Simulizi: Wanawake ni wauaji

Simulizi: Wanawake ni wauaji

Angalizo Dogo tu wadau

Mtunzi wa Story hii
amejitahidi kuelezea uhalisia wa Mwanamke
ila kuna sehemu naomba niweke sawa

ameegemeza baadhi ya mambo ya kishirikina katika Dini,hususan Uislam
Upande wa yule Ustadh na Zai
Uislam upo mbali sana na Ushirikina
isije mtu akashika bango,kuwa Dini ya Uislam inazingatia sana Waganga wa kishirikina
Hapana
ukisema hivi,utakuwa umekosea upeo wa kukosea

naomba radhi
ikiwa nimemkwaza mtu
 
Angalizo Dogo tu wadau

Mtunzi wa Story hii
amejitahidi kuelezea uhalisia wa Mwanamke
ila kuna sehemu naomba niweke sawa

ameegemeza baadhi ya mambo ya kishirikina katika Dini,hususan Uislam
Upande wa yule Ustadh na Zai
Uislam upo mbali sana na Ushirikina
isije mtu akashika bango,kuwa Dini ya Uislam inazingatia sana Waganga wa kishirikina
Hapana
ukisema hivi,utakuwa umekosea upeo wa kukosea

naomba radhi
ikiwa nimemkwaza mtu
Mh n riwaya tu bana do not take it serious kiasi hiko,
 
Angalizo Dogo tu wadau

Mtunzi wa Story hii
amejitahidi kuelezea uhalisia wa Mwanamke
ila kuna sehemu naomba niweke sawa

ameegemeza baadhi ya mambo ya kishirikina katika Dini,hususan Uislam
Upande wa yule Ustadh na Zai
Uislam upo mbali sana na Ushirikina
isije mtu akashika bango,kuwa Dini ya Uislam inazingatia sana Waganga wa kishirikina
Hapana
ukisema hivi,utakuwa umekosea upeo wa kukosea

naomba radhi
ikiwa nimemkwaza mtu

Hamna cha kuweka sawa wala nini.. Wewe ndio unataka kuleta mambo ya ushirikina na uislam.. Wapi umeona mwingine kaliongelea swala hilo.!?

Madame S nyingine lini tena.!?
 
Hamna cha kuweka sawa wala nini.. Wewe ndio unataka kuleta mambo ya ushirikina na uislam.. Wapi umeona mwingine kaliongelea swala hilo.!?

Madame S nyingine lini tena.!?
Siku mbili hizi kuna moja naifatilia nikiona iko na mtiririko naitupia,
 
EPS 05
========

Alilipitia upya faili la kesi nzima ya Hussein Muhondogwa aliyefungwa pale kwa zaidi ya miaka 25.
Maelezo yalionesha kuwa mtuhumiwa alihukumiwa pale kwa kosa la kuwaua kwa kuwakatakata viungo mkewe na mwanae aliyekadiriwa umri usiozidi miezi sita. Ilionesha wazi mtuhumiwa alidhamiria kufanya tukio hilo kwa shinikizo la imani ya kishirikina ili awe tajiri kama ilivyothibitshwa na shahidi aliyeona na kuyasikia mazungumzo muda mfupi kabla mauaji kutokea. Ingawa serikali haikuamini ushirikina lakini bado aina ya tukio lilitosha kuthibitisha kuwa mtuhumiwa alidhamiria kuua hasa baada ya majibu ya daktari kuthibitisha kuwa alikuwa na akili timamu. Kwa mujibu wa katiba na vifungu vya sheria hakimu alikuwa na uwezo 3wa kutoa hukumu ya kunyongwa mtuhumiwa mpaka kufa, lakini kutokana na kukiri makosa yake mbele ya mahakama na kuonesha majuto ndipo alipunguziwa adhabu kutoka kifo mpaka kifungo cha maisha sambamba na kazi ngumu.
Baada ya kusoma yote yale Kamishna Shaaban alishusha pumzi na kufikiri jambo.
"Lakini kama kweli ana akili timamu na alikusudia kuua kwanini achanganyikiwe na kuandika haya maneno wanawake ni wauaji? Mh! hapa bado kuna jambo limejificha." Aliwaza na kuwazua
kwa kutumia elimu yake na uwezo wake binafsi wa kufikiri ndipo alipokata shauri na kulivalia njuga suala lile apate kutambua huo ukweli alioamini umejificha ndani ya maneno ya yule mfungwa. “Hakikisha Coplo unampiga picha kwa kila akifanyacho na uwe unanirekodia nyendo zake zote huko 'site' sawa..”
“Sawa mkuu.”
Alitoa agizo kwa askari kiongozi wa wafungwa pindi wanapoelekea kufanya kazi ngumu. Paipo kugundua Hussein kila alichofanya alirekodiwa kupitia simu ya yule 'coplo' na video kutumiwa kamishna Shaaban.
Kama kawaida yake Hussein mwili unapochemka akiwa kwenye kazi ya ngumu ya kuvunja kokoto hakutaka soga na yeyote zaidi ya kufanya kazi kwa nguvu sana. Licha ya umri wake kuwa ni mtu mzima lakini bado mwili wake ulikuwa na nguvu huku uso wake ukionesha ni mtu aliyedata. Muda mwengine alitabasamu na kujichekea mwenyewe tena kwa sauti kubwa hata kuwastua wengine wasijue kipi kimchekeshechasho! Na anapokuwa katika hali hiyo ndipo anapoongea maneno yake ya ajabu na mwishoni mwa kicheko husema WANAWAKE NI WAUAJI..
Wafungwa wenzake walishamzoea na walichukulia kawaida. Hakuna aliyethubutu kumzuia wala kumuuliza kwa kujua ni kazi bure kwani wengi waliopita walijaribu na kuambulia patupu na zaidi anapokasilika aliwapiga hata hao waliomuuliza bila kujali ni wafungwa wenzie ama askari. Hali ile ilimjengea usugu ndani ya gereza na kuogopwa. Lakini zile rekodi na picha zilizidi kumpa hamasa Kamishna Shaaban ya kujua nini kimejificha kwa mfungwa yule. Aliwazua na kuona sasa kuna umuhimu mkubwa wa kumfanya huyo mfungwa azungumze nae. Ndipo aliuandaa mchezo kupitia askari wake waliomtii na siku moja majira ya saa mbili usiku mchezo ulianza. Njemba za askari watano waliingia alipolala Hussein na kumkamata kwa nguvu. Walimfunga kitambaa machoni na minyororo ya pingu mikononi na miguuni. Akiwa katika hali ya sintofahamu Hussein alifurukuta na kupiga kulele. Haikuwa kazi rahisi lakini haikuwafanya wale maafande washindwe kumpeleka msobemsobe sehemu husika waliyokusudia. Walipomfikisha walimzimisha kwa kumpiga na kitako cha bunduki nyuma ya kisogo na kukata moto kwa muda.
"Tayari mkuu, tushamuweka kwenye chumba cha mahojiano." Afande aliyeongoza zoezi alimuhabarisha mkubwa wake ambae aliagizwa na kamishna Shaaban. Ndipo nae alipomjuza Kamishna. Ilikuwa ni siri ya kamishna na yule coplo ambae aliwatumia askari wengine pasipo kugundua nini ambacho kamishana wao anafanya.
Baada ya lisaa limoja anakuja kustuka Hussein punde maji baridi yalipotabaruku usoni mwake. Alijikuta amekalishwa kwenye kiti na mbele yake alikaa mtu ambae hakumfahamu ikizingatiwa hakuvaa sare zozote. Alikuwa ni Kamishna Shebby ambae pia aliamuru afunguliwe pingu kwanza. Japo awali coplo alisita kutokana na kumjua Hussein ni mtu hatari mwenye mwili mkubwa alioutengeneza kwa kufanya kazi ngumu, asije mpalua mkuu wao hata kumtia kabali. Aliamini si salama kumuacha aongee na muheshimiwa wao akiwa hajadhibitiwa walau mikono lakini cha ajabu Kamishna Shebby alisisitiza wampe uhuru wamfungue na wawaache wazungumze. Lakini mbali ya kumuonesha kila aina ya amani haikumfanya Hussein ampende yule kijana wala hakumjibu chochote alichomuuliza kwa siku hiyo. Alimuonesha kwa vitendo kwa nini anaitwa babu bubu. Alijaribu Shebby kwa mbinu zake siku hiyo kumfanya aseme walau jina lake lakini kazi ilikuwa bure. Mwishowe alishindwa na kuamuru wamrejeshe.
Baada ya hapo kamishna Shebby hakuchoka kwa kuamini yule mfungwa si bubu wala hajapoteza weledi wa kusema. Siku nyengine tena Hussein alichukuliwa na kufikishwa kwenye kile chumba ambapo safari hii kamishna alitaka wamtoe kule na kumpeleka kwenye nyumba ya mkuu wa geleza ambapo ndipo aliishi. Huko alimpa uhuru zaidi hata ya kumtaka akaoge kwenye bafu zuri na kuvaa nguo mpya ingawa pia zilikuwa za kifungwa. Chini ya usimamizi wa askari waliokuwa wakishangazwa na kamishna wao hasa pale alipokaa nae meza kuu ya chakula na mtuhumiwa yule. Siku hiyo walikula pamoja ingawa Hussein alikula kiujeuri lakini moyoni hakuacha kujiuliza kwanini anafanyiwa ukarimu ule na mtu yule ambae alikuwa mgeni pia machoni mwake ingawa alishagundua ndiye mkuu mpya wa gereza. Siku hiyo Shebby hakumuuliza kitu chochote mzee yule zaidi ya kumuonesha heshima na baada ya chakula aliruhusu arudishwe kule na kusisitiza zoezi lile la kula pamoja liwe endelevu.
Ilikuwa si rahisi kueleweka kwa askari wake nini anafanya ingawa kwa upande wake kamishna Shebby alikuwa na uhakika wa kile afanyacho. Yote hiyo ilitokana na kipawa kikubwa na uwezo wa ajabu aliokuwa nao kwenye kuisoma saikolojia ya mtu. Hakuisha kumchombeza Hussein kwa maneno ya hapa na pale kila alipokutanishwa nae na kumuonesha heshima kubwa hasa kwa kumtunuku jina la 'baba' ambalo Hussein katika maisha yake hadi kipindi hiko akiwa na miaka hamsini na kitu hajawahi kuitwa baba ingawa alishakuwa na mtoto. Alisikia faraja kidogo moyoni Hussein licha ya kuificha machoni lakini zaidi alichanganywa na tabia na ukarimu aliokuwa anaonyeshwa na kijana yule mkuu mpya wa gereza.
"Katika maisha binaadamu tunakutana na matatizo mbalimbali. Na matatizo ndio maisha yenyewe. Maisha bila matatizo bado hayawezi kuwa maisha. Masikini na matajiri wote wana matatizo yao ingawa wengine hudhani pesa ndio mwisho wa matatizo. Si kweli! Hatupaswi kusihi kwa kuwalaumu wengine ama kuwaona hawana maana eti kwa sababu ya matatizo yao ama kutusababishia matatizo. Wala hatupaswi kuomba sana kwa Mungu asitupe matatizo, huo utakuwa ufinyu wa fikra. Kikubwa tunapaswa kumuomba Mungu nguvu na akili ya kupambana na matatizo. Jisikie kawaida wala usijione mpweke kwenye uso wa dunia. Kumbuka baba hakuna aliye huru kwenye maisha uwe gerezani ama uraiani bado hauko huru. Tunaishi kwa sheria na kila sehemu kuna sheria zake na hapo ndipo kuna tofauti ya kimantiki maana ya kuwa huru. Lakini kiundani hakuna aliye huru duniani na hata mbele za Mungu. Sote tunaishi kwenye misingi na kanuni maalum ambazo ukienda kinyume chake lazima adhabu iwe upande wako. Jisikie amani baba. Naitwa Shaaban." Aliongea kamishna Shebby na kujitambulisha kwa mara ya kwanza siku hiyo maneno ambayo yaliugusa moyo wa Hussein bubu ingawa hayakumfanya aunyayue mdomo wake na kusema chochote. Kamishna Shebby nae hakuonesha papala wala haraka. Alizidi kumroga kifikra Hussein bubu. Siku zilisonga na maisha ya jela kuwa tofauti kwa Hussein na hata ifikapo usiku hakuchukuliwa tena msobe msobe kwenda kukutana na kamishna zaidi alisindikizwa tu kwa amani na coplo mwenyewe. Muda mwengine hata Kamishna Shebby alijiuliza kwanini moyo wake una shauku sana ya kujua kilichomkuta yule mzee? lakini kila alipokutana naye moyo ulizidi msukuma kutaka kujua kilichojificha kwenye maisha ya Hussein na kauli yake ya 'wanawake ni wauaji'.
Lakini mbali ya mbinu zote za Kamishna Shaaban (shebby) lakini zoezi la kuzungumza yaliyomsibu Hussein liligonga mwamba. Hapo ndipo kamishna alipoumiza kichwa na kutumia mbinu m'badala ambayo alimtoa eneo tofauti kabisa Hussein tena kwa siri iliyojulikana na askari wachache. Mipango ilianza baada ya kamishana kuagiza Hussein bubu apimwe vipimo vya nguo na kushonewa suti nzuri. Ndipo siku hiyo ikiwa mwisho wa wiki kamishna akiwa amevaa suti kali aligizwa aletwe Hussein bubu ambae naye chini ya ulinzi alioga na kuamriwa avae suti. Hali ile ilimshangaza mno Hussein hasa baada ya kunyolewa vizuri a kuwa katika mtazamo mpya wa kibinaadam. Ndipo mwishowe msafara wa magari mawili yalipotoka nje ya gereza ambapo moja wapo alikuwapo kamishna na Hussein bubu na nyengine walikuwa walinzi waliovaa kiraia pia. Askari wengi hata wa getini hawakujua kama kuna mfungwa mmoja anatoka na kamishna zaidi walidhani ni kiongozi mwengine tu wa jeshi aliyekuwa anatoka na kamishana siku ile. Ukiwa ni mchezo wa kinyume na sheria za magereza kutoka na mfungwa nje ya gereza kinyemela lakini Kamishna Shebby aliamua kufanya yote yale kwa kukata kiu ya moyo wake ili mfungwa yue azungumze kwa mara ya kwanza tangu ahukumiwe. Na moja kwa moja aliamuru msafara kuelekea maeneo ya fukwe ya 'Sun rise'.
Walifika na kupokewa kama wateja wengine wa heshima huku askari aliombatana nao wakichukua nafasi kwenye pembe tofauti wakidumisha usalama wa kamishna na mfungwa. Mazingira ya nje yalikuwa kama lulu machoni mwa Hussein bubu. Ilikuwa ni tofauti na fukwe alizozizoea kabla hajawa ndugu wa gereza. Teknolojia ilikua na mambo yalibadilika na kumfanya akumbuke mambo mengi hasa mara baada ya kuliona jua na wanawake wengi waliomwagika wakifurahia maisha ufukweni. Ni muda mlefu sana ulipita hakuwahi kuuona uso wa mwanamke. Aliwatazama vijana wa kiume wakikumbatiana na wanawake zao kimahaba na hapo alianza kuchefuka taratibu moyoni. Muhudumu wa kike aliwahudumia vinywaji na vyakula walivyoagiza na alipoondoka Hussein alimtazama sana kwa dharau ya hali ya juu.
"ha ha ha ha aaa HAHAHAHAAAAA .." Mwishowe Hussein bubu alicheka ghafla kwa sauti ya juu na kumstua kamishna Shebby.
"Kulikoni baba vipi?" Alimuuliza lakini alichojibu Hussein Babu bubu kilimshtua hata muhudumu yule ambaye alikuwa anarejea akiwa na vinywaji.
"Wanawakeeee... wanawakeeee .. wanawaaaake wazuuuri sana mwananguu ukiwatazama kwa nje tu, ila kwa ndani ni wabaya sanaaaa tena saaanaaaa na ni wauaji wakubwaaaa.. ha ha ha hahaaa.. WANAWAKE NI WAUAJIIII"
Kwa mara ya kwanza kinywa cha Hussein bubu kilifunguka na kunyoosha maneno. Ndipo kamishna Shebby alipobonyeza kitufe cha kurekodi katika simu yake kwani alijua sasa ule wakati alioutafuta na kuusubiri kwa muda mrefu umetimu. Alianza kumuuliza na kumpekecha kujua kulikoni zaidi kilichokuwa nyuma ya pazia! Na kweli taratiiiibu Hussein alijikuta kwa mara ya kwanza akifunguka na kusimulia historia yake yote na masahibu ya maisha yake hadi kufikia vile. Kumbukizi zake zilimrudisha siku ile aliyokuwa anaangalia kile kipindi cha ya walimwengu kutoka BECKER TV na hadithi yake ndio ilianzia pale akimsimulia kamishna Shaaban Mwinchande.

ITAENDELEA....
Nice

Sent using Jamii Forums mobile app
 
_________________
EPS 06
========

Simulizi iliyoshiba hisia ilimuumiza kila taswira ya matukio ya maisha yake ilivyomjengea picha ubongoni. Na zaidi alipofikia pale alipojuana na Zai msichana mrembo wa ndotoni aliyekuja kuwa dhahiri alikumbuka mengi sana. Msichana aliyemshangaza kwa kumtaja jina lake la utani tena la utotoni pasipo kumtajia mwenyewe. Msichana aliyemuonesha mapenzi na kuwa tayari kuvumilia masharti magumu. Masharti ambayo yalificha siri kubwa ndani yake ambayo alipuuza kuijua. Ndipo alipojikuta akishindwa kabisa kuendelea kusimulia baada ya maumivu ya moyo kuzidi uhimili wa hisia. Wakale walisema, ukimuona mtu mzima analia mbele za watu! ujue kuna jambo. Hapo ndipo kamishna Shaaban alipolivaa jukumu la kumfariji na kumsihi kwa maneno matamu ambayo hayakumfanya atulie mzee Hussein aliyezidi kunung'unika katikati ya kilio akisisitiza kuwa 'wanawake ni wauaji.'

*<>* *<>* *<>*

_______
Kum bembeleza mtu mzima ilikuwa si kazi ndogo pia muda nao ulienda sana na kutokana baadhi ya watu kuanza kutega masikio kujua kulikoni hasa walipoona kuna mtumzima mmoja alietinga suti kali ya heshima anatokwa machozi hivyo kama unavyojua ukimuona mtu mzima analia mbele za watu ujue kuna jambo na kwa kukwepa kujaza watu ndipo Kamishna Shebby sambamba na vijana wake waliamua kuondoka haraka na kurejea gerezani na baadae baada ya kurudishwa kwenye chumba cha siri na kuvalishwa nguo zake za gerezani aliamuru Hussein ahamishwe toka sero za awali na kupelekwa sero za v.i.p ambako walifungwa watu wenye pesa na viongozi wakubwa.

Ndipo siku nyengine ilikuwa saa sita za usiku Babu bubu (Hussein) alichukuliwa kama kawaida na kupelekwa kwenye chumba kimoja kikubwa kilichokuwa na masofa mazuri huku kamera mbalimbali zilitegwa na kamishna Shebby pasi na kujua yeyote kwenye chumba kile ndani ya makao ya Kamishna gerezani pale ndipo Hussein alijikuta akiendelea kuhadithia ile story ambayo aliapa awali kuwa ingebaki kuwa siri moyoni mwake.

* * * * * *
.......
< MASWAHIBU >
(MIAKA 29 ILIYOPITA)
>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>>

Kiukweli japo masharti aliyonipa Zai yalikuwa magumu sana lakini kutokana na upendo wa ajabu niliokuwa nao nilijikuta navumilia na kusubiri na taratibu miezi ikasonga na nikaanza kuisoma tabia nzuri na ya kipekee aliyokuwa nayo Zai.
Kwanza alipenda dini alikuwa muislam safi sana pili alikuwa ana akili za kipekee mno na zaidi ya yote alijiheshimu tofauti na wasichana wengi niliowajua.

Siku zilisonga na hatimae mwaka mmoja ulikatika na siku hiyo Zai alinipigia simu tena kuwa anakuja getto nami nikafanya usafi harakaharaka na alipofika siku hiyo nilishangaa jinsi alivyokuja huku akiwa na begi kubwa la nguo na zaidi ni mada aliyokuja nayo nikajikuta nabaki mdomo wazi pale aliposema.

“Hussein amini mimi ni wako na sasa nimekuwa wako rasmi. Najua huna kipato kikubwa lakini una uwezo wa kunioa hata kesho, ukweli mi huku sikuja kusoma wala sina ndugu zaidi nilikuja kufanya kazi za ndani tu kwa mama mmoja wa kichaga aliyekuja kuniomba kwetu ila samahani nilikudanganya awali na kukupa masharti yote yale kwa lengo la kukujua vizuri ili uniimanishe kama umenipenda kweli au umenitamani na wanaume wote walionitongoza na kuning’ang’ania niliwakubalia wote na kuwapa masharti hayo matatu na woote walijitahidi kuvumilia lakini walishindwa baadae na hakuna hata aliyefika miezi sita lakini wewe umekuwa wa ajabu kwangu na naamini ndie mume bora kwangu… naomba unipokee kwani kule nimeondoka rasmi kutokana na manyanyaso na tabia za pale nyumbani.”

Nilibaki namuangalia Zai kile alichokuwa anakisema huku nikifikilia kichwani mwangu nimkubalie harakaharaka vile au kuna uongo anauendeleza tu kwani baadhi ya mambo ya Zai yalinistaajabisha kidogo hasa kuniamini na kunambia mi ni waajabu ilihali tulikuwa hatukai wote lakini kiukmweli toka niachane na Mamu sikuwahi kufanya ngono hadi dakika ile.
Na ukichochea upendo niliokuwa nao na uzuri wa Zai nilijikuta namkubalia na kupanga nae safari siku tatu zijazo twende huko kijijini kwao Arusha.

Ulipotimu usiku kwa mara ya kwanza baada ya Zai kusali alipanda kitandani na kulala pamoja na mimi huku akiwa kava gagulo na kiblauz alinibusu na kunambia kuwa nisitamani wala ntusifanye ngono hadi siku tutayofunga ndoa na kuninong’oneza kuwa yeye ni bikra pia.
Moyoni sikuamini hata kidogo alichosema Zai kwani alikuwa mrembo mno si rahisi kudumu na bikra hadi umli ule… niliona kuwa sasa nadanganywa na ktk umli wangu wote ule nilikuwa sijawahi kukutana na mwanamke bikra.

Usiku huo usingizi haukuja kabisa kila mara nilimuangalia Zai alivyolala umbo lake zuri lilivyojichora namba nane nilijikuta paipu yake inasimama na nyege za mwaka zikisisimua mwili wangu baada ya taswira za pepo chafu kutawala hisia zangu nilijikuta najisogeza karibu kabisa na Zai na kuanza kumpapasa kiuno na taratibu nilianza kupeleka mkono ndani ya gagulo lake na kukutana na kufuri lake lililoficha sehemu zake za utamu na kujikuta mate yakinijaa mdomoni kama fisi mwenye njaa aliyekutana na mzoga mbele yake.

Niliendelea kumpapasa taratibu nikiwa makini kabisa ili nisimstue usingizini na hatimae mkono wangu hususani vidole vyangu vile vya kati viliweza kupenya katika pachupachu ya chupi na kukutana na kajoto ka ajabu kutokea kwenye mashine ambayo sikuamini kama kweli ni mpya kabisa na haijawahi kutumiwa hapo kabla.
Katika hali nisiyoitarajia nililazimisha kwa ustadi mkubwa kupenyeza kidole changu kile ambacho ukimnyooshea mtu lazima mgombane,
Sikuamini pindi nilipoona kila dariri kuwa ni kweli ile mashine ilikuwa mpya na nilipolazimisha kupenyeza kidole kwa kuvisukuma vile vijinyama vilivyoziba njia Zai aliruka na kushtuka kwa sauti ya juu name kuutoa mkono haraka na kujigeuzia pembeni kwa speed ya hali ya juu.

“Hussein baby kwanini unataka kunifanyia hivyo?... tuseme huniamini nilivyokwambia!!? Mimi ni bikra kweli sijawahi kuguswa na mwanamme yeyote na niwewe pekee niliyekuamini na nahitaji uwe mume wangu wa ndoa ndio itakuwa raha siku utayonifungulia njia hii ya starehe ya wapendanao… baby najua una hisia lakini naomba vumilia tuu honey”
Maneno ya Zai yaliweza kumrusha ibilisi aliyenishika ghafra na kujikuta Napata moyo na nguvu na kumkumbatia huku nikimuomba samahani na kumuahidi sitamgusa tena mpaka tutapooana.
“So sorry baby.. sitorudia tena ni shetani tu alinipitia nikataka kukujaribu ili nihakikishe but sitorudia tena mpaka siku tutapohalalisha ..”
Niliongea maneno haya kwa busara ya hali ya juu nae Zai bila kinyongo aliniitika kwa kichwa na kunibusu kisha tukalala na sikumgusa tena hadi kulipokucha na mishe mishe ziliendelea hususani kwenda kukata tiketi kwajili ya safari huko kwao na siku mbili baadae niliaga tena kazizni ambapo nilipewa likizo ya wiki moja kwaajili ya kumaliza msiba niliodanganya awali na kutumia fulsa hiyo kusafiri na Zai mpaka jijini Arusha ambapo tulipanda tena gari lililotupeleka vijiji vya ndani ndani kabisa.
ITAENDELEA.....
6

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 09
========

Saa tatu kasoro usiku tulishuka eneo husika na kuchepuka kukifata kibarabara chembamba kilichoelekea huko alipopatikana ba mkubwa ambapo kulikuwa na umbali wa kilometa kama mbili kukifikia hiko kijiji.
Kwa kuwa ulikuwa usiku na giza lilishaingia huku kukiwa na kijimbaramwezi kwa mbali ilibidi tutumie tochi kumulikia na njia nzima kulikuwa kimya sana.

Nakumbuka baada ya mwendo kidogo tukiwa tumebakiza kama kilometa moja na nusu kufika mke wangu aliniomba ajisaidie haja ndogo kwani alibanwa mno na asingeweza kuendelea mbele nami nilimuonya ajisaidie palepale njiani asiingie polini kwani kuna wadudu wengi kwenye majani na ndipo nilipompokea mtoto na kusimama kumsubiria.

Nikiwa nimesimama mke wangu anajisaidia ghafra nilisikia chakala chakala na nilipogeuka nilishangaa kumuona mtu aliyevaa kininja akininyang’anya mtoto kwa nguvu na kabla sijafanya lolote kujitetea mara kwa nyuma nilipigwa na kitu kizito bila kumuona aliyenipiga na kujikuta naanguka chini huku kwa mbali nilisikia ukulele wa mke wangu kipenzi Zai akisema.

‘’’’’’Jamaaniii iiiinatoshaaaaa Nilishawaaambiaa msimuuueeee..’’’’’

Sitoweza kuisahau kamwe kauli ile ya Mke wangu Zai.. Zai wangu kipenziii msichana wa ndoto yangu niliyeamini nimeoneshwa na Mungu lakini leo hii anatoa kauli iliyoniaminisha na kuniumiza moyo wangu kupelekea kupoteza fahamu pindi nilipoanguka baada ya kugundua kuwa kumbe mchezo wooooooootee nae alihusika na aliujua vizuuuuri. looh!
Ama kweli adui wako mkubwa ni mtu wako wa karibu na Udhaniae ndie sie ila sie ndie.
Nilijihisi nakaribia kufa huku nikijiuliza kumbe Zai aliishiii kwa kuniigiziaa?!! aaaaaghh!!!!!… Ni vigumu sana kuaminilll! lakini Chunga sana baaabaa Kamishnaaa usiombe kabisa yakukute kama yaliyonikutaaaa.
Siku hiyo ndio kwa mala ya kwanza niliikubali thabiti ile kauli kuwa Wanaake ni Wauaji, nami nakazia kabisa leo hadi siku ya kufa kwangu nitasema kuwa WANAAKE NI WAUAJIIIIII.

*<>* *<>* *<>*

Kilifuata tena kilio cha sauti ya juu na kwikwi kutoka kwa Hussein na kazi ikabaki kwa Kamishna Shaaban Mwinchande kum bembeleza na kumtuliza ili apate kuelewa na kubaini kilichoendelea ktk hadithi yake baada ya kurudiwa na fahamu.
Safari hii sasa hata Kamishna Shaaban mwenyewe alijikuta nae machozi yakim bubujika kwa jinsi alivyokuwa anasikiliza kisa kile cha Hussein na zaidi alipomtazama uso wake wa kiutuuzima uliokuwa unatiririkwa machozi kama mtoto kadri alipokuwa anasimulia na alionesha dhahili kuwa ana ghadhabu kubwa juu ya wanaake kwani ktk hadithi yake ile hadi muda huo ilibeba maumivu tu na mateso yote ameyapata sababu ya mwanamke aliyempenda na pia kwa uzoefu wake wa kusoma saikology za watu Kamishna shebby alizidi kumuamini na kubaini kuwa kweli mfungwa yule alionewa na hakuwahi fanya ubaya wowote.
Lakini maswali bado yalibaki kichwani mwa Kamishna Shebby na alitaka kujua zaidi ilikuaje hadi kukawa na uthibitisho wa maiti hizo mbili ya mkewe na mtoto? na iweje huyo Zai mke wa Hussein afahamiane na hao watu na kueka mbinu kisha wamgeuke pia na wamuue sambamba na mtoto? ilikuwaje kuwaje hapo... na huyo Mr. X ni nani kwa mujibu wa barua ya kutatanisha aliyoipata Hussein.
Japo alikuwa mtaalamu sana Shaaban na alijaliwa ubongo mwepesi ktk kufikiri na kufumbua jambo lakini kwa maswali yale yaliyosumbuka kichwa chake muda ule juu ya hadithi ya Hussein hakuweza kupata majibu ya haraka zaidi ya kumsihi mfungwa wake (Hussein) ajikaze ili aendelee kumsimulia kilichotokea baada ya kurudiwa na fahamu mpaka kukamatwa na kuhukumiwa.

Siku hiyo Hussein japo maumivu yalikuwa mazito mno moyoni mwake kwa kukumbuka mapito yaliyoinyamazisha ndoto zake na kujikuta anazeekea jera akisubiri kifo tu lakini alijitahidi na alipania kuwa aweke kila kitu wazi kwa kijana yule ambae awali hakutambua kama ndio kamishna lakini sasa alijua na hakuwa na jinsi zaidi ya kumuelezea kila kitu hasa baada ya kugundua ni askali kiongozi mwenye moyo wa kipekee sana.

Huku akifuta mafua baada ya kimya cha zaidi ya dakika arobaini Hussein aliendelea kusimulia ilivyokuwa mara baada ya kupigwa na kitu kile kichwani hali iliyompelekea kuanguka na kupoteza fahamu.

*<>* *<>* *<>*
..........

Nilistuka mara baada ya kuhisi hali ya ubaridi na unyevunyevu na nilipotaka kuamka nilijihisi kichwa kuwa kizito sana lakini nilijitahidi na kukaa kitako pale njiani huku nikitazama huku na huko kuangalia kama kuna watu wanakuja niombe msaada ama sivyo nikusanye nguvu nipige mayowe raia waje wanisaidie japo nilijua kuwa pale nilipo kuna zaidi ya kilometa moja kufika kwenye makazi ya watu ambako ndiko pia alipatikana babaangu mkubwa yule mganga wa kienyeji na ndio nia ya safari ile tulikuwa tunaelekea kwake.
Sikujua ilinichukua muda gani mpaka niliporejewa na fahamu kwani nilijikuta niko mwenyewe pale chini.

Lakini niliponyanyua mkono wangu na kutokana na mbalamwezi kuchomoza muda ule nilishangaa kuona umetapakaa damu halkadhalika na mkono mwengine.
Nilijikagua haraka haraka kuona wapi nimeumia lakini bado sikuhisi jeraha lolote mwilini mwangu zaidi ya jeraha dogo kichwani ambalo lilikuwa halivuji damu kivile.
Lakini pia nilipoangalia chini vizuri nilishangaa kuliona panga usawa ule nilipolala likiwa limeloa damu pia kulionekana michilizi ya damu kuelekea kwenye kichaka kimoja eneo lile.
Nilijikuta nikilishika lile panga kwa mshangao na kuligeuza geuza kuhakikisha kama ni kweli au macho yangu yalikuwa bado yana mawenge,! lakini nilipofanya vile akili iliniaminisha kuwa kile nikionacho ni kweli wala si mawenge na hapo ndipo nilipogutuka na kulitupa haraka chini lile panga na kujikuta nimepata nguvu za kusimama na kuanza kunyata kwa umakini kufatilia ile michilizi ya damu kujua nini kilichopo pale kwenye kichaka.
Lakini kabla sijakifikia kile kichaka mara nilianza kusikia kelele kelele za watu wengi waliokuwa wanakuja kwa mwendo wa kasi wakitokea ile njia iliyoelekea kijijini na punde tu nilipogeuka niliona mianga ya tochi ikinimulika huku kwa mbali nikisikia baadhi ya maneno waliyokuwa wanaongea wale watu.

"Mwanaharamu mwenyewe si ndio yuuleeee.."
"Enheeeee yule yule si unaona midamu ilee.."
"Aliyeua auaweeee hebu tupisheni sie mbona hamtembei tutamkosaaa.."

Zilikuwa ni moja ya kauli nilizozisikia toka kwa wale watu huku wengine wakianza kukimbia kuja pale niliposimama nami nikabaki nimeganda kwanza nikiwashangaa na nilipokaza macho kutazama vizuri niliwaona wengine wakiwa wamebeba silaha za jadi na macho yao wote wakinilenga mimi hasa baada ya kunionaa.
"Uuuuuaaaa Huyooooo.."
"PIGA UUAAA.."
Ukelele huu ambao uliambatana na kurushwa kwa mkuki ambao kwa bahati nzuri ulinikosa na ndipo akili ikanicheza na kunionya endapo nitachelewa sekunde kadhaa watu wale wataponikaribia zaidi wataniua kwani walionesha wazi walikuwa hawaji kwa wema wala huruma hata chembe juu yangu.
Nilijikuta naruka na kuanza kutimua mbio huku upepo mkali ukinipitia ghafra karibu na kichwa baada ya kurushwa kwa rungu moja kubwa ambalo niliamini lingenipata huenda ningezima pale pale kama sio kufa kabisa.

Nilikimbia kwa speed ya kunusuru maisha yangu huku nikifata kile kibarabara kilichoelekea barabara kuu kule tulipotoka na nyuma yangu bado niliandamwa na watu wale wenye hasira kali ambao sikuwa na uhakika wa moja kwa moja kuwa ni wanakijiji au ni miongoni mwa wale walionivamia awali!?
Lakini kabla sijafika mbali mbele yangu kulisikika mlio wa gari sambamba na mwanga mkali wa taa zilizonizuia kuona vizuri na kujikuta naingia porini lakini mara ile gari ilisimama ghafraa na nilisikia vishindo vya watu wakiruka na kunizunguka huku ukelele wa mlio wa risasi ukisikika kuwatuliza wananchi waliokuwa wanakuja ndipo nilipotulia hasa baada ya kusikia kauli zao na kugundua kuwa walikuwa ni polisi.
"tulia hivyo hivyo usikimbie zaidi mikono juu sisi ni maafsa wa polisi.."
Ilikuwa ni sauti ya mmoja wa watu walioruka kwenye gari akinisihi na kunisogerea pale niliposimama huku nami nikitii na kuona sasa afadhali msaada umepatikana.
ITAENDELEA….
9

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 10
========

"Wananchi tunaomba mtulie, mshatoa taarifa kwetu hampaswi tena kuchukua sheria mkononi. kwa pamoja naomba mtusaidie kuona eneo lenyewe la tukio hasa ni lipi na jee mtuhumiwa husika ndie huyu mliyekuwa mnamfukuzaa?"

"Ndioooooo Afande tuachieni tuliue kabisaaa linyamaa hiloo"

Sauti hizi zilizidi kunishangaza na kunishtua kwani mpaka muda huo sikujua nini hasa nilichofanya yaaani badala ya kupewa msaada ndio kwanza nataka kuuawa?
Nilikamatwa suruali na kuanza kutembezwa mpela mpela na wale askali wakiwafata wananchi ambao nao waliongozwa na mtu mmoja kuelekea kule niliposhambuliwa hususani eneo lile la kichaka ambako sikubahatika kuona kilichopo na ndipo mara baada ya askali kufika pale huku wakiwa na matochi makubwa yenye mwanga mkali tulishuhudia maiti mbili ya mama na mtoto mdogo zikiwa zimekatwa katwa vibaya.
Nilijihisi kuchanganyikiwa hasa baada ya kuona nguo za kale katoto ndio zilezile alizovaa mwanangu siku hiyo.
Nilipiga kelele kwa kumlilia zaidi mwanangu nikiamini nae wamemuua sambamba na mke wangu lakini chaajabu ndio kwanza nilizidi kuchezea vitasa na maneno makali kutoka kwa wale mapolisi huku wengine wakinipiga picha.

"Afande Jacobo sogeza gari pia afande Dula weka hilo panga vizuri hapo mbele hakikisha mtu yeyote asilishike direct bila groves pia inabidi turisachi hili liuaji vizuri tuone kama kutakuwa na ushahidi zaidi.. hakikisheni kila tukio linapigwa picha"
Aliongea afande mmoja alioonekana mkubwa wao, wakati huo wote mi nilikuwa nalia sana huku wananchi wakinitazama kwa hasira mno.

Ajabu kilichonistua zaidi na kufanya nipoteze fahamu kwa mara nyengine ni mara baada ya kuanza kusachiwa kabla ya kupandishwa kwenye difenda.
Ama kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni kwani kwenye mifuko yangu ya mbele ya suruali nilikutwa na kipande cha kiganja cha mkono wa mtoto kikiwa kimezungushiwa hirizi.
Aaaaaghhh!!!!!!!!! sikuaminiiii hata chembe nikionacho na mara ndipo nilipojihisi kizunguzungu cha ghafra na network zangu zilizima palepale.

Nilirejewa na fahamu mara baada ya kustuliwa kwa kumwagiwa maji mengi ambapo nilikuwa nimelala kifudi fudi ndani ya bodi la difenda iliyokuwa imesimama na nilipoinua kichwa niligundua nilikuwa peke yangu lakini nilipogeuka sasa kutazama vizuri ndipo nilipoona gari nyingi za polisi zikiwa zimepaki huku askali wengi sambamba na waandishi wa habari walikuwa wamesimama wakinipiga picha nikiwa kwenye ile Difenda hadi walipopanda askali wengine na kunishusha mkuku mkuku huku wakinisukuma na kuniongoza kwenye jengo moja ambalo niliponyanyua uso niliona maandishi makubwa yaliyosomeka KITUO KIKUU CHA POLISI KINONDONI

Nilijua sasa kumbe hatukua kule polini bali tupo mjini na ni katika kituo kikubwa cha polisi ambacho awali nilizoea tu kukisikia na kukiona kwa mbali huku sikuwahi kuwaza hata siku moja kama nami ningekuja kuingia eneo lile kama mtuhumiwa tena kwa kesi mbaya mno.
Sikujua tulichukua mda gani kutoka kule porini kutokana na kupoteza kwangu fahamu na mpaka muda ule akili zangu hazikukaa sawa kabisa na kila kilichokuwa kinaendelea niliona kama ndoto ama sinema tu na si kitu halisi japo ukweli ulibaki kuwa haikuwa ndoto wala sinema.
Nakumbuka baada ya kuvuliwa mkanda na viatu nilisongomekwa katika selo moja huku nyuma yangu nikiandamwa na virungu mfululizo hasa pale nilipotaka kusimama kuongea chochote lakini nafasi hiyo sikuipata.
Niliingia ndani ambapo kulikuwa na mahabusu wengine wakinishangaa kwa jinsi nilivyokuwa, nilijituliza na kukaa kitako kwenye kona ya kuta ya selo ile na kujikuta naanza kulia kwa uchungu mkubwa hasa nilipokumbuka maiti zile ambazo nilikuwa na uhakika kuwa ni za familia yangu hususani nilimlilia sana mwanangu kipenzi kwa kuuawa bila kosa lolote.

"Oyaaa M baba mbona unaleta uduanzi sasa... hebu tukaushie usituchulie hapaa tutakunjenga ooohooo.."

Ilikuwa ni sauti ya kiteja iliyondamana na kofi lililonikuta kichogoni na kunistua kwenye dimbwi la huzuni na mawazo na kunifanya nipunguze mdadi wa kulia kwa sauti na kubaki machozi yanaendelea kububujika yenyewe huku nikiomba kupambazuke haraka.
Asikwambie mtu selo pabaya sana hakuna hata chembe ya raha, harufu mbaya ya kinyesi tulichokuwa tunalala nacho kikiwa kwenye ndoo mpaka asubuhi ndio mtu anaenda kumwaga, hakukuwa na vigodolo wala shuka ya kujifunika na siku watu wakiwa wengi unakosa hata sehemu ya kukaa na kubaki umesimama daaah!! ni afadhali walau maisha ya huku jera japo nayo si mazuri.
Nakumbuka baadae asubuhi yake nilichukuliwa na kuingizwa katika chumba maalum cha mahojiano na mateso na huko nilikutana na askali watatu mmoja wao alikuwa mrefu mtu wa milaba minne ambae ndie alienikalisha kwenye kiti cha chuma na kuanza kunihoji huku wengine wakiandika na kurecord.

"Taja lijina rako upesi.."
Alianza kuniuliza kwa ukali kidogo yule afande baunsa.
"Naitwa Hussein afande.. hus..sein.." Nilijibu huku nikiwa na hofu.
"Taja vizuri bwana Lihuseni nani?"
"Hus..sein.. Bakari..kaka."
"Nani likaka lako wewe?! sina dogo likatiri na Riuaji kama wewe Ebo!.. haya sema kwanini uliua familia yako?"
"Familia yangu!! hapana.. afande sijaua yeyote mbona..!!"
"KELELE.. Tuna ushahidi wa kutosha na tumekukamata eneo la tukio. Unataka kudanganya chombo cha dora wakati vielelezo vyote tunavyo?..! lichawi likubwa wewe ngoja nikupe chai kwanza.."
Aliongea kwa hasira yule afande huku wenzake nao wakinikandamiza zaidi kwa tuhuma za ukatili ambao sikuwahi hata kuuwaza kama kuna binaadam anaweza kufanya vile kwa familia yake mwenyewe aliyoipenda.
Nilifungwa barabara kwa kuinamishwa nikiwa nimekaa kwenye kiti kile cha chuma kilichokuwa na mfano wa kisturi (hakina uegemeo) huku viwiko vya mikono yangu vikiwa sambamba na magoti yangu na kubananizwa pamoja hali iliyofanya nibaki nusu nimekaa nusu nimeinama na ndipo mateso makali yalipoanza sambamba na mijeredi.

Niliumia sana na kulia mpaka sauti ikaanza kunikauka kutokana na mateso yale makali asubuhi ile. Niliwaambia na kuwaapia kadri nijuavyo kuwa sijahusika na tukio lolote baya zaidi ya kwamba mimi na familia yangu ndio tulivamiwa lakini maneno yangu ndio ilikuwa kama chachu ya kufanya mateso yaongezeke zaidi.
Nilitamani hata kifo kije muda ule lakini nacho kilikuwa mbali na mimi. Oooh! sikuamini kama Hussein mimi ambae sikuwa na rekodi hata ya kushtakiwa kwa mjumbe tu ktk makuzi yangu wala kuwahi japo kumtishia mtu na kiwembe achilia mbali kumkata, lakini leo hii nateswa vikali kwa kosa la kuwakatakata na kuwaua vibaya mwanamke na mtoto mdogo? tena eti ni familia yangu? yaani mke wangu na mwanangu mwenyewe!!? aaaaaghhhhh!!!!! kwa mara nyengine nilizimia tena katikati ya mateso yale makali.

ITAENDELEA...
10

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 12
========

Siku zilienda hatimae ilipita miezi miwili nikiwa segerea na ilifika tarehe ya kesi yangu ambapo siku hiyo asubuhi na mapema niliingizwa kwenye karandika sambamba na watuhumiwa wengine wenye kesi tofauti tofauti na safari kuelekea mahakamani ilianza tukiwa chini ya ulinzi mkali.

Tulifika kwenye viwanja vya mahakama kuu na kutelemshwa ambapo siku hiyo niliushuhudia umati mkubwa ulifurika huku wengi wao wakinyoosheana vidole kuelekezea kwangu ndipo nilipobaini kuwa ni kweli kesi yangu ilikuwa ni moja ya habari iliyotikisa.
Zamu yangu ilipofika nilifikishwa kizimbani na siku hiyo sikuwa nalia kama ilivyokuwa siku ile ya kwanza.
Nilimudu kutazamana na watu waliokuwepo mule ndani ya mahakama japo wengi wao walinitazama kwa jicho baya lakini niliwapuuza na kuwasikitikia kwa kutojua walitendao.

Macho yangu niliyaelekeza kila pembe ya mahakama kwa umakini mkubwa nikimtafuta ba mkubwa na kweli nilimuona nae alikuwa ananitazama na kunipa kwa kuinamisha kichwa kuwa yupo pamoja nami na nilitegemea pia ushahidi wake pekee kuwa ndio utetezi mkubwa kwangu.
Niliendelea kuangalia kona nyengine kwa makini kujua kama kuna mwengine ninayemfahamu kaja kusikiliza kesi yangu na kipindi hiko hakimu alikuwa ndio anaanza kuisoma tena ile kesi nami ktk kupepesa pepesa macho huku na kule nilimuona rafiki yangu kipenzi yule aliyenitembelea segerea na tulipokutanisha macho alitabasam kwa kunionesha ishara kuwa yuko pamoja nami.
Nilijisikia faraja kwa namna furani na kumshukuru mungu kwa kuwajua rafiki na ndugu wa kweli kwangu kwani ni vigumu kumtambua rafiki wa kweli au ndugu wa kweli kama hujapatwa matatizo makubwa.
Siku hiyo ndio nilizidi kuielewa na kuimbuka misemo mingi ya wahenga ambapo awali nilichukulia kama burudani tu kwa watoto lakini baada ya majanga nikakubali kuwa Akufaae kwa dhiki ndie rafiki pia umdhaniae sie ndie, kwani sikuamini kama mjombaangu aliyetoka tumbo moja na mamaangu angeweza kunisariti na kutofika ilihali nilimthamini na kumsaidia sana huku nikimpuuza ba mkubwa kuwa ana mila za kizamani lakini leo hii niliyempuuza ndie kaja kunifariji jera na mahakamani yupo ila yule niliyemtegemea awali hata salamu zake za kunifariji sikuzipata. Ina maana ameamini mimi ni muuaji na katili kwa kiasi kile? aaah kweli binaadam hukukimbilia pindi mungu anapokupa neema lakini hukukimbia pindi anapokupa mitihani.

Lakini wakati nilipogeuza shingo upande wa kushoto karibu na alipokaa rafiki angu nilishangazwa mno na kile nilichokuwa nakiona safari hii.
Aaaagh!! moyo wangu uliripuka na kupiga paah! huku nikiwa siamini pindi nilipokutanisha macho na mtu ambae nilimtambua vizuri sana tena sana nae alinitambua vizuri tu nilivyo.
Mtu ambae niliamini ni adui yangu lakini macho yake hayakuonesha kuwa yana uadui na mimi kwani yalipokutana na yangu tu yalianza kutoa machozi na kunihurumia akionesha kuwa eti ameumizwa na kesi yangu nae kaja kuniunga mkono.
Machozi yake ndio kwanza yalinichefua zaidi kwani akili yangu ilinambia kuwa 'Huyu nae anahusika kwa haya yaliyokukuta'
Msschhhhhh...!!! Na ndipo nilipojikuta natoa sonyo kali sana lililosikika vizuri mahakama nzima kutokana na utulivu uliokuwepo na muda ule kumbe Hakimu alikuwa ananiuliza swali juu ya shtaka langu lililopaswa nijibu kweli au si kweli lakini kutokana na kuhama kwa mawazo yangu nilijikuta nasonya wakati mahakama imenitegea sikio mimi kusikia jibu langu kama nakili au nakana shtaka..!?
Aaaaaaaaaaaaaagh!!!!
Ama kweli ulimi unaponza Kichwa

" Kutokana na kifungu namba 279 sheria ya mahakama iliyopitishwa na kuhakikiwa upya mwaka 1972 kuwa mtu yeyote hata akiwa mtuhumiwa endapo ataonesha lugha yoyote inayoashilia aidha matusi au dhalau ndani ya mahakama hilo ni kosa la jinai na adhabu yake ni kuisimamisha kwanza kesi husika na kupitisha kifungo cha miezi kumi na mitatu jera sambamba na kazi ngumu na bakora kumi. tano siku ya kuingia na tano siku atayotoka na kama muhusika alikuwa mtuhumiwa inapaswa kutorudi uraiani ila baada ya hapo atarudishwa mahakamani ndipo kesi yake husika itatajwa tena na kusikilizwa.
Nami kwa kufata kanuni na sheria hiyo nakuhukumu bwana Hussein Bakari kwenda jera kwanza mwaka mmoja sambamba na adhabu hizo nilizozitaja ili ukajifunze kwanza adabu na heshima ili utaporudi tena mahakamani uoneshe utiifu na adabu nzuri..."

Nilistushwa mno na maneno yale toka kwa hakimu yule wa kike licha ya kwamba niliomba msamaha tena kwa kupiga magoti mara baada tu ya kusonya na kukumbuka kuwa nipo mahakamani lakini hakimu hakuonesha hata chembe ya kujali kile nilichokisema na baada tu ya kutamka maneno yale aligonga nyundo mezani mara tatu ndipo askali wakaja kunitoa pale kizimbani na kunifunga pingu ambapo nilimgeukia tena yule hakimu kwa uchungu nikamuangalia na yule mtu alieniponza ambae alikuwa ni mwanamke amemshika mtoto mdogo nae wa kike wa umli wa miaka kama mitatu hivi.
Hakuwa mwengine yule mwanamke bali ni Mariamu yule mwanamke wangu wa kwanza kumpa moyo wangu na kumthamini nikitegemea atakuja kuwa mke wangu lakini kwa alichonitendea na kunisariti huku akinikana mchana kweupeee na kunisababishia maumivu makubwa ya kutendwa kwa mara ya kwanza.
Nilimuangalia kwa jicho baya sana Mariam aliyekuwa analia machozi ambayo niliamini kuwa ya kinafki kwani kama kweli alikuwa ananipenda na kuniulumia mbona hakulia siku ile niliyokuwa nachezea kichapo kwa baunsa wake hadi almanusura ninyofolewe roho lakini ndio kwanza alivunjika mbavu kwa kicheko pale nilipotimua mbio kujinusuru..
Eti leo hii anajifanya kunisikitikia na kunililia kwa lipi hasa yaani nipo ktk mkondo wa sheria anajifanya kunililia ila nilipokuwa kwenye mkondo wa mtu aliyekuwa anajichukulia sheria mkononi alinicheka..! kama si unafki nini? Nilimuangalia zaidi kwa jicho baya kila mwanamke niliyemuona mbele yangu muda huo nikiona wote ndio wale wale na hapo ndipo ilipokuja sauti ya yule mlemavu kichwani mwangu kanakwamba ananinong'oneza na kuisikia kwa mara ya kwanza kabisa ikinipa pole na kunambia hivi...

' ' 'Usimshangae hakimu wala yule aliyekufanya usonye kwa sababu wote ni wanaake Hussein.
Wengi hawawajui walivyo lakini ni wazuri tu kwa nje ila mioyo yao mibaya sana japo ina huruma na imezungukwa na hofu lakini inaponzwa na vichwa vyao wanavyoviacha wazi ambavyo vina ubongo wenye kiza ambao shetani hupendelea sana kujificha ndani yake na kuwaongoza anavyotaka na kuwafungia milango ya kufikiria katika maamuzi yao na ndio maana wanafanya vitu vya ajabu mara nyingi hata wanapojidhalilisha wao wenyewe hawajioni na wanachukulia sawa tu.
ona Mwanaume una ubongo mng'avu unaoweza kummulika na kuusaidia ubongo wa mwanamke na kumuongoza vizuri lakini kwa kuwa shetani hataki hilo na amejiekea makazi kiurahisi kichwani kwa mwanamke huyo ndio sababu utapomwambia ukweli huu lazima kwanza akasilike na kukuchukia akidhani hata yeye ana haki ya kukutawala na kukuongoza pia hataki kuongozwa akiziamini akili za kichwani mwake zinazoongozwa na shetani kuwa wanaake na wanaume wote sawa na wapo ktk daraja moja hivyo ujue Hussein wanaake wote wenye imani hii wasiotaka kujishusha mbele ya wanaume hao ndio miongoni mwa wauaji na waliopotea na hawana soni wala haya kwenye nyuso zao...
lakini utapoona umemwambia haya mwanamke nae hajakasirika wala kukuchukia na akakili kuwa yuko chini ya mwanaume basi huyo mwanamke ni miongoni mwa wanaake wa peponi waliobarikiwa na mungu ambao wamefanya jitihada kubwa binafsi za kumfukuza shetani vichwani mwao na aina hii ya wanaake hupenda sana kujishusha na hawajifanyi kujua zaidi mbele ya wanaume na wanaake hawa hupenda kufunika vichwa vyao si kwa nguo tu bali nyuso zao zimejaa soni na haya hata wanapokutana njiani na wanaume basi huwapisha huku vichwa vyao wakiviinamisha chini.
Lakini kwa karne hii ya sasa wanaake hao wamekuwa hadimu na ni wachache mnooo Hussein wengi waliobaki ni Wauaji watupu hata wale wanaojifanya wanapenda dini karne hii lakini ona tabia zao tofauti kabisa na mafundisho ya hizo dini, ona Hussein ona wengine wanaenda makanisani wakiwa wamevaa viguo vifupi na visuruali vya kuwatega wanaume na kufanya waharibu ibada zao hawana haya si kwenye makanisa tu hata kwenye misikiti na madrasa huoni Hussein wanaake wanavaa mahijabu kama mapazia? vigauni kama vyandarua pamoja na kanga nyepesi kama karatasi? yoote hii kuwaponza wanaume tu na kuwaharibia ibada zao kwa kuwasababishia dhambi kimakusudi lakini bado ukiwaambia watakukasilikia.
Na mwanaume ataposhindwa kuutumia vizuri ubongo wake akiwa na mwanamke na kujifunza jinsi ya kuishi nae basi ndio hutokea majuto mwishoni kama haya ya kwako Hussein.
Kumbuka wanaake huwa hawafikirii kwanza kabla ya kunyanyua midomo yao na siku zote wanajiona wao wanaonewa na kuhisi wanaume wanapendelewa bure tu hivyo wanapopewa nafasi au wadhfa kama wa yule hakimu hupenda kujionesha kuwa nao wanaweza kwa msukumo wa shetani na ndio wanapoonesha makucha yao wakitaka ushindani kwani amini laiti hakimu yule angekuwa mwanaume kwanza angekuonya kwa maneno tu kesi ingeendelea na kama ungerudia tena ndipo angekupa hiyo hukumu lakini ndio hivyo Hussein usishangae sana wala usiumie kwa sasa kwani hao ndio wanaake bwana nilikwambia usiwaamini sana uwe makini nao ukapuuza.... wanaake ni wauajiii Hussein usiogope kusema haya maneno popote ili uwaokoe na wanaume wengine wasikie na waelewe wakajifunze jinsi ya kuishi nao .
ITAENDELEA.......
12

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 13
========

Hussein waambie ... waambie sasa... waambieeee kwanguvu wasikiee waambieee usiogopee .. usiogopee usiogopeeeeee.... ' ' '

Baada ya kusikia maneno haya ktk fahamu zangu nilijikuta napata ujasiri na kupayuka kwa nguvu pindi napandishwa kwenye karandinga na kusema
WANAAAAAAKEE NI WAUAJIIIIIII
Na hii ndio ikawa mara yangu ya kwanza kutamka maneno haya hadharani.

* * * *

Siku zilienda ambapo muda wote toka nianze kutumikia kile kifungo cha mwaka mmoja sikuwa na rafiki jera wala sikutaka urafiki na yeyote yule nikiamini rafiki angu ni mmoja tu yule aliyekuja kunitembelea na ndugu yangu ni mmoja tu nae ni ba mkubwa tu basi lakini hawa wengine wote wataniongopea kwa kuwa tupo ktk hali moja tu wakitoka kila mtu atafata yake kwani niliokuwa nao uraiani nao walinisapoti kwa kuwa tulikuwa ktk hali moja ila leo nimepata matatizo mabaya tena ya kusingiziwa lakini wote wamenigeuka na kuniacha peke angu hivyo baada ya hapo ndio nikaanza kuwa na tabia ya kukaa peke angu na kufanya kazi kwa nguvu muda wote na inapofika wakati nikikumbuka matukio yaliyonikuta na hadithi za yule bwana ambazo zilikuwa zinanijia kichwani mara kwa mara huku nikiisikia sauti yake na hapo ndio nasemaga makusudi kuwaambia wengine kuwa 'Wanaake ni Wauaji' japo wengi waliishia kuniangalia na kudhani kuwa nimerukwa tu na akili.

Siku zilipita hatimae kifungo changu kiliisha na baada ya kufanyiwa vipimo nilikung'utwa bakora zangu tano zilizobaki na siku chache mbele baada ya kupata uwezo wa kusimama nilifikishwa tena kizimbani.
Eee.. asikwambie mtu zile bakora heri uzisikie tu kwa wenzako usiombe zikukute kwani ziko tofauti na bakora za shule nilizozizoea yaani fikiria bakora tano tu mtu wa mazoezi kama mimi nilishindwa kusimama, kama una afya mgogoro unaweza kukata upepo kabisa (kufa).

Basi baada ya kufika kizimbani na hakimu alikuwa yuleyule mama kesi ilianza tena kuunguruma ambapo kwa upande wa mashtaka ambao ilikuwa serekali wenyewe ulileta ushahidi mbali mbali zikiwemo zile nguo nilizovaa za tukio panga na kiganja cha mtoto ambacho kilihifadhiwa muda wote na nilipoulizwa kuhusu kuvitambua vile vitu ambapo nilikubali kuzitambua nguo tu kuwa ni kweli zilikuwa za kwangu lakini vile vyengine vyote nilikataa ndipo alipopanda daktari aliyenichukua alama za mikono baada ya kukamatwa na kuleta majibu ambayo yalikuwa yamefanana na alama za mikono ya mtu aliyelitumia lile panga hali ile ilinishangaza pia kwani nilishasahau kuwa kweli niliwahi kulishika lile panga lakini sikulitumia kudhuru chochote.
Ushahidi wote na maswali ya mawakili yalizidi kunibana na nilichoka zaidi baada ya kupanda dogo aliyethibitisha kuuona ugomvi baina yangu na mke wangu tukigombania mtoto huku nikiwa na panga mkononi ambapo yule dogo alikuwa chini ya miaka kumi na nane na alihesabika kama mtoto kwa mujibu wa sheria iliamini hasemi uongo.
Niliumia sana na kumtazama yule dogo alivyovuka mipaka kuongea kitu ambacho hakikutokea hadi akawa anatoa machozi pale mahakamani kukazia uongo wake.

Niliamini kuwa nimekwisha na nilishindwa kupiga kelele kumstopisha yule dogo nikihofia yasije kunikuta yale ya mwanzo na kumuacha anikandamize tu lakini baada ya yule dogo nilistuka pindi niliposikia anatajwa shahidi upande wa mshtakiwa na moyo ulipata faraja kidogo mara baada ya kumuona ba mkubwa akisogea kizimbani nami nilimtazama kwa jicho la kushukuru kwani nilijua yeye ndie tumaini pekee kwa muda ule lakini alipopanda na baada ya kuapishwa akaanza kuzungumza ba mkubwa maneno yaliyosafirishwa kwa sauti yake mwenyewe na yalipenya vizuri masikioni mwangu na kuingia ktk milango yangu ya fahamu kabla hayajaenda kutua kwenye moyo wangu na kuufanya ustuke kupita maelezo huku nikijihisi viungo vyangu vyote vimeshindwa kufanya kazi hadi macho yalishindwa kupepesa na kubaki yameganda kwa ba mkubwa kwa kutoamini kama ndie yeye au..? aaaaah!!!!! sikuamini hata kidogo kile nilichokisikia.

Nayakumbuka vizuri maongezi yale baada ya kuapishwa ba mkubwa na wakili yule wa serekali alisimama na kumuuliza kama ananitambua nae akasema ananitambua kisha wakili akamuuliza tena.
"Unamtambua tambua vipi mtuhumiwa hebu ifafanulie mahakama.."
"Ndio namtambua bwana Hussein Bakari kama mwanangu kwani ni mtoto wa marehemu mdogo wangu wa tumbo moja.."
aliongea ba mkubwa kisha wakili aliendelea kuhoji..
" Sawa, kumbe Hussein ni mwanao kwa namna moja je una lipi la kuiambia mahakama juu ya kesi inayomkabiri mwanao ?"
" Nipo hapa kwa ajili ya kutoa ushahidi kwa kile ninachokijua kuhusiana na tukio zima na kesi inayomkabili mwanangu"
Aliongea Ba mkubwa maneno yake ya awali ambayo yalinipa moyo kuwa amekuja kunitetea na kuongea ukweli lakini mara baada ya hakimu kumruhusu aongee kile alichokijua ndipo nilipostaajabu kumsikia ba mkubwa akisema....

" Muheshimiwa hakimu nakumbuka miezi miwili kabla ya tukio mwanangu Hussein alikuja katika kijiwe changu kwani mimi ni mtaalam wa tiba asilia na alionesha hali ya kuchanganyikiwa kidogo ambapo nilipomuuliza kulikoni hakunambia ukweli zaidi ya kusema maisha yanamchanganya kisha akaniuliza ktk dawa zangu hivi sina dawa ya kumfanya mtu awe tajiri? hapo nilicheka na kumwambia mwanangu kuwa hutajiri hauletwi kwa dawa bali ni juhudi tu binafsi ktk kazi na kujituma kimaisha bila kusahau kumuomba mungu . Aliondoka siku hiyo lakini miezi miwili baadae wiki moja kabla ya tukio nilipigiwa simu na mkwe wangu marehemu mkewe mwanangu Hussein na alinambia kuwa wana matatizo makubwa na ugomvi baina yao kuhusu mtoto ... Na nilipouliza zaidi kulikoni ndipo mkewe alinambia kuwa kutokana na kuchoshwa na ugumu wa maisha mumewe alienda kwa mganga mmoja ambae hakunitajia ni wapi na anaitwa nani lakini alichosema ni kuwa alienda kwa lengo la kupata dawa ya kuweza kuwa tajiri ili wajikwamue na maisha magumu waliyokuwa nayo.
Na mganga wake alimwambia masharti ya dawa hiyo ili itengenezwe inapaswa amtoe kafara mamaake mzazi au mtoto wake mwenyewe na apeleke kiganja chake ndipo atafanyiwa hiyo tiba na kuwa tajiri hivyo kwa kuwa mamaake alishafariki na pia alikuwa na mtoto pekee ndipo alipomfikishia mkewe habari zile na kumshauli wamuue tu mtoto wao ili watajirike na baadae watazaa wengine lakini mkewe alimkatalia na ndipo ugomvi ukaanzia pale. Nami kwa busara zangu siku moja kabla ya tukio mapema nilipiga simu ambapo nikasikia ugomvi mkubwa baada ya simu kupokelewa na baadae ndipo alipoanza kuongea mkewe ambapo niliwaomba waje kwangu nia na madhumuni nimuonye mwanangu Hussein kwa kile anachotaka kukifanya kwani safari ile nilimsikia kwa masikio yangu na kwa bahati nzuri nilimrekodi.
Lakini cha ajabu alimlazimisha mkewe na kuamua kuja kesho yake usiku na kutokana na mazingira ya kule kuwa polini ndipo alipata nafasi ya kufanya tukio.
Ki ukweli muheshimiwa Hakimu na wazee wa baraza inauma sana kuusema ukweli huu kwani Hussein ni mwanangu lakini nikiongopa kwa ajili ya kutetea nitakuwa nimejiekea mzigo wa dhambi tu mbele za mungu... na nina ushahidi wa record ktk simu niliyopiga siku hiyo. ila ninachoomba cha mwisho muheshimiwa mumsamehe tu mwananguu...uuuuh..."

Aliongea ba mkubwa na kumalizia kwa kilio kisha ilitegwa kwenye mike ile simu yake aliyosema kuna hiyo record na kweli mara spika zilizokuwa kwenye mahakama zilianza kutoa sauti na kweli ulisikika ugomvi wa mwanaume na mwanamke wakigombania kumuua mtoto wao ambapo nilizidi kustaajabu kwani sauti ya mwanamke kweli ilikuwa ni ya Zai wangu na pia sauti ya mwanaume ilifanana kabisa na yangu japo kiukweli hatukuwahi hata siku moja kuzozana na Zai lakini daaah!!! mchezo niliofanyiwa pale ulinichosha sana na kuamini kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni ina maana hawa watu waliikopi hadi sauti yangu na kuiigizia?
Imekuaje ba mkubwa nae ameshirikiana nao kuniangamiza ilihali awali aliapa kunisaidia?

Basi ba mkubwa alipomalizia kunipigilia msumali wa moto kwenye utosi sikuwa na cha zaidi zaidi ya kukubali kuwa sina jipya hata nikitolewa kuwa huru sitokuwa na manufaa yoyote ulimwenguni hivyo nikamuomba mungu ipitishwe hukumu ya kifo juu yangu ili nikapumzike kwani maisha ya dunia ndio basi yameshanisariti.
Lakini hakimu aliisogeza kesi tena kwa kutakiwa nikafanyiwe vipimo vya ubongo kama sikuwa na tatizo lolote la kiakili kwani kwa mujibu wa katiba serekali haikuamini uchawi na imani za kishirikina na majibu ya daktali ndio yataongoza na kuisaidia hukumu husika.
ITAENDELEA,,,,,,
13

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 14
========

Kesi iliahilishwa na kufanyiwa vipimo na mwezi mmoja baadae nilirudishwa tena kizimbani ambapo daktari alithibitisha kuwa sikuwa na tatizo lolote la ubongo linaloweza kuafect akili zangu kwa hiyo vipimo vya kichwa vilionesha niko safi kabisa.
Na hapo ndipo hakimu aliponigeukia na kuniuliza kama nina lolote la kujitetea..?
Nilimuangalia hakimu yule ambae safari hii hakuwa yule mama na nilistaajabu sana kwani haikuwa kawaida japo nilipokuwa gerezani baadae ndipo nilisikia habari kuwa yule mama wiki moja kabla ya kesi alipatwa ajali mbaya iliyomfanya alazwe wiki nzima i.c.u na siku niliyohukumiwa nae alifariki siku ileile....
Basi, nilimuangalia yule hakimu na kumwambia kuwa..
"Ndugu Hakimu, mimi ni mkosaji niliepoteza nafsi za watu, sina chochote cha kujitetea kwa kuwa tayari nipo mikononi mwa sheria. Ninachosubiri tu nilipwe ujira sawa kama nilivyoifanyia familia yangu ili niwafate huko walipo.
Naiweka nafsi yangu mikononi mwa mahakama hii tukufu niko tayari kuhukumiwa."

Maneno yangu yalimshangaza kila mtu aliyekuwa pale mahakamani mpaka hakimu mwenyewe nilimshuhudia akishusha miwani yake ya macho chini kidogo na kuniangalia vizuri kisha akaipandisha tena kuwaangalia wazee wa baraza na baada ya kimya kama cha dakika tano ndipo hakimu aliposoma hukumu yangu.

......
"Bwana Hussein Bakari, baada ya mahakama hii tukufu kufanya uchunguzi yakinifu kwa kuzingatia sheria na taarifa za mashahidi mbalimbali na vipimo vya madaktari juu ya tukio lililotokea la mauaji.
Mahakama inakutia hatiani moja kwa moja bwana Hussein Bakari kwa kosa la mauaji ya mke na mtoto.
Na kupitia kifungu namba 94 sheria ya mahakama iliyopitishwa mwaka 1981 kuwa endapo mtuhumiwa wa kesi ya mauaji ikaonekana dhahili aliua kwa makusudi basi hukumu yake ni ya kifo moja kwa moja.
Lakini pia kifungu hiki kilihakikiwa upywa mwaka 1990 kuwa endapo mtuhumiwa huyu akakili na kuonesha kutubia kosa lake kabla ya hukumu basi mahakama itaangalia chaguo juu ya hukumu yake aidha ahukumiwe kifo anyongwe ama ahukumiwe kifungo cha maisha jera na kazi ngumu.
Nami kupitia kifungu hiki cha mwaka 1990 nakitumia kukuhukumu bwana Hussein kutokana na majuto uliyoyaonesha mbele ya mahakama kwenda jera kwa maisha yako yote yaliyobaki sambamba na kazi ngumu. Na hii iwe fundisho kwa watu wote wenye tabia kama hizi kutaka mafanikio kwa njia haramu na kusababisha vifo vya watu wasio na hatia.
Mwisho wa kuhukumu... Askari mchukueni kufungo chake kimeshaanza sasa. "
............

Aliongea yule hakimu nami sikulidhishwa na hukumu ile huku nikisisitiza kwanini nisingehukumiwa kifo.?

" Hapanaa Hakimu umekoseaaa.... kumbuka aliyeua anapaswa auaweee.... niueni tuuu... Niueniii tuuu hiyo sio hakiii.."

Nilipiga kelele hadi walionichukia wakawa wananishangaa na kunihurumia ndipo nilipoingizwa kwenye karandinga na muda mfupi baaadae safari ilianza kwenda kutumikia kifungo changu.
Lakini nikiwa nachungulia kwa nje ndipo nilishangaa kuna mtu alikuwa akilikimbilia gari lililotubeba na kulisimamisha huku mkononi mwake akiwa na barua.

Askali walijaribu kumzuia lakini alilalamika huku akiinyoosha juu ile barua japo sikumsikia alichokuwa anaongea lakini nilimtambua vizuri mwanamke yule ndie alikuwa ni Mariam aliyenitenda hapo awali na sikujua alikuwa na jipya gani na kama barua ile ilinilenga mimi ni kwa nia na dhumuni gani hasa.
Nilipotezea na kuzungusha shingo yangu ndani na kuinamisha kichwa chini kwani sikupenda kabisa kuendelea kuuona uso wa mariam kule nje na hatimae gari iliingia barabara kuu na safari ya kwenda kumalizia ngwe iliyosalia ya maisha yangu ikaanza huku kichwani mwangu nikilaumu kwanini sikuhukumiwa kifo moja kwa moja.

Nilifika kwenye hili gereza kwa mara ya kwanza na baada ya kupewa namba na kukabidhiwa sale maisha mapya yakaanza rasmi lakini siku chache tu tukiwa tunavunja mawe eneo moja niliitwa na afsa magereza mmoja na kunikabidhi barua ambayo ilinitonesha zaidi na kuniliza pia na siku hiyo niliapa kuwa sitozungumza na yeyote kuhusu yaliyonikuta kwani sikupenda niendelee kujitonesha maumivu haya ya kihistoria kwenye maisha yangu.
Kwa muandiko tu wa ile barua nilijua fika imetoka kwa Mariam kwani hati yake niliielewa vizuri ndipo nilipobaini kuwa huenda hii ndio barua aliyoikimbizia siku ile nilipohukumiwa na kuna askali mmoja aliichukua kati ya wale waliomzuia.
Nilitulia kwenye kivuli na kuanza kuisoma ile barua ambayo ilikuwa imeandikwa pande zote mbili za karatasi kutokana na urefu wake sitoisahau hii barua ambayo ilikuwa ya mwanzo na mwisho ktk makazi yangu mapya haya ya jera na ilianza kwa kusema...
.............
" ''Najua sikustahiri kusogea mbele ya macho yako kutokana na yale niliyokutendea siku za nyuma lakini naomba unisamehe ndani ya nafsi yako ili hata nitapokufa niwe nimejipunguzia walau uzito kidogo ndani ya mzigo wangu mkubwa wa dhambi.
Ukweli nilikupenda lakini sikuwa mke mwema kwako.
Nilikuwa msariti wa penzi lako kwa kufata maneno na ushauli wa shoga zangu kuwa mwanaume mmoja hatoshi kwa mwanamke mrembo mwenye kuhitaji mambo mazuri kama mimi na hivyo ndivyo ilivyokuwa hata pale nilipokukasirikia nilimpigia simu na kumfata bwana mwengine ambae nae aliamini mimi ni wake pekeake na ndie yule mliyepigana kule beach.
Madhumuni ya barua hii si kukuumiza kwa kukukumbusha yaliyopita bali ni kukutaka ujue kuwa una damu yako inayoishi uliyoitumbukiza tumboni kwangu miezi michache kabla hatujatengana.
Na hata siku ile ya mwisho niliyokuja kwako nilipanga kukufanyia suprise ya kukwambia swala hili lakini habari ile ya kwamba wanaake sisi ni wauaji ilinikera mno kwa kuwa alichokuwa anaongea yule bwana kilinirenga kweli na kuna mengine yalinigusa kabisa na kuniumbua moyoni.
Nilikuchukia na kujaribu kuitoa ile mimba baada ya kuachana lakini ajabu ilishindikana na kuendelea kukua hali iliyofanya kuachwa na mabwana zangu wengine baada ya kila niliyemsingizia kuikataa kwa kugundua hesabu ya miezi.
Ukweli mwezi ule nilionasa sikutembea na mwanaume yeyote zaidi yako na hata ukipiga hesabu mwezi niliojifungua na umli wa mtoto utakumbuka kila kitu.
Najua imekuwa too late na laiti ningejua awali ningekwambia ukweli tu lakini baada ya kusikia majanga yaliyokukuta nafsi imeniuma sana na mimi ni mmoja kati ya watu wasioamini kabisa kama kweli ulifanya mauaji yale.
Niliisikia sauti yako siku ile mahakamani uliposema kuwa Wanaake ni Wauaji nami moyoni sikuchukia kama siku ile na nilikubaliana nawe kwa namna frani nahisi hata kesi yako umeponzwa na mwanamke.
Nasikitika ninapomuangalia huyu mtoto ninayemuacha katika hali ya uyatima kwani hapa nilipo nimegundulika nina kansa ya koo na sitoweza kupona kwa mujibu wa ripoti ya daktari kuwa imesababishwa na uchafu mwingi wa mbegu mbovu za kiume uliokuwa unapenya kwenye vijitundu vya ulimi wangu na kwenda kurundikana kooni na kutengeneza wadudu wabaya walioanza kushambulia koo pasi namie mwenyewe kujua.
Usishangae Hussein huo ndio ukweli, na hii yote ilisababishwa na tabia yangu ya muda mrefu kupenda kunyonya tupu za wanaume tofauti mara kwa mara kwa lengo la kuwachanganya kimapenzi ili nipate kuwachuna vizuri lakini leo hii najuta kwa kukiona kifo changu kikiwa kimenisimamia nikiwa kwenye umli mdogo bado na kumuacha mtoto ambae najua hatomuona tena babaake kutokana na hukumu uliyopewa.
Nilikuwepo nae siku ile ya kesi yako na alilia sana pindi ulipotolewa kwa kusukumwa huku ukipigwa kuingizwa kwenye karandinga baada ya kusonya mahakamani...
Nakuombea mungu akunyooshee mkono wa kheri na atende muujiza kifungo chako kiwe chepesi.
Mtoto huyu anaitwa Asha na kwaajabu ya mungu nyuma ya shingo yake karibu na sikio amezaliwa na alama kama ile uliyokuwa nayo na sasa ana miaka mitatu na miezi sita.
Japo nae ni wa kike lakini huko ulipo naomba umuombee ili asije potezwa katika mkumbo na kuwa miongoni mwa Wanaake Wauaji.

Ahsante kwa kuisoma barua yangu....
Ni mimi mfu mtarajiwa MARIAM

...............
ITAENDELEA....
14

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 20
========
Basi mwanangu miaka ikasonga hadi hii leo maisha yanasonga kila mtu amesahau habari za huyo Mr.X na hadithi yake imebaki kuwa siri ya sisi watu wanne tulio hai japo kovu lake mioyoni mwetu bado lipo.
Pia ukweli ni kwamba hakuna aliyejua siri ya kuwa Mr.X ni nani zaidi ya baba mwenyewe mzee Mnyungunyungu na endapo akifariki ndio basi na ukweli unaoutafuta utakuwa umekufa rasmi. ' ' ' '


......................................

* * * * * *

Alimaliza kuhadithia juu ya alichokijua kuhusu Mr. X yule bwana na story hii ilimfanya kwa mara nyengine Kamishna Shebby kudondosha chozi hasa mara baada ya kujua unyama waliofanyiwa familia ya mzee Mnyungunyungu na kuelewa sababu za kuhama kwao hata akapata hisia na taswira ya picha kwa kuunganisha na story ya Hussein alibaini kichwani mwake kuwa ba Mkubwa hakumsariti kwa makusudi mwanae kutokana na ushahidi alioutoa pale mahakamani inawezekana alimkandamiza Hussein kwania ya kuikomboa familia yake iliyokuwa mikononi mwa Mr. X ambae ndie alikuwa adui wa Hussein babu bubu.
Lakini swali bado lilibaki pale pale kuwa huyo Mr. X alikuwa nani?

Jibu hili alijua aliamini ni mtu mmoja tu ndie analo ambae sasa ni mzee sana na yuko hoi taabani kwa ugonjwa wa muda mrefu na hakuitajika kusumbuliwa.
Sasa alijiuliza moyoni Kamishna Shebby je ina maana safari yake iishie pale na kurudi na majibu yale tu bila kujua siri walau jina halisi tu la huyo mr x na kazi aliyokuwa anafanya? atawezaje kuifufua kesi ya miaka mingi bila kuwa na maelezo ya ushahidi yakinifu utaoeleweka mbele ya mahakama? ataonekana ni Askali kiongozi mzembe kiasi gani kwa kuyaamini maneno ya mfungwa tena wa miaka mingi juu ya kesi iliyokaribia kumzidi hata umli bila kuwa na ushahidi wa kutosha na vielelezo muhimu?
Bado aliamini ni sehemu moja tu na ni mtu mmoja tu awezae kumpa mwanga kwenye njia ya kiza anayotaka kupita kwenda ulipo ukweli wenyewe kwani aliamini endapo atafanikiwa kumjua Mr.X na kumkuta angali yu hai basi yeye ndie atafumbua mafumbo yote tena kiurainiii kutokana na mbinu alizokuwa nazo Kamishna Shebby alizozijua mwenyewe.
Aliamini kuwa hakuna ujanja wowote pa kuupata huo mwangaza zaidi ya kuongea na Mzee Mnyungunyungu walau maneno machache tu hata na alikuwa tayari hata kwa kulazimisha endapo watajaribu kumzuia kuonana nae.
Lakini akiwa bado anatafakari Kamishna Shebby juu ya kutaka apelekwe kumuona mzee Mnyungu nyungu na kabla hajazungumza kitu mara aliingia yule kijana mjukukuu wa Mnyungunyungu aliyewapokea pale nje na kuita.
"Baba .. babaa.. kuna wazee wamekuja Unahitajika haraka nyumbani babu amezidiwa sana.."
Maneno haya yaliustua mno moyo wa Kamishna Shebby na kukurupuka sambamba na yule bwana pale chini kwa lengo la kuwahi huko alipo mgonjwa huku moyoni akisali na kuomba mzee Mnyungunyungu asifariki kabla hajamwambia Mr.X alikuwa nani.

Walitoka nje na kuwakuta wale wazee wakiwasubiri huku st;sajent Kimaro nae akiwa kasimama na alipomtazama Kamishna Shebby kwa kukutanisha nae macho alimuuliza kwa ishara za kiaskali kama amefanikiwa lakini Kamishna hakumjibu zaidi ya kumpa ishara waongozane na wale wazee haraka waelekee kule wanapoenda.

Baada ya mwendo mfupi walifika kwenye nyumba moja kubwa ambapo ilionekana wazi walioishi pale wote ni watu wa familia moja huku kila waliemuona pale nje akionesha uso wa huzuni kasoro mama mmoja wa makamo ambae alionekana akiwa anacheka cheka na kuchezea vitu ovyo.
Wenyeji waliingia ndani kwanza kuona hali ya mzee Mnyungunyungu ilivyo huku kina Shebby wakiachwa kwanza pale nje baada ya kukaribishwa na kina mama waliowakuta na kupewa vistuli.
Kichwani shebby alimtambua yule mama aliyeonekana wazi kurukwa na akili kuwa ndie yule mtoto wa mzee Mnyungunyungu aliyetendewa ukatili kipindi hiko na vijana wa Mr. X kwa mujibu wa hadithi ya bwana mganga mtoto wa Mnyungunyungu aliyekuwa nae kibandani muda mfupi uliopita.

* * *

"Vipi hao vijana ni wageni wako?"
Aliuliza kwa sauti ya chini mzee mmoja pindi alipokuwa ndani na yule bwana mganga wakiwa wamesimama wakimuangalia mzee Mnyungunyungu aliyekuwa anakoroma kiajabu huku wote wakijua sasa hakuna cha kumsaidia zaidi ya kungoja tu akate roho.
"Haa!! we acha tu kaka, hawa walikuwa ni wageni wa baba lakini ndio basi tena ashawakosa."
Aliongea kwa huzuni yule mganga na kusogea kitandani alipokuwa mzee Mnyungunyungu na kupiga magoti huku machozi yakim bubujika.
"Jikaze bwanaa vipi!!? usikufuru inapaswa tumuombee aondoke kwa amani akapumzikee"
Aliongea mzee mwengine aliyekuwa amepakata kichwa cha mzee Mnyungunyungu aliyelala pale kitandani pindi alipokuwa anahangaika na roho na kumzidisha machungu yule bwana badala ya kumtuliza kwani licha ya kwamba alijua babaake alikuwa mzee sana na kwa hali aliyokuwa nayo ndio basi tena hawezi kuamka lakini pia ilikuwa ngumu moyoni mwake kuukubali ukweli ule huku akifikiria juu ya siri nzito anayoondoka nayo babaake.
Siri ya kuwa nani alikuwa Mr.X.!?

"Aaaagh!! baabaaaangu siaminiii mimii kama ndio unaniacha katika kipindi kama hiki huku ukiondoka na siri iliyofichika miaka yoteeee aaah.."
Maneno yale yaliwashangaza wazee wote waliokuwemo mule ndani wasijue ni siri gani huku wengine wakimsihi anyamaze na aache kukufuru kwani Mzee Mnyungunyungu alikuwa bado hajafa japo hakuonesha matumaini ya kupona.
"Nyamaza bwanamkubwaa usikufuruu"
Aliongea mzee mwengine aliyevaa kibaraghashia.

* * * *

Baada ya uzalendo kumshinda pale nje huku akiwazia juu ya jitihada zake kuwa zinaelekea kuzama hasa baada ya kuhisi kuna mtu analia kwenye chumba walichoingia wenyeji wake, ndipo Kamishna Shebby aliamua kujitoma mule ndani kwa taharuki kubwa kuhakikisha kama kweli mzee Mnyungunyungu ndio basi kashafariki.

"Eee Mola baba.. mpe walau dakika moja tu anitajie jina halisi la Katili huyo Mr. X.."
alijikuta analopoka Kamishna Shebby baada ya kuingia ghafra na kuwastua watu huku macho yake yakiangukia pale alipopiga magoti yule mganga huku kitandani akionekana Mzee Mnyungunyungu akitapatapa.
"MR. X !!!!!!??"
Kila mtu alitahayuri na kujikuta wanalitaja kwa pamoja hilo jina Mr. X kwani hakuna kati ya wale wazee aliyewahi kulisikia hilo jina.
Lakini cha ajabu walipotahayuri na kulitaja kwa mshtuko mkubwa lile jina walishangaa kusikia Mzee Mnyungunyungu akikohoa kwa nguvu mfululizo na kupunguza kukoroma ndipo ajabu ya mungu alifumbua macho kisha kugeuza shingo taratibu na kumtazama Kamishna Shaaban pale aliposimama mlangoni.
Watu wote walibaki wametumbua macho hata yule mganga mtoto wa mzee Mnyungunyungu alistuka na kusogea pembeni kidogo huku akimuangalia babaake kwa mshangao mkubwa kwani haikuwahi kutokea wala kusikia kuwa mtu anayetapa tapa dakika za mwisho akikaribia kutokwa roho akakohoa na kufumbua macho tena.
"Allahu akbar.!!" (Mungu mkubwa)
Alitaharuki yule mzee mwenye baraghashia huku nae akisogea eneo lililokuwa jirani na mlango waliposogea na wale wengine wakihofia huenda mzee Mnyungunyungu alitaka kuondoka na mtu ama si hivyo basi ule ulioamka ni mzuka tu ila ye mwenyewe kashakufa.
"Yesu wangu!!"
Alisikika mzee mwengine wa kilokole ambae yeye alitoka nje moja kwa moja kwa hofu na kuwahi alipokuwa anaishi kwa lengo la kufata biblia.
Lakini katika hali ya utofauti na kushangaza kamishna Shebby ndio kwanza alisogea haraka pale kitandani huku akipiga magoti na kuanza kumuongelesha mzee Mnyungunyungu kama vile amechanganyikiwa.
"Tafadhali mzee nakuomba nitajie tu huyo mtuu.. Naomba usiondoke na hii siri, nimemuona Hussein jela amenambia kila kitu najua hukumuangamiza makusudi ila jitahidi unambie alikuwa nani huyo Mr.X.."
Aliongea Kamishna huku akiwa kaishika mikono ya mzee Mnyungunyungu.
20

Sent using Jamii Forums mobile app
 
EPS 22
========

"Mh! mkuu hapaaaa daah!! okeeee.. auuu au alimaanisha kwenye picha?!!"
"Swadakta Kimaro, alichokuwa ananielekeza marehemu Mnyungunyungu nimepata siri ya maana ya hayo maneno kuwa mr.X aliwahi kupiga nae picha na dalili kuu ya kumtambua mr.X ana kovu usoni mwake kwa hiyo itatubidi tuibe siku mapema wiki hii twende mkuyuni tuombe picha zote alizowahi kupiga mzee Mnyungunyungu miaka ya nyuma."
"sawa mkuu sasa tutajuaje jina halisi la mr.X kama tutamgundua kwenye picha kwa ushahidi wa hilo kovu? kumbuka atakuwa kabadilika mno kwa sasa ila jina ndio la msingi zaidi, sasa tutajuaje hapo...?"
"Naam, swali lako ni zuri lakini usiwe na wasi kwani kabla hajafa mzee Mnyungunyungu aliwahi mwambia yule mwanae mganga kuwa mr.X anamfahamu vizuri tu. kwa hiyo tutapoiona picha ya mtu mwenye kovu ktk ulbamu ya mnyungunyungu ndipo tutapomuuliza mwanae yule atutajie majina ya mtu huyo, na alikuwa nani enzi hizo na hapo itaanza kazi moja tu ya kumtafuta."
"hapo mkuu sina swali kabisa, naona mipango imekaa vizuri sana Mr.X lazima afichuke safari hii."
Aliunga mkono st;sajent Kimaro mara baada ya kusikia mazungumzo ya Kamishna wake bwana Shaaban Mwinchande.

* * * * * *

Siku ya siku ilifika ambapo kwa mara nyengine alioneka Kamishna Shaaban na St;sajent Kimaro wakiwa moto chini ndani ya Land cruzer New Model ya kijivu wakipangusa (wakiyapita) magari na kukanyaga barabara ipasavyo kuelekea kijiji cha Mkuyuni mkoa wa Morogoro.
Muda mwingi kila mmoja alikuwa bussy na yake kichwani huku wakipeana story za hapa na pale na walipoianza barabara ya vumbi iliyokuwa inaelekea morogoro vijijini ndipo st;sajent Kimaro alivunja ukimya uliotawala muda mwingi na kuyapamba mazungumzo wakati huo akiendeesha gari.
"Sasa mkuu endapo tukishindwa kuiona hiyo picha ya mtu mwenye kovu usoni unafikiria nini cha kufanya ambacho kitatusaidia zaidi"
"Mh! sidhaani kwa haraka harakaaaa... lakini we umefikiriaje kwani"
"ahkah! mi nakusikiliza wewe bosi wangu niko tayari kutii mipango yako na kufata vile usemavyo."
"Sikia Kimaro, mapigo ya moyo wangu yanadunda kwa furaha furani ambayo naiona dhahili ni ishara ya ushindi na akili zangu zinaniaminisha kabisa kwamba safari hii tutamjua Mr.X tu."
"sawa mkuu lakini inabidi twende tukiwa na mbinu mbadala pia."
"Hebu nishauli mbinu mbadala uliyonayo."
"sawa mkuu, mi nadhani itatubidi tutumie mbinu za kijeshi zaidi kum bana yule mganga mtoto wa mzee Mnyungunyungu"
"Mbinu za kijeshi? kivipi Kimaro."
Aliuliza kamishna Shebby kwa mshangao kidogo huku akimtazama st;sajent Kimaro kwanini amefikiria hilo ilhali walishapanga awali kwamba ktk mission ile hawatatakiwa kujionesha ama kugundulika wao ni kina nani hasa.
"Mkuu kuna kitu nilikifikiria sana toka uliponipa habari ya maneno uliyoyaunganisha aliyotamka marehemu Mnyungunyungu na kunijengea wazo ambalo nahisi kabisa lipo jirani na ukweli ama ndio ukweli wenyewe."
"Wazo lipi hilo tena!! hebu nambie."
"wazo kuwa ni nani anaweza kuwa mr.X"
"Mh! Kimaro acha utani hebu nifafanulie unahisi nini?"
"Akili zangu zinanambia kuwa huenda yule mganga aliyetupokea akawa ndie mr.X mwenyewe"
"Mh! unamaanisha mtoto wa mzee Mnyungunyungu?"
"Haswaa ndie huyo."
"Kivipi sasa hadi umehisi hivyo?"
"kutokana na maneno uliyoyaunganisha aliyosema mzee Mnyungunyungu na ukijumlisha hadithi ya Hussein ukigawanya tukio la barua, namba ya simu hadi kushambuliwa kule kibamba miaka hiyo.. Pia umli wake vile nilivyomuona bado akili yangu inasema kuwa mzunguko woooote uko palepale yule mganga ndie mr.X"
"Daaah! Kimaro leo kweli umeamua kuchemsha kupe walio kwenye ndonga (kichwa) langu, Mh!! lete prove ya kile usemacho."
"Sawa mkuu ninazo sababu, Kwanza kumbuka mara ya kwanza mke wa Hussein ambae ni Zai alipoonwa na baba mkubwa wa Hussein ambae ndie mzee Mnyungunyungu alionesha hali ya mshangao sana hadi kupelekea kumpa maneno ya mafumbo Hussein juu ya yule mwanamke. Hii inanijengea picha kuwa mzee Mnyungunyungu alimtambua Zai mapema kabla ya pale, inawezekana mtoto wake ambae ndie yule mganga nae walishakuwa na mahusiano... kuthibitisha hili rejea kauli za Zai kuwa hajawahi kumkatalia mwanaume aliyemtongoza ila wote akawapa mitihani ktk kumtafuta aliyempenda kweli na walishindwa wote kasoro Hussein aliweza na kumpata Zai so mmoja wa washindwaji anaweza kuwa mtoto wa Mnyungunyungu.
Pili, barua ya Hussein huenda alipewa na yuleyule mganga kwenye daladala na kwa kuwa alizijua dawa nyingi kuna uwezekano barua ile ilibeba nguvu za giza ndani yake na pindi iliposomwa na mke wa Hussein ilianza kumlevya taratibu na kujikuta anaanza kufanya mawasiliano ya siri na yule mganga pasi na kujitambua na hata siku walipokuwa wanaenda kwa ba mkubwa inawezekana waliwasiliana tena kwa msg na yeye ndie aliyemny'ang'anya mtoto Hussein na kumshambulia akishilikiana na wenzake aliowajua yeye vilevile hata Mzee Mnyungunyungu alitoa ushahidi ule kwa kumkingia mwanae kifua na kuificha ile siri na ndio sababu ya kuhama kwao ili kupoteza kabisa habari zile zisije kuzuka tetesi pale kijijini.
Tatu, Kipindi unamuuliza swali marehemu Mnyungunyungu juu ya mr.X kuna uwezekano mlaika mtoa roho alikuwa mbele yake na akashindwa kusema uongo hivyo alitaka kumfichua mwanae na ndio maana ya maneno ANA KOVU USONI.
Na hii ni dhahili kama siku ile hujamuangalia vizuri yule mganga mimi nilimuona vizuri zaidi kuwa ana kovu kubwa tu usoni.
Kwa sababu hizi kuu tatu nina mashaka ya kuthubutu kusema kuwa mtoto wa Mzee Mnyungunyungu ndie Mr.X.."

"Uuuuuuppphhhhhh!!!!"
Alishusha pumzi kwa nguvu Kamishna Shebby huku akimtazama mara mbili mbili stafsajent Kimaro pasi na kumwambia chochote na ukimya ulifuata tena baina yao kipindi Shebby alipotulia na kuanza kuyachekecha maneno na prove alizotoa Kimaro sambamba na hadithi ya Hussein.
Kiupande furani yalimuingia yale maneno na kuzishawishi akili zake kuwa akubaliane na Kimaro lakini bado upande wa pili moyo wake Ulimkatalia kabisa kuwa yule mganga mtoto wa Mzee Mnyungunyungu kuwa ndie Mr.X

** ** ** **

Ilitimu majira ya saa saba mchana ambapo waliwasili kijiji cha Mkuyuni na kupaki gari yao eneo lile lile walipopaki pindi walipokuja awali na pembeni yake kulionekana imepaki difenda ya polisi na gari ya wagonjwa, na baada ya kushuka walivuka barabara na kuelekea moja kwa moja ile njia ya bondeni ambayo walipitishwa siku ile na yule kijana aliyeitwa Chibu.

Lakini cha ajabu siku hiyo hakukuonekana watu wengi eneo lile la stendi huku frem nyingi pia zilifungwa japo ilikuwa mchana na wakati wakishusha kile kibarabara waliwaona watu kwa mbali wengi wengi mbele yao huku wengine wakija nyuma yao na kuwapita wakionesha walikuwa na haraka ya kuwahi kule walipokuwa wanaelekea wenzao.
Hali hii iliwafanya hata wao kuzidisha mwendo ili wawakaribie wale watu wajue kulikoni.
"Wakuu .. wakuu wakuuuu salamualeikuuu waheshimiwaa.."
Ilisikika sauti kutokea nyuma yao ndipo walipogeuka kumuona aliyekuwa anawasalimia ndipo Kamishna Shebby na Kimaro walipotabasam baada ya kugundua alikuwa ni yule mpiga debe wa stend Chibu.
"aaah Chibu. waleikumsalaam vipi kwema."
"Aaah!! ndo hivyo bwana bado tunahema tuko pamoja na nilipowaona mnapita pale chini nikaona si mbaya niikatae tenda ya leo nikajumuike nanyi ndugu zangu ktk harakati za kwenda kumpumzisha mwenzetu."
"Harakati za kumpumzisha mwenzetu? mbona hatukuelewi Chibu?"
Aliuliza St;sajent Kimaro huku Kamishna Shebby akiwa nae kataharuki akijiuliza au ina maana mzee Mnyungunyungu hakuzikwa toka kipindi kile? wakati ilishapita wiki naa.
"Aaaah!! wakubwaa nyie si mmekuja tena kwenye huu msiba au hamuelekei kwa Mnyungunyungu?"
"Tunaelekea huko huko Chibu, sasa huo msiba wa nani tena?"
"Daah!! Mnanishangaza sasa, mi nimejua taarifa ya tukio lililotokea juzi ndio limewaleta huku kumbe sio..?"
"He!! unatuchanganya sasa Chibu kwani kumetokea tukio gani tena.!!?"
"Mnyungunyungu mtoto (jr) mzee wa nyanga na tunguli kakata kamba, yaani amekufa."
"Amekufa? mtoto yupi kwani"
"Mtoto wa Mnyungunyungu wakubwa aliyeachiwa mikoba."
"HAA!! Unamaanisha yule MGANGA?!!"
walistuka kwa pamoja baada ya Chibu kutikisa kichwa kukubaliana na swali waliloliuliza juu ya huyo aliyefariki.
ITAENDELEA..
22

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom