini alipofika kuongea na Hussein nia na madhumuni kujua alimjuaje juaje alishangazwa na majibu ya Hussein eti kuwa alimuota ndotoni.
Akilini mwake Zai alihisi hawa ndio wale wanaume aliowasikia wapenda ngono na kumtaka kila msichana mzuri na hivyo alimkataa kabisa palepale na kumsisitizia kuwa yeye kilichomleta Dar ni masomo na si vinginevyo, jambo ambalo moyoni mwake alijua si kweli lakini hakuona umuhimu kumwambia vile kutokana na jinsi yeye mwenyewe alivyo.
Aliporudi ndipo kwa mara ya kwanza alianza kuigundua roho mbaya aliyokuwa nayo Shangazi ake Mwinchande mara baada ya kumkuta ameamka.
"Hee! yaani wewe huna hata mwezi tayari ushavijua hadi vichochoro vya kukuniwa?... Wewe ni bint wa aina gani unafanywa hadi mchana huu tena ugenini..? haya utanambia ulipokuwa wapi na umalaya wako usije kuniulia mwanangu.."
alibwata shangazi na kuanza kumpiga Zai na ufagio uliokuwa pale ukumbini kama mtoto mdogo.
Maisha yalienda kwa mtindo huo pale nyumbani na kipindi hiko chote hakuwahi kupata nafasi ya kuzungumza na mumewe ambae ni Mwinchande aliyekuwa huko Israel ktk mafunzo maalum na hadi unakatika mwezi tayari Zai maisha ya pale kwa Shangazi yalimkifu mno na hadi kufikia kukubali moyoni mwake kuachana na Mwinchande ili apate mwanaume mwengine ambae kidogo kwao kunaweza kuwa na amani kuliko maisha ya pale kwa shangazi vile anavyofanyiwa mara kwa mara na kupewa maneno ya kashfa na kejeli asijue wapi zinapotokea huku akiambiwa kuwa asije akamuua Mwinchande kutokana na tabia yake ya umalaya ambao hakuujua kabisa na ukweli hakuwahi kukutana kimwili na mwanaume yeyote tokea kuzaliwa kwake.
Hali ile ilimfanya siku moja amkumbuke Hussein na kutamani kumfahamu zaidi.
Lakini aliwaogopa sana wanaume Zai hali hiyo ilimfanya kabla hajampigia Hussein simu alipiga kijijini kwao Arusha kwa Ustaadh mmoja aliyekuwa na utaalam mkubwa wa kusaidia watu kupitia Marohani (Majini) na ndie huyo aliyemfundisha yeye Qur'an.
Mara alipompigia simu simu na kuongea nae kwa kujiiba siku moja majira ya usiku ndipo alipomuelezea juu ya kijana aliyekutana nae toka Arusha na kwa mara ya pili Dar ambae alimwambia kuwa eti jina lake aliliota, hivyo alikuwa anataka Ustaadh kupitia marohani yake wajaribu kumtazama huyo kijana kama ni mwanaume mzuri au ni wale wahuni wenye tamaa na ndipo hapo Ustadh yule alipofanya mambo yake baada ya kutaka jina la huyo kijana na vile alivyo ndipo baada ya dakika kadhaa Ustadh alianza kuzungumza lakini safari hii kwa sauti tofauti na ya awali na Zainab aligundua kuwa sasa anayezungumza nae ni Jini.
[["Zainab, huyo Kijana ni mwanaume mzuri sana kwako kuliko huyo unayeamini mumeo kwa sasa. Japo nae anakupenda...! lakini si mume bora kwako kama huyo Hussein.
Pia labda tukwambie kitu huyo Hussein ndie mumeo ambae Allah amekuandikia uwe nae na kupata familia na ukumbuke mwenye kumiliki Ndoto nini Mwenyezi Mungu pekee... Amemuonesha Hussein wewe ni nani sasa baada ya kutojua kuwa ulibadilishwa jina.. Yaani ina maana kama hujui yule Hussein ndie yule yule rafiki ako wa utotoni uliyemjua kwa jina la Zungu. Na inaonesha wazi Mungu ndie anayewakutanisha nyinyi ili muungane muwe kitu kimoja na amini kabisa kulingana na nyota zenu zilizong'aa pamoja tangia wadogo kuwa matatimiza ndoto zenu kama mkiwa pamoja. Hussein ana ndoto ya kujenga nyumba na kama akikuoa hautopita muda mrefu atajenga kweli na wewe una ndoto ya maisha ya furaha na watoto wawili wa kwanza awe wa kiume na wa pili wa kike, na kama utaolewa na Hussein kwa mapenzi yake Mungu utapata ila kama haitakuwa hivyo basi niyi nyote hamtotimiza ndoto zenu pia utengano wenu wowote ule unaweza kuleta madhara ama dholuba kubwa, tena Dholuba kubwa sana litaloponza hata nafsi za watu wasio na hatia..... Kumbuka haya Zainabu jua kama hutokuwa muwazi na kumwambia Hussein kuwa uliwahi kuolewa kimira basi jua utakuwa bado unatengeneza dhoruba kubwa zaidi kwa jinsi nyota za huyu mumeo zinavyoonyesha. Muombe sana Mungu Zai usiufiche ukweli ingali bado mapema.
waaadhaa Salaaam.."]]
Ndivyo alivyomaliza yule Jini aliyeongea na Zainab kupitia Ustadh na maneno yake yalimfanya Zainab apigwe bumbuwazi baada ya kusikia kuwa kumbe yule kijana ndie yule Zungu wake wa utoto.
Alijikuta anatabasam na kumshukuru Mungu kumkutanisha tena na Zungu japo alijua kuwa Zungu hamkumbuki na hakutaka amkumbushe kwani alijua angesababisha maswali kuwa mengi mwisho wa siku akayajua mabo ambayo hakutaka ayajue.
Na hapo ndipo alipompigia simu Hussein na kumuomba amuelekeze anapoishi ili aweze kwenda mwenyewe wakaongee kirefu zaidi juu ya kile alichokizungumza awali.
* * * * *
("Wanaume ni watu waongo kweli, yani Mwinchande kumuamini kote leo hii ameondoka ameniacha nimekuja kukaa na shangazi na hata muda wa kuongea na mimi hana?! sasa hat huyu lazima nimpe masharti kabambe nisiamini moja kwa moja kwa sababu eti nimeambiwa na kiumbe mwenye uwezo wa kuona zaidi yangu.. Lazima nimpe mtihani")
Yalikuwa ni mawazo akilini mwa Zai siku aliyokuwa anaenda kukutana na Hussein na kweli baada ya mazungumzo yao alimpa masharti magumu sana matatu ambayo yote Hussein alikubaliana nayo na kumshangaza sana Zai aliyejikuta furaha inamzidi na kumkumbatia Hussein huku akijisahau na kumwita jina la Zungu ambalo lilistua masikio ya Hussein lakini mwishoe alipuuzia tu japo kuna muda alitamani kumuuliza amelijuaje lile jina lakini kutokana na kuwehuka ghafra kwa vile alivyokubaliwa huku akiwa kaekwa kwenye mabano ya mtihani ambao kwa upande wake aliamini lazima ataufauru kwani aliweza kukaa mwaka mzima kabla hajaonana na Zai baada ya kuachana na mchumbaake wa awali Mariam ambae kumbe alikuwa na mimba changa siku wanaachana na hakulijua hilo hadi kipindi hiko anakubaliana kuwa wapenzi na Zai tayari upande wa pili Mariam alishajifungua katoto ka kike.
Lakini baada ya miezi kadhaa Mwinchande alirejea Tanzania kwa dharula maalum mara baada ya wenzao wawili kufariki katika mazoezi maalum ambayo hayakuekwa wazi huku yeye Mwinchande akibaki na alama ya kuchomwa na kitu cha ncha kali maeneo ya shavu ambayo alama ile iliyojichora herufi ya X haikuekwa wazi nini hasa kilichopelekea zaidi ya yeye mwenyewe kukiri kuwa aliumia kwenye hayo mafunzo na wenzake wawili wote walikufa kwa bahati mbaya kwenye hayohayo mafunzo.
Na mara baada ya Mwinchande kurudi na kumkuta mkewe wa mila alifurahi mno japo hakupata muda wa kukaa nae na kuzungumza mipango kutokana na kupewa wiki moja tu na Taifa ili watapomaliza kuistili miili ya wenzao basi na wao warejee wakamalizie hiyo kozi ambayo ilijumuisha askali kutoka nchi mbalimbali.
Lakini kuna jambo ambalo Mwinchande aliliona la muhimu sana lililomfanya siku mbili kabla ya safari ya kurudi Israel aliomba ruhusa ya uongo ya masaa sita ambayo aliyatumia kurudi nyumbani na kumchukua mkewe hadi kwa rafiki ake yule mganga aliyeitwa Mnyungunyungu nia na madhumuni ikiwa ni kumuonesha live huyo mkewe aliyewahi kumuongelea japo Zai hakuelewa kitu na nia ya pili ilikuwa ni yeye mwenyewe kufanyiwa dawa itayomuwezesha kufuzu vizuri kwenye hayo mafunzo na hapo ndipo Manyungunyungu alipomfanyia kitu maalum na kuipitisha dawa aliyoiita 'Kauzibe' kuwa itamfanya awe mtu asiyeonekana iwe kwenye vita au matatizo yatayomfanya atafutwe na kadhalika na alimwambia pia ile dawa ua 'kauzibe ' itaweza kudumu mwilini mwake kwa miaka thelathini, jambo ambalo Mwinchande alilifurahia mno. na kumpa zawadi kubwa ya fedha taslimu Manyungunyungu kabla ya kuondoka na mkewe na kumrudisha nyumbani nae kurudi kambini kureport na baada ya siku mbili walirudi tena Israel
ITAENDELEA