Simulizi: Wanawake ni wauaji

Simulizi: Wanawake ni wauaji

EPS 22
========

"Mh! mkuu hapaaaa daah!! okeeee.. auuu au alimaanisha kwenye picha?!!"
"Swadakta Kimaro, alichokuwa ananielekeza marehemu Mnyungunyungu nimepata siri ya maana ya hayo maneno kuwa mr.X aliwahi kupiga nae picha na dalili kuu ya kumtambua mr.X ana kovu usoni mwake kwa hiyo itatubidi tuibe siku mapema wiki hii twende mkuyuni tuombe picha zote alizowahi kupiga mzee Mnyungunyungu miaka ya nyuma."
"sawa mkuu sasa tutajuaje jina halisi la mr.X kama tutamgundua kwenye picha kwa ushahidi wa hilo kovu? kumbuka atakuwa kabadilika mno kwa sasa ila jina ndio la msingi zaidi, sasa tutajuaje hapo...?"
"Naam, swali lako ni zuri lakini usiwe na wasi kwani kabla hajafa mzee Mnyungunyungu aliwahi mwambia yule mwanae mganga kuwa mr.X anamfahamu vizuri tu. kwa hiyo tutapoiona picha ya mtu mwenye kovu ktk ulbamu ya mnyungunyungu ndipo tutapomuuliza mwanae yule atutajie majina ya mtu huyo, na alikuwa nani enzi hizo na hapo itaanza kazi moja tu ya kumtafuta."
"hapo mkuu sina swali kabisa, naona mipango imekaa vizuri sana Mr.X lazima afichuke safari hii."
Aliunga mkono st;sajent Kimaro mara baada ya kusikia mazungumzo ya Kamishna wake bwana Shaaban Mwinchande.

* * * * * *

Siku ya siku ilifika ambapo kwa mara nyengine alioneka Kamishna Shaaban na St;sajent Kimaro wakiwa moto chini ndani ya Land cruzer New Model ya kijivu wakipangusa (wakiyapita) magari na kukanyaga barabara ipasavyo kuelekea kijiji cha Mkuyuni mkoa wa Morogoro.
Muda mwingi kila mmoja alikuwa bussy na yake kichwani huku wakipeana story za hapa na pale na walipoianza barabara ya vumbi iliyokuwa inaelekea morogoro vijijini ndipo st;sajent Kimaro alivunja ukimya uliotawala muda mwingi na kuyapamba mazungumzo wakati huo akiendeesha gari.
"Sasa mkuu endapo tukishindwa kuiona hiyo picha ya mtu mwenye kovu usoni unafikiria nini cha kufanya ambacho kitatusaidia zaidi"
"Mh! sidhaani kwa haraka harakaaaa... lakini we umefikiriaje kwani"
"ahkah! mi nakusikiliza wewe bosi wangu niko tayari kutii mipango yako na kufata vile usemavyo."
"Sikia Kimaro, mapigo ya moyo wangu yanadunda kwa furaha furani ambayo naiona dhahili ni ishara ya ushindi na akili zangu zinaniaminisha kabisa kwamba safari hii tutamjua Mr.X tu."
"sawa mkuu lakini inabidi twende tukiwa na mbinu mbadala pia."
"Hebu nishauli mbinu mbadala uliyonayo."
"sawa mkuu, mi nadhani itatubidi tutumie mbinu za kijeshi zaidi kum bana yule mganga mtoto wa mzee Mnyungunyungu"
"Mbinu za kijeshi? kivipi Kimaro."
Aliuliza kamishna Shebby kwa mshangao kidogo huku akimtazama st;sajent Kimaro kwanini amefikiria hilo ilhali walishapanga awali kwamba ktk mission ile hawatatakiwa kujionesha ama kugundulika wao ni kina nani hasa.
"Mkuu kuna kitu nilikifikiria sana toka uliponipa habari ya maneno uliyoyaunganisha aliyotamka marehemu Mnyungunyungu na kunijengea wazo ambalo nahisi kabisa lipo jirani na ukweli ama ndio ukweli wenyewe."
"Wazo lipi hilo tena!! hebu nambie."
"wazo kuwa ni nani anaweza kuwa mr.X"
"Mh! Kimaro acha utani hebu nifafanulie unahisi nini?"
"Akili zangu zinanambia kuwa huenda yule mganga aliyetupokea akawa ndie mr.X mwenyewe"
"Mh! unamaanisha mtoto wa mzee Mnyungunyungu?"
"Haswaa ndie huyo."
"Kivipi sasa hadi umehisi hivyo?"
"kutokana na maneno uliyoyaunganisha aliyosema mzee Mnyungunyungu na ukijumlisha hadithi ya Hussein ukigawanya tukio la barua, namba ya simu hadi kushambuliwa kule kibamba miaka hiyo.. Pia umli wake vile nilivyomuona bado akili yangu inasema kuwa mzunguko woooote uko palepale yule mganga ndie mr.X"
"Daaah! Kimaro leo kweli umeamua kuchemsha kupe walio kwenye ndonga (kichwa) langu, Mh!! lete prove ya kile usemacho."
"Sawa mkuu ninazo sababu, Kwanza kumbuka mara ya kwanza mke wa Hussein ambae ni Zai alipoonwa na baba mkubwa wa Hussein ambae ndie mzee Mnyungunyungu alionesha hali ya mshangao sana hadi kupelekea kumpa maneno ya mafumbo Hussein juu ya yule mwanamke. Hii inanijengea picha kuwa mzee Mnyungunyungu alimtambua Zai mapema kabla ya pale, inawezekana mtoto wake ambae ndie yule mganga nae walishakuwa na mahusiano... kuthibitisha hili rejea kauli za Zai kuwa hajawahi kumkatalia mwanaume aliyemtongoza ila wote akawapa mitihani ktk kumtafuta aliyempenda kweli na walishindwa wote kasoro Hussein aliweza na kumpata Zai so mmoja wa washindwaji anaweza kuwa mtoto wa Mnyungunyungu.
Pili, barua ya Hussein huenda alipewa na yuleyule mganga kwenye daladala na kwa kuwa alizijua dawa nyingi kuna uwezekano barua ile ilibeba nguvu za giza ndani yake na pindi iliposomwa na mke wa Hussein ilianza kumlevya taratibu na kujikuta anaanza kufanya mawasiliano ya siri na yule mganga pasi na kujitambua na hata siku walipokuwa wanaenda kwa ba mkubwa inawezekana waliwasiliana tena kwa msg na yeye ndie aliyemny'ang'anya mtoto Hussein na kumshambulia akishilikiana na wenzake aliowajua yeye vilevile hata Mzee Mnyungunyungu alitoa ushahidi ule kwa kumkingia mwanae kifua na kuificha ile siri na ndio sababu ya kuhama kwao ili kupoteza kabisa habari zile zisije kuzuka tetesi pale kijijini.
Tatu, Kipindi unamuuliza swali marehemu Mnyungunyungu juu ya mr.X kuna uwezekano mlaika mtoa roho alikuwa mbele yake na akashindwa kusema uongo hivyo alitaka kumfichua mwanae na ndio maana ya maneno ANA KOVU USONI.
Na hii ni dhahili kama siku ile hujamuangalia vizuri yule mganga mimi nilimuona vizuri zaidi kuwa ana kovu kubwa tu usoni.
Kwa sababu hizi kuu tatu nina mashaka ya kuthubutu kusema kuwa mtoto wa Mzee Mnyungunyungu ndie Mr.X.."

"Uuuuuuppphhhhhh!!!!"
Alishusha pumzi kwa nguvu Kamishna Shebby huku akimtazama mara mbili mbili stafsajent Kimaro pasi na kumwambia chochote na ukimya ulifuata tena baina yao kipindi Shebby alipotulia na kuanza kuyachekecha maneno na prove alizotoa Kimaro sambamba na hadithi ya Hussein.
Kiupande furani yalimuingia yale maneno na kuzishawishi akili zake kuwa akubaliane na Kimaro lakini bado upande wa pili moyo wake Ulimkatalia kabisa kuwa yule mganga mtoto wa Mzee Mnyungunyungu kuwa ndie Mr.X

** ** ** **

Ilitimu majira ya saa saba mchana ambapo waliwasili kijiji cha Mkuyuni na kupaki gari yao eneo lile lile walipopaki pindi walipokuja awali na pembeni yake kulionekana imepaki difenda ya polisi na gari ya wagonjwa, na baada ya kushuka walivuka barabara na kuelekea moja kwa moja ile njia ya bondeni ambayo walipitishwa siku ile na yule kijana aliyeitwa Chibu.

Lakini cha ajabu siku hiyo hakukuonekana watu wengi eneo lile la stendi huku frem nyingi pia zilifungwa japo ilikuwa mchana na wakati wakishusha kile kibarabara waliwaona watu kwa mbali wengi wengi mbele yao huku wengine wakija nyuma yao na kuwapita wakionesha walikuwa na haraka ya kuwahi kule walipokuwa wanaelekea wenzao.
Hali hii iliwafanya hata wao kuzidisha mwendo ili wawakaribie wale watu wajue kulikoni.
"Wakuu .. wakuu wakuuuu salamualeikuuu waheshimiwaa.."
Ilisikika sauti kutokea nyuma yao ndipo walipogeuka kumuona aliyekuwa anawasalimia ndipo Kamishna Shebby na Kimaro walipotabasam baada ya kugundua alikuwa ni yule mpiga debe wa stend Chibu.
"aaah Chibu. waleikumsalaam vipi kwema."
"Aaah!! ndo hivyo bwana bado tunahema tuko pamoja na nilipowaona mnapita pale chini nikaona si mbaya niikatae tenda ya leo nikajumuike nanyi ndugu zangu ktk harakati za kwenda kumpumzisha mwenzetu."
"Harakati za kumpumzisha mwenzetu? mbona hatukuelewi Chibu?"
Aliuliza St;sajent Kimaro huku Kamishna Shebby akiwa nae kataharuki akijiuliza au ina maana mzee Mnyungunyungu hakuzikwa toka kipindi kile? wakati ilishapita wiki naa.
"Aaaah!! wakubwaa nyie si mmekuja tena kwenye huu msiba au hamuelekei kwa Mnyungunyungu?"
"Tunaelekea huko huko Chibu, sasa huo msiba wa nani tena?"
"Daah!! Mnanishangaza sasa, mi nimejua taarifa ya tukio lililotokea juzi ndio limewaleta huku kumbe sio..?"
"He!! unatuchanganya sasa Chibu kwani kumetokea tukio gani tena.!!?"
"Mnyungunyungu mtoto (jr) mzee wa nyanga na tunguli kakata kamba, yaani amekufa."
"Amekufa? mtoto yupi kwani"
"Mtoto wa Mnyungunyungu wakubwa aliyeachiwa mikoba."
"HAA!! Unamaanisha yule MGANGA?!!"
walistuka kwa pamoja baada ya Chibu kutikisa kichwa kukubaliana na swali waliloliuliza juu ya huyo aliyefariki.
ITAENDELEA..
 
EPS 23
========

"Ndio hivyo wakubwa hivi unavyoona shazi yote ipo huko baada ya mwili kurudishwa ukisindikizwa na diffenda ya polisi au hamkuiona hapo juu stendi! Noma sana wakuu mzee hakuchukua hata mwezi toka kavuta mdingi ake nae kaamua kujichinjilia mbali, ajabu sana."
"Ina maana alijiua?!!"
"Eeeeh, Alijikata koromeo wakuu, afadhali tushafika mtapata full data."
Aliongea Chibu kauli iliyowastua zaidi na kuwashangaza wakati huo tayari waliingia maeneo yale ambapo waliona watu wengi sana eneo lote la kijiji kile kuzunguka nyumba ya marehemu Mnyungunyungu sambamba na polisi wachache huku kila mtu akiwa mwenye huzuni na kutoamani kutokana na habari juu ya kifo cha mganga mrithi mtoto wa mzee Mnyungunyungu ikisemekana amejichinja koromeo mwenyewe na kujiua akiwa ndani ya Kibanda chake cha Uganga.

Hali ilitisha na kuwastaajabisha mno kina Shebby mara walipofika na kusogea pale msibani upande wa mbele kulipokuwa na turubai kubwa huku wakionekana watu wengi na ndipo walipoamua kuwasogelea wazee furani waliokuwa wamesimama wakijadili jambo na afsa mmoja wa polisi na ndipo walipowasalimia na hata wale wazee hawakupata tabu sana kuwatambua hususani Shebby.
"Karibuni sana wajukuu zangu karibuni."
"Ahsante Mzee, poleni sana."
Baada ya hapo walienda kukaa pale chini kwenye turubai kulipotandikwa mikeka mingi huku vichwani wote wawili wakitafakari habari zile kuhusu kifo cha yule mganga Mnyungunyungu mtoto ambae ndie pia walitegemea kuipata hiyo njia nyengine kuhusu Mr.X
Wakiwa wamekaa pale muda mfupi jeneza lililokuwa na mwili wa yule mganga lilitolewa na kuekwa sehemu iliyoandaliwa kwa ajili ya sala ya mwisho na kumswalia marehemu na baada ya hapo safari ya kuelekea makaburini ilianza huku nyuma kukisikika vilio mfurulizo vya kina mama.
Waliongoza pamoja kwenye msafara ule mpaka makaburini na alizikwa pembeni na alipozikwa mzee Mnyungunyungu mwenyewe aliyezikwa siku chache zilizopita.
Akiwa kasimama jirani kabisa na makaburi yale kipindi mwili wa yule mganga ukiingizwa kaburini Kamishna Shebby alitoa miwani yake mikubwa meusi iliyokuwa kwenye mfuko wa shati aliyovaa na kuitinga usoni kuficha macho yake yaliyoanza kubadilika rangi kwa uchungu aliokuwa nao wa kukosa uhakika ama kutomtambua mr.X huku akiwa bado haamini hisia alizoambiwa na st;sajent Kimaro pindi walipokuwa njiani kuwa yule ambae sasa wanamzika pale kuwa ndie Mr.X lakini pia swali jipya lililozidi kumchanganya ni kwanini amejiua?
Akiwa anatazama mazishi huku anatafakari ndipo uso wa Kamishna Shebby ulipotazamana na uso wa yule kijana aliyewapokea siku ile ya kwanza kule kibandani na kuwakaribisha ambapo babaake ambae ndie walikuwa wanamzika alikuwa ndani ya kile kibanda kama mganga mkuu wa pale baada ya hali ya mganga mwenyewe mzee Mnyungunyungu kuwa mbaya muda mrefu.

Uso wa yule kijana ambae alikuwa kashikwa mkono na mzee mmoja ulionesha huzuni sana kwani muda wote ulikuwa unatililikwa machozi tu kipindi babaake alipokuwa anazikwa.
Baada ya shughuli ya mazishi kukamilika watu walianza kutawanyika mazialani na kwa upande wa Kamishna Shebby na st;sajent Kimaro wao walikuwa ni miongoni mwa watu wa mwisho mwisho kabisa kutoka kule mazialani huku wakitembea taratibu pia wakizungumza kwa sauti za chini chini.
"Kazi ukizidisha kazi unapata Kazi juu ya Kazi. daah.."
"Yaani we acha Mkuu mi mwenyewe hapa akili yote imepigwa short kwa kutoamini hiki nikionacho."
"Hivi Kimaro unahisi kwanini amejiua? maana mi hainiingii akilini kuwa kifo cha babaake ndio kimpagawishe akili hadi kufikia hatua ya kujichinja mwenyewe!!"
"Mkuu nakubaliana na wewe kuwa kifo cha babaake hakikumchanganya akili ila pia nakubaliana na mawazo yangu kuwa yule ndie mr.X kwani nahisi kwa namna furani ujio wetu wa awali ulimuumiza hasa babaake alipotaja alama aliyokuwa nayo na huenda kajiua kwa kuficha aibu baada ya kuhisi sasa siri itajulikana kama yeye ndie aliyemchomekea kesi ndugu yake kwa sababu ya mwanamke."
"Mh!! sasa kama ndio hivyo huyo mwanamke yuko wapi?"
"Hapo hata mimi sijui labda tuchunguze majina ya wake zake labda mmoja anaweza kuwa ndie si nasikia nae alikuwa na wake watatu?"
"Mh!! ok ila kwanza Kimaro tusikurupukie huko mi navyoona sasa twende tukatoe pole zetu kwa wafiwa na tutafute mbinu gani tutaweza kuitumia ili tupate picha za Mnyungunyungu tuhakikishe kama tutamuona huyo mtu mwenye kovu au lah! ndipo tuanze kuchunguza historia na nyendo za marehemu tuone kama zinamach na mr.X"
Walikubaliana na kufika msibani kama kawaida ambapo safari hii watu walipungua sana huku wengi waliobaki walikuwa ni ndugu na majirani na baada ya kuwapa pole na kutoa mchango wao Kamishna Shebby alimvutia pembeni mzee mmoja yule anayependa kuvaa baraghashia na kuanza kuongea nae mawili matatu halkadhalika st;sajent Kimaro nae alikaa pembeni na bwana mmoja ndugu wa marehemu na kuongea nae mawili matatu na hii yote ilikuwa moja ya mipango yao kutafuta ukweli wa kifo cha yule mganga.
"..Ndio mzee wangu kwa hiyo unasema mlisikia kelele baada ya kijana wake marehemu kuingia kibandani asubuhi na kumkuta babaake akiwa amelala kwenye dimbwi la damu ameshika kisu huku koromelo likiwa nje, kwani si walikuwa wawili pale kibandani? inakuwaje hadi anajikata yule kijana asisikie pale nje."
yalikuwa ni maswali aliyokuwa anahoji Kamishna Shebby kwa yule mzee ambae nae hakuchoka kufunguka na kujibu.
"Mh! mwanangu ukweli wahenga walisema usilolijua ni usiku wa giza, kwani siku hiyo ilikuwa kawaida na siku nyengine ambapo mganga ndie anaechelewaga kufika na yule msaidizi wake ambae mwanae huwa ndie anawahi kufika, sasa ajabu siku hiyo Mganga aliamka mapema sana saa kumi na mbili kasoro akidai anataka awahi kijiweni kufanya maandilizi kuna mgeni wake muhimu angekuja siku hiyo na mishale ya saa mbili mwanae alipoenda kibandani ndipo alimkuta akiwa tayari keshakufa. Daah!! yaani ilionesha dhahili alipanga kujiua nahisi kifo cha babaake kilimchanganya sana nae kamfata alipo aaah!! mjukuu wangu hili pigo kubwa sana hapa kijijini."
Aliongea yule Babu na baada ya hapo shebby alimtuliza kwa kumpa maneno matamu ya pole kisha alimuangalia Kimaro kule alipokuwa na yule bwana mwengine na ndipo walipoaga na kuahidi wangerudi kumalizia misiba ile ambayo hitima zake zilipangiwa siku moja.

Wakiwa wameshajiandaa kwa nia ya kuondoka Kamishna Shebby ghafra machale yalimcheza baada ya kupata mbinu iliyomjia palepale na kumuomba faragha mtoto wa marehemu yule mganga na kusogea nae pembeni kidogo.
"Pole sana kaka kwa kumpoteza baba katika nyakati kama hizi nakusihi uwe na moyo wa kiume na uvumilivu wa kutosha katika kipindi kigumu kama hiki."
Aliongea kwa upole Kamishna Shebby.
"Asante kaka yote nimemuachia mungu"
Sawa ila naomba utusaidie kitu kimoja tafadhali japo najua kwasasa bado hujakaa sawa lakini naomba unisaidie kwani nitamfurahisha sana babaangu aliyenifanya nifike huku."
"Kitu gani kaka, usijali nambie tu."
"Ni hivi babaangu nae ni mzee sana lakini alikuwa ni rafiki mkubwa wa Mnyungunyungu enzi hizo na walipoteana pindi tulipohamia Nairobi kipindi hiko nilikuwa mdogo sana sasa miaka ya karibuni tumerudi nchini na baba alihitaji sana kuonana na rafiki yake mpaka akafikia kunipa data zote wapi alipo nami nikaanza kumtafuta lakini kwa bahati mbaya nimeambulia kushuhudia tu kifo chake, sasa nitawezaje kumliwaza babaangu walau kidogo niporudi tena zaidi ya kumpatia walau picha ya rafikiake kipenzi ili ibaki kuwa kumbukumbu yake pia..!! Kwa hiyo kaka nakuomba sana jitahidi uje na picha za Mnyungunyungu niangalie ipi itafaa niondoke nayo.."
Maneno ya Kamishna Shebby yalikuwa na uongo asilimia themanini ndani yake lakini yalimuingia vizuri yule kijana wala hakuhisi hata kidogo kama alikuwa anadanganywa.
ITAENDELEA...
 
EPS 24
========

"sawa ndugu yangu usijali ngoja niingie ndani nikuletee bahasha nzima uchague mwenyewe maana leo tu kuna ndugu walikuwa wanazitazama sebuleni na kuzitenganisha kwa kutunza zaidi kumbukumbu."
Aliongea yule kijana na kumuomba waingie ndani na kamishna Shebby huku wakimuacha St;sajent Kimaro nje akisubiri.
Na baada ya Shebby kuingia ndani na yule kijana ndipo alipotolewa mfuko wa bahasha ya kaki ambao ulijaa picha mbalimbali za mzee Mnyungunyungu toka enzi za ujana wake.
Moyoni Shebby alifurahi na kujiandalia umakini machoni na akilini mwake mara alipoanza kutazama picha moja moja akiitafuta picha ya mtu mwenye kovu usoni.
Lakini ajabu alitazama na kurudia karibu picha zote bila kumuona mtu tofauti mwenye kovu usoni zaidi ya yule mtoto wa mzee Mnyungunyungu aliyefariki kwa kujiua.
Alijikuta anapiga ana anado asijue picha ya kuchukua huku kichwani akijilazimisha kuamini kuwa huenda yule ndie alikuwa mr.X.
"Chukua hii kaka waliopiga babu baba na rafiki yao huyu ambae simjui lakini ni nzuri tu tena kipindi hiko baba bado kijana na hata babu hakuwa mzee sana"
Aliongea yule kijana na kumkabidhi picha moja baada ya kuona mgeni wake anachagua chagua tu picha asijue ya kuchukua.
Na baada ya Kamishna shebby kupokea ile picha alijifanya kufurahi japo akili yake ilishavurugika baada ya kuikosa hiyo picha yenye mtu mwenye kovu usoni kisha akatoka na kujumuika na st;sajent Kimaro na kuondoka.

** ** **
"Haiwezekani Mkuu, mi nilikwambia yule ndie mr.x tu. Umeamini sasa!!"
Aliongea Kimaro huku akipiga piga usukani wakati walipokuwa njiani kilomita chache toka watoke Mkuyuni.
"Mh!! kwa kweli Kimaro najilazimisha sana kukubali lakini bado upande wa pili moyo wangu unanipinga."
"Kwanini sasa Mkuu wakati vielelezo vyote umeviona? Yaani prove niliyokupa imeenda vilevile sasa wewe una prove ipi ambayo inakuaminisha kuwa yule sio mr.X?"
"Unataka nikupe prove..!?"
"Ndio Mkuu lakini samahani si kwa amri yangu ni kwa matakwa yako mwenyewe Mkuu"
"Sawa. Geuza gari haraka turudi twende kituo kikuu cha polisi Mkuyuni."
"HE!! kivipi sasa Mkuu"
"tofauti ya prove zako na zangu ni hivi.. wewe Kimaro una prove za maneno sana kwa kuunganisha matukio katika hali ya kufikirika ila mimi nina prove za vitendo sana katika kuunganisha matukio kwa vitendo halisi. Sasa GEUZA GARI MARA MOJA."
Aliongea Kamishna Shebby safari hii akiwa serious kupita kawaida hadi sauti yake ilibadilika mno na maneno yake ya mwisho aliongea kwa ukali kidogo na kwa sauti ya juu hadi Kimaro alishangaa na kuogopa kidogo baada ya kuona best ake mkuu wake akimuwekea uso wa mbuzi na kutumia wazfa wake ambao mara nyingi alikuwa hamuoneshi.
"SIMAMISHA GARI KIMARO."
Sauti hii ya juu kutoka kwa Shebby ilimfanya Kimaro kufunga breki za ghafra na kumshangaa inakuwaje Kamishna anachanganyikiwa na kubadilika ghafra kiasi kile.
"Shuka."
"Eeh!!"
"Shuka Kimaro Nipe funguo"
"Lakini mkuu sijakaidi agizo lako nilikuwa natafuta sehemu nzuri ya kugeuza."
"Tusibishane Shuka."
Aliongea kwa msisitizo Shebby huku akiwa amefungua mlango wa upande wake na kushuka na kuzunguka upande wa pili na kumfanya Kimaro nae ashuke huku akiwa na taharuki kubwa kwani hakuwahi kumuona Kamishna wake akiwa serious kiasi kile toka afahamiane nae.
"Zunguka kaa upande niliokaa"
"sawa mkuu"
Alitii haraka haraka Kimaro na kumuachia funguo Kamishna Shebby nae kukaa upande wa abilia kisha ndipo Shebby alipoitoa gari kwa kasi kwenye barabara ile ya vumbi ambayo haikuwa ikitumika sana na magari mara kwa mara na baada ya gari kuchanganya huku Kimaro akiwa kajifunga mkanda akimuangalia mkuu wake aliyekuwa bussy na usukani na ndipo ghafra gari ikiwa mwendo kasi Kamishna Shebby alivuta hand break na kupelekea gari kuzunguka kama zile za mashindano na kugeukia ilipotoka na bila kuremba Shebby alishusha hand break haraka na kuchochea mafuta kama ileile ambapo sasa walikuwa wanarudi Mkuyuni huku eneo zima la barabara kukiwa kumetimka vumbi kubwa sana.

Sio siri mwendo kasi aliokuwa anatembeza Shebby hata Kimaro mwenyewe ulimtisha kwani ilifikia Kipindi hata kokoto na mashimo yaliyokuwepo barabarani hayakusikika kabisa na kwenye miinuko na matuta gari ilipaa hadi watu waliokuwa maeneo ya pembeni ya ile barabara walibaki wameshika vichwa.
Hadi wakati huo st;Sajent Kimaro hakujua prove gani aliyokuwa nayo Kamishna wake na kwa jinsi alivyom badilikia alishindwa kabisa kumuuliza na kubaki akisali kimoyomoyo wafike salama kwani aliona dhahiri shahili mwendo ule haukuwa na usalama hata kidogo.

Kwa speed ya dakika tisa tu badala ya Arobaini kwa mwendo uliotumika toka pale alipogeuza gari Shebby na Kituo kikuu cha polisi Mkuyuni ambapo hadi polisi waliokuwa Kaunta waliacha shughuli zote na kuhamaki huku wengine wakiandaa bunduki zao wakihisi huenda wamevamiwa kwa jinsi gari ile ya kina Shebby ilivyoingia na Kupaki mbele ya Kituo.

"Twenzetu.."
aliongea Shebby baada ya gari kusimama na kushuka sambamba na Kimaro kuelekea mule ndani ya kituo kwa mwendo wa kikamanda.
"Haroo, mbona hamji kistaarabu kina nani nyinyi."
aliuliza askali mmoja aliyekuwa na cheo cha Coplo pindi alipotaka kuwazuia mlangoni kina Shebby kabla hawajasogea kaunta lakini punde shebby alipotoa na kuwaonesha kitambulisho chake tu askali wote waliokuwa maeneo yale walikakamaa na kumpa heshima stahiki kisha walimkaribisha na moja kwa moja walipelekwa kwa mkuu wa kituo kama jinsi alivyotaka Kamishna Shebby mwenyewe.

Kwa bahati nzuri pindi mkuu wa kituo kile alipoonana na Shebby tu walijikuta wote wakishangaana na kutoamini macho yao baada ya yule mkuu wa kituo kumpigia saloot Shebby pindi alipotoa kitambulisho.
"Shebby!!!?"
"John!!"
"Aaagh! kweli milima haikutani kumbe upo huku?"
walipeana mikono Kamishna Shebby na yule mkuu wa Kituo ambae ilionesha dhahili walifahamiana vizuri tu.
"Enhee, vipi familia tayari?"
aliuliza Shebby huku akisogeza kiti na kukaa wakati huo wote Kimario alikuwa kakaa pembeni akitazama mazungumzo ya wakubwa zake licha ya kuwa wote umli wao uliendana endana.

ITAENDELEA.........
 
EPS 25
========
"aaah! wea acha tu habari za wanawake ndio sitaki kabisa kuzisikia"
alijibu yule mkuu wa kituo huku akionesha yuko serious na kile anachozungumza na kumshangaza Shebby ambae alihoji.
"Kivipi tena John.?"
"Ndugu yangu yaliyonitokea ndio sitamani kabisa kutafuta familia kwa sasa wee acha tu, nahisi nina mikosi sana kwa wanawake"
"Duh! John.. kwani nini kilikupata mshkaji baada ya kuachana kipindi kile kozi ilipoisha wakati ulinambia ulitaraji kufunga ndoa siku si nyingi?"
"Ndugu yangu Shebby ni story ndefu sana ila nitakuhadithia kwa ufupi ilivyokuwa"
Aliongea John ambae alikuwa na wadhifa wa OCS kituo cha mkuyuni akiwa na cheo cha Inspecta na kuanza kukumbuka ilivyokuwa toka mara ya mwisho walipoachana na Shebby walipokuwa kwenye kozi maalum ya uongozi na usimamizi ndani ya idala ya ulinzi wa ndani miaka minne iliyopita ambapo John alianza kusimulia ilivyokuwa hadi kupelekea awe na msimamo wa kutohitaji kuwa na mwanamke kwa kipindi kile.

'''''
"Ndugu yangu, mkuu wangu kiukweli kama ulikuwa hujui leo nitakwambia ujue wazi ukae ukijua kuwa wanawake ni watu wa ajabu sana inatakiwa uwe na akili nyingi sana jinsi ya kuishi nao.
Kumbuka siku ile ya mwisho tulipokuwa tunaagana kwenye ile tafrija baada ya kozi kuisha nilikuonesha kwenye simu yangu picha ya mwanamke nilietaraji kumuoa baada ya kumaliza kozi na kupandishwa cheo kwani nilijua sasa maisha nitakuwa nishayaeka kwenye mstari tena kwa kuwa na mwanamke mzuri kama Tedy aaaah, nilijiona bonge la mjanja.
Sikia sasa ishu ilivyokuwa baada ya kuachana na kupoteana kipindi tulipomaliza kozi na kupewa likizo ya mwezi mmoja sikuamini nilichokikuta mtaani Dah!!..... Kumbe yule demu Tedy si alikuwa ananiigizia bwana, muda wote naeka nae malengo hata nikawa najinyima na kumtumia pesa tulipokuwa Kozini ili afungue mtaji wa saloon kama alivyonambia kumbe nae alikuwa anatumbua maisha na mpuuzi mmoja mchafumchafu mtoto wa mtaani pale na kunigeuza mimi chuma ulete.
Sio siri niliporudi almanusura niue mtu kwa hasira mara baada ya kupata data zote na nilipokuwa namuulizia kuhusu hiyo saloon alinizungusha zungusha kunipeleka hadi waliponasa kwenye mtego niliowatega ambapo kwa macho yangu niliwafuma wakiingia Guest moja huko Keko na nilipompigia Tedy kumuuliza alipo alivyonambia ndio nilizidi kuchoka daah! Eti 'ooh, nimeenda kwa bibi vikindu anaumwa sana nitakupigia baadae'...... Nilichomjibu nikamwambia kuwa hiyo guest haiitwi vikindu inaitwa Mumbu na hapo nilikata simu na kufata ushauli wa mzee wangu tuliekuwa wote kwenye gari ambae alinisihi mno nisipaniki wala kumchukia mwanaume aliyelala na mchumbaangu kwani mwenye makosa hasa ni mchumbaangu nami nikakubaliana na mzee nikaachana na Tedy toka siku hiyo nikampiga stop tusijuane tena.
sasa hiyo tisa kumi ni Angelina au malaika ndivyo nilivyopenda kumwita mtoto kutoka Arusha aliyekuja kufanya kazi za ndani nyumbani kwetu kipindi hiko kabla sijahamishiwa hapa Mkuyuni na kuwa ocs.
Angelina alikuwa mzuri, mwenye adabu na heshima, kila mtu nyumbani alimpenda kuanzia mzee mama na dada na hata tukashawishika tufanye mipango ili nimuoe na awe mmoja wa familia yetu.
Sasaa sijui nisemeee ujingaaaaa auu utahiiraa yani nashindwa kuelewa hawa wanawake vichwa vyao vilivyo kwani kipindi chote tunafanya mipango na kuzungumza na mamaake huko kijijini walionesha hali ya kukubali kumbe bwana yule mtoto Angelina alikuwa tayari mke wa mtu muda mrefu na alikuja Dar kufanya kazi za ndani kwa lengo la kumsubiri mumewe aliyekuwa migodini huko ataporudi nae arudi waendelee na maisha.
Sio siri hii iliniuma mno nilipokuja gundua na kushindwa kumuoa mwanamke ambae tayari moyo wangu ulishaelekea kwake na kuniangusha baada ya kusikia mumewe amerudi na mambo yamemuendea vizuri baada ya mgodi kutema na karudisha mapenzi kama kawaida.
Hapo nilipagawa sana na ndipo babaangu mzee Cyprian aliponihadithia kisa kimoja enzi zake kilichotaka kufanana na changu tena kutoka huko huko Arusha alimuona bint akiwa na askali mwenzake walipokuwa kikazi na kufanya utafiti na kueka nae mipango.
Lakini kwa kuwa mzee kipindi hiko tayari alikuwa na cheo kikubwa swala la ufatiliaji zaidi na habari alizituma kupitia kijana wake wa kazi ambae walikuwa marafiki kama mimi na wewe kufikisha salamu zake kwa familia ya yule binti na zawadi mbalimbali.
Kumbe bwana rafiki ake nae si alikuwa anampenda yule bint..!! na alipokuwa anaenda kule anajiwakilisha yeye ndie mtakaji na mzee wangu alipokuja kugundua ilikuwa tayari too late.
Lakini binti mwenyewe alimjua mzee wangu ila alikubali kumsariti na rafiki yake sijui kwanini yaani wanawake usiwaamini hata kidogo.
Ila kwa dua za mzee na jinsi alivyosononeka kumkosa yule binti ndipo ikatokea safari iliyomfanya nae rafikiake amkose yule bint na kuchukuliwa na jamaa gani sijui ambae mwishoe nasikia kumbe yule bwana alikuwa na tamaa ya utajiri si akamuua kinyama yeye yule binti sambamba na mtoto aliyezaa nae na hapo ikawa si Mzee wangu wala yule rafiki ake aliyeweza kuishi na yule binti lakini yoooote yalisababishwa na binti mwenyewe laiti angekuwa na msimamo awali wa kumkataa yule rafikiake mzee aliyeanza kumchombweza na kumpondea mzee pengine haya yale yote yasingetokea hadi kuangukia mikononi mwa huyo bwana aliyekuja kumuua.
Daaaah! basi bwana ndio hivyo mzee hamasa zake nilizielewa na baada ya hapo kila mwanamke ninaemuona mbele yangu kuna muda namuona kama kinyago vile kwa jinsi walivyonipotezea malengo na pesa bila faida yoyote. Saivi ishu yangu nikijisikia navuta cheche tu la bar basi tunamalizana kila mtu kimpango wake hahahahahaaaa.."
'''''''

Alimalizia kwa kucheka ocs John na kumuacha kamishna Shebby katika taharuki kubwa hata Kimaro nae alikaa vizuri pindi alipokuwa anaisikiliza story ya ocs John.

"Enhee, Mkuu wangu safari hii wapi sasa na wewe uko wapi"
aliuliza John
"Daah, nilikuja kwenye msiba huu uliotokea sehemu yako juu ya mganga wa kienyeji aliyekutwa amejichinja kibandani mwake sasa nilitaka kujua tafiti zenu mlipofikia na awali sikuwaza hata chembe kama ningekutana na mtu tunaefahamiana kama wewe"
"Oooh! ni kweli bwana Dah! uchunguzi wetu bado unaendelea taratibu ila tuliruhusu mazishi yaendelee baada ya ripoti ya daktari kuthibitisha kuwa hakukuwa na kiashilio chochote kuwa marehemu alishambuliwa zaidi ilionekana ni msongo wa mawazo ulichachamaa ghafra na kupelekea kujichinja.
Ila tukiwa kama polisi bado uchunguzi wetu hatujaufunga rasmi."
"Sawa vizuri John"
aliongea Kamishna Shebby huku mawazo yake yakiipitia story aliyosimuliwa muda mfupi na ocs John hasa kwenye kipengele alichonukuu story iliyomuhusu babaake kidogo ilimtia shaka Shebby na kuhisi kuna vitu vinaingiliana na story ile ya Hussein kuhusu mkewe Zai.
Alitamani kumuuliza zaidi lakini alitafakari njia ipi ya kumuingiza tena kwenye ile mada hadi afunguke zaidi kuhusu story ya babaake.?
Na ndipo hatimae Shebby aliliacha lile na kurudi kwenye azma yake juu ya prove aliyotaka kumuonesha Kiamro kuwa yule aliekufa si Mr.X japo alikuwa na kovu usoni.

"Sasa John hebu achana na ripoti ya daktari nihadithie kuhusu nyinyi mlivyopata taarifa ya kifo kile na mazingira mliyokuta hivi ni kweli yaliwapa picha kuwa yule mtu alijiua?"
aliuliza Shebby sasa akiwa serious kama alivyokuja na kumfanya hata ocs John kukaa makini kwa utulivu mara baada ya kuulizwa lile swali na kama kawaida yake Shebby aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali kulipokuwa na simu yake special aliyoitumia kwaajili ya kunasa sauti kwani ilikuwa na uwezo mkubwa sana wa kurekodi pindi ocs John alipoanza kuzungumza.
ITAENDELEA.....
 
_________________
EPS 06
========

Simulizi iliyoshiba hisia ilimuumiza kila taswira ya matukio ya maisha yake ilivyomjengea picha ubongoni. Na zaidi alipofikia pale alipojuana na Zai msichana mrembo wa ndotoni aliyekuja kuwa dhahiri alikumbuka mengi sana. Msichana aliyemshangaza kwa kumtaja jina lake la utani tena la utotoni pasipo kumtajia mwenyewe. Msichana aliyemuonesha mapenzi na kuwa tayari kuvumilia masharti magumu. Masharti ambayo yalificha siri kubwa ndani yake ambayo alipuuza kuijua. Ndipo alipojikuta akishindwa kabisa kuendelea kusimulia baada ya maumivu ya moyo kuzidi uhimili wa hisia. Wakale walisema, ukimuona mtu mzima analia mbele za watu! ujue kuna jambo. Hapo ndipo kamishna Shaaban alipolivaa jukumu la kumfariji na kumsihi kwa maneno matamu ambayo hayakumfanya atulie mzee Hussein aliyezidi kunung'unika katikati ya kilio akisisitiza kuwa 'wanawake ni wauaji.'

*<>* *<>* *<>*
<EnDeLeA>
_______
Kum bembeleza mtu mzima ilikuwa si kazi ndogo pia muda nao ulienda sana na kutokana baadhi ya watu kuanza kutega masikio kujua kulikoni hasa walipoona kuna mtumzima mmoja alietinga suti kali ya heshima anatokwa machozi hivyo kama unavyojua ukimuona mtu mzima analia mbele za watu ujue kuna jambo na kwa kukwepa kujaza watu ndipo Kamishna Shebby sambamba na vijana wake waliamua kuondoka haraka na kurejea gerezani na baadae baada ya kurudishwa kwenye chumba cha siri na kuvalishwa nguo zake za gerezani aliamuru Hussein ahamishwe toka sero za awali na kupelekwa sero za v.i.p ambako walifungwa watu wenye pesa na viongozi wakubwa.

Ndipo siku nyengine ilikuwa saa sita za usiku Babu bubu (Hussein) alichukuliwa kama kawaida na kupelekwa kwenye chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na masofa mazuri huku kamera mbalimbali zilitegwa na kamishna Shebby pasi na kujua yeyote kwenye chumba kile ndani ya makao ya Kamishna gerezani pale ndipo Hussein alijikuta akiendelea kuhadithia ile story ambayo aliapa awali kuwa ingebaki kuwa siri moyoni mwake.

* * * * * *
.......
< MASWAHIBU >
(MIAKA 29 ILIYOPITA)
<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<<>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

Kiukweli japo masharti aliyonipa Zai yalikuwa magumu sana lakini kutokana na upendo wa ajabu niliokuwa nao nilijikuta navumilia na kusubiri na taratibu miezi ikasonga na nikaanza kuisoma tabia nzuri na ya kipekee aliyokuwa nayo Zai.
Kwanza alipenda dini alikuwa muislam safi sana pili alikuwa ana akili za kipekee mno na zaidi ya yote alijiheshimu tofauti na wasichana wengi niliowajua.

Siku zilisonga na hatimae mwaka mmoja ulikatika na siku hiyo Zai alinipigia simu tena kuwa anakuja getto nami nikafanya usafi harakaharaka na alipofika siku hiyo nilishangaa jinsi alivyokuja huku akiwa na begi kubwa la nguo na zaidi ni mada aliyokuja nayo nikajikuta nabaki mdomo wazi pale aliposema.

“Hussein amini mimi ni wako na sasa nimekuwa wako rasmi. Najua huna kipato kikubwa lakini una uwezo wa kunioa hata kesho, ukweli mi huku sikuja kusoma wala sina ndugu zaidi nilikuja kufanya kazi za ndani tu kwa mama mmoja wa kichaga aliyekuja kuniomba kwetu ila samahani nilikudanganya awali na kukupa masharti yote yale kwa lengo la kukujua vizuri ili uniimanishe kama umenipenda kweli au umenitamani na wanaume wote walionitongoza na kuning’ang’ania niliwakubalia wote na kuwapa masharti hayo matatu na woote walijitahidi kuvumilia lakini walishindwa baadae na hakuna hata aliyefika miezi sita lakini wewe umekuwa wa ajabu kwangu na naamini ndie mume bora kwangu… naomba unipokee kwani kule nimeondoka rasmi kutokana na manyanyaso na tabia za pale nyumbani.”

Nilibaki namuangalia Zai kile alichokuwa anakisema huku nikifikilia kichwani mwangu nimkubalie harakaharaka vile au kuna uongo anauendeleza tu kwani baadhi ya mambo ya Zai yalinistaajabisha kidogo hasa kuniamini na kunambia mi ni waajabu ilihali tulikuwa hatukai wote lakini kiukmweli toka niachane na Mamu sikuwahi kufanya ngono hadi dakika ile.
Na ukichochea upendo niliokuwa nao na uzuri wa Zai nilijikuta namkubalia na kupanga nae safari siku tatu zijazo twende huko kijijini kwao Arusha.

Ulipotimu usiku kwa mara ya kwanza baada ya Zai kusali alipanda kitandani na kulala pamoja na mimi huku akiwa kava gagulo na kiblauz alinibusu na kunambia kuwa nisitamani wala ntusifanye ngono hadi siku tutayofunga ndoa na kuninong’oneza kuwa yeye ni bikra pia.
Moyoni sikuamini hata kidogo alichosema Zai kwani alikuwa mrembo mno si rahisi kudumu na bikra hadi umli ule… niliona kuwa sasa nadanganywa na ktk umli wangu wote ule nilikuwa sijawahi kukutana na mwanamke bikra.

Usiku huo usingizi haukuja kabisa kila mara nilimuangalia Zai alivyolala umbo lake zuri lilivyojichora namba nane nilijikuta paipu yake inasimama na nyege za mwaka zikisisimua mwili wangu baada ya taswira za pepo chafu kutawala hisia zangu nilijikuta najisogeza karibu kabisa na Zai na kuanza kumpapasa kiuno na taratibu nilianza kupeleka mkono ndani ya gagulo lake na kukutana na kufuri lake lililoficha sehemu zake za utamu na kujikuta mate yakinijaa mdomoni kama fisi mwenye njaa aliyekutana na mzoga mbele yake.

Niliendelea kumpapasa taratibu nikiwa makini kabisa ili nisimstue usingizini na hatimae mkono wangu hususani vidole vyangu vile vya kati viliweza kupenya katika pachupachu ya chupi na kukutana na kajoto ka ajabu kutokea kwenye mashine ambayo sikuamini kama kweli ni mpya kabisa na haijawahi kutumiwa hapo kabla.
Katika hali nisiyoitarajia nililazimisha kwa ustadi mkubwa kupenyeza kidole changu kile ambacho ukimnyooshea mtu lazima mgombane,
Sikuamini pindi nilipoona kila dariri kuwa ni kweli ile mashine ilikuwa mpya na nilipolazimisha kupenyeza kidole kwa kuvisukuma vile vijinyama vilivyoziba njia Zai aliruka na kushtuka kwa sauti ya juu name kuutoa mkono haraka na kujigeuzia pembeni kwa speed ya hali ya juu.

“Hussein baby kwanini unataka kunifanyia hivyo?... tuseme huniamini nilivyokwambia!!? Mimi ni bikra kweli sijawahi kuguswa na mwanamme yeyote na niwewe pekee niliyekuamini na nahitaji uwe mume wangu wa ndoa ndio itakuwa raha siku utayonifungulia njia hii ya starehe ya wapendanao… baby najua una hisia lakini naomba vumilia tuu honey”
Maneno ya Zai yaliweza kumrusha ibilisi aliyenishika ghafra na kujikuta Napata moyo na nguvu na kumkumbatia huku nikimuomba samahani na kumuahidi sitamgusa tena mpaka tutapooana.
“So sorry baby.. sitorudia tena ni shetani tu alinipitia nikataka kukujaribu ili nihakikishe but sitorudia tena mpaka siku tutapohalalisha ..”
Niliongea maneno haya kwa busara ya hali ya juu nae Zai bila kinyongo aliniitika kwa kichwa na kunibusu kisha tukalala na sikumgusa tena hadi kulipokucha na mishe mishe ziliendelea hususani kwenda kukata tiketi kwajili ya safari huko kwao na siku mbili baadae niliaga tena kazizni ambapo nilipewa likizo ya wiki moja kwaajili ya kumaliza msiba niliodanganya awali na kutumia fulsa hiyo kusafiri na Zai mpaka jijini Arusha ambapo tulipanda tena gari lililotupeleka vijiji vya ndani ndani kabisa.
ITAENDELEA.....

Hussein alitaka kumtoa Zai bikra kwa kidole cha kati...

hehehehe...


Cc: mahondaw
 
Ni kweli kabisa... wanawake wana visirani sana visvyo na kichwa wala miguu...

Mwenzake kutokupokea simu, anaanza kumshutumu, kaja mbio mbio akidhani atafumania lakini holla!

Bado akaendelea kutafuta sababu kwa kisingizo cha jamaa kuangalia kipindi kinachohusu wanawake ni wauaji basi imekua kosa...

Hahahaha...


Cc: mahondaw
kwa hiyo na huyu uliyemtagi naye ni mmoja wao
 
Mbona kimya story haiendelei jamanii nataka kumjua Mr.X na mwisho wa bwana Hussein kula lupango
 
EPS 09
========

Saa tatu kasoro usiku tulishuka eneo husika na kuchepuka kukifata kibarabara chembamba kilichoelekea huko alipopatikana ba mkubwa ambapo kulikuwa na umbali wa kilometa kama mbili kukifikia hiko kijiji.
Kwa kuwa ulikuwa usiku na giza lilishaingia huku kukiwa na kijimbaramwezi kwa mbali ilibidi tutumie tochi kumulikia na njia nzima kulikuwa kimya sana.

Nakumbuka baada ya mwendo kidogo tukiwa tumebakiza kama kilometa moja na nusu kufika mke wangu aliniomba ajisaidie haja ndogo kwani alibanwa mno na asingeweza kuendelea mbele nami nilimuonya ajisaidie palepale njiani asiingie polini kwani kuna wadudu wengi kwenye majani na ndipo nilipompokea mtoto na kusimama kumsubiria.

Nikiwa nimesimama mke wangu anajisaidia ghafra nilisikia chakala chakala na nilipogeuka nilishangaa kumuona mtu aliyevaa kininja akininyang’anya mtoto kwa nguvu na kabla sijafanya lolote kujitetea mara kwa nyuma nilipigwa na kitu kizito bila kumuona aliyenipiga na kujikuta naanguka chini huku kwa mbali nilisikia ukulele wa mke wangu kipenzi Zai akisema.

‘’’’’’Jamaaniii iiiinatoshaaaaa Nilishawaaambiaa msimuuueeee..’’’’’

Sitoweza kuisahau kamwe kauli ile ya Mke wangu Zai.. Zai wangu kipenziii msichana wa ndoto yangu niliyeamini nimeoneshwa na Mungu lakini leo hii anatoa kauli iliyoniaminisha na kuniumiza moyo wangu kupelekea kupoteza fahamu pindi nilipoanguka baada ya kugundua kuwa kumbe mchezo wooooooootee nae alihusika na aliujua vizuuuuri. looh!
Ama kweli adui wako mkubwa ni mtu wako wa karibu na Udhaniae ndie sie ila sie ndie.
Nilijihisi nakaribia kufa huku nikijiuliza kumbe Zai aliishiii kwa kuniigiziaa?!! aaaaaghh!!!!!… Ni vigumu sana kuaminilll! lakini Chunga sana baaabaa Kamishnaaa usiombe kabisa yakukute kama yaliyonikutaaaa.
Siku hiyo ndio kwa mala ya kwanza niliikubali thabiti ile kauli kuwa Wanaake ni Wauaji, nami nakazia kabisa leo hadi siku ya kufa kwangu nitasema kuwa WANAAKE NI WAUAJIIIIII.

*<>* *<>* *<>*

Kilifuata tena kilio cha sauti ya juu na kwikwi kutoka kwa Hussein na kazi ikabaki kwa Kamishna Shaaban Mwinchande kum bembeleza na kumtuliza ili apate kuelewa na kubaini kilichoendelea ktk hadithi yake baada ya kurudiwa na fahamu.
Safari hii sasa hata Kamishna Shaaban mwenyewe alijikuta nae machozi yakim bubujika kwa jinsi alivyokuwa anasikiliza kisa kile cha Hussein na zaidi alipomtazama uso wake wa kiutuuzima uliokuwa unatiririkwa machozi kama mtoto kadri alipokuwa anasimulia na alionesha dhahili kuwa ana ghadhabu kubwa juu ya wanaake kwani ktk hadithi yake ile hadi muda huo ilibeba maumivu tu na mateso yote ameyapata sababu ya mwanamke aliyempenda na pia kwa uzoefu wake wa kusoma saikology za watu Kamishna shebby alizidi kumuamini na kubaini kuwa kweli mfungwa yule alionewa na hakuwahi fanya ubaya wowote.
Lakini maswali bado yalibaki kichwani mwa Kamishna Shebby na alitaka kujua zaidi ilikuaje hadi kukawa na uthibitisho wa maiti hizo mbili ya mkewe na mtoto? na iweje huyo Zai mke wa Hussein afahamiane na hao watu na kueka mbinu kisha wamgeuke pia na wamuue sambamba na mtoto? ilikuwaje kuwaje hapo... na huyo Mr. X ni nani kwa mujibu wa barua ya kutatanisha aliyoipata Hussein.
Japo alikuwa mtaalamu sana Shaaban na alijaliwa ubongo mwepesi ktk kufikiri na kufumbua jambo lakini kwa maswali yale yaliyosumbuka kichwa chake muda ule juu ya hadithi ya Hussein hakuweza kupata majibu ya haraka zaidi ya kumsihi mfungwa wake (Hussein) ajikaze ili aendelee kumsimulia kilichotokea baada ya kurudiwa na fahamu mpaka kukamatwa na kuhukumiwa.

Siku hiyo Hussein japo maumivu yalikuwa mazito mno moyoni mwake kwa kukumbuka mapito yaliyoinyamazisha ndoto zake na kujikuta anazeekea jera akisubiri kifo tu lakini alijitahidi na alipania kuwa aweke kila kitu wazi kwa kijana yule ambae awali hakutambua kama ndio kamishna lakini sasa alijua na hakuwa na jinsi zaidi ya kumuelezea kila kitu hasa baada ya kugundua ni askali kiongozi mwenye moyo wa kipekee sana.

Huku akifuta mafua baada ya kimya cha zaidi ya dakika arobaini Hussein aliendelea kusimulia ilivyokuwa mara baada ya kupigwa na kitu kile kichwani hali iliyompelekea kuanguka na kupoteza fahamu.

*<>* *<>* *<>*
..........

Nilistuka mara baada ya kuhisi hali ya ubaridi na unyevunyevu na nilipotaka kuamka nilijihisi kichwa kuwa kizito sana lakini nilijitahidi na kukaa kitako pale njiani huku nikitazama huku na huko kuangalia kama kuna watu wanakuja niombe msaada ama sivyo nikusanye nguvu nipige mayowe raia waje wanisaidie japo nilijua kuwa pale nilipo kuna zaidi ya kilometa moja kufika kwenye makazi ya watu ambako ndiko pia alipatikana babaangu mkubwa yule mganga wa kienyeji na ndio nia ya safari ile tulikuwa tunaelekea kwake.
Sikujua ilinichukua muda gani mpaka niliporejewa na fahamu kwani nilijikuta niko mwenyewe pale chini.

Lakini niliponyanyua mkono wangu na kutokana na mbalamwezi kuchomoza muda ule nilishangaa kuona umetapakaa damu halkadhalika na mkono mwengine.
Nilijikagua haraka haraka kuona wapi nimeumia lakini bado sikuhisi jeraha lolote mwilini mwangu zaidi ya jeraha dogo kichwani ambalo lilikuwa halivuji damu kivile.
Lakini pia nilipoangalia chini vizuri nilishangaa kuliona panga usawa ule nilipolala likiwa limeloa damu pia kulionekana michilizi ya damu kuelekea kwenye kichaka kimoja eneo lile.
Nilijikuta nikilishika lile panga kwa mshangao na kuligeuza geuza kuhakikisha kama ni kweli au macho yangu yalikuwa bado yana mawenge,! lakini nilipofanya vile akili iliniaminisha kuwa kile nikionacho ni kweli wala si mawenge na hapo ndipo nilipogutuka na kulitupa haraka chini lile panga na kujikuta nimepata nguvu za kusimama na kuanza kunyata kwa umakini kufatilia ile michilizi ya damu kujua nini kilichopo pale kwenye kichaka.
Lakini kabla sijakifikia kile kichaka mara nilianza kusikia kelele kelele za watu wengi waliokuwa wanakuja kwa mwendo wa kasi wakitokea ile njia iliyoelekea kijijini na punde tu nilipogeuka niliona mianga ya tochi ikinimulika huku kwa mbali nikisikia baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wale watu.

"Mwanaharamu mwenyewe si ndio yuuleeee.."
"Enheeeee yule yule si unaona midamu ilee.."
"Aliyeua auaweeee hebu tupisheni sie mbona hamtembei tutamkosaaa.."

Zilikuwa ni moja ya kauli nilizozisikia toka kwa wale watu huku wengine wakianza kukimbia kuja pale niliposimama nami nikabaki nimeganda kwanza nikiwashangaa na nilipokaza macho kutazama vizuri niliwaona wengine wakiwa wamebeba silaha za jadi na macho yao wote wakinilenga mimi hasa baada ya kunionaa.
"Uuuuuaaaa Huyooooo.."
"PIGA UUAAA.."
Ukelele huu ambao uliambatana na kurushwa kwa mkuki ambao kwa bahati nzuri ulinikosa na ndipo akili ikanicheza na kunionya endapo nitachelewa sekunde kadhaa watu wale wataponikaribia zaidi wataniua kwani walionesha wazi walikuwa hawaji kwa wema wala huruma hata chembe juu yangu.
Nilijikuta naruka na kuanza kutimua mbio huku upepo mkali ukinipitia ghafra karibu na kichwa baada ya kurushwa kwa rungu moja kubwa ambalo niliamini lingenipata huenda ningezima pale pale kama sio kufa kabisa.

Nilikimbia kwa speed ya kunusuru maisha yangu huku nikifata kile kibarabara kilichoelekea barabara kuu kule tulipotoka na nyuma yangu bado niliandamwa na watu wale wenye hasira kali ambao sikuwa na uhakika wa moja kwa moja kuwa ni wanakijiji au ni miongoni mwa wale walionivamia awali!?
Lakini kabla sijafika mbali mbele yangu kulisikika mlio wa gari sambamba na mwanga mkali wa taa zilizonizuia kuona vizuri na kujikuta naingia porini lakini mara ile gari ilisimama ghafraa na nilisikia vishindo vya watu wakiruka na kunizunguka huku ukelele wa mlio wa risasi ukisikika kuwatuliza wananchi waliokuwa wanakuja ndipo nilipotulia hasa baada ya kusikia kauli zao na kugundua kuwa walikuwa ni polisi.
"tulia hivyo hivyo usikimbie zaidi mikono juu sisi ni maafsa wa polisi.."
Ilikuwa ni sauti ya mmoja wa watu walioruka kwenye gari akinisihi na kunisogerea pale niliposimama huku nami nikitii na kuona sasa afadhali msaada umepatikana.
ITAENDELEA….

Daah!
Inasikitisha sana... bado sijapata picha kwa nini Zai mke wa Hussein aamue kumaliza mume wake...


Cc: mahondaw
 
EPS 10
========

"Wananchi tunaomba mtulie, mshatoa taarifa kwetu hampaswi tena kuchukua sheria mkononi. kwa pamoja naomba mtusaidie kuona eneo lenyewe la tukio hasa ni lipi na jee mtuhumiwa husika ndie huyu mliyekuwa mnamfukuzaa?"

"Ndioooooo Afande tuachieni tuliue kabisaaa linyamaa hiloo"

Sauti hizi zilizidi kunishangaza na kunishtua kwani mpaka muda huo sikujua nini hasa nilichofanya yaaani badala ya kupewa msaada ndio kwanza nataka kuuawa?
Nilikamatwa suruali na kuanza kutembezwa mpela mpela na wale askali wakiwafata wananchi ambao nao waliongozwa na mtu mmoja kuelekea kule niliposhambuliwa hususani eneo lile la kichaka ambako sikubahatika kuona kilichopo na ndipo mara baada ya askali kufika pale huku wakiwa na matochi makubwa yenye mwanga mkali tulishuhudia maiti mbili ya mama na mtoto mdogo zikiwa zimekatwa katwa vibaya.
Nilijihisi kuchanganyikiwa hasa baada ya kuona nguo za kale katoto ndio zilezile alizovaa mwanangu siku hiyo.
Nilipiga kelele kwa kumlilia zaidi mwanangu nikiamini nae wamemuua sambamba na mke wangu lakini chaajabu ndio kwanza nilizidi kuchezea vitasa na maneno makali kutoka kwa wale mapolisi huku wengine wakinipiga picha.

"Afande Jacobo sogeza gari pia afande Dula weka hilo panga vizuri hapo mbele hakikisha mtu yeyote asilishike direct bila groves pia inabidi turisachi hili liuaji vizuri tuone kama kutakuwa na ushahidi zaidi.. hakikisheni kila tukio linapigwa picha"
Aliongea afande mmoja alioonekana mkubwa wao, wakati huo wote mi nilikuwa nalia sana huku wananchi wakinitazama kwa hasira mno.

Ajabu kilichonistua zaidi na kufanya nipoteze fahamu kwa mara nyengine ni mara baada ya kuanza kusachiwa kabla ya kupandishwa kwenye difenda.
Ama kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni kwani kwenye mifuko yangu ya mbele ya suruali nilikutwa na kipande cha kiganja cha mkono wa mtoto kikiwa kimezungushiwa hirizi.
Aaaaaghhh!!!!!!!!! sikuaminiiii hata chembe nikionacho na mara ndipo nilipojihisi kizunguzungu cha ghafra na network zangu zilizima palepale.

Nilirejewa na fahamu mara baada ya kustuliwa kwa kumwagiwa maji mengi ambapo nilikuwa nimelala kifudi fudi ndani ya bodi la difenda iliyokuwa imesimama na nilipoinua kichwa niligundua nilikuwa peke yangu lakini nilipogeuka sasa kutazama vizuri ndipo nilipoona gari nyingi za polisi zikiwa zimepaki huku askali wengi sambamba na waandishi wa habari walikuwa wamesimama wakinipiga picha nikiwa kwenye ile Difenda hadi walipopanda askali wengine na kunishusha mkuku mkuku huku wakinisukuma na kuniongoza kwenye jengo moja ambalo niliponyanyua uso niliona maandishi makubwa yaliyosomeka KITUO KIKUU CHA POLISI KINONDONI

Nilijua sasa kumbe hatukua kule polini bali tupo mjini na ni katika kituo kikubwa cha polisi ambacho awali nilizoea tu kukisikia na kukiona kwa mbali huku sikuwahi kuwaza hata siku moja kama nami ningekuja kuingia eneo lile kama mtuhumiwa tena kwa kesi mbaya mno.
Sikujua tulichukua mda gani kutoka kule porini kutokana na kupoteza kwangu fahamu na mpaka muda ule akili zangu hazikukaa sawa kabisa na kila kilichokuwa kinaendelea niliona kama ndoto ama sinema tu na si kitu halisi japo ukweli ulibaki kuwa haikuwa ndoto wala sinema.
Nakumbuka baada ya kuvuliwa mkanda na viatu nilisongomekwa katika selo moja huku nyuma yangu nikiandamwa na virungu mfululizo hasa pale nilipotaka kusimama kuongea chochote lakini nafasi hiyo sikuipata.
Niliingia ndani ambapo kulikuwa na mahabusu wengine wakinishangaa kwa jinsi nilivyokuwa, nilijituliza na kukaa kitako kwenye kona ya kuta ya selo ile na kujikuta naanza kulia kwa uchungu mkubwa hasa nilipokumbuka maiti zile ambazo nilikuwa na uhakika kuwa ni za familia yangu hususani nilimlilia sana mwanangu kipenzi kwa kuuawa bila kosa lolote.

"Oyaaa M baba mbona unaleta uduanzi sasa... hebu tukaushie usituchulie hapaa tutakunjenga ooohooo.."

Ilikuwa ni sauti ya kiteja iliyondamana na kofi lililonikuta kichogoni na kunistua kwenye dimbwi la huzuni na mawazo na kunifanya nipunguze mdadi wa kulia kwa sauti na kubaki machozi yanaendelea kububujika yenyewe huku nikiomba kupambazuke haraka.
Asikwambie mtu selo pabaya sana hakuna hata chembe ya raha, harufu mbaya ya kinyesi tulichokuwa tunalala nacho kikiwa kwenye ndoo mpaka asubuhi ndio mtu anaenda kumwaga, hakukuwa na vigodolo wala shuka ya kujifunika na siku watu wakiwa wengi unakosa hata sehemu ya kukaa na kubaki umesimama daaah!! ni afadhali walau maisha ya huku jera japo nayo si mazuri.
Nakumbuka baadae asubuhi yake nilichukuliwa na kuingizwa katika chumba maalum cha mahojiano na mateso na huko nilikutana na askali watatu mmoja wao alikuwa mrefu mtu wa milaba minne ambae ndie alienikalisha kwenye kiti cha chuma na kuanza kunihoji huku wengine wakiandika na kurecord.

"Taja lijina rako upesi.."
Alianza kuniuliza kwa ukali kidogo yule afande baunsa.
"Naitwa Hussein afande.. hus..sein.." Nilijibu huku nikiwa na hofu.
"Taja vizuri bwana Lihuseni nani?"
"Hus..sein.. Bakari..kaka."
"Nani likaka lako wewe?! sina dogo likatiri na Riuaji kama wewe Ebo!.. haya sema kwanini uliua familia yako?"
"Familia yangu!! hapana.. afande sijaua yeyote mbona..!!"
"KELELE.. Tuna ushahidi wa kutosha na tumekukamata eneo la tukio. Unataka kudanganya chombo cha dora wakati vielelezo vyote tunavyo?..! lichawi likubwa wewe ngoja nikupe chai kwanza.."
Aliongea kwa hasira yule afande huku wenzake nao wakinikandamiza zaidi kwa tuhuma za ukatili ambao sikuwahi hata kuuwaza kama kuna binaadam anaweza kufanya vile kwa familia yake mwenyewe aliyoipenda.
Nilifungwa barabara kwa kuinamishwa nikiwa nimekaa kwenye kiti kile cha chuma kilichokuwa na mfano wa kisturi (hakina uegemeo) huku viwiko vya mikono yangu vikiwa sambamba na magoti yangu na kubananizwa pamoja hali iliyofanya nibaki nusu nimekaa nusu nimeinama na ndipo mateso makali yalipoanza sambamba na mijeredi.

Niliumia sana na kulia mpaka sauti ikaanza kunikauka kutokana na mateso yale makali asubuhi ile. Niliwaambia na kuwaapia kadri nijuavyo kuwa sijahusika na tukio lolote baya zaidi ya kwamba mimi na familia yangu ndio tulivamiwa lakini maneno yangu ndio ilikuwa kama chachu ya kufanya mateso yaongezeke zaidi.
Nilitamani hata kifo kije muda ule lakini nacho kilikuwa mbali na mimi. Oooh! sikuamini kama Hussein mimi ambae sikuwa na rekodi hata ya kushtakiwa kwa mjumbe tu ktk makuzi yangu wala kuwahi japo kumtishia mtu na kiwembe achilia mbali kumkata, lakini leo hii nateswa vikali kwa kosa la kuwakatakata na kuwaua vibaya mwanamke na mtoto mdogo? tena eti ni familia yangu? yaani mke wangu na mwanangu mwenyewe!!? aaaaaghhhhh!!!!! kwa mara nyengine nilizimia tena katikati ya mateso yale makali.

ITAENDELEA...

Then nani atakua kafanya hayo mauji?

Kule walipokua wanaelekea ni kwa mjomba wake, na ndiyo matatizo yalipowakuta, yeye kudhulika na kusemekana familia yake kuawa... na pia kakutwa na kiganja cha binadamu kilichovingirishwa hirizi ndani ya mfuko wake... Na hapo hapo Hussein alishasemaga mjomba wake yupo vizuri kwenye mambo ya ulozi pia...

Lakini kabla ya hapo mjomba alishamuonyaga kuhusu Zai... huyo Mr.X inawezekana akawa ni mjomba wake? Lakini mbona sauti iliyokua ikisema muacheni sijawaambia mumue ni ya Zai mke Hussein?


Cc: mahondaw
 
EPS 13
========

Hussein waambie ... waambie sasa... waambieeee kwanguvu wasikiee waambieee usiogopee .. usiogopee usiogopeeeeee.... ' ' '

Baada ya kusikia maneno haya ktk fahamu zangu nilijikuta napata ujasiri na kupayuka kwa nguvu pindi napandishwa kwenye karandinga na kusema
WANAAAAAAKEE NI WAUAJIIIIIII
Na hii ndio ikawa mara yangu ya kwanza kutamka maneno haya hadharani.

* * * *

Siku zilienda ambapo muda wote toka nianze kutumikia kile kifungo cha mwaka mmoja sikuwa na rafiki jera wala sikutaka urafiki na yeyote yule nikiamini rafiki angu ni mmoja tu yule aliyekuja kunitembelea na ndugu yangu ni mmoja tu nae ni ba mkubwa tu basi lakini hawa wengine wote wataniongopea kwa kuwa tupo ktk hali moja tu wakitoka kila mtu atafata yake kwani niliokuwa nao uraiani nao walinisapoti kwa kuwa tulikuwa ktk hali moja ila leo nimepata matatizo mabaya tena ya kusingiziwa lakini wote wamenigeuka na kuniacha peke angu hivyo baada ya hapo ndio nikaanza kuwa na tabia ya kukaa peke angu na kufanya kazi kwa nguvu muda wote na inapofika wakati nikikumbuka matukio yaliyonikuta na hadithi za yule bwana ambazo zilikuwa zinanijia kichwani mara kwa mara huku nikiisikia sauti yake na hapo ndio nasemaga makusudi kuwaambia wengine kuwa 'Wanaake ni Wauaji' japo wengi waliishia kuniangalia na kudhani kuwa nimerukwa tu na akili.

Siku zilipita hatimae kifungo changu kiliisha na baada ya kufanyiwa vipimo nilikung'utwa bakora zangu tano zilizobaki na siku chache mbele baada ya kupata uwezo wa kusimama nilifikishwa tena kizimbani.
Eee.. asikwambie mtu zile bakora heri uzisikie tu kwa wenzako usiombe zikukute kwani ziko tofauti na bakora za shule nilizozizoea yaani fikiria bakora tano tu mtu wa mazoezi kama mimi nilishindwa kusimama, kama una afya mgogoro unaweza kukata upepo kabisa (kufa).

Basi baada ya kufika kizimbani na hakimu alikuwa yuleyule mama kesi ilianza tena kuunguruma ambapo kwa upande wa mashtaka ambao ilikuwa serekali wenyewe ulileta ushahidi mbali mbali zikiwemo zile nguo nilizovaa za tukio panga na kiganja cha mtoto ambacho kilihifadhiwa muda wote na nilipoulizwa kuhusu kuvitambua vile vitu ambapo nilikubali kuzitambua nguo tu kuwa ni kweli zilikuwa za kwangu lakini vile vyengine vyote nilikataa ndipo alipopanda daktari aliyenichukua alama za mikono baada ya kukamatwa na kuleta majibu ambayo yalikuwa yamefanana na alama za mikono ya mtu aliyelitumia lile panga hali ile ilinishangaza pia kwani nilishasahau kuwa kweli niliwahi kulishika lile panga lakini sikulitumia kudhuru chochote.
Ushahidi wote na maswali ya mawakili yalizidi kunibana na nilichoka zaidi baada ya kupanda dogo aliyethibitisha kuuona ugomvi baina yangu na mke wangu tukigombania mtoto huku nikiwa na panga mkononi ambapo yule dogo alikuwa chini ya miaka kumi na nane na alihesabika kama mtoto kwa mujibu wa sheria iliamini hasemi uongo.
Niliumia sana na kumtazama yule dogo alivyovuka mipaka kuongea kitu ambacho hakikutokea hadi akawa anatoa machozi pale mahakamani kukazia uongo wake.

Niliamini kuwa nimekwisha na nilishindwa kupiga kelele kumstopisha yule dogo nikihofia yasije kunikuta yale ya mwanzo na kumuacha anikandamize tu lakini baada ya yule dogo nilistuka pindi niliposikia anatajwa shahidi upande wa mshtakiwa na moyo ulipata faraja kidogo mara baada ya kumuona ba mkubwa akisogea kizimbani nami nilimtazama kwa jicho la kushukuru kwani nilijua yeye ndie tumaini pekee kwa muda ule lakini alipopanda na baada ya kuapishwa akaanza kuzungumza ba mkubwa maneno yaliyosafirishwa kwa sauti yake mwenyewe na yalipenya vizuri masikioni mwangu na kuingia ktk milango yangu ya fahamu kabla hayajaenda kutua kwenye moyo wangu na kuufanya ustuke kupita maelezo huku nikijihisi viungo vyangu vyote vimeshindwa kufanya kazi hadi macho yalishindwa kupepesa na kubaki yameganda kwa ba mkubwa kwa kutoamini kama ndie yeye au..? aaaaah!!!!! sikuamini hata kidogo kile nilichokisikia.

Nayakumbuka vizuri maongezi yale baada ya kuapishwa ba mkubwa na wakili yule wa serekali alisimama na kumuuliza kama ananitambua nae akasema ananitambua kisha wakili akamuuliza tena.
"Unamtambua tambua vipi mtuhumiwa hebu ifafanulie mahakama.."
"Ndio namtambua bwana Hussein Bakari kama mwanangu kwani ni mtoto wa marehemu mdogo wangu wa tumbo moja.."
aliongea ba mkubwa kisha wakili aliendelea kuhoji..
" Sawa, kumbe Hussein ni mwanao kwa namna moja je una lipi la kuiambia mahakama juu ya kesi inayomkabiri mwanao ?"
" Nipo hapa kwa ajili ya kutoa ushahidi kwa kile ninachokijua kuhusiana na tukio zima na kesi inayomkabili mwanangu"
Aliongea Ba mkubwa maneno yake ya awali ambayo yalinipa moyo kuwa amekuja kunitetea na kuongea ukweli lakini mara baada ya hakimu kumruhusu aongee kile alichokijua ndipo nilipostaajabu kumsikia ba mkubwa akisema....

" Muheshimiwa hakimu nakumbuka miezi miwili kabla ya tukio mwanangu Hussein alikuja katika kijiwe changu kwani mimi ni mtaalam wa tiba asilia na alionesha hali ya kuchanganyikiwa kidogo ambapo nilipomuuliza kulikoni hakunambia ukweli zaidi ya kusema maisha yanamchanganya kisha akaniuliza ktk dawa zangu hivi sina dawa ya kumfanya mtu awe tajiri? hapo nilicheka na kumwambia mwanangu kuwa hutajiri hauletwi kwa dawa bali ni juhudi tu binafsi ktk kazi na kujituma kimaisha bila kusahau kumuomba mungu . Aliondoka siku hiyo lakini miezi miwili baadae wiki moja kabla ya tukio nilipigiwa simu na mkwe wangu marehemu mkewe mwanangu Hussein na alinambia kuwa wana matatizo makubwa na ugomvi baina yao kuhusu mtoto ... Na nilipouliza zaidi kulikoni ndipo mkewe alinambia kuwa kutokana na kuchoshwa na ugumu wa maisha mumewe alienda kwa mganga mmoja ambae hakunitajia ni wapi na anaitwa nani lakini alichosema ni kuwa alienda kwa lengo la kupata dawa ya kuweza kuwa tajiri ili wajikwamue na maisha magumu waliyokuwa nayo.
Na mganga wake alimwambia masharti ya dawa hiyo ili itengenezwe inapaswa amtoe kafara mamaake mzazi au mtoto wake mwenyewe na apeleke kiganja chake ndipo atafanyiwa hiyo tiba na kuwa tajiri hivyo kwa kuwa mamaake alishafariki na pia alikuwa na mtoto pekee ndipo alipomfikishia mkewe habari zile na kumshauli wamuue tu mtoto wao ili watajirike na baadae watazaa wengine lakini mkewe alimkatalia na ndipo ugomvi ukaanzia pale. Nami kwa busara zangu siku moja kabla ya tukio mapema nilipiga simu ambapo nikasikia ugomvi mkubwa baada ya simu kupokelewa na baadae ndipo alipoanza kuongea mkewe ambapo niliwaomba waje kwangu nia na madhumuni nimuonye mwanangu Hussein kwa kile anachotaka kukifanya kwani safari ile nilimsikia kwa masikio yangu na kwa bahati nzuri nilimrekodi.
Lakini cha ajabu alimlazimisha mkewe na kuamua kuja kesho yake usiku na kutokana na mazingira ya kule kuwa polini ndipo alipata nafasi ya kufanya tukio.
Ki ukweli muheshimiwa Hakimu na wazee wa baraza inauma sana kuusema ukweli huu kwani Hussein ni mwanangu lakini nikiongopa kwa ajili ya kutetea nitakuwa nimejiekea mzigo wa dhambi tu mbele za mungu... na nina ushahidi wa record ktk simu niliyopiga siku hiyo. ila ninachoomba cha mwisho muheshimiwa mumsamehe tu mwananguu...uuuuh..."

Aliongea ba mkubwa na kumalizia kwa kilio kisha ilitegwa kwenye mike ile simu yake aliyosema kuna hiyo record na kweli mara spika zilizokuwa kwenye mahakama zilianza kutoa sauti na kweli ulisikika ugomvi wa mwanaume na mwanamke wakigombania kumuua mtoto wao ambapo nilizidi kustaajabu kwani sauti ya mwanamke kweli ilikuwa ni ya Zai wangu na pia sauti ya mwanaume ilifanana kabisa na yangu japo kiukweli hatukuwahi hata siku moja kuzozana na Zai lakini daaah!!! mchezo niliofanyiwa pale ulinichosha sana na kuamini kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni ina maana hawa watu waliikopi hadi sauti yangu na kuiigizia?
Imekuaje ba mkubwa nae ameshirikiana nao kuniangamiza ilihali awali aliapa kunisaidia?

Basi ba mkubwa alipomalizia kunipigilia msumali wa moto kwenye utosi sikuwa na cha zaidi zaidi ya kukubali kuwa sina jipya hata nikitolewa kuwa huru sitokuwa na manufaa yoyote ulimwenguni hivyo nikamuomba mungu ipitishwe hukumu ya kifo juu yangu ili nikapumzike kwani maisha ya dunia ndio basi yameshanisariti.
Lakini hakimu aliisogeza kesi tena kwa kutakiwa nikafanyiwe vipimo vya ubongo kama sikuwa na tatizo lolote la kiakili kwani kwa mujibu wa katiba serekali haikuamini uchawi na imani za kishirikina na majibu ya daktali ndio yataongoza na kuisaidia hukumu husika.
ITAENDELEA,,,,,,

Du!!

Unataka kusema mwanamke wa Hussein wa kwanza (Mariam) ndiyo karatibu haya mauaji akishirikiana na Baba Mkubwa wa Hussien...

Haki tena inachanganya? Je na sauti ya mke wa Hussein (Zai), imekuaje imesikika clear kwamba ni yeye?


Cc: mahondaw
 
EPS 14
========

Kesi iliahilishwa na kufanyiwa vipimo na mwezi mmoja baadae nilirudishwa tena kizimbani ambapo daktari alithibitisha kuwa sikuwa na tatizo lolote la ubongo linaloweza kuafect akili zangu kwa hiyo vipimo vya kichwa vilionesha niko safi kabisa.
Na hapo ndipo hakimu aliponigeukia na kuniuliza kama nina lolote la kujitetea..?
Nilimuangalia hakimu yule ambae safari hii hakuwa yule mama na nilistaajabu sana kwani haikuwa kawaida japo nilipokuwa gerezani baadae ndipo nilisikia habari kuwa yule mama wiki moja kabla ya kesi alipatwa ajali mbaya iliyomfanya alazwe wiki nzima i.c.u na siku niliyohukumiwa nae alifariki siku ileile....
Basi, nilimuangalia yule hakimu na kumwambia kuwa..
"Ndugu Hakimu, mimi ni mkosaji niliepoteza nafsi za watu, sina chochote cha kujitetea kwa kuwa tayari nipo mikononi mwa sheria. Ninachosubiri tu nilipwe ujira sawa kama nilivyoifanyia familia yangu ili niwafate huko walipo.
Naiweka nafsi yangu mikononi mwa mahakama hii tukufu niko tayari kuhukumiwa."

Maneno yangu yalimshangaza kila mtu aliyekuwa pale mahakamani mpaka hakimu mwenyewe nilimshuhudia akishusha miwani yake ya macho chini kidogo na kuniangalia vizuri kisha akaipandisha tena kuwaangalia wazee wa baraza na baada ya kimya kama cha dakika tano ndipo hakimu aliposoma hukumu yangu.

......
"Bwana Hussein Bakari, baada ya mahakama hii tukufu kufanya uchunguzi yakinifu kwa kuzingatia sheria na taarifa za mashahidi mbalimbali na vipimo vya madaktari juu ya tukio lililotokea la mauaji.
Mahakama inakutia hatiani moja kwa moja bwana Hussein Bakari kwa kosa la mauaji ya mke na mtoto.
Na kupitia kifungu namba 94 sheria ya mahakama iliyopitishwa mwaka 1981 kuwa endapo mtuhumiwa wa kesi ya mauaji ikaonekana dhahili aliua kwa makusudi basi hukumu yake ni ya kifo moja kwa moja.
Lakini pia kifungu hiki kilihakikiwa upywa mwaka 1990 kuwa endapo mtuhumiwa huyu akakili na kuonesha kutubia kosa lake kabla ya hukumu basi mahakama itaangalia chaguo juu ya hukumu yake aidha ahukumiwe kifo anyongwe ama ahukumiwe kifungo cha maisha jera na kazi ngumu.
Nami kupitia kifungu hiki cha mwaka 1990 nakitumia kukuhukumu bwana Hussein kutokana na majuto uliyoyaonesha mbele ya mahakama kwenda jera kwa maisha yako yote yaliyobaki sambamba na kazi ngumu. Na hii iwe fundisho kwa watu wote wenye tabia kama hizi kutaka mafanikio kwa njia haramu na kusababisha vifo vya watu wasio na hatia.
Mwisho wa kuhukumu... Askari mchukueni kufungo chake kimeshaanza sasa. "
............

Aliongea yule hakimu nami sikulidhishwa na hukumu ile huku nikisisitiza kwanini nisingehukumiwa kifo.?

" Hapanaa Hakimu umekoseaaa.... kumbuka aliyeua anapaswa auaweee.... niueni tuuu... Niueniii tuuu hiyo sio hakiii.."

Nilipiga kelele hadi walionichukia wakawa wananishangaa na kunihurumia ndipo nilipoingizwa kwenye karandinga na muda mfupi baaadae safari ilianza kwenda kutumikia kifungo changu.
Lakini nikiwa nachungulia kwa nje ndipo nilishangaa kuna mtu alikuwa akilikimbilia gari lililotubeba na kulisimamisha huku mkononi mwake akiwa na barua.

Askali walijaribu kumzuia lakini alilalamika huku akiinyoosha juu ile barua japo sikumsikia alichokuwa anaongea lakini nilimtambua vizuri mwanamke yule ndie alikuwa ni Mariam aliyenitenda hapo awali na sikujua alikuwa na jipya gani na kama barua ile ilinilenga mimi ni kwa nia na dhumuni gani hasa.
Nilipotezea na kuzungusha shingo yangu ndani na kuinamisha kichwa chini kwani sikupenda kabisa kuendelea kuuona uso wa mariam kule nje na hatimae gari iliingia barabara kuu na safari ya kwenda kumalizia ngwe iliyosalia ya maisha yangu ikaanza huku kichwani mwangu nikilaumu kwanini sikuhukumiwa kifo moja kwa moja.

Nilifika kwenye hili gereza kwa mara ya kwanza na baada ya kupewa namba na kukabidhiwa sale maisha mapya yakaanza rasmi lakini siku chache tu tukiwa tunavunja mawe eneo moja niliitwa na afsa magereza mmoja na kunikabidhi barua ambayo ilinitonesha zaidi na kuniliza pia na siku hiyo niliapa kuwa sitozungumza na yeyote kuhusu yaliyonikuta kwani sikupenda niendelee kujitonesha maumivu haya ya kihistoria kwenye maisha yangu.
Kwa muandiko tu wa ile barua nilijua fika imetoka kwa Mariam kwani hati yake niliielewa vizuri ndipo nilipobaini kuwa huenda hii ndio barua aliyoikimbizia siku ile nilipohukumiwa na kuna askali mmoja aliichukua kati ya wale waliomzuia.
Nilitulia kwenye kivuli na kuanza kuisoma ile barua ambayo ilikuwa imeandikwa pande zote mbili za karatasi kutokana na urefu wake sitoisahau hii barua ambayo ilikuwa ya mwanzo na mwisho ktk makazi yangu mapya haya ya jera na ilianza kwa kusema...
.............
" ''Najua sikustahiri kusogea mbele ya macho yako kutokana na yale niliyokutendea siku za nyuma lakini naomba unisamehe ndani ya nafsi yako ili hata nitapokufa niwe nimejipunguzia walau uzito kidogo ndani ya mzigo wangu mkubwa wa dhambi.
Ukweli nilikupenda lakini sikuwa mke mwema kwako.
Nilikuwa msariti wa penzi lako kwa kufata maneno na ushauli wa shoga zangu kuwa mwanaume mmoja hatoshi kwa mwanamke mrembo mwenye kuhitaji mambo mazuri kama mimi na hivyo ndivyo ilivyokuwa hata pale nilipokukasirikia nilimpigia simu na kumfata bwana mwengine ambae nae aliamini mimi ni wake pekeake na ndie yule mliyepigana kule beach.
Madhumuni ya barua hii si kukuumiza kwa kukukumbusha yaliyopita bali ni kukutaka ujue kuwa una damu yako inayoishi uliyoitumbukiza tumboni kwangu miezi michache kabla hatujatengana.
Na hata siku ile ya mwisho niliyokuja kwako nilipanga kukufanyia suprise ya kukwambia swala hili lakini habari ile ya kwamba wanaake sisi ni wauaji ilinikera mno kwa kuwa alichokuwa anaongea yule bwana kilinirenga kweli na kuna mengine yalinigusa kabisa na kuniumbua moyoni.
Nilikuchukia na kujaribu kuitoa ile mimba baada ya kuachana lakini ajabu ilishindikana na kuendelea kukua hali iliyofanya kuachwa na mabwana zangu wengine baada ya kila niliyemsingizia kuikataa kwa kugundua hesabu ya miezi.
Ukweli mwezi ule nilionasa sikutembea na mwanaume yeyote zaidi yako na hata ukipiga hesabu mwezi niliojifungua na umli wa mtoto utakumbuka kila kitu.
Najua imekuwa too late na laiti ningejua awali ningekwambia ukweli tu lakini baada ya kusikia majanga yaliyokukuta nafsi imeniuma sana na mimi ni mmoja kati ya watu wasioamini kabisa kama kweli ulifanya mauaji yale.
Niliisikia sauti yako siku ile mahakamani uliposema kuwa Wanaake ni Wauaji nami moyoni sikuchukia kama siku ile na nilikubaliana nawe kwa namna frani nahisi hata kesi yako umeponzwa na mwanamke.
Nasikitika ninapomuangalia huyu mtoto ninayemuacha katika hali ya uyatima kwani hapa nilipo nimegundulika nina kansa ya koo na sitoweza kupona kwa mujibu wa ripoti ya daktari kuwa imesababishwa na uchafu mwingi wa mbegu mbovu za kiume uliokuwa unapenya kwenye vijitundu vya ulimi wangu na kwenda kurundikana kooni na kutengeneza wadudu wabaya walioanza kushambulia koo pasi namie mwenyewe kujua.
Usishangae Hussein huo ndio ukweli, na hii yote ilisababishwa na tabia yangu ya muda mrefu kupenda kunyonya tupu za wanaume tofauti mara kwa mara kwa lengo la kuwachanganya kimapenzi ili nipate kuwachuna vizuri lakini leo hii najuta kwa kukiona kifo changu kikiwa kimenisimamia nikiwa kwenye umli mdogo bado na kumuacha mtoto ambae najua hatomuona tena babaake kutokana na hukumu uliyopewa.
Nilikuwepo nae siku ile ya kesi yako na alilia sana pindi ulipotolewa kwa kusukumwa huku ukipigwa kuingizwa kwenye karandinga baada ya kusonya mahakamani...
Nakuombea mungu akunyooshee mkono wa kheri na atende muujiza kifungo chako kiwe chepesi.
Mtoto huyu anaitwa Asha na kwaajabu ya mungu nyuma ya shingo yake karibu na sikio amezaliwa na alama kama ile uliyokuwa nayo na sasa ana miaka mitatu na miezi sita.
Japo nae ni wa kike lakini huko ulipo naomba umuombee ili asije potezwa katika mkumbo na kuwa miongoni mwa Wanaake Wauaji.

Ahsante kwa kuisoma barua yangu....
Ni mimi mfu mtarajiwa MARIAM

...............
ITAENDELEA....

Mpaka hapa bado inaonekana muuaji siyo Mariam... bingwa wa blow job anaeenda kufa kwa cancer ya koo...


Cc: mahondaw
 
Endelea basi Madame S weekend yangu hii tangia niamke niko apa na pale kwenye bandika bandua zako, ndo nimeishia hapa sasa usipoendelee sijui kingine gan nifanye hii siku iishe so please endeleza Madam
 
Endelea basi Madame S weekend yangu hii tangia niamke niko apa na pale kwenye bandika bandua zako, ndo nimeishia hapa sasa usipoendelee sijui kingine gan nifanye hii siku iishe so please endeleza Madam
Ngoja nimalize kufturu ntaweka usijali
 
EPS 26
========

"Ni hivi mkuu, tulipokea simu iliyoleta hiyo taarifa majira ya saa tatu asubuhi na vijana walipofika walichukua picha na kuhoji maswali mawili matatu ya msingi na katika maelezo waliyotupa raia hususani mtu wa kwanza kumuona marehemu ambae alikuwa mwanae waliosaidiana kazi alisema kuwa babaake siku hiyo aliwahi mapema kwa nia ya kuandaa mazingira kuwa kuna mgeni wake mteja wa siku nyingi toka enzi za babaake angekuja lakini asubuhi ileile yule kijana alipofika na kuingia mule kibandani ndipo aliposhangaa kukuta babaake akiwa chini damu zimetapakaa huku mkononi akiwa na kisu."
"Sasa we kama ocs baada ya vijana wako kuleta taarifa hii ulichukua hatua gani zaidi"
"Kwanza mkuu niliwaamuru wapeleke mwili moja kwa moja hospitali kwa vipimo zaidi kama huenda alivamiwa na watu na kumchinja kisha kumshikisha tu kisu."
"wazo zuri sasa baada ya majibu kutoka kuonesha kuwa hakushambuliwa ndio mkaungana moja kwa moja na ripoti ya daktari mkimaanisha hakuna tena upelelezi wowote si ndio?"
"Mmmh, hapana mkuu, kama nilivyosema awali bado tunafanya upelelezi wa chini kwa chini."
"Upelelezi gani John hivi ulifika hata eneo la tukio.?"
"mh, hapana."
"Umeona sasa, unakikaribisha kitambi rafikiangu usipende uheshimiwa wewe ni damu changa kama mimi bwana inabidi vitu vyengine tujieke mstari wa mbele wenyewe tusipende kutuma tuma tu"
aliongea kwa msisitizo Shebby na kuongezea kauli zilizowashangaza hadi polisi waliokuwa ofisi ya jirani na ocs waliotega masikio ya umbea na kuzungumza chinichini kujua alichokuwa anazungumza Kamishna na ocs wao.
Kauli hiyo ya Shebby haikumshangaza tu ocs bali hadii St;sajent Kimalo mwenyewe na kushangaa kamishna wake ana provement zipi hadi imefikia kusema kwa kujiamini kiasi kile.
"Yaani, ndio hivyo ocs John nakuhakikishia kuwa yule mganga HAJAJIUA bali AMEUAWA."
aliekea msisitizo kabisa maneno yake Shebby na kuwafanya rafiki zake ocs John na st;sajent Kimaro kuachama midomo wasijue wamjibu nini kwa kuogopa kuwa huenda wakaeleweka vibaya mbele ya mkuu wao.
"Najua vichwa vyenu vinatamani kuniuliza nina uhakika upi hadi nasema hivi lakini haya majibu yangu kwenu yatakuja kwa mtindo wa maswali na mtashindwa kuyajibu na kwasababu hiyo sitowapa mimi majibu ila kuna mtu mmefanya kosa sana kumuacha huru, nahitaji aletwe hapa mara moja na nitamuhoji mimi mwenyewe na kila mtu hapa atapata picha kwanini nasema yule mganga hakujiua wala hakutingwa na mawazo bali ameuawa na aliyesababisha kifo chake ni mr.X"
"MR.X..!!?"
alishangaa sana ocs John mara baada ya kamishna Shebby kupitiliza maneno na kujikuta anaropoka jina la mr.X ambalo kwa upande wa ocs John lilikuwa geni kabisa.
"Usijali John, ni hadithi ndefu sana ila nitakuhadithia japo si leo kwanza nataka utume vijana wako akakamatwe huyu mtu mara moja."
"sawa Mkuu, nani mtu mwenyewe vijana wakaifanye hiyo kazi sasa hivi aletwe hapa."
"Nahitaji akakamatwe mtoto wa marehemu aliyekuwa msaidizi wake, huyo wa mwanzo kabisa kumuona marehemu."
"sawa Mkuu."
Baada ya hapo ocs alimuita sub inspekta wake akusanye vijana saba haraka wachukue difenda kwenda kumkamata mtoto wa marehemu yule aliyejichinja ambae pia ni mjukuu wa marehemu Mnyungunyungu aliyetarajiwa kuwa mganga atayefatia na mara tu vijana walipopewa agizo lile walioonesha ushupavu wa hali ya juu hasa walipogundua kuwa aliyetoa amri ile alikuwa ni Kamishna na walionesha utiifu na ushupavu mbele yake ili wasionekane wachovu na ndipo gari ilipochomoka kwa speed kali kuwahi Mkuyuni stend ili waelekee kule msibani kutimiza amri waliyopewa.

Lakini ajabu toka waondoke wale vijana wa polisi walichelewa sana kurudi na kwa haraka zao zilizochangiwa na woga mbele ya Kamishna walijikuta wanaacha hadi radio call zao hali iliyomtia hasira Kamishna Shebby na kuwaamuru kimaro na ocs watoke pamoja nae waelekee huko walikoenda vijana wao.
Hali ile na amri za Shebby ziliwafanya polisi wote kuwa kimya na kuwa makini sana katika kazi zao muda ule wakimuhofia sana na kumtafsiri kuwa yule kamishna ni mkali mno na mkorofi bila kujua kumbe Shebby alikuwa mtu peace sana ila tu kichwa chake kilivurugwa hasa baada ya kujiingiza kwenye ishu ya kutaka kumjua Mr. X.

Walipofika nje huku escot ya difenda nyengine ikiwa tayari ishabeba vijana wakingoja amri ndipo waliishuhudia difenda waliyoituma ikirudi na kuwasili kituoni na vijana kushuka haraka haraka na macho ya Shebby yalishangaa kutomuona mtu waliyemuagiza zaidi ya wamama wawili.
Akiwa kakunja uso na kutaharuki Shebby alimwita sub inspector aliyeongoza ile mission muda ule kutaka aletewe ripoti yeye mwenyewe moja kwa moja bila kupitia kwa ocs kwanza kwa kuona kama anachelewa na ndipo wote watatu walitaharuki kusikia ripoti iliyorudi.
"Mkuu tumefanya kila jitihada za kufanikisha kuja na mtuhumiwa lakini hatukufanikiwa kumpata baada ya kutoweka masaa machache kabla hatujafika."
"AMETOWEKA!!!?"

"Ametoweka toweka vipi! wakati nilimuacha mimi mwenyewe pale misibani na hayakupita hata masaa sita?!"
alihoji kwa mshangao Kamishna Shebby.
"Ndio hivyo mkuu na tumerudi baada ya kuona muda unaenda pia tulisahau mawailiano na tuko tayari kwa amri mtayotupa ila tumewaleta hawa wake wa marehemu wanaweza kutwambia wapi alipo mtoto wao."
"Huo ni upumbavu. sikutaka aletwe mjane yeyote hapa. Chukueni vitu vyenu kusanya vijana wako msako uanze mara moja hadi apatikane huyo kijana."
Alitoa amri Kamishna Shebby na kumuamuru Kimaro aendeeshe gari yao ambapo safari hii walipanda wanne sambamba na Mkuu wa upelelezi na jumla ya gari tatu zilitoka kituoni kuelekea Mkuyuni stendi huku jumla ya vijana wenye bunduki zaidi ya kumi na tano wakiwa kwenye difenda mbili katikati kukiwa na gari iliyowabeba kina Shebby na kituo kilibaki na askali wachache sana wakiongozwa na mama mmoja aliyekuwa nae na cheo cha sub inspecta.

Wahuni na watu wote Mkuyuni walipigwa na bumbuwazi mara baada ya kuona msafara wa polisi ukisimama kwa fujo zote maeneo ya stendi.
"Oya wana Kimenuka anga hizi tujikataeni.."
aliongea teja mmoja aliyekuwa anacheza kamali na wenzake pale stend mara baada ya kuona difenda zile za polisi.
Kilichoendelea pale askali walitawanyika na msako mkubwa ukaanza huku wahuni wengine wakikimbia ovyo kwa kuhofia huenda walikuja kukamatwa wao.
Kamishna Shebby pamoja na wenzake ocs John, st;sajent Kimaro na yule mkuu wa upelelezi wao waliongoza moja kwa moja mpaka pale msibani sambamba na askali watatu wenye bunduki.
Wakati huo Shebby nae alikuwa kashachukua pisto yake ndogo anayoiachaga kwenye dashibodi ya gari huku kimaro nae hivyo hivyo alichukua yake na kuichokea nyuma ya mkanda wa suruali na watu wote pale msibani walizidi kustaajabu kwani muda si mrefu uliopita walikamatwa wake wa marehemu na kuzua sintofahamu kwa kila mtu aliyekuwa pale msibani.
"Babu, naomba usiwe na wasi wasi tutajie wapi alipoenda yule mtoto wa huyu marehemu."
ilikuwa ni sauti ya Kamishna Shebby mara baada ya kumfata yule babu aliyekuwa amevaa kibaraghashia alipokuwa anaongea huku amezungukwa na watu waliokuwa wanaulizia kilichotokea muda mfupi kabla hawajaja kina Shebby.

ITAENDELEA.....
 
EPS 28
========

Alijikuta anakata simu aliyokuwa anazungumza na babaake na kuwaita wenzake haraka waje washuhudie kile alichokuwa anashuhudia na wote walipofika na kutazama kule juu walistaajabu sana baada ya kuona mwili wa yule kijana ukining'inia kwenye moja ya tawi lililojificha la ule mti huku shingoni mwake kupitia juu ya kichwa kukionekana kamba iliyofungwa kwenye lile tawi.

"Haa!! Ina maana nae kaamua kujinyonga!!?"
alitahayuri Ocs mara baada ya kuushuhudia mwili wa yule kijana ukining'inia pale juu.
Hali ile ilimtisha kila mtu na kuwachanganya vichwa askali wote wasijue kwanini yanatokea yale katika ile familia hususani kwa upande wa Kamishna Shebby alibaki na bumbuwazi na kuzidi kuamini kuwa hawa watu hawajiui bali yupo muuaji tena hayupo mbali kabisa na wao na huyo anayewaua atakuwa kwenye mtandao wa mr.X tu si vinginevyo kwani aliamini kulopoka kwake siku ya kwanza pale chumbani alipokuwa anaugua mzee Mnyungunyungu huwenda ikawa ndio chanzo cha matatizo kwenye hii familia na kupelekea vifo vya wote waliokuwa na walau tetesi juu ya mr.X
((('hivi huyu Mr. X ni mtu wa aina gani mwenye mbinu kiasi hiki na kugundua mitego yetu yote na kutuwahi kabla hatujafanikisha walau kupata njia ya kuanzia. Daah!! siku ya kumgundua huyu mtu sitothubutu kumfikisha kwenye sheria ya nchi, nitamuhukumu mwenyewe haiwezekani ghaa!!')))
Alijisemea mwenyewe Kamishna ndani ya moyo wake kipindi nae akichukua picha kupitia simu yake eneo lote la tukio.

Alimuamuru ocs na kufanywa mawasiliano ya haraka kustopisha zoezi lililokuwa linaendelea kule kwa vijana wao na kuwataarifu waje eneo la tukio.
Baada ya vijana wote kufika pale huku umati mkubwa wa watu ukijazana maeneo yale na kila mtu kutoamini kile akisikicho ama akionacho eneo lile.
Baada ya vijana wa jeshi la polisi kufanya jitihada na kufanikisha kuushusha ule mwili amri ilitoka na kuubeba mpaka zilikopaki difenda na kuupeleka hospital kwaajili ya uchunguzi zaidi huku kina shebby na askali wachache wakibaki bado eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi.
Katika tafiti na maswali yalikuwa kichwani mwake kamishna Shebby bado alihisi lazima kati ya wale wazee mmoja wapo akawa kwenye mtandao wa mr.X na ndie aliyevujisha siri za yeye kutaka kumjua mr.X na ndio sababu za vifo vya wale watu ambao aliamini wangmsaidia kwa namna moja kuijua njia ya kumjua mr.X.

Ndipo hapo Kamishna Shebby alipowaita pembeni kina Kimaro na kujadili nao.
"Eti mmepata picha gani kuhusu haya matukio hususani hili la sasa ni kweli yule mtu amejinyonga mwenyewe au nini kimefanyika?"
"Daah! kiukweli mkuu hii inachanganya sana, nikisema hajajinyonga mwenyewe sasa nani kampandisha kule juu!! dah! kama nae kajinyonga ni kwasababu zipi! yaani bado mimi sijapata picha"
aliongea ocs huku akiwa katika hali ya sintofahamu.
"Vipi Kimaro unasemaje?"
aliuliza tena Shebby
"Mh! mkuu mimi bado natafakari sijapata jibu lolote kwakweli"
alijibu kimaro huku akitazama kwenye ule mti na ndipo akabaki yule mkuu wa upelelezi ambae alikuwa hajaongea kitu.
"Mkuu, mi naona kama huyu mtu hajajinyonga kwa ridhaa yake na nimeanza kutia shaka huenda hata babaake nae hakujichinja kwa ridhaa yake na vifo vyao wote vimesababishwa na mtu mmoja ambae nahisi atakuwa na mbinu kubwa sana za kijeshi na yupo karibu mno na hii familia."
Aliongea yule mkuu wa upelelezi ambae maneno yake yaliungwa mkono moja kwa moja na Kamishna Shebby.
"sawa kabisa, sasa hapa kuna mchezo wa akili nyingi sana unaoendelea na usikute muuaji anatuangalia tunavyopagawa na pengine tuko jirani nae muda mwingi baada ya tukio.
Sikia Kimaro nina mashaka na wale wazee watano huenda mmoja wapo akawa ni mtu wa karibu na mr.X na ndie aliyevujisha habari kwa mr.X kwamba kuna watu wanamfatilia kutaka kumjua sasa mr.X ameamua kuwaua wote walio na fununu walau kidogo kuhusu yeye na hii inanihakikishia kuwa MR.X yuko hai."
"Duh! mkuu sasa hapa tufanyeje."
"Inabidi sasa hivi ocs tuongozane na vijana tuwakamate wazee hawa wote twende nao tukawabane tuweze kumjua anayevujisha siri kwa mr.X kabla hatujachelewa kwani kwenye hii familia watu pekee waliokuwa na siri za mr.X wote washakufa na aliyebaki ndio kichaa hana kumbukumbu zozote hawezi kusaidia kitu naamini sasa hata huyo mzee anaweza kutoroka na muuaji aliyetumwa na mr. X na habari zake kubaki kizani milele."
Baada ya Kamishna Shebby kuongea yale wote walikubaliana na kumuunga mkono kisha ocs alichukua radio call na kuongea na sub inspector wake kumpa maelekezo kamili.

* * * * * *

Baada ya mwanae kukata simu na kubaki na taharuki asijue kulikoni mzee Mwinchande alimuangalia yule mkuu wa gereza msaidizi kwa mshangao hali iliyomfanya mkuu saidizi nae ashangae na kumuuliza.
"Vipi baba kulikoni? anasemaje mkuu."
"Kijana kumbe kuna mission za kijeshi zinaendelea huko tena mbali nawe unajifanya hujui?"
aliuliza kwa mshangao mzee Mwinchande na kujikuta anafichua kile alichozungumza na mwanae ambae alimuomba asimwambie mtu zaidi atakuja kumuelezea mwenyewe.
"Mission zinaendelea? mbona sifahamu mzee wangu kuhusu hiko usemacho?"
"Ufahamu vipi na uko ofisi moja na mwanangu tofauti vyumba tu? ina maana hujui kama Kamishna wako yupo morogoro muda huu kwenye kazi maalum tena inaonekana nyeti sana kwa jinsi alivyokuwa anaongea hadi akanikatia simu!!"
aliongezea mzee mwinchande na kumfanya yule mkuu msaidizi abaki ameduwaa mithili ya mtu aliyebaini kitu furani na kutokana na mzee Mwinchande kuwa na uzoefu wa miaka mingi wa kiaskali aligundua baada ya kuutazama uso wa yule msaidizi wa Shebby na kum bana maswali pale pale.
"Hivi kuna mabadiliko gani alikuwa nayo Kamishna yako hivi karibuni au mna tatizo gani baina yenu hadi aanze kuondoka pasi na kukuaga mtu wa jilani kama wewe?"
"Mh! kiukweli mzee wangu hatuna tatizo lolote mimi na mkuu wangu ilaaa..."
aliongea na kusita kidogo baada ya kuhisi si vyema kuongea habari za mkuu wake na kuijadili tabia yake pasi na lidhaa ya mkuu wake mwenyewe.
"sasa mwanangu unataka kunificha habari za mwanangu mwenyewe?"
"hapana mzee"
"Basi kama sivyo unasita nini. Hebu niambie ukweli umeona mabadiliko gani kuhusu mwanangu siku za karibuni hadi aondoke na kuwa na mission pasi na kukutaarifu mission gani."
alikazia mzee Mwinchande na kumfanya yule msaidizi kueleza kila kitu alichokuwa anakijua na kuhisi ndicho kilichom badilisha Kamishna wake mpaka kuwa na mission za siri.
"Kiukweli mzee wangu huenda hili ninalohisi ndio ama sio sina uhakika ila tokea mkuu alipoanza kuwa karibu na mfungwa mmoja humu gerezani alikuwa na mambo ya ajabu ajabu ya kuandika kwenye kuta ovyo ovyo kuwa wanawake ni wauaji mara kwenye miti anachunachuna na kuandika hayo maneno halikadhalika na tabia yake ya kuropoka kwa sauti kubwa muda mwengine hayo hayo maneno na gerza zima lilimtambua yule bwana nusu chizi lakini ajabu mkuu akafanya jitihada anazozijua yeye hadi akafanikisha kuzungumza nae na inaonekana hadithi ya huyo bwana ilimgusa sana mkuu na hapo ndipo akaanza kuwa bussy sana na kutoka nje ya gereza mara kwa mara so, nahisi huenda kuna upelelezi amaeamua kuufanya binafisi juu ya kesi ya yule bwana ambayo ilisemekana ameonewa kwa mujibu wake mwenyewe."
"Oooohoooo! Duh! sasa mwananguuu ina maana anataka kumsaidia huyo mtu."
"Nahisi mzee, lakini sijui kilichomshawishi maana kesi yenyewe ni ya zaidi ya miaka ishirini na saba."
"Hee!! hivi Shebby mwanangu akili zake zimeingiwa nini hadi ashawishike kufanya upelelezi wa kesi ya miaka kibao namna hiyo? hee!!"
Alitahayuri na kukunja uso mzee Mwinchande kisha akatoa tena simu yake na kuanza kubinya binya namba.

ITAENDELEA...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom