Simulizi: Wanawake ni wauaji

Simulizi: Wanawake ni wauaji

WANAWAKE NI WAUAJI..!? (56)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
___________________________
_________________

Alitamani kumuuliza kitu palepale lakini ulimi wake ulikuwa mzito na kubaki kimya lakini akilini tayari ilikuja picha ya mwanamke aliyewahi kumpenda miaka mingi.
Picha ya mwanamke aliyemuamini kupita kiasi.
Picha ya mwanamke aliyeweka doa katika historia ya maisha yake mpaka kufikia pale alipo.
Picha ya mwanamke huyo iliyomjia akilini haikuwa picha ya mwanamke yeyote mwengine bali ni picha ya Zainabu.
Mwanamke aliyeuteka moyo wa Hussein na kumuonesha mapenzi ya dhati yaliyomfanya awali Hussein ajione yeye ndie mwanaume bora kuliko wote lakini mwisho wa siku mwanamke huyo ndie aliyekuja kutoa kauli iliyomfanya Hussein miaka yote abaki na imani kuwa wanawake ni wauaji.
Alimtazama mama Shebby mke wa mzee Mwinchande na kwenye macho yake aliweza kuiona taswiera ya Zai wake aliyesingiziwa alimuua mwenyewe sambamba na mtoto wao wa kiume ambae aliushuhudia mwili wake ukiwa umekatwa kichwa na viganja ambavyo vilikutwa mifukoni mwake.
Lakini hata hivyo aliamua kulipotezea lile wazo kichwani na kumuomba Mungu kimoyo moyo amuondolee akili ya kumuwaza sana Zai kwani kuna muda aliamini kabisa Zai amekufa lakini kuna muda pia hakuamini na alihisi kuwa Zai hajafa ila waliyemuulia pale ni mtoto wake kipenzi aliyekuwa na miezi mmne tu.
Lakini japo alijitahidi kupotezea bado kuna vitu akiviona kwa yule mama ambae yeye hakuonesha kumjua Hussein hapo kabla hata kidogo, vilimfanya amkumbuke sana Zai mke wake na kitu kikubwa kwanza ni uvaaji wa Kiremba.
Jinsi ambavyo alikuwa akimtazama mama Shebby ule ufungaji wake kiremba cha kitenge ulimfanya pia amkumbuke sana Zai ambae nae alipenda sana kufunga kiremba tena kwa mtindo wa kipekee ambao wengi walikuwa hawafungi vile na ajabu mtindo ule wa mkewe Zai kwa mara nyengine aliukuta kwa mama Shaaban.
Kitu cha pili kusoma (kuimba) qaswida hasa nyakati za asubuhi.
Hili nalo aliligundua kwa mama Shebby siku hiyo asubuhi alipoonana nae tena na kumshangaa kupita kiasi alikuwa anatembea huku akiimba qaswida jambo ambalo hata mkewe Zai ndio alikuwa analipenda sana.
Lakini mbali na sababu hizo pia kulikuwa na sababu nyengine akizifikiria zinamkatalia kuwa mama Shebby si Zai na moja ya sababu hizo ni umri wa Shebby ambae uliandikwa kwenye daftari maalum siku wanafungishwa ndoa kuwa Asha alikuwa na miaka 29 anakaribia 30 jambo ambalo lilikuwa sahihi kabisa kwani alipokuwa anapelekwa jera baada ya kuhukumiwa barua ya mchumbaake wa zamani Mariam ilionesha kuwa tayari Asha ana miaka mitatu na yeye amekaa miaka 26 gerezani.
Lakini kwa upande wa Kamishna Shebby yeye umri wake ulionesha ni miaka 28 jambo ambalo lilikuwa tofauti kabisa kwani miaka hiyo 28 ndio kwanza alionana na Zai Arusha na hakuwa na mtoto wala hata alivyokutana nae mwaka uliofuata baada ya kushinda mitihani aliyopewa na Zai alimkuta ni bikra yaani yeye ndie alikuwa mwanaume wake wa kwanza kwa hiyo aliamini wazi kuwa Zai hakuwahi kuwa na mtoto mwenye umri mkubwa kama Shebby kwani mtoto wao kipenzi wa pekee aliyezaa na Zai alichojua aliuawa miaka 26 iliyopita.
Kwa kigezo cha umri wa Shebby kilimuondoa kabisa kwenye mashaka ya kumfananisha mamaake Shebby na aliyewahi kuwa mkewe ambae bado hakuwa na uhakika kama alikufa au mzima bi Zainab.

* * * * *

Usiku baada ya sherehe zile kuisha na watu wote kutawanyika alionekana Cj4 ambae alikuja na pikipiki moja iliyomtambulisha kama mpiga picha kutoka ofisi ya wazili wa mambo ya ndani na hata kitambulisho alichokuwa amevaa kilionesha hivyo na kila aliyemuona aliamini hivyo kutokana na kumtambua muhusika wa kile kitambulisho na muonekano wa Cj4 hakuna aliyemtilia hofu hadi wakati anaondoka pale ukumbini.

Safari yake ilimpeleka hadi sehemu moja pembeni ya barabara kulipokuwa na daraja na kusimamisha pikipiki ile nyuma ya gari moja ndogo iliyokuwa imeegeshwa pembeni na kushuka lakini aliachana na ile gari yeye alienda moja kwa moja hadi chini ya barabara uvunguni mwa lile daraja ambalo lilikuwa limekauka maji, na alipotoa simu yake ya mkononi kumulika mule uvunguni alionekana mtu mmoja ambae alifanana nae sana jinsi alivyojiweka, akiwa kafungwa kamba mikono na miguu huku mdomoni kazibwa na plasta kubwa.
"Good mr, kazi imeisha kama nilivyokuahidi siwezi kukudhuru kwa kuwa mimi si mtu m baya ila ukitaka kuujua ubaya wa mtu upoje uende ukatoe siri kuwa aliyekwenda kwenye ile sherehe ya harusi hukuwa wewe."
aliongea Cj4 na kumtoa plasta ile iliyokuwa mdomoni mwa yule jamaa aliyekuwa na kitambi kiasi sambamba na mustachi mkubwa.
Alibakia anahema tu yule bwanakipindi Cj4 akimfungua zile kamba na alipomaliza alimrudishia kitambulisho chake sambamba na funguo ya pikipiki kisha akatoa memory iliyokuwa ndani ya ile kamera na kumkabidhi kamera tupu.
"Zingatia ndugu niliyokwambia"
aliongea Cj4 na kutoka mule darajani huku yule bwana akiwa amesimama haamini hadi pale aliposikia gari ikiwashwa na kuondoka ndipo nae alipotoka mbio kule na kuwasha pikipiki yake na kuondoka.

Baada ya kufika ndani ya chumba chake alichokodi kwenye ile guest Cj4 alianza kubadilisha muonekano wake kwa kuondoa ule mustach wa bandia na kuanza kubambua mfuko wa plastik maalum uliobanwa tumboni mwake na kumuonesha kama aliyekuwa na kitambi cha wastani pindi alipovaa shati ile kubwa sambamba na kikoi.

Mara baada ya kumaliza kupambua vitu vya bandia mwilini mwake ndipo alipotumbukiza ile memory kwenye compyuta yake na kufungua mafaili ya video alizoshoot kwenye ile sherehe ya harusi ya Shebby ndipo kwa umakini mkubwa Cj4 alianza kufatilia matukio na nyuso za watu aliokuwa anawachukua ili kuhakikisha na kubaini kwa mbinu zake za kikomando kati ya wale wageni waliohudhulia pale nani alikuwa Mr X.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (57)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
___________________________
______________

Alitulia kwa umakini mkubwa Cj4 kutazama yale matukio yaliyokuwa yanaendelea kipindi cha shughuli ile lakini kadri alivyokuwa anaangalia bado hakuona tofauti kwa mtu yeyote wala kupata taswira nani kati ya wale watu waliokuwepo kwenye ile shughuli ni Mr X?
Aliangalia hadi mwisho bila kumuhisi mtu yeyote aliyeoneka kuwa na utofauti fulani ambao ungemsaidia kumtambua mr X na ndipo alipoamua kuianzisha upya safari hii akipunguza speed ya utembeaji wa picha na kueka ule wa taratibu na kiminato (slow motion)
Aliangalia tena kwa umakini mno wakati huo kila hatua aliyoichukua na mwishoe aliimaliza tena hadi mwisho bila kupata picha wala taswira ya kumjua huyo mgeni aliyeamini kuwa lazima atakuwepo kwa kuwa kauli za mr.X zenye mafumbo mazito kwake Cj4 aliweza kuyatatua kiasi yale mafumbo na kujua lazima Mr X atakuwa kwenye mzunguko wa maisha ya Kamishna Shebby iwe katika ngazi ya jeshi la polisi ama kwa marafiki wakuu wa babaake mzazi mzee Mwinchande kutokana nae alikuwa ni moja ya askali wakubwa enzi hizo hivyo alikuwa na mtandao wa karibu na watu wengi ambamo Cj4 aliamini lazima miongoni mwao atakuwa ndie Mr X.

Lakini safari hii alipofika mwisho kuna kitu kimoja alikiona akagundua hakipo sawa.
Hapo ndipo alipoanza kurudisha nyuma na kueka slow motion zaidi vile vipande vya Hussein bubu na kuna kitu akaanza kukibaini na kukitilia shaka.
Ni vile Hussein muda mwingi alionekana alikuwa anamuangalia sana mamaake Kamishna Shebby tena kwa kumuiba iba.
Alikaa vizuri Cj4 na kumzoom Hussein sehemu za macho yake na kugundua kuwa kuna kitu alikuwa anakifikiria ama anakifananisha kwa jinsi alivyokuwa anamtazama mamaake Kamishna Shebby.
("Mh! hapa hapa ndipo pa kuanzia.")
alijiambia akilini Cj4 na kumsogeza kwa karibu mamaake Kamishna Shebby sehemu za uso na kumplay katika slow motion kumchunguza vile alivyokuwa anamuangalia Hussein na hapo napo kuna kitu alikisoma kuwa mama Shebby hakuweza kabisa kumuangalia Hussein hata kwa sekunde kumi, na mara alipogonganisha macho na Hussein aliyakwepesha kiujanja na kugundua sehemu alipoyaelekeza ni upande aliokaa mumewe ambae ni babaake Kamishna Shebby.
"Mh!"
Aliguna Cj4 na sasa alianza kumzoom babaake kamishna Shebby ambae ni mzee Mwinchande lakini kila alivyoitafuta tofauti yoyote kutoka kwa mzee Mwinchande kwa kile alichokiona kwa Hussein na mama Shebby hakuweza kuona chochote kutoka kwa Mwinchande.
Alimueka katika slow motion ile ya chini kabisa lakini muda wote aligundua kuwa mzee Mwinchande alikuwa na furaha na muda mwingi alionekana yuko bussy na kile kilichokuwa kinaendelea ukumbini hususani kuwatzama bibi na bwana harusi.

Alirudia tena Cj4 kwa upande wa Hussein na mama Shebby walivyokuwa wanapelekeana macho na hapo aliikumbuka vizuri story ya Hussein juu ya maisha yake yaliyopita mpaka anaingia jera na kuanza kupata hisia inawezekana Hussein akawa anamfananisha mama Shebby na mkewe ambae ilisemekana alimuua.
"Hapa hapa kuna alama ya Mr X."
alijisemea mwenyewe Cj4 lakini kila alipotaka kumshuku babaake Shebby alijikuta moyo unakuwa mzito kukubali japo akili ilianza kumpeleka huko.
("Inawezekanaje huyu akawa ndie mke wa Hussein? Mh! ila pia inawezekana na kama ndio nina mashaka na babaake Shebby akawa ndie Mr X. ilaaaaa.... Agh! Nina wasiwasi na hapa hapa")
aliwaza na kujisemea moyoni Cj4 na kujilaza kitandani wakati huo tayari ilikuwa alfajiri.
"Mzee Mwinchande upo katika mstari wangu wa mashaka. Hii sasa itakuwa mission yangu peke yangu."
alitamka maneno haya Cj4 na kueka nia sasa mtu atayedili nae katika kumchunguza ni baba wa Kamishna Shebby ambae ni mzee Mwinchande, na hili alipanga kulifanya bila kumwambia hata Kamishna Shebby ambae ndie aliyekuwa anashirikiana nae katika mission zao za siri juu ya kumtafuta na kumnasa Mr X.

* * * * *

"Ibada ni jambo jema sana mzee mwenzangu."
"Kweli kabisa."
"Mwenye kufanya ibada hujieka jilani na Mungu na kujilinda na Sheitwaan"
"Naam."
"Mimi na mke wangu kama unavyotuona, sisi ni waislam safi kabisa na kila siku tunafanya ibada na ndio sababu nyumbani kwetu kuna amani na ndoa yetu imedumu miaka mingi."
"Daah! kweli kaka hongereni sana."
"Ahsante lakini hata wewe si mzee kama unaamua."
"Kuamua kivipi kaka."
"Amua uoe ili upate utulivu si unajua ng'ombe hazeeki maini?"
"KUOA!? hahahaa hapana kaka mimi maisha yangu nitayamalizia hivi tu."
alijibu Hussein bubu huku kipindi akizungumza na Mzee Mwinchande pale sebuleni majira ya mchana.

Mzee Mwinchande alikuwa anamuelezea Hussein habari nyingi nzuri na jambo kubwa alikuwa anamsisitiza juu ya imani yake kwa Mungu.
Maneno ya mzee Mwinchande yalizidi kumfanya Hussein amsome kuwa ni mtu mmoja mzuri sana na moyo wake ulifanana na wa Kamishna Shebby kwa vile alivyoonekana mwenye kujali na kuthamini wengine.
"Hivi unajua vizuri kusali?"
aliuliza mzee Mwinchande
"Mh! hapana kiukweli nimesahau dua nyingi sana za kusoma wakati unasali"
alijibu Hussein bubu.
"Basi mi nataka kuanzia leo uwe unajiunga nami tusali pamoja hususani alifajiri na usiku ndio mida mizuri sana kusali na kuomba"
aliongea mzee Mwinchande huku akipekua chini ya screen kubwa iliyokuwa ukutani pale sebuleni ambapo kwa chini kulijengewa kama kikabali maalum cha kuhifadhia vitabu na hapo alitoa kitabu kimoja kilichoandikwa SALA NA MAFUNZO YAKE, kisha alimkabidhi Hussein.
"Hiki kitabu kitakusaidia sana katika kujua kusali sala zote za kiislam."
"Asante sana kaka, daah! Nashukuru kwa kweli kwa kuonesha kunijali."
alijibu kiunyenyekevu Hussein wakati huo mke wa mzee Mwinchande alikuwa anashuka ngazi akitokea sehemu za juu ya nyumba yao na kama kawaida yake Hussein alipokutanisha tena macho na mama Shebby moyo ulimripuka tena na safari hii kuna kitu chengine alikiona ambacho kiliustua zaidi mtima wake.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (58)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_______________________
__________________

Alibaki amemkodolea macho mama Shebby ambapo kikubwa alichokuwa anshangaa Hussein ambacho alikigundua ni alama ya baka la mstari mweusi juu ya paji lake la uso eneo lilipoanzia nywele kuota.
Alama hii safari hii aliiona vizuri baada ya ushungi aliojifunika mke wa mzee Mwinchande (mama Shebby) kufunuka bahati mbaya na alikuwa hajavaa kiremba kama ilivyokuwa kawaida, na hata chanzo cha kuvaaga kiremba Zai ilikuwa ni kwasababu ya kuficha baka la mstari pale juu ya paji la uso ndio maana ufungaji wake Kiremba ulikuwa wa kipekee sana, sasa imekuaje na mama Shebby nae awe na mitindo ya kufunga kiremba kama Zai harafu kumbe na yeye ana baka la mstari mweusi?
("Mh! hapana sasa nina wasiwasi")
alijisemea moyoni Hussein na kumuaga kwanza mzee Mwinchande akizuga kwenda chooni lakini ukweli hakuwa na haja yoyote zaidi alienda kukaa kufikiria kile alichokuwa amekiona pale nyumbani kwa mkwewe Kamishna Shebby.
("Inakuaje kuaje mama Shebby afanane vitu vingi na mke wangu Zai? au ni kweli yeye huyu! Eee Mungu naomba unisaidie nipande ufumbuzi wa uhakika wa hili suala")
aliwaza na kuomba kimoyo moyo Hussein pindi alipokuwa chooni akilifikiria sana lile jambo na alijaribu kukumbuka mambo mengi aliyokuwa anayapenda mkewe Zai kipindi hiko ili iwe rahisi kuzidi kuyapima na kuyafuatilia kwa mama Shebby kama kuna uwezekeno wa kufananisha mambo mengine zaidi.
("Mh! lazima nifanye hivi nione, ina maana kama kweli huyu ni yuleyule Zai mke wangu basi naamini babaake Shebby ndie adui angu Mr X mwenyewe. Mh!! lakini sasa mbona babaake Shebby haoneshi hata chembe kama ana moyo m baya? hafanani hata kidogo na vitendo vya mwana izaya Mr X.")
aliendelea kufikiria Hussein na hatimae alitoka kule chooni na kurudi sebuleni alipokuwa Mzee Mwinchande na kuendelea na maongezi yao.
"Basi inshaallah mzee mwenzangu, wewe tulia kisome kwa umakini sana hiko kitabu tuwe tunajumuika wote hapa kuswali suna za usiku na faradhi ya alfajiri"
"Nashukuru kaka, usihofu."

* * * *

Siku zilienda huku fukuto likizidi kufukuta kifuani na kichwani mwa Hussein juu ya kumtilia mashaka siku baada ya siku mama Shebby ambapo safari hii kila ile tabia sugu aliyokuwa anaikumbuka kuwa Zai alikuwa nayo alibaini kuwa hata mamaake Shebby alikuwa nayo na hii ikazidi kumpa uhakika wa asilimia nyingi kuwa akitafutacho ndicho akionacho.
Lakini uzito wa kuamini hilo unakuja pale kila jinsi alivyomtazama mzee Mwinchande alkuwa hafanani kabisa kuwa ni mtu mwenye moyo wa kikatiri na roho mbaya kama alivyo mr X kwani kama kweli mamaake Shebby ni Zai basi bila shaka babaake Shebby ni Mr X na hata akiwa siye bado Zai atajua wapi alipo kwa kuwa katika maneno ya mwisho ya mke wake Zai kabla hajapoteza fahamu baada ya kupigwa na kitu kizito siku ile walipovamiwa na Ninja wa mr X pindi walipokuwa wanaelekea kwa baba mkubwa ambae alikuwa mganga mzee Mnyungunyungu.
Lakini bado swali lengine lilikuja kichwani mwa Hussein bubu kama basi yule atakuwa Zai harafu yule mzee Mwinchande asiwe Mr X hivi usalama wao ungekaakaa vipi miaka yote hadi wanafikia pale wakati yeye tu aliponzwa kwa kuishi na Zai tena alikuwa mkewe kabisaa lakini bado Mr X alimfanyia matukio makubwa na wote waliokuwa na habari walau za tetesi kuhusu mr X waliuawa.
Sasa inakuaje kwa mtu anayejua kila kitu kuhusu mr X akaachwa hai hadi muda ule wakati mr X mwenyewe bado yu mzima?

Maswali yalikuwa mengi sana kwa Hussein babu bubu na kila alipoamka na kuwa anasalishwa na mzee Mwinchande yeye mawazo yake yalihama kabisa akiwa haamini kile akifikiriacho na mara akawa anaamini lakini bado akawa anaomba Mungu azidi kumpa uyakinifu zaidi katika lile swala na kila siku alitamani kumuuliza mama Shebby jina lake harisi ni nani lakini alishindwa wala hakujua aanzie wapi.
Baada ya siku saba fungate la kinyumbani nyumbani la Dokta Asha na Kamishna Shebby liliisha na kufanikiwa kuondoka na mkewe kuishi kwele yale makazi aliyoandaliwa na serikali kule karibu na gereza ambapo kulikuwa na nyumba za kisasa zilizojengwa na serikali kwa niaba ya makamishna wote nchini.
Na ulipotimu ule usiku ambao Shebby aliondoka Hussein bubu alipatwa na ndoto ya maajabu sana........
'''''''''
(^^"Tumuue tu mke wangu.^^")
(("^^ Hapana mume wangu kwa adhabu ya awali imetosha mbonaa!?^^"))
(^^"Hapana mke wangu atatusumbua huyu tusipofanya haraka."^^)
(("^^Mh ! sidhani kwani wewe unatakaje^^")
(^^"Vizuri, chukua dawa hii ujitahidi ifike kwenye chakula atachokula au maji atayokunywa hapo ataanza kumung/unyuka taratibu na hatochukua miezi mitatu atakufa"^^)
(("^^Haya ila moyo unaniuma daah!^^^"))
(^^"Usiumie Zai mke wangu"^^)
''''''''''
"Hee!"
alikurupuka Hussein mara baada ya kumuota mama Shebby na mzee Mwinchande wakijadili suala la kumuua.
Alikaa kitandani huku akihema na kuifikiria ndoto ile na pale pale lilimjia wazo atoke anyate kuelekea juu chumbani kwa mzee Mwinchande na Zai lakini hakujua aende kufanya nini ila alijikuta moyo unamsukuma atoke aende huko.
Aliangalia saa ilikuwa ni saa saba za usiku ndipo alipoanza kufungua mlango na kunyata taratibu kuelekea kule juu kulipokuwa na chumba cha mzee Mwinchande na mkewe.
Katika hali ya ajabu na mshangao mkubwa Hussein pindi alipokaribia tu kumbe muda huo mzee Mwinchande na mkewe walikuwa hawajalala wala hawakuwa chumbani zaidi walukuwa kwenye korido moja ya kisasa pale juu iliyotengenezwa kwa niaba ya kupumzika na kula kipupwe cha upepo wa bahari.
Kilichomstua zaidi Hussein si kutolala kwao bali ni maneno waliyokuwa wanaongea.
"Unaona Zai mke wangu, hii picha ya video ni siku ilee, hapa nahisi ndio alikugundua na kujifanya anaenda chooni kujisaidia kumbe kufikiria tu kwa kile alichoanza kukihisi. Nilikwambia mapema mke wangu, sasa acha kwanza nimpofue ili iwe rahisi kumpoteza jumla"
aliisikia vizuri kauli hii ya mzee Mwinchande iliyomfanya agande kwa mshtuko wa hasira na maumivu ya ajabu baada ya kujua ukweli sasa kumbe yule ni kweli Zainab mkewe na mzee Mwinchande ni Mr X.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (59)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
________________________
___________

Alianza kunyata taratibu Hussein bubu huku mapigo yake ya moyo yakienda kasi kupita kawaida akiwa haamini kabisa kama kweli leo hii amemtambua adui yake kwa mtindo ambao hakuwahi kuufikiria hata siku moja wala kuuota.
Alifanikiwa kufika mwisho wa ngazi taratibu na kuendelea kunyata kwa umakini mkubwa na kilichomsaidia zaidi alikuwa pekupeku ambapo mara alipofanikiwa kuukuta mlango wake na kuingia ndani tu aliufunga taratibu na ndipo alipofanikiwa hata kushusha pumzi ambayo alikuwa kaibana muda wote alivyokuwa ananyata kurudi mara tu aliposikia sauti ya mzee Mwinchande na mama Shebby ambae sasa aligundua kuwa ni Zainab yule yule mke wake wakijadili juu ya kumuua.
"Uuuuuphhhhhhhhh"
Alihema kwa nguvu Hussein huku akiwa kaegemea ukuta wa pale chumbani pindi alipoufunga mlango na kujikuta akisota kwa mgongo taratibu mpaka akakaa kitako pale chini huku mikono kiwa ameiweka kichwani.
("Heeee! Mungu kumbe muda wote niko katika chaka la Simba mla watu aliyevaa ngozi ya kondoo? hapana aaa uuupphhhh")
aliongea moyoni Hussein huku machozi yakimtoka akiwa anasugua sugua mikono kwa nguvu pale chini lakini mara aligundua kitu kilichomfanya ainuke haraka na kuzima taa kisha kujilaza kitandani moja kwa moja na kujifunika mwili wote.
("Huyu ni mshenzi mwenye mbinu nyingi sana, kama aliweza kunitegea kamera chooni nadhani hata humu chumbani kamera haikosi, sasa hapa inabidi niwe makini kabla hajawahi kunistukia kama nimemstukia ili niweze kumuua kiurahisi. Lakini nitamuua ua vipi mshenzi huyu? Aaaah.. Kivyovyote lazima nimuue. Naamini Mungu aliyeniotesha haya na kunnikutanisha nae ndie atayeniongoza na kunionyesha njia rahisi ya kummaliza huyu mshenzi loh! Kumbe mr X ni babaake kijana aliyenisaidia kutoka jera? au isije kuwa ndie Mwinshehe wangu?")
aliwaza Hussein na kufika mbali zaidi mara alipotia shaka isije kuwa na Kamishna Shebby akawa ndie Mwinshehe, jina la mtoto wake alieuawa akiwa na miezi minne tu.

("Zainabu...Zainabu...Zainabuu Mke wangu kumbe hukufa? aaaagh! Wanawake ni Wauaji kweli aaaaagh, au kwa sababu uliniona masikini Zai, si ungenambia tu nikuache uende salama nami nibaki salama...!!! Aaaaagh! Eeeeh Mungu kwaniniii Kwaniniiiiiiiii??!!!")
aliendelea kusema na moyo wake Hussein huku machozi yakimtoka mfurulizo na moyo kumuenda mbio kupita kawaida.
Mwili wote wa Hussein bubu ulibadilisha homon ghafra na kuanza kutetemeka kwa hasira mithili ya mgonjwa wa homa aliyemwagiwa maji ya baridi.
("Aaaagh! Zaiiii...Zaiii... Zaii!!!!? siaminiiiii aaaaaaaaaaaagh. Wanawake ni Wauaji..... Wanawake ni Wauaji..... wanawakeeeee!?")
(..........................) (.......................) (......)
(..."Zai ulijua kumbe ile barua ni ya nani lakini ulikanusha Zai? aaagh! Ulinipa moyo nipuuze kumbe kila kitu ulijua... aaagh! umemgeuka mumeo kwa ajili ya tamaaa kwa mtu baradhuli na katili kama huyu? Eti Mr X. aaaaagh! Samson alimuamini Delila kuwa mwanamke anayempenda bila kujua kumbe Delila anatumiwa kumchunguza na maadui zake. Yaliyokuja mkuta Samson mwanaume yeyote kweli yanaweza kumkutaaa. Zai!!!? Lazima nawe ufe")
Uchungu na mawazo aliyokuwa nayo Hussein uliendelea hadi pale alipostuliwa baada ya mlango kugongwa.
"Nani?"
aliuliza Hussein kwa sauti iliyojaa mikwaruzo.
"Swalaaa swalaaa.. Salaaa. swala ni bora kuliko usingizi"
aliisikia sauti ya Mzee Mwinchande akimuamsha waende wakasali na kugundua kuwa tayari ilitimu alfajiri.
("Kum**aako lazima Nikuue Mshenzi wewe.")
aliongea moyoni kwa hasira na kushuka pale kitandani hussein na kuwasha taa ili ajiandae kwaajili ya kuungana na adui yake katika kumuomba Mungu (kusali) pamoja.

* * * * *

"Mme wangu, mme wangu Nakupenda sana"
"Hata mimi nakupenda sana mke wangu Asha"
"Lakini sidhani kama nastahili upendo huo"
"Kwanini usistahili sasa! Unastahili kabisa na una haki nikupende zaidi ya hapa"
"Kweli?!"
"Kweli kabisa mke wangu. Kwanini unaniuliza hilo?"
"Kwa sababu nina wasiwasi."
"Wasiwasi!!? wasiwasi gani tena mke wangu.. Ondoa wasi kabisa Asha siwezi kuja kukutenda kwa mwanamke yeyote yule. Kwako mimi nimefika kabisa kama ni meli imetia nanga."
"Najua ni rahisi kusema hivyo kwa sasa, lakini sidhani kama kila siku utasema hivyo. Naamini kuna siku utanichukia kupita kiasi na nina wasiwasi utaniua."
"WHAT!!?"
Alistuka Kamishna Shebby baada ya kusikia kauli ile ya Asha pindi walipokuwa wanazungumza alfajiri ile wakiwa kitandani.
"Asha baby, mbona leo umeamka ukiwa na maneno makali sana?"
"Kwasababu ya maumivu baby"
"Maumivu? yapi tena"
"Ya mshono tuu"
Alizuga Asha pindi alipotaka kumwambia ukweli Kamishna Shebby juu ya yote ambayo hakuyajua kuhusu yeye lakini alijikuta anaamua kumkwepa baada ya moyo wake kuwa mzito ghafra na kushindwa jua aanzie wapi.
"Pole sana baby, sasa maumivu yako ya mshono ndio yasababishe nikuchukie? niache kumchukia mshenzi mr.........."
alisita Shebby baada ya kutaka kuropoka juu ya mr X na kukumbuka kauli na ushauri wa Cj4 kuwa asimzungumzie wala kumtaja Mr.X hata kwa mkewe ama wazazi wake bila kujua huyo anayemficha anajua mengi zaidi ya anavyomuona.
"Unasema umchukie Mr..!!? mr. ndio nani?"
aliuliza kimakusudi Asha na kuzidi kumpoteza kisaikology Shebby aliyeamua kutunga uongo wa palepale ambao Asha alijifanya kuukubali.

Maisha yao mule ndani kila mmoja alikuwa na siri ambayo mwengine haijui na mtu aliyekuwa anawaunganisha kwenye hiyo siri kila mmoja hajui kama mwenzake huyo mtu anamjua ama anawasiliana nae, na wote kwa pamoja walimuamini sana huyo mtu na kumsikiliza kutokana na mioyo yao kukiri kuwa huyo mtu amewazidi kila kitu kuanzia mbinu hadi uwezo wa kupambana kimwili.
Na hakuwa mwengine huyo mtu bali ni Komandoo aliyeaminiwa kati ya makomando kutoka Jwtz naye ni Komando Jumanne au Cj4. ambae sasa nae aliwaingiza kwenye mchezo Shebby na Asha baada ya kugundua siri ambazo aliona ili apate majibu inabidi acheze mwenyewe mchezo kama alioutengeneza Mr X ule wa vipofu lakini tofauti yeye aliwaweka vipofu rafiki zake, watu asio na visasi nao na kwa sababu maalum zenye faida kwao wote.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (60)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
__________________________
_________________

Siku hiyo tofauti na siku zote Kamishna Shebby alitoka alfajiri sana majira ya saa kumi na moja kasoro na baada ya Kamishna Shebby kutoka tu ndipo Asha alipoamka haraka na kuchukua simu yake na kupiga tena ile namba ya siri aliyopewa na Cj4 kule hospitali kwa shauku akiwa anataka ushauri kwa Cj4 nini afanye juu ya ukweli anaouficha kwa mumewe juu yake na mr X.
["Hallow kaka Inspekta"]
aliongea Asha mara baada ya simu kupokelewa upande wa pili.
[["Lady Ninja, leta ripoti ulichopata."]]
ilisikika sauti upande wa pili na kumfanya Asha ashushe kwanza pumzi baada ya kuona yule mtu ambae yeye alikuwa anadhani ni Inspekta kuwa anajua mengi sana kuhusu yeye hasa baada ya kusikia anamwita Lady Ninja.
["Naomba unisaidie ushauri kwani natamani kumwambia ukweli mume wangu lakini nahisi huu ukweli unaweza kuwa ndio mwisho wa upendo baina yetu isitoshe nami nampenda kweli sasa. msaada tafadhali huu uongo unaniumiza nafsi"].
[["Hupaswi kuwa na haraka kumwambia sasa, unachotakiwa uwe unakwenda mara kwa mara kule kwa wakwe zako naamini sasa Mr X rada yake haipo kwenu kwanza ipo kwa babaako."]]
aliongea Cj4 na kumpa maelekezo yale Asha ambae aliyakubari kwa moyo mmoja na baada ya kukata simu alianza kutafakari yale maneno ya Cj4 kuwa kwanini Mr X sasa hana habari na wao bali ataendelea kwanza kudeal na Hussein ambae ni babaake aliyekuwa kule kwenye Jumba kubwa la mzee Mwinchande?
("Mr X sawa anadeal na babaangu, lakini kwanini Inspector ananambia niende mara kwa mara?! Mh!! nina wasiwasi na haya maneno kitaalam kama anamaanisha mr X hayuko mbali na pale..!")
aliwaza Asha baada ya kukata simu.

Wakati huo nae Shebby alikuwa njiani akienda huko huko kwa Cj4 kama kawaida toka amefariki Kimaro na kupona kwake mguu hakutaka kabisa kuendeeshwa hata alipobembelezwa na serikali kutokana na heshima aliyokuwa ametunukiwa lakini alikataa katakata na alifanya hivi kutokana na mission zake za siri sambamba na Cj4.
Shebby akiwa kwenye gari yake mawazo yote alifikiria sana mazungumzo ya mkewe na aliona kama kulikuwa na kitu cha zaidi alichotaka kusema yule mwanamke lakini alighairisha ghafra na kuzuga story nyengine na kumbe Shebby hata alivyokuwa anamuitikia haikumaanisha alikuwa hajastukia kama kuna kitu Asha alikuwa ameficha lakini alichofikiria kwa nini anaficha?
Lakini kwa kuwa alikua na mtu wanaesaidiana kwenye mission yao ya kumnasa mr X na kwa sababu ya kuamini huyo mtu ana uwezo mpana sana wa mbinu na fikra aliamua kwanza kukutana nae alfajiri amuelezee na kile alichokuwa anakihisi yeye ili wapate ufumbuzi zaidi wa mambo.

Ulikuwa ni ujanja wa Cj4 alioutengeneza kwa Shebby na Asha na sasa ilikuwa ni yeye tu anawacontrol wote wawili pasi na kujitambua wenyewe.
Asha ametoka kuongea nae na mara alipokata simu hazikupita dakika ishirini na Shebby nae aliingia.

* * * *

"Asalamu alykum bwana, swala muda ndio huu Mwenyezi Mungu anatuamuru tuamke tumuombe nae atatujibu..."
aliongea mzee Mwinchande mara baada ya Hussein kufungua mlango na kutoka.
"hahaaa Kweli kabisa daah!"
alijibu Hussein kwa kujichekesha machoni lakini moyoni alikuwa na hasira kupita kifani juu ya mzee Mwinchande baada ya kumgundua kuwa ndie alikuwa mr.X mwenyewe.
Lakini kilichomsaidia Hussein ni vile jinsi alivyoweza kuyaficha ya moyoni na kuvaa uhalisia wa kitu tofauti kabisa na hii kwa kuwa alijua mtu hatari mr X yupo mbele yake kwa hiyo itakuwa hatari zaidi kama akiwahi kugundua yaliyo moyoni mwake.

Walisimama sehemu ile ya kusalia na mzee Mwinchande alisimama mbele yake akiwa ndie Imam (kiongozi wa sala) huku Hussein bubu akisimama nyuma ya mzee Mwinchande akiwa maamuma (muongozwaji wa sala) na hapo ndipo Mwinchande alipofungua sala.
"Allaaaaaaaahu Akbaaar." (Mwenyezi Mungu ni Mkubwa)
alitamka mzee Mwinchande na Hussein aliongoza vile japo moyo ulimuuma na kujikuta machozi yanaanza kumdondoka tena kipindi Mwinchande akisoma pale mbele kuiongoza sala yao.
("Yaaani nakubali kabisa kusalishwa na adui yangu? Yani eti nimuombe Mungu pamoja na adui yangu tena yeye ndie awe ananiongoza kumuomba Mungu? hapana... Hapanaaa")
aliongea mwenyewe Hussein moyoni mwake huku akimuangalia mzee Mwinchande kwa hasira pale mbele akijaribu kutafakari nini amfanye ili aweze kutimiza azma yake na nafasi aliyoiomba zaidi ya miaka ishirini?
Nafasi ambayo aliona ndio ile leo hii iko mbele yake na mr X adui yake aliyesubiri muujiza wa kumjua utokee kwa miaka mingi na sasa imekuwa hivyo yuko mbele yake na amempa kisogo.
("Inawezekana bahati hii nisiipate tena akaja kuniwahi huyu mshenzi.")
alifikkiria tena Hussein huku akigeuka geuka kutazama maeneo yale yalivyokaa kaa akiwa kama mwenye kutafuta kitu wakati sala ilipokuwa inaendelea na alijua kwa upande wake lile jambo la kugeuka geuka tayari lilikuwa lishamuharibia sala lakini aliona yuko sahihi kwani hawezi akasalishwa na shetani harafu hiyo sla ifike kwa Mungu.

Aliamini kabisa mr X ni shetani wala hapaswi kabisa kuishi na aliamini kuwa asingeweza kuendelea kuvumilia kwa siku tatu zaidi bila kustukiwa na mr X kilichokuwa moyoni mwake.
Na katika kugeuka geuka kwake hatimae alibahatika kukiona alichokuwa anaaangaza angaza macho kukitafuta na hakikuwa chengine bali ni kipande cha chuma kilichokuwa kinatumiwa kwaajili ya kupasulia nazi na alikiona jana yake usiku pindi yule mfanyakazi wa ndani alipokisahau kukirudisha sehemu husika mara baada ya kukitumia kipindi akiangalia filam kwa sebuleni na kukisahau juu ya sink dogo karibu na mlango wa jikoni nyuma kidogo na eneo walilokuwa wanasali.
("Shabbashhhhhh, najua hii yote ni Mungu amemfanya yule bint kukisahau na kunikumbusha mimi nikitumie kama silaha ya kummaliza adui wa watu aliyesimama mbele yangu")
aliongea Hussein wakati huo walikuwa wamesimama tena baada ya lakaa (sujuda) ya kwanza ambapo mzee Mwinchande akiwa hana habari aliendelea kusoma kwa madaha kabisa taratibu bila kujua wala kuhisi nini kinaendelea nyuma yake ambapo Hussein bubu alikuwa ananyata taratibu sana kinyume nyume hadi kulipokuwapo kile chuma na kukikamata kwa nguvu na kuanza kunyata tena kumsogelea mzee Mwinchande huku mapigo yake ya moyo yakizidi kasi kadri alivyozidi kupiga hatua hadi alipofika mita chache kabisa na kujiandaa kwa nguvu zote kumshambulia adui yake.
("Leo ndio Historia inaandikwa.")
aliongea kimoyo moyo na kujihesabia mwenyewe Hussein lakini mara ghafla alistuka kusikia sauti ya miguu ya mtu akishuka ngazi kwa haraka kutoka juu kuja kule sebureni tena akiwa anakimbia.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (61)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_________________________
_______________

"Mume wanguuu Mume wanguuuuuu Babaaaaa......"
alikuwa ni Zainab mamaake Kamishna Shebby akikimbia kuwahi kule chini mara baada ya kuona kinachotaka kutokea kupitia kwenye screen yao maalum iliyokuwa chumbani inayoonesha maeneo ya nyumba ile kupitia kamera ndogo zilizotegwa kila kona kwaajili ya usalama na kurekodi kila kinachoendelea mule ndani.

Lakini pindi anatoa ule ukelele kumpa tahadhari mzee mwinchande ambae alikuwa anajiandaa kusujudu ndipo Hussein bubu alipowahi kwa kumtandika vyuma vya kichwa mfurulizo na kwa nguvu zote.
"KUFAAA KUFAA KUAFAA"
Alipiga kelele Hussein kipindi anamshambulia mzee Mwinchande kwa nguvu zote mpaka walipodondoka pale chini ambapo kwa sekunde zisizozidi arobaini tayari damu nyingi zilikuwa zinamvuja mzee Mwinchande aliyekuwa anapapatika sebule nzima huku Hussein bubu akiwa kamng'ang'ania bado anampelekea dozi ya kutosha kwa kumpiga kwa nguvu na kile chuma hali iliyosababisha sasa damu kuwa inamrukia Hussein na mbaya zaidi alianza kupasua hadi fuvu la kichwa.
"Hoooooooooooooooooooooooooooooooooo..."
alipiga kelele na kuanguka pale mwisho wa ngazi Zainab huku akiwa haamini kile alichokuwa anakiona kikitokea mbele ya macho yake.
"Uuughhhhrrrrr..Ughhhrrrrrr.."
alikoroma koroma kwa nguvu Mwinchande kila Hussein alivyokuwa anamporomeshea kipigo cha kihistoria.
"Kufaaaaaaa Mshenzi weweee kufaaaaaaaa, Kufaaaaaaa"
alikuwa nusu kapagawa Hussein na alizidi kupata nguvu pindi alipokuwa anatoa dozi kwa mzee Mwinchande ambae sasa alionesha wazi tayari alikuwa anamalizikia roho huku akiwa amepasuka vibaya sehemu za kichwani na paji la uso damu zikiwa zimetapakaa sehemu ile ya kusalia hadi maeneo ya jikoni katika kikirikakara zilizokuwa zinaendelea.

Kelele za Zainab na Hussein ziliweza kumuamsha dada wa kazi aliekuwa chumba cha chini karibu na jiko ambapo alipotoka hakuamini kile kilichokuwa kinaendelea mara baada ya kumshuhudia Hussein bubu akiwa anamshambulia kwa nguvu zote mzee Mwinchande pale chini huku kwa mbele maeneo ya ngazi zilizoelekea vyumba vya juu alionekana mamaake Kamishna Shebby akiwa ameanguka huku kaishiwa nguvu akilia bila kutoa sauti.
Ubaya wa nyumba ile ilivyotengenezwa ni kuwa na vioo vya tinted pia madirisha yalikuwa hayafunguliwi kutokana na AC iliyokuwa inawashwa masaa 24 na kama ukitaka upepo halisia unapandisha sehemu za juu kabisa, na kwa sababu hiyo hata walinzi waliokuwa nje hawakujua chochote kilichokuwa kinaendelea ndani.

["Hlloooo, halloooooo, halooo kakaa shebiiii babaaa hukuuu aaaah muwahi babaaaaanakufaaaa... "]
aliongea huku nae akilia yule msichana wa kazi mara baada ya kukimbilia tena ndani mwake na kuamua kumpigia Kamishna Shebby kumpa taarifa ili awahi kuja kutoa msaada kwa kile kilichokuwa kinaendelea pale.
"HAHAHAHAHAHAHAHAAAAA"
alicheka kwa nguvu Hussein mara baada ya kuona Mzee Mwinchande katulia na kaacha kupapatika.
"hahahahahahahahahahaaaaa"
Alicheka tena huku safari hii akimpiga piga kwa nguvu sehemu za mdomo na kuanza kumvunja meno bila kujali hata zile damu zilizokuwa zinamrukia huku akiwa na Furaha ambayo toka anaingia Jera hajawahi kufurahi kwa nguvu Hussein kama siku hiyo.
"ASANTE BABA MUNGU"
Aliinua kichwa juu na kushukuru Hussein bubu kwa kuona ile ndoto yake na maombi kuwa aje kumuua Mr.X kwa mikono yake muda ule ilikuwa imetimia na hatimae kweli Mzee Mwinchande ambae ndie alikuwa Original MR.X aliuawa kwa mikono ya Hussein babu bubu baada ya usumbufu wa zaidi ya miaka 28.
Baada ya Hussein Kuhakikisha hakuna Jipya tena kwa Mr X aliinua uso wake na kumtazama mama Shebby pale chini ambae alikuwa amekosa nguvu kabisa hakuweza hata kunyanyuka zaidi ya kuwa anasota kuelekea juu ya ngazi zile kwa hofu huku akilia mara baada ya kumuona Hussein amenyanyuka kwa hasira na macho yote alikuwa kayaelekeza kwake.

* * * * *

"Leo kuna kitu kimoja tu, kilinichanganya kuhusu mke wangu."
alionekana Kamishna Shebby akiongea na Cj4 kwenye sehemu yao maalum waliyokuwa wanakutana kwa mazungumzo pasi na mtu yeyote kuona.
"Kitu gani hiko?"
aliuliza Cj4
"Kwenye mazungumzo yake nikiwa kama askali mzoefu sasa niligundua kuna kitu ananificha kinachonihusu kabisa"
"Mh! hebu nipe nukuu yake."
"Alianza maongezi akiwa makini na kunimaanishia kuwa niamini kama ananipenda, lakini alivyoendelea alinambia kuwa ila anaona hastahiri mimi kumpenda vile na nilipomuuliza sababu akanambia ana wasiwasi kwa vile ninavyompenda kuwa sitompenda hivyo siku zote. Nilipomuuliza kwanini ana wasiwasi huo ndipo akanambia kuwa anahisi kuna siku nitakuja kumchukia sana na hata kumuua.... Dah! hapa ndipo nilipochoka na kuhisi lazima kuna kitu tu. Hawezi kuanzisha mada yenye maneno makali kama yale yaani mimi Nimuue mke wangu mwenyewe?"
aliongea Shebby wakati huo Cj4 alikuwa anmsikiliza kwa umakini mkubwa.
"kwa hiyo hukumuuliza kwanini amefika mbali hivyo?"
"Nilimuuliza kiongozi."
"Akasemaje"
"aagh! jibu lake nililiitikia tu lakini halikuwa na ukweli wowote nilijua tu ni Zuga"
"sawa aliemaje?"
aliuliza Cj4 lakini wakati Shebby anataka kujibu mara simu yake ambayo ilikuwa na line ile ya nyumbani tu ndipo ilipoita na kuipokea ambapo sauti ya upande wa pili ilimfanya abadilike ghafra uso.
"Vipi Shebby?"
"Kumekucha Mkuu Mr X ameamua kuivamia nyumba yetu alfajiri hii kule kwa mzee."
aliongea Shebby ndipo mkuku alikimbilia kwenye gari pamoja na Cj4 ili kuwahi nyumbani kwao ambako ilionesha wazi kuna matatizo mazito.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (62)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_________________________
___________________

"Nani huyo kapiga simu?"
aliuliza kwa sauti nCj4 wakati huo Shebby aligeuza gari kwa fujo na kugonga mti upande wa nyuma kabla hajatia gea ya mbele na kukanyaga mafuta kwa fujo bila kujali kishindo cha nyuma alipogonga kumetokea madhala kiasi gani.
"Nani kakupigia Shebby?"
aliuliza tena Cj4 huku akibamiza dashboard kwa kofi kali baada ya kuona Shebby yupo kimya huku akili yake ikiwa mbali sana.
"Ni mfanya kazi... Ni dada wa kazi kiongozi... aaagh! anaongea huku analia na nilisikia sauti za vitu vikiongwa gongwa..."
aliongea kwa pupa Shebby wakati huo barabara waliyokuwa wanapita mbele yake kulikuwa na kijiforeni kilichomfanya ahamie bara bara ya pili huku akivipana vile vizuizi vidogo vya barabara na kusababisha gari iruke ruke na kutaka kudondoka pasi nae kujali kuwa anaingia upande usiomruhusu ambao haukuwa na magari mengi na wala hakupunguza mwendo Shebby aliendelea kukanyaga mafuta huku akizikwepa kwepa gari zilizokuwa zinakuja mbele yake.

Kelele za honi zilisikika kwa fujo kama zile kelele za mavuvuzela katiaka kombe la dunia kule south pindi Shebby alipokuwa anakosana kosana kugongana na gari nyengine zilizokuwa zinakuja mbele yake na hiyo yote ilikuwa kutaka kuwahi nyumbani kuzuia matatizo yaliyokuwa yanatokea muda ule akihofia mr X asiwadhuru watu wote wa familia yake hususani baba na mamaake pamoja na mkwewe ambae ni Hussein bubu.
"Cj4 ushauri wako safari hii umeniponza. Aaaagh! umeona kumuacha Hussein bubu nyumbani matatizo yanatokea na kuwaumiza watu wasiohusika kabisaaaaa aaah! ona tunawaponza watu wengi zaidi? Ni bora tungemueka sehemu ya kumlinda wakati tukimsaka Mr X."
alilalama Kamishna Shebby huku machozi yakimtoka wakati kichwa chake kilipotengeneza mazingira ya nyumbani na kuona jinsi wazazi wake wanavyoumizwa na watu wa Mr X.
Wakati Kamishna Shebby akilalama Cj4 yeye alikaa kimya na kuvuta picha na kuona lazima Hussein ndie aliyeanzisha kasheshe huko baada ya kugundua kitu kuhusu Mr X, na si wala kwamba kuna mtu zaidi kavamia ile nyumba na kusababisha mauaji.

Gari iliiingia mkuku na kugonga geti hadi walinzi walistuka mno na hapo Kamishna Shebby alipiga teke mlango mdogo wa geti baada ya kushuka kwenye gari huku akiwa ameikamatia bastora ndogo mkononi na kustaajabu kukuta walinzi wakiwa wamejificha kwaajili ya kupambana na uvamizi waliotaraji kutokea na wao kushangaa kuona ni Kamishna Shebby.
Tofauti ya Shebby kwa upande wa Cj4 yeye hakuingilia pale getini zaidi alizunguka eneo la nyuma ya ukuta na kurudi nyuma kutafuta speed ya kukimbia kidogo kabla hajaruka beki kavu tatu zilizompeleka moja kwa moja hadi ndani ya fance sehemu kulipokuwa na bustani ya kupumzika na bwawa kubwa la kuogolea na ajabu zaidi Cj4 alijipanga kwa vita akiwa mikono mitupu.

* * * *

"Zaaainaab.. Zaiiiiinaaaab.. Zainaaaaaabuuuu leo na wewe lazima ulipe damu ya mwanangu."
aliongea Hussein bubu huku akipiga hatua kumsogelea mama Shebby kwa hasira pale chini alipokuwa anasote huku akilia kwa uchungu.
"Hapaanaaaa, hapaaanaa .. aaah! Haaapaana Mume wanguu."
alijitahidi kutoa sauti mama Shebby japo hakufanikiwa kuitoa kwa nguvu kama vile alivyoilazimisha ila ilitosha kusikiwa na Hussein.
"Mume wako? Mume wakoo!! hahahaha Mume wako unaemlilia huyu Shetani mtoa roho za watu? hahahaa nakusafirisha sasa hivi umfate huko aliko ila kwanza nataka unijibu swali moja Zai... KWANINI ULINIGEUKA NA KUSABABISHA KIFO CHA MWANANGU NA KUNIHARIBIA MAISHA YANGU YOTE???"
Aliuliza Hussein kwa hasira iliyokuwa inamfanya hadi atetemeke mwili mzima pindi alipokuwa amemfikia mama Shebby ambae ni kweli kabisa ndie Zai wake yule yule.
"Hapana Hussein, hapana sikujua kabisa kama yangekuja kutokea mazito kiasi hiki wala sikuweza kuyafanya yasiendelee kutokea aaahggggg nimejiponzajeeee mieeeee."
aliongea kwa uchungu Zai na kuendelea wakati huo Hussein alikuwa anazidi kutetema kwa hasira akingojea jibu la Zai kabla hajaanza na yeye kumponda ponda kichwa chake kwa kile chuma kilichotapakaa damu.
"Hussein, unastahiri kabisaaaaa kufanya haya Mume wanguuu......."
"STOOOOOP. Nihadithie kwanini na wala usinite Mume wangu. Utafanya nikuue kabla hata sijasikiliza jibu lako."
alimkatisha kwa hasira na kumpelekea Kofi moja kali lililomfanya Zai kupasuka lipsi ya mdomo baada ya kujing'ata kwa kupigiza kichwa pale kwenye ngazi.
"sawaaaa... sawaaa .. sawa..aaaghhhhh, wala sikumwambia Mr X akuue, wala sikupanga mwanangu azushiwe kuuliwa nawe pamoja na mimi mwenyewe, wala sikuyajua hayo yoteee Hussein. Naomba uniaminiiiii... Ila tatizo wewe hukuwa Mume wangu wa Kwanza kunioa na kunilipia mahali japo ulikuwa mwanaume wa kwanza kuniingiza katika ulimwengu wa mapenzi.
Sikuona jinsi gani ya kukwambia ukweli hadi unielewe na kuniruhusu nikaishi kwa mume wangu. Hussein najua leoo upo sahihi na mimi ndie niliekuwa nastahiki kulipa nafsi za hao wote.. Lakini unadhani ningefanyajeee? huyo Mr X ndie mume wangu kabisa wa kwanza aliyejulikana hadi na wazazi wangu..... wewe umemjua bibi tu Hussein lakini mimi nilikujua muda mrefu kabla hatujahamia Arusha.
Na ahadi yako ya utotoni hasa vile ulivyonambia kama utani naona leo inakuwa kweli aaaaaaaah!! Nataka ujue kabla hujaniua kuwa mimi ni KINOGE rafiki ako wa utotoni ZUNGU."
aliongea kwa uchungu zaidi Zai na kumshangaza tena Hussein baada ya kutajiwa kwa mara ya pili jina la Zungu na kukumbuka siku aliyokubaliwa kuwa na mahusiano na Zai alimwita jina hilo lakini alijikuta anachoka zaidi na kushangaa baada ya kujua kitu ambacho hakuwahi kukijua kumbe Zai ni Kinoge msichana waliyependana mno toka watoto na mara ya mwisho walipoteana wakiwa darasa la tatu.
"Haaa, KINOGE??!!"
Alitahayuri akiwa bado na hasira Hussein na ndipo kichwani mwake ilipokuja taswira na picha ile ya Kinoge pindi walipokuwa watoto.

^^^^^^^^^^
^^^^^^

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (63)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_______________________
____________

^^^^^^^
(>>><<<) ^^^^^ (>>><<)
..............................
ZUNGU => Kinoge Ona huyu ndio mtoto wetu, huyu ndio mimi hapo na huyu wewe harafu huyu aliyelala hapa adui nimekufuma nae anataka kuninyang'anya nimempiga nimemuua sasa nakupiga na wewe hapo hahaha nakuacha unalia harafu nam beba mwanangu tunaondoka hukoooo.
KINOGE => hahaha Zungu bwana, sasa kama wewe baba na mimi mama unafikiri adui atatoka wapi? tutakuwa tunapendana kama baba angu na mama angu si eti eeh?
ZUNGU => haya ila mi nitampenda sana mwanangu kama baba alivyokuwa ananambia kuwa mimi ndie ndugu yake na sio mamaangu kwani ana ndugu zake. Na wewe utakuwa na ndugu zako na mimi ndugu yangu mwananguuu.
KINOGE => Jamani Zungu, utakuwa unanipiga?
ZUNGU => Akuuu, ila nikikukuta na adui nitampiga hadi afe na wewe nitakupiga kibao kimoja tu..
^^^^^^
(<<<>>>) ^^^^ (<<<>>>)
.....................

Yalikuwa ni mawazo ya Hussein bubu pindi alipokumbuka mara ya mwisho kuongea na Kinoge siku hiyo majira ya jioni walipokuwa wanacheza mchezo wa kibaba baba huku akiwa ametengeneza watu wa kufinyanga kwa udongo na Kinoge alikuwa anapikapika kwenye vifuu.
Maneno ambayo aliwahi kuyaongea kitoto toto katika michezo ya watoto leo hii yamekuwa na ushabihiano mkubwa sana na kilichokuwa kinatokea japo hakuwahi kuwaza, kuhisi wala kujua kama Zai ndie rafiki ake wa utotoni yule aliyekuwa akimwita mchumbaake kabla ya wazazi wake kuhama na hakujua walihamia wapi na hata alipokua mkubwa ilifika wakati Hussein alisahau kabisa habari za Kinoge.

Lakini mbali na hayo yote bado msimamo wa Hussein ulibaki palepale, alishadhamiria kumuua na Zai na alikuwa anasubiri jibu moja tu lenye sababu za msingi kwani yote yale aliyokuwa anazungumza Zai ilikuwa kama anazunguka tu.
"Uwee Kinogeee uwe Zaaiii nataka kujua kwanini ulifanya yote yale na kuwa tayari kuimwaga damu ya mwanangu kinyama namna ile hata kichwa chake nisikionee?? Wee ni mwanamke wa aina gani!!??? Lazima leo Ufe na hii si kwa niaba yangu tuu, bali ni kwa niaba na damu ya mwanangu mliyeniekea viganja vyake mfukoni ili mkanifunge vizuri Wanyama Mbwa wakubwa nyiee... Hii ni kwaajili ya damu ya mwangu Mwin she heeeeeee...."
aliongea kwa uchungu Hussein na kukikamatia vizuri kile chuma huku akiwa kanyoosha mikono yake juu kwa niaba ya kuanza kumshushia kisago mama Shebby au Zainabu au kwa jina la utoto Kinoge.
Lakini akiwa kakamata kile chuma akinyanyua mikono kabla hajakishusha kichwani mwa Zai, ndipo alipopiga ukelele wa kukanusha kile alichokisema na kukiamini Hussein.
"HAPANAAAA, SIJAWAHI KUUA DAMU YANGU."
Kauli hii ilimfanya kwanza Hussein asite na kumuuliza Zai.
"Unamaana Gani? Nini kilitokea juu ya Mwanangu?!!"
"Hakuna kibaya chochote kilichompata mwanetu Mwinshehe... Mwanao mzimaaaa na ni rafiki ako mkubwa tuuu..."
"NINI? Unamaanisha nani? Kamishna??"
"hiiiiihiiii Nisameeeeheeee .. Ni kweliiiii Kamishna Shebby ndie mtoto wetu yuleyule Mwinshehe hiiiiigggr ... Eeee Munguuuu wanguuuuuuu"
Aliongea mama Shebby na kumzidisha machungu na taharuki Hussein aliebaki katumbua macho huku akiwa haamini kile anachokisikia masikioni mwake.
"NINI???!"
"Ndio hivyoooo aaah!! kweli mimi ni mkosaaaaji lakini Shaaban ndie mwnetu yule yule Mwinshehe na hata ile alama bado anayo pale nyuma ya shingo karibu na bega japooo aaaagh haaataa Mwin-chaaande umemuuua bila kutambuaa ukweli huuuuuuu"
kilio cha mama Shebby sambamba na maneno yake kilizidi kumkasilisha Hussein bubu ambae alizidi kutetemeka kwa hasira kuhu machozi yakimtoka na kuchirizika mashavuni huku yakisukuma damu iliyomgandia Hussein ambayo ilimrukia pindi alipokuwa anamuua mzee Mwinchande Mr. X.
"Ina maaaaanaaa Zaii.. aaah UmeniekaaUchiiii umenitukanisha vya Kutoshaaaa!!!!! HaaH! siamini mimiii Zainab?? Kinoge?? Mwanamke wa ndoto zangu leo acha maneno yangu yatimieeee"
aliongea kwa uchungu sana Hussein huku akizidi kunyanyua juu kile chuma na kukaza mikono.
"Wanawake ni Wauaji... Aaaagh! Wanawake ni Wauaji nyinyiii... Ona kwa sababu yako watu wangapi wamekufa Zai..Ona ulivyonitukanishaaa... Onaa sasaa wanangu mwenyewe nimewaoza mwenyeweeeeee!!! haaaaaaaa...
siwezi kumlaumu Asha wala Shebby iiiiiihhh Umenitukanajeeee!!? Kinogeee Hustahiri kabisa kubaki hai.. Hustahiri kabisa kuishi Zaiiii hata ninavyokuua leo sipaswi kuhukumiwa kwa hilo kwani hukumu yangu ya kukuua ilishapitishwa na kuitumikia miaka mingi sanaaaaaaa Zai kuishi sasa HUSTAHIRIIII"
Aliongea kwa hasira sana Hussein na sasa alikuwa anataka kushusha kile chuma kichwani mwa Zai ambae alijua sasa mwisho wake umewadia na hakuwa na ujanja wa kumkimbia Hussein bubu pale zaidi ya kufumba macho kusubiri kusikia chuma kikitua kichwani mwake na kusambaratisha fahamu zake zote kabla ya kuiacha dunia na kwenda kwenye makazi ambayo hajui yakoje.
Lakini kabla Hussein bubu hajashusha kile chuma kichwani kwa aliekuwa mkewe miaka hiyo bi Zainab ndpo ghafraaaaaaaaaaa mvunjiko wa kioo cha dirisha ulisikika sambamba na mtu aliyevaa mavazi ya polisi magereza mwenye cheo kikubwa alieonekana akiingia kwa mtindo wa kuruka huku mikononi akiwa kakamata mguu wa kuku (bastora ndogo) kishupavu kabisa na pindi alipoangukia tu mule ndani sekunde ileile kwa mbali alipomuona Hussein bubu akiwa anataka kumuua mamaake mzazi huku kushoto kwake akiuona mwili wa babaake mzazi ukiwa umepasuliwa vibaya sehemu za kichwa, nae palepale akiwa kakunja goti mguu mmoja alipiga kelele za uchungu huku akimfatulia risasi yule mtu aliemsimamia mamaake akitaka kumshushia vyuma vya kichwa na alimtambua kabisa kuwa yule ni nani ila aliamini kuwa amechanganyikiwa.
"HUSSEEEEENIIII BUUBUUUUU"
Alipiga ukelele Kamishna Shebby huku akiachia risasi mfurulizo kumuelekezea Hussein lakini sekunde ile ile kwa style ya ajabu kabisa alistukia kiatu kikubwa aina ya buti kikitua mikononi mwake Kamishna Shebby na kumshuhudia mwanaume wa shoka Cj4 akitokea upande ule wa juu kwenye ngazi na si kwa kushuka ngazi bali ni kwa kuruka nje ya ngazi na kutua pale alipokuwa anadondoka Hussein bubu na kumdaka kimaajabu na kubimbilika nae hadi maeneo ya mlango wa jikoni ambapo Cj4 aliingia na Hussein bubu na kujibanza nae nyuma ya Friza la kuekea nyama jikoni.
"aaaaaghrrr Na-kuuu-ku-mbuu-uu-k-kk-kaa raf--f-fiki--ang-gu"
aliongea kwa shida Hussein bubu mara macho yake yalipokutana na macho ya Cj4 aliekuwa kampakata nyuma ya lile friza lililokuwa karibu na mlango wa kuingilia jikoni.
"Polee rafiki angu mimi nipo hapa. Utapona tu"
"We-ni-As--ss-sskari?"
"Kweli rafiki angu mimi naitwa Cj4 ni askali niliyetumwa na serikali kwaajili ya kujua ukweli wako uliomfanya Shebby ashambuliwe kule Mkuyuni ila sasa kila kitu kipo sawa rafikiangu jikazee"
aliongea harakaharaka Cj4 huku akimuangalia kwa huruma Hussein bubu ambae damu zilianza kumvuja mdomoni na hata nyengine kuchuruzika kwenye mikono ya Cj4 na kugundua kuwa kuna risasi zilimpata Hussein mgongoni na kujilaumu Cj4 moyoni kuwa alichelewa kumuokoa Hussein.

"Cj4 kama umeungana na huyo Muuaji wa familia yangu tambua na wewe ni adui yangu sasaaaaa.. Aaaaaaggggggghh"
aliongea kwa hasira Shebby pindi alipoinuka na kuiokota bastora yake pale ilipodondokea na kuanza kuelekea kule jikoni alibimbilikia Cj4 na Hussein bubu.
"Mwananguuuuuu Shebbyyyyy usimuuue Husseeeeein ni babaaakoooo"
alipiga ukelele Zai ambae ni mamaake Kamishna Shebby ili kumzuia mwanae kutoendelea kufanya kile alichokifanya muda mfupi uliopita baada ya kufatua risasi mfurulizo zilizomfanya abaki kainama huku akiziba masikio na macho kwa uoga.
"Shebiii mwananguuuuu nisikilizeeeee"
alizidi kupiga kelele Zai lakini Shebby hakujali wala kusikia maneno ya mamaake kwa hasira alizokuwa nazo kwa kuhisi pia huenda na mamaake alikuwa kachanganyikiwa kwani anawezaje kumtetea mtu aliyekuwa anataka kumuua muda si mrefu? na tayari kamuua hadi mumewe? aliona wazi mamaake kachanganyikiwa na alikuwa tayari kupambana na Cj4 ambae alionekana kumtetea Hussein bubu.
("Huyu sasa anazidi upuuzi, acha kwanza nimfunze kuwa wanaume wanapokuwa kazini hutanguliza umakini mbele na si upendo.")
ilikuwa ni sauti ndani ya moyo wa Cj4 huku akimtoa mapajani mwake Hussein bubu pindi aliposikia vishindo vya hatua za minyato vya Shebby vikiwa vimekaribia pale mlango wa jikoni.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (64)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_________________________
________________

"Shebby mwanangu mimi Sijachanganyikiwaaaa wala huyooo unaetaaka kumuua hajaachanganyikiwaaaa... Nataka Ujue mimi ndie Zainab mke wa Hussein na wewe ndie mtoto wake aliyesingiziwaa kamuuaa na huyooo unayejuaa babaako ndie MR X.."
kauli hii ya mama Shebby aliyokuwa anaiongea kwa sauti ya uchungu sana na maumivu ndiyo iliyomfanya Shebby asiamame ghfra na kujikuta hadi ile bastora iliyokuwa mkononi mwake ikimdondoka chini kwa mshtuko mkubwa na kugeuka kumtazama mamaake aliekuwa anasota kumfata pale aliposimama mlango wa kuingilia jikoni.
"Mwananguuu Shebby, Hussein ndie babaako kweli kabisaaa. Ni kweli kabisaaa kweli sisi wanawakeee ni wauajiii aaaaaaaaaghhhh Nisamehe mwananguuuu"
aliongea huku akilia Zai akiwa amekamata miguu ya Shebby aliejikuta anashindwa kuongea lolote zaidi ya kuchezesha midomo tu kwa mtetemo ambao ulikuwa haukujulikana kama ni hasira au maumivu.

Maneno yale pia yalisikiwa vizuri sana na Cj4 na hata Hussein mwenyewe aliekuwa anahangaika na roho yake huku kila alivyojitahidi kuongea ndivyo damu zilipozidi kumvuja mdomoni na kubaki anaongea na Cj4 kwa kumtazama tu na alifanya hivyo hata pale Cj4 alipotaka kumlaza chini kwa kujiandaa kumuadhibu Shebby, Hussein bubu alimtazama kwa jicho lile la kumzuia asifanye hivyo.
"MAMAA !!! Ina maana...."
alitaka kusema kitu Shebby na kujikuta akishindwa ndipo alipokimbilia ndani mule jikoni kumuangalia Hussein bubu na kumkuta akiwa kashikiliwa na Cj4.
"Amini hivyo Shebby ukweli huyu ndie babaako."
alikazia Cj4 pindi Shebby alipoingia ghafra na hapo Hussein alijikuta kama anapata nguvu tena mara baada ya macho yake kukutana na uso wa Shebby na kumuashiria asogee pale na ainame.
Kwa mwendo wa 'sielewi' na taharuki nyingi alisogea Shebby na ajabu alipoinama tu Hussein aliweza kumuinamisha zaidi na kumuingiza mkono begani mwake kupitia ile kora ya shati ya Shebby na hapo mkono wa Hussein ulikutana na uhisio wa alama kama ile ya lengelenge mtu kaungua ama viuvimbe vyeusi vinavyowatoka watu (sunzua) kikiwa kwa urefu kuelekea maeneo ya begani.
Shebby alistuka na kutaka kuutoa mkono wa Hussein lakini Cj4 alimzuia aache na baada ya Hussein kuridhika aliutoa ule mkono huku akiwa katabasamu hali iliyowashangaza na hata mamaake Shebby nae aliingia kule jikoni kwa mtindo ule ule wa kusota mithili ya mlemavu huku akiwa bado analia huku akimsisitizia Shebby kuwa yule ndie babaake.
"ww-wa-ww-waa-aa-n-.."
alibabaika kusema Hussein na kujikaza kumwambia Shebby na Cj4 pale kwa mara nyengine na wote wakiwa wametaharuki Hussein bubu akarudia tena.
"uwwwan-aa-ang-uu Wa-na-wa-ke ni- Wa---u-aj-i."
na hiyo ndio ilikuwa kauli ya mwisho ya Hussein bubu na kuaga rasmi dunia akiwa mikononi mwa Cj4 huku pembeni yake alikaa mwanae ambae ni Shebby na kwa mbele mlangoni alionekana Zainab mamaake Shebby.
"BAABAAA"
Aliita kwa nguvu Shebby na kujipiga piga kichwa kwa majuto kwani alijua fika risasi zilizofatuliwa kwa mikono yake mwenyewe Shebby ndio zilizosababisha umauti wa mtu ambae alikuwa hajui kwanini moyo ulimsukuma mno kumsaidia na leo hii anajua akiwa amemuua kwa mkono wake akijua anamtetea mtusahihi kumbe sivyo.
Lakini toka hivyo Shebby alisimama na kutoamini kama yule ni babaake na yule ndie Mr X na wazo hili lilipomjia alikumbuka kauli ya yule marehemu Mnyungunyungu kuwa mr X ana alama usoni nahapo alijikuta anaingiwa roho mbaya nusu chizi Shebby alirudi pale ilipokuwa maiti ya mtu aliyeamini siku zote ni babaake na kuanza kumpekua usoni ambapo alikuwa na mdevu nyingi na katika hali ambayo hakuitaraji ni kweli aligundua alama ya X iliyokuwa usawa wa chini ya kidevu karibu na koromeo na hapo ndipo alipoanza kuamini sasa kuwa kweli yule mtu aliyedhani babaake alikuwa ndie mr X na jina X lilitokana na ile alama yake ambayo huwezi kuiona kwa kumtazama tu, lakini alijiuliza kwanini yamekuwa yote yale? ndipo hapo kwa uchungu mno Shebby alianza kulia huku akimuuliza swali mamaake kwanini imetokea yote hayo.
"Maaaaaa Why? kwanini mama yamekuwa yote hayaa? aaaaghh"
Maumivu aliyokuwa nayo Shebby hayapaswi hata kusimuliwa kwa jinsi alivyokuwa anaumia huku akifikiria kwanza kamuoa dadaake, pili kamuua babaake wa kweli, tatu ni kwanini mamaake aliishi na siri iliyokuwa inapoteza roho za watu kila siku???
"Mwanangu Shebby ni kweli sistahiri kabisa kuishiii aaaaah! leo nimejifunza wakati tayari ni too late, ila naamini mwanangu mimi ndio chanzo cha yote hayaa... Eee Mungu naomba unipe tu hukumu inayostahiki juu yangu ..... Shabaan mwanangu vyovyote utachoamua unisamehe ama usinisamehe lakini ukweli mimi ndie chanzoooo aaaaaaaah! Ama Kweli sisi Wanwake ni Wauaji."

*<>*<>*<>*<>*<>*
^^^^^^^
CHANZO
^^^^^^^
*<>*<>*<>*<>*<>*<>
( MIAKA 50 NYUMA )
.................................
...............

Ilionekana familia moja ya bwana na bibi Juma wakiwa katika kupanga panga vitu vyao husasi mabegi na kadhalika huku vijana wengine watatu walionekana kubeba viti, mbao za kitanda sambamba na magodoro wakipeleka nje na kupakia kwenye gari moja aina ya Canter iliyopaki karibu kabisa na ile nyumba ikionesha dhahiri bwana na bibi Juma walikuwa wanahama sehemu ile na kuhamia sehemu nyengine kwenye makazi mapya.

Wakati heka heka za kuhama zikiwa zinaendelea, upande wa pili kulipokuwa na nyumba inayotazamana na ile ambayo walikuwa wanaishi bwana na bibi Juma alionekana kijana mdogo wa kiume mwenye umri usiopungua miaka 12 akiwa amekaa mlangoni ameshika tama huku akiwa na huzuni kubwa wakati anaishuhudia familia ile ikihama pale mtaani kwao.
Moyo ulimuuma sana yule mtoto ambae alikuwa maarufu pale mtaani kwa watoto wenzie kwa jina la Zungu japo jina lake halisi halikuwa hilo.
Kilichokuwa kinamuumiza zaidi si kuhama kwa bwana na bibi Juma bali ni kuondoka pamoja na mtoto wao mdogo wa kike aliyekuwa na umri wa miaka 8 ambae alikuwa ni rafiki ake mkubwa sana shule na mtaani walicheza wote na mara nyingi walipenda kujiita baba na mama.
"Kinoge mbona humuagi rafiki ako Zungu si unamuona alivyopooza"
aliongea bwana Juma kumuambia mwanae yule wa kike ambae nae alionesha kutoipenda kabisa ile safari na alijisikia moyo kumuuma hata kumuaga kwa mdomo rafiki ake zaidi ya kumuangalia kwa jicho huruma na kumnyooshea mkono wa kwaheri pindi alipokuwa anapandishwa ndani ya gari ile mara baada ya kila kitu kumalizika kupakiwa.
("wewe ndie rafiki niliekuzoea, leo hii unaondoka na kuniacha mwenyewe. Najua huko utapata rafiki mwengine utayecheza nae kama mimi kibaba baba lakini jua kama nikimuona nitamuua kwa kua atakuwa tayari adui yangu.")
aliwaza maneno mazito sana yule mtoto Zungu pindi alipoishuhudia gari ile ikiondoka eneo lile la mtaani kwao na kumuachia msiba mzito wa upweke moyoni mwake.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (65)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
__________________________
________________

"Hussein mwanangu, usiwe mnyonge hivyo. Ndugu yako nipo hapa si nishakwambia...? mimi ndio ndugu yako babaa"
ilikuwa ni sauti ya mwanaume mtu mzima iliyosikika nyuma ya mlango alipokaa mtoto Zungu ambae jina lake halisi alikuwa anaitwa Hussein.
Sauti ile ilimfanya Hussein ageuke huku machozi yaliyojazana machoni muda mrefu alipokuwa anawaangalia kina Kinoge wakihama bila kupepesa macho, yalianza sasa kutiririka mashavuni mwake na kumtazama kwa uchungu yule mtu aliyemsemesha.
"baba, babaa unajua inauma sana. sasa wewe umewezaje kukaa mwenyewe na kuvumilia bila kulia pindi mama alipoondoka?"
aliuliza mtoto Hussein na kumfanya yule mtu ambae alikuwa ni babaake mzazi amnyanyue pale na kumkumbatia kwa nguvu huku akimsihi atulize kwanza moyo kwa kumshikashika kichwa akizichezea nyele zake ndogo za kipilipili huku mkono mwengine akimpigapiga mgongoni.
"Mwanangu Hussein, mbona ni rahisi sana baba...! ni rahisi mwanangu twende ndani nikakuhadithie"
aliongea babaake Hussein na kumchukua mwanae mpaka chumbani kuwapisha wapangaji wengine waendelee na shughuli zao mida ile pale ukumbini waliposimama jilani na mlango wa kutokea.

"Mwanangu mamaako amekuacha ungali una miaka mitano lakini japo nilimkumbuka ila haikuwa sababu ya kunifanya niwe mnyonge na kukosa kabisa furaha. Unajua kwanini?"
alianzisha maongezi babaake Hussein pindi walipokua wamekaa kitandani pale chumbani kwao.
"hapana baba, sijui"
"Kwa sababu wewe ulikuwepo, unajua kwanini uwepo wako ulikuwa sababu ya mimi kukosa huzuni na kuwa na furaha mbali ya kuwa mamaako hakuwepo tena?"
"Hapana baba sijui."
"Kwa sababu wewe ndie ndugu yangu na yule alikuwa mke wangu na ndio maana ameolewa tena na mwanaume mwengine na hata huko anaweza kuondoka tena na kuolewa pengine."
"aaah, sasa baba na mimi mama sio ndugu yangu?"
"Hapana mwanangu, wewe ni zaidi ya ndugu yako kwa sababu wewe ni mwanae na yeye ni mamaako unapaswa kumuheshimu na kumtembelea mara kwa mara."
"sawa baba, kwa hiyo Kinoge sipaswi kumlilia kwa kua sio ndogo yangu na huko aendako anaweza kupata rafiki kama mimi na wakihama tena atamuacha na kwenda kupata rafiki mwengine ikawa hivyohivyo eeeh.."
"Ni kweli kabisa mwanangu, hutakiwi kumuweka sana moyoni mwanamke mwengine zaidi ya mamaako mzazi ambae hawezi kuondoka na kukuacha moja kwa moja hata uwe uweje, ila hawa wengine mwanangu usiwaamini kabisa na kuwaeka sana moyoni kwani wataweza kukusababishia maumivu na mateso makubwa pindi watapogeuka na kwenda kwengine."
"sawa baba"
"Ndio hivyo mwanangu hupaswi kuumia mimi nipo na hata kama nisipokuwepo amini wa kukusaidia kweli ni mwanaume mwenzako japo wanawake ndio wanaoonekana kuwa na mioyo mepesi ya kusaidia lakini bado msaada wa ukweli upo kwa mwanaume baba. haya nyamaza wewe ni mmwanaume shika hela hii kanunue chapati uje tunywe chai"
"Asante baba nimeelewa, nami nakuahidi sitoumia tena kwa sababu ya Kinoge"
aliongea Hussein na kufuta machozi baada ya kuchukua pesa kwenda kununua hivyo vitafunwa huku akimuacha na tabasamu zito babaake.

* * * * *

Safari yao iliwachukua masaa mengi garini siku hiyo tokea asubuhi ile walipoliacha jiji la Dar na kuingia jijini Arusha majira ya saa moja usiku ambapo safari bado iliendelea mpaka kwenye vijiji vya mbali na Arusha mjini na huko ndiko kulikokuwa na makazi mapya ambayo walihamia familia ya bwana na bibi Juma pamoja na mtoto wao kipenzi aliyeitwa Kinoge.
"haaa! mamaa ndio tumefika hapaa!!?"
aliuliza kwa mshtuko Kinoge pindi alipoyaangalia mazingira waliyofikia kwa nje ambapo muda huo wale vijana waliopakia vitu kule jijini walikuwa wanavishusha wakipewa maelekezo pa kuviingiza na bibi mmoja ambae ndie alikuwa mwenyeji wao aliyewapokea.
"Kinoge kwani wee unapaonaje si pazuri tuu.. tena huku kuna maembe na machungwa kibaoo unayopenda furaaaahi basii."
mama alijaribu kumliwaza mwanae ambae sasa alikuwa tayari kakunja uso kutokana na kuchukizwa na mazingira yale ya kijijini.
Aliangalia kwanza hakukuwa na umeme, hakukuwa na barabara nzuri, nyumba zilikuwa zipo mbalimbali hali iliyomuumiza Kinoge na kuona ni afadhali wangemuacha jijini Dar na rafiki ake Zungu asingekuwa mpweke kuliko kuletwa pale ambapo aliamini hata marafiki wa kucheza nao kama Zungu hawakuwepo.
"iiihhhhhhyyaaaaaaaaaa.. sipaaatakiii mimiiii... Nirudiisheeeni kwa Zunguuuuu"
alianza kulia kwa sauti Kinoge na mamaake kujitahidi kumnyamazisha wakati huo babaake alikuwa anasombelea vitu na kuvipanga kwenye ile nyumba pamoja na wale vijana.

Baada ya shuguli zote za uhamiaji kukamilika na ile gari waliyokuja nayo kuanza safari kuelekea mjini na hatimae sasa Kinoge aliamini kuwa kweli wamefika na hasa pale alipokuja babaake na kumwambia.
"Mwanangu Kinoge, maisha ni mlima leo unapanda kesho unashuka harafu maisha ni popote usiangalie mazingira kwanza ukayakimbia unafikiri hata kule mjini kulikuwa vile? kule napo kulikuwa kama huku.. Watu wakahamia na kupasafisha wakaishi na kupatengeneza hadi leo umepaona vile. Basi hata huku napo kutakuwa kama vile endapo tutakaa na kupatengeneza. Haya twende ndani ukasalimiane na bibi eeeh"
Maneno ya babaake ndio yaliyompa nguvu Kinoge na kupiga moyo konde kuwa tayari kuanza maisha mapya.

Bwana Juma ambae ni baba mzazi wa Kinoge yeye alikuwa ni mwalimu wa shule ya msingi na wakati huo alikuwa amepata uhamisho wa huko Arusha ambapo aliuomba yeye mwenyewe ili apate nafasi ya kurudi nyumbani kwa mamaake ambae alikuwa mzee na alihitaji uangalizi wake na kwa kuwa miaka mingi aliipoteza Dar mpaka anazaliwa Kinoge na kufikia umri ule alikuwa hajawahi kufika pale kijijini lakini sasa hawakuwa na budi wote kwa pamoja walihamishia makazi kijijini kabisa.
Na huo ndio ukawa mwanzo wa Kinoge kupotezana na Zungu.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (66)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_______________________
________________

Maisha ya pale kijijini yalikuwa magumu sana kwa Kinoge na si ugumu wa kula au kuvaa bali ni ugumu wa kuchangamka na marafiki.
Hakukuwa na watoto wengi kama ilivyokuwa Dar na mambo yao yaliendeeshwa kimira sana tofauti na Dar walivyokuwa wanaishi kizungu na kujiachia sana.
Na hata alipoamishwa shuleni bado mambo yalikuwa magumu na alikosa kabisa marafiki wazuri walioendana na rafiki ake aliyemuacha Dar ambae alikuwa amemzoea kwa jina la Zungu.

Upweke uliendelea kwa Kinoge miezi mitatu zaidi kabla ya siku moja ambapo alishuhudia ugeni wa watu kadhaa nyumbani kwao walioeka kikao na wazazi wake kwa muda mrefu huku yeye akiwa amekaa nje na mtoto wa kiume aliyekuja na wale wazee ambae yeye alionekana mkubwa kuliko Kinoge na kuliko hata rafiki ake wa Dar Zungu.
"Eti wewe unaitwa nani?"
Kinoge alimuuliza rafiki ake yule mpya waliekuwa wanacheza wote pale nje.
"Naitwa Mwin-Chaa-nde umeona mjina wangu huoo!!!? wewe jee?"
alijibu yule mtoto na kumuuliza tena Kinoge swali
"Mi naitwa Kinoge."
"KINOGE!!!?"
"Eeeh"
"hahahahahahaaaaaaaaaaaa"
"sasa mbona unanicheka?!"
"Una jina la Kishaaaambaa Duh!.. Kinoge??!"
alicheka sana na kustaajabu yule mtoto wa kiume aliyejitambulisha jina la Mwinchande na kulicheka jina la Kinoge kabla wazazi wake hawajatoka mara baada ya kumaliza kikao mule ndani na kuagana nae huku Kinoge akiwa amekasirika kwa kuchekwa na Mwinchande juu ya jina lake.

Na huo ndio ukawa mwanzo wa Kinoge kukutana na Mwinchande ambae nae alihamishiwa shule ile aliyokuwa amepelekwa lakini tofauti Mwinchande alikuwa darasa la sita huku Kinoge ambae awali alikuwa anaingia darasa la tatu ila alianzishwa tena la pili kutokana na kuwaishwa sana shule.
Mazoea yao yaliyoambatana na utani ndio ikawa sababu Kinoge kutaka kubadilishiwa jina na wazazi wake ambao awali walijua ni mambo ya utoto lakini walipoona mtoto wao anang'ang'ana sana na kukosa furaha na amani shuleni na mtaani ndipo alipofika la tatu walifanya masahisho ya jina Shuleni na kumwita jina la Zainab.
Jina ambalo lilitolewa na bibiake, mama wa babaake waliekuwa wanaishi nae pale kijijini.

Kuanzia siku hiyo Kinoge alifurahi sana na kulitangaza kila sehemu jina lake jipya huku akiwa hataki kabisa mtu amwite jina la Kinoge.
Safari hii alimtambia rafiki ake yule ambae hakujua wanakoishi lakini ilikuwa kawaida kila baada ya siku mbili wazazi wake walikuwa wanakuja kukutana na wazazi wa Zai kuzungumza na katika hali ya kushangaza siku hiyo Zai alishangaa kuona wazazi wa rafiki ake wakija kwao huku mikononi wakiwa wameshika kamba zilizokuwa zinawavuta Ng'ombe wawili wakubwa na kuwaingiza katika zizi moja la miba lililokuwa awali kwaajili ya mbuzina kuwachanganya wale ng'ombe.
Awali ya yote Zai alikuwa hajui nini Kinaendelea kwani mifugo ilizidi kuletwa taratibu na hatimae baada ya mwaka mmoja lilijengwa zizi kubwa lililokuwa na Ng'ombe sita sambamba na mbuzi wanane wote wakiwa wameletwa na wale wazazi wa yule rafiki ake wanaetaniana taniana aliyeitwa Mwinchande ambae mwaka huo ndio alikuwa yupo darasa la saba huku Zai akiwa darasa la tatu.

Kumbe nyuma ya pazia kilichokuwa kinaendelea na ambacho kimeongelewa na wazazi wa pande zile mbili ni juu ya kuwaunganisha watoto wao ili watapokuwa wakubwa waishi pamoja.
Na hivyo wazazi wa Mwinchande walikuwa wanalipia kabisa mahali ya mtoto wa bwana Juma ambae ni Zai ili awe mke halali wa mtoto wao wa kiume ambae ni Mwinchande.
Habari ile ambayo kumbe hata Mwinchande alikuwa anaijua na pindi alipokuwa anamwita Zai mke wangu nae Zai akimwita Mwinchande mume wangu akihisi ni utani tu bila kujua kuwa tayari kuna ukweli ndani yake hadi siku moja alipoitwa na wazazi wake na kumwambia kuwa anapaswa awaheshimu sana wale watu aliokuwa anawaona wanakuja na Ng'ombe pale nyumbani kwani wamelipia gharama za yeye kuja kuishi na Mwinchande baadae pindi atapomaliza masomo yake.
Ilikuwa ni kawaida kimila kipindi hiko kuwaoza watoto wangali wadogo japo serikali ilipiga marufuku suala hilo na kuwapa adhbu kali kisheria wale waliobainika kuwaoza mabint zao wangali watoto lakini pia ilikuwa ngumu kuwagundua kama ilivyokuwa kwa Zai na Mwinchande ambao wazazi wao waliwahimiza kuhusu shule.

Baada ya shughuli za kimila kukamilika kipindi hiko Mwinchande alimaliza darasa la saba na Zai ndio alikuwa anaendea darasa la Nne waliunganishwa kwa kufungishwa ndoa ya siri nyakati za usiku na kuanzia siku hiyo kila mmoja alipewa nasaha na kuonywa na wazee kuwa asije kuthubutu kumtaka mtu mwengine wa kuishi nae hapo baadae kwani tayari wao ni mke na mume na watapokuwa wakubwa hawataoana tena bali wataishi pamoja na kuanzia siku hiyo jukumu la huduma za Zai lilisimamiwa na wazazi wa Mwinchande.

* * * * *

Mikosi ilianza kumkumba Hussein miezi michache baada ya kumpoteza kwa kuhama rafiki ake kipenzi aliyekuwa akitaniana nae kama mkewe na hatimae babaake kipenzi ambae ndie aliamini rafiki wa ukweli nae alifariki dunia.

lilikuwa ni zaidi ya pigo kwa mtoto Hussein japo ndugu wengi walitaka kumchukua lakini hatimae aliondoka na mamaake ambae nae haikupita miezi mitatu alifariki ghafra na kuzidi kuongeza pengo la uyatima moyoni mwa Hussein na hapo ndipo alipochukuliwa kulelewa na mjombaake kaka wa mamaake lakini bado hakuwa tena na furaha kwa kuwapoteza wazazi wake mfurulizo namna ile pia aliumizwa mno na maneno ya watu yaliyokuwa yanasemwa mitaani kuwa wale wazazi wake wote walikuwa na virus vya Ukimwi na ndio ilikuwa chanzo cha kuachana kwao miaka mitano iliyopita.
Aliumia sana Hussein kwa kuwa tayari alikuwa darasa la nne na mambo ya Ukimwi walishaanza kufundishwa tokea darasa la tatu na alijua kuwa ni ugonjwa m baya na wa aibu mtu kukutwa nao kwa hiyo wanaohadithia wazazi wake walikuwa na ugonjwa huo aliwachukia sana na kuwaona ni watu wabaya upande wake.

Maisha na kwa Mjomba hayakuwa ya kudumu sana baada ya kuchukuliwa na babaake mkubwa aliyekuwa mganga wa kienyeji lakini huko nako alikaa muda mchache kabla shangazi yake kumchukua baaaaasi ilimradi Hussein alikua kwa kulelewa kama mpira wa kona mpaka ile siku alipowashangaza watu kwa kusema anataka aishi mwenyewe kwenye nyumba ya kupanga.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (67)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_____________________
___________

Maisha yalienda ilimradi siku zinaenda na Hussein alisoma kwa Shida mpaka anamaliza darasa la saba hapo ndipo alipoanza kuhangaika mitaani kufanya kazi mbalimbali ili mradi mkono uende kinywani na hakuchoka kujituma.
Muda wote alipenda kujichanganya na watafutaji wenzake huku akiwa na ndoto siku moja maisha ataweza kuyamudu nae kujenga nyumba kutimiza mawazo ya babaake ambae mpaka anafariki hakuweza kuwa na nyumba japo alitamani kufanya hivyo.

Wahenga walisema 'Mungu hamtupi Mja wake' na ndivyo ilivyokuwa kwa Hussein miaka sita baada ya kuhitimu darasa la saba alibahatika kupata kazi kwenye kampuni moja ambayo iliweza kumlipa pesa zilizomuwezesha kuyamudu sasa maisha yake na kuheshimiwa hata na baadhi ya ndugu zake kwa juhudi alizozionesha na hapo sasa alianza kuyafurahia maisha.

Kipindi hiko alikuwa ana umri wa miaka 21 na hapo ndipo alipoanzisha mahusiano na msichana mrembo aliyeitwa Mariam huku akiwa kasahau mambo mengi ya utoto akiwemo yule rafiki ake wa utotoni aliyeitwa Kinoge.
Mapenzi yake na Mariam yalikuwa mazuri mwanzoni lakini baadae kidudumtu kiliingia mara baada ya mwaka mmoja wa mahusiano yao pindi alipokuwa anaangalia kipindi cha YA WALIMWENGU kupitia Becker TV ambapo kulikuwa na mada ambayo msimuliaji alilaani kuwa Wanawake ni Wauaji.
Mada hiyo ndio iliyompotezea muda Hussein na kusahau juu ya ahadi ya kukutana na mpenzi wake yule ambae tayari karibu robo tatu ya ndugu zake walishamjua.
Ugomvi wao wa ghafra uliosababishwa na kile kipindi mara baada ya Mariam kufika pale kwa mchumbaake na kukuta muda mwingi akiwa bussy na tv kuliko yeye na zaidi alichefuliwa na kile kipindi hali iliyomfanya Mariam aondoke kwa hasira na katika kumtafuta kwake Hussein kwa mara ya kwanza ndipo alipoyaelewa maneno ya kile kipindi mara baada ya kuchezea kichapo cha aibu ndani ya fukwe za coco pindi alipomfumania Mariam akiwa na mwanaume mwengine na hapo ndipo alipoapa kutopenda tena, lakini mapenzi yana nguvu sana na hii ilidhihiri mwaka mmoja baadae baada ya maisha ya kibachela walipopata safari ya kikazi Arusha huko ndipo alipokutana na msichana ambae awali alitokea kumuota kabla hawajaonana kweli akiwa na rafiki ake.
Msichana huyo ndie Zai kama alivyoota lakini hakuwahi kufikiria kama Zai yule ndie Kinoge rafiki ake wa utotoni.

* * * * *

Kwa upande wa maisha ya Zai mara baada ya kuozeshwa kimila akiwa bado mtoto maneno ya wazee na wazazi wake yalimjengea hofu ya kuja kukiuka kuwa hajaolewa au kuwa na mwanaume mwengine.
Na kwa hali ile ilibidi ampende zaidi Mwinchande na hasa mara baada ya wazazi wake kufariki kwa ajali mbaya ya gari iliyotokea Arusha mjini na hatimae Zai alibaki yatima pindi akiwa darasa la sita wakati huo Mwinchande alikuwa kidato cha tatu akisomea Arusha mjini na ilikuwa kila mwisho wa wiki alirudi kijijini na kuleta zawadi mbalimbali kwa mkewe ambae nae sasa alikuwa anaelewa nini maana na aliamini kuwa Mwinchande ndie mumewe na hana uwezo wa kupinga hilo.
Alisahau kabisa habari za Hussein ama Zungu kama alivyopenda kumwita mwenyewe na aliridhia ndani ya moyo wake pindi atapomaliza masomo kuishi na Mwinchande kama ilivyo mipango kwani alikuwa tayari ni mumewe.
Lakini kipindi cha kiangazi watu wakiwa katika kuandaa mashamba bahati mbaya lilitokea janga la moto pale kijijini.
Moto ulioacha misiba ya kihistoria na huzuni kubwa kwa wanakijiji mara baada ya nyumba nyingi kuungua na mifugo ikiwemo nyumba ya kina Mwinchande ambapo msiba mzito ulitokea mara baada ya wazazi kushindwa kujinusuru na kuteketea huku Mwinchande pekee ndie akisalimika halikadhalika kwa kina Zai napo bibi pamoja na mjukuu wote walifanikiwa kutoka salama japo nyumba yao na zizi vyote viliungua.

Ulikuwa ni zaidi ya msiba kilio kila kona serikali na manispaa ya jiji la Arusha waliwasaidia wahanga wa moto na kuwatengea eneo kulekule kijijini.
Kwa upande wa Mwinchande alikuja Shangazi yake aliekuwa anaishi jijini Dar na kujitolea kuondoka nae kumuendeleza kielimu Huko japo shangazi alijua kuwa tayari mwanae ana mke aliyeozeshwa kimila lakini alipuuzia na kuona ni mila potofu na ndio sababu ya kumuacha Zai aendelee kusoma pale kijijini na hata siku Mwinchande anaondka na Shangazi ake mara baada ya kumaliza misiba bibi alimpa moyo mjukuu wake Zai kwa kumwambia asiwe na wasiwasi mumewe anaenda kutengeneza maisha yao na atarudi kumchukua.

Lakini mambo yalizidi kwenda kombo baada ya miaka kuzidi kupita toka kuondoka kwa Mwinchande na shangazi yake huku maisha pale kijijini yakizidi kuwa magumu mpaka pale alipomaliza darasa la saba na kujikuta akikaa zaidi ya miaka miwili mbele bila kuuona uso wa mumewe hadi siku moja alipokuwa katika mizunguko Arusha kipindi hiko alikuwa na umri wa miaka 17 alistuka pindi alipoitwa jina na mtu asiyemfahamu japo kwa mbali sura yake haikuwa ngeni ila alificha.
Hakujua mwnzo kama yule ndie Zungu wake kipindi cha utoto na Zungu hakujua kuwa yule ndie Kinoge wake wa utoto na kwa bahati mbaya hayo majina yalikuwa yashakufa kwao wote. Zungu alifahamika zaidi kwa jina la Hussein ambalo Kinoge alikuwa hajalizoea na Kinoge pia alifahamika kwa jina la Zainab ambalo Zungu hakuwahi kulisikia kabisaaaaa.

ITAENDELEA
 
WANAWAKE NI WAUAJI..!? (68)
BY - MTOTO WA BECKER (The Special Thinker)
_______________________
_____________

Baada ya kukutana na yule kijana ambae hakutaka kumwambia jina lake alilijua vipi wakati hawajawahi onana Zai aliondoka huku akiwa na namba ya simu ya yule kijana ambae alimsihi na kumwambia atapompigia ndipo atamwambia amelijuaje jina lake.
Na kutokana akilini mwa Zai kuhisi kama kuna taswira ilikuwa inamjia juu ya yule kijana hakusita sana kuichukua ile namba huku akiwa nae anaumiza kichwa pindi alipoondoka kufikiria wapi aliwahi kumuona yule mtu.

Lakini kwa bahati mbaya alipofika nyumbani alisahau kabisa ile namba mara alipoiweka kwenye begi na yote ilichochewa na mawazo mengine aliyokuwa nayo juu ya mumewe Mwinchande kwani licha ya uzuri aliobarikiwa Zai lakini bado aliweza kujidhibiti na kujitunza kwa wanaume mbalimbali akikwepa vishawishi akiamini yeye ni mke wa mtu lakini huyo mumewe amekuwa mpotevua na miaka ikawa inazidi kupogoma.

* * * * *

Walionekana vijana wapya wa polisi wakiwa wanapangiwa maeneo baada ya kuhitimu mafunzo ya pili ya jeshi la polisi na kuajiliwa kuwa askali rasmi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Kila mtu alifurahi pindi majina yalipokuwa yanatajwa na mahala husika ambapo miongoni mwa majina ya wale askari wapya lilisikika jina la Mwinchande na mahala alipopangiwa ambapo ilikuwa ni mkoa wa Pwani Kibaha.
Alikuwa ndie yeye Mwinchande mume wa Zai mara baada ya kusoma mpaka kidato cha sita na kwenda kujiunga na jeshi la polisi baada ya kufanyiwa mpango na shangazi yake.

Nyota ilikuwa upande wake Mwinchande toka ajiunge na jeshi la polisi kwani baada ya mwaka mmoja zilitokea nafasi adhimu ya vijana watano waliohitajika kwenda israil kuchukua mafunzo mapya yaliyokuwa yanatolewa jinsi ya kupambana na waharifu wanaotumia akili nyingi tofauti na zile mbinu zilizokuwa zinatumiwa na nchi nyingi za kiafrika hususani Tanzania walichofundishwa ni jinsi ya kumdhibiti na kupambana na muharifu kwa utumia nguvu zaidi na silaha inapobidi.
Nafasi ilikuwa imetolewa kila nchi askari watano na kwa bahati nchi ya Tanzania miongoni mwa askari wengi walioomba hiyo nafasi, mwisho wa siku majina matano yalivyotoka na jina la Mwinchande lilikuwa miongoni mwa Askari wanaohitajika kwenda huko Israel ambapo kozi nzima ilikuwa ni ya miaka miwili.

Na huo ndio ukawa mwanzo wa Mwinchande kuvuka mipaka ya nchi na kuzidi kutanua milango yake ya kufikiri na kujengeka fikra pana huku moyoni mwake akimkumbuka mke aliyeozeshwa na wazazi wake na mara zote Mwinchande aliamini yule ndie mkewe na hatoolewa na mwengine kwa kuwa wao hawakuachana.
Na kwa jinsi alivyokuwa anamchukulia Zai moyoni na kumpenda aliamini atamkuta tu hata kama atakaa zaidi ya miaka mitano huko Israel na hii ilimpa moyo kutokana kabla hajaondoka alimpa maagizo rafiki ake aliyekuwa mganga wa kienyeji ambae alifahamiana nae mara baada ya kuugua ghafra kipindi akiwa mgeni pale pwani na kuonekana matatizo yaliyomkumba yalikuwa ni ya kienyeji baada ya watu washirikina kumjaribu na hapo ndipo alipopewa msaada na mkuu wake wa kituo ambae alikuwa ni Inspector Cyplian kwa kumpeleka kwa mtaalam wa mitishamba na ramli aliyesifika ambae alikuwa anapatikana katika kijiji cha Hakipo kilichokuwa maeneo ya Kibamba pembezoni kabisa mwa jiji la Dar.
Hapo ndipo urafiki wa Mwinchande na Mganga yule ambae alifahamika kwa jina maarufu la Mnyungunyungu ulianza baada ya kuwa anamtembelea mara kwa mara na hata zilipotokea zile nafasi alimlilia Mnyungunyungu aangalie uwezekano wa kulifanya jina lake ling'ae na liwe miongoni mwa majina yatayochaguliwa kwenda kwenye hiyo kozi.
Na kweli jina lake lilipotoka Mwinchande alizidi kuamini kuwa Mnyungunyungu kweli ni kiboko na ndio kikawa chanzo kabla hajaondoka alimuhadithia kila kitu kuhusu mkewe aliyeozeshwa angali shule na alimuomba Mnyungunyungu afanye dawa ambayo itamuwezesha pindi atapoonana na yule mkewe asije kubadilika yaani ampende vilevile kama zamani hata kama kuna mwanaume atakuwa kashaingilia kati kipindi yeye hayupo.
Na hili ndilo lililomuaminisha Mwinchande ambapo pia alimuomba shangazi yake kama atapata muda aende akamchukue mkewe kule kijijini japo alijua kwa Shangazi yake kufanya vile itakuwa ngumu kutokana yeye hakuipenda kabisa ile mila iliyotumiwa.
Na baada ya wiki kadhaa toka uteuzi ule ufanyike hatimae ndipo Mwinchande alipoungana na wenzake kwa safari hiyo ya nchini Israel kwaajili ya hayo mafunzo maalum.

* * * * *

Siku zilikatika kwa upande wa Zai maisha ya kusubiri yalizidi kumchosha lakini bibi ndie alikuwa mstari wa mbele kumsihi na kumpa moyo kuwa mumewe atarudi tu kwani ile ni mira na haivunjiki kamwe.
"Bibi mi sidhani kama kweli Mwinchande atarudi kunichukua wakati huko mjini nasikia kuna wanawake wengi wazuri kama nini.."
"Hapana mjukuu wangu Zainab Mwinchande ni wako, yule ni mume wako.. Atarudi tu kukufata wee subiri mjukuu wangu, kikubwa ni kuzidi kujisitiri na kusali kila siku.. Usiache kabisa kusali na kumuomba Mungu yeye ndie mjuzi."
alisisitiza sana bibi Zai mara Zai alipokuwa anahoji juu ya suala lile la kurejea tena kwa Mwinchande.

Lakini baada ya muda tena ndipo ilipokuja barua pale kijijini iliyotokea jijini Dar ikimtaka Zainab afanye safari ya kwenda huko ambapo anaishi mumewe.
Na barua iliandikwa na shangazi wa Mwinchande mara baada ya kuona Mwinchande akimuulizia sana juu ya kumfata huyo mkewe ambae yeye hakumpenda kabisa wala kumuhitaji kwani alihisi kile kilichofanyika ni dhulma tu kuwachagulia watoto wanaume/wanawake wa kuishi nao.
Lakini aliona kwa kuwa Mwinchande mwenyewe king'ang'anizi, aliamua kutuma tu hiyo barua kama ataweza huyo bint aende kama atashindwa basi na ndani ya barua pia kulikuwa na namba yake ya simu.

Moyo wa furaha ulimripuka sana Zai baada ya kupata ile barua na kufanya mawasiliano na shangazi mtu.
Nahapo sasa ilibaki kazi ya kufuafua na kujiandaa kwenda Dar es salaam jiji ambalo aliondoka akiwa bado mtoto na toka miaka hiyo ilikuwa ni mara ya kwanza kurejea tena jijini.
Lakini wakati akipekuapekua ndipo alipokiona kile kikaratasi chenye namba za simu za yule kijana aliyewahi kutana nae siku moja na hapo ndipo alipokumbuka kumpigia akiwa na shauku ya kujua alimjuaje? kwani upande wake alishindwa kabisa kumkumbuka vizuri.
Mara baada ya simu kupokelewa na Zai kujitambulisha alimuuliza tena lile swali huku akimuomba amwambie walipoona na hadi kumfahamu kwani hawatoweza kukutana tena kutokana na safari yake ya jijini Dar.
Lakini alishangaa baada ya yule kijana nae kumwambia kua yuko huko huko Dar na pindi atapofika basi wataonana na atamwambia alimjuaje.

ITAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom