Simulizi: Wanawake ni wauaji

Simulizi: Wanawake ni wauaji

EPS 29
========

* * * * * *

Vijana walikuwa tayari na muda ule ule wakaanza kumkamata mzee mmoja mmoja waliyekuwa wakioneshwa na kamihna Shebby na Kimaro.
Watu wengi walishangaa tukio lililokuwa linaendelea kufanywa na wale askali licha ya kuwa walikuwa kwenye huzuni na msiba mzito na kitendo kile kilichoanza cha kamatakamata kilizidisha kilio kwa familia nyengine hususan watoto na wake wa wale wazee waliokuwa wanakamatwa.
"Halooo babu yule mwenzako mwenye baraghashia yuko wapi?"
aliuliza Kimaro pindi alipomfata mzee ambae tayari alishadhibitiwa na vijana wa polisi mara walipooneshwa.
"Haa! jamani mjukuu wangu kwani tumekosea nini mbona mwatuumiza kiasi hiki?"
alihoji yule mzee.
"babu jibu swali usiulize swali nisije kukuzimisha sasa hivi unavyotuona sisi ndo tushapagawa kuliko mtu yeyote hapa."
aliongea kiukali Kimaro na mara dakika zile zile Kamishna Shebby akiwa na askali mwengine walifika pale.
"vipi Kimaro inaonekana bado mzee mmoja."
"Kweli mkuu na ndio nilikuwa namuuliza huyu alipo mwenzake kabla vijana hawajaondoka nae"
alijibu Kimaro lakini dakika zile zile walisikia ukelele furani kutokea upande wa kaskazini kulipokuwa na nyasi nyingi na miti mikubwa michache na kabla hawajajua wafanyeje mara alikuja mtoto mmoja raia wa pale kijijini ambae ilisemekana ni mjukuu wa yule mzee waliekuwa wanamuulizia huku akiwa anahema sana kichwa chote kimetapakaa majani.
"vipi dogo?"
aliuliza haraka Kamishna Shebby huku akitoa pisto yake pale kiuononi.
"Babuu.. babuu yupo kuleee tulikuwa tunakimbia na jitu moja halina usoo aaaah! linataka kumuua babuu..."
aliongea kwa shida kutokana na hofu iliyojengeka kwenye kifua chake na kabla hajamalizia Kamishna Shebby alipiga risasi moja juu na kuwaamuru wenzake haraka wawahi eneo iliposikika ile sauti.

Walikata mapori haraka haraka huku wakiruka visiki na Kamishna Shebby aljikuta anakuwa na mbio kuliko wenzake na kuwahi ile sehemu ambapo alimkuta yule mzee akiwa amelala chini akiwa katapakaa damu pia akitokwa damu mdomoni na puani na kifuani mwake kulionekana ameshikilia mpini wa kisu kilichozama chote eneo la kifua upande ule wa moyo.
"Jasho lilikuwa linamvuja na kutaharuki shebby pamoja na wenzake waliofika muda ule huku wengine wakikagua maeneo ya jirani kuona kama kuna mtu mwengine.
"Nambie babu.. nambie tafadhali najua unajua nitajie nani Mr. X nitajie mzee wangu jitahidi nitajie hata cheo alichokuwa nachoooo.."
aliongea huku machozi yanamtoka shebby mara baada ya kupiga magoti na kumpakatia yule mzee aliyekuwa bado hajafa ila yupo katika hali mbaya na kweli alianza kujilazimisha kuongea kwa shida huku mdomo wake ukirusha mafunda ya damu yaliyokuwa yanamrukia usoni pia shebby.
"Huu.. missss..ta.X ni... nii..aaaghhhrrr...niii....."
Lakini akiwa anahangaika kusema kabla hajamalizia ni nani huyo mr.X mara kichwa cha yule mzee kilifumuliwa ghafra na ubongo kutawanyika sambamba na damu kutokana na risasi iliyotua bila kutoa mlio wowote mbele ya macho ya Kamishna Shebby OCS na st;sajent Kimaro.

* * * * * *

Wakati huo upande wa pili makao makuu ya gereza mzee Mwinchande alighadhibika na kumpigia mwanae lakini simu safari hii haikupatikana kabisa.
"Kijana hebu naomba nisaidie aitwe huyo mfungwa mwenyewe nimuone anambie nini alichomuhadaa mwanangu hadi afikie huko kote."
aliongea mzee Mwinchande ndipo yule mkuu msaidizi alipoamua kumpigia simu ya mkononi coplo aliyesimamia jera za v.i.p na kumpa maelekezo na baada ya dakika kumi na tano aliletwa mzee Hussein eneo ndani ya ofisi ile kuu.
"Huyu hapa mkuu."
aliongea yule coplo aliyemleta huku akiwa ameongozana na askali wengine wawili waliomshika Hussein kipindi wanamkokota kwenda nae mahala pale.
"oke sawa, mnaweza kusubiri nje."
alitoa amri mkuu msaidizi na hatimae ndani wakabaki watatu yaani mkuu msaidizi, mzee Mwinchande na Hussein babu Bubu.
"Mtu mwenyewe ndio huyu?"
aliuliza mzee Mwinchande licha ya kuwa tayari alishaelekezwa kuwa ataletwa mfungwa mwenyewe aliyesumbua kichwa cha Kamishna Shebby na ndie yule aliyeletwa muda ule.
"ndio huyo mzee."
"sawa unaitwa nani bwana"
aliuliza mzee mwinchande huku akimuagalia kwa dhalau Hussein
"We bwanaaee si nakuuliza mie?"
aliuliza tena mzee Mwinchande baada ya Hussein kubaki kimya akiwatazama tu huku moyoni mwake akiwa kaghadhibika baada ya kuoneshwa dhalau.
"mzee wangu huyu muda mwengine anakuwaga sanamu hivyo hivyo sasa ngoja tum boost. coplo Yonaaa.."
alidakia mkuu msaidizi na kumwita coplo ambae alimuelekeza amboost Hussein aweze kusema na kweli coplo Yona alichomoa mkanda na kuanza kumtandika Hussein hadi mzee Mwinchande mwenyewe akazuia mara baada ya kuona tayari Hussein alipasuka hadi kwenye mdomo.
"Haya mzee mwenzangu mi nakwambia kwa ustaarabu lakini wewe unataka uambiwe kama ulivyozoeshwa. sasa narudia kabla sijaendelea wewe unaitwa nani?"
Alirudia kweli kauli yake mzee Mwinchande lakini Hussein alikuwa kiburi sana hasa anapogundua mtu anayeongea nae anamletea dhalau.
Vitasa viliendelea bila Hussein kujibu chochote hadi mzee Mwinchnde alianza kufoka.
"Yaani mwanangu anajitolea kusaidia mabubu yasiyo na fadhila wala mawazo kama hili??? Duuh! sasa Shebby kasema sema nae vipi mbona sielewiii hapa."
Kipindi alipokuwa analalama mzee Mwinchande na kumtaaja Shebby ndipo hapo ubongo wa Hussein ulivubuka kwa kujua kumbe yule mzee ni baba wa kamishna yule aliyejitolea kumsaidia.
"Kumbe wee ndie baba wa Kamishna Shebby."
aliongea kwa sauti yenye mikwaruzo Hussein mara baada ya kusikia kumbe yule mzee ni baba wa mkuu wa gereza Kamishna Shebby.
"Jamani msinipige kama huyu bwana ni baba wa Kamishna Shebby tafadhali niacheni niongee nae."
alisisitiza Hussein na hapo ndipo vijana wa coplo walipomuacha kumtandika mikanda na kumsimamisha aongee.
"Enhee! sema umemuhadaa na hadithi gani mwanangu mpaka haeleweki mambo yake."
"Lakini hapo sielewi kaka kwanini unasema nimemuhadaa."
"oke, utaelewa tu."
aliongea mzee Mwinchande huku akisukuma kiti chake na kukaa vizuri.
"Sikia bwana bubu, kwanza samahani kwa kukufokea mzee mwenzangu ila unajua mtoto anauma sana. sasa mi nilitaka kujua ni hadithi gani inayokuhusu uliyomsimulia mwanangu hadi kupelekea kuwa bussy kiasi hiki.? Naomba unijibu kweli na unihadithie walau kiufupi kwasababu mimi ni baba mzazi wa Shaaban pia ni Kamishna mkuu msaidizi mstaafu wa jeshi la polisi nchini kwa hiyo usiwe na hofu wala uoga wa kunihadithie ukweli ulichomwambia mwanangu tujue nini cha kufanya maana mpaka sasa nahisi mwanangu kajibebesha mzigo asioujua wapi pa kuutulia."
aliongea mzee Mwinchande na ndipo hapo Hussein alipofikiria na kukata shauri kuamua kuzungumza ukweli kile ambacho alikizungumza kwa Kamishna Shebby na hasa akikazia kuwa wanawake ni wauaji kwani aliamini huyo mtu aliyeitwa mr.X alijuana vizuri na mkewe lakini mkewe alimficha so ubaya wote kaufuga mkewe na pia mission aliyokuwa anaifanya Shebby ni kutafuta ukweli kuwa huyo mr. X alikuwa nani?

"Uuuuuppphhhhh!!!!! ... yaani hadithi yako imenishangaza sana na kuniumiza pia pole sana bwana."
alihema mzee Mwinchande na kumpa pole bwana Hussein bubu baada ya kuguswa na kisa chake.

ITAENDELEA...
 
EPS 30
========

"sasa Hussein hivi we humkumbuki hata kidogo huyo mr.X walau tetesi zake alikuwa nani au yukojeyukojeee..?"
"Kiukweli kaka sio kwamba sikumbuki bali simjui kabisa na sijawahi kumuona wala kupata tetesi zake hapo kabla zaidi ya barua ile ya utata."
"Duuh! sasa kama muhusika uliyekuwepo enzi hizo humjui?!!! Je, mwanangu atawezaje kumjua?? atapitia njia zipi wakati wewe mwenyewe huna hata formula? Huoni kama ni kazi ya ajabu isiyokuwa na kichwa wala miguu. Mi nina wasiwasi na kazi aliyojitumbukiza mwanangu inaweza kumletea hatari kama huyo mr.X kwa jinsi ulivyonisimulia kama ndio kweli na yuko hai hadi sasa.. naamini endapo atazipata hizi habari anaweza kumuua kabisa mwanangu tena itakuwa rahisi kwa kuwa yeye hamjui.. looh! "
aliongea kwa unyonge mzee Mwinchande na kubaki anamtazama mkuu msaidizi na Hussein ambao wote walibaki wanakuna vichwa wakilifikiria swala lile na ndipo kwa mara nyengine mzee Mwinchande aliamua kupiga namba ya Shebby lakini bado majibu yalirudi yaleyale kuwa haipatikani.
Safari hii sasa walianza kuingiwa na wasiwasi juu ya huko walipo kina Shebby kwani kigiza tayari kilishaanza kuingia.

* * * * * *

"Ooooooh! Shit!! Look for the Snipeeeeeeeeeerr.."
aliitoa amri kwa sauti ya juu Shebby huku akiruka samba soti na kuangukia pembeni kwenye machaka lakini alishangaa ndani ya dakika zile zile kusikia ukelelee mkali toka kwa st;sajent Kimaro na alipokimbilia upande ule alimkuta Kimaro anamalizikia huku akiwa kafumuka vibaya maeneo ya kifua.
Hali ile iliwaogopesha askali wote waliokuwepo pale ukichochea na kigiza kilichoanza kuingia kilichowafanya washindwe kuona vizuri ukichangia hali ya miti mikubwa iliyoshona ndo ilizidi kuongeza kiza na kuwafanya wakose plani baada ya kujikuta wakiwa katikati ya mtego wa sniper hatari ambae walijua yupo juu ya mti mkubwa lakini hawakujua ni mti upi kutokana na giza na wingi wa miti mingi mikubwa.
askali mmoja mmoja sasa alidondoshwa na kusababisha kamishna Shebby na wenzake kuanza kujipigia risasi ovyo kuzielekezea juu ya miti lakini muuaji hakuwa na papala aliendelea kuwadondosha taratibu na hatimae katika kimbia kimbia huku akijibana chini ya miti na Kumtukana muuaji kwa nguvu zote akiwa na lengo kama atajibu ajue sauti inapotokea iwe rahisi kupambana nae lakini muuaji alikuwa na akili nyingi sana hakujibu chochote zaidi ya kuwaangusha kimya kimya kimya na hatimae Kamishna alijikuta yuko mwenyewe.
"Oooooh!! Sheeeb..shebbbbby Unatuuuuuaaaaa."
Iliisikia sauti ya maumivu ya ocs John iliyomfanya kufumba macho Kamishna Shebby huku machozi yakimtoka kwa uchungu na kujilaumu kuwa yeye ndie aliyewaponza wote waliokuwa wanapoteza maisha muda ule, na laiti isingekuwa imani yake ya kutaka kumjua mr.X basi yale yanayotokea muda ule huenda yangekuwa njozi.
lakini siku zote neno Ningejua huja baada ya kitendo.

"Jitokezeeeee Mwanaharaaaamuuu Mkubwaaaaaa weeeee kama mwanaumeeee jitokezeeee Tupambaneeee wenyeeweee.."
Alilalama Kamishna Shebby kwa sauti ya juu huku akiwa kasimama kati kati ya msitu wa miti mikubwa huku nguo zake zote zikiwa zimetapakaa damu za baadhi ya wenzake waliouawa akiwemo Kimaro aliyekufa mbele yake yule mzee wa kibaraghashia na mkuu wa upelelezi aliyepigwa risasi ya kichwa kipindi wakikimbia pamoja.
"AaaaaaaaghhhhJitokeeezeeeee Ku*a weeeee kama Mwanaumeee kweliiiiiiii.."
Aliongea kwa nguvu Kamishna Shebby huku akiwa kachanganyikiwa na kuitupa chini pisto yake na kujipiga piga kifua kwa hasira huku akiunguruma na kuhema kama duma mzee aliyetoka kukimbiza swala jangwani.
"ha ha ha ha ha ha haaaa.."
Kilisikika kicheko kikitokea maeneo ya nyuma hatua chache na aliposimama Kamishna Shebby lakini ajabu kicheko hiki kilikuwa ni cha mwanamke na alipogeuka ghafra Kamishna Shebby hakuamini macho yake mara baada ya kumuona mtu akishuka tokea juu ya mti mmoja mkubwa sana kwa kutumia kamba maalum aliyojifunga kiunoni huku akiwa kavaa full Combat Ninja (Mavazi kamili ya Kininja) na miwani maalum yenye kubadilisha hali ya hewa ya kuonea hadi usiku huku mikononi mwake akiwa kakamatia bunduki kubwa ya udunguaji na kumueka chini ya ulinzi Kamishna kipindi akishuka taratiiibuu.
Shebby haraka alitaka afanye ujanja wa kuiwahi ile pisto aliyoitupia pembeni lakini ile anaruka tu yule Ninja aliidungua ile pisto na kuipeleka mbali zaidi na Kamishna Shebby kuangukia patupu lakini hakuchoka wala hakujali Shebby alitaka kumrukia hivyo hivyo yule Ninja aliyemtia hasira zaidi baada ya kubaini alikuwa ni mwanamke lakini ile ananyanyuka tu alipigwa risasi ya goti na kuubong'onyoa mguu wake na kuanguka chini Shebby huku akipiga kelele za maumivu na kipindi hiko tayari yule Ninja mdunguaji alishafika chini kabisa.

"Kamishna Shebby... ha ha ha haaa wewe ni kijana mzuri sana mwenye bahati katika maisha yako.
Ila kinachokuponza ni kutaka kujifanya bingwa wa kuutafuta ukweli ulioshindwa kuonekana kwa zaidi ya umli wako pasi na kujiuliza je, hawakuwepo watu kama wewe waliotaka kuujua huo ukweli? na kama walikuwepo kwanini waliacha kuutafuta?
Nadhani ulitakiwa kwanza utafute majibu ya maswali hayo mawili ndio uchague uutafute ama nawe uache kama walivyoacha wenzako kibao waliopita.... Lakini wewe umejitia shujaa umekurupuka na kuwaponza wenzako Kibao wafe bila hatia.
Ona sasa maisha yako yalipofikia, nani ataweza kukutetea hapa hahahahahaaaaaa Nilitakiwa nikubebeshe kesi hii ya kuwaua wenzako wote kisha na wewe kujipiga risasi ya mguu ili kupoteza ushahidi kwa maslahi ambayo unayajua mwenyewe lakini una bahati sana kwa sasa nakuacha salama ili nikupe nafasi ya mwisho ya kukuonya na hili ni ONYO kutoka kwa Mr. X unayemtafuta kuwa USIJE KUTHUBUTU KURUDIA TENA KUTAFUTA UKWELI WOWOTE KUHUSU MR. X
Na kwa msaada alioutoa Mr.X kwako amesema kuwa Kama utakuwa bado m bishi na ukataka kujaribu kumtafuta tena basi amekupa zoezi dogo ambalo kama utaliweza basi utaweza Kumpata na kumjua.
Na zoezi lenyewe ni hili...... SIMAMA JUANI UKIKAMATE KIVULI CHAKO KWA MIKONO YAKO MWENYEWE.
ila Ukishindwa............... KUMBUKA
BAHATI HAIJI MARA MBILI..."

Alimalizia kuongea yule Ninja ambae alikuwa na sauti nzuri sana ya kike japo hakujifunua uso apate kuonekana lakini alionesha dhahili alikuwa ni mwanamke tena msichana kabisaaaa.
Kipindi hiko chote Kamishna Shebby alikuwa anamtazama yule Ninja muuaji huku mwili wote ukiwa umekufa ganzi pale chini alipoangukia akiwa kalala chali baada ya mguu wake kuharibika vibaya eneo la goti huku akiwa haamini kama kikosi kizima kimechezeshwa kindumbwe ndumbwe na mwanamke.
"Aaaagh!! Kweli nyie wanawake niwauaji hatari sana tena msiorudi nyuma wala kufiria hasa pale mnapopewa nafasi ama amri huitumia vizuri ili mzidi kuimanishwa na muonekane bora kuliko wanaume. Ila kumbuka kuwa wewe si wa kwanza kutumiwa na mr.X na laiti ungejua yakinifu huyo anaekutuma kesho anaweza kukuua hata wewe endapo atasikia upo kwenye mazingira hatarishi na maisha ya siri yake..... hahahahaaaa tatizo wanawake hamfikirii hah haha Ila nami nakwambia hii uliyoipata leo ni bahati kubwa sana ni bora tu uitumie lakini nakuahidi ukiniacha hai lazima nije kukutafuta na utalipa Damu zote zilizovuja leo.

ITAENDELEA....
 
EPS 31
========

Naapa sitokuja kukuacha hai kama leo utaniacha hai na umwambie mr.X asijidanganye mwisho wake UPO na atakufa kifo kibaya na cha mateso aaghhh.."
Aliongea Kishujaa Kamishna Shebby japo kwa tabu lakini maneno yake ndio kwanza yaliongeza kicheko kwa yule muuaji Ninja wa kike na hapo ndipo alipomshuhudia akiitupa chini ile bunduki ya udunguaji na kuchomoa pisto maalum ndefu na kuiload kisha kumuelekezea pale chini ndipo Kamishna Shebby aliposali sala zake za mwisho na kufumba macho kusubiria aisikie risasi itavyofigisa nyama zake.

Akiwa kafumba macho pale chini Kamishna Shebby huku akiamini kuwa ndio ulikuwa mwisho wa maisha yake mara alisikia kitu kikipenya kwenye paji lake la uso mithili ya mwiba wa nyuki na kumsababishia maumivu makali hasa baada ya kuhisi haikuwa risasi na kuamua kufumbua macho ambapo alijikuta akishindwa kuona vizuri na kuanza kupoteza nuru machoni mwake na hatimae taratibu mawasiliano kati ya mwili na fahamu zake yalikata na kupoteza maisha kwa muda (kuzimia).

* * * * * *
- MUDA HUO HUO (GEREZANI) -
...............

Baada ya kuona usiku umeingia na hakuna majibu yoyote hata
walipopiga simu ya St;sajent Kimaro iliishia kuita bila kupokelewa zaidi ya mara ishilini ndipo sasa si mzee Mwinchande tu bali hata mkuu msaidizi wa gereza aliingiwa na hofu.
"Mi nahisi kijana kutakuwa na tatizo tu si bure kwani hata jinsi simu ya Kamishna wako ilivyokatika katika sijaelewa!!"
"Mh! sina imani sana mzee wangu.. Eti we bubu ni sehemu gani waliyoenda kamishna na Kimaro?"
alimgeukia Hussein yule msaidizi na kumpachika swali.
"Mkuyuni.. Mkuyuni Morogoro"
alijibu Hussein na pale pale kamishna msaidizi alipopekua kwenye computa ya ofisi yake kwenye mafairi na vitengo vya wakuu wa vituo vyote nchini na kuingia Mkoa wa morogoro na alipoisearch Mkuyuni ilikuja sambamba na picha na namba za mkuu wa kituo.
"Ngoja kidogo mzee wangu hapa nimelipata jina na namba za ocs wa Kituo Mkuyuni huyu bwana John tuongee nae tuone anaweza kutusaidia vipi ili tuweze kuwapata"
aliongea mkuu msaidizi wa gereza huku akibinya namba zile za simu za ocs John na kupiga lakini ajabu nayo iliita zaidi ya mara tisa pasi na kupokelewa na hata alipoitafuta ya mpelelezi mkuu wa kituo cha Mkuyuni nayo iliishia kuita na zaidi zaidi baada ya kupiga sana ilikosekana na kuwa haipatikani kabisa.
Hii iliwafanya waingie na shaka zaidi na ndipo walipoamua kupiga namba za kituoni rasmi na kuachana na zile za mikononi na hii haikuchelewa kuita ikapokelewa.
[['Hallow hapa ni kituo kikuu cha polisi Mkuyuni sijui nani mwenzetu kutoka wapi na tukusaidie nini tafadhali...?']]
Ilisikika sauti ya kike mara baada ya simu kupokelewa.
"Unasikika moja kwa moja kutoka Gereza kuu la makosa mazito Kigamboni na mimi ninayeongea ni mkuu msaidizi wa gereza napenda kujua wapi alipo mkuu wa kituo nizungumze nae."
[['Ooooh!, Jambo mkuu']]
"jamboo"
[['sasa samahani mkuu ametoka kidogo kuna wageni walikuja hapa wameelekea huko mabondeni kwa mission oparetion maalum']]
"Ni ugeni gani huo tafadhali naomba nijuze,"
"aaagh, ni ugeni wa ghafra wa Kamishna"
"Kamishna yupi huyo hebu nielezee kidogo jinsi alivyo"
aliongea mkuu msaidizi huku akiirekodi kabisa ile simu,
"Kamishna mmoja kijana, mwenye rangi ya maji ya kunde alikuwepo na mwenzake mfupi kidogo mweusi."
"Okey, unaweza kutuma ujumbe wangu sasa hivi kwa mkuu wako?maana ni muhimu saana tena sana kuzungumza nae muda huu."
[['sawa piga baada ya dakika tano']]
Ilisikika sauti upande wa pili na simu kukatika wakingoja majibu wapate kuzungmza na ocs huku mioyo yao ikiwa inawaenda kasi hasa mzeee Mwinchande.

* * * * * *
- MKUYUNI -
...........................

Alisimama sub Inspector wa kike ambae kwa muda huo alichukua nafasi ya mkuu wa kituo kwa muda na kutoka nje ya kituo karibu na barabara kuu mara baada ya kuona raia wengi wakikimbilia pande zile za kituoni huku wengi wakiwa na nyuso za hofu.
"Afande.. Afandee tumesikia risasi kule mabondeniuuhhh apphhhh wanakufa watu kule na mapolisi wenzenuu puuhphhhuu"
aliongea bwana mmoja huku akiwa anahema sana na kumtia hofu mwana mama yule sub Inspector ambapo kituo kizima kilibaki na askali wawili pekee na gari moja ukiachilia askali wanne na gari lengine ambalo lilipeleka maiti ya yule aliyenyongwa hospitali ya morogoro mjini.
"we unasemaje ati.?"
"Ndio hivyoo mamaaa kuna Kibwengoo huko mabondeni anaua watuu"
aliongea mwengine huku wakiendelea kukimbilia maeneo ambayo walihisi ni salama kwani waliamini huenda kiumbe anayeua watu kule mabondeni akapandisha juu muda wowote na kuendelea kuua wengine.
Akiwa haelewi nini afanye kama kiongozi kwa bahati nzuri muda uleule mwakanga mkali wa taa za gari iliyokuja inakuja speed ilimmulika na kusimama karibu naye na ilikuwa ni difenda yao ile iliyopeleka maiti.
"Vipi, nasikia wakuu wamepatwa na matatizo huko?"
aliuliza sub inspecta mwengine yule wa kiume ambae ndie alikuwa kaimu namba moja wa ocs John kabla ya yule mama pindi akiwa ndani ya Diffender.
"sielewi kwa kweli hata simu hazipokelewi na niliposikia kelele na kutoka nje ndo nimezipata tetesi sasa hivi na baadhi wa watu waliokuwa wanakimbia."
"mama we endelea kubaki na kudumisha usalama hapa sisi tunaelekea huko huko"
aliongea yule sub inspekta wa kiume na kumuamuru dereva wake aliyeondoa gari kwa fujo zote alizozijua mwenyewe.

Muda mfupi baadae timu nzima ile ya askali waliotoka hospitali iliwasili eneo la nyumba ya mzee Mnyungunyungu ambapo kwa ajabu kulionekana kimya sana mara baada ya watu wengi kukimbia kipindi waliposikia risasi zinarindima maeneo ya jilani na pale.

Wakiwa wamejifunga na kuwasha tochi maalum kichwani kwa niaba ya kuwasaidia kuona kutokana na giza nene lilikuwa limefunga nyakati zile eneo la msitu.

ITAENDELEA.
 
EPS 32
========

sub inspecto aliwaamuru vijana wake wale wachache kuwa waende kwa uangalifu mkubwa sana mara baada ya kukutana na maiti ya kwanza ya askali mwenzao kabla ya pili ambayo ilikuwa ya yule babu na walihamaki zaidi na kupigwa na bumbuwazi walipoikuta maiti ya mkubwa wao ambae ni ocs John akiwa ana alama mwilini mwake za tundu mbili za risasi ambapo moja sehemu ya mgongo na nyengine iliyomegua vibaya sehemu ya shingo na kusababisha kuzidi kuzitisha nafsi za wale polisi ambao walikuwa si wazoefu wa kazi za hatari kama zile na hawajawahi kushuhudia wenzao wamekufa kwenye mapambano yoyote tena kwa vifo vya kutisha namna ile.
Wakiwa wananyata wakiupitia karibu kabisa mwili wa ocs John lakini mara ghafra walijikuta wote wakistuka sana huku mwengine akajikuta anafatua risasi bila kutaraji na kurukia pembeni na kilichowastua hakikuwa chengine bali muito wa simu wa ghafra uliosikika kutoka katika sare za ocs John na kumfanya hadi sub inspector wao aangue kicheko pasi na kutaraji na kuisogelea tena maiti ya ocs wake kwa lengo la kuitoa ile simu iliyokuwa inaita.
"Lakini angalia kiongozi isije kuwa bomu hilo tumeekewa mtego na kitendo cha kuipokea kwako kisije kutupukutisha na sis..!!?"
alitahadharisha askali mmoja huku akirudi mbali zaidi na eneo alipokuwa subinspector kwa hofu.
Hali ile kidogo hata kiongozi ilimtisha na kutafakari maneno ya mwenzake lakini kwa kuwa yeye ndie aliyekuwa na sauti na majukumu pale ilim bidi aoneshe moyo wa kishujaa mara baada ya ile simu kuita mpaka ikakatika na ikaanza kuita tena na ndipo alipojipa ujasiri na kuugeuza mwili wa ocs kisha kuitoa ile simu kwenye moja ya mifuko ya nguo alizovaa Ocs John ambae kwa muda huo tayari alikuwa marehemu.
Aliitazama namba ya anayepiga ilikuwa haijaseviwa na kuomba mungu kimoyomoyo iwe heri pindi anapoipokea ile simu na hapo hapo alibana pumzi na kuipokea.

* * * * * *

Baada ya kusubiria jibu kwa zaidi ya saa moja bila mafanikio mzee Mwinchande alimuamuru tena yule mkuu msaidizi wa gereza kupiga tena namba za mkuu wa kituo Mkuyuni na bila hiyana yule mkuu msaidizi wa gereza ilibidi adondoke tena hewani (apige simu).

Safari hii simu iliita mara ya kwanza ikakatika bila kupokelewa lakini alipojaribu mara ya pili akiwa hana matumaini kama simu itapokelewa ila aliamua kufanya vile kumridhisha mzee Mwinchande ambae alionesha wazi kuchanganyikiwa na presha kupamba kifua chake akiwa anamuangalia mara alisikia sauti ya mtu ikiuliza upande wa pili na kubaini kuwa safari hii simu imepokelewa.

"Hallow unazungumza moja kwa moja kutoka makao makuu ya gereza la watu sugu Dar nami ninayeongea ni mkuu msaidizi wa gereza, nilikuwa nataka kupata habari juu ya kamishna wetu aliyesafiri kwa kazi maalum huko kwenye kanda yako vipi kuna taarifa gani?"
aliongea mkuu msaidizi huku akiwa kaeka loud speaker na automatic record.
[['Ni hivi kiongozi yaani hadi sasa habari huku ni mbaya sana na sisi ndio tumefika eneo la tukio lililojiri mapema usiku huu ambapo askali wote waliokuwepo kwenye tukio la mtu aliyejiua huku mkuyuni katika mazingira ya kutatanisha na walipokuwa katika utafiti wa kina juu ya chanzo chenyewe sasa wote wameuawa kinyama akiwemo ocs wetu ambae umempigia na mimi niliepokea ni msaidizi wake pindi tulipoingia eneo la tukio na kusikia muito wa simu. Tafadhali tunaomba mtuongezee nguvu kwa kuwa sasa hali ni mbaya sana hapa Mkuyuni amani imesimama kabisa raia wanakimbizana ovyo na muuaji bado hajulikani']]
Ilisikika sauti iliyomfanya mzee Mwinchande aangue kilio cha sauti akiwemo Hussein bubu ambae alikuwa bado hajarudishwa kwenye chumba cha jere aliyofungwa.

"Haiwezekaniiiiii Mwanangu afe hivi hivi iiiiih.. hebu muulize kama wamemuona na mwananguuuuuuuu.."
alilia kama mtoto mzee Minchande lakini yule mkuu msaidizi wa gereza pindi alipomuuliza yule aliepokea simu alijibiwa kuwa imeonekana maiti nyengine ya yule aliyekwenda na Kamishan Shebby na hapo mkuu wa gereza msaidizi chozi lilimdondoka na kuamini sasa Kimaro nae hayupo tena duniani lakini alipoulizia kuhusu ripoti kamili ya kamishna aliambiwa bado hawajamuona wanaendelea kutafuta pia walikuwa wanajiandaa kufanya mawasiliano na wenzao wa morogoro mjini ili wasaidiane katika kazi ile kwani tayari polisi waliokuwepo walikuwa wachache mno na hawana uzoefu tofauti na wale waliokuwa wengi tena wapo na watu wenye uwezo mkubwa kwenye matukio lakini kundi lote likasambaratishwa!! hii inaonesha jinsi gani muuaji alivyo mkali na alivyojipanga.

"HAAA HAIWEZEKANI HATA KIDOGO"
aliongea kwa sauti ya juu mzee Mwinchande na kuchukua simu palepale alitafuta jina moja na kuanza kupiga na hakuwa mwengine aliyekuwa anampigia bali ni Kamanda mkuu wa polisi kanda ya Morogoro.

"Halloooow, yaani ndugu yangu mwanangu mnaacha anaelekea kufa hapo mkuyuni hakuna msaada wowote mliompatia? aahg!! siamini mdogo wangu"
[["Vipi kaka, mbona sielewi?"]]
"Wewe kama Kamanda wa mkoa nitakuelewaje unafikiri? Tuma vijana wakutosha haraka mkamsaidie mwanangu kama bado yuko hai lakini nataka nikwambie askali wako wengine wa Mkuyuni pamoja na Ocs wao wameuawa usiku huu."
[[Khaaa!]]
alisikika Kamanda mkuu wa Moro akitaharuki na simu kukatika ambapo akiwa bado kachanganyikiwa mzee Mwinchande aliamua kumpigia simu wazili wa mambo ya ndani na kumlalamikia na wazili alishangazwa na kusikitishwa mno na habari zile kisha akamuahidi mzee Mwinchande itatumwa special force usiku uleule kwa helkopta maalum ya kijeshi kwenda kumtafuta mwanae ambae pia alikuwa na wadhfa mkubwa tu nchini, ukumbuke wadhfa wa Kamishna hutolewa na Mh Rais mwenyewe.

* * * * * *

Kwa upande wa Hussein babu bubu yeye kilio chake kilikuwa cha peke ake hata pale aliporudishwa kule kwa wafungwa wenzake muda wote alikuwa analia kama mtoto huku akiilaumu nafsi yake kwa kukubali kumuhadithia kitu alichokaa nacho zaidi ya miaka 25 bila kumwambia mtu lakini leo hii anajikuta anamponza na kumsababishia matatizo makubwa kijana wa watu ambae hakuwa na hatia hata kidogo na hadi dakika hiyo hakuwa na hakika kama yu hai au nae amekufa kama wenzake.

"Eee Mungu baba Muumba mbingu na nchi, najua wewe ndie muweza na mpangaji wa kila kitu... Nakuomba umuepushe mja wako asie na hatia katika balaa lililo mbele yake muda huu na yote hiyo ni kutokana na huruma yake ya msaada.
Basi nami nakuomba baba msaidieee Mponye na umueke mbali na Kifo mpaka atapofikia umli wa utu uzima sana na hata kama atakufa basi asife kwa sababu ya kesi hii tena.
Nakuomba baba nitendee Muujiza na niweze kulipa kisasi kwa Mr. X mimi mwenyewe pasi na kuhusika mtu mwengine yeyote."

Yalikuwa ni maombi aliyokuwa anaomba Hussein ndani ya moyo wake huku machozi yakim bubujika muda wote na hadi unaingia usiku mkubwa alitamani atoke akaulizie wamefikia wapi kuhusu Kamishna Shebby lakini hakupata nafasi hiyo kwa kuwa yeye mfungwa na hakuwa na haki za kuuliza habari za maaskali hata wadogo sembuse askali wakubwa! tenawenye heshima kama Shebby.!!?
Alibaki kasimama akiwa kashika nondo za geti la chumba alichokuwa analala huku akiangalia korido ile ndefu iliyokuwa kimya kwa nyakati zile za usiku mkubwa akivuta taswira ya Kamishna Shebby mtu pekee wa kwanza kumuonesha thamani kubwa ndani ya jera. Aliwazia atapata wapi tena mtu mwenye moyo wa ukarimu ampende kama Shebby? aliamini hakuna na hatotokea mpaka siku atayoingia kaburini. Shebby alikuwa kijana wa ajabu sana kwake vipi leo hii afe tena kabla yake..!? aliumia sana Hussein na kumlilia Kamishna Shaabn kama mtoto wake wa kumzaa au zaidi ya hapo.

Hadi kunakucha Hussein alibaki kasimama palepale alishindwa kabisa kulala na kusogea popote zaidi ya kububujikwa machozi yaliyobeba kumbukumbu nyingi za huzuni na hasira kuhusu MR.X
Usiku huo aliomba mabo mengi sana na kubwa alitamani na kumuomba sana mungu amfanyie muujiza ili amuue Mr.X kwa mkono wake hapo hata nae akifa itakuwa afadhali na atakifurahia kifo chake kuliko kufa akimuacha mr.X duniani akizidi kuwamaliza watu wasio na hatia wataotaka kuufichua ukweli wake ambao aliamini chanzo cha yote ni mkewe yule aliekuwa binti mrembo kutoka Arusha.
ITAENDELEA......
 
EPS 33
========
* <*> <*> <*> <*> *
............................
<**MCHEZO wa MR X**>
================

[{z''zZz}"Mr.X ni kivuli cha jina la mtu mmoja hatari sana mwenye mbinu ngumu za haraka na mitego yenye sumu na isiyoonekana hata kwa darubini na rada........Hakutumia sana nguvu katika kuuficha ukweli wake na siri nzito isiyojulikana kuwa yeye ni nani na laiti angetumia nguvu basi serekali ni kubwa na ina nguvu sana hivyo muda mrefu angeshajulikana lakini tofauti yeye anatumia nguvu kidogo lakini inatangulia kwanza Akili kubwa.
Akili iliyobeba maarifa mengi na ya ajabu........... na jinsi ya kupigana na mr X ili umshinde inabidi ujiingize kwenye akili zake na umzunguke na kutega mabomu ya akili zako ili siku ukiyalipua atakosa akili mpya na hapo ndio utamkamata kiurahisi zaidi.
Pia mr X ana mtandao mkubwa sana wa watu wanaomfanyia kazi waliogawanyika katika sehemu kuu mbili.
Moja ni wale wanaojijua kuwa wanafanya kazi katika mtandao wa mr X na pili kuna wale wasiojijua kama wanafanya kazi katika mtandao wa mr X
Lakini kwa utaalam wa akili za mr X kayatengeneza haya magroup na kuyaweka sehemu moja na bado hakuna anayejua kama kuna group lengine zaidi linafanya kazi ya mr X na pia kati ya hao wafanya kazi wa magroup yote wanaomfanyia kazi mr X bado kati yao hakuna hata mmoja anayemjua mr.X mwenyewe ni nani wala hakuna ofisi yoyote akiyojenga mr X inayoweza kuwakutanisha watu wake zaidi ya mtu mmoja tu mwenye siri zote ambae ni rahisi sana tena sana hasa kwako wewe kufika alipo lakini ni Ngumu ngumu tena ngumu sano kumpata na kumjua mtu mwenyewe.
Na hii yote ni kwa sababu mr X anawachezesha mchezo.
Mchezo wenye akili nyingi kuliko michezo yote unayoijua au uliyowahi kuisikia.
Mchezo ambao hauna mashabiki na inabidi uucheze bila papala na kwa akili nyingi.
Na mr X ndie mwenye mchezo huu.
Mchezo ambao humuingiza yeyote atayetaka kumtafuta na kumjua yeye ni nani na sasa nawe umejiingiza kwenye mchezo pasi na mr.X mwenyewe kutaraji lakini kwa kuwa umetaka basi inabidi ujiandae kuucheza huu mchezo kwani ushakuwa mchezaji mpya.
Jibu lako liko wazi Shebby amka sasa..
karibu kwenye MCHEZO wa MR X
Amka sasaaa Shebby umalizie zoezi moja tu rahisi utaloanza nalo.
amka muda ndio huu anza sasa kujifunza zoezi hili...
Amkaaaa Shebbyyyyyyy.... Amkaaaa Ukikamate kivuli Chakooo"{zZz''z}]

Alistuka kwenye usingizi mzito Shebby mara baada ya kuisikia sauti ya ajabu iliyokuwa inampasha habari za mr.X kwenye njozi ndefu na kujaribu kupiga kelele lakini alijikuta anashindwa kutokana na taya zake za mdomo kukaza pia alishindwa kugeuza mwili wala kujinyanyua kutokana na mwili wote kufa ganzi na jinsi alivyofungwa kwenye kile kitanda maalum ambacho bado hajajuwa kilikuwa wapi.
"Pumzika tu Mkuu, upo salama sasa tunarudi nyumbani."
Ilikuwa ni sauti ya kijana mmoja mweupe aliyevaa gwanda maalum nyeusi huku begani mwake kukiwa na alama ya bendera ya Tanzania na Kamishna Shebby japo alishindwa kuzungumza lakini alipomtupia jicho alijua fika wale walikuwa ni vija wa kikosi maalum wa jeshi la polisi wanaotumwa kwa shughuli maalum yaani Special force.
Na akili ilipozidi kumtulia ndipo alibaini kuwa walikuwa ndani ya Helkopta ya Kijeshi na kwa muda huo walikuwa angani.

Alitamani kusema kitu Shebby lakini hakuwa na uwezo huo kutokana na maumivu makali aliyoanza kuyasikia hususani upande wa mguu wake wa kushoto na kumbukumbu zake kuanza kurudi nyuma harakaharaka na kukumbuka kuwa alipigwa risasi ya mguu.
Hakuishia hapo zilimjia picha zote za wenzake walivyouawa kinyama na alipomkumbuka st;sajent Kimaro ndipo machozi yalipozidi kumtoka na uchungu usio na kifani ulifurika moyoni mwake huku akijiapiza moyoni mwake kuwa endapo akipona tu lazima amtafute mr.X kwa udi na uvumba pia yule mwanamke aliyewaua wenzake lazima nae aje kumuua kinyama tena kwa mkono wake na alijieka tayari kuucheza huo mchezo na lazima aje awashinde kwa njia yoyote ile.

* * *

Helkopta ilifika jijini Dar na kutua kwenye hospitali maalum ya kulipia aliyoamrisha mzee Mwinchande kuwa mwanae inapaswa akatibiwe pale hilo jeraha alilopata huko na hadi muda ule tayari mzee Mwinchande sambamba na mkuu msaidizi wa gereza na baadhi ya askali wakubwa walikuwa wanasubiri kwa hamu kumuona Kamishna Shebby na kuushuhudia mwili wa st;sajent Kimaro ambao nao ulikuwamo kwenye ile helkopta huku kila kiongozi na askali aliosimama eneo lile hata wale wasiokuwepo ila walipata tu habari bado walishangazwa na kujiuliza sana nini kiliwakuta huko maporini Mkuyuni na kwanini kamishna kaenda kufanya kazi ambayo hakupaswa kabisa hata ingemuhusu bado kwa wadhfa wake ilibidi awatume vijana aliowazidi cheo wakaifanye kwa niaba yake lakini ilikuwa tofauti sana kwa Kamishna yule ambae siku zote hakupenda ukubwa na anapofanya kazi hataki afanye kisa yeye mkubwa bali kwa manufaa ya kazi na taifa kwa ujumla.

Baada ya vitanda viwili kushushwa kwenye helkopta huku kile kimoja kikiwa kimefunikwa kabisa na kuwatoa machozi askali na viongozi wa jeshi waliomjua Kimaro na cha pili kikiwa kimeachwa wazi sehemu za juu ambapo ulionekana uso wa Kamishna Shebby ukiwa una alama na michilizi ya damu na kwa upande wa mkono wake mmoja ambao ulikuwa haukutundikiwa dripu aliunyanyua kidogo na kuchezesha kiganja kuwaondoa hofu wale waliokuwa wanamtazama kwa simanzi pindi alipopokewa na madaktari na kuanza kusukuma kitanda chake kukipeleka wodini na kabla hakijaingia kwa daktari mkuu ndipo kiliposimamishwa sehemu moja ya korido na Shebby alipogeuza shingo kushoto kwake kuangalia nani aliyekuwa anakuja mara baada ya kusikia sauti ya viatu ndipo hakuamini macho yake na kujikuta anaanza upya kudondosha machozi na kulia kwa uchungu sana.

"pole sana baba, hutakiwi kuendelea kulia Mungu mpenzi atakuponya tu mwanangu naomba kuwa na imani wewe ni askari shujaa"
ilikuwa ni sauti ya mzee Mwinchande akimsihi kwa uchungu mwanae mara baada ya kufika pale kwenye kitanda na kum busu kwenye paji la uso huku nae machozi yakimtoka baada ya kuona hali ya mwanae na kutoamini kama kweli bado mzima.
Shebby aliishia kulia pasi na kusema kitu huku akijilaumu tena kichwani kwanini hajawahi kumshirikisha babaake japo kwa ushauri tu juu ya mpango aliokuwa nao hadi akaenda na kujiongoza bila kufata ushauli wa watu wazoefu kama babaake ambae alidumu kazini kwa zaidi ya miaka 30.
Alifumba macho baada ya kitanda kuendelea kusukumwa na kuingizwa kwenye chumba cha upasuaji ambapo kulikuwa na Daktari maalum bingwa wa mifupa wa kujitegemea aliyepigiwa simu kwa swala moja tu la kumtibu Kamishna Shebby.
Daktari huyu bingwa aliaminika sana na Nchi ya Tanzania baada ya kusomea fani ile ya utabibu tokea angali na miaka kumi huko nchini India baada ya kuchukuliwa na wafadhili waliompenda na kwenda kumlea hivyo alichagua somo la utabibu toka angali mtoto na alisomea somo hilo tu hususani vitengo vya mifupa na mishipa na hadi baada ya miaka kumi na tatu alifanikiwa kuwa Daktari kamili na bingwa hasa baada ya kufanya maajabu angali India na hata aliporudi Tanzania nchi ilijivunia lakini ilishindwa kumuajiri baada ya kugomea na kubaki anakodiwa kwa kazi maalum tu na kulipwa pesa nyingi sana kwa kazi moja ya uhakika.
Japo alionekana bado mdogo tofauti na madaktari wengi kuonekana na umli mkubwa lakini anapokuwa katika kazi zake hugeuka na kuwa mkubwa sana kutokana na ufanisi wake na ilikuwa vigumu mno akiwa nje ya ofisi kum baini ama kumtambua kama daktari hasa kutokana na vile alivyo mrembo mpole mwenye umbo namba nane na umli lazima udhani ni sistaduu tu kwani ilionesha wazi hakuzidi miaka thelathini kama si ishirini na nane.
 
EPS 34
========
Baada ya Shebby kuingizwa kwenye kile chumba cha upasuaji walimuacha mwenyewe yule Special Doctor kutokana na kutopenda kufanya kazi moja wakiwa wengi hasa kazi ndogo kama ile aliyoiona kwa Shebby ambae alimeng'enyeka vibaya eneo la goti kutokana na risasi aliyopigwa kule porini.
"Pole sana kaka ila usiogope utakuwa sawa tu na utatembea kama zamani."
aliongea yule dokta na kuupachika mguu wa shebby kwenye mashine maalum mara baada ya kumchoma sindano nne za paja zilizoua mawasiliano yote yanayoweza kumletea maumivu Shebby na kuifanya kazi yake kwa uhuru na umakini bila Shebby kuhisi chochote.

Lakini ajabu kadri alivyokuwa anachangua nyama za shebby na kucheza na mifupa kipindi akimtibu macho yake yaliendelea kutoa machozi na kumhurumia mno tofauti na uhalisia wa daktari anapomtibu mgonjwa.

* * * * * *

Taarifa za tukio lililotokea Mkuyuni lilisambaa kama umeme na siku ya pili yake tu karibu robo tatu ya Nchi na nchi jirani habari zilishafika kutokana na mapaparazi na waandishi wa habari za kina kuthibitisha habari zile juu ya vifo vya utata vya maaskali wapatao kumi na tatu sambamba na majeruhi mmoja ambae alikuwa Kamishna Shaabani aliyejeruhiwa vibaya eneo la mguu.
Kila mtu alisikitishwa na kushangazwa na habari ile na hata waandishi wa habari walipom bana Kamanda mkuu wa jeshi la polisi Tanzania bado hakuwa na majibu yaliyowaingia vizuri na kuwatosheleza waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari na wananchi kwa ujumla na walipozidi kum bana zaidi aliishia kusimamia point yake kuwa 'uchunguzi bado unaendelea'

Taarifa zile sio siri zilichanganya na kuumiza vichwa vya watu wengi sana akiwemo Muheshimiwa Rais ambae ndio kwanza ulikuwa mwaka wake wa sita na wa kwanza katika temu yake ya pili na ya mwisho.
Baada ya kuona kichwa chake kimeumizwa sana na tukio lile Mh Rais aliamua kufanya kikao cha dharula ikulu na kuwaita wakuu wa jeshi la polisi wa kila mkoa sambamba na Kamishna mkuu kabisa akiwemo wazili wa mambo ya ndani na yule wa usalama na kulijadili kwa kina swala lile ambapo kila mtu hakuwa na jibu lililotosheleza na kumridhisha Rais hasa alipouliza juu ya chanzo cha mission ile ilihusu nini na kwanini Kamishna atoke pasi na kumtaarifu yeyote?

Kutokana na ugumu wa maswali kuwaelemea walipata jibu moja tu nalo ni kuongea na Kamishna Shebby mwenyewe baada ya kumaliza shughuli ya upasuaji na kuunga upya mifupa iliyotarajiwa kuchukua siku nne ambapo siku ya tano walitaraji kuwazika kwa heshima askali wote waliofariki kule Mkuyuni na ndipo Muheshimiwa mwenyewe sambamba na Kamanda mkuu wa Jeshi la polisi wakae na Kamishna Shebby na yeye ndie atayewapa ukweli wa kisa chote na hapo ndipo watapata upeo na njia za kutumia pindi watapowatuma wapelelezi wao maalum katika kijiji cha mkuyuni kufanya tafiti na kubaini ukweli wa mambo na chanzo cha tukio lile.

* * * * * *

Naam siku ya siku ilifika ikiwa ni siku nne zimepita tokea litokee tukio lililobaki kuwa hadithi isiyokuja kusahaulika kwa baadhi ya familia waliopoteza wapendwa wao na hususani kituo cha mkuyuni na kijiji chake kwa ujumla bila kusahau idala nzima ya jeshi la polisi, viongozi na wananchi kwa ujumla.
Siku hiyo ndio ilikuwa siku maalum ya kuwaaga wale waliofariki kabla ya kwenda kuwazika sehemu tofauti zilizopendekezwa na wanafamilia wa kila maiti.

Viongozi mbalimbali walihudhulia tukio lile lililofanyika katika viwanja vya leaders wakiongozwa na Mh Rais mwenyewe sambamba na Kamanda mkuu wa jeshi la polisi bila kumsahau Mkuu wa majeshi ya ulinzi ambae alitoa hotuba fupi iliyowafurahisha wananchi wengi wa Tanzania walioguswa na tukio lile hasa pale alipoahidi kushilikiana na jeshi la polisi kuutafuta ukweli wa mambo kama lile tukio lilihusiana na ugaidi ama laa! na jeshi pia la wananchi liko tayari kupeleka vijana wake kusaidiana kumjua muuaji ambae amechafua hali ya hewa na kutishia maisha ya wananchi wa kawaida.
Mbali na hotuba fupi ya Mkuu wa Majeshi (jwtz) na ile ya Kamanda mkuu wa jeshi la polisi lakini kitu chengine kilichowaliza wananchi ni ule wasifu uliokuwa unasomwa wa wale askali hususani urafiki wa Kimaro na Kamishna Shebby ambae yeye pekee ndie alinusurika huku akimpoteza swahiba wake mkubwa aliyejua siri zake nyingi st;sajent Kimaro.
Watu wengi walitamani sana kumuona Kamishna Shebby na kusikia chochote toka kwake ambae nae alikuwepo pale leaders akiwa kwenye kiti maalum cha walemavu akiwa upande ule wa watu maalum huku kulia na kushoto kwake walikaa wazazi wake na nyuma yake alikaa yule Daktari wa kike ambae mzee Mwinchande aliamua kupoteza pesa nyingi zaidi za kumlipa yule binti ili tu amuhudumie zaidi mwanae mpaka pale atapopona.
Hii iliwaaminisha wengi hadi Mh Rais kuwa jinsi gani yule mzee alivyokuwa na uchungu na mapenzi mazito kwa mwanae richa ya serekali kutoa kiasi kikubwa sana cha pesa na kuahidi kuwa kama ikishindikana wampeleke nje ya nchi lakini bado mzee Mwinchande hakuwa nyuma kuhakikisha mwanae anakuwa sawa na kurudi katika hali yake.

Ulifika muda wa Kamishna Shebby kusogea jukwaani na kusema chochote mbele ya umati mkubwa wa wananchi kabla ya shughuli ya kuaga kuanza rasmi ambapo taratibu yule dada alianza kumsogeza kwa kiti kile maalum na waandishi wa habari walikaa sawa sawa kuhakikisha wanachukua vizuri lile tukio na ndipo Shebby alipofika na kukabidhiwa kipaza sauti cha kwanza alitoa miwani ile meusi iliyokuwa imeziba uso wake na wananchi wote waliyashuhudia macho yake yaliyokuwa mekundu mno kutokana na kilio cha muda mrefu lakini mara aliposhika maiki na kuanza kuongea aliushangaza umati na kumstua hadi Mh Rais na kila mtu aliyekuwa pale na kumtumbulia macho wakiwa kama hawajaelewa wala kusikia lile neno licha ya kutumia kipaza sauti kilichosikika kupitia spika kubwa zilizofungwa kila kona za eneo la viwanja.
Aliwatazama watu waliokuwa wamehamaki na ndipo aliporudia tena lilelile neno kuwathibitishia kuwa kile asemacho ndicho alichomaanisha.

"Ni kweli kabisa SIJUI KITU."
aliekea kauli yake msisitizo Kamishna Shebby na kuendelea kulia huku akitazama msururu wa masanduku yenye maiti yaliyowekwa lile eneo maalum la kuagia.
"Wazazi wangu na marafiki leo wamejaribu kunisimulia na kuniuliza nipate kukumbuka kilichotokea lakini bado najihisi huenda si mimi niliyekuwepo huko kwani sikumbuki nini kilitupata jamani sina cha kuongea mimi ni kweli kabisa Sijui Kituu"
aliongezea Kamishna Shebby na kwa msisitizo zaidi na kuendelea kulia tena kwa uchungu sana akiwaangalia watu na kuwathibitishia waamini kwa kwa macho kile asemacho ambapo ilikuwa ngumu sana kwa watu kumuelewa.
"Huyu itakuwa kachanganyikiwa si bure.. eti haelewi kitu? yeye si ndie alikuwa kiongozi huko!!"
alihoji mmoja wa raia aliyehudhulia tukio lile la kuwaaga askali waliokufa Mkuyuni.
Na baada ya hapo ndipo yule daktari alimuondoa kamishan eneo lile taratibu na kumsogeza kwa kuisukuma ile baiskeli maalum ya walemavu mpaka pale kwenye masanduku kufungua muda ule wa kuaga kwani yeye ndie alipewa nafasi ile kuanza kuwaaga wenzake na kila alipofikishwa kwenye sanduku na kuitazama picha kubwa ya marehemu iliyowekwa juu ya sanduku kutokana na miili kutisha haikuweza kufunuliwa na kila alipoiona picha Shebby alijihisi kama anaota na hasa alipoifikia picha ya stlsajent Kimaro hapo ndipo alichanganyikiwa zaidi na kulia kama mtoto.
"KHAA!! Kimaro rafiki angu mpaka wewe? ooh... Mbona sielewi jamaniii aaaagh!!!!"
aligugumia kwa sauti Shebby na kuzidi kuwachanganya watu huku wengine wakithubutu kusema kuwa anafanya kusudi.
"bwana hata kama sijasoma lakini siwezi kuwa mjinga kiasi hiki, hivi toka lini mtu aliepoteza kumbukumbu kweli kabisa na kusahau tukio lote sasa anawakumbuka vipi watu aliokuwa nao? hahahaaa huyu Kamishna si bure kuna kitu tu anaficha na huenda yeye akawa ndie aliyesababisha wenzake kufa.. we fikiria wooote wafe abaki yeye tu!!.. kama nani? Malaika au......"
ilikuwa ni sauti ya dada mmoja mrefu akiwa na sambamba na rafiki zake wakiwa wamesimama pale Leaders ambao nao walikuwa ni miongoni mwa waliohudhulia tukio lile.

Shughuli za uagaji zilimalizika baada ya masaa matatu mbele ambapo misafara a viongozi mbalimbali ilianza kuondoka eneo la viwanja huku gumzo kubwa kwa wananchi na waandishi wa habari likiwa ni kuhusu Kamishna Shebby kusahau kilichowakuta hali ya kuwa yeye pekee alisalimika na ndie aliyepaswa kutoa maelezo yakinifu mbele ya umma.

* * * * * *
 
EPS 35
========

Baada ya miezi mitatu kupita kidogo habari za tukio la Mkuyuni lilianza kupungua midomoni mwa watu lakini bado lilizidi kufukuta vichwa vya baadhi ya viongozi na wakuu wa usalama nchini akiwemo Mh Rais ambae aliamua kuunda tume maalum ya upelelezi yakinifu na kuipandikiza katika lile gereza alilokuwa anafanyia kazi Kamishna Shebby ambae kwa sasa alikuwa na likizo maalum isiyo na muda rasmi kutokana na kuuguza mguu wake.

Mwezi mmoja baada ya ile tume kuundwa na kufanya upelelezi wake wa siri ndani ya gereza ndipo ripoti iliporudi kwa muheshimiwa Rais kama alivyopendekeza na tume ilibaini kuwa Kamishna Shebby alijitumbukiza na kutengeneza ukaribu sana na mfungwa mmoja ambae alikuwa na tabia ya ajabu ya kutamka na kuongea kuwa wanawake ni wauaji.
Tume haikuelewa wala haikupata uhakika ni nini hasa kilichomfanya hadi Kamishna Shaaban kwenda Morogoro na kutokea mauaji yale lakini ilihisi kwa asilimia kubwa kuwa yule mfungwa aliejengewa ukaribu na Kamishna Shebby ndie pekee anaweza kutoa siri yakinifu kuwa nini hasa alichokuwa anatafuta Kamishna Shebby lakini vilevile kunatakiwa itumike mbinu kubwa itayomfanya yule mfungwa kutoboa siri kiurahisi bila kuhisi chochote.
Lakini ilitahadhalisha kuwa na ugumu ndani yake kutokana na tabia ya ukimya wa huyo mfungwa kwa hiyo inahitajika mbinu kubwa na m badala ambayo haitaweza kumstua huyo mfungwa.

Baada ya ile ripoti ndipo Mh Rais aliongea na mkuu wa Majeshi ambae alimshauri kuwa apelekwe kijana mmoja Komandoo ambae alimuhakikishia kuwa ataifanya kazi hiyo kwa siku sitini tu. siku thelattthini ndani ya gereza na siku thelathini ndani ya kijiji cha mkuyuni na baada ya hapo ukweli wote utakuwa mikononi mwao.
"Mh! una hakika anaweza kuifanya kazi hii kwa muda mfupi hivyo?"
"Haswaa muheshimiwa nawajua sana vijana wangu mashupavu na huyu nitamtoa katika moja ya kitengo nyeti sana."
Alimuhakikishia Rais na baada ya makubaliano alipigiwa simu na kuitwa Kamanda mkuu wa jeshi la polisi na kupewa ripoti nzima na kusukwa mpango ambao walikubaliana kuwa apelekwe huyo komandoo gerezani akaifanye hiyo kazi akiwa kama mfungwa kisha baada ya mwezi atolewe kinyemera na apelekwe huko Morogoro Mkuyuni kumalizia ngwe ya pili ya ukweli juu ya kilichowapeleka na kilichowaua wale Askali kwani hadi kipindi hiko mtu waliyetegemea kuwasaidia ambae ndie Kamishna muhusika alikuwa amepoteza kumbukumbu katika mazingira ya ajabu na kushangaza.

* * * * * *

"Dokta Asha hivi kwanini kichwa changu kimekuwa kizito kila nikijaribu kufikiria kilichotokea hadi wenzangu wamekufa nami nimekuwa hivi daah!"
aliuliza Shebby pindi alipokuwa anafanyishwa mazoezi ya kutembea na Special Doctor yule wa kike aliyeitwa Asha pindi walipokuwa kwenye bustani iliyokuwa nyuma ya Jumba la mzee Mwinchande na hii ilikuwa baada ya miezi minne.
"Hapana usikate tamaa naamini utapozidi kupona taratibu na kumbukumbu zako zote zitarudi tu usihofu"
aliongea yule Doctor katika hali ya kumfariji Kamishna Shebby ambae kiukweli alionesha kuumizwa mno na tatizo lake la kupoteza kumbukumbu zote muhimu za kule Mkuyuni hadi azma ya safari yao.
"Lakini si unaona kila mtu aniamini ninavyosema sijui kitu.. Lakini ukweli sijui kitu mimi wala sikumbuki kabisa naona kama ni ndoto tu haya"
alisisitiza Shebby, wakati huo kwa ndani juu ya ghorofa ya numba yao dirishani alionekana mzee Mwinchande sambamba na mkewe wakimuangalia mtoto wao Shaaban alivokuwa anafanyishwa yale mazoezi taratibu na kuwafanya watabasamu na kumshukuru Mungu kwa hatua aliyofikia na kuzidi kuwapa matumaini ya kupona kabisa mtoto wao kipenzi na wa pekee.

** ** **

Ndani ya gereza kubwa alilokuwa anafanyia kazi Kamishna Shaaban lilionekana Basi kubwa lililokuwa limesindikizwa na difenda mbili na kusimama kwenye eneo la kupaki ambapo ulinzi ulikaa sawa pindi walipoanza kushushwa wafungwa wapya walioletwa pale gerezani kuanza kutumikia kifungo chao.
Baadhi ya wafungwa waliokuwa upande wa pili wakitenganishwa na seng'enge mbili sambamba na kuta maalum ya kioo waliacha kwanza shughuli za kufyeka fyeka na kuangalia wafungwa wapya waliokuwa wanashuka kwenye lile basi.

Ilikuwa ni listi ya wafungwa kumi na mbili wapya ambapo walishuka na kupanga mstari huku kamanda maalum wa magereza akipita na kuanza kuwakagua huku akiwauliza majina.
"namba nane.."
"ADORH JUMA"
"Tisa.."
"IDDI JUMBE."
"Kumi.."
"JUMA KOBERO"
"Kumi na moja"
"IBRA RADI"
"Kumi na mbili"
"HHAHAHAHAA.."
"Kumi na Mbilii..?"
"HAHAHAHAHAAAA''
Kilisikika tu kicheko kilichowashangaza askali wote na wafungwa waliokuwa wanamshuhudia kijana mmoja wa makamo mwili mkubwa ambae alikuwa mfungwa mpya aliyekuwa anakamilisha ile listi ya wafungwa wapya kumi na mbili lakini ajabu alipoulizwa jina hakujibu zaidi ya kubaki anacheka tena kwa sayti kubwa hadi yule afande akaanza kughadhibika.
"Kumi na mbiliiiii.."
"HAHAHAHAHAA WANAWAKE NI WAUAJIIII"

Ilisikika sauti hii akijibu yule mfungwa iliyomstua Hussein Babu bubu aliyekuwa anaendelea kufyeka pasi na kuangalia wale wafungwa waliokuwa wanahesabiwa upande wa pili lakini maneno aliyolopoka yule mfungwa mpya namba kumi na mbili yalimfanya aache kila kitu na kusimama kumuangalia huyo mfungwa ni nani aliyenukuu maneno kama anayosemaga yeye na ni kwanini hasa ndipo macho yake yalipokutana na yule kijana aliyekuwa anapigwa mikanda kwa dhalau aliyoonesha pindi alipoulizwa kwa mara ya tatu.

Naam huyo hakuwa mwengine bali ni Komandoo Jumanne au J four ama kwa chata maalum ya utambulisho wa kijeshi kwenye bawa alilochorwa kifuani aliandikwa CJ4 na alifikishwa hapo kwa kazi maalum ambayo zaidi ya mkuu msaidizi wa gereza hakukuwa na Askali yeyote mwengine aliyemtambua wala kubaini ujio wake.
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 36
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________

Hussein bubu aliendelea kumshangaa yule kijana pindi alipokuwa anabisha kutaja jina lake na kung'ang'ana na kusema kuwa wanawake ni wauaji mpaka yule kamanda alipopewa agizo na mkuu msaidizi wa gereza kuwa amuache ndipo alipoachwa na kujumuishwa na wafungwa wenzake kisha kupewa sare zao kabla hawajachanganywa na wenzao ndani ya lile gereza.

Muda wote cj4 alikuwa kimya na mara nyingi alionekana mtu wa mawazo sana hata walipokuwa wanatolewa na kupelekwa kwenye kazi za kuvunja kokoto ambapo Hussein bubu yeye alikuwa kwenye kitengo cha kusambaza maji ya kunywa kwa wafungwa wenzake.
Hali ya mfungwa yule mpya kutopenda kuzungumza na kufanya kazi kwa nguvu huku akionesha ni mtu mwenye mawazo mengi ilianza kumvutia Hussein bubu na kujikuta anaweka ukaribu nae kwa siku tano tu baada ya kuja kwake na Hussein alijifariji moyoni kuwa yule ni mtu pekee anayeweza kukaa nae kwani alihisi yaliyomkuta ni makubwa kama yaliyomkuta yeye.
Lakini kichwani kwa Cj4 alikuwa na nia moja tu ya kutimiza agizo alilopewa na Mkuu wa majeshi lililotoka kwa Amiri jeshi Mkuu mh Rais wa jamhuri a Muungano wa Tanzania.
Ukaribu alioutengeneza kwa mbinu maalum na kumteka Hussein bubu pasi na kutarajia ilikuwa moja ya hatua kubwa aliyoidhamiria Cj4 na taratibu Hussein alianza kufunguka kumpekua Cj4 ili kujua kulikoni kilichompata japo awali Cj4 alionesha ugumu wa kutopenda ukaribu na Hussein lakini baada ya wiki moja aliamua kuwa mpole na kipindi cha mapumziko ama chakula walikaa pamoja na taratibu Cj4 alianza kumsimulia Hussein mkasa wake wa uongo lakini uliomhuzunisha sana Hussein na kujikuta nae anamsimulia mkasa wake mpaka yuko pale na ndipo walipotengeneza urafiki.

"Laiti kungekuwa na askali muelewa na mwenye roho nzuri nadhani angesikia kilio changu na kunisaidia lakini daaah!! nawachukia sana hawa askali wetu wooote wapuuzi na makatili watupu"
alilalama siku moja Cj4 alipokuwa anapata chakula cha jioni sambamba na Hussein bubu.
"Dah! pole mwanangu lakini kumbuka si askali wote wabaya."
alitetea Hussein bubu
"Hapana mzee we kufungwa kote huku na kuteseka kwa kesi usiyoitenda hadi unafikia huko mbona hajatokea hata askali mmoja kujipendekeza walau kiuongo kwa kukuonea huruma ama kukusaidia kivyovyote?? hawa wanyama tuu usiwaamini babu"
alizidi kukazia Cj4 lakini alifanya haya yote kwa makusudi ili kumtia katika kumi na nane zake Hussein pasi na kutambua na kuanza kufunguka ajenda kuu aliyoifata na siku hiyo ilikuwa ni siku ya kumi na mbili tangu afungwe pale na siku tano tangu wawe marafiki.
"Sikia nikwambie mwanangu, mi mwenyewe awali niliamini hivyo na nilikaa kimya zaidi ya miaka ishirini lakini baadae alitokea askali ambae sikuwahi kuwaza hapo awali kama anaweza kuwepo askali mwenye roho ya imani tena mkubwa kama huyo bwana ambae alinihurumia na kufanya kila jitihada za kunisaidia na kuutafuta ukweli wa kesi yangu japo ni ya miaka mingi sana. aaah! usihofu mwanangu wewe kesi yako bado changa sana usijikatie tamaa hivyo naamini kama yule kijana asingepatwa matatizo na angekuwepo nadhani toka siku ile ya kwanza unaingizwa hapa angeshakwita kutaka kujua kilichokusibu na ungestaajabu mwenyewe."
"Mh! siamini mzee kama kuna mtu kama huyo... yaani atake kukusaidia juu ya kesi yakoi ya miaka mingi? angeanzia wapi??"
"Aaagh! baba inabidi uamini tu kwani hiki nikuambiacho si ndoto"
"Mh! basi huenda atakuwa alikuongopea tuu kwa kuwa wewe upo ndani usingejua chochote."
"Naamini asilimia zote hakuwahi kuniongopea kwani hata matatizo yaliyosababisha asiwepo hapa leo hii naamini ni kwasababu yangu asilimia tisini."
aliropoka Hussein na kutupa plate ya chakula na kusogea pembeni huku machozi yakianza kumtoka baada ya kujitonesha kidonda chake makusudi na kuanza kumkumbuka Kamishna Shebby ambae mpaka muda huo hakujua anaendeleaje japo alijua kuwa alinusurika kule kwenye shambulizi Mkuyuni.

* * * * * *

Ukaribu wa Dokta Asha na Kamishna Shebby ulianza kuwavuta katika hisia moja mioyoni mwao japo kila mmoja alibaki akimuonea soni mwenzake hasa Kamishna Shebby.
Hata mzee Mwinchande na mkewe walibaini kitu hiko na walitamani mtoto wao amuoe yule Dokta hasa walivyoona jinsi alivyokuwa anamuhudumia kwa upendo na ilikuwa kawaida halali hadi muda Shebby amelala na kabla Shebby hajaamka ye anakuwa tayari yuko macho.
Yaani kwa jinsi Dokta Asha alivyojituma kumuhudumia Shebby hadi mzee Mwinchande akaona kile kiasi anachomlipa hakitoshi japo ilikuwa ni zaidi ya milioni kumi kwa wiki.
* * *
Siku moja ambapo ilikuwa siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Kamishna Shebby huku wakialikwa watu wachache sana katika hoteli maaalum waliyoikodi kwa niaba ya tafrija ile.
Shebby akiwa bado kumbukumbu zake hazijakaa sawa aliongozwa na Dokta Asha katika kila steji wakati tafrija ilipokuwa inaendelea hadi wakati wa zoezi la kukata keki japo aliweza kusimama bila kutegemea gongo na kutembea mwenyewe lakini bado balance ya mwili ilikuwa haijakaa sawa na ndio sababu Dk, Asha hakuwa mbali nae.
Ki ukweli dk Asha na Kamishna Shaaban walipendezana sana na hata wahudumu wa hoteli walijua kuwa ni wapenzi lakini haikuwa hivyo na kabla Shebby hajamlisha yeyote keki mc alimuomba azungumze chochote kuhusu siku yake ile ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake na ndipo taratibu baada ya kukamata kinasa sauti na kuangalia huku na huko Kamishna Shebby alianza kuzungumza na kila mtu alitulia akimtazama na kumsikiliza kwa umakini.

"Kwa kweli kikubwa namshukuru sana Mungu kwa kunifikisha umli huu japo bado naumia moyoni mwangu kwa kushindwa kukumbuka yaliyonikuta hadi muda huu pia napenda nichukue nafasi hii kumshukuru sana tabibu wangu aliyejitoa kwa hali na mali kuhakikisha nakuwa mzima na kutembea kama zamani ila ningependa pia nimwambie kitu kilicho moyoni mwangu na kila mtu nataka asikie ili nimuaminishe pia nimuhakikishie kuwa hiki ninachoongea kinatoka kweli moyoni mwangu na si vinginevyo..."
alipofika hapa kamishna Shebby alinyamaza kidogo na kumtazama dk Asha aliyeonesha nae kuwa na shauku kubwa ya kusikia hiko kitu ndipo Shebby alipoendelea
"Dokta Asha.. Dokta Asha Nakupenda sana na naomba ukubali niwe wako ili tuunganike na kuwa mke na mume siku za usoni tuzidi kutengeneza ukaribu na kuzalisha familia bora pamoja. Naomba unikubali Asha na kama utanikataa naomba uthibitishe mbele ya wote wanaonisikia sasa hivi humu ndani.
Kwanini niutese moyo wangu kwa kuficha ukweli halisi uliomo? Nakupenda sana dokta Asha nikubali tafadhali.."
Maneno ya Shebby yalimstua kila mtu aliekuwa ukumbini na kufanya watu wote wamgeukie Dokta Asha ambae alijikuta anainamia chini kwa aibu na mshangao kwa kutoamini kama kweli mgonjwa wake ambae hata yeye mwenyewe alishaanza kuwa na hisia nae za uhitaji wa kuwa karibu zaidi lakini hakufikiri wala kuzani kama Shebby angefikia hatua ile ya kutamka maneno yale hadhalani vile.

mzee Mwinchande alitabasamu sambamba na mkewe mara baada ya kumsikia mtoto wao wa pekee akisema yale maneno na kuanza kumpigia makofi kwa ujasiri aliouonesha na kuwafanya na watu wengine taratibu kuanza kumpigia makofi Kamishna Shaaban na hapo ndipo mc alipochombweza kidogo kwa maneno ya bashasha na kupiga wimbo mmoja wa kizungu ulioimbwa na westlife ujulikanao kama Queen of my Heart na hapo ndipo Dokta Asha alipoinuka huku uso wake ukibubujikwa na machozi mepesi ya furaha na kwenda kumkumbatia Kamishna Shebby kwa kuashilia kuwa alikubali kwa moyo mmoja ombi la kamishna Shebby.
Na hivyo ndivyo mapenzi baina ya kamishna Shebby na Dokta Asha yalivyoanza rasmi.

* * * * * *
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 37
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
Cj4 alimsogelea Hussein bubu na kumshika bega
"Pole sana mzee wangu lakini kwanini unaamini kuwa matatizo yaliyompata yamesababishwa na wewe"
aliuliza kwa upole Cj4 na kumfanya Hussein akiuvunja tena mwiko wake aliojiwekea na kuanza kumuhadithia kwa ufupi kilichotokea baina yake na Kamishna Shebby kwa kuamini kuwa yule aliyekuwa anaongea nae ni mfungwa mwenzake aliyeponzwa na mwanamke na kubambikiwa kesi ya kuhuzunisha kama yeye bila kujua sivyo alivyofikiri bali alikuwa anatoboa siri kwa Komandoo aliyeletwa pale kwa kazi hiyo maalum ya kutafuta kilichomsibu kamishna Shebby hadi aende kwenye mission ya siri iliyopelekea vifo vya askali wenzake na kusababisha kupoteza kwake kumbukumbu.
"Kwa hiyo daah! kumbe kuna mtu anajiita mr.X ndie aliyekuwa anamuumiza kichwa huyo Kamishna?"
"We acha tu mwanangu ila nakuomba habari hii usije kuongea na mtu mwengine yeyote kwani sipendi kabisa matatizo mengine yatokee. Sina imani na huyo Mr.X huenda akawa jini ila namuomba Mungu siku moja nije kumuua mimi mwenyewe kwa mikono yangu."
alisisitiza Hussein bubu na muda huo huo firimbi ilipulizwa na muda ulikuwa umeisha wa kupumzika hivyo walinyanyuka na kuendelea na kazi.

Lakini baada ya siku tatu baadae Hussein bubu anastushwa na taarifa za kutoweka kimaajabu kwa mfungwa ambae ndie yule rafiki yake walietokea kuzoeana ghafra.
Hakuzielewa haraka tetesi zile ambazo zilizuka kwa wafungwa wengine ambao walikuwa wamefungwa ukanda mmoja na yule kijana swahiba wa Hussein kutokana na yeye kuwa upande mengine ambao alihamishiwa kipindi cha nyuma kwa msaada wa Kamishna Shebby.
"Kh!! sasa katorokatoroka vipi? au alikuwa jini yule?? "
lilikuwa ni moja ya swali lililomuumiza kichwa Hussein baada ya kuthibitisha kuwa yule kijana hayupo tena ndani ya gereza na kuna timu ya maaskali iliyotumwa kufanya msako juu yake.

* * * * * *

Ndani ya kijiji cha mkuyuni stendi kuu iliyokuwa mkabala na soko alionekana kijana mmoja aliyevaa nguo chakavu akishuka kwenye roli lililotokea mjini na kuja pale mkuyuni kwa ajili ya kupakia ndizi.
Akiwa kabeba fuko lake la rambo na mkononi kashika pingili ya mua aliokuwa anaumenya taratibu kwa mdomo huku akipiga hatua mdogo mdogo kutokea kule kwenye lile roli mara baada ya kuwashukuru wahusika waliokaa mbele akionesha dhahili alibebwa kwa msaada tu, ndipo yule kijana alianza kuchanja mbuga na kuelekea mabondeni akiifata njia moja iliyoelekea ndani kidogo ya maeneo ya soko huku watu wengi aliokuwa anapishana nao walionesha kumshangaa japo hakujua walimshangaa kwa jinsi alivyo au kutokana na ugeni wake pale Mkuyuni.

"Samahani babu shikamoo"
alisalimia yule kijana alipomkuta babu mmoja akiwa kabeba jembe akielekea njia ile aliyokuwa anaenda yeye.
"Asante mzukulu, kugenda kwani?"
aliuliza yule mzee ambae ilionesha kiswahili chake hakikuwa kizuri zaidi aliongeama kwa lugha ya kirugulu ambayo haikumpa tabu sana yule kijana.
"natafuta sehemu mzee nitayoweza kupata chumba cha bei nafuu sana niweze kujisitiri"
"Ng'andaaa mh! tuke huku kwani we mgeni mzukulu?"
"Ndio babu"
"Tapata tuke hakuna ng'anda zimema"
aliongea yule babu na kuongozana na yule kijana hatimae wakafika kwenye kijiji kimoja ambapo kulikuwa na nyumba ambayo ilikuwa kama imetelekezwa kutokana na matukio yaliyowahi kutokea mtaa ule na alionekana mama mmoja aliyerukwa akili (chizi fresh) akiwa pekee anayeishi pale.
"Ahano ng'anda hii mzukulu tuke kwa mjumbe ukamlongele akusaidile utawasa tu mzukulu"
alionesha ile nyumba yule mzee kisha kwenda nae sambamba kwa mjumbe ambae hakuwa mbali na eneo lile na ndie alikuwa kama mmiliki wa haki ya nyumba ile na walipofika mzee alisalimiana na mjumbe kisha kumkabidhi mgeni wake huku akimsisitiza amsaidie.
"sawa kijana karibu, Enhee umetoka wapi, unaitwa nani, na ipi hasa shida yako"
"Mzee mi naitwa Ndonga ni mgeni kabisa nimetokea Kilosa nilipoenda kumtafuta kakangu ambae sikufanikiwa kumpata baada ya kutoka kwetu Kigoma na kumtafuta kwa muda mrefu hadi nikakosa muelekeo pale kilosa ndipo nilipoelekezwa kuwa alihamia hapa mkuyuni sasa naomba unisaidie sehemu ya kulala hata kwa kulipia pesa kidogo kwani uwezo wa kulipia guest sina na ndio nimeelekezwa hapa na yule mzee tafadhali sana mjumbe naomba msaada wako nihifadhi mtoto wako"
aliongea kwa lugha ya upole na unyenyekevu yule kijana na kumfanya mjumbe amtazame huku akifikiria jinsi ya kumsaidia.
"Mh! kijana wanguuuu kiukweli hapa mkuyuni nyumba ni gharama japo unapaona kijijini ila kuna nyumba moja ambayo inaweza kuwa rahisi kuipata kwa kuwa ilikuwa ya marehemu babaangu kabla hajamuuzia mganga furani ambae nae alishafariki, lakini sasa pale kuna matatizo kidogo yalitokea na watu wote waliikimbia ile nyumba kasoro mama mmoja ambae kidogo akili zake hazipo sawa ndio yupo pale. sasa sidhani kama patakufaa ama wewe ulionaje?"
"Mh! mzee wangu yani mi siwezi kubagua sehemu ilimradi nihifadhi ubavu wangu kwa visiku hivi nikiendelea kumtafuta ndugu yangu"
"Sawa sasa itabidi nikuandikishe kisha nikupeleke sehemu yenyewe hapo mbele tu ila naomba uwe muangalifu usije kuthubutu kumghubudhi yule mama japo akili zake hazipo vizuri"
"ondoa shaka kabisa mjumbeee Aaagh! Mungu akubariki sana baba kwa msaada wako"
alishukuru huku akipiga magoti yule kijana na kutoa noti ya shilingi elfu tano iliyochakaa sana kutokana na fundo alilolifunga sehemu za pensi lake alilofunga kwa mkwiji wa kamba ya mti.

Baada ya kuafikiana na mjumbe alipelekwa kwenye ile nyumba iliyokuwa imepooza na kwa nje walimuona yule mama ambae aliwaangalia tu bila kusema kitu na baada ya mjumbe kumuonesha chumba cha kutumia huku akimwambia kuwa kama atakaa wiki moja pasi na kuonana na huyo nduguye itabidi ampeleke kwa mwenyekiti wa serikali ya mtaa ili atambuliwe na ikiwezekana aandikishwe kama mkazi wa eneo lile ili kila mtu aelewe ujio wake.
Baada ya hapo Mjumbe alitoka mule ndani na kumuacha yule kijana akikung'uta mavumbi kwenye kile chumba kilichokuwa na mkeka na kigoda cha miguu mitatu tu.
"Shabbashh Nice Step creat another good Chance"
alijisemea mwenyewe yule kijana na kugonganisha mikono yake huku akiwa na furaha mno moyoni mpaka usoni.
Hakuwa mwengine yule kijana bali ni Komandoo Jumanne ama Cj4.

* * * * * *

Baada ya siku kadhaa kupita tangu kufanyike ile tafrija ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa Kamishan Shaaban na kuanza rasmi mahusiano ya kiuchumba baina yake na Dokta Asha, siku hiyo walionekana wakiwa wawili maeneo ya fukwe huku dereva ambae alikuwa ni mlinzi pia aliyetumwa na jeshi la polisi kwa niaba ya kuchunga usalama wa Kamishna Shebby alikaa sehemu moja ya juu akiwaangalia wapendanao Shebby & Asha wanavyokokotana na kurushiana maji maeneo ya fukwe huku wakiwa na nyuso za furaha.

"Nakupenda sana Asha"
"Hata mimi Shebby tena nilikupenda toka siku ya kwanza nilipokuona"
"Haa acha utani Ashaa"
"Kweliii"
"sasa kwanini hukunambia mapema hadi nimekuanza mimi"
"aaah! si nlikuwa naogopaa!"
"tehtehteheee huyoo"

Basi ilikuwa full upendo maeneo ya fukwe pindi walipokuwa wanataniana na kuchombwezana baina ya Kamishna Shebby na Dokta Asha.
Hata jioni yake waliporudi nyumbani kwenye jengo kubwa la kifahari la mzee Mwinchande bado waliendelea na utani wa hapa na pale mpaka wanaingia kulala ambapo ulikuwa ni usiku wa tatu toka waanze kulala pamoja lakini walilala kindugu ndugu kwanza kutokana na maelezo ya Dk Asha kuwa inahitajika Shebby kujiponesha zaidi na atapokuwa sawa aende kujitambulisha kwao pindi ataporudi na wakioana ndipo watapata uhuru wa kucheza sebene pamoja muda wote hasa nyakati za giza.
ITAENDELEA.
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 38
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
Lakini muda mwingi Kamishna Shebby anapokuwa amesinzia Dk Asha hutumia wakati huo kumuangalia vizuri Shebby na kumpekua sehemu za kichwa huku akimuonea sana huruma hadi muda mwengine machozi yalimtoka bila kujitambua Asha lakini hakuwa na chochote cha kumwambia Shebby zaidi ya kunyamaza na kumsikitikia.

* * * * * *

Asubuhi na mapema ndani ya Kijiji cha Mkuyuni kwenye nyumba ile ile ya mzee Mnyungunyungu ambayo shabaha na mipango ya Cj4 ilienda barabara na kutua sehemu husika kabisa na hesabu zake alizopiga awali ili kubaini kilichowakumba askali na kilichoikumba ile familia zaidi akitafuta ukweli wa huyo mr X.

Alijinyoosha pale ndani na kutoka nje asubuhi na mapema na kuelekea kule kwenye choo ambapo njia yake ilionesha kuwa na majani majani yaliyoashilia kuwa kile choo alichokuwa anaenda yeye hakikutumiwa muda mrefu kidogo.
Alitembea taratibu huku akipiga hesabu nyingi kichwani kutokana na maelezo aliyokuwa nayo juu ya tukio la mtu wa mwisho wa familia ile ambae inasemekana alikutwa amejinyonga ama amenyongwa pindi alipoenda chooni.
Kwa kutumia akili za kijeshi na mbinu hadimu alizokuwa nazo Cj4 alisimama ndani ya kile choo na kuangalia juu ambapo kulikuwa na matawi makubwa ya miti yaliyokatisha na kuvuka kile kipaa cha choo ambacho kilikuwa hakijaezekwa na alitumia dakika tano kutazama vizuri kule juu na kuanza kurudi nyuma huku akivuta taswira na kutengeneza picha kichwani mwake ambapo alianza kuona yule mtu alipoingia pale chooni na aliangalia kwa juu na kuona kamba iliyotengenezwa mtindo wa kitanzi kikubwa ikishushwa taratibu na kumvaa pindi aliposimama na kabla hajafurukuta kitanzi kikapandishwa na kumkaba shingoni.
Alizunguka kwa nyuma ya choo Cj4 harakaharaka huku ile taswira ikiwa bado kichwani mwake na kuangalia upande wa juu na kuona kuwa alilala mtu shupavu na makini aliyevaa nguo maalum na vifaa vya kininja akiwa anaivuta ile kamba kwa kuizungusha kwenye skurul aliyoifunga kwenye tawi ambayo ndio ilishikilia ile kamba maalum aliyomshushia na kumkaba yule bwana aliyekuwa chooni na kupanda juu taratibu huku akiwa anapapatika na kushindwa kutoa sauti kwa jinsi alivyokabwana na pindi alipofikishwa juu kabisa ya lile tawi alikuwa tayari ashakufa na alichofanya yule ninja aliyekuwa anamuona kwa taswira tu kuwa alichomoa skurul baada ya kuivinga kamba yenyewe kisha kumuacha yule mtu akiwa ananing'inia pasi na kumgusa mithili ya mtu aliyejinyonga mwenyewe.

Alizunguka tena Cj4 na kuendelea kuiona taswira kuwa yule Ninja alishuka na alipofika chini akaondoka kabisa eneo lile.
Ndipo akaanza kufata hatua alizohisi moja kwa moja alipita yule muuaji.
Wakati huo Cj4 alikuwa makini mno na akiwa anaendelea kutokomea kabla hajafika mbali alistuka baada ya kusikia mtu akipiga chafya na alipogeuka kumtazama alimuona kwenye kichaka kilichokuwa jirani na ule mti mkubwa na ilionesha wazi yule mtu alikuwa anamtazama kwa muda mrefu tu hasa kwa jinsi nae alivyostuka baada ya kutazamana uso kwa uso na Cj4

"Afadhali mzee nadhani wewe utanisaidia"
aliongea Cj4 na kupiga hatua kumfata yule mtu ambae alikuwa ameshika Mundu (panga la kienyeji) na kifuko kilichokuwa na maembe ambapo alijibainisha pale pembezoni mwa mti mara baada ya kujua kuwa kaonekana pindi alipokuwa anamshangaa yule kijana.
"Mh! mbona sikufahamu baba?"
aliuliza kwa hofu kidogo yule babu ambae alimtazama vizuri Cj4 na kupatwa woga nae wa ghafra hasa alivyomtazama sehemu za kifua na mikono huku uso wake ukionesha ni mtu wa tofauti sana kwa jinsi alivyokuwa bussy muda uliopita kabla hajamstua kwa kupiga chafya.
"Mi mgeni hapa mzee wangu nimeingia jana tu na nimesaidiwa na mjumbe kulala hapa lakini alinambia kuwa wenyewe waliikimbia hii nyumba na watu wengi wanaiogopa sasa ndipo nami nilipokuja chooni kujisaidia moyo umeniripuka na kujikuta nakuwa na woga sana ndio maana nilikuwa naondoka nikajisaidie kule porini."
"Hee! baba basi mi naenda shamba we kajisaidie tu huko hata wanakijiji wengine mbona wanajisaidiaga porini."
aliongea yule mzee na kuanza kuondoka huku moyoni mwake akiwa na hofu bado "
"Samahani lakini babu naomba nisikilize kama utakuwa na uwezo wa kunisaidia"
alisisitiza Cj4 na kumshika mkono yule babu aliyekuwa ameanza kuondoka eneo lile.
"Mwe!! haya nokutegeleza"
alijibu mtindo wa sitaki nataka yule babu na kusimama tena
"Ni hivi babu hebu njuu kwa huku kwanza nataka tuongee kitu muhimu na nitakupa pesa nyingi ili unifichie siri hii babu, ukweli mimi ni Polisi na nimetumwa hapa kupeleleza juu ya kilichotokea hapa juu ya mtu aliyenyongwa siku za nyuma, na nimekuja kuondoa uoga uliotawala eneo hili"
aliongea safari hii kwa sauti ya chini Cj4 na kumfanya yule mzee atulie na kusikiliza kwa umakini huku moyo wake ukifurahi ghafra kwa kujua kumbe yule ni mwanausalama.

Ndipo yule mzee alianza kumfata taratibu kwa kunogewa na story aliyokuwa anahadithiwa na Cj4 huku wakiingia kwa msituni kidogo kukwepa watu wasiwaone pia yule mzee alimuongoza Cj4 hadi maeneo yale yalipowahi kutokea mauaji ya Askali miezi kadhaa iliyopita baada ya kuulizwa kama anapafahamu.
"Mh! baba nakuahidi ambe hajatuona mtu tukiongea,! na eneo hili watu wengi wanaogopa kufika hadi sasa hivi, basi hatojua mtu yeyote habari zako baba Niamini."
aliongea yule babu pindi walipofika eneo lililoshona majani mengi na miti mikubwa.
"Ni kweli mzee, lakini tatizo hata Askali aliyekuja kupeleleza awali alifanya ujinga kwa kumuamini mzee kama wewe na mwishoe akamsaliti na kusababisha Mauaji kwa askali wengine."
Alinena kwa sauti tofauti iliyokuwa serious zaidi Cj4 na kumfanya yule mzee astuke hadi akaangusha kile kifuko chake cha maembe na na kabla hajageuka alistukia kashakamatwa kichwa kwa mikono shupavu ya Cj4 na kuanza kubinywa hadi sehemu za taya zikaanza kupishana na hakuwa na uwezo walau wa kutoa sauti ama kupiga kelele.
"Kawaambie huko uendako kuwa Umekumbana na mstari Mwekundu wa CJ4"
Mara Cj4 aliponena maneno hayo tu palepale alipindua kwa nguvu kichwa cha yule babu na kuivunja shingo yake kisha kumuachia na kudondoka kwenye manyasi ambapo alianza kupapatika pale chini kwa zaidi ya dakika kumi mpaka akatulia na kuaga dunia rasmi.

"Kama na wewe uliekwa na mr.X ufanye uchunguzi wa watu wataokuja kuchunguza hapa basi ajue kuwa mbinu zake zimezeeka"
aliongea Cj4 na kuchukua ile mundu ya yule babu na hapo aliuvinga mkono wake mmoja kwa kile kifuko kilichokuwa na maembe baada ya kumwagika pale chini kisha akatumia mkono ule wenye mfuko wa naironi kukamata sikio la yule babu na kuanza kukata ngozi yote upande wa sikio la kulia sambamba na sikio lenyewe kisha alimgeuza na kufanya vile vile upande wa sikio la lengine na kumuacha.
("sasa na waje tu wakupime pindi watapojua")
aliwaza moyoni Cj4 huku akiifuta futa damu ile mundu kwenye manyasi na kuzishika vizuri zile ngozi zenye vipande vya masikio na kuanza kupiga hatua kadhaa kuelekea kule alipotoka na alipokaribia kwenye ule mti wa awali alisimama na kuchimba kishimo cha futi moja na kuzizika zile ngozi kisha akafukia na kuweka weka nyasi juu yake ambapo ilikuwa vigumu sana mtu kubaini kama sehemu ile imechimbwa.
Alifanya hayo yote ili hata kama wataigundua ile maiti mapema na kuja wachunguzi kupima watachojua ni kuwa amevunjwa shingo tu, lakini hawatapata alama zozote za muhusika aliyemvunja hususani zile za mikono.
Baada ya kuhakikisha mambo safi huku akiwa makini asionekane na mtu yeyote alinyanyuka na kuelekea hadi pale kwenye kile choo kwa uangalifu na kuitumbukiza ile Mundu chooni
lakini alipotoka chooni tu na kufunua kile kigunia kilichofungwa kama mlango alikutana uso kwa uso na mtu akiwa kasimama pale pale mlango wa choo.

* * * * * *
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 39
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
)('nashukuru nimemchunguza ananipenda na kuniamini kweli, usiwe na wasi tena tuko pamoja')(
yalikuwa ni maneno ya ujumbe mfupi wa kwenye simu aliyokuwa anasoma Kamishna Shebby pindi alipostuka usingizini baada ya alert ya simu ya dk Asha iliyokuwa kitandani kuita na alipogeuka na kumtazama Asha alikuwa bado yupo kwenye usingizi mzito japo ilikuwa tayari ni alfajiri ya saa kumi na moja.
Aliichukua simu na kukuta ulikuwa ni ujumbe uliorudishwa baada ya kushindwa kufika kwa mlengwa na kubaki hewani kwa zaidi ya masaa 24 na alipoamua kuufungua kuona alichokuwa ameandika mchumba wake ndipo alipokutana na hayo maneno ambayo hakujua ni nani aliyekuwa ametumiwa na Asha ujumbe huo kutokana na namba husika kutoseviwa jina.
alianza kuipekua simu ya asha na kuangalia charting za meseji za nyuma lakini hakukuta ujumbe wowote zaidi ya ule ambao ulirudishwa na mtandao husika baada ya kushindwa kumfikia mlengwa.
Muda huo huo Asha nae alizinduka na kumshangaa Kamishna Shebby akiwa bussy na simu yake lakini alibaki anamtazama bila kumstua wala kusema lolote na kugeukia tena upande wa pili na kuendelea kulala.
"ukimaliza baby naomba nimtumie message mama"
aliongea kwa sauti ya kivivu Asha na kumfanya Shebby atabasamu baada ya kujua kumbe Asha alishamuona muda mrefu kuwa anapekua simu yake na ndipo Shebby alipoacha upekuzi zaidi baada ya kuona jinsi Dk Asha alivyokuwa hana wasi hata kidogo kwa kuchezea simu yake na kuamini kuwa hakuna tatizo lolote japo awali alichanganywa kidogo na ile message.
"Eeh! baby harafu kuna message yako imerudishwa"
aliongea Shebby huku akimkumbatia kwa nyuma Asha pale alipolala ubavu na kumpitishia simu yake ambapo Asha alipokea na kuitazama message yenyewe.
"Aaaagh! mamaa naee.. mh! mme wangu na wewe hupitwi?"
"kivipi tena honey"
"sasa hii message ulivyoisoma umeelewa nini?"
"hahahaa Asha my love, message umeandika wewe mimi nitaielewaje wakati sijui hata uliyemtumia nani na mlianzia wapi."
"hehehee Hiloo, oteaa sasa.."
"Mh! nimeshindwa kuotea baby hebu nijuze..!"
"heheheee acha wivu bwana huyu mama"
"MAMA!!"
"Hee! sasa unastuka nini huyu mamaangu na niliongea nae jana na kumpa habari za mahusiano yetu na ndipo aliponiuliza kuwa nina hakika unanipenda kweli? lakini nilimuahidi nitamjibu ndipo baadae nilimtumia hii massege, sasa ajabu ipi..!! sema kabla sijakuvunja mguu tehtehteheee"
aliongea huku akiongezea utani Asha na kugeuka upande ule aliolala Shebby na kutazamana usoni na mwishoe wote waliangua kicheko hasa baada ya Asha kuzungusha zungusha macho yake na Kujitunisha mashavu kama mtu aliyetumbukiza kitu kikubwa zaidi ya uwezo wa mdomo wake.
"ha ha hahaa Dokta mzimaaa kumbe muda mwengine kama kitotoooo hahahahaaaa"
"tokaaa hapaaa hiloo mbona we Polisi zimaaa lakini umeshindwa kuluka mto kitandani umekuwa ovyo hata umeshindwa kuramba asali iliyotelekezwa na nyuki kwa kuhofia guu kuoza aahahahahaaaaa"
"Asha ashaa Ashaa Ashaaaa!!!! Ngoja sasa"
aliongea kamishna Shebby baada ya utani wa Asha kumgusa kidogo na kuanza kumchezea chezea maungo yake raini yaliyofichwa na nguo nyepesi alizovaa usiku.
"ha ha ahaa bwanaaaaniniiiiiii..Niacheee basiiii"
aliongea kwa sauti ya kudeka Asha kipindi hiko Shebby alikuwa serious zaidi baada ya Achumani kichwa wazi kuanza kufurukuta na kututumsha bukta aliyovaa akitaka kutoka akasalimiane na mwajuma mficha asali.

Mchezo wao wa kutekenyana na kubimbilishana kitandani ulidumu kwa zaidi ya dakika arobaini kabla ya wote kujikuta wakiwa kama walivyozaliwa na kuanza kurambana rambana taratibu kama vitoto vya mbwa mwitu huku Achumani kichwa wazi wa shebby akizidi kudondosha mate ya uchu wa kuiramba asali ya mwajuma iliyofichwa katikati ya pachupachu ya mapaja ya Dokta Asha na kumfanya Kamishna asahau kama mguu wake mmoja ulikuwa na jeraha pia mifupa bado haikuungana vizuri na hata lile swala kuhusu message aliyoisoma na kumchanganya alfajiri ile alilisahau kabisaaa kuliulizia tena kujua ile namba ilikuwa ya nani?
Zaidi mawazo na akili yote ya Kamishna Shebby ilihamishwa na mautamu yaliyokuwa mbele yake kutoka kwenye mwili laini wenye joto la huba wa Dokta Asha.

Kilichofuata ni miguno ya kimahaba na purukushani za hapa na pale kipindi Kamishna Shebby na Dokta Asha wakivunja amri ya sita mule ndani na kuishi kwenye sayari ya ajabu kwa takribani nusu saa kabla ya kila mmoja kuridhika na kubaki hoi huku wakiwa wamekumbatiana na kuangaliana machoni kama majogoo yaliyotoshana nguvu.
"Aaagh! siamini Asha kumbe bado mtoto kabisa?"
aliongea Shebby na kumpelekea Asha mdomo na kuanza kunyonyana ndimi huku wakifonzana mate kwa hisia kali.
"Nakupenda sana Shebby kumbe na wewe fundi kiasi hiki Mhh! kama Simbaa!!"
aliongea kwa sauti ya kudeka Asha na kumlalia kifuani Kamishna Shebby.

* * * * *
(MKUYUNI)
...............

Alistuka kidogo na kushusha pumzi Cj4 baada ya kumtazama machoni yule mtu na kugundua kumbe alikuwa yule mama mtoto wa marehemu Mnyungunyungu aliyerukwa akili na alipomkazia macho ndipo yule mama alipojichekesha na kuanza kujifunua nguo huku akikimbia na kucheka kwa sauti ya juu.
("Mh! huyu naeeee ok nitajua cha kufanya")
aliwaza moyoni Cj4 wakati akielekea kwenye ile nyhumba na kuingia chumbani kwake kuendelea kurekodi kile alichokuwa anakitafiti.

Mpaka dakika hiyo Cj4 aliweza kujua sababu zilizompeleka Kamishna Shebby pale mkuyuni na alielewa kuwa yule mfungwa Hussein bubu hakuwa na makosa yoyote ila alijua kuwa mchezo ule unachezwa na huyo mtu anayejiita Mr X ambae alikiri moyoni mwake Cj4 kuwa huyo mr X ni mtu anaetumia akili nyingi sana kuliko nguvu na ana wafuasi wengi.
Lakini alitafakari sana mule ndani na kuona jinsi ya kumpata mr X kirahisi ni sawa na hakuna kwani atakuwa anamtafuta mtu kwenye mzunguko asioujua kwani huwezi kumshinda mtu mwenye akili kwa kumtafuta ilihali humjui ila yeye anakujua kama unamtafuta na alibaini kuwa jinsi ya kumtafuta mr X ni kumtafuta pasi na yeye kujua kama anatafutwa na njia aliyoiona ni sahihi ni kumuingiza mr X kwenye mzunguko wa mission yake ili aweze kumtambua pasi na yeye kutambulika.
("Yap thats is a Solution")
alijisemea kimoyo moyo Cj4 na kunyanyuka haraka kuanza kujipachika mwilini vitu vichache muhimu na pale pale alichomoa simu na kupiga kwa mkuu wa Majeshi na kumuelekeza jibu alilolipata kwa siku moja tu baada ya kutua Mkuyuni na Mkuu wa Majeshi aliporidhika alimuamuru kuwa afanye hima arudi makao makuu na yeye ataongea na Muheshimiwa Rais ili wafanye vile alivyopendekeza.
Na ndipo baada ya hapo kwa kutumia mbinu za Kikomandoo Cj4 aliweza kutoweka Mkuyuni baada ya kuwasili na kukaa masaa 24 pekee.
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 40
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
* * * * * *
-(IKULU~DSM)-
.......................

Kikao cha siri kwa dharula kilikuwa kinaendelea ambapo alionekana Mh Rais sambamba na wazili wa ulinzi na mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama bila kumsahau Kamanda mkuu wa jeshi la polisi huku pembeni yake akionekana Jaji mkuu wa taifa.
Mada iliyokuwa inaendelea ni juu ya swala zima lililojiri miezi ya karibuni kule Mkuyuni juu ya shambulio la polisi na kutojulikana sababu na muhusika wa shambulio hilo huku wakiongozwa mjadala ule na ripoti maalum kutoka kwa Komandoo waliyempandikiza kufanya utafiti na kugundua kuwa chanzo cha Kamishna wao kuliingiza jeshi kwenye misukosuko ni kutaka kuujua ukweli wa kesi ya zaidi ya miaka ishirini ya mfungwa mmoja aliyekuwa kwenye gereza lake ili apate kuifufua na kumsaidia baada ya kugundua kuwa alihukumiwa kimakosa na kiuonezi.
Ripoti ya Cj4 ilikiri kuwa ni kweli huyo mfungwa ambae aliitwa Hussein alihukumiwa kimakosa lakini si kimakusudi bali kutokana na mchezo mchafu wa akili nyingi uliokuwa unachezwa na mtu asiyejulikana jina lake halisi wala makazi na wadhfa wake zaidi ya kutumia kivuli cha jina la MR.X
Na iliongezea kuwa mr.X bado yupo na ana mtandao mkubwa na ni vigumu sana kum baini kwa kutuma wapelelezi bali ripoti ilishauri cha kufanya ni kumuingiza Mr X kwenye mtego utaofanya atume wapelelezi na majasusi wake na hapo ndio itakuwa rahisi kumpeleleza na kupambana nae.
Na njia ya kumuingiza mr X kwenye huo mtego ni kumtoa gerezani na kumuacha huru kwa kupitia kipengele cha msamaha wa rais mfungwa Hussein na wafanye jingo itayowawezesha watu wengi wasikie na hiyo itakuwa njia ya mr X kutuma watu wakamuue Hussein ili asiongee mengi zaidi aliyoyajua na hapo ndipo wao watapata nafasi ya kuunasa mtandao wa mr X na mr X mwenyewe kwani watapandikiza ulinzi yakinifu kwa Hussein popote atapokuwa.

"Jaji unasemaje, unakubaliana na hiyo ripoti ya kijana wetu?"
aliuliza muheshimiwa Rais mara baada ya wakuu wote wa jeshi kukubaliana na ripoti ile kasoro Jaji ambae bado alikuwa anafikiria kitu.
"Mh! muheshimiwa ripoti sio mbaya sana ila nilikuwa na wazo japo najua hata nikipingana nayo itakuwa ishapita kutokana na uchache wangu na wingi wenu lakini napenda kupendekeza wazo langu kuwa kwanza tunalazimika kuonana na wastaafu wa kipindi hiko na kuwahoji kwa pamoja hasa wakuu wa usalama kwani naamini kwa akili za huyo mr.X lazima atakuwa alikuwa mmoja wa wakuu wa usalama nchini na si mtu wa kawaida na pengine alipendwa sana na wananchi na alikuwa na sifa hapa nchini ambayo hataki ipotee wala ichafuliwe. kwa hiyo napendekeza wapatikane watu kama wazili wa ulinzi mstaafu wa kipindi hiko, mkuu wa majeshi kwa bahati mbaya hatunae ila yule wa polisi uzuri bado yu hai yupo huko Morogoro."
aliongea Jaji kauli iliyomfanya mh Rais kutikisa kichwa kwa ishara ya kukubali.
"Enheee harafu huyu kamanda wa pilisi namkumbuka vizuri miaka ile si mzee Cyplian kama sikosei... na isitoshe tulikuwa nae katika shughuli ya kuwaaga marehemu siku ile na alinambia kuwa kumbe yule mkuu wa kituo Mkuyuni aliyeuawa alikuwa mwanae."
alidakia kamanda mkuu wa jeshi la polisi
"Basi vizuri Jaji itabidi tufanye hivyo pia ila kwa njia ya kijeshi na usalama zaidi tutayafanya hayo yote kwa pamoja aachiwe huyo mfungwa na kipindi hikpo hiko wastaafu muhimu tutakuwa nao faragha na itakuwa rais zaidi kubaini kama mmoja wao akawa ndie Mr X"
aliongezea mkuu wa Majeshi na baada ya makubaliano hayo kikao kilifungwa.

* * * * * *

Saa zilikatika, siku zilisonga na baada ya wiki kadhaa tena mbele hatimae Kamishna Shebby alipona vizuri mguu wake na kuweza kutembea kwa ufasaha huku mapenzi baina yake na dk Asha yakipamba moto siku hadi siku hali iliyowafurahisha na kuwachochea wazazi wa Shebby kutaka kuona mtoto wao akimuoa kabisa yule daktari wa kipekee.
Hata moyoni mwake dk Asha alizidi kumpenda Kamishna Shebby na kuwa radhi kuolewa nae.

Siku moja majira ya usiku sana ikiwa ndio ilikuwa siku ya mwisho kwa dk Asha kuwepo pale kwenye jumba la mzee Mwinchande baada ya kumaliza shughuli ya kumtibu kijana wake na ilipaswa arejee kwao ili kama taratibu za ndoa zianze kufanywa na ataporejea awe Mke rasmi wa Kamishna Shebby, ndipo usiku huo baada ya Shebby kupitiwa na usingizi Dokta Asha alinyata na kuchomoa pakiti ya sindano kwenye moja ya mabegi yake ya dawa na kuchukua kichupa kimoja kilichokuwa na dawa maalum ya ganzi na usingizi ndani yake na kuichoma kwa kuiingiza ndani ya bomba la sindano kabla ya kumchoma taratibu Shebby ambae alikuwa kalala fofofo na baada ya dakika kadhaa ndipo alipochukua kifaa maalum mithili ya bastora ambapo ndani yake kulikuwa na bomba la sindano kubwa na nyuma sehemu ya kushikia kulikuwa na waya wa umeme ambao aliupeleka mpaka kwenye socket na kuichomeka kisha kuiwasha na kumsogelea kitandani Shebby.
"am so sorry baby kwa kufanya haya bila ya ridhaa yako but it's all about Love"
aliongea mwenyewe Dk Asha na kum busu kwenye paji la uso Shebby ambae tayari alikuwa ndani ya nusu kaputi na ndipo taratibu alikamata lile bomba lililo katika muundo wa bastora na kumpekua Shebby sehemu za kichwani pale alipokuwa anapenda sana kumshika na kupatazama kwa muda mwingi huku akionesha kumuhurumia muda mwengine hadi akawa analia na taratibu aliuelekeza mdomo wa lile bomba na kubonyeza kitufe furani mithili ya kile cha kuruhusu risasi itoke huku akiutuliza kwa umakini mkono wake kwa kuundamiza ule mdomo wa bomba huku akizungusha kijidude kilichokuwa pale ulipoanzia waya ulioelekea kwenye umeme na ndipo mara kwa ndani ya bomba kulianzakuonekana damu zikiingia baada ya kusikika mlio wa 'prruchuu' ndani ya bomba na kuonekana kijisindano kidogo ndani yake kilichotoka kichwani mwa Shebby.
Alichukua pamba na kuibandika pale kichwani mwa Shebby haraka haraka na kuchukua sprit maalum na kuimwagia pindi tu alipotoa lile bomba mfano wa bunduki ili kukata vijidamu vilivyoanza kutoka kupitia kijitobo chembamba kilichosababishwa na ile sindano kubwa iliyotoka ndani yake na kufonza damu sambamba na kile kijisindano kilichotoka kichwani mwa Shebby.

"Ohh! my God, pole sana honey hope now mambo yataanza kurudi nakuwa sawa polepole. Najua hautajua nami sitomwambia mtu honey."
aliendelea kujisemea Dk Asha mithili ya kuwa alikuwa anaongea na Shebby ilihali Shebby hakuweza kusikia wala kuhisi chochote.
Asha alikuwa mtaalam sana kwani aliweza kupakausha na kupashona na vijiuzi maalum vyenye rangi kama ngozi ya binaadam kabla ya kukibandika chengine kwa matilio maalum yaliyoweza kuziba kabisa na kuwa vigumu sana mtu kubaini kama sehemu ile ya kichwa cha Shebby kulikuwa na jeraha lolote.

Baada ya hapo alisafisha vizuri na kukitoa kile kisindano kilichotoka kichwani mwa Shebby kilichokuwa ndani ya bomba na kukitazama kwa umakini kabla ya kukihifadhi kwenye matereo yake na baada ya kuhakikisha kila kitu kipo sawa alimchumu Kamishna Shebby kisha na yeye kulala.

Asubuhi kulipambazuka na kamishna Shebby aliamka kama ilivyoada na kumkuta dk Asha akiwa anajiandaa andaa kuonesha kuwa aliamka muda mwingi
"so baby mi mkataba wangu ndio hivyo tena, sasa kama kupona kwako ndo na mapenzi yameisha tutajua pindi nitapokuwa kwetu"
aliongea na kufanya utani kidogo dk Asha kipindi hiko Shebby alibaki kalala chali pale kitandani akiwa kaegama kwenye mito akimuangalia Asha huku moyo wake ukitamani asiondoke.
Lakini hakukuwa na jinsi ukweli ulibaki kuwa mkataba wa Asha kuendelea kuwapo pale ulikuwa umeisha na ni zaidi ya milioni miamoja sabini ziliingizwa kwenye account yake kwa muda ule mfupi alioutumia kukaa pale kwa mzee Mwinchande na kumuhudumia Kamishna Shebby.
Lilikuwa ni jambo la furaha sana kwa familia nzima mara baada ya Shebby kujiandaa na kutoka sambamba na dk Asha pale kwenye sebule yao kubwa ambapo kulikuwa kumekatwa upande kwa niaba ya vikao vya dharula na kuungana na familia nzima iliyokuwa tayari eneo lile kwa dhumuni la kufanya tafrija fupi ya kumuaga dk Asha na kumshukuru kwa yote aliyofanikisha kuhakikisha Kamishna Shebby anarudi kwenye hali ya kawaida
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 41
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
Tafrija iliongozwa na mzee Mwinchande mwenyewe kwa kutoa maneno ya hekima na nasaha kwa Asha huku akimsisitiza aendelee kuwa na moyo ule wa kipekee na asije kubadilika pindi watapotuma watu kwaajili ya kujitambulisha huko kwao kwani walihitaji kuunganisha undugu na ukaribu kabisa kwa njia ya kuolewa na mtoto wao Kamishna Shebby.
"Nashukuru sana baba nami sitoweza kubadilika kwani ukweli nampenda sana Shebby"
aliongea kwa sauti laini Asha na kuwafanya wote watabasamu na baada ya tafrija kuisha gari maalum aina ya Lange ambayo ilikuwa ni mali ya Dk Asha iliondoka sambamba na escot kutoka kwa kamishna Shebby mpaka maeneo ya jilani kabisa na alipokuwa anaishi Asha ambapo alidai kuwa anaishi na mamaake na isingekuwa vyema Shebby kufika moja kwa moja japo ilijulikana kuwa alikuwa ni mgonjwa wake.
Na hapo ndipo walipoachana Shebby na Asha japo mawasiliano yaliendelea kuwapo huku mawazo yao yakilenga siku ziende haraka ili waoane na kuwa pamoja.

* * * * *

Kwa mara nyengine Cj4 anaonekana akiwa kavaa mavazi ya kipolisi yenye cheo cha Inspector huku akiwa anaendeesha gari aina ya Land cruiser nyeupe ya kipolisi speed kali kwenye barabara ya vumbi na safari yake ilimpeleka hadi mbele ya kituo kikuu cha polisi Mkuyuni ambapo baada ya kushuka alipigiwa saloot na askali aliowazidi cheo mahala pale na moja kwa moja alienda kukutana na mkuu mpya wa kituo na baada ya kusalimiana alijitambulisha.
"Naitwa Inspector Sudy kama ulivyoipata taarifa ya ujio wangu nimekuja kwa nia ya kukutana na baba wa marehemu mkuu wa kituo aliyekutangulia kwa ajili ya kwenda nae makao makuu Dar."
aliongea kwa ukakamavu Cj4 japo ukweli hakuwa askali polisi bali ulikuwa ni mpango wa siri tu uliofanywa na viongozi wakubwa ili iwe rahisi kufanikisha zoezi la kwenda na mzee Cyplian kwa mahojiano maalum ya siri ili wapate kumvumbua huyo Mr.X
"Sawa Inspector basi utaongozana na vijana wachache wataokupeleka mahala anapoishi mzee Cyplian"
alijibu mkuu wa kituo na baada ya hapo amri ilitolewa na ndipo Difender moja iliyowabeba askali watatu iliongoza njia na kufuatiwa na gari ya Cj4 moaka kule ambako alikuwa anaishi baba wa marehemu Ocs John ambae ni mzee Cyplian

Baada ya mwendo wa dakika ishirini waliingia mbele ya nyumba moja ya kifahari licha ya kuwa ilikuwa kijijini mbali na barabara kuu lakini ilitosha kumjuza mpita njia wa eneo lile kuwa mtu aliyejenga pale si mtu wa kipato cha chini.
Mara baada ya gari kusimama na walinzi ambao pia walikuwa ni askali wa jeshi la polisi walifungua geti na kuukaribisha ule ugeni ulioongozwa na inspector fake Cj4 mpaka ndani ya sebule kubwa baada ya kukaribishwa na kuruhusiwa na mzee Cyplian kwa njia ya simu ya upepo pindi askali alipomjuza juu ya ugeni ule na muda mfupi Cj4 alipokuwa ameketi sebuleni mzee Cyplian alianza kushusha ngazi taratibu huku akiwa amevalia suti nadhifu na mkononi mwake akiwa na bluefcase ndogo na kufika pale sebureni.
"Karibu sana kijana, nina taarifa zote za ujio wako na nilikuwa nakusubiri wewe hahahaa karibu sana mwanangu."
aliongea mzee Cyplian na kupeana mikono na Cj4.

Hakukuwa na muda wa Kupoteza zaidi ya Cj4 kuongozana na mzee Cyplian mara baada ya kuagana na familia nzima aliyoikuta pale akiwemo mama mzazi wa marehemu Ocs John na baada ya kutoa pole kwa mara nyengine aliaga na safari ilianza huku akiescotiwa na ile Difender mpaka morogoro mjini ambapo Difender ilirudi Mkuyuni nae kunyoosha tairi kuwahi Dar es Salaam huku kichwani mwake akipiga hesabu juu ya maswali ya kumuuliza yule mzee kabla hawajafika sehemu husika.

* * * * * *

Akiwa amekaa sebuleni akifatilia taarifa ya habari ikiwa ndio wiki yake ya mwisho kuendelea kuwapo nyumbani baada ya kupona vizuri, kamishna Shebby alistushwa na habari iliyokuwa inatangazwa muda huo juu ya wafungwa walioachiwa huru kwa msamaha wa rais huku kivutio kikubwa kikiwa kwa mfungwa mmoja ambae kesi yake ilitikisa miaka mingi naye si mwengine bali ni Hussein Bakari a.k.a babu bubu jina la utani alilopachikwa akiwa huko gerezani.
Macho yalimtoka Shebby baada ya kukumbuka kitu na kujikuta anaropoka kwa sauti ya juu na kumuita babaake aje pale sebureni aone.
"Baabaaa babaaa njoo , Nimekumbukaaa.. Aaagh!! nimekumbukaaa Nimekumbukaaa babaaa"
aliongea kwa furaha Shebby na kuwafanya wazazi wake warudi huku wakiwa na taharuki kwa shangwe na maneno ya mtoto wao.
"Vipi mwanangu?"
"Nimekumbuka baba, kumbukumbu zangu sasa zimerudi aaahhh!"
"Allahu akbaaru Allaaaah akbaaaaar"
alishukuru na kufurahi mzee Mwinchande huku wakikumbatiana na mkewe baada ya kijana wao kuthibitisha kuwa kumbukumbu zake zimerejea sawia.
"Kipi kimekukumbusha mwanangu?"
aliuliza kwa furaha na kutoamini mzee Mwinchande
"Taarifa ya habari, ngoja nimpigie Asha nimwambie nae Mungu amenisaidia nimekumbuka kila kitu sasa sina wasiwasi tena pindi nitapokutana na Kamanda kwa mahojiano aaaaah!!! masikiiini rafiki angu Kimarooo..."
aliongea Shebby lakini mwishoe alijikuta anaanza kulia mara baada ya kumbukumbu zake kumrudisha Mkuyuni na kuliona tukio zima lililojili miezi kadhaa nyuma na zaidi alimkumbuka rafiki ake kipenzi Kimaro na kuanza kulia kwa uchungu sana.
"pole babaa polee ndio uanaume na misukosuko ya kazi zetu hizo pole baba"
alimfariji mwanae mzee Mwinchande huku akimkumbatia wakati huo mamaake alibaki anawatazama huku machozi nae yakimtoka
"Babaa!! inatisha sanaaa, babaaa inaniumaa sanaa lazima nilipe KISASI"
aliongea kwa hisia zenye uchungu sana Shebby lakini babaake alimtuliza na kumsihi asije kuthubutu kufanya hivyo
"chonde chonde mwanangu mi mwenyewe ni askali mzoefu sana nakusihi na kukuomba sana kwa usalama wako futa kabisa hayo mawazo"
"kivipi baba?"
"Kwa sababu ni hatari ya maisha yako hebu fikiria unataka kulipa kisasi je unamjua huyo unaetaka kumlipizia?"
"Nitamtafuta mpaka nimjue sitokubali ni heri nife nikiwa namtafuta hata nitapokutana na wenzangu huko mbinguni watanipokea vizuri kuliko kukaa kimya na kufa bila kufanya kitu wakati mimi ndie niliyewaponza wengine"
alisisitiza Shebby huku akiwa amekasirika mno baada ya kumbukumbu zake kuendelea kumiminika kichwani mwake mithili ya bomba la maji lililokuwa limefungwa muda mrefu na sasa limefunguliwa koki.
"Hee! Shebby mwanangu kumbuka hata ufanyeje huwezi badilisha ukweli kuwa rafiki zako wamekufa na mtu uliyekuwa unamtetea kaachiwa huru sasa iweje bado unang'ang'ania kumtafuta mtu usiyemjua hata jina?"
"Namjua babaa.."
"Unamjua!!!"
"Hee, Nitatumia jina hilohilo analolitangaza mwenyewe na Kifo chake lazima nikishuhudie mbele ya macho yangu."
"Hee basi tulia baba unasema unamjua jina? ndio nani sasa?"
aliuliza mamaake wakati huo babaake alikuwa kataharuki na haamini jinsi mwanae alivyobadilika ghafra namna ile.
"Mama, Baba nawapenda na nawaheshimu sana naomba mnisamehe kwa kubishana nanyi ila niacheni nipambane na huyu mtu anayejiita Mr x."
"MR X!!!?"
"Ehh! Mshenzi mwenyewe anaitwa Mr X"
aliongea Shebby kwa hasira na kuelekea chumbani kwake moja kwa moja huku akijiapiza kulipa kisasi na kumlaani mr X akiwaacha wazazi wake wakiwa wanatazamana wasijue la kufanya au la kumwambia kijana wao.
ITAENDELEA....
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 42
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________

"Pole sana mzee wangu kwa kumpoteza shujaa akiwa bado na umli mdogo vile"
alivunja ukimya Cj4 mara tu walipoanza kukaribia mkoa wa Pwani na kuzifufua hasira za maumivu zilizokuwa kifuani mwa Kamanda mkuu wa Jeshi la polisi mstaafu mzee Cyplia.
"Aaagh! yaani mwanangu unavyosema hivyo unazidi kunitonesha kidonda cha mwanangu John! aaagh! mungu ampumzishe kwa amani."
"Daah! binafsi mzee wangu nimeamua kujikita katika upelelezi wa kujua kilichotokea kwani inasemekana chanzo kabisa ni mfungwa aliyekuwa gereza alilosimamia Kamishna wetu yule mtoto wa kamanda wako msaidizi enzi zenu "
"Aaagh! ndio mtoto wa Mwinchande!"
"eeh, sasa kumbe alikuwa katika mpango wa kumsaidia yule mfungwa baada ya kujua story yake na ukweli halisi wa kesi ulikuwa kule morogoro lakini alipoenda kufanya tafiti na kusaidiana na askali wa kule ndo yakatokea ya kutokea"
"Mh! sasaa kidooogo naanza kupata mwangaza"
aliongea mzee Cyplian na kumfanya Cj4 azidi kutuliza umakini kwani tayari moyoni mwake alishaanza kumuhisi huenda yule mzee akawa ndie Mr X lakini aliamua kuongea vile ili kumpoteza na kujifanya hajamstukia kitu ili iwe rahisi kumteka kimazungumzo
"Mwangaza gani tena mzee wangu"
"Kwa yaliyotokea ila naamini hadithi ya huyo mfungwa ndio funguo ya kumjua muhusika aliyewafanyia unyama wanangu.,,,,"
kauli ya mzee Cyplian ilibeep ubongo wa Cj4 wakati huo tayari walikuwa wanaingia Chalinze lakini mara ghafra kabla mzee Cyplian hajaendelea wala Cj4 hajauliza chochote ghafra walishangaa kuona basi lililokuwa linatokea njia ya Tanga likipitiliza na kuingia mkuku mkuku barabara kuu huku likiwa limewasha taa na kupiga honi mfurulizo kuashilia kuwa aidha dereva limemshinda au limekata breki na kutokana na speed aliyokuwa anakuja nayo Cj4 alijikuta anashindwa kusimama na kuhamia barabara ya pili ili apate kulikwepa lakini bahati haikuwa yake baada ya kukutana na kiuno cha tela la roli lililofunga breki za ghafra kwa kuogopa kulivaa basi lililokosa muelekeo na kusababisha tela kugeuka kuelekea usawa wa gari la kina Cj4 huku kikisikika kishindo kikubwa sambamba na milio ya breki iliyosababisha cheche kuwaka barabarani na kelele za hofu toka kwa wafanya biashara na watu mbalimbali zilizosikika Chalinze nzima.

Hakuna aliyeelewa jinsi gani ile gari ndogo Landcruiser nyeupe iliyokuwa inaendeeshwa na Cj4 ilivyofika fika kule kwenye tawa za umeme tena ikiwa imechakazwa mno sehemu za mbele, na baada ya watu kukimbilia hususani wale wahuni na vibaka mpaka pale ilipokwamia ile gari walimshuhudia mzee mmoja kwa ndani akiwa kabanwa ipasavyo kwenye kiti na bashboard huku ule upande wa dereva kukiwa patupu na ndipo vijana wale wa kihuni walipong'ang'a kuuchomoa mlango mmoja uliojikunja ili wapate kuingia na kuitoa blufkes waliyoiona kwa ndani wakiamini lazima kutakuwa na hela tu.
Lakini kabla hawajafanya hivyo walistushwa na sauti ya mtu akiwaamuru waondoke haraka ikitokea nyuma yao na walipogeuka kutazama walimshuhudia askali mmoja ambae mavazi yake ya juu yalichafuka kwa damu iliyokuwa inaendelea kuvuja kutokea kichwani na ndipo wale wahuni wote walipotimua mbio.
Hakuwa mwengine bali ni Cj4 dereva wa ile gari nyeupe iliyokwamia pale kwenye matawa ya umeme akiwa na jeraha lililokuwa linavujisha damu nyingi huku ikiwa haieleweki alitokajetokaje kutokana na kubondeka vibaya hasa ule upande aliokaa yeye.
Alimuangalia mzee Cyplian na moyo kumuuma zaidi mara baada ya kugundua kuwa alishafariki pale eneo la tukio na hapo hapo kwa speed bila kujali damu zilizokuwa zinamvuja Cj4 alianza kukimbia kuelekea barabara kuu ambapo jumla ya magari sita yalipata ajali iliyosababishwa na lile basi lililopoteza muelekeo ambalo lilianguka na kuseleleka upande wa pili hadi kwenye vibanda vya mama lishe na kusababisha maafa makubwa mara baada ya derva kulazimisha kukata kona licha ya mwendo kasi lililokuwa nao.
Kitu cha kwanza kufanya Cj4 akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa alisimama na kulitazama eneo lile la ajali na kuanza kupiga hesabu alizozijua yeye wakati huo maaskali ndio walikuwa wanawasili eneo lile licha ya kwamba kituo hakikuwa mbali na mahala palipotokea ajali.
(''Hii ni ajali ya Kutengeneza kabisaaa,'')
aliwaza Cj4 na kukimbilia kwenye ile basi na kuvunja kioo cha mbele kwa kupiga teke kali na alibahatika kumchomoa dereva ambae licha ya kwamba hali yake ilikuwa sio nzuri lakini alijitahidi kuzungumza
"Jitahidi kuongea mimi ni askali nimekushika, nambie mara ya mwisho mlisimama wapi kwa ufasaha kabisa"
alionga Cj4 kumuuliza yule dereva ambae alitoa maelekezo kwa shida huku akimwambia kuwa gari iliferi breki baada ya kuhisi waya maalum uliopita kwenye propela ulioshikilia vipira vilivoenda kukamata ringi za taili za mbele kuwa ulikatika ghafra na hakujua chanzo.
maneno yale ya yule dereva yalizidi kumuaminisha Cj4 kuwa ile ajali ilitengenezwa tu sio bure lakini kama imetengenezwa wamefanyafanya vipi hao watu? hapo akakosa jibu ndipo alipotaka kumuuliza tena yule dereva mara askali wengine walifika eneo lile na kuanza kuwatoa majeruhi wa kwenye basi wakishilikiana na wananchi huku naye Cj4 akipigiwa saloot na askali aliowapita cheo na wakimsihi wampeleke nae akatibiwe kwani alikuwa kaumia sana kichwani licha ya kuwa yeye mwenye alijiona yuko sawa.
Na wakati akiwa kasimama akiangalia pilika pilika zilizokuwa zinaendelea za uokozi na wapiga picha eneo lile mara macho yake yaligongana mara mbili na macho ya binti mmoja aliyevalia kiislamu usoni mwake akifichwa na nikabu nyeusi akiyaacha macho tu huku akitembea kwa madaha bila wasi kuelekea sehemu aliyopaki gari yake ndogo lakini kila alivyokuwa anapita alipogeuka macho aliyaelekezea kule kwa Cj4 na kwa ile Landcruide iliyobondeka kwenye Tawa za umeme na hapo hapo aret ya hatari iligonga kichwani na Cj4 na kuhisi yule mwanamke ndie aliyesababisha ile ajali na kuanza kupata ufumbuzi basi huenda mzee Cyplian hakuwa mr.X kama alivyomuhisi awali ila alitia shaka kuwa huenda mzee Cyplian kuna vitu alivijua kuhusu mr X na ndio maana mr X amewatuma vijana wake kufanya ujanja wowote ili mradi wahakikishe mzee Cyplian hatoboi ukweli wala siri yoyote kuhusu mrX.
Lakini akiwa na maswali lukuki Cj4 kila alipomtazama yule bint moyo ulimtuma amzuie tu kwani macho ya yule binti yalionesha wazi kuna kitu anataka ahakikishe kule ilipodondokea ile gari na ndipo alipowaponyoka polisi wenzake na kukimbilia upande wa pili ilipokuwa ile gari ya yule bint ambayo ndio ilikuwa inaondoka taratibu eneo lile lakini kwa bahati mbaya zaidi Cj4 alianza kujisikia kizunguzungu kabla hajafika na kujikuta anadondoka katikati ya barabara ambayo ilikuwa inazungushiwa utepe wa kuzuia magari yasipite upande ule na macho yake yaliishia kuitazama kwa mbali ile gari pindi alipokuwa anadondoka na kupoteza fahamu.

* * * * * *

Akiwa amekaa huku mawazo na hasira juu ya yaliyopita hususani mr X na vifo vya rafiki zake huku akiwazia kukutana na Hussein bubu, ndipo Shebby alistushwa na sauti ya babaake pindi alipokuwa anaongea kwa njia ya simu kwa mshtuko mkubwa na kumfanya atoke na kukimbilia sebuleni aliposimama mzee Mwinchande akiendelea kuongea na simu.
"Vipi baba nini kimetokea?"
aliuliza kwa taharuki Shebby baada ya kuuona uso wa babaake ukionesha kushangazwa na kustushwa na alichokuwa anakisikia
"ajali mwanangu"
"Ajali? nani tena!"
"Mkuu mstaafu wa jeshi la polisi Kamanda Cyplian anasadikika amepata ajali mbaya wakati akiwa njiani kuja Dar"
"Kha!! ilikuwaje sasa, si yule babaake marehemu ocs wa Mkuyuni?"
"haswaaa, yaani aaagh! namkumbuka vizuri alikuwa mkubwa wangu na mtu wa karibu kipindi hiko daah!"
"Daah! shit, amepona?"
"Bado hatujapata hakika"
Baada ya Shebby kuzipata habari zile muda ule ule alichukua simu yake na kumpigia kamanda wa mawasiliano ya idala ya dharula na alipouliza walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na tayari kuna timu ya vijana ilikuwa njiani kuelekea huko.

Aliingia ndani Shebby na kujiandaa kwa kuvaa gwanda zake hali iliyowashangaza wazazi wake na kumuuliza kulikoni lakini alichojibu kiliwashangaza wote.
"Baba najua ni ajali tu imetokea lakini kuonana na mzee Cyplian ni jambo la muhimu sana kwangu ktk njia za kumjua mr X"
alijibu Shebby na kutoka mkuku na kuchukua gari aina ya Jeep na moja kwa moja aliondoka kwa speed maeneo ya kwao mara baada ya mlinzi kufungua geti huku akiwa hataki kusikia chochote toka kwa babaake ala mamaake.

Mwendo aliokuwa anatembea Shebby nimeshindwa hata kuuelezea mara baada ya kupita maeneo ya Kibaha na kutembea upande ambao ulikuwa haumruhusu lakini alifosi hivyohivyo huku akipiga honi mfurulizo lakini ghfra alipokuwa anapandisha kilima cha kuingia Mlandizi almanusura nae apate ajali baada ya kukosana na gari ndogo aina ya toyota creaster uso kwa uso na kusababisha wote wayumbe na yule dereva mweney wa toyota bado kidogo atumbukie mtaroni lakini nae alikuwa mtaalam sana na alifanikiwa kuidhibiti gari na kutulia tena barabarani na kuangalia nyuma kwa kutumia site mirror ambapo aliishuhudia ile Jeep nayo ikiendelea kuambaambaa pembeni ya barabara na kukaa sawa huku speed ikiwa pale pale.
Chaajabu alitabasamu yule dereva badala ya kuchukia na kuendelea kupiga gea na hakuwa mwengine bali ni yule yule binti aliyejiziba uso kwa nikabu ambae Cj4 alimtilia shaka kule Chalinze.
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 43
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
Upande wa Shebby alikuwa nusu mzima nusu kichaa kwani alipoituliza tu gari mwendo ukawa uleule tena utadhani ndio kaambiwa aongeze vile huku akizipita gari kibao zilizokuwa zinaenda polepole kutokana na foreni nae kuweza kupita barabara ya pili akisaidiwa na sare alizovaa hakuweza kusimamishwa na askali yeyote mpaka alipoukaribia msafara uliokuwa unaelekea eneo lilelile la ajali na kufika nao pamoja.

"Wapi mzee Cyplian? wapi mzee Cyplian?!"
aliuliza Shebby mara tu ya kusimamisha gari ambalo wengi walilikwepa kwa jinsi lilivyokuwa linakuja kasi na polisi wa pale wote walishindwa cha kufanya mara baada ya kumuona dereva wake akiwa kawazidi cheo wote waliokuwapo pale.
"Wapi mzee Cyplian"
aliuliza tena Kamishna Shebby safari hii akimfata Seneor Inspector ambae ndie alikuwa mkubwa wa pale kipindi shughuli za uokoaji zikiendelea.
"mkuu ndio sasa ivi ambulance iliyobeba mwili wake imetoka."
"Whaat! ina maana amefariki?"
"Ndio mkuu ila ambulance ile ndio yupo inspector aliyekuwa anamuendeesha nae hali yake si mbaya sana ila amepoteza fahamu"
aliongezea yule s.inspector huku akiionesha kwa kidole ambulance iliyokuwa inatoka na palepale Kamishna Shebby aliingia kwenye gari na kuifatilia ile ambulance mpaka hospital ya Tumbi na pindi ilipopaki alishangaa kuona yule mgonjwa ambae ndie Inspector aliyekuwa anamuendeesha mzee Cyplian akishuka mwenyewe huku akiwa na bandeji kubwa kichwani akiwakataa polisi na madaktari waliomleta pale kuingia hospitali na kuichomoa ile sindano ya dripu aliyowekewa kwenye gari na kuanza kuondoka huku akiwa kama mtu aliyechanganyikiwa lakini anajiamini mno.
Hapo ndipo Shebby aliposhuka na kumfata yule inspector ambae ndie Cj4 huku akiwazuia askali wote waliokuwa wanajaribu kumzuia na kumuingiza hospital na kutokana na ukubwa wa Shebby wote walitii na hapo kwa mara ya kwanza Shebby alionana uso kwa uso na Cj4 huku akiwa hamjui ni nani hasa nae Cj4 alitabasam kuonana na Shebby huku akiwa anajua kila kitu ni nani hasa nyuma ya pazia.

"Nakufahamu wewe ni Kamishna Shebby nilisimama kwenye nafasi yako kuendeleza ulichokiacha, tuwahi haraka Dar kabla hajatoweka."
aliongea Cj4 na kuingia kwenye Jeep huku Shebby akiwa ametumbua macho akiwa haelewi nini anamaanisha yule inspector na imekuaje aongee kwa kujiamini vile ilihali yeye ni mkubwa kuliko yule inspector.
"Twende Kamishna tuiwahi crester iliyombeba muuaji."
Alipoongea maneno haya sasa Shebby alielewa kitu haraka na kuwahi kwenye gari na kuigeuza kwa fujo huku askali na madaktari wote wakishangaa kile kilichokuwa kinaendelea.

Ilikuwa ni ajabu na kweli ndani ya vichwa vya watu kwa kila aliyeiona ile gari jinsi ilivyogeuzwa na kuondoka eneo lile kwa speed ya hatari mithili ya gari ya mashindano huku Cj4 akiufurahia ule mwendo ambao kwake yeye Kamishna Shebby aliona kama vile gari ilikuwa haitembei kabisa.
"Inspector! Umesema ni Creaster nyeupe?"
aliuliza Shebby huku akiwa makini na barabara ambapo aliwasha taa zote full mbali na kuwa haukuwa usiku.
"Yap yap nyoosha mguu nyooshaa"
alijibu Cj4 kwa msititizo na kikatawala kimya baina yao zilibaki kusikika tairi za gari zikilalamika honi mfurulizo na muhemo wa injini tu.

Lakini walipofika maeneo ya Kibamba pale njia panda ya kijiji cha Hakipo walishangaa kuuona moshi mzito umetanda pia waliuona umati wa watu kwa mbali na askali wa usalama barabarani sambamba na gari ya zima moto huku askali moto wakiwa bussy kuzima moto uliokuwa unawaka na kusababisha hali ya hewa pale kuwa na ukungu uliosababishwa na Moshi.
Walisimama na kushuka mkuku mkuku eneo lile na kuwahi kushuhudia kilichotokea wakiwa na wasiwasi isije kuwa ni yuleyule mtu aliyekisiwa na Cj4, na kweli baada ya kushuka na kusogea kuangalia kilichokuwa kinawaka walishangaa kukuta ni gari ndogo na walipoichunguza vizuri ilikuwa ni ileile Toyota Creaster aliyokosa kosa kugongana nayo Shebby na ndio ile aliyopanda yule mwanamke aliyemtilia mashaka Cj4
"Vipi afande ilikuwaje?"
aliuliza Kamishna Shebby kwa mmoja wa askali barabarani (trafic)aliyekuwapo maeneo yale baada ya kupokea heshima yake
"Ni ajabu kidogo mkuu, tulipigiwa simu na raia wema kwamba kuna moto umezuka kutoka kwenye hiyo gari na umekutwa mwili wa mwanamke mmoja ambae inasadikika alikuwa dereva wa hiyo gari akiwa kaungua vibaya mno."
alijibu yule afande na kumfanya Shebby akune kichwa na kushusha pumzi lakini Cj4 alicheka na kumvutia pembeni Kamishna Shebby.
Vitendo vya Cj4 kutomtetemekea wala kueka nidhamu ya uoga kwa Shebby ilizidi kumshangaza Shebby na kujiuliza huyu ni askali gani mwenye cheo kidogo kuliko yeye lakini haoneshi kuogopa wala kumnyenyekea mkubwa wake na kufikia hadi hatua ya kumshika mkono na kumvutia pembeni? lakini alijikuta anashindwa kumkatalia wala kumuuliza na kukubali kusogea nae pembeni.
"Vipi inspector?"
aliuliza Shebby kwa taharuki mara baada ya kuvutiwa pembeni na Cj4 wakati yeye alikuwa bado anahoji kilichotokea.
"Tushamkosa, kashatuzidi akili"
"Kivipi?"
"Huyu mwanamke muuaji"
"Muuaji, lakini mbona na yeye amekufa! hapa lazima kutakuwa na mtu aliyemuua"
aliongea Shebby kauli iliyopingwa na Cj4
"Hapana Kamishna, huyu mwanamke ni special Killer na anajua kupoteza ushahidi. nina imani yule aliyeungua si yeye"
aliongea Cj4 na kumfanya Shebby abaki na taharuki akishangaa maneno ya Cj4, na kuanza kuhisi huenda huyu si askali wa kawaida.
"Sikia Shebby, washa chombo twenzetu turudi taratibu eneo la tukio ukaniache hapa hakuna kitachoweza kutusaidia ila maswali yote unayojiuliza nitakujibu tukiwa njiani"
aliongea Cj4 na kumfanya Sheby awe mpole na kuingia kwenye Jeep na kuanza kuendeesha kuelekea walipotoka huku akiwa anajiuliza mara mbili mbili kuhusu inspector wake ambae licha ya kuwa ameumia sehemu za kichwa na hata ile bandage aliyofungwa kwenye ambulance ilianza tena kuvujisha damu lakini hakuonekana kujali.
"Enhee, kwanini Inspector unalazimisha turudi tena eneo la tukio?"
"Kule ndipo tutapata uelekeo wa sababu za ajali na alipotokea muuaji aliyetuzidi akili."
"Kivipi sasa katuzidi akili?"
"Si umeona katengeneza kifo fake!!"
"Kifo fake? kwa hiyo unataka kusema yule aliyeungua si muhusika?"
"Ndio maana yake ni kamchezo kadogo sana, nahisi kumbukumbu zako zimerudi unakumbuka nini kuhusu Mkuyuni?"
alijibu Cj4 na kumuunganishia swali Kamishna Shebby lililofanya amtazame na kuamua kumjibu kiunagaubaga
"Mkuyuni nakumbuka vifo tu"
"Nina mashaka na muuaji wa Mkuyuni anaweza kuwa yuleyule mwanamke aliyesababisha ajali"
aliongea Cj4 maneno yaliyomfanya Kamishna Shebby kufunga breki za ghafra za gari na kupaki pembeni huku akimuangalia kwa mshangao Inspector wake.
"Unasema??"
aliuliza Shebby mithili ya mtu aliekuwa na matatizo ya masikio mara baada ya kusimamisha gari.
 
EPS 44
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
"Nina wasiwasi na yule mwanamke aliyesababisha ajali ndie aliyewashambulia Mkuyuni."
"Khaaa! wewe ni Inspector kweliiiii ama umevaa sare tu?"
aliuliza Shebby akionesha kuanza kuwa na wasiwasi na Cj4 kutokana na maneno yake kugusa mulemule
"Hapana mimi ni Inspector kwa sasa... Naitwa Inspector Sudy kama ilivyoandikwa"
alijibu Cj4 na kumshangaza sana Shebby
"Sawa Inspetor hata mimi naanza kukubaliana na wewe kuwa ule mwanamke ndie aliyetushambulia Mkuyuni"
aliongea Shebby na kumfanya Cj4 amuangalie kwa umakini na ndipo Shebby alipozidi kufunguka
"Nilimshuhudia muuaji wa Mkuyuni kabla hajanipiga risasi ya mguu, alikuwa ni Ninja wa kike ila kwa bahati mbaya nilimjua kwa sauti tu na muonekano lakini sikubahatika kuona walau macho yake yalivyo kutokana na miwani aliyovaa"
"So, unadhani kwanini alikuacha? wakati wenzako wote aliwaua?"
aliuliza Cj4
"Mh! kwakweli hata mimi sikudhani kama angeniacha ila nakumbuka alichosema kuwa eti nina bahati na kunipa agizo toka kwa mr X kwamba nisije kuthubutu kumtafuta tena mr X kwa usalama wangu. Lakini pia kuna kauli alinambia ambayo ilinichanganya sana hadi sasa"
"Ipi hiyo?"
"Alinambia iwapo nataka kupambana na Mr X basi inatakiwa nianze kufanya mazoezi ya kusimama juani na kupambana na kivuli changu mpaka nikikamate"
"Aaaahaa sasa naanza kupata taswira"
aliongea Cj4 huku akifikiria kitu na kumshangaza zaidi Kamishna Shebby.
"Taswira gani tena Inspector!"
"Juu ya mr X"
"kivipi?"
"Nina wasiwasi mr X ni mtu aliye katika mzunguko wa maisha yako ya kila siku."
"Mhh! mbona sikuelewi unamaanisha nini?"
"Namaanisha mr X ni mtu anayekujua vizuri na inawezekana nawe ukawa unamjua pia, na anapatikana katika sehemu kuu tatu"
"Mbona sikuelewi wee Inspector? ni sehemu gani hizo?!"
"Usipanic Shebby, nina wasiwasi mkubwa kuwa mr X ni mtu anayepatikana katika mzunguko wa maisha yako ya kila siku yaani kazini, serikalini ama nyumbani."
"Nyumbani?"
"Yap, huenda akawa na ukaribu hata na babaako mzazi, au huenda akawa moja ya wakuu wako wa kazi ama kiongozi mkubwa serikalini aidha mstaafu ama bado yupo madarakani"
maneno ya Cj4 yalizidi kumchanganya kabisa Shebby na kabla hajauliza tena lolote ndipo Cj4 alianza kufungua vifungo vya shati ya sare ya kipolisi aliyovaa na kuisogeza pembeni vest yake na kumuonesha eneo la kifua Shebby ambae macho yalimtoka baada ya kuona mchoro wa bawa na alama za Komandoo wa Jeshi.

"Usistuke nimeingia kwenye hii kazi kwa msaada wa kupoteza kwako fahamu, mimi si polisi ila kama unataka kazi hii ifanikiwe na tumgundue huyu mshenzi mdogo inatakiwa asijue mtu yeyote kama kumbukumbu zako zimerudi"
aliongea tena Cj4 huku akifunga vifungo vya shati yake na wakati huo wote Shebby bado alikuwa katumbua macho akiwa haamini kuwa kumbe yule aliyekuwa anazunguka na kuzungumza nae muda wote ni Komandoo wa heshi!!
"Zingatia Kamishna kwa usalama wako na urahisi wa kazi hii. take care twenzetu tukapate mchoro eneo la tukio lakini kumbuka hii tunajua mimi na wewe"
aliongea tena Cj4 na ndipo Kamishna Shebby alipoanza kuondoa gari huku akiitika kwa kichwa akiwa bado haamini kilichokuwa kinaendelea hadi serekali wampandikize Komandoo katika kazi ile.

* * *

Baada ya Kamishna Shebby na Cj4 kufika tena Chalinze eneo la tukio na kufanya utafiti wa siri walioujua wao kabla ya Cj4 kukubali kujishusha na kuingizwa tena kwenye ambulance ambayo ilitokea ikulu pasi na mtu yeyote kujua na madaktari waliokuwa mule karibu wote walikuwa ni wanajeshi lakini walifanya hayo kwa agizo la mkuu wa majeshi kuwa wao ndio waondoke na yule dereva wa marehemu mzee Cyplian kwa lengo la kuwazubaisha hadi polisi wengine wasijue nini kinaendelea kwani isingekuwa vyema Cj4 kutibiwa na raia ama polisi wa kawaida.

Baada ya Kamishna Shebby kuondoka eneo la tukio huku akiwasiliana na baadhi ya wakubwa zake akijifanya bado kumbukumbu zake hazijarudi kama alivyoagizwa na Cj4 alifika nyumbani huku kichwa kikiwa kinamuwaka moto akiyakumbuka maneno ya Cj4 na kuona kweli mr X anatumia akili nyingi sana na inawezekana kabisa yupo katika mzunguko wa maisha yake ya kila siku.
('Mh! sasa itakuwa nani? au mh Wazili? mhh sidhani.. au Kamanda mkuu anatuzunguka? Mh! !!')
aliwaza Shebby usiku pindi alipokuwa ndani lakini mara akiwa katika mawazo mazito alipokea ujumbe wa sms kutoka kwa Dk Asha ambae alikuwa mchumbaake akimlaumu kwa kupata riport kuwa alielekea eneo la ajali iliyotokea mchana huo mbali ya kuwa bado likizo yake ilikuwa haijaisha.
Alitabasamu na kuendelea kuchart na baby wake Asha japo ukweli moyoni alikuwa na mawazo mengine kabisa.

* * * * *

Siku kadhaa zilisonga huku ukweli wa chanzo cha ajali ya Chalinze ukibaki kuwa wa kubahatisha na hata kile kikao cha siri alichopanga mh Rais kifanyike kiliahilishwa kwanza na kuupisha msiba uliozuka ghafra wa Kamanda mkuu mstaafu wa jeshi la polisi mzee Cyplian na kuzidi kuwachanganya wakubwa wa serikali washindwe kuthibitisha moja kwa moja juu ya ajali ile ilikuwa imetengenezwa ama laah.
Hii hata mkuu wa Majeshi ilianza kumpa wasiwasi mara baada ya kupokea ripoti toka kwa Komandoo waliyemchomeka na kumwambia kuwa ajali ile ilisababishwa na watu wa mr X so, ni lazima kwenye kikao cha siri walichofanya kutakuwa na spy anayevujisha siri kwa mr X ama mr X mwenyewe anaweza kuwamo kwenye vikao vyao.
Na ripoti hii ilifikishwa kwa mh Rais tu na kukubaliana na ushauli wa mkuu wa majeshi kuwa haina haja ya kutangaza tena ile ripoti wala kueka tena kikao huku akimuahidi kuwa kijana wake shupavu ataifanya hiyo kazi na mr X atakuja kuletwa mbele ya macho yake siku moja.

Kamishna Shebby alirudi rasmi kazini huku akiigiza bado kumbukumbu zake hazijarudi na kuwashangaza tena wazazi wake ambao awali walikuwa na uhakika kuwa mtoto wao kumbukumbu zimerudi.
Hali hii ilimliza sana mamaake Shebby na kumuombea kila siku alipokuwa anasali akiwa haelewi inakuaje mtoto wao mara kumbukumbu zirudi mara zipotee tena?
Hata mzee Mwinchande hii ilimshangaza sana lakini ukweli ulibaki katika moyo wa Shebby na Cj4 huku wakiendeleza mission yao ya siri ya kumnasa mr.X pasi na mtu yeyote kujua.

* * * *

Ilikuwa ndio siku rasmi ya kutoka kwenye makazi ambayo hakutegemea kama angetoka tena mara baada ya msamaha wake kutangazwa na kupitishwa wiki chache zilizopita na Mh Rais wa Tanzania.
Geti kubwa lile la mwisho lilifunguliwa kwa mitambo ya umeme na oparator aliyekuwa kwenye
ITAENDELEA...
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 45
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
moja ya jengo la usalama wa gereza lile na mwanga wa nje ukaanza kummulika Hussein babu bubu huku akiwa haamini kama kweli leo hii anakuwa huru kwa mara nyengine japo alikuwa hajui wapi aelekee kwani wenzake wote waliotangazwa kuachiwa walipokelewa na ndugu jamaa na marafiki kadha wa kadha waliokusanyana nje ya geti la gereza kuwasubiri isipokuwa yeye tu.
Akiwa kava nguo mpya alizonunuliwa na serikali huku mkononi kabeba kijibegi kidogo chenye nguo za kubadilisha na shuka ikiwa ndio vitu pekee alivyoambulia kama msaada kutoka serikalini juu ya maisha yake mapya anayoenda kuyaanza huko uraiani.
Alimshukuru mungu na kuanza kupiga hatua mdogo mdogo akiifata barabara ndogo ya lami iliyoenda kukutana na barabara kubwa katika njia panda ambapo kulikuwa na stendi ya daladala japo hakujua hata akifika hapo stendi atapanda gari ya wapi ama atafikia wapi na mfukoni alikuwa na kiasi cha shilingi elfu tano aliyorudishiwa ikiwa ni pesa aliyokutwa nayo kipindi anakamatwa miaka iliyopita ambayo kwa kipindi hiko ilikuwa haina thamani kabisa ya kumsaidia mtu walau siku tatu.
Lakini akiwa anaendelea kupiga hatua huku kichwa akiwa kakiinamisha chini akienda huku anatafakari mara alisikia muungurumo wa gari ikitokea nyuma yake upande ule wa gereza na kuchapukia pembeni kwa kuipisha lakini alishangaa ile gari ikisimama karibu yake na kushushwa kioo na mara sauti ya mtu ambae alikuwa dereva wa ile gari ilisikika akimwita na aliposogea kuchungulia hakuamini kuona ni Kamishna Shaaban na ndipo alipoingia garini akiwa haamini kama amekutana tena na kijana aliyetokea kumuhusudu kupita binaadam yeyote tangia aanze maisha ya jera.
"Kamishna baba!! aah, siamini mwanangu kumbe umerudi"
aliongea huku chozi la furaha likimdondoka Hussein babu kwa kutoamini kabisa hasa mara baada ya Shebby kuvua miwani meusi aliyovaa na kofia.
"Nimerudi baba nakaribia wiki sasa, hongera sana kwa kupata uhuru hatimae unarejea uraiani"
alijibu Shebby kwa furaha ya kukutana tena na Hussein
"Ahsante mwanangu leo hii nimekumbuka sana maneno yako pindi nilipokuwa natoka rasmi pale getini daah! mwanangu pole sana kwa matatizo.. Naomba unisamehe sana"
aliongea Hussein huku akiendelea kufuta machozi yaliyokuwa yanatililika mashavuni mwake ghafa kila alivyokuwa anamuangalia Kamishna Shebby
"Hapana baba, hupaswi kuniomba msamaha kwani ile ilikuwa ni moja ya kazi. Usijali babaangu kwakuwa leo hii upo huru hata moyo wangu umefurahi sana najua kazi niliyobakiza ni moja tu"
"Kazi gani tena baba"
"Nataka kumjua huyo mr X nilipe kisasi"
"Haa! sasa kisasi cha nini tena mwanangu wakati mi nishakuwa huru! isitoshe naomba swala hilo niachie kwani mi mwenyewe nataka nilipe kisasi kwa mr.X nishasali sana miaka yote nikiwa jera kumuomba Mungu anitendee muujiza siku moja nitoke jera na nikamuue mr X kwa mikono yangu na mpaka sasa naona Mungu kashaanza kunijibu dua zangu. Futa mawazo ya mr X mwanangu sitaki nikuponze tena hii ni kazi yangu sasa ni zamu yangu"
aliongea Hussein babu kwa hisia kali na safari hii machozi yaliacha kumtoka huku akimuangalia kwa umakini Shebby ambae sasa alianza kuiondoa gari taratibu na kuelekea kule alipokuwa anaelekea Hussein na alipoifikia ile barabara kuu alikunja upande unaoenda kutokea Kongowe.
"hahaha, hapana baba si rahisi kama unavyofikiria lakini pia sifanyi kwa sababu ya wewe tu bali nafanya kwa sababu ya rafiki zangu wote waliokufa"
alijibu Shebby huku akizidi kuongeza mwendo wa gari
"Mwanangu nakuomba chondechonde mi sina ubora wowote niliobakisha wala thamani hapa duniani hivyo hata kama kumuua kwa kumpiga nisipoweza, niko tayari hata nijilipue tufe wote lakini si wewe kurudi tena kwenye matatizo baba nakuomba"
alisisitiza Hussein lakini Shebby hakuonesha kujali sana zaidi ya kuongeza mwendo mpaka walipoipita Kongowe na kuanza kuufata muelekeo wa mbagara na walipofika Mbagala Zakiem aliingiza gari kwenye parking ya hoteli moja mpya ya kisasa iliyokuwa pale Zakiem na kumuomba Hussein waongozane kuingia kwenye ile hoteli na kumshangaza sana Hussein mara baada ya kushuhudia Kamishna Shebby akimlipia chumba na bili ya chakula cha wiki nzima pale hotelini.
"Usijali baba utakaa hapa kwa wiki moja kipindi nikikutafutia makazi rasmi ya kuishi usiwe na wasiwasi simu hii utatumia kwa mawasiliano endapo kutatokea tatizo, line yake imeunganishwa na kifurushi cha wiki na ina namba mbili tu zilizoseviwa na zote ni za kwangu.. Kuwa na amani baba"
Ni maneno ya Shebby pindi walipoingia kwenye chumba cha hoteli kilichokuwa ghorofa ya pili ambapo Hussein alibaki kataharuki tu akiwa haamini moyo wa yule kamishna na vile anavyojitolea kiasi kile kumsaidia ilihali hawana undugu wowote.
"Mi nahitajika kuwahi tena gerezani baba, ila hii Elfu hamsini itakusaidia kwa matumizi madogo madogo na ya dharula"
"Asante babaaa.. aaaah Asante sana mwanangu Mungu akuzidishieeee eeeh!! Akulinde na kila shari jamaniiii Asante babaaa"
alishukuru hadi akapiga magoti Hussein lakini Shebby alimuinua na kumsihi asijali kabisa kisha aliagana nae na kutoka hadi ilipopaki gari yake.
["Hallow, yah Cj4 kazi kwako sasa tayari nishafanikisha yupo chumba namba 90 ghorofa ya pili"]
yalikuwa ni maneno ya Shebby kwa njia ya simu akiongea na Cj4 mara baada ya kuingia ndani ya gari yake na kuanza kugeuza kuondoka maeneo yale.

Ulikuwa ni mchezo wa akili nyingi waliokuwa wanaufanya Kamishna Shebby na Cj4 na muungano wao hakukuwa na mtu mwengine yeyote aliyekuwa anaujua, na kumbe Cj4 alikuwa na jukumu la kuchunga usalama wa Hussein babu na kumfatilia pale kwenye ile hoteli ama ikitokea ametoka ama kama kuna mtu yeyote atayekuja kuufatilia uwepo wake pale basi atashughulika nae.
Naam na huo ulikuwa ni ulinzi na usalama mkubwa uliomzunguka Hussein pasi na yeye mwenyewe kujua hadi atapojulikana mr X ni nani.

* * * * * *

[["Mwanangu vipi kuhusu yule binti naona siku zinaenda na wewe uko bussy sana wala huoneshi kujali kama awali, ooohoo angalia wasije kuwahi wenzako!"]
["Daah, baba bwana... Mbona siku bado ila nitajitahidi basi wiki hii nimtafute mshenga tuandike barua ipelekwe au unasemaje baba"]
[["Akaah mimi sio muoaji shauri yako mwanangu ila kumbuka alivyokusaidia yule binti..!"
["Nakumbuka baba"]
[["Basi ufanye hima kama utashindwa kumtafuta huyo mshenga basi itabidi uje huku tukutafutie"]]
["sawa baba"]
Yalikuwa ni maongezi kwa njia ya simu baina ya Kamishna Shebby pindi alipokuwa ndani ya ofisi yake pale gerezani akizungumza na babaake ambae ni mzee Mwinchande aliyekuwa nyumbani muda huo na kumkumbushia swala la kumuoa Dk Asha.
Ukweli jambo la mr X ndilo lililomchanganya sana Shebby na kusahau jambo la ndoa kwa wakati huo huku akiumia kila alipokumbuka vifo vya askali wenzake na kuzidi kupata motisha ya kumtafuta mr X.

Kesho yake majira ya asubuhi na mapema Kamishna Shebby mara baada ya kufanya mawasiliano ya siri na Cj4 kama ilivyokuwa kawaida na taratibu yao waliyojiekea na kupeana riport zote muhimu walizozibaini katika mikakati yao ya siri juu ya mr X, ndipo Shebby alipomuelekeza Cj4 kuwa ataelekea huko hotelini kukutana tena na Hussein akitaka ampe kazi itayofanya awe anatoka mara baada ya kusikia kuwa tokea siku alipomuacha hajatoka kwenda popote kutembea wala hakukuonekana dariri za mtu yeyote kutaka habari zake wala wale maspy wa mr X.

ITAENDELEA..
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 46
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________
______________
Na kweli majira ya saa nne asubuhi Shebby aliwasili pale hotelini na kukutana na Hussein bubu.
"Karibu baba karibu sana"
alikaribisha Hussein akiwa mwenye furaha pindi alipofungua mlango na kumkuta aliyemgongea kuwa ni Kamishna Shebby
"Ahsante sana baba"
alijibu Shebby na kuingia ndani.
"sasa baba ilikuwa nije kesho lakini nimekuja leo kwa sababu frani zitazofanya nikuongezee muda wa kuendelea kuwepo hapa lakini nilikuwa naomba unisaidie jambo moja"
"Usijali baba, usijali kabisa nakusikiliza na kabla hujasema naamini niko tayari kama litakuwa ndani ya uwezo wangu"
alijibu na kukaa vizuri Hussein huku akimuangalia na kumsikiliza Kamishna Shebby kwa umakini mkubwa.
"Sawa mzee wangu, ni hivi... Kipindi nilipokuwa nauguza jeraha la mguu nilitokea kupendana na binti ambae ndie alikuwa daktari wangu alienisaidia kwa kiasi kikubwa sana hadi nikafikia hatua hii ya kuwa kama awali..."
"Ndio baba endelea"
"Sasaa, nilimuahidi kuwa nitafanya mpango wa kujitambulisha kwao ili tufanye taratibu za kufunga ndoa na kuwa mke na mume.... sasa Shida yangu baba nakuomba wewe uwe mshenga wangu unisaidie kuandika barua ya posa nikupeleke hadi nyumbani kwao na wewe ndie utayeingia na kunitambulisha sambamba na barua."
"Mh! mwanangu lakini mbali na kukutibu tu umechunguza tabia yake kiumakini?"
"Kwa hilo baba sina shaka"
"Haya mwanangu mimi kwako sina pingamizi kwa hilo, fanya tuiandike hiyo barua na hata leo hii ukitaka unipeleke niko tayari kwa hilo kwa moyo mmoja ila nasaha zangu kwako ziko palepale usiwaamini wanawake wala usiwachukie kumbuka kuwa Wanawake ni Wauaji"
aliongea Hussein na kumfanya Shebby atabasamu na ndipo alipotoka na kurejea tena akiwa na bahasha sambamba na karatasi na kwa msaada wa Hussein wakaanza kuiandika barua.

* * * * * *

"Mamaaa, mamaa, mama kaa tayari tayari leo usitoke kwenda popote"
"Kivipi Asha mwanangu mbona ratiba zako sizielewi!"
"mama bwana, ni hivi... yule mchumba niliekwambia barua yake inakuja leo"
"Hee, ni wewe kweliii Asha au mwengineee"
"Ni mimi mama mbona huamini!?"
"Mh! unajua toka uliponambia siku ile nilichukulia mzaha kwa itikadi zako za kutojichanganya na watu, sasa sijui imekuwaje kuwaje hadi ulikubali kuacha shughuli zako na kumtibu mgonjwa yule tena ukidiliki kukaa kwao kwa zaidi ya miezi miwili na kama haitoshi unarudi na kuniambia ndio mchumbaako? au mlikuwa mnafahamiana muda mrefuu!!!"
"hahaha hapana mama ni mapenzi tu, basi si unajua wewe ndie mama na wewe ndie baba. Ikija barua ijibu malizana nao bhaasi ahhaha"
"Hahahaaa haayaa mwanangu nimekuelewa"
Yalikuwa ni mazungumzo ya dk Asha akiwa na mamaake ndani ya nyumba moja ya kifahari ambayo walikuwa wanaishi wao wawili tu yaani mama na mwana.
Haikujulikana kama yule mama alikuwa na watoto wengine ama laah, lakini mara nyingi pale alikuwa anaishi na Asha ambae yeye alikuwa mtu wa kutoka mno na alihakikisha mamaake anakuwa ni mwenye furaha siku zote.

Baada ya masaa matano kupita yule mama akiwa amekaa sebuleni mara alarm ya mlango iligongwa na alipoinuka kufungua alikutana na mlinzi wao wa getini akiwa kasimama mlangoni.
"Samahani mama, kuna mzee furani anahitaji kuonana na nyinyi vipi nimruhusu apite?"
"Mruhusu tu"
"Sawa Asante mama"
alijibu mlinzi na kukimbilia tena getini na kumruhusu kuingia ndani ya jengo huyo mzee aliyemzungumzia ambae alikuwa ni Hussein bubu mara baada ya kuoneshwa nyumba husika na Shebby ambae alikuwa kasimamisha gari mita hamsini na eneo lilipokuwa geti la kuingilia kwa kina Asha.
"Habari mama"
"Salama karibu"
alijibu yule mama ambae alikuwa na mwili wa wastani mara baada ya kusalimiwa na Hussein na kumruhusu akae.

Hussein hakuchelewa kujielezea kilichomleta pale na yule mama hakuonesha kupinga wala kuwa na maswali mengi zaidi ya kukubali na kuipokea ile barua
"Ahsante sana mama kwa ukarimu wako, vipi lakini mzee bado hajarudi kazini.?"
"haha Hapana usijali mzee kwa bahati mbaya hatunae siku nyingi"
"Oooh pole sana mama"
alijibu Hussein na kunyanyuka akijiandaa kuaga mara baada ya kupewa tarehe ya kuja kuchukua barua ya majibu lakini kabla hajaaga alikumbuka kitu frani
"samahani mama hivi unaitwa nani.?"
"Ahaa mi naitwa Zena Hamisi Kidongo"
alijibu huku akiwa katabasamu yule mama lakini ikawa tofauti kidogo kwa Hussein mara baada ya kulisikia lile jina.
"ZENA HAMIS KIDONGO!!?"
"Eeeh kwani vipi baba mbona umeonesha kulishangaa kidogo jina langu baya sana nini?"
"Hapana mama, hilo jina sio geni sana labda nikuulize unamfahamu Mariam Hamis Kidongo"
"MARIAM? Haah!! huyo ni Marehemu dadaangu kabisa we umemjuaje na alifariki miaka mingi sasa"
alistaajabu yule mama na kumuangalia kwa makini Hussein ambae alijikuta anakaa chini kabisa akiwa kapigwa na bumbuwazi zito usoni mwake na machozi kuanza kumtoka akiikumbuka barua ya mariam iliyomuelekeza kuhusu ugonjwa wake na habari juu ya mtoto wake wa kike ambae alikuwa anaitwa Asha na kuanza kuamini kuwa huyu aliyekuja kumchumbia huenda akawa ni mwanae kabisa kwani hata jina alilotajiwa na Shebby pindi walipokuwa wanaandika barua ni Asha Hussein
"Zenaa.. Oooh! Mi naitwa Hussein.. aaagh ndioooo Hussein Bakari... Hussein yule wa dadaako Mariam"
aliongea huku machozi yakimtoka Hussein kama mtoto
"Haa! Ina maana wewe ni Shemeji Hussein tuliyesikia umefungwa maisha sijui Kunyongwaa aaagh Ashaaaaaaaa ni mtoto wako aliekuachia dada!!aaaaaaaa Munguuuuu"
alistaajabu yule mama na kuangusha kilio kilichomstua Asha mara baada ya kusikia anaitwa na kuanza kushuka haraka juu alipokuwa na kufika sebureni ambapo hakuamini alichokuwa anakiona na hakujua kisa na mkasa mpaka mamaake na yule mzee ambae alijua ni mshenga kugalagala chini wote wakiwa wanalia kwa uchungu mithili ya familia moja iliyopokea taarifa ya kifo cha ghafra kwa mtu waliyempenda na kumtegemea.

"Mamaa .. maaamaa!!! Vipi nini kimetokea tena?"
alifika haraka pale sebureni Asha huku akiuliza kwa mshangao na kumuinua mamaake ambae hakuwahi kumuona akiwa analia kwa uchungu kiasi kile tangia apate fahamu zake mara baada ya kurudi kutoka India alipokuwa amepelekwa akiwa bado mdogo na wafadhili walioishi nae kwa zaidi ya miaka kumi kabla ya kufariki kwao nae na alipofuzu masomo yake ya udaktari hakutaka kuendelea kubaki nje zaidi ya kurejea nyumbani Tanzania ambapo alipokelewa na mamaake yule ambae alimuonesha mapenzi kama mtoto wake wa kumzaa mbali na ukweli kuwa mamaake mzazi hakuwa yeye.
"Mamaa mamaaa hebu nyamazeni basi mnambie nini kimetokea! Eti we mzee umeleta habari gani tena iliyomkosesha furaha mamaangu?"
aliuliza kwa hasira Asha na kumuangalia Hussein bubu ambae yeye aliacha kulia kwa sauti na kukaa kitako akimtazama Asha akiwa haamini kama hii leo anakutana na mwanae ambae hakuwahi hata kum beba akiwa mtu mzima tena mrembo na asilimia kubwa alifanana na mamaake ambae alikuwa mwanamke wa kwanza kumpenda kwa dhati Hussein mbali ya kuwa alikuja kumtenda vibaya
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!?
EPS 47
========
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
______________________

"Asha, hapana mwananguuuu.... Usiongeeee kwa sauti hiyooooo... aaaaaaah Najua itakuwa ngumu kuelewa harakaharakaaa mamaaa .. ila huyo mzee unayemuona mbele yakooo ndiee....ndieeeee.... ndie babaako Mzaziiiiii....hiiiii"
aliongea kwa kujikaza kisabuni yule mama mbali ya kuwa alikuwa na uchungu mzito moyoni mara baada ya kujitonesha kidonda cha kumkumbuka marehemu dadaake.
"Whaat!! Mamaaa!!?.."
alitaharuki Asha na kugeuka kumtazama Hussein kwa mshangao wa hali ya juu na kumtazama tena mamaake ambae sasa nae alikaa kitako na kuanza kujifuta machozi kwa kanga huku akimuangalia mwanae Asha ambae alikuwa bado kataharuki.
"Asha mwanangu, huyo ni babaako.. Huyo ndie Hussein babaako ambae tulikuficha ukweli miaka yote ila leo nitahadithia kila kitu na yoote ambayo huenda hata Shemeji Hussein hukuyajua... naomba Asha unisikilize kwa umakini sana mwangu."
aliongea kwa uchungu Zena huku akijifuta tena machozi ambayo yalikuwa hayakomi kumtoka na kumfanya Asha aungane nao na kukaa kabisa pale chini huku upande wake wa kushoto alionekana Hussein na kulia kwake alionekana mamaake ambae ni Zena.
"Asha... Asha kwanza naomba utambue mimi si mamaako mzazi, nimeumia sana leo na naikumbuka sana barua ya dada aliyoniachia sambamba na maneno yake ambayo yote yalisafiri na maji mara baada ya mafuriko siku chache baada ya kifo chake kabla hawajaja wale wafadhili kukuchukua kwa msaada ulipokuwa darasa la nne baada ya kupita miaka sita ya maisha magumu na maajabu yako shuleni.
Mwanangu japo ilionekana sahihi kukuacha uende kulelewa na watu wengine tena ukiwa na umli wa miaka kumi tu na japo faida yake nimeiona na naiona mapaka sasa unanilea lakini ukweli nimeenda kinyume kabisa na maagizo aliyoniachia dadaa ambae ni mamaako. aaagh! Hussein unisamehe sikuwahi kumleta Asha wala kumwambia ukweli ambao dada alinisisitiza pindi atapokua nimwambie...
Eee Mungu nisamehe lakini sidhani kama nimechelewa, naahidi sasa nitawaambia ukweli wote nilioujua kuhusu Asha Dada na Hussein."
sauti ya mkwaluzo iliyoonesha dhahili imebeba maumivu mazito kutoka moyoni ilisikika ikitoka midomoni mwa Zena na kumfanya hata Dk Asha aanze kulengwa na machozi huku Hussein bubu yeye ndio kabisa alibaki kaganda kama sanamu akili na masikio yote aliyaelekeza kwa Zena japo macho muda wote yaliganda kwa Asha.
Alimeza funda la mate Zena huku akirekebsha sauti yake kwa kukohoa kidogo kwa kujikaza kiume na kuanza kusimulia kisa chote kilichokuwa nyuma ya pazia juu ya maisha ya Mariam na Asha.

* * * * *
(MIAKA 23 ILIYOPITA)
<<<<====>>>>
..................Simulizi Ya Zena....................
^^^
Sintoisahau ile siku dada aliponipigia simu akiwa anaongea kwa shida sana akinisihi niende haraka kwake kwa sauti ambayo ilinitisha na kunipa wasiwasi hali iliyonipelekea niache shughuli zote nilizokuwa nafanya nyumbani na kukimbilia kituo cha daladala pasi na kumuaga yeyote wala kumsubiri mama ambae alikuwa ameenda kwenye shughuli ya harusi ya mtoto wa rafikiake mwananyamala,
nilisimama kituoni na muda mfupi ilitokea daladala iliyokuwa inaelekea kule nilipokuwa naenda ambako ndipo alipopanga dada Mariamu na mara baada ya daladala ile kusimama kituoni nilipanda na baada ya mwendo wa dakika kadhaa gari ilifika kwenye kituo nilichokuwa nashuka na kushuka huku nikitembea mwendo wa haraka haraka kumuwahi dada ambae nilikuwa najua kuwa anaumwa lakini sikuwahi kuwaza kama ugonjwa aliokuwa anatuambia ungeweza kumzidia na kumfikisha katika hali mbaya kiasi kile kama nilivyotafsiri kupitia sauti yake niliyoisikia simuni muda mfupi.

Sikuamini pindi nilipoingia ndani moja kwa moja na kumkuta mtoto wa dada ambae ni Asha kipindi hiko akiwa na miaka minne tu akiwa analia pale chini huku akimtingisha mamaake aliekuwa amelala huku nzi wengi wakiwa wamemjalia sehemu ya koo na mdomo ameuacha wazi ulimi kiwa umemtoka mithili ya mtu aliyekuwa amebanwa na kitu shingoni.
'Daaadaa!!....daadaaaa..!' Niliita kwa uchungu na kumsogelea pale chini huku machozi yakinitoka nikiwa sielewi nini kimempata dadaangu kufikia katika hali ile ya kushindwa hata kuitika na kubaki akinitazama tu huku macho yake yakitokwa machozi mfululizo na kunijengea imani ni kiasi gani alikuwa anapata maumivu makubwa sana ya ugonjwa ambao hadi dakika huo nilikuwa sijaujua hadi pale nilipojitutumua kumuinua kwa lengo la kumrudisha kitandani kabla sijafanya taratibu za kuita gari ya kumuwahisha hospitali na hapo ndipo niliposhangaa kuona uchafu uliokuwa unatoka chini kidogo ya shingo ya dada karibu na eneo la bega tena ajabu ulikuwa unatokota kadri alivyokuwa anataka kujaribu kusema kitu ama kumeza mate na kunifanya nitaharuki na kugundua sababu za nzi wengi kumzonga dada Mariamu.
'Aaaaaaaah..daadaangu nini tena kimekupata?!!'
Nilijikuta najisemea mwenyewe huku machozi yakinitoka kila nilipokuwa namuangalia na Asha alivyokuwa analia tena huku akiwa kashika bakuli ya plastiki mkononi akitingisha miguu ya mamaake bila kujali uwepo wangu.
"maamaaa tata ujiiii... mama ujiiiii.."
Sauti na maneno ya Asha yalizidi kuniliza na kubaini kuwa zaidi kilichokuwa kinamliza Asha ni njaa na ilionesha wazi hakukupikwa chochote siku hiyo toka asubuhi na masikini ya Mungu mtoto mdogo kama Asha ambae bado akili yake ilikuwa haijakomaa, hakuwa anajua nini kimempata mamaake hadi wamekaa na njaa muda wote na hakuwa na chochote cha kufanya kwa umli wake zaidi ya kumtingisha kwa kumuamsha mamaake apike basi huo uji ambao niligundua ndio kilikuwa chakula kikubwa alichokizoea yule mtoto.
Sikuwa na cha kufanya zaidi ya kutoka kuomba msaada kwa majirani mara baada ya milango mengine miwili ya ile nyumba iliyokuwa na vyumba vitatu tu alipopanga dada kuonekana makufuri yakining'inia na kuashiria wahusika hawakuwepo na kwa bahati mbaya hata wale majirani niliowafata ambao asilimia kubwa niliwakuta wanawake baada ya waume zao kuwa kwenye mishughuliko hawakuweza kabisa kunipa msaada.
Hali hii ilinishangaza mno kwanini wale majirani wamekuwa na roho mbaya kiasi kile kwani kila niliyemfata kumuomba tena huku nikiwa nalia kama mtoto alionesha kunihurumia na nia ya kunisaidia lakini nilipomuelekeza nyumba yenyewe basi hubadilika na kuzuka sababu nyengine tofauti huku wengine wakidiriki kunicheka kabisa na kunitajia kiasi kikubwa cha pesa kama nitakuwa nataka msaada wao.
Nilihumia na sikujua sababu za msingi kwanini waltu wa pale walimchukia sana dadaangu na kushindwa kunisaidia walau kumbeba kumfikisha barabarani stendi ya Taxi kwani kiukweli eneo lile alipokuwa anaishi dada hakukuwa na njia ya kuruhusu gari lolote kufika hata bajaji.
Sikuwa na jinsi nilijikaza tena kiume na kupiga moyo konde nilikimbia kama mwizi ama kichaa moja kwa moja hadi pale stendi na kuwaita vijana wawili ambao nilipatana nao kiasi furani cha pesa na kukubaliana nami kwenda kum beba huyo mgonjwa kumleta kwenye Taxi ambayo nayo niliongea na dereva wake aliekubali kutusubiri.

Nilitangulia ndani na kumfunika dada vizuri hususani sehemu za juu kuuficha uchafu uliokuwa unavuja na kutoa harufu kali kwa kitenge changu ambacho nilijifunga kiunoni na kujikuta nabaki na skin tight ndefu ambayo awali nilikuwa siwezi kutembea mtaani nikiwa nimevaa yenyewe tu pasi na kujifunga walau kanga ama kitenge lakini siku hiyo nilijikuta najisahau kabisa kwa kuchanganyikiwa na laiti kama nisingekuwa na walau hiyo skin tight basi hata uchi kabisa ningetembea pasi na kujijua wala kujihisi.
Lakini kila nilipokuwa namuangalia dada alinionesha machoni kuwa kuna jambo anataka kunambia lakini anashindwa na nilipomtazama kwa makini alinipa ishara kwa kuangalia kwenye dressing table yake na kuniangalia mimi, alifanya vile kama mara tatu ndipo nilipoenda kuangalia hapo kwenye dressing table kuna nini na nilipekuwa kuangalia ndipo nilipoiona bahasha kubwa ya barua ikiwa imeandikwa jina langu kwa nje na ndipo nilipomuangalia dada ambae aliniashilia kwa macho kuwa ndio hiko kitu alichomaanisha lakini kwangu sikuona umuhimu wa kukaa chini kuanza kusoma barua wakati dadaangu amelala anateswa na maumivu makali..!!
Nilichofanya niliitumbukiza kwenye handbag yangu ile barua na
kuwaruhusu wale vijana waingie ambapo walipoingia niligundua mshtuko wao na adha ya harufu ya ajabu waliyokutana nayo mule ndani ambayo mimi sikuihisi nilipoingia hadi pale nilipojionea kidonda cha dada kilichokuwa kinavuja uchafu na hata hivyo sikukerwa hata chembe kwa ile harufu zaidi ya kuniongezea simanzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom