Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,170
- Thread starter
- #181
Sehemu ya 69
“Umeweza kukaa mwenyewe!!” alibwatuka, uso wake ulionesha kunishangaa kwa kitendo cha kuniona nimeketi kitandani.
Nilibaki na utulivu wangu, sikujihangaisha kujibu maneno ya miss bantu huyo.
Alinisogelea uso wake ukisawijika kwa furaha kubwa. Alichota uji kwa kijiko kwenye lile bakuli na kuninywesha.
“Kunywa baba huu uji utakusaidia” alisema.
Kwa kweli yule mwanamke alinionyesha mapenzi makubwa mno. Nilikunywa ule uji kwa pupa, dakika chache badaye bakuli likabakia tupu. Mwanamke akabaki akiniangalia usoni kwa huruma.
“Hivi unaitwa nani wewe?” hatimaye nilimuliza.
Badala ya kujibu, binti akaninishika kichwa changu na kukivutia kwenye kifua chake. Akanikumbatia huku akibubujikwa na machozi. Kitendo hicho kikaniongezea maswali utitiri.
“Jina lako nani jama?” nilimuliza tena.
“Kweli umenisahau mume wangu?”
Shit!
Kumbe niliwahi kuwa na mke maishani? Nilimuoa nani, Lawalawa? Hapana. Lawalawa alikuwa mpenzi wangu tu, tulipendana kwa muda mfupi, mwarabu koko yule akaniacha na kwenda kuolewa na mwarabu mwenziye wa huko nchini Yemen sasa vipi tena na huyu miss tabasamu aniite mimi ni mume wake? Ni kimeo gani hiki Yarabi? nilijiuliza kimoyomoyo.
Nilijitoa kwenye kifua chake na kumwangalia. Nilimtizama sura yake kwa muda, nikaiingiza sura hiyo katika ubongo wangu, kidogo ni kama niliwahi kuiona mahala fulani hivi lakini bado sikumbuki ni wapi.
“Wewe ni nani lakini?” nilimuliza tena.
“Mimi ni Pili. Pili mkeo uliyezaa naye mtoto mmoja akafariki kwa saratani ya damu.”
Ewaa!!.
Sasa kila kitu kilifunguka. Kumbukumbu ya mke wangu Pili ikanifungukia ubongoni kama nuru ya jua la asubuhi lichomozavyo tokea mlimani.
N ikamkumbaka vema mwanamke huyo. “Pili!!” nilimwita.
Alinitikia kwa kichwa akanikumbatia tena kwa nguvu.
“Nilipatwa na nini mimi?” nikamuliza swali jingine.
“Ulirogwa mume wangu, walikuroga wenzio?” alisema.
“Wenzangu! Wenzangu gani?”
“Wacheza mpira wenzako, mapaka shume wale.”Pili alinieleza huku akiwatusi tena wachezaji wa mpira.
Maneno yale pia yakawa yanafungua kumbukumbu zingine zilizokuwa zimejifunga funga ndani ya kichwa changu. Angalau sasa nikawa najiwa na vipande vya kumbukumbu ya maisha ya nyuma.
“Umeweza kukaa mwenyewe!!” alibwatuka, uso wake ulionesha kunishangaa kwa kitendo cha kuniona nimeketi kitandani.
Nilibaki na utulivu wangu, sikujihangaisha kujibu maneno ya miss bantu huyo.
Alinisogelea uso wake ukisawijika kwa furaha kubwa. Alichota uji kwa kijiko kwenye lile bakuli na kuninywesha.
“Kunywa baba huu uji utakusaidia” alisema.
Kwa kweli yule mwanamke alinionyesha mapenzi makubwa mno. Nilikunywa ule uji kwa pupa, dakika chache badaye bakuli likabakia tupu. Mwanamke akabaki akiniangalia usoni kwa huruma.
“Hivi unaitwa nani wewe?” hatimaye nilimuliza.
Badala ya kujibu, binti akaninishika kichwa changu na kukivutia kwenye kifua chake. Akanikumbatia huku akibubujikwa na machozi. Kitendo hicho kikaniongezea maswali utitiri.
“Jina lako nani jama?” nilimuliza tena.
“Kweli umenisahau mume wangu?”
Shit!
Kumbe niliwahi kuwa na mke maishani? Nilimuoa nani, Lawalawa? Hapana. Lawalawa alikuwa mpenzi wangu tu, tulipendana kwa muda mfupi, mwarabu koko yule akaniacha na kwenda kuolewa na mwarabu mwenziye wa huko nchini Yemen sasa vipi tena na huyu miss tabasamu aniite mimi ni mume wake? Ni kimeo gani hiki Yarabi? nilijiuliza kimoyomoyo.
Nilijitoa kwenye kifua chake na kumwangalia. Nilimtizama sura yake kwa muda, nikaiingiza sura hiyo katika ubongo wangu, kidogo ni kama niliwahi kuiona mahala fulani hivi lakini bado sikumbuki ni wapi.
“Wewe ni nani lakini?” nilimuliza tena.
“Mimi ni Pili. Pili mkeo uliyezaa naye mtoto mmoja akafariki kwa saratani ya damu.”
Ewaa!!.
Sasa kila kitu kilifunguka. Kumbukumbu ya mke wangu Pili ikanifungukia ubongoni kama nuru ya jua la asubuhi lichomozavyo tokea mlimani.
N ikamkumbaka vema mwanamke huyo. “Pili!!” nilimwita.
Alinitikia kwa kichwa akanikumbatia tena kwa nguvu.
“Nilipatwa na nini mimi?” nikamuliza swali jingine.
“Ulirogwa mume wangu, walikuroga wenzio?” alisema.
“Wenzangu! Wenzangu gani?”
“Wacheza mpira wenzako, mapaka shume wale.”Pili alinieleza huku akiwatusi tena wachezaji wa mpira.
Maneno yale pia yakawa yanafungua kumbukumbu zingine zilizokuwa zimejifunga funga ndani ya kichwa changu. Angalau sasa nikawa najiwa na vipande vya kumbukumbu ya maisha ya nyuma.