SEHEMU YA THEMANINI NA NNE
Likizo ya Samson ilikuwa na mambo mengi, Kwanza ilikuwa ndicho kipindi cha yeye kubadili tabia kama ambavyo wazazi wake waitaka,lakini yeye alikuwa mmoja wa watu wasahaulifu na wasiokuwa na upembuzi wa mambo. Sasa endelea........
Jumamosi moja kama ilivyokuwa kawaida kwa mzee Mgaya kutembelea miradi yake, asubuhi na mapema Samson aliamka ili asaidie kazi za pale ndani kisha waondoke na mzee Mgaya,
Unajua dada kukaa humu ndani pasipo kufahamiana majina wala si sawa,kwa mara nyingine ningeomba nikufahamu, si kwa ubaya dada na pia samahani kama nitakuwa nakukosea. alijiongelesha Samson
Weeee mtotooooo dah umenishinda tabia, naitwa Sarah , japo sikupenda ujue jina langu ila ndiyo hivyo, na nikupe angalizo , sitaki uniite Dada Wala Sarah niite aunty inatosha kwani mwenzio Rahma si ananiita hivyo? lakini wewe umeona huridhiki hadi ujue jina langu. haya naomba nisaidie kupeleka hivi vitu kwenye meza ya chakula. aliongea Kwa sauti ya ukali kidogo yule aunt akionesha hajapenda usumbufu wa Samson.
Baada ya kupata breakfast watu wote waliagana huku kila mmoja akielekea kwenye mihangaiko yake, mama Kulwa kipindi kile hakuwa akikaa nyumbani kwasababu kwanza alimpata msimamizi wa kazi ambaye ni mtu mzima hivyo Kila kitu kilikaa sawa kabisa na kumfanya awe huru kufanya mambo mengi.
Mzee Mgaya na Samson wao walielekea pembeni ya mji zilipo Karakana
**************************************
Mzee Mgaya alibaini hasara fulani pale Karakana ikabidi aitishe kikao cha dharula, huku akiwa mkali kwa kulikuwa na upotevu wa kiasi kikubwa cha pesa kwa mujibu wa hesabu zake, mhasibu wake licha ya kujaribu kukataa lakini bado Mzee Mgaya alidai pesa zake zipatikane.
Mimi Kwa umri huu sidhani kama napaswa kupigizana kelele na nyinyi tena, na niseme tu ukweli hii Karakana ni kama ipo kwaajili yenu Mimi Sina njaa ya kutegemea hapa Sasa kuanzia leo Mimi nasitisha kazi hapa hadi pale ambapo pesa zangu nitazipata , najua Nina kazi na oda za watu wengi lakini nipo tayari kuwarudishia pesa zao, na Mimi nikaendelea na habari zangu si lazima nihangaike na mambo ya mbao.mimi nilianzisha mradi huu ili utusaidie wote Mimi na nyinyi Sasa kama tunaibiana mimi nawezaje kuendesha project isiyo na faida.aliweka kituo mzee Mgaya.
Kwanza nikushukuru Mzee mwenzangu kwa kututembelea na niseme tu kuwa upo sahihi kwa madai yako, lakini tunakuomba sana boss wetu usifunge kiwanda chako hii ni sehemu ambayo vijana wote wanapata riziki zao hivyo Kwa kufanya hivyo ikiwa watu hawana kazi wala namna nyingine, itaweza kuathiri maisha yetu, pendekezo letu ni kwamba ungedili na mtunza hazina wako tu huku sisi wengine tukiendelea na kazi. alisema mmoja wa mafundi wa mzee Mgaya huku akishangiliwa na vijana wote kwa kauli yake kuwa angeshughulika na yule anayemtunzia pesa zake.
Kwanza hiki siyo kiwanda ni SIDO,hivyo ukidhulumu kiasi kidogo tu tayari Karakana inakufa hii na ifahamike kuwa wote tunaganga njaa tu, nawategemeeni
Ninyi kuweza kusonga mbele bila nyinyi sifiki kokote nitazidi kufilisika na hatimaye wote tukakosa sehemu za kufanya kazi , Kuna takribani vijana ishirini na tano hapa, hamko wengi sana ila tambueni kuwa mkikosa kufanya kazi hapa mtahangaika Hadi kufikia kupata kibarua sehemu nyingine tayari mmehangaika sana hivyo heshimuni kazi. Mzee Mgaya aliwashauri vijana wake.
Baadaye alitoka huku akiacha maagizo kwa muhasibu wake kuwa ahakikishe anaweka hesabu sawa Kisha aje nyumbani kwake baadaye.
Wakiwa kwenye gari Mzee Mgaya alimuongelesha Samson,
Mwanangu sitoacha kuku kumbusha na kukweleza ukweli, bila shaka umewaona baadhi ya watoto pale kwenye Karakana yetu, wengine ni umri wako kabisa. Na huwa unaona namna kazi zinavyoendeshwa huku wale watoto muda mwingine wakielemewa, Sasa si kwamba wale ni wazembe kwa kushindwa kusoma, Bali ni familia nyingi kukosa uwezo wa kuwaendeleza watoto wao, na matokeo yake kuangukia kwenye utumwa wa vibarua.
Lakini wapo waliochezea shule wenyewe, si lazima wawe kwangu pale hapa nazungumzia sehemu nyingine, utoro, nidhamu mbovu shuleni hupelekea mwanafunzi kufukuzwa shule, je kwa mfano wewe unafukuzwa shule utafanya kazi gani? mzee Mgaya aliuliza swali huku akikanyaga brake kupunguza mwendo akimwangalia Samson.
Samson hakuwa na jibu zaidi ya kutazama chini tu.
Najua huwezi kuwa na majibu, tena umepata bahati sana kusaidiwa na Mimi angekuwa mtu mwingine ameshashindwa zamani sana, mtu anamshindwa mwanaye wa kumzaa nini mtu baki kuwa makini mwanangu. alishauri Mzee Mgaya.
Aliingia kwenye highway na kuongeza speed akielekea kwa Tausi, ambako waliwakuta Tausi na dada yake aitwaye Latifa wamejaa tele, kabla ya kushuka Mzee Mgaya alimgeukia Samson Kisha akacheka kidogo.
Unamuona huyu mgeni nadhani uliwahi kumuona kule nyumbani, huyu anaitwa Latifa ni wanawake ambao ndoa zimewashinda na hawana cha kufanya mjini, mwisho wa siku kuja kuongeza bajeti kama hivi,hawana kazi mama yako mdogo Tausi naye biashara zimemshinda Kila jambo ukilianzisha yeye ni mtu wa kufeli tu. mwanangu hakuna mwanaume anayesifiwa kwa ushababi wa kupigana, au uzuri wake kwa Dunia ya Sasa hivi, watu wanataka sehemu yenye nuru, ulipo mzoga ndipo hukusanyika Tai, pesa kwanza. Kisha utapendwa na watu wote, Mimi na uzee huu Kuna sehemu nikipita siitwi Mzee, hata nikiwaelekeza kuwa Mimi ni sawa na baba zenu, wanabisha wakidai niliwahi kuzaa hivyo isiwe sababu. Zingatia masomo, zingatia future yako mengine yapo tu najua unalewaga sana ukiambiwa wewe handsome hayo Yana mwisho. aliongea Mzee Mgaya Kisha wakashuka.
Halafu Mzee Mgaya huwa sikuelewi kabisa , nimefungua geti umeingia ndani lakini takribani dakika tano hushuki huwa unamchora nani, na hii tabia unayo siku nyingi sana, huwa nakushangaa sana. alilaumu Tausi huku wakikumbatiana na mumewe na kuingia ndani.
Latifa au dada yake Tausi walibaki na Samson nje wakipiga stori huku yule Latifa akionesha ni mnyonge hata akicheka alikuwa akijilazimisha tu, Mzee Mgaya alitoka nje akiwa na begi fulani akaweka kwenye siti za nyuma ya gari Kisha akamgeukia latifa.
Shemeji usione kimya Mimi mumeo nimeongea naye na Kila kitu kitakaa sawa, alikuwa mgumu lakini kanielewa Mimi ni kama mzazi wake hivyo hakubisha ninachomwambia.kuna mambo ambayo yanaweza kupelekea kumpa talaka mke ,kama mtu kuzaa nje ya ndoa,fumanizi na mengine lakini kosa lako wewe dogo na ulishakiri Sasa sioni sababu ya yeye kutokukuelewa.
aliongea Mzee Mgaya huku Samson asijue kinachoongelewa
Sawa shemeji kwanza nashukuru kunipigania naamini muda wowote atakuja kunichukua. alijibu Latifa akionesha kafurahi na kuchangamka sana tofauti na mwanzo.
Mzee Mgaya na Samson walipanda gari na kuondoka huku Mzee Mgaya akimuaga mkewe Tausi kuwa anaingia mjini ila atarudi.
Wakiwa kwenye gari Samson aliuliza..
Baba kwani yule mamdogo Latifa ana matatizo gani?
Mmmmh mwanangu najua vitu vingine kukwambia nitakuwa kama nakutukana lakini haina jinsi lazima nikwambie kwani ni njia ya kujifunza kupitia kwa wengine pia,
Yule Latifa ana mumewe ambaye yupo nje ya mji huu japo si mbali kwani hata kazi anafanyia huku na anarudi nyumbani, inavyoonesha Hawa Wana asili ya kiburi sana kama ilivyo kwa mama yako mdogo Tausi, Sasa kwa Dini ya Hawa wenzetu, huwa ni rahisi mume kutoa talaka pale anapohisi anafanyiwa vitu ambavyo hawapaswi kufanyiana wenye ndoa, yapo mengi ambayo hayaelezeki.
Ila kwasasa nadhani mke wake kajifunza anahitaji kurudi kwa mumewe na na jamaa hataki lakini Mimi nimeshaongea naye kanielewa nadhani atakuja kumchukua siku ya jumatatu. alijibu Kwa kifupi mzee Mgaya huku akimshusha Samson na yeye kuendelea na mishe zake.
Samson aliingia ndani akakuta lunch ipo tayari akapiga , kisha akaanza uchokozi wake kwa aunt ambaye alikuwa akifumua nywele zake pale barazani.
Kwani Rahma yuko wapi, aliuliza Samson.
Amelala,
alijibu Kwa kifupi yule Aunt au Sarah kwa jina lingine.
Sawa ila Sarah wewe ni mwanamke unayevutia sana , juu ya kunionya nisikuite hivyo ila sina namna nyingine ya kufanya, tafadhali naomba kwa moyo wa kibinadamu na wenye huruma, unielewe juu ya maumivu nayopitia , ni siku nyingi zimepita tangu ufike umekuwa unaninyima raha huku nikijuta kufahamiana na wewe, ni Bora hata usingekuja kwani unazidi kuniongezea mateso tu moyoni mwangu. Na pia samahani sana kama nitakuwa nimekukwaza . najikuta sijiwezi kabisa kwako.aliweka kituo Sam.
(Sarah akacheka sana tu)
Kwanza huna haja ya kuniomba msamaha kwakuwa hujakosea kitu chochote, wewe kiufupi unanipenda sana si ndiyo. aliuliza Sarah.
Samson akatingisha kichwa kukubaliana huku akitabasamu kwa furaha mno.
Sawa, hata Mimi nakupenda sana,kwanza wewe ni mzuri na sura yako ya kike hiyo, hakika ni mzuri lakini pia nawezaje kuthibitisha kama unanipenda? , familia nzima nawapenda na ndiyo maana Niko hapa, lakini kubwa zaidi ni wewe kuwa hujiwezi kwangu yaani unanipenda kuliko wote kwenye hii familia hii Sasa unaonaje ukaandika kwenye karatasi kuthibitisha kama unanipenda, alishauri Sarah
Samson akakurupuka kuingia ndani kwake na kuleta kikaratasi chenye sentensi mbili huku maandishi yake yakisomeka vizuri sana, Kisha akamkabidhi Sarah.kisha wakakumbatiana, Samson asijue ule ni mtego
Nadhani dada mama Kulwa akirudi nitamweleza kuwa unanipenda sana. aliongea Sarah kisha akainuka na kwenda usawa wa jikoni kuangalia vitu vyake.
Sasa Aunt sikiliza unamwambiaje mama mambo yetu? Eeeh Mimi nimekwambia wewe tuongee wawili..
Samson aliingia jikoni akimfuata yule Sarah.
Sasa huku unafuata nini Samson {huku akionesha anacheka kwa dharau}unajua mtu akikupenda kupitiliza na hajiwezi anaweza kukusababishia kesi ya mauaji?
(murder case)unaweza kunywa sumu, kujinyonga na sababu zozote zitakazopelekea kuondoa uhai wake Sasa ni vyema familia ijue ili siku ukifa Mimi niwe mikono salama. Sarah alikuwa jeuri haswa.
Tafadhali kama hutaki kuwa na Mimi usimwambie mama wala yeyote mambo haya , yaani tuachane na hizi habari. aliongea Kwa uoga Sam.
Sawa kama hutaki nimwambie mama, utafanya kazi zangu nitakazokwambia, kwanza Yale maua kule nyuma si huwa unayamwagilia kwa kufunga mpira kwenye bomba, Sasa nataka usifunge mpira nataka uwe unachota na ndoo Kisha unamwagilia. aliongeza Sarah.
Sasa aunty mbali kote kule nitarudia mara ngapi unadhani hadi maua yalioane tafadhali usinifanyie hivyo bwana, alilalamika Samson.
Mimi sijui Tena ni Bora kazi uianze mapema maana wakikukuta unamwagilia kwa kutumia ndoo wakati mpira upo utawaeleza sababu ni nini?na Mimi sitaki ufunge mpira Kwa kufanya hivyo nakuja kumwambia mama Kulwa uliyoniambia, na kama unahidi utanikataa karatasi yako ninayo.
Sarah alipigilia msumari
Samson hakuwa na namna, kumwagilia maua jioni ile huwa ni kazi yake lakini huwa ni rahisi tofauti na njia ya siku hiyo, aliianza kazi huku akimwangalia Aunt Kwa huruma lakini hakukuwa na unafuu.
Itaendelea............