Angalau huko fasihi.com panawalipa hawa watunzi.Wasomaji wanaachiwa kusoma free mpaka chapter fulani ila utamu ukikolea tu inajilock inakutaka ununue coins ili uendelee kusoma...Ukilipia inafunguka unaendelea kusoma.Coin moja unaweza soma chapter moja.Coin moja ni sh.100.Hivyo kama ulikuwa unafuatilia stori yenye chapter 78 utaachiwa labda mpaka ya 8.Kuanzia ya 9 hadi ya mwishoni kila chapter utasoma kwa sh.100.So kumaliza itahitaji kulipa 7000.
Kwahiyo mtunzi wa kazi naye analipwa asilimia fulani na wenye hiyo platform.Jamiiforums wangeweza pia kufanya hivi ili hawa ndugu zetu wafaidike na kazi zao hapa Jamiiforums, huku JF nayo ikifaidika kwa kuwa platform.Uongozi wa Jamiiforums unaweza ukaliona hilo hitaji la wasomaji wa hadithi kuzisomea hapa ikaweka utaratibu utakaohakikisha pande zote tatu JF,msanii na msomaji zinafaidika.Mkuu
Maxence Melo liangaliwe hili
Mfano stories za Elton Tonny ambazo ndizo nzuri kupita za wote humu JF (kwa mtazamo wangu) huwa chapter moja ni ndefu sana kwa hiyo kuilipia sh.100 hiyo chapter ni sawa kabisa.Changamoto ni kwa wale watunzi ambao chapter yao moja ni fupi sana so kumaliza kitabu zinaweza kwenda hata 200 wakati volume ni ileile ya mwenye chapter 78.Moja ulipie 7000 na nyingine 19,000!Watu hawataimudu hiyo ya vichapter vifupi vifupi na hivyo kufuatilia zile ambazo wanazimudu.Mfano ile hadithi nzuri ya Shamba la hela,mtunzi anaweka visura vifupi fupi sana ikitokea akiweka kule inabidi aongeze ukubwa wa chapter zake ili watu wengi waweze kuinunulia coins na kuisoma kwa unafuu!Ikiwa ndefu hawatanunua kwakuwa itahitaji fedha nyingi zaidi kuliko zenye chapter ndefu kama za Elton.
Nimpongeze Elton Tony kwa kuandika kazi nzuri sana.Nimesoma Dylan,Change,Mimi na mimi na Invisible.Huyu jamaa ni level nyingine kabisa katika utunzi wa stori tamu,Uandishi wenye mguso na mpangilio mzuri wa maneno ya kiswahili fasaha.