Jack Daniel
JF-Expert Member
- Sep 23, 2021
- 4,042
- 16,872
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA KUMI NA MBILI
Mzee Mgaya na kaka yake walikuwa kwa ndugu yao fulani, wakipanga taratibu za kwenda kuzuru/kutembelea makaburi ya wazazi wao huku kaka yake na mzee Mgaya akikusudia kufanya tambiko fulani ili kujiweka kwenye mazingira mazuri.
Akiamini waliolala pale yaani wazazi wake wanaweza kumsikiliza na yeye akanyoosha mambo fulani, ila wazo lile lilikuja kukosa nguvu baada ya kila mmoja kumkumbuka mganga ambaye alitaka kuwatapeli kuhusu tukio la kupotea kwa Samson.
Unajua ndugu yangu Mimi moja kwa moja kutokana na migongano kazini kwangu huko mjini, dhumumi langu kubwa lilikuwa ni kuja kufanya shughuli ya kutambika ili kunyoosha mambo fulani, lakini Kila nikiangalia na kukumbuka tukio lenu naona kama mambo haya tuyaache yapitwe na wakati tu. alishauri yule mgeni kaka wa mzee Mgaya.
Baada ya kushauriana kuwa waachane na yale mambo lakini walishika njia ya kurudi nyumbani huku wakiongea masuala mbalimbali.
Hivi ndugu yangu unajua wewe katika watoto wako wote hawajasoma na hawana elimu, na inabidi utambue kuwa Dunia ya Sasa tunakoelekea inawahitaji wasomi zaidi. ili kurahisisha maisha , je una mpango gani kuhusu kijana wako Samson maana wale dada zake hakuna namna tena Kwa umri wao hawawezi kuendelea na Elimu yeyote. alihoji yule mgeni.
Unachoongea ndugu yangu ni kweli hata Mimi natamani sana hasa huyu mwanangu Samson asome, lakini uwezo kaka. alijitetea mzee Mgaya.
Uwezo upi kwamba huwezi kumsomesha mwanao au yeye hana uwezo wa kuafford masomo, maana kama ni ada Mimi sidhani kama kweli wewe ndugu yangu unakosa ada ya kulipia kweli kwenye shule hizi za kawaida, si ipo ile shule yenu mpya kule wilayani Wala Haina hata gharama na ni ya kutwa, inakushindaje? aliuliza kaka yake na mzee Mgaya huku akikazia sana lile suala.
Unajua wewe kaka unaongea tu, wewe mwenzangu una kipato kikubwa watoto wako wakubwa karibu wote umewasomesha, jaribu kulinganisha hali yangu na yako Mimi nadhani hakuna anayependa watoto wake wasisome ila tatizo ni umasikini uliopindukia.alikaza mzee Mgaya huku akiwa hapendi kejeli za kaja yake kumlazimisha vitu ambavyo yeye hana uwezo navyo.
Waliendelea kuzunguka, wakakikuta kilabu fulani Cha pombe za kienyeji wakaingia huku wengi wao wakimshangaa yule mgeni, waliomkumbuka walisalimiana kwa heshima huku wakifurahia kumuona yule mgeni, basi alichofanya yule mgeni alimuita mama muuza pombe akamwambia awape pombe watu wote waliokuwa mle ndani.
Watu wote walifurahia sana wakaanza kubwia zile pombe kwa fujo huku wakimshukuru sana yule mgeni, hata yeye alizikumbuka sana pombe za asili ya kwao hivyo akazipiga kisawa sawa , huku wote wawili wakishika njia ya nyumbani kwa mzee Mgaya wakirudi wakiwa wamelewa kiasi.
Muda wa saa mbili za usiku walifika nyumbani huku Kila mmoja akiwa Hana hamu ya kula yaani ile pombe ni kama huwa inashibisha, hivyo Kila mtu akaamua kulala tu.
Kitendo cha wao kurudi usiku kilimuhuzunisha Samson ambaye alibandika matokeo yake ya mitihani
lengo baba yake mkubwa ayaone lakini wakawa wamerudi wamelewa halafu ni usiku akanyongea sana Samson.
Mama Mgaya alitambua ile hali ya mwanaye akamfuata akampoza poza tu huku akimpa moyo kuwa atamwambia shemeji yake hitaji la mwanae, basi siku hiyo ikaisha
Kutokana na pombe nyingi za kienyeji zilimchukua kaka yake na mzee Mgaya, akajikuta anachelewa kuamka, wakati huo wenyeji walishaamka kitambo wakiwa wanalimalima nje ya nyumba yao kama ilivyo kawaida ya watu wa kijijini Mashamba kuwa karibu tu na nyumba.
Mgeni aliamka mida ya saa mbili na nusu huku akitoka nje na kuangaza macho na kuwasalimia wenyeji wake kwa kupunga mikono
Alishangazwa na makaratasi mengi yaliyobandikwa kuzungushwa kwenye ukuta wa nyumba ikabidi ayasogelee na kuanza kusoma karatasi moja moja.
Wakati akiendelea kufuatilia Yale makaratasi familia nzima ilikuwa inamuangalia huku Samson akiwa ana furaha zaidi maana lengo lake lilitimia kwa kiasi kikubwa akawa ana furaha sana.
Wakati huo Mzee Mgaya na mkewe waliacha shughuli zao huku wakirudi ndani ili kumuandalia mgeni maji ya kuoga lakini na chai pia
Yule mgeni aliganda sana pale, akiwa anaangalia hatua moja ya karatasi baada ya jingine.
***************************
Kwa majina kamili anaitwa James Mgaya ni kaka wa kwanza kwenye familia ya marehemu Victory Mgaya ambaye alikuwa Jumbe, yaani kiongozi fulani wa eneo kutokana na muundo wa serikali ya kikoloni.
Hivyo wakati huo waingereza wakiendesha shule fulani za misheni walikuwa wanachukua kijana mmoja mmoja kwenye Kila familia, kutokana na wadhifa wa uongozi wa mzee Mgaya marehemu ikabidi achukuliwe kijana wake anayeitwa James akawa anasomeshwa kwa msaada wa wamisionari, alisoma hadi darasa la nne akafanya mtihani akafaulu akaendelea na masomo ya middle school mpaka darasa la nane.
akiwa na elimu kubwa tu kwa kipindi hicho.
Akarudi kijijini kwake akabahatika kuwa ni mmoja wa walimu wa shule ya kijijini kwao kutokana na uhaba wa walimu kwa kipindi hicho , wakiwa wanajulikana kama walimu wa UPE
(Universal Primary Education)
alifundisha kwa takribani miaka mitano akijulikana kwa jina la mwl James Mgaya huku wanakijiji wakifurahi kumpata mwalimu ambaye ni mzaliwa wa hapo.
Baadaye akafuatwa na shirika fulani la kidini likimtaka afanye kazi kwenye shirika lao rasmi , hivyo wakahamia Dar es salaam, lakini baada ya kufika mjini mambo yalibadilika lile shirika likapoteza dira huku yeye akiwa tayari ana wenyeji na connection kibao hivyo akajiunga kwenye moja ya shirika la reli hapa mjini.
Kwenye shirika la railway hakukaa sana baada ya kutokea kwa vita vya Uganda na Tanzania, akachaguliwa kuwa mmoja wa jeshi la akiba kwa kipindi hicho (alikuwa na sifa au la haikujulikana mapema)
Basi baada ya vita vile kumalizika James alikuwa kwenye wakati mzuri na mnufaika mzuri sana hivyo mambo yakaanza kumnyookea, huku akioa na kuanzisha familia rasmi.
Basi tangu hapo akawa ni mtu muhimu kwenye ukoo na familia nzima kiujumla.
*****************************
Kaka yake na mzee Mgaya aliangalia yale maendeleo ya Samson akagundua kuwa mtoto ana kitu kichwani ila huenda hana sapoti akamuita Samson pamoja na wazazi wake akiwalaumu kwanini kijana anaonesha alikuwa na maendeleo mazuri Sasa kwanini hawaoneshi mpango wa kumpeleka Sekondari.
Wazazi wa Samson walijitetea kuhusu kipato huku wakimuomba kama ana uwezo basi amsaidie.
Yule mgeni aliwaza kitambo kidogo Kisha akawaambia kuwa inabidi aende wilayani akaangalie matokeo yake ili mipango ya kumuhamisha shule iendelee. Ilikuwa taarifa nzuri sana kwa mzee Mgaya na familia yake huku wakimuomba MUNGU afanikishe mpango wao.
Je, atafanikiwa, tukutane sehemu ijayo.
Mzee Mgaya na kaka yake walikuwa kwa ndugu yao fulani, wakipanga taratibu za kwenda kuzuru/kutembelea makaburi ya wazazi wao huku kaka yake na mzee Mgaya akikusudia kufanya tambiko fulani ili kujiweka kwenye mazingira mazuri.
Akiamini waliolala pale yaani wazazi wake wanaweza kumsikiliza na yeye akanyoosha mambo fulani, ila wazo lile lilikuja kukosa nguvu baada ya kila mmoja kumkumbuka mganga ambaye alitaka kuwatapeli kuhusu tukio la kupotea kwa Samson.
Unajua ndugu yangu Mimi moja kwa moja kutokana na migongano kazini kwangu huko mjini, dhumumi langu kubwa lilikuwa ni kuja kufanya shughuli ya kutambika ili kunyoosha mambo fulani, lakini Kila nikiangalia na kukumbuka tukio lenu naona kama mambo haya tuyaache yapitwe na wakati tu. alishauri yule mgeni kaka wa mzee Mgaya.
Baada ya kushauriana kuwa waachane na yale mambo lakini walishika njia ya kurudi nyumbani huku wakiongea masuala mbalimbali.
Hivi ndugu yangu unajua wewe katika watoto wako wote hawajasoma na hawana elimu, na inabidi utambue kuwa Dunia ya Sasa tunakoelekea inawahitaji wasomi zaidi. ili kurahisisha maisha , je una mpango gani kuhusu kijana wako Samson maana wale dada zake hakuna namna tena Kwa umri wao hawawezi kuendelea na Elimu yeyote. alihoji yule mgeni.
Unachoongea ndugu yangu ni kweli hata Mimi natamani sana hasa huyu mwanangu Samson asome, lakini uwezo kaka. alijitetea mzee Mgaya.
Uwezo upi kwamba huwezi kumsomesha mwanao au yeye hana uwezo wa kuafford masomo, maana kama ni ada Mimi sidhani kama kweli wewe ndugu yangu unakosa ada ya kulipia kweli kwenye shule hizi za kawaida, si ipo ile shule yenu mpya kule wilayani Wala Haina hata gharama na ni ya kutwa, inakushindaje? aliuliza kaka yake na mzee Mgaya huku akikazia sana lile suala.
Unajua wewe kaka unaongea tu, wewe mwenzangu una kipato kikubwa watoto wako wakubwa karibu wote umewasomesha, jaribu kulinganisha hali yangu na yako Mimi nadhani hakuna anayependa watoto wake wasisome ila tatizo ni umasikini uliopindukia.alikaza mzee Mgaya huku akiwa hapendi kejeli za kaja yake kumlazimisha vitu ambavyo yeye hana uwezo navyo.
Waliendelea kuzunguka, wakakikuta kilabu fulani Cha pombe za kienyeji wakaingia huku wengi wao wakimshangaa yule mgeni, waliomkumbuka walisalimiana kwa heshima huku wakifurahia kumuona yule mgeni, basi alichofanya yule mgeni alimuita mama muuza pombe akamwambia awape pombe watu wote waliokuwa mle ndani.
Watu wote walifurahia sana wakaanza kubwia zile pombe kwa fujo huku wakimshukuru sana yule mgeni, hata yeye alizikumbuka sana pombe za asili ya kwao hivyo akazipiga kisawa sawa , huku wote wawili wakishika njia ya nyumbani kwa mzee Mgaya wakirudi wakiwa wamelewa kiasi.
Muda wa saa mbili za usiku walifika nyumbani huku Kila mmoja akiwa Hana hamu ya kula yaani ile pombe ni kama huwa inashibisha, hivyo Kila mtu akaamua kulala tu.
Kitendo cha wao kurudi usiku kilimuhuzunisha Samson ambaye alibandika matokeo yake ya mitihani
lengo baba yake mkubwa ayaone lakini wakawa wamerudi wamelewa halafu ni usiku akanyongea sana Samson.
Mama Mgaya alitambua ile hali ya mwanaye akamfuata akampoza poza tu huku akimpa moyo kuwa atamwambia shemeji yake hitaji la mwanae, basi siku hiyo ikaisha
Kutokana na pombe nyingi za kienyeji zilimchukua kaka yake na mzee Mgaya, akajikuta anachelewa kuamka, wakati huo wenyeji walishaamka kitambo wakiwa wanalimalima nje ya nyumba yao kama ilivyo kawaida ya watu wa kijijini Mashamba kuwa karibu tu na nyumba.
Mgeni aliamka mida ya saa mbili na nusu huku akitoka nje na kuangaza macho na kuwasalimia wenyeji wake kwa kupunga mikono
Alishangazwa na makaratasi mengi yaliyobandikwa kuzungushwa kwenye ukuta wa nyumba ikabidi ayasogelee na kuanza kusoma karatasi moja moja.
Wakati akiendelea kufuatilia Yale makaratasi familia nzima ilikuwa inamuangalia huku Samson akiwa ana furaha zaidi maana lengo lake lilitimia kwa kiasi kikubwa akawa ana furaha sana.
Wakati huo Mzee Mgaya na mkewe waliacha shughuli zao huku wakirudi ndani ili kumuandalia mgeni maji ya kuoga lakini na chai pia
Yule mgeni aliganda sana pale, akiwa anaangalia hatua moja ya karatasi baada ya jingine.
***************************
Kwa majina kamili anaitwa James Mgaya ni kaka wa kwanza kwenye familia ya marehemu Victory Mgaya ambaye alikuwa Jumbe, yaani kiongozi fulani wa eneo kutokana na muundo wa serikali ya kikoloni.
Hivyo wakati huo waingereza wakiendesha shule fulani za misheni walikuwa wanachukua kijana mmoja mmoja kwenye Kila familia, kutokana na wadhifa wa uongozi wa mzee Mgaya marehemu ikabidi achukuliwe kijana wake anayeitwa James akawa anasomeshwa kwa msaada wa wamisionari, alisoma hadi darasa la nne akafanya mtihani akafaulu akaendelea na masomo ya middle school mpaka darasa la nane.
akiwa na elimu kubwa tu kwa kipindi hicho.
Akarudi kijijini kwake akabahatika kuwa ni mmoja wa walimu wa shule ya kijijini kwao kutokana na uhaba wa walimu kwa kipindi hicho , wakiwa wanajulikana kama walimu wa UPE
(Universal Primary Education)
alifundisha kwa takribani miaka mitano akijulikana kwa jina la mwl James Mgaya huku wanakijiji wakifurahi kumpata mwalimu ambaye ni mzaliwa wa hapo.
Baadaye akafuatwa na shirika fulani la kidini likimtaka afanye kazi kwenye shirika lao rasmi , hivyo wakahamia Dar es salaam, lakini baada ya kufika mjini mambo yalibadilika lile shirika likapoteza dira huku yeye akiwa tayari ana wenyeji na connection kibao hivyo akajiunga kwenye moja ya shirika la reli hapa mjini.
Kwenye shirika la railway hakukaa sana baada ya kutokea kwa vita vya Uganda na Tanzania, akachaguliwa kuwa mmoja wa jeshi la akiba kwa kipindi hicho (alikuwa na sifa au la haikujulikana mapema)
Basi baada ya vita vile kumalizika James alikuwa kwenye wakati mzuri na mnufaika mzuri sana hivyo mambo yakaanza kumnyookea, huku akioa na kuanzisha familia rasmi.
Basi tangu hapo akawa ni mtu muhimu kwenye ukoo na familia nzima kiujumla.
*****************************
Kaka yake na mzee Mgaya aliangalia yale maendeleo ya Samson akagundua kuwa mtoto ana kitu kichwani ila huenda hana sapoti akamuita Samson pamoja na wazazi wake akiwalaumu kwanini kijana anaonesha alikuwa na maendeleo mazuri Sasa kwanini hawaoneshi mpango wa kumpeleka Sekondari.
Wazazi wa Samson walijitetea kuhusu kipato huku wakimuomba kama ana uwezo basi amsaidie.
Yule mgeni aliwaza kitambo kidogo Kisha akawaambia kuwa inabidi aende wilayani akaangalie matokeo yake ili mipango ya kumuhamisha shule iendelee. Ilikuwa taarifa nzuri sana kwa mzee Mgaya na familia yake huku wakimuomba MUNGU afanikishe mpango wao.
Je, atafanikiwa, tukutane sehemu ijayo.

