Simulizi: Penzi ama kaburi?

Simulizi: Penzi ama kaburi?

Dah , Alex namfananisha na mwinjaku ana maneno mazuri na ushauri mzuri ndio anawapata madada wengi. Shadya na yeye kamburuza mwalimu wake wa Madras. Inasikitisha anayavaa mapenzi kwa kasi
 
Sehemu ya 56.

Maisha yalikuwa matamu mno, kwa Shadya hakutaka kusikia kitu chochote kuhusu Alex, alimpenda kutoka moyoni mwake, hapakuwa na mwanaume aliyekuwa na uwezo wa kuuchukua moyo wake zaidi ya huyo.

Penzi lake kwa Gibson lilipotea kabisa, na hakumkumbuka mwanaume huyo kwa lolote lile. Kwa kuwa penzi lake kwa Alex lilikuwa kama upofu fulani hakuweza kugundu kitu chochote kile, hata zile ishara ambazo zilionyesha kuwa na walakini kwa mwanaume huyo kwake ziligonga mwamba.

Alijitahidi kumuonyesha mapenzi yote ambayo hakuwahi kumuonyesha mwanaume yeyote yule, akili yake ilihama kabisa na muda huo alichanganyikiwa na penzi hilo jipya.

“Nitakupenda mpaka kifo changu,” alisema Shadya huku akimwangalia Alex machoni mwake.

Kila wikiendi wakawa watu wa kutoka kwenda sehemu mbalimbali kwa ajili ya kula raha tu, hawakuwa watu wa kukaa chuoni, mara nyingi nyakati za usiku walichukuana na kwenda kula raha.

Huko ndipo taratibu Shadya akajifunza kunywa pombe. Zilikuwa chungu siku ya kwanza, alizitema lakini kadiri alivyokuwa akiendelea kunywa zikazoeleka mdomoni mwake, sasa akawa na uwezo wa kunywa hata chupa hata tatu bila tatizo lolote lile.

Maisha ya starehe yalimchukua, yule Shadya aliyetoka Zanzibar hakuwa huyu wa sasa, alizoea kuvaa hijabu na mavazi yote ya heshima lakini cha kushangaza naye akaanza kuvaa suruali za kubana na kuyaacha mapaja yake wazi.

Hapakuwa na mtu aliyemshangaa, wanafunzi wa chuo walizoeana, mwaka wa kwanza watu huwa kama washamba fulani hivi, wana adabu, begi kubwa la kubebea madaftari lakini wanapoingia mwaka wa pili, kila kitu hubadilika kabisa, ndivyo ilivyokuwa kwa Shadya.

Alex alimpeleka mbio, alichanganyikiwa. Wakati mwingine alinogewa na pombe, alikunywa mpaka kuzima kabisa, alibebwa na Alex na kuingizwa ndani ya gari na kuondoka naye, alipokuwa akiamka asubuhi, alijishangaa akiwa chumbani.

Wakati hayo yote yakiendelea Rahim alikuwa akiyaona tu, moyo wake ulikuwa na ucungu mno, alimuona dada yake akibadilika lakini hakuwa na cha kufanya.
 
Sehemu ya 57.

Kitu kilichokuwa kikimnyima furaha kabisa ni hali aliyokuwanayo ya kufanya mapenzi ya jinsia moja, aliona kabisa endapo angemwambia kuhusu tabia zile, mabadiliko yake basi naye angemwambia kuhusu mchezo wake mchafu.

Akaogopa kufanya hivyo, moyo wake uliumia ndani kwa ndani, alivumilia, alisononeka lakini hakuthubutu kumwambia hata mara moja.

“Leo kuna muziki babu kubwa klabu! Ungependa twende?” aliuliza Alex.
“Mh! Nitaweza kweli?”
“Kwa nini usiweze! Utaweza tu! Twende mpenzi,” alisema Alex.

Siku iliyokuwa ikifuata alikuwa na mambo mengi ya kufanya kwenye masomo yake, hakutaka kwenda huko lakini kwa kuwa aliombwa na mpenzi wake, hakuwa na jinsi, akakubaliana naye na kwenda huko.
Usiku wa saa tano ndiyo walikuwa wakiingia klabu. Kulikuwa na watu wengi, ila wanachuo ndiyo walikuwa wengi zaidi.

Kila mmoja alikuwa na mpenzi wake, watu walicheza muziki na wanaume wengine walikuwa peke yao, yaani walifika hapo kwa ajili ya kuwinda, mwanamke yeyote ambaye angejipendekeza, basi wangeondoka naye.

“Alex! Sikusomi ujue!” alisema jamaa mmoja, alimvuta Alex pembeni.

“Kwani wasiwasi wako nini?” “Naona kama unataka kunigeuka!”
“Hapana! Naomi yupo wapi?” aliuliza.
“Nishamseti! Leo anakwenda kulala na wewe. Na huyo Shadya inakuwaje sasa?” aliuliza jamaa huyo, aliitwa Christian.

“Huyu demu kama unamtaka ni lazima umnyweshe pombe, zinamchanganyaga sana, halafu zinahamiaga chini. Akilewa, jibebee mzigo wake, kapige mambo halafu jikatae! Yaani asijue kama aliondoka na wewe, asubuhi nitakuja!” alisema Alex.

“Poa! Haina shida.”
Ulikuwa ni mpango kabambe, Alex alimchukulia Shadya kuwa msichana wa kawaida, mapenzi kwake yalipotea kabisa na kitu pekee alichokuwa akikifikiria ni kutembea na wanawake wengine.

Mwanake ambaye alitamani kuwa naye kwa kipindi hicho alikuwa Naomi, msichana mrefu, macho ya goroli aliyekuwa na muonekano kama msichana wa Kinyarwanda.

Alimtaka, alimtumia rafiki yake, Christian kumuonganisha naye, halikuwa tatizo, naye kijana huyo akahitaji kuwa na Shadya, usiku mmoja tu, ampe raha usiku kucha.
 
Sehemu ya 58.

Wakakubaliana wawapeleke wanawake hao klabu na ndivyo ilivyokuwa. Shadya hakujua kilichokuwa kikiendelea ila Naomi alisetiwa kabisa. Msichana huyo akapewa pombe nyingi, akanywa, alijiamini kwa kuwa alikuwa na Alex, alikunywa na aliposhikwa huku na kule, alilegea, yaani ni kama mwili ukakosa mawasiliano.

“Ngoja nikaruke naye,” alisema Christian.
Akamchukua Shadya ambaye alikuwa hajiwezi na kwenda naye katika loji moja iliyokuwa Sinza, akaingia naye ndani, kilichofuata ni kufanya naye mapenzi, alingoneka usiku kucha huku msichana huyo muda wote akijua alikuwa akifanya mapenzi na Alex kumbe siyo.

Wakati hayo yakiendelea, naye Alex alikuwa na Naomi chumba kingine, kwenye loji hiyohiyo. Alifanya naye ngono usiku kucha na muda wa saa moja asubuhi, alikuwa tayari kutoka kwenda katika chumba alichokuwa Shadya na Christian.

Shadya aliamka majira ya saa mbili asubuhi. Kichwa chake kilikuwa na pombe, akakaa kitanda, akajipekua chini, alikuwa ameingiliwa, tena ilionyesha siku hiyo aliingiliwa kwa muda mrefu isivyo kawaida.

Akaanza kukumbuka usiku uliopita alikuwa wapi. Akapata jibu kwamba alikuwa klabu, alipelekwa na Alex, alikunywa mpaka akazidiwa, akahisi waliondoka na kuingia ndani ya hiyo loji.
Wakati akijiuliza hivyo, mara mlango ukafunguliwa na Alex kuingia, uso wake ulikuwa na tabasamu pana, akamsogelea kitandani.

“Unajisikiaje mpenzi?” alimuuliza.
“Nimechoka sana!” alijibu kwa uchovu.
“Unataka tena?”
“Mh! Leo inaelekea ulifanya kwa kunikamia mno!”

“Kwa nini?”
“Hebu paangalie palivyo! Leo umenikomesha!” alisema msichana huyo huku akimuonyesha Alex katikati ya mapaja yake.

“Nilikuwa na hamu! Nataka tena mpenzi,” alisema Alex, akamlaza msichana huyo na kufanya naye mapenzi, kwani kwa jinsi alivyomuona asubuhi hiyo, akamtamani sana.

Huo ndiyo ulikuwa mchezo wake, kila mwanaume ambaye alimtaka Shadya, haraka sana Alex hakutaka kuremba, kazi yake kubwa ilikuwa ni kupewa pesa na yeye ndiye alifanya mchakato wa wanaume hao kufanya mapenzi na msichana huyo kwa staili ileile.
 
Sehemu ya 59.

Shadya alitumika kingono bila kujua, wanaume wakaambiana na hivyo kuonana na Alex ambaye alifanya kama alivyomfanyia Christian na wanaume wengine.

“Ila mtoto mtamu sana! Aisee jamani Wazanzibar watamu!” alisema jamaa mmoja, alikuwa akiwaambia wenzake, alifanya ngono na Shadya zaidi ya mara tatu, hakumchoka, kila alipokuwa akimuona, alimtamani zaidi.
“Na mimi namtaka!” alisema jamaa mmoja, aliitwa Kizota.

“Haina noma. Kazungumze na Alex, andaa alefu thelathini yake, pombe za elfu ishirini za kumnywesha yule malaya, hela ya gesti anakuachia mzigo!” alisema Omary, mwanaume ambaye naye kama kawaida alifanya mapenzi na msichana huyo.

Kizota akaondoka na kumfuata Alex, alimwambia dhamira yake, kwa kuwa alitanguliwa dau, Alex hakuwa na ujanja, alikuwa akiingiza pesa kupitia msichana huyo, hivyo akakubaliana naye na hivyo kwenda klabu ambapo huko Shadya alinyweshwa pombe kali, alipolewa na kutokujitambua, Kizota akamchukua na kwenda naye loji.

Akafanya naye mapenzi mno, usiku mzima, asubuhi ilipofika, haraka sana akachukua kamera, akamuweka mtupu kitandani pale na kuanza kumpiga picha mfululizo.

Alipiga picha chafu, za kila aina, hakujipiga yeye, ila alimpiga msichana huyo, akachukua kiungo chake na kumuwekea mdomoni kuonekana alikuwa akiongea na maiki, akachukua na kumuwekea katikati ya mapaja yake, yaani alipiga picha za kila aina huku sura ya msichana huyo ikionekana waziwazi, alipomaliza, akamuita Alex ambaye alikuja chumbani ili ionekane yeye ndiye aliyempeleka mule na kufanya naye mapenzi kumbe mwanaume mwingine.
.
.
.
Je nini kitaendelea?
 
Naona Shadya kwisha habari yake. Mkuu Shunie endelea ku-du ze nidiful tafadhali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom