muyakb24
JF-Expert Member
- Jul 31, 2018
- 412
- 296
25EPS 25
========
"aaah! wea acha tu habari za wanawake ndio sitaki kabisa kuzisikia"
alijibu yule mkuu wa kituo huku akionesha yuko serious na kile anachozungumza na kumshangaza Shebby ambae alihoji.
"Kivipi tena John.?"
"Ndugu yangu yaliyonitokea ndio sitamani kabisa kutafuta familia kwa sasa wee acha tu, nahisi nina mikosi sana kwa wanawake"
"Duh! John.. kwani nini kilikupata mshkaji baada ya kuachana kipindi kile kozi ilipoisha wakati ulinambia ulitaraji kufunga ndoa siku si nyingi?"
"Ndugu yangu Shebby ni story ndefu sana ila nitakuhadithia kwa ufupi ilivyokuwa"
Aliongea John ambae alikuwa na wadhifa wa OCS kituo cha mkuyuni akiwa na cheo cha Inspecta na kuanza kukumbuka ilivyokuwa toka mara ya mwisho walipoachana na Shebby walipokuwa kwenye kozi maalum ya uongozi na usimamizi ndani ya idala ya ulinzi wa ndani miaka minne iliyopita ambapo John alianza kusimulia ilivyokuwa hadi kupelekea awe na msimamo wa kutohitaji kuwa na mwanamke kwa kipindi kile.
'''''
"Ndugu yangu, mkuu wangu kiukweli kama ulikuwa hujui leo nitakwambia ujue wazi ukae ukijua kuwa wanawake ni watu wa ajabu sana inatakiwa uwe na akili nyingi sana jinsi ya kuishi nao.
Kumbuka siku ile ya mwisho tulipokuwa tunaagana kwenye ile tafrija baada ya kozi kuisha nilikuonesha kwenye simu yangu picha ya mwanamke nilietaraji kumuoa baada ya kumaliza kozi na kupandishwa cheo kwani nilijua sasa maisha nitakuwa nishayaeka kwenye mstari tena kwa kuwa na mwanamke mzuri kama Tedy aaaah, nilijiona bonge la mjanja.
Sikia sasa ishu ilivyokuwa baada ya kuachana na kupoteana kipindi tulipomaliza kozi na kupewa likizo ya mwezi mmoja sikuamini nilichokikuta mtaani Dah!!..... Kumbe yule demu Tedy si alikuwa ananiigizia bwana, muda wote naeka nae malengo hata nikawa najinyima na kumtumia pesa tulipokuwa Kozini ili afungue mtaji wa saloon kama alivyonambia kumbe nae alikuwa anatumbua maisha na mpuuzi mmoja mchafumchafu mtoto wa mtaani pale na kunigeuza mimi chuma ulete.
Sio siri niliporudi almanusura niue mtu kwa hasira mara baada ya kupata data zote na nilipokuwa namuulizia kuhusu hiyo saloon alinizungusha zungusha kunipeleka hadi waliponasa kwenye mtego niliowatega ambapo kwa macho yangu niliwafuma wakiingia Guest moja huko Keko na nilipompigia Tedy kumuuliza alipo alivyonambia ndio nilizidi kuchoka daah! Eti 'ooh, nimeenda kwa bibi vikindu anaumwa sana nitakupigia baadae'...... Nilichomjibu nikamwambia kuwa hiyo guest haiitwi vikindu inaitwa Mumbu na hapo nilikata simu na kufata ushauli wa mzee wangu tuliekuwa wote kwenye gari ambae alinisihi mno nisipaniki wala kumchukia mwanaume aliyelala na mchumbaangu kwani mwenye makosa hasa ni mchumbaangu nami nikakubaliana na mzee nikaachana na Tedy toka siku hiyo nikampiga stop tusijuane tena.
sasa hiyo tisa kumi ni Angelina au malaika ndivyo nilivyopenda kumwita mtoto kutoka Arusha aliyekuja kufanya kazi za ndani nyumbani kwetu kipindi hiko kabla sijahamishiwa hapa Mkuyuni na kuwa ocs.
Angelina alikuwa mzuri, mwenye adabu na heshima, kila mtu nyumbani alimpenda kuanzia mzee mama na dada na hata tukashawishika tufanye mipango ili nimuoe na awe mmoja wa familia yetu.
Sasaa sijui nisemeee ujingaaaaa auu utahiiraa yani nashindwa kuelewa hawa wanawake vichwa vyao vilivyo kwani kipindi chote tunafanya mipango na kuzungumza na mamaake huko kijijini walionesha hali ya kukubali kumbe bwana yule mtoto Angelina alikuwa tayari mke wa mtu muda mrefu na alikuja Dar kufanya kazi za ndani kwa lengo la kumsubiri mumewe aliyekuwa migodini huko ataporudi nae arudi waendelee na maisha.
Sio siri hii iliniuma mno nilipokuja gundua na kushindwa kumuoa mwanamke ambae tayari moyo wangu ulishaelekea kwake na kuniangusha baada ya kusikia mumewe amerudi na mambo yamemuendea vizuri baada ya mgodi kutema na karudisha mapenzi kama kawaida.
Hapo nilipagawa sana na ndipo babaangu mzee Cyprian aliponihadithia kisa kimoja enzi zake kilichotaka kufanana na changu tena kutoka huko huko Arusha alimuona bint akiwa na askali mwenzake walipokuwa kikazi na kufanya utafiti na kueka nae mipango.
Lakini kwa kuwa mzee kipindi hiko tayari alikuwa na cheo kikubwa swala la ufatiliaji zaidi na habari alizituma kupitia kijana wake wa kazi ambae walikuwa marafiki kama mimi na wewe kufikisha salamu zake kwa familia ya yule binti na zawadi mbalimbali.
Kumbe bwana rafiki ake nae si alikuwa anampenda yule bint..!! na alipokuwa anaenda kule anajiwakilisha yeye ndie mtakaji na mzee wangu alipokuja kugundua ilikuwa tayari too late.
Lakini binti mwenyewe alimjua mzee wangu ila alikubali kumsariti na rafiki yake sijui kwanini yaani wanawake usiwaamini hata kidogo.
Ila kwa dua za mzee na jinsi alivyosononeka kumkosa yule binti ndipo ikatokea safari iliyomfanya nae rafikiake amkose yule bint na kuchukuliwa na jamaa gani sijui ambae mwishoe nasikia kumbe yule bwana alikuwa na tamaa ya utajiri si akamuua kinyama yeye yule binti sambamba na mtoto aliyezaa nae na hapo ikawa si Mzee wangu wala yule rafiki ake aliyeweza kuishi na yule binti lakini yoooote yalisababishwa na binti mwenyewe laiti angekuwa na msimamo awali wa kumkataa yule rafikiake mzee aliyeanza kumchombweza na kumpondea mzee pengine haya yale yote yasingetokea hadi kuangukia mikononi mwa huyo bwana aliyekuja kumuua.
Daaaah! basi bwana ndio hivyo mzee hamasa zake nilizielewa na baada ya hapo kila mwanamke ninaemuona mbele yangu kuna muda namuona kama kinyago vile kwa jinsi walivyonipotezea malengo na pesa bila faida yoyote. Saivi ishu yangu nikijisikia navuta cheche tu la bar basi tunamalizana kila mtu kimpango wake hahahahahaaaa.."
'''''''
Alimalizia kwa kucheka ocs John na kumuacha kamishna Shebby katika taharuki kubwa hata Kimaro nae alikaa vizuri pindi alipokuwa anaisikiliza story ya ocs John.
"Enhee, Mkuu wangu safari hii wapi sasa na wewe uko wapi"
aliuliza John
"Daah, nilikuja kwenye msiba huu uliotokea sehemu yako juu ya mganga wa kienyeji aliyekutwa amejichinja kibandani mwake sasa nilitaka kujua tafiti zenu mlipofikia na awali sikuwaza hata chembe kama ningekutana na mtu tunaefahamiana kama wewe"
"Oooh! ni kweli bwana Dah! uchunguzi wetu bado unaendelea taratibu ila tuliruhusu mazishi yaendelee baada ya ripoti ya daktari kuthibitisha kuwa hakukuwa na kiashilio chochote kuwa marehemu alishambuliwa zaidi ilionekana ni msongo wa mawazo ulichachamaa ghafra na kupelekea kujichinja.
Ila tukiwa kama polisi bado uchunguzi wetu hatujaufunga rasmi."
"Sawa vizuri John"
aliongea Kamishna Shebby huku mawazo yake yakiipitia story aliyosimuliwa muda mfupi na ocs John hasa kwenye kipengele alichonukuu story iliyomuhusu babaake kidogo ilimtia shaka Shebby na kuhisi kuna vitu vinaingiliana na story ile ya Hussein kuhusu mkewe Zai.
Alitamani kumuuliza zaidi lakini alitafakari njia ipi ya kumuingiza tena kwenye ile mada hadi afunguke zaidi kuhusu story ya babaake.?
Na ndipo hatimae Shebby aliliacha lile na kurudi kwenye azma yake juu ya prove aliyotaka kumuonesha Kiamro kuwa yule aliekufa si Mr.X japo alikuwa na kovu usoni.
"Sasa John hebu achana na ripoti ya daktari nihadithie kuhusu nyinyi mlivyopata taarifa ya kifo kile na mazingira mliyokuta hivi ni kweli yaliwapa picha kuwa yule mtu alijiua?"
aliuliza Shebby sasa akiwa serious kama alivyokuja na kumfanya hata ocs John kukaa makini kwa utulivu mara baada ya kuulizwa lile swali na kama kawaida yake Shebby aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali kulipokuwa na simu yake special aliyoitumia kwaajili ya kunasa sauti kwani ilikuwa na uwezo mkubwa sana wa kurekodi pindi ocs John alipoanza kuzungumza.
ITAENDELEA.....
Sent using Jamii Forums mobile app
