Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
- Thread starter
- #101
Sehemu ya 45.
Shadya alijikaza mpaka chumbani kwake, akapanda kitandani na kuanza kulia kwa maumivu makali kama mtu aliyefiwa na mtu muhimu katika maisha yake.
Hakuamini kama kweli alichana na Gibson baada ya kumuona mwanaume huyo haeleweki hata kidogo. Kipindi hicho alihitaji sana kubembelezwa, alifikiria mtu sahihi wa kumbembeleza, akahisi kaka yake, Rahim alifaa lakini akagundua hakuwa mtu sahihi.
Mtu wa mwisho kabisa kuja akilini mwake akawa Alex, aliamini kwa jinsi alivyokuwa mshauri mzuri basi angeweza kumliwaza kwa maneno matamu na kumwambia ni kitu gani alitakiwa kufanya.
Akachukua simu yake na kumpigia, ikapokelewa na kuanza kuzungumza naye. Alimwambia ukweli kwamba aliachana na mpenzi wake, ilimuuma mno moyoni mwake, alikuwa na maumivu kupita kawaida.
“Pole sana! Ila mwanaume amekuacha wewe?” aliuliza Alex kwenye simu huku akionekana kushangaa.
“Ndiyo!”
“Kuna wanaume wapumbavu sana! Kumbe mpaka karne hii kuna wanaume wajinga kiasi hiki! Mungu wangu!” alisema Alex.
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Yaani mwanaume amekuacha wewe?”
“Ndiyo!”
“Ni ujinga ulioje? Pole sana. So nikusaidie nini?”
“Nahitaji nikuone! Tuzungumze mengi, unishauri ya kunishauri!”
“Basi haina shida.
Nakuja,” alisema kijana huyo na kukata simu, kidogo sana Shadya akajisikia ahueni, ila bado moyo wake ulikuwa na maumivu makali ya Gibson, yaani mwanaume huyo alimuumiza vilivyo.
.
.
.
Je nini kitaendelea?
Shadya alijikaza mpaka chumbani kwake, akapanda kitandani na kuanza kulia kwa maumivu makali kama mtu aliyefiwa na mtu muhimu katika maisha yake.
Hakuamini kama kweli alichana na Gibson baada ya kumuona mwanaume huyo haeleweki hata kidogo. Kipindi hicho alihitaji sana kubembelezwa, alifikiria mtu sahihi wa kumbembeleza, akahisi kaka yake, Rahim alifaa lakini akagundua hakuwa mtu sahihi.
Mtu wa mwisho kabisa kuja akilini mwake akawa Alex, aliamini kwa jinsi alivyokuwa mshauri mzuri basi angeweza kumliwaza kwa maneno matamu na kumwambia ni kitu gani alitakiwa kufanya.
Akachukua simu yake na kumpigia, ikapokelewa na kuanza kuzungumza naye. Alimwambia ukweli kwamba aliachana na mpenzi wake, ilimuuma mno moyoni mwake, alikuwa na maumivu kupita kawaida.
“Pole sana! Ila mwanaume amekuacha wewe?” aliuliza Alex kwenye simu huku akionekana kushangaa.
“Ndiyo!”
“Kuna wanaume wapumbavu sana! Kumbe mpaka karne hii kuna wanaume wajinga kiasi hiki! Mungu wangu!” alisema Alex.
“Kwa nini unasema hivyo?”
“Yaani mwanaume amekuacha wewe?”
“Ndiyo!”
“Ni ujinga ulioje? Pole sana. So nikusaidie nini?”
“Nahitaji nikuone! Tuzungumze mengi, unishauri ya kunishauri!”
“Basi haina shida.
Nakuja,” alisema kijana huyo na kukata simu, kidogo sana Shadya akajisikia ahueni, ila bado moyo wake ulikuwa na maumivu makali ya Gibson, yaani mwanaume huyo alimuumiza vilivyo.
.
.
.
Je nini kitaendelea?


