Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,081
- 464,047
- Thread starter
- #161
SEHEMU YA 45
Mzee Gwamaka aliposikia hilo, akazidi kuumia, hakutaka kabisa kumuona mwanaye akiingia kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa kuwa aliamini kwamba kuna siku angeumia sana, alitamani binti huyo aendelee kukaa peke yake lakini baada ya Dickson kutokea na kumuonyeshea uaminifu mkubwa, akamruhusu kuwa karibu na binti yake.
Mvulana huyohuyo aliyemwamini ndiye aliyekuja kumuumiza binti yake na kumliza kitandani hapo. Hakuamini, alijilaumu na wakati mwingine kujiona akiwa amefanya kosa kubwa mno.
Hakutaka kubaki na maumivu, alipotoka hospitalini hapo breki ya kwanza ilikuwa ni nyumbani kwa wazazi wa Dickson, alipofika, akaanza kuwaambia kilichokuwa kimetokea.
“Haiwezekani! Dickson hawezi kumuacha Nandy,” alisema mama yake huku akimwangalia mzee Gwamaka.
“Amemuacha, na hata alipopoteza fahamu, hakutaka kujali, akaondoka zake. Kwa nini kijana wenu amefanya hivi?” aliuliza mzee Gwamaka huku akionekana kuwa na hasira mno.
Wazazi wa Dickson hawakutana kubaki nyumbani walichokuwa ni kwenda mpaka hospitalini kwenda kujua ukweli kama kile alichokizungumza mzee Gwamaka kilikuwa kweli au la.
Walipofika huko na kuonana na Nandy, akawahadithia kilichokuwa kimetokea, hawakuamini, walimfahamu Dickson, alikuwa na mapenzi ya dhati kwa Nandy kiasi kwamba kwao lilionekana kuwa jambo lisilowezekana hata kidogo kwa mtoto wao kumuacha Nandy.
Wazazi wake hawakutaka kusubiri, walichokifanya ni kumpigia simu kijana wao kwa lengo la kutaka kumsikia akizungumza hayo kwa mdomo wake. Walipompigia simu, aliwaambia kama alivyomwambia Nandy kwamba hakutaka kuwa naye kwani alipata msichana mwingine ambaye alipanga kumuoa.
“Una akili Dickson?” aliuliza baba yake kwa hasira swali ambalo hakupanga kuliuliza hata siku moja.
“Moyo baba! Siwezi kumuoa msichana ambaye moyo wangu haupo kwake, naomba mniache, kama ambavyo hakukuwa na mtu aliyekuchagulia mama, na mimi naomba msinichagulie,” alisema Dickson na kukata simu.
Walichanganyikiwa, kile walichoambiwa na Dickson hakikuwaingia akilini kabisa. Hawakutaka kubaki hospitalini hapo, wakaondoka kurudi nyumbani kwao.
Mzee Gwamaka aliposikia hilo, akazidi kuumia, hakutaka kabisa kumuona mwanaye akiingia kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa kuwa aliamini kwamba kuna siku angeumia sana, alitamani binti huyo aendelee kukaa peke yake lakini baada ya Dickson kutokea na kumuonyeshea uaminifu mkubwa, akamruhusu kuwa karibu na binti yake.
Mvulana huyohuyo aliyemwamini ndiye aliyekuja kumuumiza binti yake na kumliza kitandani hapo. Hakuamini, alijilaumu na wakati mwingine kujiona akiwa amefanya kosa kubwa mno.
Hakutaka kubaki na maumivu, alipotoka hospitalini hapo breki ya kwanza ilikuwa ni nyumbani kwa wazazi wa Dickson, alipofika, akaanza kuwaambia kilichokuwa kimetokea.
“Haiwezekani! Dickson hawezi kumuacha Nandy,” alisema mama yake huku akimwangalia mzee Gwamaka.
“Amemuacha, na hata alipopoteza fahamu, hakutaka kujali, akaondoka zake. Kwa nini kijana wenu amefanya hivi?” aliuliza mzee Gwamaka huku akionekana kuwa na hasira mno.
Wazazi wa Dickson hawakutana kubaki nyumbani walichokuwa ni kwenda mpaka hospitalini kwenda kujua ukweli kama kile alichokizungumza mzee Gwamaka kilikuwa kweli au la.
Walipofika huko na kuonana na Nandy, akawahadithia kilichokuwa kimetokea, hawakuamini, walimfahamu Dickson, alikuwa na mapenzi ya dhati kwa Nandy kiasi kwamba kwao lilionekana kuwa jambo lisilowezekana hata kidogo kwa mtoto wao kumuacha Nandy.
Wazazi wake hawakutaka kusubiri, walichokifanya ni kumpigia simu kijana wao kwa lengo la kutaka kumsikia akizungumza hayo kwa mdomo wake. Walipompigia simu, aliwaambia kama alivyomwambia Nandy kwamba hakutaka kuwa naye kwani alipata msichana mwingine ambaye alipanga kumuoa.
“Una akili Dickson?” aliuliza baba yake kwa hasira swali ambalo hakupanga kuliuliza hata siku moja.
“Moyo baba! Siwezi kumuoa msichana ambaye moyo wangu haupo kwake, naomba mniache, kama ambavyo hakukuwa na mtu aliyekuchagulia mama, na mimi naomba msinichagulie,” alisema Dickson na kukata simu.
Walichanganyikiwa, kile walichoambiwa na Dickson hakikuwaingia akilini kabisa. Hawakutaka kubaki hospitalini hapo, wakaondoka kurudi nyumbani kwao.
