Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,170
- Thread starter
- #221
Sehemu ya 77
Nilitembea nikipita mjini Malindi, Mji Mkongwe kisha Darajani. Nikapanda daladala ya Kiembe Samaki. Muda mfupi badaye niliwasili nyumbani kwa Sheikh Majeed Mapaka.
Nilimkuta sheikh huyo akiwa nje ya nyumba yake anasikiliza redio. Aliponiona akanilaki kwa ukarimu. “Ni wewe!” “Naam! sheikh ni mimi.
Asalaam alyekum.” “Walyekum wasalaam, karibu sana, habari za siku.” “Siyo salama ndugu yangu,” nilimwambia. Mganga huyo wala hakuniuliza kwa nini nasema siyo salama. Alichofanya ni kunikaribishia ndani, katika chumba cha kiganga kisha akaanzisha maongezi: “Haya nambie hujambo?” “Mimi mzima kimwili sheikh ila kiakili siko sawa”
“Nini tena?” “Ina maana hukuwahi kupata taarifa zangu sheikh?” badala ya kujibu na mimi nikamtupia swali. “Nizipatia wapi? Wewe na mwenzio hamkuwahi kurudi tena hapa.” “Sasa iko hivi... “ nilianza kueleza. “Jamaa walijibu mashambulizi bwana. Tena mashambulizi yao ilikuwa nusu nife.
Walinipiga kipapai nikawa kichaa aliyeshindikana huko mtaani.” “Acha wewe!” “Alaa! Washenzi sana wale watu wa Mbeya.” “Huyu huyu Mnyakyusa tuliyemzika jina makaburini! Kawezaje huyu mtoto lakini!!” “Huyo huyo!” “Eboo! Aliwezaje?” “Nitajulia wapi?” “Siyo bure wametumia uchawi wa kiwango kikubwa sana.” Mtaalamu yule alisema.
Nilimweleza kila kitu kilichonitokea maishani. Kadhalika, sikuacha kumueleza ukweli wa mambo mawili yaliyonipeleka Zanzibar siku hiyo. “Kwa hiyo unataka ufanyiwe kazi mbili tofauti?” Sheikh Majeed Mapaka aliniuliza baada ya kusikiliza maelezo yangu kwa makini.
“Tawire.” “Kumrudisha mchumba aliyeolewa nchini Yemen na kulipiza kisasasi kwa watesi wako?” Shekh Majeed Mapaka alihoji kwa msisitizo. “Swadakta.” “Sasa huyo mwanamke unayemtaka wa nini ilihali umenieleza unaye mke, tena ndiye alikusaidia kukupeleka kwa mtaalamu wa huko Kigoma.”
“Joto la penzi linalofukuta moyoni mwangu dhidi ya Lawalawa najua mwenyewe ninavyoteseka kwa kumkosa huyu mwanamke. Niko tayari kufanya lolote lakini Lawalawa arudi mikononi mwangu.”
“Gharama yake itakuwa kubwa kidogo, hasa kwa kazi ya kumrudisha mpenzi aliyeko mbali. Unajua kazi yenyewe ni kuvunja ndoa ya mtu? Mara nyingi kazi za hivi huwa zinasumbua sana.”
Nilitembea nikipita mjini Malindi, Mji Mkongwe kisha Darajani. Nikapanda daladala ya Kiembe Samaki. Muda mfupi badaye niliwasili nyumbani kwa Sheikh Majeed Mapaka.
Nilimkuta sheikh huyo akiwa nje ya nyumba yake anasikiliza redio. Aliponiona akanilaki kwa ukarimu. “Ni wewe!” “Naam! sheikh ni mimi.
Asalaam alyekum.” “Walyekum wasalaam, karibu sana, habari za siku.” “Siyo salama ndugu yangu,” nilimwambia. Mganga huyo wala hakuniuliza kwa nini nasema siyo salama. Alichofanya ni kunikaribishia ndani, katika chumba cha kiganga kisha akaanzisha maongezi: “Haya nambie hujambo?” “Mimi mzima kimwili sheikh ila kiakili siko sawa”
“Nini tena?” “Ina maana hukuwahi kupata taarifa zangu sheikh?” badala ya kujibu na mimi nikamtupia swali. “Nizipatia wapi? Wewe na mwenzio hamkuwahi kurudi tena hapa.” “Sasa iko hivi... “ nilianza kueleza. “Jamaa walijibu mashambulizi bwana. Tena mashambulizi yao ilikuwa nusu nife.
Walinipiga kipapai nikawa kichaa aliyeshindikana huko mtaani.” “Acha wewe!” “Alaa! Washenzi sana wale watu wa Mbeya.” “Huyu huyu Mnyakyusa tuliyemzika jina makaburini! Kawezaje huyu mtoto lakini!!” “Huyo huyo!” “Eboo! Aliwezaje?” “Nitajulia wapi?” “Siyo bure wametumia uchawi wa kiwango kikubwa sana.” Mtaalamu yule alisema.
Nilimweleza kila kitu kilichonitokea maishani. Kadhalika, sikuacha kumueleza ukweli wa mambo mawili yaliyonipeleka Zanzibar siku hiyo. “Kwa hiyo unataka ufanyiwe kazi mbili tofauti?” Sheikh Majeed Mapaka aliniuliza baada ya kusikiliza maelezo yangu kwa makini.
“Tawire.” “Kumrudisha mchumba aliyeolewa nchini Yemen na kulipiza kisasasi kwa watesi wako?” Shekh Majeed Mapaka alihoji kwa msisitizo. “Swadakta.” “Sasa huyo mwanamke unayemtaka wa nini ilihali umenieleza unaye mke, tena ndiye alikusaidia kukupeleka kwa mtaalamu wa huko Kigoma.”
“Joto la penzi linalofukuta moyoni mwangu dhidi ya Lawalawa najua mwenyewe ninavyoteseka kwa kumkosa huyu mwanamke. Niko tayari kufanya lolote lakini Lawalawa arudi mikononi mwangu.”
“Gharama yake itakuwa kubwa kidogo, hasa kwa kazi ya kumrudisha mpenzi aliyeko mbali. Unajua kazi yenyewe ni kuvunja ndoa ya mtu? Mara nyingi kazi za hivi huwa zinasumbua sana.”