SEHEMU YA SABINI NA NNE
Siku ya jumatatu wakati Samson anarudi nyumbani alimkuta mama Kulwa akiwa na Cathy wanaongea huku Cathy akiwa anacheka kila muda Samson hakujua nini kinamchekesha yule dada, aliwasalimia Kisha akaketi huku akitoa barua fulani waliyopewa shuleni na kumpa mama Kulwa.
Jamani vipi tena barua, umeharibu nini wewe, na kama ni hivyo siendi kwa mambo ya kipuuzi Mimi, mmezoea mambo ya kijinga utamsubiri baba yako nakwambia.
alilaumu mama Kulwa akiwa hata hajafungua barua ajue ina nini ndani.
Aliisoma kwa muda Kisha akaiweka pembeni, kumbe ni habari za mwaliko Mimi nikajua tayari kayazua huko. alisema mama Kulwa huku akimwangalia Cathy wote wakacheka.
Basi mama yangu fanya kama nilivyokuelekeza, umelea watoto wako vizuri kwa ethics safi kwanini aje akutese mtoto wa mtu , afanyiwe abortion tu ili kuepuka matatizo yasiyo ya lazima, kwanza huyu atakuwa mzazi wa kwanza Kuna vitu chungu mzima vitajitokeza kama operation, pia mtu kuumwa muda mrefu, na pia unakuta labda mtoto aliyezaliwa naye ana matatizo, eeh mama lazima hili suala uliangalie kuanzia muda huu, litakuletea shida baadaye utashindwa kufanya kazi zako ukiuguza mgonjwa. alishauri Cathy ambaye ni mtu wa karibu mno na mama Kulwa, pia ni born town akiwa anajua vitu vingi hususan bidhaa mpya na matoleo ya nchi mbalimbali hivyo ni mtu ambaye huwa anasikilizwa sana.
Samson akiwa anakula alisikia Kila kilichoongelewa na wawili wale lakini pia alitamani kujua Rahma yuko wapi maana hakumuona.
Sasa shoga yangu kwanza nimekusikia, japo kwa suala la kutoa huo ujauzito sijakuafiki bado, mimi nashauri aitwe Tausi hata kama hawana udugu wowote lakini ni mtu anayemfahamu Rahma tangu akiwa mdogo, Mimi nataka atoke hapa kwangu tu basi, wewe mwenyewe unaona amekuwa mtu wa kulala tu hafanyi kazi sijui hiyo mimba ndiyo inatafuta pakukaa hata sijui.na ndiyo maana nimemtuma sokoni aende kwa miguu ili apate kujinyoosha.
aliweka kituo mama Kulwa.
*************************************
Jioni ile kulikuwa na watu wanne wote wanawake, akiwemo mama mwenye nyumba
Mama Kulwa,
Tausi, pamoja na dada yake,
Na Rahma ambaye ndiye main character kwenye kikao kile, huku Samson akifukuzwa asishiriki hivyo ikawa ngumu kujua Nini kimezungumziwa.
Akiwa karibu na getini mithili ya mlinzi akiwa anajisomea nyakati zile, alisikia sauti ya mama Kulwa ikimuita ikabidi akusanye vitu vyake vyote, akaingia ndani, sura alizokutana nazo hazikuwa na tabasamu siyo mama Kulwa wala Tausi wote walimtazama Samson kwa macho mabaya sana.
Nilikwambia Sam,
Njia ya muongo sikuzote ni fupi nilikuuliza ukakataa na kuapa viapo vyote lakini ukweli umejulikana Sasa nakuomba uchukue vifaa vyako vyote nakuomba tu kwa ustaarabu uondoke sikuhitaji. hakuonesha masihara mama Kulwa.
Dada ni kweli kabisa huyu mtoto ni mshenzi, tena ni hafai hata kuwa naye karibu nakuomba fanya chochote dada Yangu. Tausi aliongea kwa uchungu kuliko mtu yeyote huku Samson pekee akijua kwanini Tausi anaumia kuliko wote, pengine ni baada ya kuujua ukweli aliokuwa anauhisi siku nyingi ila akawa hajathibitisha.
Samson alichukua begi lake huku akiwa haamini anachokiona, licha ya kuganda ganda pale getini lakini hakuna aliyemuonea huruma, wote walikuwa wa moto sana kiasi cha Samson kukosa mtetezi.
Mama Kulwa alifungua geti kwa nguvu huku akimsukuma Samson kwa nguvu ili atoke nje huku akimrushia kiasi fulani cha pesa ikiwa ni nauli ya kurudi kwao mkoani.
Mpuuzi sana wewe nimekuvumilia mangapi, tumekusaidia mangapi, kwahiyo ukakosa adabu ndani mwangu Mimi na baba yako tu********,halafu na wewe ufanye hivyo hivyo mtoto mwenye laana wewe, nasema hapa kwangu hutokanyaga na mzee Mgaya hawezi kunifanya chochote kwakuwa hapa ni kwangu na kama atakurudisha nitahakikisha hapa kwangu hukanyagi mpuuzi sana wewe. aliongea mama Kulwa akiwa anarusha maneno huku Samson akiwa nje ya fence majirani kadhaa walianza kutoka kwani ilikuwa si kawaida kwa mtaa wao kusikia matusi kama sehemu zingine.
Samson alikaa chini Kisha akacheka, si kicheko cha furaha bali akiwa haamini yaliyotokea kwani kwa muda huo ilikuwa kama ndoto kwake.
Muda ule aliwaza wapi aende, ingekuwa Tausi hayupo pale angeenda kwake, lakini alishajua Tausi kachukia zaidi, aliwaza huku akiwa hajui afanyaje .
Baadaye wazo likamjia, aende kwa mjumbe wa mtaa wao, alipofika pale alijieleza na kusikilizwa vizuri sana tu lakini mjumbe alikataa kumpa hifadhi.
Mwanangu siwezi kukuhifadhi hapa, wakati kwenu ni hapo tu na Dunia imebadilika mno, hatujui una matatizo gani kiafya, ukitufia kwa mawazo je, unataka kutusababishia matatizo, wewe nenda mbembeleze mama yako muombe msamaha , atakuelewa tu. alishauri yule mjumbe.
Mume wangu acha kuzunguka sisi wenyewe tuna watoto wa kike hapa na milango si mizuri akiamka usiku kwenda kuwabaka watoto wetu! Mtu mwenyewe anakwambia kampa mimba mtu, Mimi simuhitaji.
aliongea mke wa mjumbe aliyeonekana ni mwenye mdomo sana.
Samson aliwaza kitambo kidogo akaona suluhisho ni kwenda kwa Cathy tu, kwanza yule bwana wake Cathy ameshaondoka zake ughaibuni, alijua wazi Cathy atampokea tu, akaanza kupiga hatua za haraka huyooo mpaka kwa Cathy.
Aligonga geti muda mrefu sana lakini halikufunguliwa, baadaye sana alitoka dada wa kazi huku akimlaumu Samson kwa usumbufu kwani watu walishapumzika,
Simama hapohapo ngoja nikamwite na jua huwa haruhusu kumfungulia mtu usiku, subiri aje akufungulie mwenyewe, aliongea yule mdada.
Eeenhee sema wewe nini usiku huu mbona unatutisha, Cathy aliuliza.
Samson ikabidi ajieleze yale yaliyompata masaa machache yaliyopita.
Kwahiyo nikusaidie nini, mshamba mkubwa wewe, wazazi wako ni masikini, Mzee Mgaya kajitolea kukusomesha, badala ya kusoma unaendekeza mambo ya kijinga , halafu kumbe wewe ni malaaaayaaaa eeeh unaonekana mpole kumbe ni mshenzi, Sasa nikwambie kitu kunilala Mimi isiwe sababu ya kunizoea na kuja hapa ni marufuku , Mimi siyo ndugu yako. aliongea Cathy kwa sauti ya chini ili housemaid wake asisikie lakini ilikuwa sauti yenye amri kuu. Akafunga geti.
Samson alipoteza tumaini kwani sehemu aliyoitegemea ndiyo hivyo tena huku akiwa hana mtu yeyote anayemjua , alianza kutembea akiwa hajui aelekee wapi na usiku ulianza kuthibitika zaidi baada ya kuwa watu aliokuwa anapishana nao wanapungua na hata magari yalianza kupungua barabarani, huku hali ya utulivu ukianza kushamiri , hakuwa na saa akashindwa kujua ni saa ngapi, ila aligundua ni usiku mnene.
Aliamua kwenda kwenye baa moja ambako alikuwa anasikia makelele kwa mbali Lakini napo aligundua watu wanapungua huku gari fulani ndogo ikiwa inapakia vyombo vya muziki kuashiria kulikuwa na tafrija fulani kwenye baa ile na Sasa imeisha, akiwa yupo yupo hana la kufanya alisikia sauti ya mtu anayemfahamu, ikabidi asogee pengine atapata msaada.
Ila huyu alichotufanyia siyo kabisa yaani ndugu zanguni, Sasa kwanini atulete baa , kakosa hata viukumbi vidogo akaona aje huku, na sisi wengine hatulewi mapombe kama wao haoni kuwa hajatutendea haki? japokuwa Leo nimeonja na hapa inanitesa kweli hiyo wine,
alikuwa ni Madam Silvia akiwa na wanawake watatu wakilaumu jambo ambalo Samson hakulijua.
Wote watatu walishtuka baada ya kuona Kuna mtu anawasogelea,
Wewe ni nani na unamtaka nani ,
aliuliza mwanamke aliyekuwa mbele zaidi kuliko wenzake.
Naitwa Samson Mgaya nimeisikia sauti ya mwalimu wangu nilikuwa naomba msaada,alijibu Samson.
Wewe mtoto usiku huu unafanya nini hapa na ni mwanafunzi, huoni hata aibu jamani hebu njoo kwenye mwanga, alijibu Madam huku wengine wakicheka na kusanifu.
Samson alijieleza sana huku akipindisha ukweli maana alijua kwa kusema wazi kosa lake hatopata msaada hivyo akaamua kutunga kosa lingine lenye unafuu.
Mmmmh watu wengine bwana Sasa unamtoa mtoto wa mtu kwao Kisha unakuja kumzurulisha usiku huu eti kakukosea Sasa si Bora umrudishe kwao Tena kwa kumpandisha kabisa kwenye gari, sasa hapa akivamiwa na vibaka . walilaumu wanawake wale wawili.
Mara gari fulani ndogo ilikuja ikiwa Ina kazi ya kuwabeba watu wale na kuwapeleka makwao.
Sasa ndugu zanguni kwakuwa huyu kijana namfahamu naondoka naye na kwangu siyo mbali nyie pandeni gari Mimi naondoka naye taratibu.
Baada ya muda fulani walifika huku wakipiga stori mbalimbali pale sebuleni na muda mwingi Madam alimtoa hofu Samson kuwa asijali atamsaidia tu.
Sasa mwenzangu sijui hata utalala wapi maana chumba hiki kimejaa vyombo tu, na kingine kipo na kina kitanda japo hakuna godoro, sijui ujikunje hapa hapa kwenye kiti masikini, ni saa Saba hii ujue ,
wewe tena usitafute usingizi, wewe jali umepata tu hifadhi unataka kuniambia usiku huu ungeenda wapi,
aliongea madam huku akionesha naye ana usingizi maana muda nao ulienda (kulikuchwa)
Samson hakujibu neno, akawa anamwangalia tu madam,
Yule Madam aliingia ndani akakaa zaidi ya dakika kumi asitoke hii ikampa hofu Samson kuwa kwahiyo nitalala kwa kuegama tu, baadaye alisikia sauti ya Madam yenye usingizi na uchovu ikimuita, akaingia ndani akakuta Madam kalala huku akiwa kajitupa huku akiwa na harufu ya pombe kwa mbali.
Wewe Samson Mimi Sina namna ya kukusaidia kwanza nimechoka, we kung'uta miguu panda kitandani ulale. aliongea Madam Silvia huku akionesha pombe aliyokunywa inamzingua sana.
Itaendelea......................