Simulizi: Soka Lilivyonikutanisha Na Shetani

Simulizi: Soka Lilivyonikutanisha Na Shetani

Sehemu ya 59

Nilipanda basi hadi Tabora mjini, kwa kuwa nilikuwa nimefika mapema. Nikachukua tax iliyonipeleka hadi mtaa wa Airport, nyumbani kwao Lawalawa.
Niliteremka garini nikaikabili nyumba hiyo. Siku zote nilikuwa na hofu ya kufika nyumbani kwao na mwanamke huyo.

Ila kwa kuwa nilikuwa nimekwisha amua kujilipua kwa ajili yake, sikuogopa chochote kumfuta mwanamke kwao.
Niligonga geti, muda mfupi badaye akatokeza mwanamume mmoja ambaye alionekana ni kama mfanyakazi wa ndani ya nyumba ile ya kifahari. “Habari yako, unasemaje?” mtu huyo aliniuliza bila kusubiri niitikie salamu yake.

“Naitwa Ajibu Maganga, nashida na Lawalawa.”
“Lawalawa!” “Ndio.”
“Kwani huna tarifa?”
“Sina, kuna nini kwani?”
“Baada ya ndoa yake, alisafiri kwenda kwa mumewe huko Uarabuni. Yemen.” Jamaa alisema.

Nilihisi nguvu zinaniishia miguuni, jasho likanichuruzika maungoni mwangu.
“Unasema kweli?” “Sina sababu ya kukudanganya,” jamaa alinieleza, uso wake ulionesha wazi wazi ukweli wa kile alichokuwa akizungumza. Macho yaliniiva, akili ilinizunguka.

Jamaa akaniuliza tena:
“Kwani wewe unatokea wapi?”
Sikupoteza muda wa kumjibu swali lake, niliondoka nikimwacha mwanaume huyo akinishanga.

Nilitembea huku nikihisi kifua chote kikichemka, nilijiona kama ninaye kaangwa kwenye sufuria la mafuta. Kuthibitishwa juu ya kuolewa kwa mwanamke yule ilikuwa ni zaidi ya maumivu moyoni.

Nilichukua tax nikamtaka dereva anipeleke hoteli yoyote nzuri. Dakika 20 badaye nilikuwa Ristalemi hoteli, baada ya malipo ya chumba, nilingia ndani, huko nilijifungia na kulia kama mtoto mdogo. Nililia penzi la Lawalawa, mwanamke huyo niliyemweka moyoni, nikamuhifadhi sehemu muhimu ndani ya moyo wangu.

Eti naye alikuwa amenipa pigo takatifu.
Niliitelekeza familia yangu hosipitali ya Bungando, mwanangu akafariki dunia kwa kukosa matibabu, nikamwacha mwanamke aliyenipenda kwa dhati. Yote kwa ajili ya Lawalawa.

Sasa naye alikuwa amenigeuka, amekimbilia kwa mwanaume mwingine. Halafu mpumbavu mimi nabaki nalia chumbani kama hayawani. Hapana haiwezekani. Siwezi kuwa bwege kwa kiwango hiki.
 
Sehemu ya 59

Nilifikiria nifanyeje ilihali Lawalawa na bwana wake wapo nchi za mbali, nitamfanya nini mwanamke huyo tapeli.
Kutwa nzima nilishinda ndani nikiwa namna ya kumrudisha Lawalawa mikononi mwangu. Akili yangu ilishindwa kabisa kukubaliana na kitendo cha kuachwa na mwanamke huyo.

Kwa masaa mengi badaye, nikawa nimekwisha pata mbinu ya kumrudisha Lawalawa mikononi mwangu. *****

Sikumbuki usingizi ulinipitia baada ya muda gani, ila ninachokumbuka katikati ya usiku mkubwa kuna sauti ya fulani ilikuwa inapita akilini mwangu.

Awali sauti ya hiyo ilipita kichwani mwangu kama ndoto. Nilikuwa nasikia kama kuna mwanaume anayegumia maumivu fulani makali sana.

Katikati ya miguno ile ya maumivu, nikawa nasiki kama kuna sauti ya wazee zaidi ya wawili wakiwa wanamwambia mambo fulani mtu yule mwenye maumivu kwa lugha ambayo haikuwa ngeni masikioni mwangu.

Hali hiyo ilinitisha sana, nikafumbua macho ghafla sauti zile ziliyeyuka. Jasho lilikuwa linanichuruzika taa ilikuwa imezima ndani kulikuwa na giza zito.
Ndoto niliyoiota ilikuwa ya mauzauza, hata hivyo nilibeza kwa kuona ni ndoto tu kama zilivyo ndoto zingine za kawaida.

Akili yangu ikarudi kwenye giza la chumbani, kwa nini ndani kuwe na giza.
Sikumbuki kama nilizima taa za chumbani kabla ya kupitiwa na usingizi. Sasa vipi chumba kiwe na giza. Nilisimama na kusogelea swichi ya umeme na kuwasha taa ile. Ajabu bulb ya umeme haikuwaka.
 
[emoji91][emoji91][emoji91][emoji91][emoji91]
 
Hii ya leo c ulikua unafidia inabidi utume episode za leo tatu(3)
 
Sehemu ya 60

Unatakiwa upake mwilini,”aliniambia.
“Duh!. We jamaa kweli kiboko.”
Kama nilivyosema mwanzo, Cholo alikuwa vizuri sana kwenye mambo hayo ya dawa za kienyeji.

Nilipaka yale mafuta na kwenda kulala. Uongo mbaya, usiku wa siku hiyo nililala usingizi mzuri tu. Sikukutana na mauzauza ya aina yoyote kama ilivyokuwa kule mjini Tabora.

Kuna kitu kingine nimesahu kukieleza.
Nimesahau kueleza kwamba, kwenye mazungumzo yangu na Cholo juu ya mambo ya kuroga na kujikinga sikuwa nimemshirikisha kabisa kwenye sakata langu na mpenzi wangu Lawalawa. Ambaye alinikimbia na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine.

Sikupenda kumshirikisha kwa kuwa jambo lile nililiona kama ni la binafsi zaidi ukilinganisha na mambo ambayo nimekuwa nikishirikiana naye.

Pia sikupenda anione udhaifu wangu. maamuzi niliyokuwa nimeyaazimia yangeweza kumstajabisha mwanaume yeyote. Nilipanga kumwendea Lawalawa kwa mganga wa kienyeji ili arudi mikononi mwangu.

Kama ningemshirikisha Cholo kwenye jambo lile angenichukulia mimi ni dhaifu wa kiwango cha mwisho kama sio mshamba kabisa wa wanawake.

Kwa mwanamke kumwendea mwanaume kwa mganga sio habari katika jamii zetu, ila mwanaume kumwendea mwanamke kwa mganga ni habari ya kusisimua.

Kwa kweli sikupenda kabisa kumwambia Cholo. Kwanza najua ambacho angenishauri. Angenitaka niachane na Lawalawa na nitafute mwanamke mwingine.

Nafsi yangu haikuwa tayari kwa lolote zaidi ya kumpata Lawalawa. Kwa wakati huo, moyo wangu ulikuwa na nafasi moja ya upendo, nilipoifungua na kumwingiza Lawalawa moyoni mwangu nilimfungia mlango na ufunguo nikautupa baharini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom