Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

Hii Hadithi ikiisha na ya bm ndio mwisho wa kusoma Hadithi za jf Mana unakuwa mtumwa fulani
 
Hii Hadithi ikiisha na ya bm ndio mwisho wa kusoma Hadithi za jf Mana unakuwa mtumwa fulani
BM ni too much aisee na kinachovutia hizi simulizi za BM na Jack Daniel ni za ukweli. 😄 😄 😄
 
SEHEMU YA TISINI NA TATU

Samson aliingia ndani na kutulia huku akiwaza mambo yake,

Ukweli ni kwamba juu ya yote yanayoendelea hapa nyumbani kuhusu Mimi, bado hawa watu wanaupendo wa kweli, tena usiokuwa na shaka kwani wamenivumilia kwa kiasi kikubwa, na licha ya mama kuonesha wazi kutopenda niendelee na shule nadhani Kuna muda yuko sahihi,

Rahma ana mtoto wangu ambaye kapatikana kinyume na taratibu ambapo tulishaonywa, Lakini yote kwa yote bado Mzee wangu anataka niendelee na shule, huenda Kuna kitu wanakiona kwangu ambacho sijakigundua ila basi nitaendelea na masomo Wala sitawangusha Hawa wazee, Samson alijiwazia akiwa pale kwenye kiti.

Alitoka nje huku akigundua giza nalo linaingia , akaamua kuingia jikoni alipo Sarah ili hata mama Kulwa akija akute kila mmoja yupo bize, baada ya muda fulani ilisikika honi ya gari ambapo Samson alitambua kuwa ni mama Kulwa kwani huwa na mtindo wa peke yake,
Samson alifungua geti huku gari likiingia Kisha akasikia sauti ikiita.
MWANANGUUU!!!

Sauti haikuwa ngeni masikioni mwake, hata moyo wake ulipiga kidogo, alifunga geti vizuri kisha akakimbia kuelekea mahali linapopark gari , ndipo alipokutana uso kwa uso na mama yake mzazi huku akishangaa amefikaje mjini?
Mbona hakuambiwa?

Jamani baba yanguuuu,
Ni muda mrefu tena sijakuona , umebadilika sana mwanangu na hapa hata siamini kama nimeonana na wewe , hakika MUNGU ni mwema.
Yalikuwa ni maneno toka kwa mama mzazi wa Samson akiwa anashindwa kabisa kuizuia furaha yake baada ya kuonana na mwanae pekee wa kiume.

Mama kwanza siamini, mbona sikuwa na taarifa ya ujio wako mama yangu, imekuwaje? Vipi nyumbani ni salama? Hajambo baba yangu? Da Jane naye vipi? mmmmh ujue bado siamini kama ni wewe mama! aliongea kwa utani Samson huku wakicheka.

Hapana ujio wangu ni wa kawaida mbona, nimeambiwa kuwa hujui kama nakuja, ila tangu mwezi wa kumi niliambiwa nije, nikawa nimebanwa na kazi zangu, lakini pia baba yako hakutaka nije hivyo ikawa changamoto, lakini pia msisitizo niliopata toka kwa huyu mama yako (mama Kulwa) nikaona ngoja nije tu na baba yako aliridhia mimi kusafiri hasa baada ya kupewa hela. alifafanua mama mzazi wa Samson.
Lugha iliyotumika hapa kwenye maongezi Kati ya Samson na mama yake, ilimzingua kidogo mama Kulwa hivyo akawa haelewi chochote.maana walikuwa wakiongea kinyumbani.

Jamani dada karibuni ndani,karibu sana tena sana, alikaribisha mama Kulwa.

Mzee Mgaya naye alifika huku akiwa na bashasha na uchangamfu wa hali ya juu, kifupi sura zote zilikuwa na tabasamu hata mama Kulwa licha ya kuwa siku zote huwa anaweka sura ya kikauzu yenye mikwara lakini siku hiyo alikuwa vizuri huku utani ukitawala mle ndani.

Kwanza shemeji pole na safari na wote yaani familia kiujumla tunamshukuru MUNGU kwa wewe kufika salama, na nadhani Samson atakuwa kashangaa wewe kufika hapa maana imekuwa ghafla kwake, lakini nadhani imekuwa ni Moja ya surprise kubwa kwake, na namuona alivyofurahi. Aliweka kituo mzee Mgaya huku wakitazamana na Samson na kucheka.

Kwakweli niwashukuru zaidi nyie , kwa upendo mlionionesha, unajua nikiwa njiani nilikuwa nawaza sana Sina simu kama mnavyojua nimesafiri tarehe ambayo mlipendekeza nyinyi kuwa iwe tarehe 20 December, kwahiyo kitendo cha kupanda gari huku ninakoenda nikiwa Sina mawasiliano na wahusika kilinipa wasiwasi kidogo. (huku akicheka) hivyo Kila gari linapokaribia na Mimi hofu inaongezeka nikiwaza nisije Kuta hakuna wa kunipokea nitakuwa mgeni wa nani jiji hili.Na huu mji unavyobadilika Kila siku licha ya kuwa niliwahi kuja enzi za usichana wangu, Lakini kwasasa hakuna ninapopajua.

Lakini baada ya gari kufika stendi ile kusimama tu niliiona sura ya dada yangu {akimaanisha mama Kulwa)
Ndipo nilipofarijika na kujikuta nashusha Presha yangu yote kwa yote nawashukuru wote kwa ukarimu wenu. aliweka kituo mama mzazi wa Samson na kuwafanya watu wacheke.

Dada watu wote tulijua huna simu hivyo kwanza tuliizingatia tarehe tuliyopanga na pia muda wa kuripoti mabasi huwezi amini saa Saba nilikuwa pale nikiwa na huyu msichana (akimaanisha Cathy)
Na jambo zuri kwenye barua tulikwambia upande magari kampuni ya (akitaja jina)hivyo sikuwa na wasiwasi Dada na nilishukuru kukuona. aliweka kituo mama Kulwa

Wakati huo Cathy alikuwa pembeni akimwangalia mama yake Samson kuanzia juu mpaka chini labda zile raba kuukuu alizovaa pamoja na kiremba cha chama kikongwe kukiwa na picha ya mgombea ambaye ndiye alikuwa Rais kwa wakati huo.
Samson alizigundua dharau za Cathy kwa mama yake lakini hakusema kitu chochote, kwani Cathy muda mwingi alimwangalia Mama yake Sam huku akibinua midomo ya dharau.

Sasa mama mimi naondoka ngoja niwahi nataka nikaorodheshe vitu fulani kwaajili ya kuweka sawa Yale mambo yetu. Cathy aliaga huku akichukua gari la Mama Kulwa na kuondoka nalo nyumbani kwake.

Hivi huyu mtoto naye mbona huwa anajisahau sana , mwanamke mtu mzima sahizi saa tatu usiku upo kwenye majumba ya watu nini shida? alilaumu Mzee Mgaya.

Hapana mume wangu huyu ni leo tu Kuna mambo yake alikuwa anayarekebisha na nikamsaidia, baada ya kumaliza nikamwomba anisindikize stand kwaajili ya kumpokea mgeni hivyo tumekuja wote mpaka hapa. Mama Kulwa alijibu Kwa upole na utulivu kidogo tofauti na siku zote labda ni kwasababu ya uwepo wa mgeni.kisha mama Kulwa akiinuka na mgeni kwaajili ya kumuonesha sehemu zingine kama bafu n. k

Baadaye watu wote walijumuika kupata Chakula Cha usiku pamoja huku amani na furaha zikitawala mle ndani , huku kitendo cha mama yake Sam kubeba mizigo kama zawadi kikiwafurahisha sana Mzee Mgaya na mkewe, kubwa zaidi ni pale alipochukua kuku wawili majogoo wa haja hakika mama Kulwa alifurahi sana.

Mume wangu Hawa kuku hii ni zawadi yangu, nishaambiwa tangu tukiwa stand hivyo hakuna atakaye gusa hata kipande, labda wajina wangu huyu (akimaanisha mtoto wa Rahma) maana wewe huchelewi kupeleka kwa Tausi, yaani huwa hutaki Tausi kimkose kitu mama Kulwa aliongea kiutani huku kauli ile ikionesha kumkwaza Mzee Mgaya lakini alipiga kimya kiume huku akicheka kinafiki.

Jamani nashukuru kwa malezi ya mwanangu, yaani Samson kabadilika sana Hawa mrefu na pia kanenepa , amekuwa mbaba mwanangu, yaani nawapongeza sana MUNGU awazishie na kuwajazia pale mnapotoa. aliongea Mama yake Sam.

Samson kawa mbaba kweli tena mwanaume wa nguvu,huku uanaume wake akiutumia kwa fujo maana hata huyu mtoto unayemuona hapa ni mtoto wa Samson , maana tuseme tu ukweli katukosea na hili ndilo tulilokuitia. aliongea Mzee Mgaya kwa sauti ya kivivu huku mama yake Samson akimgeukia mwanaye na kumshangaa.

Mmmmh mume wanguuuu mbona unaibua mambo haya usiku huu ili iweje? Mimi niliyempokea huyu mgeni sijamwambia chochote cha kumuhusu mwanaye, huyu apumzike kwanza apunguze uchovu, na kesho Wala asiwahi kuamka yeye ahakikishe uchovu umeisha Kisha nitaanza kumchambulia Mimi habari za Samson A_Z tena kwa mpangilio wa matukio siyo kimikato kama wewe, dada naona chumba kishaandaliwa stori zingine tutazungumza kesho. Mama Kulwa aliondoka na mgeni na kumwacha Samson na Mzee Mgaya sebuleni huku Samson akikosa amani haswa baada ya mama yake kukata jicho Kali kwa Yale aliyoyasikia toka kwa Mzee Mgaya.

Samson akiwa chumbani kwake alikosa raha kabisa Kila akifikiria mdomo wa mama Kulwa jinsi atakavyoongea mambo mengi kama anasoma kwenye Diary alikosa amani huku akigundua kuwa ujio wa mama yake huenda ni maswala yake.

Nini kitajiri asubuhi baada ya mama mzazi wa Samson kuamka? Tukutane sehemu inayofuata.

Loading.......................
 
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
 
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
Sawa
 
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
😂😂😂😂
Nakuelewa sana Mkuu na nilihisi tu utakuwa huko huko. Pole kwa kutukanwa huko PM na Vijana wasiojielewa
 
Pole mkuu
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
 
JNHP mradini
Kuna Engineers upo nao hapo nafahamiana nao namie Niko she hapa fela mwanza lot 5 section 4. Karibu pm tupeane madini ya fani yetu hata cv3D Kama hutojali mie Ni somasoma. Naamini kuwa " a man will fly strength of his mental power and not physical power"
 
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
asante sana.
 
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
Shukrani mkuu tuendelee ivo ivo tu mdgo mdgo mpka mwsho
 
Kwa wale wote mnaofuatilia simulizi hii nawaombeni mniwie radhi ni majukumu yananibana kwani nipo huku JNHP mradini. ila kwa Sasa nitaimalizia kwa ipo mwishoni bado vipande vichache. Msikose kuchungulia

Lakini pia Mimi siuzi hadithi na yule aliyekuja PM na kunitukana, naomba ajue kuwa nimejisikia vibaya sana, na Mimi siishi kwa kuuza stori, Bali nimeshare nanyi kwaajili ya kiburudisho na kujifunza.

keisangora Manyanza ram Boogman makorere Numbisa Mkushi w jani moneytalk hewizet MR KUO na wengine wote niliowasahau.
khee makubwa yani mtu mzima mwenye meno 32 kabisaaa kakufata pm kukutukana,haki kuna watu hawana akili kabisa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom