Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #201
Sehemu ya 75
”
“Ajibu, hebu achana na mawazo ya visasi.”
“Pili, hebu ona maisha yangu sasa yalivyo haribika. Kwa nini alinitendea jambo baya kama lile? Lengo lake lilikuwa ni lipi hasa?”
“Ajibu nimesema achana naye, Mungu ndiye mlipaji wa kila jambo?” “Kwa hiyo unataka nikae kizembe tu kusubiri mungu anilipie?”
“Muachie Mungu mume wangu, usipende kujikita kwenye shari zisizo za msingi na walimwengu” mke wangu alilalama. Hakupenda hata kidogo kuona mume wake naingia kwenye matatizo ya aina yoyote.
Sikumjibu, nililiweka kiporo chambo hilo. “Jambo la pili mke wangu,” nilisema huku nikiwamwangalia usoni. Nikaendelea. “Hatuwezi kuendelea kuishi na wazee hawa siku zote. Tunafanya nini mama?”
Mke wangu Pili, alinyamaza kidogo, akanisogelea na kulaza kichwa chake kifuani mwangu, kwa sauti yake ya upole naye akaniuliza:
“Hutaki tena kucheza mpira?”
“Hapana. Sihitaji, kuna msemo unasema, jitihada za mja haziwezi kushinda kudra za mwenyezi Mungu, nadhani hapa ni mwisho wangu wa mchezo wa soka. Mungu alinikadiria maisha yangu ya soka yaishie vile”
“Nimefurhi kusikia hivyo Ajibu. Na kama unatambua kudra za mwenyezi Mungu basi achana na visasi, sawa mume wangu?”
Sikumjibu. Akaendelea kuongea. “Lakini kuhusu jambo uliloniuliza nilikwisha liwaza tangu siku ya kwanza nilipofika hapa Kigoma, njia ni moja tu ya kuanzisha maisha yetu upya.”
“Ipi hiyo?” niliuliza kwa kiherehere.
“Kufanya biashara ya dagaa, kuzinunua dagaa za Kigoma hapa na kuzipeleka mjini Dar, hii inalipa sana na mtaji wake si mkubwa.”
“Una akili sana we mwanamke,” nilisema kwa furaha. Nikamkumbatia na kummiminia mabusu motomoto.
Siku chache badaye, mpango wangu namke wangu Pili, tuliwashirikisha mzee Mo na mkewe, nao bila choyo walitupa baraka zote.
“Lakini tungehitaji msaada wenu zaidi?” niliwaambi.
“Kama upi baba?” Bibi Mo aliuliza.
“Msaada wa kifedha, tunahitaji kama laki mbili na nusu tu.”
“Hilo mmepata. Kuna jingine?”
“Hakuna wazee.”
Kwa kweli, tulitokea kushibana nao mno. walituchukulia kama wanawe wa kuwazaa, hasa kwa kuwa binti yao wa pekee, ambaye alikwisha fariki miaka mingi akiwachia mjuuku aitwaye Mohammed ama Mo.
”
“Ajibu, hebu achana na mawazo ya visasi.”
“Pili, hebu ona maisha yangu sasa yalivyo haribika. Kwa nini alinitendea jambo baya kama lile? Lengo lake lilikuwa ni lipi hasa?”
“Ajibu nimesema achana naye, Mungu ndiye mlipaji wa kila jambo?” “Kwa hiyo unataka nikae kizembe tu kusubiri mungu anilipie?”
“Muachie Mungu mume wangu, usipende kujikita kwenye shari zisizo za msingi na walimwengu” mke wangu alilalama. Hakupenda hata kidogo kuona mume wake naingia kwenye matatizo ya aina yoyote.
Sikumjibu, nililiweka kiporo chambo hilo. “Jambo la pili mke wangu,” nilisema huku nikiwamwangalia usoni. Nikaendelea. “Hatuwezi kuendelea kuishi na wazee hawa siku zote. Tunafanya nini mama?”
Mke wangu Pili, alinyamaza kidogo, akanisogelea na kulaza kichwa chake kifuani mwangu, kwa sauti yake ya upole naye akaniuliza:
“Hutaki tena kucheza mpira?”
“Hapana. Sihitaji, kuna msemo unasema, jitihada za mja haziwezi kushinda kudra za mwenyezi Mungu, nadhani hapa ni mwisho wangu wa mchezo wa soka. Mungu alinikadiria maisha yangu ya soka yaishie vile”
“Nimefurhi kusikia hivyo Ajibu. Na kama unatambua kudra za mwenyezi Mungu basi achana na visasi, sawa mume wangu?”
Sikumjibu. Akaendelea kuongea. “Lakini kuhusu jambo uliloniuliza nilikwisha liwaza tangu siku ya kwanza nilipofika hapa Kigoma, njia ni moja tu ya kuanzisha maisha yetu upya.”
“Ipi hiyo?” niliuliza kwa kiherehere.
“Kufanya biashara ya dagaa, kuzinunua dagaa za Kigoma hapa na kuzipeleka mjini Dar, hii inalipa sana na mtaji wake si mkubwa.”
“Una akili sana we mwanamke,” nilisema kwa furaha. Nikamkumbatia na kummiminia mabusu motomoto.
Siku chache badaye, mpango wangu namke wangu Pili, tuliwashirikisha mzee Mo na mkewe, nao bila choyo walitupa baraka zote.
“Lakini tungehitaji msaada wenu zaidi?” niliwaambi.
“Kama upi baba?” Bibi Mo aliuliza.
“Msaada wa kifedha, tunahitaji kama laki mbili na nusu tu.”
“Hilo mmepata. Kuna jingine?”
“Hakuna wazee.”
Kwa kweli, tulitokea kushibana nao mno. walituchukulia kama wanawe wa kuwazaa, hasa kwa kuwa binti yao wa pekee, ambaye alikwisha fariki miaka mingi akiwachia mjuuku aitwaye Mohammed ama Mo.