Sehemu ya 65
Nusu saa badaye, nilikuwa ndani ya ofisi ya daktari, alikuwa ni mwanamke mmoja wa makamo. Alionekana alikuwa na muda mrefu kwenye taalumu ya uganga.
“Tatizo nini?” aliniuliza. “Kifua kinauma.”
Nilipomjibu akaandika kwenye kitabu chake. Akaniuliza tena:
“Kinaumaje?”
“Ni kama kinawaka moto ndani kwa ndani.”
“Unamawazo?” alizidi kuniuliza. Nikatafakari kidogo swali lake kisha na mimi nikamuuliza.
“Kuna binadamu asiye na mawazo dokta?”
“Nina maanisha unamsongo wa mawazo kwenye maisha yako, hasa kwa siku za hivi karibuni?”
“Hapana.” Nilimjibu. Akaniuliza tena:
“Unafanya kazi gani?”
“Mimi ni mchezaji wa mpira.”
“Tatizo limeanza lini?”
“Usiku wa kuamkia leo.”
Akaendelea kuandika majibu yangu kwenye tabu lake la kumbukumbu.
“Kuna dawa nitakupa, zisipokusaidia rudi tena hapa. Sawa?”
“Sawa dokta.”
Aliniandikia tembe za vidonge fulani vitatu vya aina tofuati. Siwezi kabisa kusahau majina ya zile dawa. Tembe moja ilikuwa inaitwa Ampidox , nyingine inatwa Predistone pamoja na Panadol.
Nazikumbuka vizuri kabisa.
Tuliondoka na kurudi nyumbani tayari kwa kuanza dozi ya dawa hizo. Hali yangu ilikuwa bado ni tete, kila wakati nilikuwa nahisi maumivu makali na kifua kikitaka kulipuka kwa joto kali.
Tulipowasili, Cholo aliniacha sebuleni nipumzike, kisha yeye akaondoka na kwenda kuripoti klabuni. Nilichukua chupa ya maji safi na kumeza tembe hizo.
Ilikuwa ni kama baada ya dakika 20 baada ya kutumia vidonge hivyo... Nilipatwa na muamivu makali nashindwa hata kuyaelezea mfano wake.
Ndani ya mwili wangu kulikuwa ni kama vile kuna uji wa plastiki umemwagwa kwenye mifupa yangu. Nilikuwa nalia kama mtoto mdogo. Jasho lilikuwa linanichuruzika kama maji mwilini mwangu. Dunia ilikuwa inazunguka kwa kasi kama panga boi.
Ndani ya muda mchache nilipoteza fahamu, pumzi nazo zilikuwa zinakata kama utambi wa mwisho kwenye mshumaa unaovyoishilizia. Sasa dalili ya malaika mtoa roho ilikuwa waziwazi mbele yangu. Katika hali hiyo, nikawa nahisi kama kuna kundi la watu wameingia mule ndani kisha wamenizinguka.
Wakati fahamu zinanipotea kabisa, nikawa nahisi kama lile kundi la watu linaniangalia namna ninavyozama kwenye wingu la giza nene,