Sehemu ya 57.
Kitu kilichokuwa kikimnyima furaha kabisa ni hali aliyokuwanayo ya kufanya mapenzi ya jinsia moja, aliona kabisa endapo angemwambia kuhusu tabia zile, mabadiliko yake basi naye angemwambia kuhusu mchezo wake mchafu.
Akaogopa kufanya hivyo, moyo wake uliumia ndani kwa ndani, alivumilia, alisononeka lakini hakuthubutu kumwambia hata mara moja.
“Leo kuna muziki babu kubwa klabu! Ungependa twende?” aliuliza Alex.
“Mh! Nitaweza kweli?”
“Kwa nini usiweze! Utaweza tu! Twende mpenzi,” alisema Alex.
Siku iliyokuwa ikifuata alikuwa na mambo mengi ya kufanya kwenye masomo yake, hakutaka kwenda huko lakini kwa kuwa aliombwa na mpenzi wake, hakuwa na jinsi, akakubaliana naye na kwenda huko.
Usiku wa saa tano ndiyo walikuwa wakiingia klabu. Kulikuwa na watu wengi, ila wanachuo ndiyo walikuwa wengi zaidi.
Kila mmoja alikuwa na mpenzi wake, watu walicheza muziki na wanaume wengine walikuwa peke yao, yaani walifika hapo kwa ajili ya kuwinda, mwanamke yeyote ambaye angejipendekeza, basi wangeondoka naye.
“Alex! Sikusomi ujue!” alisema jamaa mmoja, alimvuta Alex pembeni.
“Kwani wasiwasi wako nini?” “Naona kama unataka kunigeuka!”
“Hapana! Naomi yupo wapi?” aliuliza.
“Nishamseti! Leo anakwenda kulala na wewe. Na huyo Shadya inakuwaje sasa?” aliuliza jamaa huyo, aliitwa Christian.
“Huyu demu kama unamtaka ni lazima umnyweshe pombe, zinamchanganyaga sana, halafu zinahamiaga chini. Akilewa, jibebee mzigo wake, kapige mambo halafu jikatae! Yaani asijue kama aliondoka na wewe, asubuhi nitakuja!” alisema Alex.
“Poa! Haina shida.”
Ulikuwa ni mpango kabambe, Alex alimchukulia Shadya kuwa msichana wa kawaida, mapenzi kwake yalipotea kabisa na kitu pekee alichokuwa akikifikiria ni kutembea na wanawake wengine.
Mwanake ambaye alitamani kuwa naye kwa kipindi hicho alikuwa Naomi, msichana mrefu, macho ya goroli aliyekuwa na muonekano kama msichana wa Kinyarwanda.
Alimtaka, alimtumia rafiki yake, Christian kumuonganisha naye, halikuwa tatizo, naye kijana huyo akahitaji kuwa na Shadya, usiku mmoja tu, ampe raha usiku kucha.