Simulizi: Penzi ama kaburi?

Hadithi inafundisha inakufanya uyatathmini maisha. Maana shadya hakuwa malaya . Na mambo haya yapo sana
Asante shunie
 
Shunie asante

Sasa nakuruhusu ufichwe hadi upotee
Asante Baba kuna nyingine hii

 
Sehemu ya 58.

Wakakubaliana wawapeleke wanawake hao klabu na ndivyo ilivyokuwa. Shadya hakujua kilichokuwa kikiendelea ila Naomi alisetiwa kabisa. Msichana huyo akapewa pombe nyingi, akanywa, alijiamini kwa kuwa alikuwa na Alex, alikunywa na aliposhikwa huku na kule, alilegea, yaani ni kama mwili ukakosa mawasiliano.

“Ngoja nikaruke naye,” alisema Christian.
Akamchukua Shadya ambaye alikuwa hajiwezi na kwenda naye katika loji moja iliyokuwa Sinza, akaingia naye ndani, kilichofuata ni kufanya naye mapenzi, alingoneka usiku kucha huku msichana huyo muda wote akijua alikuwa akifanya mapenzi na Alex kumbe siyo.

Wakati hayo yakiendelea, naye Alex alikuwa na Naomi chumba kingine, kwenye loji hiyohiyo. Alifanya naye ngono usiku kucha na muda wa saa moja asubuhi, alikuwa tayari kutoka kwenda katika chumba alichokuwa Shadya na Christian.

Shadya aliamka majira ya saa mbili asubuhi. Kichwa chake kilikuwa na pombe, akakaa kitanda, akajipekua chini, alikuwa ameingiliwa, tena ilionyesha siku hiyo aliingiliwa kwa muda mrefu isivyo kawaida.

Akaanza kukumbuka usiku uliopita alikuwa wapi. Akapata jibu kwamba alikuwa klabu, alipelekwa na Alex, alikunywa mpaka akazidiwa, akahisi waliondoka na kuingia ndani ya hiyo loji.
Wakati akijiuliza hivyo, mara mlango ukafunguliwa na Alex kuingia, uso wake ulikuwa na tabasamu pana, akamsogelea kitandani.

“Unajisikiaje mpenzi?” alimuuliza.
“Nimechoka sana!” alijibu kwa uchovu.
“Unataka tena?”
“Mh! Leo inaelekea ulifanya kwa kunikamia mno!”

“Kwa nini?”
“Hebu paangalie palivyo! Leo umenikomesha!” alisema msichana huyo huku akimuonyesha Alex katikati ya mapaja yake.

“Nilikuwa na hamu! Nataka tena mpenzi,” alisema Alex, akamlaza msichana huyo na kufanya naye mapenzi, kwani kwa jinsi alivyomuona asubuhi hiyo, akamtamani sana.

Huo ndiyo ulikuwa mchezo wake, kila mwanaume ambaye alimtaka Shadya, haraka sana Alex hakutaka kuremba, kazi yake kubwa ilikuwa ni kupewa pesa na yeye ndiye alifanya mchakato wa wanaume hao kufanya mapenzi na msichana huyo kwa staili ileile.
Aiseee......

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sehemu ya 69.

Watu waliwacheka walipoona wakimsomesha mtoto wa kike kwa kuwa wasichana wengi wa Zanzibar hawakuwa wakipelekwa shule, wao waliamua kuwa tofauti nao, walimsomesha kwa nguvu zote lakini mwisho wa siku Shadya akaja kujimaliza akiwa chuoni, tena alibakiza mwaka mmoja kabla ya kuchukua Diploma yake ya kwanza.

“Kwa nini amejiua?” lilikuwa swali walilojiuliza wazazi wake kila siku, Rahim hakuwajibu kwa kipindi hicho mpaka baada ya mwezi mmoja ndipo akaamua kuwaambia ukweli kile alichoambiwa na Shadya.

“Alikuwa ameathirika!” alisema Rahim kwa unyonge kabisa.
“Aliathirika? Kivipi yaani?”
“Aliniambia hivyo! Akaondoka, baada ya saa kadhaa ndipo nikapata taarifa kwamba alijiua,” alijibu Rahim.

Huo ukawa mwisho wa Shadya, watu walihuzunika kwa sababu ya kifo chake. Alex aliendelea kuishi vizuri japokuwa aliathirika, hakujua kwa kuwa aliogopa kupima.

Kupitia sura yake ya kipole, bado aliendelea kutembea na wanawake wengi chuoni hapo, kila msichana mzuri aliyekuwa akimuona, alijitahidi kumfuata kwa upole na kujifanya mshauri na mwisho wa siku kulala naye na kumwambukiza Ukimwi.

Wanaume kama Alex bado wapo, wana nguvu, wanatembea na wanawake mavyuoni na mitaani. Hawajali kuhusu afya zao, wanaendelea kusambaza virusi vya Ukimwi kwa kila mwanamke watakayelala naye.

Wasichana kama Shadya nao wapo, wanamaliza shule na kujiunga na masomo ya chuo. Wanapofika mwaka wa kwanza, hawajui lolote lile, kila mwanaume anayewafuata na kuwasaidia anaonekana mwema mbele ya macho yao.

Hawafikirii kuhusu ndoto zao, ni kwa jinsi gani wazazi wao wamejinyima kwa ajili yao, wapate elimu bora na kuwaondoka katika giza la umasikini, wanapofika chuoni, maisha ya starehe yanawavamia na kuingia mitegoni na mwisho wa siku kuharibu ndoto zao.

Kumbuka kwamba UKIMWI UPO MAVYUONI, MITAANI NA MAOFISINI. Ikibidi acha ngono, ukishindwa, tumia kondomu.

Ujumbe huu uwafikie vijana wote ambao wanapambana kwa ajili ya maisha yao ya badaye.

MWISHO
-
-
-
NYEMO CHILONGANI.

Inahuzinisha na kusikitisha sana...

Chapter closed...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom