Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
- Thread starter
- #61
EPS 22
========
"Mh! mkuu hapaaaa daah!! okeeee.. auuu au alimaanisha kwenye picha?!!"
"Swadakta Kimaro, alichokuwa ananielekeza marehemu Mnyungunyungu nimepata siri ya maana ya hayo maneno kuwa mr.X aliwahi kupiga nae picha na dalili kuu ya kumtambua mr.X ana kovu usoni mwake kwa hiyo itatubidi tuibe siku mapema wiki hii twende mkuyuni tuombe picha zote alizowahi kupiga mzee Mnyungunyungu miaka ya nyuma."
"sawa mkuu sasa tutajuaje jina halisi la mr.X kama tutamgundua kwenye picha kwa ushahidi wa hilo kovu? kumbuka atakuwa kabadilika mno kwa sasa ila jina ndio la msingi zaidi, sasa tutajuaje hapo...?"
"Naam, swali lako ni zuri lakini usiwe na wasi kwani kabla hajafa mzee Mnyungunyungu aliwahi mwambia yule mwanae mganga kuwa mr.X anamfahamu vizuri tu. kwa hiyo tutapoiona picha ya mtu mwenye kovu ktk ulbamu ya mnyungunyungu ndipo tutapomuuliza mwanae yule atutajie majina ya mtu huyo, na alikuwa nani enzi hizo na hapo itaanza kazi moja tu ya kumtafuta."
"hapo mkuu sina swali kabisa, naona mipango imekaa vizuri sana Mr.X lazima afichuke safari hii."
Aliunga mkono st;sajent Kimaro mara baada ya kusikia mazungumzo ya Kamishna wake bwana Shaaban Mwinchande.
* * * * * *
Siku ya siku ilifika ambapo kwa mara nyengine alioneka Kamishna Shaaban na St;sajent Kimaro wakiwa moto chini ndani ya Land cruzer New Model ya kijivu wakipangusa (wakiyapita) magari na kukanyaga barabara ipasavyo kuelekea kijiji cha Mkuyuni mkoa wa Morogoro.
Muda mwingi kila mmoja alikuwa bussy na yake kichwani huku wakipeana story za hapa na pale na walipoianza barabara ya vumbi iliyokuwa inaelekea morogoro vijijini ndipo st;sajent Kimaro alivunja ukimya uliotawala muda mwingi na kuyapamba mazungumzo wakati huo akiendeesha gari.
"Sasa mkuu endapo tukishindwa kuiona hiyo picha ya mtu mwenye kovu usoni unafikiria nini cha kufanya ambacho kitatusaidia zaidi"
"Mh! sidhaani kwa haraka harakaaaa... lakini we umefikiriaje kwani"
"ahkah! mi nakusikiliza wewe bosi wangu niko tayari kutii mipango yako na kufata vile usemavyo."
"Sikia Kimaro, mapigo ya moyo wangu yanadunda kwa furaha furani ambayo naiona dhahili ni ishara ya ushindi na akili zangu zinaniaminisha kabisa kwamba safari hii tutamjua Mr.X tu."
"sawa mkuu lakini inabidi twende tukiwa na mbinu mbadala pia."
"Hebu nishauli mbinu mbadala uliyonayo."
"sawa mkuu, mi nadhani itatubidi tutumie mbinu za kijeshi zaidi kum bana yule mganga mtoto wa mzee Mnyungunyungu"
"Mbinu za kijeshi? kivipi Kimaro."
Aliuliza kamishna Shebby kwa mshangao kidogo huku akimtazama st;sajent Kimaro kwanini amefikiria hilo ilhali walishapanga awali kwamba ktk mission ile hawatatakiwa kujionesha ama kugundulika wao ni kina nani hasa.
"Mkuu kuna kitu nilikifikiria sana toka uliponipa habari ya maneno uliyoyaunganisha aliyotamka marehemu Mnyungunyungu na kunijengea wazo ambalo nahisi kabisa lipo jirani na ukweli ama ndio ukweli wenyewe."
"Wazo lipi hilo tena!! hebu nambie."
"wazo kuwa ni nani anaweza kuwa mr.X"
"Mh! Kimaro acha utani hebu nifafanulie unahisi nini?"
"Akili zangu zinanambia kuwa huenda yule mganga aliyetupokea akawa ndie mr.X mwenyewe"
"Mh! unamaanisha mtoto wa mzee Mnyungunyungu?"
"Haswaa ndie huyo."
"Kivipi sasa hadi umehisi hivyo?"
"kutokana na maneno uliyoyaunganisha aliyosema mzee Mnyungunyungu na ukijumlisha hadithi ya Hussein ukigawanya tukio la barua, namba ya simu hadi kushambuliwa kule kibamba miaka hiyo.. Pia umli wake vile nilivyomuona bado akili yangu inasema kuwa mzunguko woooote uko palepale yule mganga ndie mr.X"
"Daaah! Kimaro leo kweli umeamua kuchemsha kupe walio kwenye ndonga (kichwa) langu, Mh!! lete prove ya kile usemacho."
"Sawa mkuu ninazo sababu, Kwanza kumbuka mara ya kwanza mke wa Hussein ambae ni Zai alipoonwa na baba mkubwa wa Hussein ambae ndie mzee Mnyungunyungu alionesha hali ya mshangao sana hadi kupelekea kumpa maneno ya mafumbo Hussein juu ya yule mwanamke. Hii inanijengea picha kuwa mzee Mnyungunyungu alimtambua Zai mapema kabla ya pale, inawezekana mtoto wake ambae ndie yule mganga nae walishakuwa na mahusiano... kuthibitisha hili rejea kauli za Zai kuwa hajawahi kumkatalia mwanaume aliyemtongoza ila wote akawapa mitihani ktk kumtafuta aliyempenda kweli na walishindwa wote kasoro Hussein aliweza na kumpata Zai so mmoja wa washindwaji anaweza kuwa mtoto wa Mnyungunyungu.
Pili, barua ya Hussein huenda alipewa na yuleyule mganga kwenye daladala na kwa kuwa alizijua dawa nyingi kuna uwezekano barua ile ilibeba nguvu za giza ndani yake na pindi iliposomwa na mke wa Hussein ilianza kumlevya taratibu na kujikuta anaanza kufanya mawasiliano ya siri na yule mganga pasi na kujitambua na hata siku walipokuwa wanaenda kwa ba mkubwa inawezekana waliwasiliana tena kwa msg na yeye ndie aliyemny'ang'anya mtoto Hussein na kumshambulia akishilikiana na wenzake aliowajua yeye vilevile hata Mzee Mnyungunyungu alitoa ushahidi ule kwa kumkingia mwanae kifua na kuificha ile siri na ndio sababu ya kuhama kwao ili kupoteza kabisa habari zile zisije kuzuka tetesi pale kijijini.
Tatu, Kipindi unamuuliza swali marehemu Mnyungunyungu juu ya mr.X kuna uwezekano mlaika mtoa roho alikuwa mbele yake na akashindwa kusema uongo hivyo alitaka kumfichua mwanae na ndio maana ya maneno ANA KOVU USONI.
Na hii ni dhahili kama siku ile hujamuangalia vizuri yule mganga mimi nilimuona vizuri zaidi kuwa ana kovu kubwa tu usoni.
Kwa sababu hizi kuu tatu nina mashaka ya kuthubutu kusema kuwa mtoto wa Mzee Mnyungunyungu ndie Mr.X.."
"Uuuuuuppphhhhhh!!!!"
Alishusha pumzi kwa nguvu Kamishna Shebby huku akimtazama mara mbili mbili stafsajent Kimaro pasi na kumwambia chochote na ukimya ulifuata tena baina yao kipindi Shebby alipotulia na kuanza kuyachekecha maneno na prove alizotoa Kimaro sambamba na hadithi ya Hussein.
Kiupande furani yalimuingia yale maneno na kuzishawishi akili zake kuwa akubaliane na Kimaro lakini bado upande wa pili moyo wake Ulimkatalia kabisa kuwa yule mganga mtoto wa Mzee Mnyungunyungu kuwa ndie Mr.X
** ** ** **
Ilitimu majira ya saa saba mchana ambapo waliwasili kijiji cha Mkuyuni na kupaki gari yao eneo lile lile walipopaki pindi walipokuja awali na pembeni yake kulionekana imepaki difenda ya polisi na gari ya wagonjwa, na baada ya kushuka walivuka barabara na kuelekea moja kwa moja ile njia ya bondeni ambayo walipitishwa siku ile na yule kijana aliyeitwa Chibu.
Lakini cha ajabu siku hiyo hakukuonekana watu wengi eneo lile la stendi huku frem nyingi pia zilifungwa japo ilikuwa mchana na wakati wakishusha kile kibarabara waliwaona watu kwa mbali wengi wengi mbele yao huku wengine wakija nyuma yao na kuwapita wakionesha walikuwa na haraka ya kuwahi kule walipokuwa wanaelekea wenzao.
Hali hii iliwafanya hata wao kuzidisha mwendo ili wawakaribie wale watu wajue kulikoni.
"Wakuu .. wakuu wakuuuu salamualeikuuu waheshimiwaa.."
Ilisikika sauti kutokea nyuma yao ndipo walipogeuka kumuona aliyekuwa anawasalimia ndipo Kamishna Shebby na Kimaro walipotabasam baada ya kugundua alikuwa ni yule mpiga debe wa stend Chibu.
"aaah Chibu. waleikumsalaam vipi kwema."
"Aaah!! ndo hivyo bwana bado tunahema tuko pamoja na nilipowaona mnapita pale chini nikaona si mbaya niikatae tenda ya leo nikajumuike nanyi ndugu zangu ktk harakati za kwenda kumpumzisha mwenzetu."
"Harakati za kumpumzisha mwenzetu? mbona hatukuelewi Chibu?"
Aliuliza St;sajent Kimaro huku Kamishna Shebby akiwa nae kataharuki akijiuliza au ina maana mzee Mnyungunyungu hakuzikwa toka kipindi kile? wakati ilishapita wiki naa.
"Aaaah!! wakubwaa nyie si mmekuja tena kwenye huu msiba au hamuelekei kwa Mnyungunyungu?"
"Tunaelekea huko huko Chibu, sasa huo msiba wa nani tena?"
"Daah!! Mnanishangaza sasa, mi nimejua taarifa ya tukio lililotokea juzi ndio limewaleta huku kumbe sio..?"
"He!! unatuchanganya sasa Chibu kwani kumetokea tukio gani tena.!!?"
"Mnyungunyungu mtoto (jr) mzee wa nyanga na tunguli kakata kamba, yaani amekufa."
"Amekufa? mtoto yupi kwani"
"Mtoto wa Mnyungunyungu wakubwa aliyeachiwa mikoba."
"HAA!! Unamaanisha yule MGANGA?!!"
walistuka kwa pamoja baada ya Chibu kutikisa kichwa kukubaliana na swali waliloliuliza juu ya huyo aliyefariki.
ITAENDELEA..
========
"Mh! mkuu hapaaaa daah!! okeeee.. auuu au alimaanisha kwenye picha?!!"
"Swadakta Kimaro, alichokuwa ananielekeza marehemu Mnyungunyungu nimepata siri ya maana ya hayo maneno kuwa mr.X aliwahi kupiga nae picha na dalili kuu ya kumtambua mr.X ana kovu usoni mwake kwa hiyo itatubidi tuibe siku mapema wiki hii twende mkuyuni tuombe picha zote alizowahi kupiga mzee Mnyungunyungu miaka ya nyuma."
"sawa mkuu sasa tutajuaje jina halisi la mr.X kama tutamgundua kwenye picha kwa ushahidi wa hilo kovu? kumbuka atakuwa kabadilika mno kwa sasa ila jina ndio la msingi zaidi, sasa tutajuaje hapo...?"
"Naam, swali lako ni zuri lakini usiwe na wasi kwani kabla hajafa mzee Mnyungunyungu aliwahi mwambia yule mwanae mganga kuwa mr.X anamfahamu vizuri tu. kwa hiyo tutapoiona picha ya mtu mwenye kovu ktk ulbamu ya mnyungunyungu ndipo tutapomuuliza mwanae yule atutajie majina ya mtu huyo, na alikuwa nani enzi hizo na hapo itaanza kazi moja tu ya kumtafuta."
"hapo mkuu sina swali kabisa, naona mipango imekaa vizuri sana Mr.X lazima afichuke safari hii."
Aliunga mkono st;sajent Kimaro mara baada ya kusikia mazungumzo ya Kamishna wake bwana Shaaban Mwinchande.
* * * * * *
Siku ya siku ilifika ambapo kwa mara nyengine alioneka Kamishna Shaaban na St;sajent Kimaro wakiwa moto chini ndani ya Land cruzer New Model ya kijivu wakipangusa (wakiyapita) magari na kukanyaga barabara ipasavyo kuelekea kijiji cha Mkuyuni mkoa wa Morogoro.
Muda mwingi kila mmoja alikuwa bussy na yake kichwani huku wakipeana story za hapa na pale na walipoianza barabara ya vumbi iliyokuwa inaelekea morogoro vijijini ndipo st;sajent Kimaro alivunja ukimya uliotawala muda mwingi na kuyapamba mazungumzo wakati huo akiendeesha gari.
"Sasa mkuu endapo tukishindwa kuiona hiyo picha ya mtu mwenye kovu usoni unafikiria nini cha kufanya ambacho kitatusaidia zaidi"
"Mh! sidhaani kwa haraka harakaaaa... lakini we umefikiriaje kwani"
"ahkah! mi nakusikiliza wewe bosi wangu niko tayari kutii mipango yako na kufata vile usemavyo."
"Sikia Kimaro, mapigo ya moyo wangu yanadunda kwa furaha furani ambayo naiona dhahili ni ishara ya ushindi na akili zangu zinaniaminisha kabisa kwamba safari hii tutamjua Mr.X tu."
"sawa mkuu lakini inabidi twende tukiwa na mbinu mbadala pia."
"Hebu nishauli mbinu mbadala uliyonayo."
"sawa mkuu, mi nadhani itatubidi tutumie mbinu za kijeshi zaidi kum bana yule mganga mtoto wa mzee Mnyungunyungu"
"Mbinu za kijeshi? kivipi Kimaro."
Aliuliza kamishna Shebby kwa mshangao kidogo huku akimtazama st;sajent Kimaro kwanini amefikiria hilo ilhali walishapanga awali kwamba ktk mission ile hawatatakiwa kujionesha ama kugundulika wao ni kina nani hasa.
"Mkuu kuna kitu nilikifikiria sana toka uliponipa habari ya maneno uliyoyaunganisha aliyotamka marehemu Mnyungunyungu na kunijengea wazo ambalo nahisi kabisa lipo jirani na ukweli ama ndio ukweli wenyewe."
"Wazo lipi hilo tena!! hebu nambie."
"wazo kuwa ni nani anaweza kuwa mr.X"
"Mh! Kimaro acha utani hebu nifafanulie unahisi nini?"
"Akili zangu zinanambia kuwa huenda yule mganga aliyetupokea akawa ndie mr.X mwenyewe"
"Mh! unamaanisha mtoto wa mzee Mnyungunyungu?"
"Haswaa ndie huyo."
"Kivipi sasa hadi umehisi hivyo?"
"kutokana na maneno uliyoyaunganisha aliyosema mzee Mnyungunyungu na ukijumlisha hadithi ya Hussein ukigawanya tukio la barua, namba ya simu hadi kushambuliwa kule kibamba miaka hiyo.. Pia umli wake vile nilivyomuona bado akili yangu inasema kuwa mzunguko woooote uko palepale yule mganga ndie mr.X"
"Daaah! Kimaro leo kweli umeamua kuchemsha kupe walio kwenye ndonga (kichwa) langu, Mh!! lete prove ya kile usemacho."
"Sawa mkuu ninazo sababu, Kwanza kumbuka mara ya kwanza mke wa Hussein ambae ni Zai alipoonwa na baba mkubwa wa Hussein ambae ndie mzee Mnyungunyungu alionesha hali ya mshangao sana hadi kupelekea kumpa maneno ya mafumbo Hussein juu ya yule mwanamke. Hii inanijengea picha kuwa mzee Mnyungunyungu alimtambua Zai mapema kabla ya pale, inawezekana mtoto wake ambae ndie yule mganga nae walishakuwa na mahusiano... kuthibitisha hili rejea kauli za Zai kuwa hajawahi kumkatalia mwanaume aliyemtongoza ila wote akawapa mitihani ktk kumtafuta aliyempenda kweli na walishindwa wote kasoro Hussein aliweza na kumpata Zai so mmoja wa washindwaji anaweza kuwa mtoto wa Mnyungunyungu.
Pili, barua ya Hussein huenda alipewa na yuleyule mganga kwenye daladala na kwa kuwa alizijua dawa nyingi kuna uwezekano barua ile ilibeba nguvu za giza ndani yake na pindi iliposomwa na mke wa Hussein ilianza kumlevya taratibu na kujikuta anaanza kufanya mawasiliano ya siri na yule mganga pasi na kujitambua na hata siku walipokuwa wanaenda kwa ba mkubwa inawezekana waliwasiliana tena kwa msg na yeye ndie aliyemny'ang'anya mtoto Hussein na kumshambulia akishilikiana na wenzake aliowajua yeye vilevile hata Mzee Mnyungunyungu alitoa ushahidi ule kwa kumkingia mwanae kifua na kuificha ile siri na ndio sababu ya kuhama kwao ili kupoteza kabisa habari zile zisije kuzuka tetesi pale kijijini.
Tatu, Kipindi unamuuliza swali marehemu Mnyungunyungu juu ya mr.X kuna uwezekano mlaika mtoa roho alikuwa mbele yake na akashindwa kusema uongo hivyo alitaka kumfichua mwanae na ndio maana ya maneno ANA KOVU USONI.
Na hii ni dhahili kama siku ile hujamuangalia vizuri yule mganga mimi nilimuona vizuri zaidi kuwa ana kovu kubwa tu usoni.
Kwa sababu hizi kuu tatu nina mashaka ya kuthubutu kusema kuwa mtoto wa Mzee Mnyungunyungu ndie Mr.X.."
"Uuuuuuppphhhhhh!!!!"
Alishusha pumzi kwa nguvu Kamishna Shebby huku akimtazama mara mbili mbili stafsajent Kimaro pasi na kumwambia chochote na ukimya ulifuata tena baina yao kipindi Shebby alipotulia na kuanza kuyachekecha maneno na prove alizotoa Kimaro sambamba na hadithi ya Hussein.
Kiupande furani yalimuingia yale maneno na kuzishawishi akili zake kuwa akubaliane na Kimaro lakini bado upande wa pili moyo wake Ulimkatalia kabisa kuwa yule mganga mtoto wa Mzee Mnyungunyungu kuwa ndie Mr.X
** ** ** **
Ilitimu majira ya saa saba mchana ambapo waliwasili kijiji cha Mkuyuni na kupaki gari yao eneo lile lile walipopaki pindi walipokuja awali na pembeni yake kulionekana imepaki difenda ya polisi na gari ya wagonjwa, na baada ya kushuka walivuka barabara na kuelekea moja kwa moja ile njia ya bondeni ambayo walipitishwa siku ile na yule kijana aliyeitwa Chibu.
Lakini cha ajabu siku hiyo hakukuonekana watu wengi eneo lile la stendi huku frem nyingi pia zilifungwa japo ilikuwa mchana na wakati wakishusha kile kibarabara waliwaona watu kwa mbali wengi wengi mbele yao huku wengine wakija nyuma yao na kuwapita wakionesha walikuwa na haraka ya kuwahi kule walipokuwa wanaelekea wenzao.
Hali hii iliwafanya hata wao kuzidisha mwendo ili wawakaribie wale watu wajue kulikoni.
"Wakuu .. wakuu wakuuuu salamualeikuuu waheshimiwaa.."
Ilisikika sauti kutokea nyuma yao ndipo walipogeuka kumuona aliyekuwa anawasalimia ndipo Kamishna Shebby na Kimaro walipotabasam baada ya kugundua alikuwa ni yule mpiga debe wa stend Chibu.
"aaah Chibu. waleikumsalaam vipi kwema."
"Aaah!! ndo hivyo bwana bado tunahema tuko pamoja na nilipowaona mnapita pale chini nikaona si mbaya niikatae tenda ya leo nikajumuike nanyi ndugu zangu ktk harakati za kwenda kumpumzisha mwenzetu."
"Harakati za kumpumzisha mwenzetu? mbona hatukuelewi Chibu?"
Aliuliza St;sajent Kimaro huku Kamishna Shebby akiwa nae kataharuki akijiuliza au ina maana mzee Mnyungunyungu hakuzikwa toka kipindi kile? wakati ilishapita wiki naa.
"Aaaah!! wakubwaa nyie si mmekuja tena kwenye huu msiba au hamuelekei kwa Mnyungunyungu?"
"Tunaelekea huko huko Chibu, sasa huo msiba wa nani tena?"
"Daah!! Mnanishangaza sasa, mi nimejua taarifa ya tukio lililotokea juzi ndio limewaleta huku kumbe sio..?"
"He!! unatuchanganya sasa Chibu kwani kumetokea tukio gani tena.!!?"
"Mnyungunyungu mtoto (jr) mzee wa nyanga na tunguli kakata kamba, yaani amekufa."
"Amekufa? mtoto yupi kwani"
"Mtoto wa Mnyungunyungu wakubwa aliyeachiwa mikoba."
"HAA!! Unamaanisha yule MGANGA?!!"
walistuka kwa pamoja baada ya Chibu kutikisa kichwa kukubaliana na swali waliloliuliza juu ya huyo aliyefariki.
ITAENDELEA..