Simulizi: Penzi ama kaburi?

Simulizi: Penzi ama kaburi?

Wakuu nipo natafakari juu ya kufanya maandamano ya kupinga vitendo vya shunie vya kutuacha hewani kwa muda mrefu. Naombeni uungwaji mkono
 
Wakuu nipo natafakari juu ya kufanya maandamano ya kupinga vitendo vya shunie vya kutuacha hewani kwa muda mrefu. Naombeni uungwaji mkono
Nakuunga mkono ila wasiwepo watu wasiijulikana
 
Sehemu ya 36.

Ilikuwa ni furaha zaidi kwao, kila mmoja alitamani kumuona mwenzake kwa mara nyingine. Gibson hakumfikiria Shadya kwa sababu kwake alikuwa msichana wa kawaida, wa ku-hit and run.

Maandalizi ya kumpokea mpenzi wake yakaanza kufanyika, wakati hayo yote yakiendelea ndipo akakumbuka kulikuwa na msichana aliyeitwa kwa jina la Shadya.

Huyu alikuwa Mpemba, mzuri wa sura lakini hakutaka kabisa kuona akimsababishia kutengana na mwanamke wa ndoto yake, aliyetaka kutengeneza naye maisha.

“Wanawake wa chuo huwa ni wa kupiga na kuacha, tunaishi hivyo kama wanachuo, kwani naye anataka mimi kuwa wake maishani ama?” alijiuliza.

“Na kama aking’ang’ania, kweli nitaamini hawa wasichana wa mwaka wa kwanza magumashi,” alijisemea na kuachia tabasamu pana.

Alikuwa tayari kugombana na msichana yeyote katika dunia hii lakini si Paula, huyo alikuwa kila kitu kwake hivyo kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kulazimisha kupunguza ukaribu baina yake na Shadya.

Hiyo ndiyo ilikuwa hatua ya kwanza ya kumuacha msichana ambaye hukuwa na malengo naye. Kama kwa siku ilikuwa ni lazima mpigiane simu mara tano basi ilikuwa ni lazima ipunguzwe na kufika mpaka mara mbili, kama ulikuwa na haraka mno ya kujibu meseji yake kila inapotumwa, ilikuwa ni lazima upunguze uharaka, meseji moja ichukue hata dakika ishirini kujibiwa.

“Nitaanza na haya mambo mawili kwanza. Nikijidai nipo beneti naye huyu malaya anaweza kuniharibia,” alijisemea, alianza kumuita Shadya malaya kwa sababu tu alimkubalia kumvua nguo na kufanya naye mapenzi, mara mbili, ila kwenye hayo yote, hakuwa msichana wa kumuacha moja kwa moja, yaani pale ambapo angemtaka, angekuwa akimtafuta huku akimuomba msamaha.
*
*

Je, nini kitaendelea?
Du!!!!!!hii story nimeipenda pls tunaomba mwendelezo
 
Hawa waleta hadithi humu wanaboa Sanaa.wanaringa kama mademu bikra..hadithi yenyewe hata maneno 200 haima /episode ..anachukua week au week mbili kuwela..
 
Wakuu nipo natafakari juu ya kufanya maandamano ya kupinga vitendo vya shunie vya kutuacha hewani kwa muda mrefu. Naombeni uungwaji mkono
Mateso nateseka Shunie
Muendelezo Mama la mama.
Du!!!!!!hii story nimeipenda pls tunaomba mwendelezo
Hawa waleta hadithi humu wanaboa Sanaa.wanaringa kama mademu bikra..hadithi yenyewe hata maneno 200 haima /episode ..anachukua week au week mbili kuwela..
Dahh bado tunasubiri mwendelezo
Jamani mimi mwenyewe sipendi arosto toka mwanzo nilisema hii story ina arosto wanaomjua nyemo wanajua alivyo na tabia yake amesema yupo busy na kusambaza vitabu akitulia atapost muendelezo
 
Sehemu ya 37.

Shadya alikuwa na matumaini kwa Gibson kwamba kuna siku angeishi na yeye mpaka pale ambapo kifo kingewatenganisha. Hakujua zaidi kama mwanaume huyo alikuwa na mpenzi wake aliyekuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati.

Alijitahidi mno kumuonyesha mapenzi ya dhati ili tu naye ampende kama alivyofanya lakini haikuwa hivyo. Alijitahidi kumpigia simu na kuzungumza naye.

Gibson alikuwa akipokea, alizungumza naye lakini kila alipohitaji kuonana naye, alikataa kwa kujipa visingizio vingi, kwamba hakuwepo nyumbani, alilala kwa washikaji zake na visingizio vingine.

Hakutaka kumwambia Shadya kwamba hakumpenda, kwa ulimwengu wa sasa, mwanamke huwa hakataliwi kwa maneno kwa sababu mwanaume anajua kuna siku atakuwa na uhitaji naye, hivyo atampigia simu na kuomba kuonana naye.

Hilo ndilo lilivyokuwa kwa Gibson, alikuwa mwanaume wa mahesabu makali, alijua tu kuna siku isiyokuwa na jina angemuhitaji msichana huyo, na kwa sababu aliwahi kulala naye, asingeweza kumpinga hata kidogo.

“Umebadilika sana, kwa nini?” aliuliza Shadya kwenye simu, alikuwa akiongea na Gibson.

“Nimekuwaje mpenzi?” aliuliza mwanaume huyo.
“Unakuwa bize sana!”
“Najua! Naomba unisamehe!”
“Kwa nini hutaki kunijali kama zamani?”
“Kwani zamani nilikuwaje mpenzi?

Nilikuwa nakupigia simu mara kwa mara, meseji na mambo mengine, ninayafanya hayo hata sasa hivi love,” alisema Gibson.
“Ila kasi imepungua! Kwa nini? Unahisi sistahili tena kuwa nawe kwa sababu nimekuruhusu kuuona mwili wangu?” aliuliza msichana huyo.

“Ni maneno makali sana unazungumza!”
“Naomba uniambie!”
“Shadya! Wewe ni msichana mrembo mno!”

“Hujanijibu!”
“Shadya! Unajua....”
“Hilo si jibu! Niambie ni kwa sababu nimekuvulia nguo zangu na kuniona nikiwa mtupu?” aliuliza msichana huyo.

Gibson akanyamaza, alitamani amjibu kwa kumwambia kwamba uchaguzi alishinda na hapakuwa na nafasi ya rais kupiga tena kampeni lakini alishindwa kumwambia hivyo.
 
Sehemu ya 38

Huyu Shadya alitakiwa kuwa mchepuko, si msichana wa kukataliwa hata siku moja. Aliamini kwamba kuna siku jijini Dar es Salaam kungekuwa na mvua kubwa, baridi kali, inawezekana Paula akawa kwenye siku zake, hivyo msaada mkubwa ambao ungebaki ungekuwa kwa huyo Shadya, hivyo alitakiwa kujilazimisha kumpetipeti.

“Nijibu....” alisema Shadya baada ya ukimya wa sekunde kadhaa kutoka kwa Gibson.

“Hiyo si sababu!”
“Sababu ni nini sasa?” “Ubize tu!”
“Huo ubize umeanza siku hizi? Tena baada ya kunivua nguo zangu?” aliuliza.
“Hapana!”

“Kwa nini imekuwa hivyo?”
“Naomba tuonane tuongee!”
“Saa ngapi?”

“Hata sasa hivi njoo hapa Sinza Kumekucha, kwenye mgahawa wa Napoleon!” alisema Gibson na kukaa simu.

Shadya aliulia, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, hapo ndipo alipokumbuka maneno aliyoambiwa kwamba wanaume wa Dar es Salaam walikuwa hatari, hasa wale waliokuwa wakisoma vyuoni.

Alionywa kabla lakini kitu cha ajabu kabisa, maonyo yote yalipitia upande wa kushoto na kwenda upande wa kulia, leo moyo wake ulikuwa ukimuuma.

Aliamini huyo Gibson inawezekana alimpata mwanamke mwingine na ndiyo maana aliamua kutaka kumuacha, hakutaka kuona hilo likitokea, kama mwanamke alitakiwa kupambana mpaka kuhakikisha anashinda vita hivyo na hatimaye kubaki na Gibson wake.
“Nitalipambania hili penzi!” alisema Shadya.

Akajiandaa na baada ya dakika kadhaa, akatoka na kuelekea katika Kituo cha Daladala cha Utawala hapo chuo ambapo akasubiri daladala, ilipofika, akaingia ndani.

Akakaa, daladala haikuondoka kwanza, ilikuwa ikiendelea kuita abiria mahali hapo. Mara akiwa humo, mwanaume mmoja akaingia, alikuwa nadhifu, alivalia suruali ya kitambaa na shati nyeupe, alivalia na tai nyeusi, macho yake yalipotua kwa Shadya tu, msichana huyo akashtuka, jamaa akatoa tabasamu, akaenda kukaa naye kwenye kiti.

“Vipi Shadya!” alimsalimia jamaa huyo, Shadya akashtuka, hakuamini kama alikuwa akijulikana na watu wengine.

“Umenijuaje?” aliuliza kwa mshtuko.
“Mwanachuo mwenzangu! Ninakujua kwa kuwa nasikiaga watu wakikuita!” alijibu jamaa huyo.
“Oh! Sawa!”
“Karibu!”
 
Sehemu ya 39

“Na unasomea nini?”
“Nasomea mambo ya kijamii...kama una matatizo ya kimapenzi, naweza kukusaidia,” alisema jamaa huyo huku akimwangalia Shadya, wakaanza kucheka.
“Ooh!”

“Yeah! Nina kurasa zangu zangu zinaitwa Mapenzi na Mahusiano, unaweza kuingia Facebook, Instagram, zipo huko,” alisema jamaa huyo.

“Sawa!”
Shadya akabaki kimya kwa sekunde kadhaa, alimwangalia jamaa huyo, kwa jinsi alivyoonekana tu, kweli alionekana kufahamu kuhusu mapenzi, mtoa ushauri mkubwa tu.

Kitu alichokuwa akihitaji kipindi hicho ni ushauri wa kimapenzi tu. Akili yake ilivurugika, mapenzi juu ya Gibson yalimuumiza kupita kawaida.

Alihisi kama alikuwa akikosea, inawezekana mwanaume huyo alihitaji mapenzi ya namna hii lakini yeye alipeleka mapenzi ya namna ile.

Wanaume walikuwa tofauti, kulikuwa na wengine waliwapenda wanawake wa hivi wengine wa vile, inawezekana mapenzi aliyokuwa akimpa Ngwali si yale ambayo mtu kama Gibson alitakiwa kupewa na ndiyo maana mwanaume huyo alionekana kubadilika.

“Ila nyie wanaume!” alisema Shadya.
“Tumefanyaje?” aliuliza jamaa huyo.
“Mnafanana!”

“Hahaha! Huwa hatufanani!”
“Kweli tena! Yaani sijui sisi watoto wa kike mnatuchukulia vipi!” alisema Shadya.

“Unamaanisha nini?”
“Hivi mnataka mpewe nini mpaka mjue mtu fulani anawapenda?” aliuliza.
“Inategemea! Wengine ukionyesha kutujali tu, tunajua unatupenda!” alijibu.
“Sasa mwanaume unamfanyia vyote hivyo na bado hakujali! Tatizo huwa ni nini?” aliuliza Shadya.

“Kwanza kwa jina naitwa Alex!” alijitambulisha jamaa huyo.
“Hahaha! Aya Alex niambie!”
“Cha kwanza ni lazima ujue sisi wanaume hatujakamilika, hakuna mwanaume mwenye sifa zote za uanaume bora,” alisema Alex.

“Sawa!”
Inapotokea hivyo, ni lazima wewe mwanamke utumie muda wako kututengeneza sisi. Inawezekana mimi sipendi kutabasamu, muda wote nataka niwe cool, ni lazima wewe uwe mtu wa kutengeneza tabasamu kwangu,” alisema Alex.
“Sawa!”
 
Sehemu ya 40

“Wanawake huwa wanahitaji kupetiwapetiwa ila wanaume wanahitaji hilo kwa asilimia kubwa zaidi ya wanawake, unalijua hilo?” aliuliza Alex.
“Unamaanisha nini?”

“Mwanaume ni shupavu, mtu imara ila jua kuna kipindi moyo wake huvunjikavunjika na hivyo huwa anahitaji kukumbatiwa, kutiwa moyo, mnachokosea nyie wanawake mnataka kutufanya wanaume tujione makomandoo, hapana, huwa tunaumia kama nyie, tuna hisia mno, tunahitaji sana kupetiwapetiwa na nyie,” alisema Alex.
“Nakusikiliza!”
“Ushawahi kumpetipeti mpenzi wako?” aliuliza.

“Hapana! Lakini huwa si tunafanya mapenzi!”
“Shadya, kufanya mapenzi huwa haitoshi. Ngoja nikuulize swali!” alisema.
“Uliza.”

“Siku ina saa ngapi?”
“Ishirini na nne!”
“Huwa mnafanya mapenzi kwa saa ngapi kwa siku?”

“Kama moja ama mbili!”
“Sawa! Tufanye mbili. Baada ya kutoa hayo masaa mawili yanabaki mangapi?”
“Ishirini na mbili!”
“Huwa mnafanya nini kwenye hayo yaliyobaki?”

“Daah!”
“Nisikilize Shadya, upendo si kufanya ngono tu, ngono huwa na asilimia 2.007 kwenye uhusiano wa kimapenzi. Kwenye saa zilizobaki ndipo ambapo unatakiwa kumuonyesha kwamba unamjali, unamthamini na kumsikiliza,” alisema.
“Ooh! Kumbe!”

“Hivi ushawahi kumtoa out mpenzi wako?”
“Hapana!”
“Yeye alishawahi kukutoa?”
“Yaap!”

“Kwa nini wewe hujawahi kumtoa out? Unadhani mwanaume ndiye mwenye wajibu wa kukutoa out? Shadya, mwanaume hupenda kufanyiwa vitu ambavyo hatarajii kufanyiwa kwenye maisha yake.

Hebu mfuate mpenzi wako, mwambie leo nataka nikutoe out, tukale, ufurahi, mnunulie zawadi, tatizo nyie wanawake ndiyo mnataka kufanyiwa kila kitu nyie kwa kuhisi wanaume ndiyo wenye wajibu huo, ndiyo maana wengi hukimbia baada ya kufanya mapenzi na nyie,” alisema Alex huku akimwangalia msichana huyo.

“Aiseeee!”
“Inafika kipindi mwanaume anajiuliza...hivi mbali na ngono, msichana ana kitu gani cha kuofa kwangu? Akiangalia ni kweli hakuna, ni kwa sababu hujawahi kumpelekea zawadi, kumtoa out, kumfanyia mambo mengine ambayo anakufanyia, sasa wengi wakishaona hivyo, wanakimbia zao, mwisho mnaanza kulalamika nyie,” alisema Alex.

“Sasa unataka nifanye nini?”
“Umeuliza swali zuri sana....” alisema Alex, hapohapo akaanza kutoa tabasamu pana usoni mwake.
.
.
.
Itaendelea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom