SIMULIZI: Mkufu wa Malkia wa Goshen

SIMULIZI: Mkufu wa Malkia wa Goshen

Haya ss mambo n motooo, Venin kenda chukuliwa aletwe kwa hasm kaka ake Venet, Weeeee Shunie weee ww ni sheeda
 
Wanaoenda kwa venin wanaweza ishia njiani jaman vile vibibi ndo basi tena I cant wait jahit na venet wakutane huo ugonvi wake
 
Asante sana shunie
Barikiwa mke mweee
Pamoja sana [emoji91][emoji91][emoji91]
Ahsante sana malikia shuniee
Ahsante kwa madini matamu shunie""""[emoji847][emoji847][emoji847][emoji847]
nashukuru kwa tulichopata shunie
Haya ss mambo n motooo, Venin kenda chukuliwa aletwe kwa hasm kaka ake Venet, Weeeee Shunie weee ww ni sheeda
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]
 
*MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN II-- 41*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Hali ya tahadhari ikatangazwa himaya nzima, watu wakihusiwa kukaa ndani mpaka pale taarifa itakapotolewa.

Muda ukasonga. Bado hakukuwa na kitu!

Kulikuwa kimya mno kiasi cha kudhani aidha umekuwa kiziwi.

ENDELEA

Baada ya muda kusonga zaidi, ndipo wanajeshi baadhi wakaleta taarifa kasrini ya kwamba Rhoda ameonekana tena kule gerezani! Alikuwa amesimama pamoja na maiti akipaza sauti kuteta lugha isiyojulikana.

Basi haraka mfalme akaagiza majemedari wamkamate mwanamke huyo na wahakikishe wanamtia nguvuni asizae shaka.

Lakini angalizo wasimuue kwani anamhitaji akiwa hai.

Wanajeshi, kwa woga wakabeba agizo hilo na kwenda eneo la tukio. Walifika na kuwakuta wenzao huko ambao hawakuwa wanajua cha kufanya zaidi ya kumtazama Rhoda akiendelea na mambo yake yasiyoeleweka.

Apiga kelele akitazama anga. Aomba na kunung'unika katikati ya maiti.

Wakafikishiwa agizo la mfalme kuwa wamkamate na si kumtazama. Kwani kuna yeyote anayejua anachokifanya?

Haraka, wakaona ni busara kutumia mshale wenye kileo na dawa. Huku Rhoda akiendelea na ibada, akaja shtuka ncha ya mshale imepenya mguuni mwake. Akalalama kwa maumivu!

Akauchomoa mshale huo na kutazama ulipotokea kwa hasira kali kiasi kwamba aliyerusha akaona kifo chaja! Mara akageuka kuwa kundi la popo wengi, lakini hakufika mbali, popo hao wakadondoka na kurejea katika mwili wa Rhoda!

Alikuwa amechoka, macho yanaona kizunguzungu, kichwa chamzunguka. Alijikongoja kumfuata adui yake aliyemrushia mshale lakini safari haikukamilika, akapoteza fahamu!

Wanajeshi wakafurahi kwa ushindi. Haraka wakamkusanya na kwenda kumtia kwenye gereza lake la pekee la shimo. Humo wakamfunika na wavu mkubwa na mzito wa chuma. Wakamiminia dawa wavu huo, na kisha wakaenda kumpasha habari mfalme.

Himaya nzima ikajawa na furaha. Sasa walikuwa salama! Lakini salama hii haikuwa salmini. Bado Venet alikuwa hai, si mfu. Na wala ule wavu mzito wa chuma hauwezi kumzuia abadani, lakini sema tu ni mpaka pale mwezi utakapochomoza na kuonekana mzima angani.

Venet alishindwa kutengeneza jeshi kwa kutumia miili ya wafungwa aliowaua kwasababu hakukuwa na mwezi mzima angani!

Alishindwa kuiweka Goshen mkononi kwasababu hakukuwa na mwezi mzima angani!

Laiti mwezi huo ungelikuwa umelitawala anga, lilikuwa ni jambo la kufumba na kufumbua macho tu, Goshen yote ingeshanyauka! Hakuna ambaye angemzuia Venet na jeshi lake.

Abadani!

**

"Sasa tunaweza tukalala," mfalme alimwambia Tattiana akitabasamu.

"Pole sana, mfalme," Tattiana akamsabahi. "Haikuwa kazi nyepesi kabisa. Haki kazi hii ni kubwa na ngumu tofauti na kila aliyepo huko nje anavyoiangazia."

Mfalme akamshukuru Tattiana kwa msaada wake na kumtia nguvu. Asingeliweza mwenyewe kabisa. Akamzawadia Tattiana kumbatio la nguvu alafu akaenda zake kuoga na kurejea kulala.

Hakuchukua muda mrefu, usingizi ukampitia. Lakini Tattiana akibakia macho kwa muda mrefu. Alikuwa anawaza mambo kadhaa, kuhusu Rhoda na kuhusu nyumbani kwao.

Akapanga kesho aende nyumbani kusalimia. Kuna mambo fulani inabidi akayafikishe huko.

Sasa alipofikia hitimisho lake hilo akajaribu kulala. Akajaribu kweli lakini akashindwa. Alikuwa anasikia baridi mno. Akanyanyuka na kwenda kufunga madirisha kisha akaenda kulala tena.

Mwishowe akaona kuna haja ya kubadili kitanda. Hakuweza kulala na mfalme. Mfalme alikuwa wa baridi, na hata sasa kitanda chake kizima.

Akatoka ndani aekelekee kwenye kile chumba chake alichokabidhiwa hapo awali. Akiwa njiani kuelekea huko akahisi kuna mtu ama watu mahali wakiteta. Akashtuka.

Alitulia na kusikiliza kidogo, akasikia kwa mbali watu wakinong'ona. Sauti yatokea upande wake wa kushoto, ambao kuna njia ya kutoka nje ukasimama kwenye kibaraza ghorofani.

Taratibu akasogea huko lakini moyo wamdunda haswa. Akashika kitasa cha mlango na kuufungua. Akamkuta Lucy, kijakazi wa kasri, akiwa amesimama mwenyewe!

"Lucy!" Akaita. "Wafanya nini huku muda huu?"

Lucy akatabasamu. "Nimepumzika tu, kipenzi cha mfalme. Sina usingizi."

Tattiana akatazama kushoto na kulia.

"Ulikuwa unaongea na nani?" Akauliza. Lucy naye akatazama kushoto na kulia kisha akapandisha mabega.

"Nilikuwa mwenyewe, hamna mtu! Hamna ninayeongea naye!"

Tattiana akamsogelea na kushika vyuma. Wote wakawa wanatazama himaya ya Goshen kwa chini.

Kulikuwa kimya kidogo upepo ukipuliza.

"Mbona upo hapa?" Lucy akamuuliza. "Umemuacha mumeo na nani?"

Tattiana akatabasamu. Naye akasema hana usingizi ndo maana alikuwa anatembea tembea. Lucy akamuuliza huwa anafanya hivyo kila siku?

"Hapana, vipi na wewe huwa unakaa hapa kila siku?"

"Hapana!"

Tattiana akaaga akaenda zake. Asingeweza kuendelea kukaa pale kwani alikuwa anasikia baridi. Akiondoka, Lucy akamtazama mwanamke huyo mpaka anaishia.

Jicho lake halikuwa la shwari. Alifunga mlango na kuendelea kukaa huko nje, na muda si mrefu sauti za kunong'ona zikarejea tena.

**

Ngo! Ngo! Ngo! Mlango wa Waheed ulilia. Mwanaume huyo akanyanyuka kitandani na kufungua dirisha kuangaza. Ilikuwa ni asubuhi iliyoanza kuonja mwanga wa jua.

Akapaza sauti yake:

"Nakuja!"

Baada ya muda mfupi akatoka ndani ya chumba chake na kwenda kukutana na Malkia na wenziwe waliokuwa wameketi sebuleni.

"Nyie huwa hamlali?" Akasema kipiga mihayo.

"Ulituambia tudamke mapema kwa ajili ya safari," Zura akakumbusha.

"Ooh! Mmejiandaa tayari, sio?"

Halikuwa swali hili hivyo hakuna aliyemjibu, basi akawaambia wanyanyuke na mara moja waendee farasi wao waondoke.

"Hujiandai?" Fluffy akamuuliza akistaajabu. Waheed akajitazama,

"Kwani kuna shida?"

Hata hakunawa uso, wakaenda na safari yao iliyodumu njiani kwa masaa. Jua likiwa limechachamaa, yani mchana sasa, ndipo wakawasili mbele ya nyumba ya mzee huyo wanayemhitaji.

Ilikuwa ni nyumba ndogo dhaifu. Mlango wake ulikuwa mbovu na madirisha madogo yaliyofunikwa pia. Usingeweza kudhani hapo anaishi mzee anayetunza siri ya kofia ya Pharaoh wa kale.

Kofia yenye mamlaka ndani yake, aghalabu na aghali mno.

Kulikuwa kimya eneo hilo. Wakabisha hodi na mara mlango ukafunguliwa na mzee mmoja aliyevalia joho la rangi ya kijivu. Akawakarimu.

"Samahani, tumemkuta mzee Desmo?" Akauliza Waheed. Mzee yule akawasihi waingie ndani, wakaketi chini na kuwaambia mzee huyo amefariki hivi jana na tayari wameshamzika.

"Asubuhi ya mapema tulimkuta akiwa amelala kitandani anavuja damu. Koo lake lilikuwa limechanwa linamimina damu nyingi hata kuongea hakuweza mpaka anakufa. Haijajulikana nani kamuua mpaka sasa, na sijui sababu gani ya kumuua mtu kama yule asiyekuwa na mali wala familia."

Habari hizo zikawadhoofisha wakina Malkia. Sasa kama mwanaume huyo waliyeambiwa wamtafute ameuawa, watafanikiwaje?

"Vipi hakumsikia mtu nyakati hizo za usiku?" Malkia akauliza. Mzee yule akatikisa kichwa,

"Mimi ni jirani yake lakini sikusikia hata kidogo. Hata mlango wake haukuwa umevunjwa ulifungwa vile vile kwa ndani. Hatujui muuaji huyu alifanyaje hili tukio, lakini ni wazi hakuwa mtu wa kawaida!"

Baada ya maelezo hayo, wakatoka ndani na kuwaendea farasi wao.

"Sasa tunafanyaje?" Akauliza Seth aliyekuwa mgongoni mwa Alk.

"Hata sijui," akajibu Malkia. Wakawafikia farasi wao na kuwakwea. Safari ya kurudi kwa Waheed ikaanza.

"Je mimo nikiwaambia namna mtasadiki?" Akauliza Waheed. Wote wakamtazama.

"Mimi ninajua njia kama ajuavyo Desmo. Najua wapi kofia hiyo ilipo ndani ya piramidi. Njia gani tupitie kuingia na njia gani tutatumia kutokea."

"Una uhakika?" Akauliza Seth.

"Asilimia zote!" Akajibu Waheed kwa kujiamini.

"Sasa mbona haukutueleza hayo mapema kwamba unayajua?" Fluffy akauliza.

Waheed akatabasamu.

"Niliona niwaache mpaka mhakiki kwa mtu mliyekua mnamwamini ninyi."

"Kwahiyi utatupeleka huko?" Akauliza Seth.

"Usijali, kama mtahutaji nitawapeleka, kwanini nisifanye hivyo?"

Kwa wakati huo wakiongea, Malkia alikuwa anatazana mikono ya Waheed. Mwanaume huyu alikuwa haogi wala hanawi. Bado mabaki yale ya damu aliyomwona nayo jana yalikuwapo.

Akamkagua na kucha zake, akaona zilivyo nyeusi lakini pia zikiwa na mabaki ya damu. Akapata maswali kichwani.

Ni Waheed ndiye aliyemuua Desmo. Akawaza.

Desmo aliuawa usiku.

Siku ile asubuhi ambayo walipanga kwenda kumtembelea mwanaume huyo, Waheed alitoweka na kurejea asubuhi ya mapema akiwa na mabaki ya damu.

Alitokea wapi?

Akakumbua mbali zaidi, ilikuwa ni usiku wa jama yake kabla Waheed kutoweka, ndiyo walikuwa wamepanga kwenda kwa Desmo. Je Waheed alimmaliza Desmo ili apate fursa ya kwenda nao ndani ya Piramidi?

"Waheed," Malkia akaita. "Kwanini unatusaidia? Ni nini unataka kwetu kama fadhila?"

Waheed akashangazwa na swali hilo la ghafla.

"Nawasaidia kwasababu mnahitaji msaada. Au nimekosea?" Akageuza mambo.

Malkia akamkazia macho na kumuuliza:

"Hauna mpango wowote kwenye hili? Una uhakika?"

Waheed akanyamaza kwanza akitazamana na Malkia. Mara maongezi yao yakakatwa na sauti ya Zura aliyekuwa anashangaa kwa mbali kuona kimbunga cha vumbi.

Hawakuongea tena mpaka wanawasili nyumbani. Baadae wakapata chakula na kutulia. Waheed akaanza kuwapatia maelezo juu ya kile watakachoenda kufanya kesho yake.

"Kwanza inabidi tufahamu mpaka sasa hakuna yeyote aliyewahi kufanikiwa kutoka ndani ya piramidi hilo akiwa hai. Kila anayeingia anaishia humo humo na kujiunga kwenye jeshi la wafu."

Kihistoria,

"Piramidi hilo lililaaniwa na linalindwa na roho ya Pharao mdhalimu kuwahi kutokea katika historia ya Misri. Pharao huyo akiwa na jeshi lake walikuwa ni tishio mno ndani na nje ya Misri kwa ubabe, ukatili na unyang'anyi!

Lakini habari yao ikaja kukomeshwa na mungu wa vita na bahari. Wakatupiwa ndani ya piramidi yeye na jeshi lake wasitoke humo kamwe. Wakaishi mpaka kufa.

Lakini kimwili tu, kiroho wapo hai. Mfalme huyo bado anaendelea kutawala humo ndani ya piramidi na jeshi lake likimlinda.

Kofia yake ya madaraka ipo kichwani mwa fuvu lake la kichwa, na japo kalala bado anailinda kama vile ajuaye kuwa kila mtu anaitaka kofia hiyo. Na punde atakapoipata, basi atakuwa ana madaraka makubwa sana, hata lile jeshi la wafu litamtumikia!"

Habari hizo zikawasisimua Malkia na wenzake. Ila Zura akawa na swali.

"Kwanini umeshindwa kuchukua kofia hiyo na nguvu zako zote?" Aliuliza. Waheed akatabasamu.

"Si rahisi kama udhanivyo," Akamjibu. "Ndani ya piramidi lile hakuna mlozi anayeweza kufanya ulozi wake. Kila mtu ni wa kawaida punde tu aingiapo ndani."

***
 
*MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN II -- 42*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Habari hizo zikawasisimua Malkia na wenzake. Ila Zura akawa na swali.

"Kwanini umeshindwa kuchukua kofia hiyo na nguvu zako zote?" Aliuliza. Waheed akatabasamu.

"Si rahisi kama udhanivyo," Akamjibu. "Ndani ya piramidi lile hakuna mlozi anayeweza kufanya ulozi wake. Kila mtu ni wa kawaida punde tu aingiapo ndani."

ENDELEA

"Kwahiyo hata pharao mwenyewe aliyepo madarakani hajataka kwenda kuichukua kofia hiyo?" Akauliza Seth.

"Ndio," akajibu Waheed. "Hakuna anayethubutu kwenda huko, achia mbali wakisema pharaoh yule alikuwa amelaaniwa."

Akameza mate kwanza.

"Kwahiyo ile kofia ambayo anayo Pharao wa sasa si ile ya zamani japo naye amerithi. Ile imetengenezwa na masonara wa kawaida tu wakati ile ya Pharaoh aliyetupiwa ndani ya Piramid yake ikiwa imetengenezwa na miungu!" Waheed aliendelea kudadavua.

"Kwahiyo kama tukiipata kofia hiyo, utawala wa Misri utatupokonya?" Akauliza Malkia.

"Hapana, sidhani kama watafanya hivyo," akajibu Waheed. "Sema wanaweza kuwaomba ama kuingia makubaliano kwa kuwapatia kitu chenye thamani zaidi kwa mabadilishano."

"Kama kipi chenye thamani kuliko kofia hiyo?" Malkia akaendelea kuuliza. Waheed akapandisha mabega.

"Sijajua. Ila hawatakosa cha kuwavutia ili muwakabidhi kofia hiyo."

"Na kama tukikataa kuwapa?" Malkia akauliza tena.

Waheed akanyamaza kidogo akifikiria. Hakuwa na majibu kamili. Akakatisha maongezi kwa kuwasihi wapumzike kwani wametoka safari ndefu. Hivyo akamwacha Malkia na kiu ya taarifa zaidi.

Akaenda zake ndani ya chumba kujilaza. Akawaza mambo kadhaa aliyoyafanya kwa siku hiyo, lakini akawaza na lile alilolifanya usiku wa kuamkia siku hiyo.

Ulikuwa ni usiku wa aina yake kwake, usiku wa kipekee. Ndani ya usiku huo alitoka kwenye makazi yake na kisha kwenda kwa Desmo akitumia nguvu za kilozi kumtambua!

Akakumbuka namna alivyomuona mzee huyo akitoka kuvua samaki, mkononi amebebelea kikapu. Mzee huyo akazama ndani na kisha akamfuata humo na kumkaba, kumuua!

Akabeba kumbukumbu yake yote kuhusu Piramidi alafu akayeya.

Basi akajikuta anatabasamu. Alijivunia alichokitenda. Lilikuwa jambo muhimu. Sasa anamiliki kumbukumbu hiyo muhimu ambayo itamsaidia kupata kofia ya Pharao.

Kwa kuwatumia wakina Malkia, ambao aliamini wana dhamira na uwezo huo, kivipi ataikosa kofia? Hakuona namna kabisa.

Basi akatabasamu tena.

**

Usiku ni huu.

Baada ya usiku wa jana ambao ulikuwa na tafrani ndani yake, watu wakitaarifiwa wakae ndani tu, sasa usiku huu uliofuatia ulikuwa ni 'dhahabu'. Ulikuwa ni muda mwanana wa kwenda kutekeleza yale aliyoyaagiza baba.

Kila kitu kilishawekwa katika mifuko na safari ilishafungwa mpaka maeneo ya tukio. Eneo hili halikuwa mbali sana na vilabu vya pombe. Tuseme kama nusu kilomita hivi.

Mazingira yalikuwa tulivu. Haswa yalihamasisha tendo. Kwa kunong'oneza, wakiwa ubavuni mwa nyumba, Oragon akamuuliza Ottoman,

"Si ndiyo hapa?"

Ottoman akajibu kwa kutikisa kichwa. Akaongezea:

"Na kile ndo chumba chake!" Akaonyeshea dirisha.

Basi wakasonga taratibu mpaka hapo dirishani. Kulikuwa kumefungwa. Taratibu wakakazana kupafungua wapate kupenyeza dawa.

Lakini kwa mbali,

"Nani wale?" Akauliza mwanaume mmoja akimwonyeshea mwenzake kwa kidole kule walipo wakina Ottoman. Wanaume hawa wawili, walikuwa ni walevi wametokea kilabuni, sasa wanaelekea majumbani.

Ni usiku mkubwa.

"Watakuwa wezi!" Akajibu huyu mlevi wa pili. Basi wakiwa wanayumba kama jahazi baharini wakaanza kusonga kusogelea eneo la tukio, walipokaribia wakapaza sauti kuita wezi! Ottoman na Oragon wakakurupuka kwa woga.

Haraka wakakimbia kwa kasi hata walevi wale walipowakimbiza hawakufua dafu. Wakawadandia farasi zao na kutokomea haraka kuokoa roho zao.

Walevi wakarudi eneo la tukio. Wakawakuta Nebukadeza na mwanae wa kiume wakiwa nje, mikononi wamebebelea silaha.

Wakawapasha habari.

Wakaelekea kule dirishani, huko wakakuta kamfuko kadogo chini. Wakaokota na kukatazama. Nebukadeza akagundua ni sumu.

"Hawakuwa wezi, walikuwa wauaji!"

"Wanataka kutuulia nini?" Akashangaa mwanawe. Nebukadeza akawatazama walevi wale wawili na kuwauliza:

"Mliwaona watu hao?"

"Kwa mbali!" Mlevi mmoja akajibu.

"Mie nilimwona!" Mwingine akadakia akinyoosha kidole kana kwamba mwanafunzi yu darasani. "Ni watoto wa mzee Harid!"

Mwenzake akamtazama.

"Una uhakika?" Akamuuliza.

"Kwanini nisiwe nao? Unadhani nimelewa!" Akafoka mwenzake.

"Unamjua mzee yule ni mmojawapo wa wazee wa baraza?" Nebukadeza akawaambia. "Endapo mtakuwa mmesema uongo basi itawagharimu."

Mlevi aliyesema hayo akaapia akichinja shingo yake kwa kidole, nimemwona kwa macho yangu meupe hivi ... hivi!"

***

Kesho yake Nebukadeza akanyanyuka kwenda kutoa taarifa juu ya jaribio lake la kuuawa. Akamfikishia shauri hilo kamanda wa ukanda wao, na kama haitoshi kwa kuhofia ushawishi wa mzee Haridi unaweza ukaingilia kesi hiyo, akaomba akaonane na mfalme.

Kwakuwa alishawahi kufika hapo, hata walinzi hawakuwa na tabu naye, wakamhusia angoje mfalme ahabarishwe. Punde akaruhusiwa. Akaonana na mfalme aliyekuwa ameketi kwenye bustani yake pamoja na Tattiana.

Akamweleza mfalme yale yaliyotokea usiku wa jana. Habari hiyo ikamshtua mfalme.

"Una uhakika lakini?" Akauliza.

"Ni kwa mujibu wa maelezo ya mashahidi," Nebukadeza akajibu.

"Lakini kwanini wajaribu kukuua?" Mfalme akauliza akitafakari. Lakini kwa muda huo Tattiana akaanza kupata picha kamili kichwani.

Baba yake Oragon na Ottoman, mzee Harid, anafanya biashara ya kuuza Cedar! Akahisi moyo umemlipuka kama bomu kwani alifahamu wazi mzee huyo atakuwa anashirikiana na baba yake, bwana Melkizedek.

Sasa watoto wa mzee huyo wanataka kumuua Nebukadeza kwakuwa alikuwa anatoa siri za biashara hiyo.

"Hiyo sumu ipo wapi?"akauliza mfalme. Nebukadeza akamwambia amemkabidhi kamanda. Haraka mfalme akaagiza sumu hiyo iletwe pale kasrini na mtaalamu pia afike hapo mara moja.

Hazikupita dakika kumi vyote alivyoagiza vikawa vimefika.

Mtaalamu akatazama na kuichambua sumu ile, kisha akampa mrejesho mfalme.

"Ndiyo ile, mfalme. Iliyomuua yule mtumishi wako!"

Mfalme akakasirika sana. Tattiana naye akajawa na jazba. Kama ndiyo ilimuua yule mtumishi wa mfalme, basi ndiyo iliyommaliza na Roboth pia!

Ina maana kifo cha Roboth kilifanywa na wakina Oragon na Ottoman! Akapasuka moyo. Kwanini wafanye hivyo? Roboth aliwakosea nini kumuua?

Akili yake nyepesi ikamwambia huo ulikuwa ni mkakati wa Mzee Harid kuhakikisha anaolewa na mfalme ili apate kudumisha uhusiano baina yake na familia yake kwa mirija ya fadhila!

Yani mdhalimu yule anadiriki kukatisha maisha ya mtu kwa lengo la fadhila!

Akajikuta anajawa na chuki. Kidonda chake kilichoanza kupoa kikaanza kuchipuka upya.

Mfalme akaagiza watumishi wake wakawamate na kuwaleta Oragon na Ottoman mbele yake haraka iwezekanavyo. Wana kesi mbili za mauaji wanatakiwa kuzitolea majibu.

***

"Tazama huko!" Akaropoka mwanajeshi mmoja yeye akienda upande wa kulia wa nyumba. Walikuwa watano kwa idadi na wote wakaizingira nyumba ya mzee Harid na kuipekua.

"Hawapo!" Akatoa ripoti mwanajeshi mmoja kumwambia mkuu wao. "Tumetazama kila sehemu, watakuwa wametoroka!"

Lakini punde,

"Mkuu, tazama hichi!" Alipayuka mwanajeshi mmoja akimsogelea mkuu wake. Mkononi alikuwa amebebelea majani.

Mkuu wao akayatazama na kisha akayanusa.

"Cedar! ... ni Cedar!"

Akaagiza msako wa kutafuta matunda hayo kila sehemu, basi msako ukarudiwa kwa mara ya pili. Kila kitu kikafunuliwa, kila sehemu pakawekwa wazi kupekuliwa.

Jikoni, wakapata baadhi ya matunda hayo ambayo waliyakusanya wapate kuyabeba kama kielelezo.

"Toa taarifa mipaka yote ifungwe, hamna mtu yoyote kutoka nje ya himaya," akaagiza mkuu wa kikosi. Basi taarifa ikatolewa kwa mlio wa pembe ambayo ilivuma ndani ya himaya nzima na hata maeneo ya karibu.

Mipaka ikafungwa.

**

"Mama!" Tattiana alipaza sauti punde alipoingia ndani ya eneo lao la nyumbani. Alikuwa anakimbia farasi kamwacha getini kwa walinzi.

"Mama!" Akaendelea kuita mpaka alipoingia ndani. Hakumkuta mtu sebuleni, na hata nyumba haikuonekana na dalili ya mtu yoyote!

Akagonga milango na kupita kila chumba. Hamna mtu. Sasa walikuwa wameenda wapi?

Akaketi sebuleni tumbo likimsokota. Jasho likimtoka.

***
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom