Simulizi: Milango ya mafanikio

Simulizi: Milango ya mafanikio

SEHEMU YA THEMANINI NA TISA

Mzee Mgaya alikaa kwenye kiti huku macho yakiwa kwa yule Binti mgeni, Mzee Mgaya hakuwa mtu mwenye kuwachangamkia wasichana wadogo, hivyo hakuweza kumsalimia Zena licha ya kuwa yeye ndiye kamkuta, Samson yeye alizuga kuingia chumbani kwake huku masikio yakiwa huku ili ajue kitazungumzwa Nini.

Shikamoo baba, Zena alisalimia kwa sauti yenye uchangamfu.

Marhaba mwanangu, japo napata shida kukutambua. alijibu salamu ile Mzee Mgaya huku akijenga tabasamu la kulazimisha ili asimtishe Binti wa watu.

Naitwa Zena, nasoma shule ya secondary ya (akitaja jina la shule)
Nasoma pamoja na Samson, Kuna zamu tulipangiwa kuja shuleni tarehe ya Leo, hivyo sikumuona Sam, nikadhani labda kasafiri kwenda mkoani lakini nashukuru nimemuona.
Zena alijua sana kudanganya hata Sam mwenyewe alijua ni uongo kwani hakukuwa na zamu yeyote.

Wewe Sam hebu njoo , huyu si unamfahamu Sasa mbona unaenda kujificha chumbani kwako?
Au hujui kama kakufuata wewe.
Mzee Mgaya alimuita Samson.

Samson alishusha pumzi huku akimshukuru MUNGU kwani Zena hakuja na Yale ambayo alikuwa anayafikiria kuwa kaja nayo.

Mzee Mgaya aliinuka na kuingia chumbani kwake akiwaacha Samson na Zena wakipiga stori pale sebuleni, japokuwa Zena alikuwa kachangamka huku akiwa anajiamini, lakini Samson hakupenda kwani alijikuta kama anabanwa, alitamani kumwambia Zena aondoke lakini aliona si jambo zuri, akaamua kuvumilia tu.

Jana nimekuona maeneo fulani ya mnada ulikuwa kwenye meza ya mama mmoja hivi Ukiwa unaangalia nguo za watoto wachanga, ujue ulishangaza sana watu, nilitamani nikushtue lakini tuliongozana na mama hivyo nikaona nisije kuamsha masuala mengine nikatulia, ila watu walikushangaa sana, pia yule muuzaji alikumaindi sana na ni afadhali uliondoka mapema nadhani ungezubaa pale ungehisiwa ni mshirikina. Zena aliweka kituo

Samson alitabasamu huku akishikwa na uoga fulani, kwani Kila akikumbuka tukio lile aligundua ilikuwa ni hatari kubwa kwake hata hivyo alishukuru kuwa salama hadi muda ule.

Zena alionesha kumpenda Samson sana , hivyo wakawa wanapiga stori zao za shule huku Zena aliyesifika kwa kuongea sana akifunga sebule ya Mzee Mgaya kwa muda.

Honi ilisikika ikiashiria mama Kulwa anarudi, Samson alienda kufungua geti na kumpokea mama yake pamoja na Rahma.

Wapi tena mume wangu, yaani siku hizi nimegundua hutaki hata kuniona,hutaki kukaa na Mimi , kwanza hushindi hapa, hulali , umekuwa kama mpitanjia tu kwanini mume wanguuuu, huyo Tausi kakupa Nini kiasi cha kushinda huko yaani hata humchoki, ndiyo najua Mimi ni Mzee , umri wangu unaenda lakini sijazeeka kihivyo, sijui nani atatangulia kufa Kati ya Mimi na wewe, lakini kama ukianza wewe unadhani msiba utakuwa wapi baba, kama siyo hapa,ukiumwa kidogo unakimbilia hapa kwangu,Ukiwa mzima wewe ni wa Tausi. Huyu mtoto mchanga wa Rahma anasumbuliwa na hapa tunatoka hospital,unajua fika mtoto kazaliwa kabla ya miezi hivyo lazima atakuwa na afya mgogoro lakini hata kukaa dakika tatu nikueleze mambo yanaendaje hutaki, shughuli zangu nyingi zinakwama kwaajili ya Rahma na Samson, Mimi nilishamaliza kulea watoto, nahitaji kupumzika lakini Samson kanipa ulezi mpya kabisa au kwakuwa hulali hapa, usichojua ni kwamba mtoto huyu analia sana nyakati za usiku kutokana na afya yake mgogoro.

Na Rahma mwenyewe ndiyo kwanza anazaa hajui hata kumbembeleza mwanaye, anajikuta na yeye analia tu hivyo mume wangu tambua kuwa silali kabisa. Nadhani napaswa kuhurumiwa, ni matatizo ambayo kaniletea mwanao Samson.
mama Kulwa licha ya kulalamika sana lakini Mzee Mgaya hakujibu chochote badala yake alidai afunguliwe geti atoe gari Kisha akatokomea.

Heee kumbe Kuna mgeni ndani , vipi hujambo Binti yangu, mama Kulwa alisalimia huku akiona aibu fulani kwa maneno aliyotoka kuropoka muda si mrefu akiwa nje.

Zena mtoto black beauty na mzuri wa sura mwenye kujenga tabasamu zuri ,wamezoeshwa kuitwa chocolate colour,aliitikia salamu ya mama Kulwa, huku akijitambulisha kuwa ni rafiki wa Samson.

Mama Kulwa aliguna kidogo Kisha akamwangalia Samson Kwa jicho fulani lenye Shari,
Karibu sana mwanangu Mimi sijawahi kukuona naona umemtembelea Samson, aliuliza mama Kulwa.

Yes mama unajua Samson ni mwanafunzi anayekubalika sana darasani kwetu, karibu Kila mwanafunzi anamkubali kwa uwezo wake kwahiyo nimejikuta napenda kumuona hasa ukizingatia zaidi ya wiki mbili sijamuona, najua anaishi hapa nikaamua kumcheki, Zena alifafanua.

Sura ya Rahma ilibadilika haraka sana, akionesha kachukia ghafla, akamchukua mtoto wake toka mikononi mwa mama Kulwa na kwenda kumkabidhi Samson.

Samson alishangaa, si yeye tu hata mama Kulwa na Sara walishangaa pia kwani hajawahi kufanya hivyo Rahma.
Vipi mbona unaninyang'anya mtoto na kumpa Sam vipi. aliuliza mama Kulwa.

Kwani Kuna kosa lolote, kwani huyu ni mtoto wa nani, Samson ni baba yake, anastahili kushinda naye hata kutwa nzima Wala hakuna shida. Rahma aliongea kwa hasira huku akionesha wivu wa kitoto.na kukimbilia chumbani kwake

Mama Kulwa aligundua kinachomsumbua Rahma ikabidi awe mpole akainuka na kwenda chumbani kwa Rahma ili akambembeleze.

Zena mwanafunzi mjanja aligundua picha ile, akamwangalia Samson na kutabasamu Kisha akampungia mkono wa bye Sam kuashiria anaondoka.

Sasa mwanangu Rahma unadhani Samson anakaa hapa, huyu anaendelea na masomo yake Tena bado siku chache anaenda kuripoti na atakuwa anakaa huko , na unanishangaza kweli mwanangu, wewe hukupaswa hata kukaribiana na Samson, kwani kuzaa na mtu bila ndoa ni aibu tu Wala siyo sifa nzuri , mbaya zaidi unaonesha wivu mbele yangu hii inadhihirisha hukujuta hata kosa lako, usifanye hivyo mwanangu . mama Kulwa aliongea kwa upole huku akimsihi Rahma atulie.

*************************************

Baada ya siku kadhaa kupita ilikuwa ni mida ya mchana Samson na mama Kulwa walikuwa barazani Samson akipokea ushauri fulani kutoka kwa mama Kulwa ,

Siku zote mwanangu unadhani nakuchukia ama sikupendi hapana, tambua hata yote aliyoyafanya baba yako, kuhamishwa shule na kupelekwa wanakosoma akina Kulwa bado Kuna baraka zangu pia, lakini Kaa ukijua kuwa umetufanyia visa na vituko vingi sana humu ndani, hakuna mwenye akili timamu angevumilia, lakini Kuna vitu tumeamua kuziba masikio na kufumba macho lengo wewe utimize ndoto zako, Sasa nakuomba mwanangu kaza kamba hii Dunia wala haina jipya utamaliza wasichana wote wa Kila aina lakini baadaye utajuta tu kwani watakuwa wamekucheleweshea muda wako bure tu.upo umri wa kusoma na ukikupita mara nyingi inakuwa ni basi tena, hivyo kwasasa zingatia masomo, una siku chache sana kuanzia Sasa utakuwa shule mpya tafadhali tabia zako zote za kijinga ziache hapa hapa nadhani itakusaidia wewe kujitengenezea tabia njema shuleni kwenu. mama Kulwa aliongea kwa hisia na sauti ya upole sana.

Cathy mwanamke mcharuko alifika pale nyumbani kwa mama Kulwa huku akiwa kachangamka fulani hivi.

Enhee hebu jitetee siku zote hizo hujaja kunisalimia mama yako ulikuwa na maana gani? alitania mama Kulwa.

Mama wewe acha tu huwezi amini mambo yangu mengi yamekwama, mwezi huu, na hapa nilipo ni kama nimechanganyikiwa tu, Mr nikiwasiliana naye anaonekana yupo bize sana, na Kuna tetesi nimepata kuwa Kuna mzigo alipeleka nchi fulani Sasa inaonesha kazidiwa ujanja na mafioso wa huko mbele kwahiyo December imekuwa mbaya sana kwangu, gari limeharibika na baada ya kupeleka garage bei niliyotajiwa MUNGU anajua , nimeamua kuliacha tu. aliweka kituo Cathy.

Kwahiyo Binti yangu umeona suluhisho la matatizo yanayokukabili ni kunywa pombe si ndiyo? Unajidanganya, pombe ni starehe inanywewa pindi mtu akiwa na amani na kamwe usijidanganye kuwa itapunguza matatizo yako badala yake itakushushia heshima tu.halafu mwanangu haya ni mavazi gani tena,wewe ulipofikia una heshima zako ujue,angalia mavazi ya kuvaa kulingana na mazingira.aliweka kituo mama Kulwa.

Wewe mama acha tu, kwanza nina kazi yangu pale nyumbani nilikuwa namuomba Sam akanisaidie, aliongea Cathy huku akiinuka

Samson, ongozana na dada yako ukamsaidie kazi anayosema nadhani pia itakuwa vizuri maana amelewa, na uwe makini kumsaidia huko barabarani. aliweka kituo mama Kulwa.

Dakika kadhaa walikuwa nyumbani kwa Cathy, huku dada wa kazi wa Cathy akiwa bize pale Nje, yule dada alimuita Sam kwa ishara Kisha akamtahadhalisha,
Tafadhali mdogo wangu naomba usiwe unakuja hapa ujue Cathy aligombana na mumewe kisa wivu wa mapenzi na mumewe huja hapa bila taarifa kwahiyo kuwa makini usije kuwa muhanga. alionya yule dada

Samson alikaa kwenye kiti akisubiri kazi aliyoahidiwa lakini Cathy alikuwa kimya mara akae mkao huu mara hivi ili mradi amtege Samson. Lakini Samson kwa siku ile alikaa imara kama ukuta wa Berlin kwani alishapewa onyo.

Sioni ukinielekeza kazi uliyoniitia na kama haipo Mimi naondoka, aliongea Samson akitaka kuinuka.

Halafu wee naye una miaka mitatu Sasa hapa mjini lakini ushamba haujakutoka tu eeh, hebu njoo kwanza huku, Cathy alimshika Samson mkono na kumkokotea chumbani kwake, lakini Sam alimzidi nguvu na kukimbia lakini hakuwa na pakwenda kwani milango ilifungwa .

Ahaaaaa kwahiyo unanikimbiaaaaa nenda basi, si unataka kutoka?
Nenda mshamba wewe,
Kwanza najilaumu sana mtu hujiongezj, yaani nitaongea na mama Kulwa wakufukuze mpumbavu wewe
Na hujui tu kuwa neno lolote nikimwambia mama Kulwa huwa ananikubali Sasa tutaona. aliongea Cathy kwa sauti ya kilevi huku akifungua mlango na kumsukuma Samson kwa nguvu huku akimtukana.


Itaendelea......... ...............
 
SEHEMU YA THEMANINI NA TISA

Mzee Mgaya alikaa kwenye kiti huku macho yakiwa kwa yule Binti mgeni, Mzee Mgaya hakuwa mtu mwenye kuwachangamkia wasichana wadogo, hivyo hakuweza kumsalimia Zena licha ya kuwa yeye ndiye kamkuta, Samson yeye alizuga kuingia chumbani kwake huku masikio yakiwa huku ili ajue kitazungumzwa Nini.

Shikamoo baba, Zena alisalimia kwa sauti yenye uchangamfu.

Marhaba mwanangu, japo napata shida kukutambua. alijibu salamu ile Mzee Mgaya huku akijenga tabasamu la kulazimisha ili asimtishe Binti wa watu.

Naitwa Zena, nasoma shule ya secondary ya (akitaja jina la shule)
Nasoma pamoja na Samson, Kuna zamu tulipangiwa kuja shuleni tarehe ya Leo, hivyo sikumuona Sam, nikadhani labda kasafiri kwenda mkoani lakini nashukuru nimemuona.
Zena alijua sana kudanganya hata Sam mwenyewe alijua ni uongo kwani hakukuwa na zamu yeyote.

Wewe Sam hebu njoo , huyu si unamfahamu Sasa mbona unaenda kujificha chumbani kwako?
Au hujui kama kakufuata wewe.
Mzee Mgaya alimuita Samson.

Samson alishusha pumzi huku akimshukuru MUNGU kwani Zena hakuja na Yale ambayo alikuwa anayafikiria kuwa kaja nayo.

Mzee Mgaya aliinuka na kuingia chumbani kwake akiwaacha Samson na Zena wakipiga stori pale sebuleni, japokuwa Zena alikuwa kachangamka huku akiwa anajiamini, lakini Samson hakupenda kwani alijikuta kama anabanwa, alitamani kumwambia Zena aondoke lakini aliona si jambo zuri, akaamua kuvumilia tu.

Jana nimekuona maeneo fulani ya mnada ulikuwa kwenye meza ya mama mmoja hivi Ukiwa unaangalia nguo za watoto wachanga, ujue ulishangaza sana watu, nilitamani nikushtue lakini tuliongozana na mama hivyo nikaona nisije kuamsha masuala mengine nikatulia, ila watu walikushangaa sana, pia yule muuzaji alikumaindi sana na ni afadhali uliondoka mapema nadhani ungezubaa pale ungehisiwa ni mshirikina. Zena aliweka kituo

Samson alitabasamu huku akishikwa na uoga fulani, kwani Kila akikumbuka tukio lile aligundua ilikuwa ni hatari kubwa kwake hata hivyo alishukuru kuwa salama hadi muda ule.

Zena alionesha kumpenda Samson sana , hivyo wakawa wanapiga stori zao za shule huku Zena aliyesifika kwa kuongea sana akifunga sebule ya Mzee Mgaya kwa muda.

Honi ilisikika ikiashiria mama Kulwa anarudi, Samson alienda kufungua geti na kumpokea mama yake pamoja na Rahma.

Wapi tena mume wangu, yaani siku hizi nimegundua hutaki hata kuniona,hutaki kukaa na Mimi , kwanza hushindi hapa, hulali , umekuwa kama mpitanjia tu kwanini mume wanguuuu, huyo Tausi kakupa Nini kiasi cha kushinda huko yaani hata humchoki, ndiyo najua Mimi ni Mzee , umri wangu unaenda lakini sijazeeka kihivyo, sijui nani atatangulia kufa Kati ya Mimi na wewe, lakini kama ukianza wewe unadhani msiba utakuwa wapi baba, kama siyo hapa,ukiumwa kidogo unakimbilia hapa kwangu,Ukiwa mzima wewe ni wa Tausi. Huyu mtoto mchanga wa Rahma anasumbuliwa na hapa tunatoka hospital,unajua fika mtoto kazaliwa kabla ya miezi hivyo lazima atakuwa na afya mgogoro lakini hata kukaa dakika tatu nikueleze mambo yanaendaje hutaki, shughuli zangu nyingi zinakwama kwaajili ya Rahma na Samson, Mimi nilishamaliza kulea watoto, nahitaji kupumzika lakini Samson kanipa ulezi mpya kabisa au kwakuwa hulali hapa, usichojua ni kwamba mtoto huyu analia sana nyakati za usiku kutokana na afya yake mgogoro.

Na Rahma mwenyewe ndiyo kwanza anazaa hajui hata kumbembeleza mwanaye, anajikuta na yeye analia tu hivyo mume wangu tambua kuwa silali kabisa. Nadhani napaswa kuhurumiwa, ni matatizo ambayo kaniletea mwanao Samson.
mama Kulwa licha ya kulalamika sana lakini Mzee Mgaya hakujibu chochote badala yake alidai afunguliwe geti atoe gari Kisha akatokomea.

Heee kumbe Kuna mgeni ndani , vipi hujambo Binti yangu, mama Kulwa alisalimia huku akiona aibu fulani kwa maneno aliyotoka kuropoka muda si mrefu akiwa nje.

Zena mtoto black beauty na mzuri wa sura mwenye kujenga tabasamu zuri ,wamezoeshwa kuitwa chocolate colour,aliitikia salamu ya mama Kulwa, huku akijitambulisha kuwa ni rafiki wa Samson.

Mama Kulwa aliguna kidogo Kisha akamwangalia Samson Kwa jicho fulani lenye Shari,
Karibu sana mwanangu Mimi sijawahi kukuona naona umemtembelea Samson, aliuliza mama Kulwa.

Yes mama unajua Samson ni mwanafunzi anayekubalika sana darasani kwetu, karibu Kila mwanafunzi anamkubali kwa uwezo wake kwahiyo nimejikuta napenda kumuona hasa ukizingatia zaidi ya wiki mbili sijamuona, najua anaishi hapa nikaamua kumcheki, Zena alifafanua.

Sura ya Rahma ilibadilika haraka sana, akionesha kachukia ghafla, akamchukua mtoto wake toka mikononi mwa mama Kulwa na kwenda kumkabidhi Samson.

Samson alishangaa, si yeye tu hata mama Kulwa na Sara walishangaa pia kwani hajawahi kufanya hivyo Rahma.
Vipi mbona unaninyang'anya mtoto na kumpa Sam vipi. aliuliza mama Kulwa.

Kwani Kuna kosa lolote, kwani huyu ni mtoto wa nani, Samson ni baba yake, anastahili kushinda naye hata kutwa nzima Wala hakuna shida. Rahma aliongea kwa hasira huku akionesha wivu wa kitoto.na kukimbilia chumbani kwake

Mama Kulwa aligundua kinachomsumbua Rahma ikabidi awe mpole akainuka na kwenda chumbani kwa Rahma ili akambembeleze.

Zena mwanafunzi mjanja aligundua picha ile, akamwangalia Samson na kutabasamu Kisha akampungia mkono wa bye Sam kuashiria anaondoka.

Sasa mwanangu Rahma unadhani Samson anakaa hapa, huyu anaendelea na masomo yake Tena bado siku chache anaenda kuripoti na atakuwa anakaa huko , na unanishangaza kweli mwanangu, wewe hukupaswa hata kukaribiana na Samson, kwani kuzaa na mtu bila ndoa ni aibu tu Wala siyo sifa nzuri , mbaya zaidi unaonesha wivu mbele yangu hii inadhihirisha hukujuta hata kosa lako, usifanye hivyo mwanangu . mama Kulwa aliongea kwa upole huku akimsihi Rahma atulie.

*************************************

Baada ya siku kadhaa kupita ilikuwa ni mida ya mchana Samson na mama Kulwa walikuwa barazani Samson akipokea ushauri fulani kutoka kwa mama Kulwa ,

Siku zote mwanangu unadhani nakuchukia ama sikupendi hapana, tambua hata yote aliyoyafanya baba yako, kuhamishwa shule na kupelekwa wanakosoma akina Kulwa bado Kuna baraka zangu pia, lakini Kaa ukijua kuwa umetufanyia visa na vituko vingi sana humu ndani, hakuna mwenye akili timamu angevumilia, lakini Kuna vitu tumeamua kuziba masikio na kufumba macho lengo wewe utimize ndoto zako, Sasa nakuomba mwanangu kaza kamba hii Dunia wala haina jipya utamaliza wasichana wote wa Kila aina lakini baadaye utajuta tu kwani watakuwa wamekucheleweshea muda wako bure tu.upo umri wa kusoma na ukikupita mara nyingi inakuwa ni basi tena, hivyo kwasasa zingatia masomo, una siku chache sana kuanzia Sasa utakuwa shule mpya tafadhali tabia zako zote za kijinga ziache hapa hapa nadhani itakusaidia wewe kujitengenezea tabia njema shuleni kwenu. mama Kulwa aliongea kwa hisia na sauti ya upole sana.

Cathy mwanamke mcharuko alifika pale nyumbani kwa mama Kulwa huku akiwa kachangamka fulani hivi.

Enhee hebu jitetee siku zote hizo hujaja kunisalimia mama yako ulikuwa na maana gani? alitania mama Kulwa.

Mama wewe acha tu huwezi amini mambo yangu mengi yamekwama, mwezi huu, na hapa nilipo ni kama nimechanganyikiwa tu, Mr nikiwasiliana naye anaonekana yupo bize sana, na Kuna tetesi nimepata kuwa Kuna mzigo alipeleka nchi fulani Sasa inaonesha kazidiwa ujanja na mafioso wa huko mbele kwahiyo December imekuwa mbaya sana kwangu, gari limeharibika na baada ya kupeleka garage bei niliyotajiwa MUNGU anajua , nimeamua kuliacha tu. aliweka kituo Cathy.

Kwahiyo Binti yangu umeona suluhisho la matatizo yanayokukabili ni kunywa pombe si ndiyo? Unajidanganya, pombe ni starehe inanywewa pindi mtu akiwa na amani na kamwe usijidanganye kuwa itapunguza matatizo yako badala yake itakushushia heshima tu.halafu mwanangu haya ni mavazi gani tena,wewe ulipofikia una heshima zako ujue,angalia mavazi ya kuvaa kulingana na mazingira.aliweka kituo mama Kulwa.

Wewe mama acha tu, kwanza nina kazi yangu pale nyumbani nilikuwa namuomba Sam akanisaidie, aliongea Cathy huku akiinuka

Samson, ongozana na dada yako ukamsaidie kazi anayosema nadhani pia itakuwa vizuri maana amelewa, na uwe makini kumsaidia huko barabarani. aliweka kituo mama Kulwa.

Dakika kadhaa walikuwa nyumbani kwa Cathy, huku dada wa kazi wa Cathy akiwa bize pale Nje, yule dada alimuita Sam kwa ishara Kisha akamtahadhalisha,
Tafadhali mdogo wangu naomba usiwe unakuja hapa ujue Cathy aligombana na mumewe kisa wivu wa mapenzi na mumewe huja hapa bila taarifa kwahiyo kuwa makini usije kuwa muhanga. alionya yule dada

Samson alikaa kwenye kiti akisubiri kazi aliyoahidiwa lakini Cathy alikuwa kimya mara akae mkao huu mara hivi ili mradi amtege Samson. Lakini Samson kwa siku ile alikaa imara kama ukuta wa Berlin kwani alishapewa onyo.

Sioni ukinielekeza kazi uliyoniitia na kama haipo Mimi naondoka, aliongea Samson akitaka kuinuka.

Halafu wee naye una miaka mitatu Sasa hapa mjini lakini ushamba haujakutoka tu eeh, hebu njoo kwanza huku, Cathy alimshika Samson mkono na kumkokotea chumbani kwake, lakini Sam alimzidi nguvu na kukimbia lakini hakuwa na pakwenda kwani milango ilifungwa .

Ahaaaaa kwahiyo unanikimbiaaaaa nenda basi, si unataka kutoka?
Nenda mshamba wewe,
Kwanza najilaumu sana mtu hujiongezj, yaani nitaongea na mama Kulwa wakufukuze mpumbavu wewe
Na hujui tu kuwa neno lolote nikimwambia mama Kulwa huwa ananikubali Sasa tutaona. aliongea Cathy kwa sauti ya kilevi huku akifungua mlango na kumsukuma Samson kwa nguvu huku akimtukana.


Itaendelea......... ...............

Cathy anaenda kuumbuka
 
SEHEMU YA TISINI

Tena afadhali umerudi maana nakosa mtu wa kumtuma hapa, vipi ni kazi gani alikuitia ukamfanyie Cathy? mama Kulwa aliuliza.

Sijafanya kazi yoyote kwasababu dada Cathy alipata dharula.
alijibu Kwa kudanganya Samson.

Mmmmh huyu Cathy pombe zinampeleka vibaya ukute hajapata dharula yoyote bali kaenda kulewa tu lazima nitaongea naye, na kibaya zaidi akipata changamoto kidogo kwenye mambo yake hukimbilia kunywa pombe hajui kama ndiyo anaweza kujipoteza.
aliongeza mama Kulwa.

Sasa Sam mwanangu naomba uende kwenye ile grocery ya yule mama kule karibu na barabara kuu Kuna mzigo wangu atakupa, tafadhali kuwa makini njiani si unajua sikukuu hii inakaribia unaweza kuporwa
nashindwa kumtuma Sarah, kwasababu ana kazi nyingi lakini pia ni mtu mzima nashindwa kum direct moja kwa moja baadhi ya vitu.

Samson alitoka na kuelekea alikotumwa, huku akipita kwenye Chochoro alizoona kwake ni shortcut,

Hivi yule Cathy Mimi huwa ananionaje, kwa Mara ya kwanza niliweza lala naye na kudhani labda alinipenda, lakini mbona ile siku mama kanifukuza niliomba nilale kwake alikataa huku akisema nisikanyage kwake na nipunguze mazoea? Halafu leo kalewa pombe zake anakuja kumuomba mama eti nikamfanyie kazi kumbe kanitoa kijanja kusudi nikamtizie haja zake,
Ina maana moja kwa moja hanipendi na huwa namuona jinsi anavyonidharau, Sasa leo bwana wake hayupo ananiita Mimi. Siwezi kwasasa sitakubali na ikiwa atanichongea kwa mama , na Mimi nitaeleza ukweli wote hawezi kunifanya nikawa mtumwa wake.
Nikimtaka Mimi ananidharau na kuniita mshamba, yeye akinitaka basi anataka nimkubalie tu siwezi na sitaweza. alijiwazia Samson huku alichanja mbuga na kuelekea alikotumwa na hatimaye akafika sehemu husika.

Enhee vipi kijana kwahiyo unasema yeye anafanya nini? aliuliza yule mwenyeji wa Samsoni mara baada ya kumsalimiana.

Mama yupo tu nyumbani, kaniambia nije Kuna mzigo utanipa .
alijibu Samson huku akiona kama anachelewa.

Mume wangu nakuomba kwanza ujue huyu rafiki yangu huwa ana masikhara sana na sijui ni dharau hata sijui, eti ndo amemtuma huyu kijana nimpe zile pesa, akipoteza?
Pesa zenyewe ni nyingi kiasi, Sasa hizi ni dharau mno, Mimi nimekuita ili tushauriane tumpe au tutafute namna nyingine ya kufikisha huu mzigo maana huyu kijana sijui mtoto nakuwa na mashaka naye.
Yule mama alimweleza mumewe ambaye ni mwalimu mkuu wa shule anayohama Samson.

Mmmh mke wangu, umefanya vizuri kuniita, huyu ni mwanafunzi wangu namjua vizuri ni mtukutu mno na hizo pesa usimkabidhi badala yake tutapeleka wenyewe. Halafu hii familia ya mzee Mgaya Wana dharau sana tena mno, pesa nyingi kama hii unafanyaje utani na kumtuma mtu ili mradi, ndiyo maana mke wangu tangu siku ile sikupenda kusikia umeazima hela kwa yule mwanamke yaani ni watu wanajionaje sijui, na yule kijana niliyekusimulia asubuhi kuwa wanamuhamisha shule ndiye huyu yaani ana records chafu na mbaya sana shuleni kwangu.
Tena nikwambie tu kuwa yule msichana ambaye nusura amfunge mtoto wetu Sadick kwa kumsingizia eti alitaka kumbaka, Sasa hivi ana mtoto na baba wa mtoto ndiye huyu kijana,Wenyewe wamefichaficha lakini taarifa nimepata.
aliongea yule mwalimu mkuu akionesha chuki za wazi kwa Samson.

Mume wangu jambo lenyewe ni la Siri basi, mbona Kuna Binti anaitwa Catherine (Cathy)alikuwa anakunywa
Pombe hapa tangu saa nne asubuhi nilikuwa naye kaniambia mambo mengi tu kuwahusu hawa, kiufupi familia ya mzee Mgaya imekosa adabu sana tu, na mwenyewe anavyoonaga kayapatia maisha,
Na hata shoga yangu mwenyewe, yale maduka yake mawili tayari hujiona ni nani sijui lakini kifupi ni familia iliyokosa msimamo.

Mwalimu mkuu wa shule iliyo karibu na nyumbani kwa Mzee Mgaya aliinanga ile familia huku wakipokezana na mkewe na wakionesha hawajapendezwa na kitendo cha mama Kulwa kumtuma Samson mtu ambaye hawamwamini hata kidogo.

Kwahiyo huo mzigo naupata au niondoke, Samson aliuliza baada ya kuona wale wenyeji wake wanaendelea na shughuli nyingine.

Wewe nenda tu kamwambie nitaleta mwenyewe tena leo hii hii,
Yaani mpaka natetemeka , eti nikupe hii hela wewe ili uipoteze halafu nionekane sikukupa ili nilipe mara mbili eeh, ni kitu hakiwezekani,
aliongea kwa dharau yule mama na kumruhusu Samson aondoke.

***************************************

Ujue Samson umeingia hapa naona unafanya mambo yako tu hunipi majibu ya kule nilikokutuma vipi,
Kwanza mbona upo mbali mwenzetu huli Chakula leo, hebu kamuamushe na mzazi mwenzio huko, maana naye anadeeeeka sijui hata kitanda hakimchoshi! Lakini kwanza ya yote nipe mzigo wangu niliokutuma.
aliweka kituo mama Kulwa.

Ujue mama ndiyo maana unaona nakosa hata hamu ya kula, yaani mwalimu mkuu na mkewe wamenikatalia katakata kuwa hawawezi kunipa chochote eti hawaniamini, mara sitafikisha mara nini yaani kifupi sijawaelewa, na yule mama kaniambia atakuja mwenyewe atakuletea. Samson alifafanua Kisha akaenda kumuita Rahma na kurudi naye sebuleni.

Haya mama mwenye mtoto asiye na jina,nikisema mumpe jina langu hamtaki na vipi umekuwa boss humu ndani siyo, siku nyingine ujikaze mtoto wa kike bwanaa au kwakuwa Sarah yupo ndiyo unataka Chakula awe anakuletea chumbani kwako.
aliongea kiutani mama Kulwa lakini ujumbe ukifika.

Unajua Sarah wewe ni mgeni humu ndani kwakuwa huna siku nyingi sana, niseme tu kuwa huyu Samson licha ya mambo yake ya kipuuzi mengi aliyotufanyia lakini ni mtu mwenye nidhamu sana na pesa kwanza siyo mwizi, nimeshamtuma sehemu nyingi sana, lakini pia amekuwa akitumwa na baba yake kule saiti afuate pesa kiasi kikubwa Wala siyo vijisenti nilivyomtuma leo, Lakini anafikisha salama kabisa Sasa yule shoga yangu sijamuelewa?
mama Kulwa aliongea huku akiegama kwenye kiti akishindwa hata kula.

Mimi nadhani hajakosea sana, Kuna mawili aidha hana hiyo hela kaamua kuleta visingio tu, au ni kweli hamuamini Samson hasa ukizingatia wanamfahamu kama mtoto mkorofi hivyo inakuwa ngumu kumwamini.
Sarah aliongea naye kwa mtazamo wake.huku akiinuka na kwenda kumchukua mtoto wa Rahma chumbani.

Lakini geti lilisikika likigongwa kwa fujo na Kwa nguvu sana , Samson aliinuka na kwenda kufungua huku akimuuliza jina mgongaji kama ulivyo utaratibu wa watu wengi kabla ya kufungua.

Itaendelea............................
 
SEHEMU YA TISINI

Tena afadhali umerudi maana nakosa mtu wa kumtuma hapa, vipi ni kazi gani alikuitia ukamfanyie Cathy? mama Kulwa aliuliza.

Sijafanya kazi yoyote kwasababu dada Cathy alipata dharula.
alijibu Kwa kudanganya Samson.

Mmmmh huyu Cathy pombe zinampeleka vibaya ukute hajapata dharula yoyote bali kaenda kulewa tu lazima nitaongea naye, na kibaya zaidi akipata changamoto kidogo kwenye mambo yake hukimbilia kunywa pombe hajui kama ndiyo anaweza kujipoteza.
aliongeza mama Kulwa.

Sasa Sam mwanangu naomba uende kwenye ile grocery ya yule mama kule karibu na barabara kuu Kuna mzigo wangu atakupa, tafadhali kuwa makini njiani si unajua sikukuu hii inakaribia unaweza kuporwa
nashindwa kumtuma Sarah, kwasababu ana kazi nyingi lakini pia ni mtu mzima nashindwa kum direct moja kwa moja baadhi ya vitu.

Samson alitoka na kuelekea alikotumwa, huku akipita kwenye Chochoro alizoona kwake ni shortcut,

Hivi yule Cathy Mimi huwa ananionaje, kwa Mara ya kwanza niliweza lala naye na kudhani labda alinipenda, lakini mbona ile siku mama kanifukuza niliomba nilale kwake alikataa huku akisema nisikanyage kwake na nipunguze mazoea? Halafu leo kalewa pombe zake anakuja kumuomba mama eti nikamfanyie kazi kumbe kanitoa kijanja kusudi nikamtizie haja zake,
Ina maana moja kwa moja hanipendi na huwa namuona jinsi anavyonidharau, Sasa leo bwana wake hayupo ananiita Mimi. Siwezi kwasasa sitakubali na ikiwa atanichongea kwa mama , na Mimi nitaeleza ukweli wote hawezi kunifanya nikawa mtumwa wake.
Nikimtaka Mimi ananidharau na kuniita mshamba, yeye akinitaka basi anataka nimkubalie tu siwezi na sitaweza. alijiwazia Samson huku alichanja mbuga na kuelekea alikotumwa na hatimaye akafika sehemu husika.

Enhee vipi kijana kwahiyo unasema yeye anafanya nini? aliuliza yule mwenyeji wa Samsoni mara baada ya kumsalimiana.

Mama yupo tu nyumbani, kaniambia nije Kuna mzigo utanipa .
alijibu Samson huku akiona kama anachelewa.

Mume wangu nakuomba kwanza ujue huyu rafiki yangu huwa ana masikhara sana na sijui ni dharau hata sijui, eti ndo amemtuma huyu kijana nimpe zile pesa, akipoteza?
Pesa zenyewe ni nyingi kiasi, Sasa hizi ni dharau mno, Mimi nimekuita ili tushauriane tumpe au tutafute namna nyingine ya kufikisha huu mzigo maana huyu kijana sijui mtoto nakuwa na mashaka naye.
Yule mama alimweleza mumewe ambaye ni mwalimu mkuu wa shule anayohama Samson.

Mmmh mke wangu, umefanya vizuri kuniita, huyu ni mwanafunzi wangu namjua vizuri ni mtukutu mno na hizo pesa usimkabidhi badala yake tutapeleka wenyewe. Halafu hii familia ya mzee Mgaya Wana dharau sana tena mno, pesa nyingi kama hii unafanyaje utani na kumtuma mtu ili mradi, ndiyo maana mke wangu tangu siku ile sikupenda kusikia umeazima hela kwa yule mwanamke yaani ni watu wanajionaje sijui, na yule kijana niliyekusimulia asubuhi kuwa wanamuhamisha shule ndiye huyu yaani ana records chafu na mbaya sana shuleni kwangu.
Tena nikwambie tu kuwa yule msichana ambaye nusura amfunge mtoto wetu Sadick kwa kumsingizia eti alitaka kumbaka, Sasa hivi ana mtoto na baba wa mtoto ndiye huyu kijana,Wenyewe wamefichaficha lakini taarifa nimepata.
aliongea yule mwalimu mkuu akionesha chuki za wazi kwa Samson.

Mume wangu jambo lenyewe ni la Siri basi, mbona Kuna Binti anaitwa Catherine (Cathy)alikuwa anakunywa
Pombe hapa tangu saa nne asubuhi nilikuwa naye kaniambia mambo mengi tu kuwahusu hawa, kiufupi familia ya mzee Mgaya imekosa adabu sana tu, na mwenyewe anavyoonaga kayapatia maisha,
Na hata shoga yangu mwenyewe, yale maduka yake mawili tayari hujiona ni nani sijui lakini kifupi ni familia iliyokosa msimamo.

Mwalimu mkuu wa shule iliyo karibu na nyumbani kwa Mzee Mgaya aliinanga ile familia huku wakipokezana na mkewe na wakionesha hawajapendezwa na kitendo cha mama Kulwa kumtuma Samson mtu ambaye hawamwamini hata kidogo.

Kwahiyo huo mzigo naupata au niondoke, Samson aliuliza baada ya kuona wale wenyeji wake wanaendelea na shughuli nyingine.

Wewe nenda tu kamwambie nitaleta mwenyewe tena leo hii hii,
Yaani mpaka natetemeka , eti nikupe hii hela wewe ili uipoteze halafu nionekane sikukupa ili nilipe mara mbili eeh, ni kitu hakiwezekani,
aliongea kwa dharau yule mama na kumruhusu Samson aondoke.

***************************************

Ujue Samson umeingia hapa naona unafanya mambo yako tu hunipi majibu ya kule nilikokutuma vipi,
Kwanza mbona upo mbali mwenzetu huli Chakula leo, hebu kamuamushe na mzazi mwenzio huko, maana naye anadeeeeka sijui hata kitanda hakimchoshi! Lakini kwanza ya yote nipe mzigo wangu niliokutuma.
aliweka kituo mama Kulwa.

Ujue mama ndiyo maana unaona nakosa hata hamu ya kula, yaani mwalimu mkuu na mkewe wamenikatalia katakata kuwa hawawezi kunipa chochote eti hawaniamini, mara sitafikisha mara nini yaani kifupi sijawaelewa, na yule mama kaniambia atakuja mwenyewe atakuletea. Samson alifafanua Kisha akaenda kumuita Rahma na kurudi naye sebuleni.

Haya mama mwenye mtoto asiye na jina,nikisema mumpe jina langu hamtaki na vipi umekuwa boss humu ndani siyo, siku nyingine ujikaze mtoto wa kike bwanaa au kwakuwa Sarah yupo ndiyo unataka Chakula awe anakuletea chumbani kwako.
aliongea kiutani mama Kulwa lakini ujumbe ukifika.

Unajua Sarah wewe ni mgeni humu ndani kwakuwa huna siku nyingi sana, niseme tu kuwa huyu Samson licha ya mambo yake ya kipuuzi mengi aliyotufanyia lakini ni mtu mwenye nidhamu sana na pesa kwanza siyo mwizi, nimeshamtuma sehemu nyingi sana, lakini pia amekuwa akitumwa na baba yake kule saiti afuate pesa kiasi kikubwa Wala siyo vijisenti nilivyomtuma leo, Lakini anafikisha salama kabisa Sasa yule shoga yangu sijamuelewa?
mama Kulwa aliongea huku akiegama kwenye kiti akishindwa hata kula.

Mimi nadhani hajakosea sana, Kuna mawili aidha hana hiyo hela kaamua kuleta visingio tu, au ni kweli hamuamini Samson hasa ukizingatia wanamfahamu kama mtoto mkorofi hivyo inakuwa ngumu kumwamini.
Sarah aliongea naye kwa mtazamo wake.huku akiinuka na kwenda kumchukua mtoto wa Rahma chumbani.

Lakini geti lilisikika likigongwa kwa fujo na Kwa nguvu sana , Samson aliinuka na kwenda kufungua huku akimuuliza jina mgongaji kama ulivyo utaratibu wa watu wengi kabla ya kufungua.

Itaendelea............................

Weka Mzigo
 
SEHEMU YA TISINI NA MOJA

Mgongaji wa geti alikuwa ni Cathy,
aliingia huku akimwangalia Samson Kwa jicho baya na kubinua midomo ya dharau, kwakuwa Samson alijua haikumpa taabu badala yake alijiona ni wa thamani huku akijisifu kimoyomoyo kwa msimamo wake.

Enhee vipi mwanangu mbona usiku hivi kuna nini, nauliza hivi kwasababu si kawaida yako kuja mara mbili hapa na saizi inaelekea saa nne kasoro hii.
aliuliza kwa mshangao mama Kulwa.

Kwanza mama Mimi nina njaa sana kama kwenye poti Kuna chakula, ngoja nile kwanza halafu nitasema ujue Leo kutwa nzima nilikuwa hivi (akionesha ishara kuwa alilewa)
Sasa vitu vimepungua ninaisikia njaa vilivyo. aliongea Cathy huku akimzuia Sarah asipakue chakula.

Aisee shoga yangu wala usijisumbue Mimi hapa ni nyumbani na huyu hapa ni mama yangu mlezi tangu miaka hiyo, hivyo nikiwa na njaa huwa napika kabisa siyo tu kula , hapa ndiyo kwa mama Jose, au mama mkwe ingawaje mwanaye Jose alinikataa mchana kweupe lakini sikuwa na namna. aliongea Cathy na kufanya watu wacheke.

Mwanangu Jose angekuweza wapi na hizo pombe, yule tangu utotoni aliipiga vita pombe licha ya baba yake na Mimi kuwa ni watumiaji lakini hajamrithi yeyote haya niambie usiku huu una shida gani.

Kwanza mama nina furaha ya mambo mawili , la kwanza nimewasiliana na Mr anasema kumbe alipata na matatizo kidogo ndiyo maana nikawa simpati, kwa maana hiyo mambo yangu yatanyooka.

Lakini pia Jambo la pili ni kuhusu gari langu , mafundi wamehangaika nalo likakubali japo kiasi walichonitajia kwa kazi waliyofanya ni kikubwa(akitaja bei) lakini nashukuru gari limepona, kwahiyo hapa nadaiwa nusu ya hela nimelipa nusu ya hela nikawadanganya kuwa hela nyingine ipo nyumbani kwahiyo wameniachia gari kwakuwa wananijua vinginevyo nisingechukua na yule fundi mkuu navyomjua kesho saa kumi na mbili asubuhi atakuwa getini ana njaa kama nini yaani Sasa mama naomba niokoe maana Mr atarekebisha wiki hii hii.
alifafanua Cathy.

Sawa nimekuelewa lakini Mimi mwenyewe kwenye akiba yangu harakaharaka hivyo Sina ila Kuna kijipesa changu kwa mtu mmoja na nilimtuma Samson jioni hii lakini ameshindwa kumpa kwa visingizio vya kijinga kwahiyo na Mimi nikuahidi kuwa njoo asubuhi saa tatu na Mimi nitaenda kuchukua asubuhi. aliongea mama Kulwa Kwa sauti yenye usingizi ikionesha mida nayo imeenda.

Yaani mama sijui twende wote kwa huyo mtu, au labda nitakuja hapa asubuhi kwa lengo la kuwakimbia wale halafu wewe ukichukua utanikuta hapahapa maana sitaki wale mafundi nionane nao nikiwa Sina hela. aliongea Cathy kwa uoga akiona labda mama Kulwa anampa Imani tu.

Siku inayofuata mida ya asubuhi sana kama ambavyo ratiba za kazi zilivyo Kila mtu alikuwa bize na shughuli zake muda ule huku Rahma na mama Kulwa wakiwa vyumbani bado, labda kwasababu Rahma ni mgonjwa na mama Kulwa ni boss.

Geti liligongwa kufungua akaja yule mwanamke ambaye alimnyima hela Samson ile Jana yake, walisalimiana.

Wewe kijana hapa hata ndani siingii, naomba niitie mama yako maana nikiingia ndani tutaanza stori na hii asubuhi Nina mambo mengi ya kufanya. alisisitiza yule mama.

Mama Kulwa alitoka huku akijifunga kitenge chake vizuri na kuja usawa alipo mgeni wake,

Mwenzangu, Jana umetulaza na njaa maana nilimtuma kijana wangu ukamnyima mzigo bwana, na ilikuwa nije asubuhi hii afadhali umeniwahi.alitania mama Kulwa.

Weeee hapana kwa taarifa tunazosikia kuhusu kijana wako huyu hakuna anayeweza kumwamini kirahisi, tena Kuna taarifa zingine tumesikia jana tu kuwa humu Kuna watoto wanaishi kama wanandoa ni huyu mtoto na binti fulani yule kama mwarabu sijui mmanga, na tunaambiwa hilo jambo mmeridhia na mmebariki kabisa, tunajua huwa Kuna bahati mbaya nyingi sana kwa watu wengi kukuta madada wa kazi wanazalishwa na mashambaboy au watoto wa wenye nyumba na hata mababa wenyewe, lakini kamwe hakuna mama mwenye nyumba hata mmoja anaweza kufurahia haya masuala, lakini kwa taarifa nilizosikia
Jana mmmmh sidhani kama unapaswa kufurahia haya mambo. nimeamua kukwambia yasiyonihusu kwakuwa wewe ni mtu mzima mwenzangu, msiri, mstiri wangu na mzigo wetu ni huu hapa. yule mama alikabidhi kiasi fulani cha pesa kwa mama Kulwa huku akitaka afunguliwe geti atoke.

Hapanaaaa, hapana Sam mwanangu usifunge geti, halafuu unaona unavyonidhalilisha wewe mtoto, ama kweli ukubwa ni jalala kwa kukuonya na kukukanya kote, leo hii naonekana nafurahia mambo yako uliyoyafanya mwanangu, loooh haya yote nitamlaumu Mzee Mgaya ndiye aliyenidhalilisha kwa kukuleta wewe lakini yote haya nasamehe na kuwasamehe wote wewe na Rahma.

Enhee na wewe mwenzangu hizi taarifa ni nani kamwambia kuwa Mimi Nina akili za kuweza kufurahia ujinga na upumbavu uliotokea humu ndani,? Mama Kulwa aliuliza kishari kiasi cha kumtisha yule mama mgeni ama mke wa mwalimu mkuu.

Mmmh dada yangu Mimi utanionea bure jambo zuri ni kwamba mambo haya nimeyasikia Jana toka kwa msichana fulani huwa nakuona naye mara nyingi anaitwa Catherine, na hajaniambia Mimi tu kulikuwa na watu wengi, hivyo Mimi usinichukie Mimi ni kama mjumbe tu. alijitetea yule mama baada ya kuona mama Kulwa anapaniki.

Wakati Sarah akijaribu kumuelewesha mama Kulwa kuwa asimchukie yule mama ambaye kwanza kwa kuongea ule ukweli ni jambo jema na kizuri zaidi muhusika katajwa kuwa ni Cathy, ilisikika honi ya gari nje, kufungua geti alikuwa ni Cathy akiwa anashuka kwenye gari kwa mbwembwe na kuingia ndani,
Cathy alionesha kushangaa uwepo wa mama ambaye ni mmiliki wa grocery ambako Jana yake alikuwa katoka kulewa hapo, sura yake ilibadilika huku akiwasalimia akina mama wale Kwa upole kwani alishagundua jambo.

Samson funga geti na jamani wote nawaombeni basi tukaribie ndani maana Kuna stori sizielewi vizuri.
Mama Kulwa aliwakaribisha wageni wake ndani.

Mdaiwa ambaye analipa deni aliingia ndani huku akilalamika kuwa anachelewa kazi zake.

Lakini pia mkopaji Cathy ambaye aliahidiwa kuwa atatimiziwa asubuhi suala lake, alionesha yupo kwenye wakati mgumu kwani alinywea ghafla.

Lakini pia Samson alijikuta anapoteza furaha ghafla kwani yale mambo kila yakiibuka basi mishale mikali kutoka kwa mama Kulwa ilimchoma yeye kwani ndiye aliyekuwa msababishaji.

Pia hata Binti mrembo na mzazi kwa kipindi hicho huku akizaa mapema kutokana na kuwa na Presha ile ya kusemwa mara kwa mara na mama Kulwa, huku afya yake ikiporomoka siku hadi siku kwani mdomo wa mama Kulwa ulimnyima raha, naye alitoka chumbani kwake taratibu huku akitambua mishale na mawe yote watatupiwa yeye na Samson, kuliko hata wale wambeya na wasengenyaji.

Itaendelea,kuifuatilia...........................
 
SEHEMU YA TISINI NA MOJA

Mgongaji wa geti alikuwa ni Cathy,
aliingia huku akimwangalia Samson Kwa jicho baya na kubinua midomo ya dharau, kwakuwa Samson alijua haikumpa taabu badala yake alijiona ni wa thamani huku akijisifu kimoyomoyo kwa msimamo wake.

Enhee vipi mwanangu mbona usiku hivi kuna nini, nauliza hivi kwasababu si kawaida yako kuja mara mbili hapa na saizi inaelekea saa nne kasoro hii.
aliuliza kwa mshangao mama Kulwa.

Kwanza mama Mimi nina njaa sana kama kwenye poti Kuna chakula, ngoja nile kwanza halafu nitasema ujue Leo kutwa nzima nilikuwa hivi (akionesha ishara kuwa alilewa)
Sasa vitu vimepungua ninaisikia njaa vilivyo. aliongea Cathy huku akimzuia Sarah asipakue chakula.

Aisee shoga yangu wala usijisumbue Mimi hapa ni nyumbani na huyu hapa ni mama yangu mlezi tangu miaka hiyo, hivyo nikiwa na njaa huwa napika kabisa siyo tu kula , hapa ndiyo kwa mama Jose, au mama mkwe ingawaje mwanaye Jose alinikataa mchana kweupe lakini sikuwa na namna. aliongea Cathy na kufanya watu wacheke.

Mwanangu Jose angekuweza wapi na hizo pombe, yule tangu utotoni aliipiga vita pombe licha ya baba yake na Mimi kuwa ni watumiaji lakini hajamrithi yeyote haya niambie usiku huu una shida gani.

Kwanza mama nina furaha ya mambo mawili , la kwanza nimewasiliana na Mr anasema kumbe alipata na matatizo kidogo ndiyo maana nikawa simpati, kwa maana hiyo mambo yangu yatanyooka.

Lakini pia Jambo la pili ni kuhusu gari langu , mafundi wamehangaika nalo likakubali japo kiasi walichonitajia kwa kazi waliyofanya ni kikubwa(akitaja bei) lakini nashukuru gari limepona, kwahiyo hapa nadaiwa nusu ya hela nimelipa nusu ya hela nikawadanganya kuwa hela nyingine ipo nyumbani kwahiyo wameniachia gari kwakuwa wananijua vinginevyo nisingechukua na yule fundi mkuu navyomjua kesho saa kumi na mbili asubuhi atakuwa getini ana njaa kama nini yaani Sasa mama naomba niokoe maana Mr atarekebisha wiki hii hii.
alifafanua Cathy.

Sawa nimekuelewa lakini Mimi mwenyewe kwenye akiba yangu harakaharaka hivyo Sina ila Kuna kijipesa changu kwa mtu mmoja na nilimtuma Samson jioni hii lakini ameshindwa kumpa kwa visingizio vya kijinga kwahiyo na Mimi nikuahidi kuwa njoo asubuhi saa tatu na Mimi nitaenda kuchukua asubuhi. aliongea mama Kulwa Kwa sauti yenye usingizi ikionesha mida nayo imeenda.

Yaani mama sijui twende wote kwa huyo mtu, au labda nitakuja hapa asubuhi kwa lengo la kuwakimbia wale halafu wewe ukichukua utanikuta hapahapa maana sitaki wale mafundi nionane nao nikiwa Sina hela. aliongea Cathy kwa uoga akiona labda mama Kulwa anampa Imani tu.

Siku inayofuata mida ya asubuhi sana kama ambavyo ratiba za kazi zilivyo Kila mtu alikuwa bize na shughuli zake muda ule huku Rahma na mama Kulwa wakiwa vyumbani bado, labda kwasababu Rahma ni mgonjwa na mama Kulwa ni boss.

Geti liligongwa kufungua akaja yule mwanamke ambaye alimnyima hela Samson ile Jana yake, walisalimiana.

Wewe kijana hapa hata ndani siingii, naomba niitie mama yako maana nikiingia ndani tutaanza stori na hii asubuhi Nina mambo mengi ya kufanya. alisisitiza yule mama.

Mama Kulwa alitoka huku akijifunga kitenge chake vizuri na kuja usawa alipo mgeni wake,

Mwenzangu, Jana umetulaza na njaa maana nilimtuma kijana wangu ukamnyima mzigo bwana, na ilikuwa nije asubuhi hii afadhali umeniwahi.alitania mama Kulwa.

Weeee hapana kwa taarifa tunazosikia kuhusu kijana wako huyu hakuna anayeweza kumwamini kirahisi, tena Kuna taarifa zingine tumesikia jana tu kuwa humu Kuna watoto wanaishi kama wanandoa ni huyu mtoto na binti fulani yule kama mwarabu sijui mmanga, na tunaambiwa hilo jambo mmeridhia na mmebariki kabisa, tunajua huwa Kuna bahati mbaya nyingi sana kwa watu wengi kukuta madada wa kazi wanazalishwa na mashambaboy au watoto wa wenye nyumba na hata mababa wenyewe, lakini kamwe hakuna mama mwenye nyumba hata mmoja anaweza kufurahia haya masuala, lakini kwa taarifa nilizosikia
Jana mmmmh sidhani kama unapaswa kufurahia haya mambo. nimeamua kukwambia yasiyonihusu kwakuwa wewe ni mtu mzima mwenzangu, msiri, mstiri wangu na mzigo wetu ni huu hapa. yule mama alikabidhi kiasi fulani cha pesa kwa mama Kulwa huku akitaka afunguliwe geti atoke.

Hapanaaaa, hapana Sam mwanangu usifunge geti, halafuu unaona unavyonidhalilisha wewe mtoto, ama kweli ukubwa ni jalala kwa kukuonya na kukukanya kote, leo hii naonekana nafurahia mambo yako uliyoyafanya mwanangu, loooh haya yote nitamlaumu Mzee Mgaya ndiye aliyenidhalilisha kwa kukuleta wewe lakini yote haya nasamehe na kuwasamehe wote wewe na Rahma.

Enhee na wewe mwenzangu hizi taarifa ni nani kamwambia kuwa Mimi Nina akili za kuweza kufurahia ujinga na upumbavu uliotokea humu ndani,? Mama Kulwa aliuliza kishari kiasi cha kumtisha yule mama mgeni ama mke wa mwalimu mkuu.

Mmmh dada yangu Mimi utanionea bure jambo zuri ni kwamba mambo haya nimeyasikia Jana toka kwa msichana fulani huwa nakuona naye mara nyingi anaitwa Catherine, na hajaniambia Mimi tu kulikuwa na watu wengi, hivyo Mimi usinichukie Mimi ni kama mjumbe tu. alijitetea yule mama baada ya kuona mama Kulwa anapaniki.

Wakati Sarah akijaribu kumuelewesha mama Kulwa kuwa asimchukie yule mama ambaye kwanza kwa kuongea ule ukweli ni jambo jema na kizuri zaidi muhusika katajwa kuwa ni Cathy, ilisikika honi ya gari nje, kufungua geti alikuwa ni Cathy akiwa anashuka kwenye gari kwa mbwembwe na kuingia ndani,
Cathy alionesha kushangaa uwepo wa mama ambaye ni mmiliki wa grocery ambako Jana yake alikuwa katoka kulewa hapo, sura yake ilibadilika huku akiwasalimia akina mama wale Kwa upole kwani alishagundua jambo.

Samson funga geti na jamani wote nawaombeni basi tukaribie ndani maana Kuna stori sizielewi vizuri.
Mama Kulwa aliwakaribisha wageni wake ndani.

Mdaiwa ambaye analipa deni aliingia ndani huku akilalamika kuwa anachelewa kazi zake.

Lakini pia mkopaji Cathy ambaye aliahidiwa kuwa atatimiziwa asubuhi suala lake, alionesha yupo kwenye wakati mgumu kwani alinywea ghafla.

Lakini pia Samson alijikuta anapoteza furaha ghafla kwani yale mambo kila yakiibuka basi mishale mikali kutoka kwa mama Kulwa ilimchoma yeye kwani ndiye aliyekuwa msababishaji.

Pia hata Binti mrembo na mzazi kwa kipindi hicho huku akizaa mapema kutokana na kuwa na Presha ile ya kusemwa mara kwa mara na mama Kulwa, huku afya yake ikiporomoka siku hadi siku kwani mdomo wa mama Kulwa ulimnyima raha, naye alitoka chumbani kwake taratibu huku akitambua mishale na mawe yote watatupiwa yeye na Samson, kuliko hata wale wambeya na wasengenyaji.

Itaendelea,kuifuatilia...........................
Mama Kulwa ana mdomo jamani lol!
 
Inachelewa hadi tunaisahau tulipo ishia
😂😂😂 Mbona Jack Daniel alishasema akiwa yupo ofisini ndio huwa anapata muda wa kuandika. Halafu huyu ni Engineer wa mabarabara inawezekana yupo site anajenga daraja la Kigongo Busisi
 
SEHEMU YA TISINI NA MBILI

Watu wote haswa wale wageni wote walionekana wenye hofu sana, huku yule mama akiwa anaongea peke yake mambo ambayo hayakusikika vizuri, lakini muda wote alilaumu kuwa anachelewa.

Ujue dada yangu wala huchelewi popote nadhani ni vyema tukaliweka hili suala sawa kusudi Kila mmoja awe na amani, kwahiyo wewe ukidai hivyo unachelewa, nashindwa kukuelewa.
Mmenisimanga vizuuuri kabisa jana, mkanigeuza geuza kama nyama kwenye kikaango, huku mkinitwisha mabalaa ambayo hata nyinyi mnajua kuwa siwezi kuruhusu ila tu mkaamua kunionea.mama Kulwa aliongea kwa uchungu

{Kisha akamgeukia Cathy)
Wewe wala sikushangai sana una vinasaba vya unafiki tangu miaka mingi sana, lakini kipindi kile nilikuwa nakuchukulia bado mtoto, umesoma na Glory wewe, lakini ukawa unamponza mwenzio Kila siku , mara oooh kafanyaje, mara wewe ndiye mwenye akili kuliko yeye, mara kakufanyaje, huku wewe ukijinasibu kuwa ndiye mwenye tabia nzuri kuliko mwenzako, haya wewe uliyekuwa mwenye nidhamu, akili na msikivu shuleni kwenu uko wapi na mwenzio yuko wapi? mama Kulwa aliuliza kwa sauti ya chini yenye hasira huku macho yake yakibadilika.

Sanasana bwana wako ndiye anayekuweka mjini, huna tofauti na mnyama anayefugwa, nafahamu kuwa unapenda sana kuonekana mtoto wa mjini kutokana na kusaidia wengi lakini juu ya ujanja wako, mbona biashara zako haziendi kila unachofanya kinakwama na yote ni kutokana na wewe kupenda starehe na mteremko. Ni laana inakutafuna kutembea na mwanaume sawa na baba yako,na huyo bwana wako unayemtegemea unajua fika ana familia yake vipi siku akiamua kubase zaidi kwenye familia yake, vipi utaishije?
Si tu kurudi kwenye familia yake, Bali tunajua anafanya biashara haramu huko kwenye nchi za watu yaani ni MUNGU tu anamsaidia, mbona sisi tunakaa kimya hatuongei , muda na saa yeyote yule atakuwa nyuma ya nondo na ndipo anguko lako litakapo kukuta wewe mtoto, kila siku nakwambia hiki ni kipindi ambacho Ukiwa naye huyo bwana wako unatakiwa utumie nafasi vizuri ili siku mambo yakiwa mrama, usihangaike sana wewe huelewi. Mama Kulwa alizidi kumwaga mambo hadharani.

Leo hii wewe hukupaswa kuniomba hela ndogo kama hiyo eti ukaikomboe gari, unachezea hela hapa kumbe hata akiba huweki mwanangu, Sasa nikwambie kuwa sihitaji mazoea Tena na wewe na hii ni mara ya kwanza na ya mwisho kukanyaga ndani mwangu.
Mama Kulwa aliweka kituo huku Cathy akipiga magoti mbele ya mama Kulwa akiomba msamaha hakuwa na namna nyingine.

Mama Kulwa alikuwa nyumbani kwake, pia ni mtu mwenye mdomo Cathy hakuweza kujibu chochote kwani kwa kujibu au kutafuta ligi kwa mama Kulwa ilikuwa ni kusababisha akaanika mambo yake mengi hadharani,.

Samson alisikia honi nje, akakimbia kwenda kufungua geti, alikuwa ni Mzee Mgaya ambapo walisalimiana Kisha wakaingia ndani, Mzee Mgaya alishtuka na kushangaa mtu kuwa amepiga magoti huku akilia akagundua hakuna amani mahali pale.

Jamani kuna usalama kweli hapa mbona wengine wanalia shemeji yangu hapa kashika Tama vipi ndugu zanguni eeh,mke wangu vipi Kuna jambo gani. aliuliza kwa pupa Mzee Mgaya.

Ni mambo ya kawaida tu Mume wangu, Kuna mambo tunayaweka sawa, alijibu mama Kulwa.

Ya kweli haya shemeji maana mmenitisha sana jamani. Mzee Mgaya alimuuliza yule mke wa mwalimu mkuu aliyekuwa kimya akisikiliza Cathy anavyochambuliwa na mama Kulwa.

Shemeji kama alivyokwambia mkeo ni hivyo hivyo Kuna mambo tunayaweka sawa si unajua tena binadamu, hatuwezi kuishi kwenye mstari mnyoofu muda wote lazima ipo siku mtakwazana, na jambo zuri ni kuyaweka mambo sawa ili maisha yaendelee. alijibu yule mama mgeni.

Mzee Mgaya aliwaangalia wote kwa zamu,huku Cathy akimshangaza kwanini apige magoti?
kisha akaingia ndani chumbani kwake baada ya muda fulani akatoka na kumuashiria Samson amfuate nakuingia naye kwenye gari.

Kuna gari fulani la mbao limeingia kule saiti, nadhani mwaka unaokuja
Nitauanza vizuri sana MUNGU akipenda, unajua mwanangu nimekosa kazi kibao kisa sikuwa na materials Kuna zahanati inajengwa nje ya huu mji ndani ndani huko, nimeikosa tenda ile kisa sikuwa na mbao, mwisho wa siku kapewa mtu mwingine aliyekuwa tayari, Sasa leo mzigo zaidi ya Cubic metre sitini utashuka kwenye yard yangu, yaani Nina furaha sana nadhani hata nikinywa pombe itashuka vizuri. aliweka kituo mzee Mgaya huku akionekana mwenye furaha sana.

Enhee hebu niambie Nini kimetokea pale maana mama yako naye hata simuelewi kukaribisha shetani tu ndani mwangu. aliuliza Mzee Mgaya

Samson alieleza Kila kitu namna alivyotumwa Jana yake afuate mzigo akanyimwa pia mishe zote za Cathy mpaka wanakamatana umbeya asubuhi ile.

Mzee Mgaya alicheka sana, tena sana huku akishindwa hata kucontrol gari vizuri,
Mwanangu Kuna mambo ya ajabu sana lakini yote kwa yote mama yako ni mke wangu tena ni msomi wa kiasi chake lakini Kila mtu ana madhaifu yake, Kuna mambo ukisikia yanatia kinyaa , yule mke wa mwalimu mkuu ni mama tu wa nyumbani, yaani ni mama fulani wa kiswahili ambaye hufanya biashara ndogondogo ili kujiweka bize ni watu nawafahamu tangu miaka mingi.

Na yule mtoto mdogo Cathy, ni mtu wa kupuuzwa tu, Mimi nilitegemea mama yako ayapuuze haya mambo kwani hayana faida yeyote , kusemwa Nini watu tunasemwa Kila inapoitwa leo, lakini tunanyamaza tu kwani ukigundua jambo husika halina madhara halikusumbui. mzee Mgaya aliingalia saa yake ya mkononi huku akitabasamu na kutikisa kichwa.

Asubuhi hii watu badala ya kufanya kazi, badala ya kuangalia mambo yanaendaje wao wanaweka vikao visivyokuwa na msingi, hii inaumiza na kusikitisha sana. Kisha Mzee Mgaya akamgeukia Samson huku akikunja ndita zake .

Halafu na wewe hebu jitofautishe basi, wewe ni mwanaume, kwenye Mila za kabila la kwetu mwanaume anahitaji heshima, na anapaswa kujitambua na kulinda misimamo yake, Sasa nakuonya iwe mwanzo na mwisho kusikiliza habari za wanawake, mambo ya kijinga na ya kipumbavu kama yale mwanaume hupaswi kukaa na kusikiliza , hata ukiona wanataka kukushirikisha, wewe toka ingia hata mtaani fanya mambo mengine, acha kukaa ukisikiliza mambo ya kike utaathirika na kujikuta unakuwa mtu mwenye kupenda umbeya jambo ambalo ni hatari kwa mtoto wa kiume.madhara wewe huwezi kuyaona Bali wanaokuzunguka na pale utakapoanza kudharaulika ndipo utakapojuta na kukubali maneno yangu, mtu nafika pale nikajua labda Kuna msiba au ajali kumbe mambo ya kijinga.

Yule mama yako sitamwambia kuwa labda aache mambo yake hapana, mke wangu Mimi namjua naweza kumtibua akanikasirikia wiki nzima ndiyo maana mara nyingi hata akianzisha ugomvi huwa sijibu sana sana nanyamaza tu siyo kwamba ananimudu Bali sioni faida ya kugombana naye hasa ukizingatia sisi ni watu wazima japo hili la Leo sitalifumbia macho kwasababu Kila siku ananilalamikia kuwa huko dukani kwake wanamuibia, sasa wasimuibie vipi mtu yupo tu huku nyumbani akisutana na watu ambao hata hawafanani na yeye.mzee Mgaya aliweka kituo Kisha akaongeza speed ya gari kuwahi sehemu husika.

Maneno ya Mzee Mgaya yalimuingia vizuri sana Samson, hata yeye alianza kuona aibu fulani hasa akikumbuka nyumba nzima imetawaliwa na wanawake huku ME akiwa ni yeye tu, je ikiwa wangeanza kupigana huku nguo zikiwavuka pengine ilikuwa aibu na akijiona kama anatukanwa. akajikuta anamkubali Mzee Mgaya kwa ushauri wake wa bure kwani hakuweza kukumbuka kabla.

Walifika saiti huku Samson akishangaa kumuona Tausi akiwa kule asijue kafika saa ngapi , Mzee Mgaya alishuka fasta na kwenda mahali gari linaposhusha mzigo maana ndiyo jambo lilimtia hamu kwa muda huo,huku Tausi akija mahali alipo Samson na baada ya kugonganisha macho yao Kila mmoja alitabasamu.

Shikamoo mamdogo,
Samson aliamkia kinafiki.

Mmmmh acha zako na wewe, hebu kwanza shuka kwenye gari boss kashuka wewe upo umeng'ang'ania kama vile wewe ndiye boss,
Enhee niambie naona umezidi kuwa handsome maana hata zile chunusi zimepotea kabisa yaani unavutiaaaa. alitania Tausi huku akimwangalia Sam kimahaba.

Likizo inipende wapi, Bora hata ningekuwa shule maana kazi za pale hata huwa haziishi yaani, asubuhi mpaka jioni mtu hupumziki, ukipumzika jua kuwa mama Kulwa hayupo. aliongea Samson Kisha wakagonga mikono na kucheka.

Wakati huo Mzee Mgaya akifurahi na mzigo wake tu unaoshuka kwenye magari maana huenda kwa mujibu wa hesabu zake alikuwa anaenda kutengeneza pesa nyingi hivyo hakuona kinachoendelea Kati ya Tausi na Samson.

Vipi Rahma naye hajambo na mtoto wake, nimemiss natamani hata aje akae hata siku mbili lakini mama Kulwa hatakubali yaani kamfanya Rahma kama mwanaye wa kumzaa loh yule dada. alisikitika Tausi huku wakielekea mahali alipo Mzee Mgaya.

Vipi mama Kulwa alimalizaje mambo yake na Cathy? Vipi kuhusu Samson na Tausi Nini kiliendelea

Itaendelea................ ...............
 
SEHEMU YA TISINI NA TATU

Mimi natakiwa niende mjini ili tukafanye mahesabu na hawa walioniletea mzigo, hivyo nawapeleka nyumbani Kisha nakuja kuwachukua wageni wangu, halafu kwani na Samson unaenda Temeke Mimi nafikiria ningekupa tu nauli ushike njia ya kwenda kwenu.
alishauri Mzee Mgaya.

Twende tu nyumbani my maana wote tuna njaa, au Samson hapaswi kula kwangu mnanitenga jamani siku zote nakaa mpweke Sina hata mtu wa kuongea naye. aliongea Tausi lakini Mzee Mgaya hakujibu chochote.

Baada ya muda fulani wakafika nyumbani kwa Tausi huku Samson akigundua ile nyumba imefanyiwa marekebisho kwani ilionekana imepandishwa kuta huku ikiwekwa bati jipya na paa la kisasa hakika ilivutia sana.

Mmmmh mamdogo hongereni sana nyumba imependeza sana yaani, Tena mkiongeza na urefu wa hii fence hakika itapendeza zaidi. Aliisifia ile nyumba Samson

Ndiyo tunaelekea hukohuko sema pesa yenyewe ni ya kuungaunga maana si unajua tena sisi siyo kama watu wenye pesa zao. alijibu Tausi

Sema nini Samson siyo tena ukaropoke kwa mama Kulwa, oooh nimeona nyumba mara nini kimebadilika, ya hapa acha hapa hapa Mimi mke wangu yule namjua mwenyewe kitu kizuri awe nacho yeye tu. alitahadharisha Mzee Mgaya.

Karibuni ndani basi au ndiyo mmegeuka mafundi maana naona mnaikagua sana hii nyumba, hebu ingieni ndani basi tuandae chakula, alikaribisha Tausi.
Mzee Mgaya yeye alidai haingii ndani kwani anawahi kwenda mjini kwaajili ya kukamilisha taratibu zake za biashara

Tausi aliandaa Chakula Kisha wakaanza kula huku Samson akisifia mandhari ya mule ndani namna kulivyopendeza tofauti na mwanzo,

Siyo nyumba tu iliyopendeza hata wewe mamdogo umependeza sana kwani umenenepa lakini pia umezidi kung'aa jamani, Yaani mtu akikuangalia haraka haraka anaweza sema una miaka 25.alitania Samson

Weweee punguza uongo, sura ya mtu mzima inajulikana tu hata iweje,umri na namba huwa hazidanganyi , hata hivyo ahsante sana Kwa kuniambia hivyo si wewe tu wengi wanasema nimenawiri hata Mzee Mgaya aliniambia hivyo, japo na wewe khaah sura yako kama mwanamke na ulivyokosa hata ndevu za kuzugia ndiyo kabisaa.

Waliendelea kupiga stori huku wakitaniana lakini mwisho wa siku walibaki wakiangaliana tu hakuna aliyemsemesha mwenzake, kila walipogonganisha macho yao Kila mmoja alitabasamu, shetani mharibifu ambaye lawama zote hutupiwa yeye pindi watu wakifanya mabaya, alikuwa karibu mno huku Tausi akiinuka na kwenda kuhakikisha geti la nyumba yake kama limefungwa vizuri ili pindi yeyote akifika pale basi afuate utaratibu wa kugonga.

Baba nani vile unaitwa , maana hakuna namna wewe ni baba mtu japo ulifanya jambo baya sana kutuchanganya watu wawili Tena mtu na mwanaye ni kitendo kibaya sana ulifanya, leo hii nashindwa hata kumuita mtoto wa Rahma mjukuu au mwanangu, japo mjukuu ndiyo jina linalokuja vizuri. aliweka kituo Tausi.

Hivi mbona historia ya Rahma inaonesha hana undugu na familia yenu badala yake ninyi ni watu ambao mlitoa msaada tu kwa kipindi hicho Sasa sioni sababu ya kusema Mimi nimekuchanganya na mwanao Rahma. Ila siyo kesi Mimi nachukulia Rahma kama mwanao na nipo hapa kwaajili ya kukuomba msamaha na nastahili adhabu kutoka kwako. aliongea kwa kujiamini Samson.

Yaani wewe, mmmmh hata sijui upoje, unataka nikupe adhabu gani? aliuliza Tausi akiwa kalegeza macho na sauti yenye mkwaruzo,

Yeyote, unayoona inafaa mkosaji hachagui adhabu, Bali hufanya kile anachoamrishwa, Samson aliongea huku akimsogelea Tausi na kumshika kifuani, huku Tausi akijaribu kuutoa mkono wa Samson lakini alishachelewa kwani kama ni gari la Tausi wakati huo mifumo ya breki iliharibika , hivyo ni option mbili aidha aingie mtaroni apate ajali au anyooshe kujaribu kunusuru uhai wake.

Samson nini si ukakae kule bwaaana, Mume wangu atakuja bwanaaaa usifanye hivyo Mimi sitaki, hujui Mimi ni mama yako, alilalamika Tausi , lakini kufumba na kufumbua tayari Samson alimaliza kazi pale pale sebuleni, huku Tausi akiinuka na kukimbilia bafuni, na Samson akiinuka na kwenda kufungua geti huyo kwenye kituo cha daladala za kuelekea kwao.

***************************************

Wewe ulikuwa wapi muda wote maana muda ule nakuita weeee Hadi nilipoambiwa na Sarah kuwa umeondoka na baba yako, umesahau nilikwambia ufanya kazi gani mbona unapenda kunidharau wewe mtoto? mama Kulwa aliongea huku akishika sikio la Samson na kulivuta,.

Tulienda saiti na mzee sasa Mimi ningemkatalia, basi naomba unisamehe mama, alijitetea Samson.

Wewe kule Karakana ukafanye kazi gani, siku zote huwa tunaenda kule uliwahi kufanya kazi yeyote, halafu Mzee Mgaya naye anatoka huko hata haulizi anamzoazoa huyu wanaondoka hajui hata nilitaka kumtuma nini, hebu na wewe jifunze kuuliza ukiona anakuita siku nyingine, Anza kuniaga Mimi kwanza ili kama Kuna kazi za kufanya nikuzuie na kama hazipo basi nakuruhusu, wewe unashindwa nini, yaani una kichwa Kizito wewe sijui hata huko shuleni kama utamudu na usidhani shule unayoenda Sasa hivi ni ya mchezo mchezo kule wanafunzi na walimu wapo bize shauri yako. mama Kulwa aliongea huku akionesha anatoka.

Shoga yangu Sarah utamuelekeza huyu mpumbavu kazi ile amalizie Mimi naenda mjini mara Moja narudi siyo muda. mama Kulwa akaondoka

Unajua nini Samson ugomvi wa marafiki usiuingilie huwezi amini Cathy sijui nani mnamuita aliomba msamaha wakayamaliza na mama Kisha wakamgeuka yule mama mke wa mwalimu mkuu wamemsimanga na kumtukana vizuri, Kisha wao wakaendelea na kushauriana mambo yao hata chai ya asubuhi Cathy tumejumuika naye wote Kisha wakaongea mambo mengi sana na hapa mama Kulwa haendi dukani kwake anaenda mtaa fulani lilipo duka la Cathy kwani mama anadai atamkopesha pesa ili afufue duka lake aache kumtegemea mwanaume, yaani Sam wewe acha tu huwezi amini wamepatana. aliongea Sarah huku akionesha kushangaa namna hasira za mama Kulwa zilivyoyeyuka kama mshumaa.

Samson alisikiliza maneno yale huku akitamani angekuwepo ajionee mwenyewe kwani kwa kusimuliwa alihisi hapati ladha ambayo angeipata kwa kujionea mwenyewe.

Vipi Rahma yuko wapi mbona simuoni. aliuliza Samson

Ewaaaah nilikuwa nakuja huko huko , Rahma bwana yupo ndani analia, eti kisa jina la mwanaye, si mama bwana kampa jina lake huyu mtoto,
Iko hivi baada ya kumaliza ugomvi na Cathy mama Kulwa alimchukua mtoto na kukaa naye nje Kisha akamuita Rahma na kumuuliza ni lini mtoto atapatiwa jina?
Rahma hakuwa na majibu.

Ndipo mama kulwa akadai kuwa alikuwa na jina la utotoni, kabla ya lile alilosomea shuleni ambalo liko kwenye vyeti vyake hivyo akadai lile jina la zamani anampa mtoto wako, hivyo kuanzia leo ataitwa Jackline.kwani lilikuwa ni jina lake la mwanzo na pia anastahili kutoa jina yeye kwani ndiye mlezi kwa kipindi hiki.alifafanua Sarah.

Sasa mama naye anapendekezaje jina wakati wahusika hatupo?
aliuliza Samson.

Mwenye kadai Hilo ndiyo jina atakaloitwa mtoto, hivyo kuanzia leo ataitwa Jack, Sarah aliongea huku akicheka kwani vituko vya ile nyumba vilimshangaza .

Sasa yeye Rahma kwanini analia kaona jina siyo zuri au ni nini?
aliuliza Samson.

Hapana tulimuuliza Mimi na mama Kulwa akadai ni jina zuri ila hajatupa sababu ya kulikataa japo tumegundua udini ndiyo unamsumbua , alifafanua Sarah huku Samson akiwa kazubaa tu hajui afanyaje, akijua Hana uwezo wa kuja kumbishia mama Kulwa hata akirudi.

Itaendelea.....................................
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom