Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,168
- Thread starter
- #141
Sehemu ya 61
Pamoja na mateso aliyoniachia bado sikuweza kabisa kumtoa nafsini mwangu, sikuwa na funguo wa kumwondoa mwanamke huyo ndani ya moyo wangu. Sura nzuri ya chotara huyo, iliniganda kama gundi.
Ningefanya nini mimi zaidi ya kulipigania penzi langu.
Asubuhi ya siku ya pili, niliamkia mazoezini. Kama kawaida nilijituma na kupambana, nilizidi kumfurahisha kocha mzungu.
Baada ya mazoezi kumalizika meneja alitutangaziwa wachezaji jambo jipya.
Ilikuwa ni kuhusu maisha ya wachezaji wa timu hiyo. Alisema klabu ilikuwa imeazimia kutuweka kambi vijana wote.
Tulielezwa kwamba kuanzia kesho, wachezaji wote wa timu ya Mzizima tungeweka kambi sehemu moja hadi mwisho wa msimu.
Maana yake ni kwamba tungekuwa tunaishi pamoja. Wote kama familia moja. Muda wote hadi msimu utakapo malizika.
“Hii latiba itaanza kesho asubuhi, hivyo kila mchezaji, kesho, achukue kila kitu chake muhimu aje nacho klabuni. Wote tutakutania hapo na kwenda kwenye apartment iliyopangwa.
Katika kambi kutakuwa na taratibu mbalimbali ambazo tutawatangazieni. Lakini moja ya kanuni kubwa ni wachezaji kutotoka kwenda sehemu yoyote bila luksa maalumu,” meneja wa timu aliongea.
Nilihisi tumbo lote linachemka ndani kwa ndani. Ilikuwa ni lazima nishugulike na mambo yangu binafsi haraka iwezekanavyo.
Sikujua kwa nini latiba hiyo mpya ilikuja ghafla vile. Hata hivyo, wakati tupo katika vyumba vya kubadirishia nguo ili kila mchezaji arudi kwakwe ama makwao. Kuna minong’ono ikazuka, minong’ono hiyo ndiyo ikanipa jibu la awali. Juu ya kambi kuitishwa ghafla vile.
“Angalau watu tukaishi kambini. wengine walikuwa wanapata fursa ya kwenda kwa waganga kuroga wenzao ili wavunjike,” mchezaji mmoja aliropoka.
Nilitetemeka. Sikujua kauli hiyo kama ilinilenga mimi ama jamaa alijiropokea tu.
Watu wakacheka. Wengine kama wawili wakashadadia.
“Kweli kabisa.” Mwingine akasema: “Ila dawa ya moto ni moto. Ukirogwa na wewe roga.” Jasho jembamba lilinivuja makwapani. nilitamani kujua wale jamaa walijuaje kama kuna watu katika timu wanakwenda kwa waganga?
Pamoja na mateso aliyoniachia bado sikuweza kabisa kumtoa nafsini mwangu, sikuwa na funguo wa kumwondoa mwanamke huyo ndani ya moyo wangu. Sura nzuri ya chotara huyo, iliniganda kama gundi.
Ningefanya nini mimi zaidi ya kulipigania penzi langu.
Asubuhi ya siku ya pili, niliamkia mazoezini. Kama kawaida nilijituma na kupambana, nilizidi kumfurahisha kocha mzungu.
Baada ya mazoezi kumalizika meneja alitutangaziwa wachezaji jambo jipya.
Ilikuwa ni kuhusu maisha ya wachezaji wa timu hiyo. Alisema klabu ilikuwa imeazimia kutuweka kambi vijana wote.
Tulielezwa kwamba kuanzia kesho, wachezaji wote wa timu ya Mzizima tungeweka kambi sehemu moja hadi mwisho wa msimu.
Maana yake ni kwamba tungekuwa tunaishi pamoja. Wote kama familia moja. Muda wote hadi msimu utakapo malizika.
“Hii latiba itaanza kesho asubuhi, hivyo kila mchezaji, kesho, achukue kila kitu chake muhimu aje nacho klabuni. Wote tutakutania hapo na kwenda kwenye apartment iliyopangwa.
Katika kambi kutakuwa na taratibu mbalimbali ambazo tutawatangazieni. Lakini moja ya kanuni kubwa ni wachezaji kutotoka kwenda sehemu yoyote bila luksa maalumu,” meneja wa timu aliongea.
Nilihisi tumbo lote linachemka ndani kwa ndani. Ilikuwa ni lazima nishugulike na mambo yangu binafsi haraka iwezekanavyo.
Sikujua kwa nini latiba hiyo mpya ilikuja ghafla vile. Hata hivyo, wakati tupo katika vyumba vya kubadirishia nguo ili kila mchezaji arudi kwakwe ama makwao. Kuna minong’ono ikazuka, minong’ono hiyo ndiyo ikanipa jibu la awali. Juu ya kambi kuitishwa ghafla vile.
“Angalau watu tukaishi kambini. wengine walikuwa wanapata fursa ya kwenda kwa waganga kuroga wenzao ili wavunjike,” mchezaji mmoja aliropoka.
Nilitetemeka. Sikujua kauli hiyo kama ilinilenga mimi ama jamaa alijiropokea tu.
Watu wakacheka. Wengine kama wawili wakashadadia.
“Kweli kabisa.” Mwingine akasema: “Ila dawa ya moto ni moto. Ukirogwa na wewe roga.” Jasho jembamba lilinivuja makwapani. nilitamani kujua wale jamaa walijuaje kama kuna watu katika timu wanakwenda kwa waganga?