Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 55
Wakati najiandaa kutoka baada ya kumuachia maagizo msichana wangu, moyo ulishtuka kumuona shoga yangu ambaye mara nyingi huja na habari za kushtusha.
Pamoja na kuwa tayari nimeachana na mume wangu kidunia japokuwa kwa Mungu ndoa yetu bado ilikuwa ikitambulika. Lakini sikupenda kusikia habari mbaya za mzazi mwenzangu.
Nilipomuona nilimkaribisha.
“Karibu shoga.”
“Asante.”
“Za siku? Umepotea!”
“Mambo mengi, nilikuwa nalima kijijini, si unajua maisha ya mjini bila mihangaiko unaweza kuwa malaya bure.”
“Lakini kijijini kumekupendeza, umekuja lini?”
“Wiki sasa.”
“Mmhu, una jipya gani? Maana kila nikikuona moyo unapaa.”
“Ni kweli, kuna vitu unaweza kuvikalia kimya lakini vingine huwezi, wacha niitwe mbeya lakini ukweli utabaki palepale.”
Mmh! Kauli ile ilinitisha na kujiuliza kuna kitu gani tena ambacho kimemfanya afunge safari kuja kwangu.
“Kuna nini tena shoga yangu?” moyo uliingia woga.
“Shoga inasikitisha na kuuma, sijui ni laana yako na wanao au ya baba yake?”
“Kwa nini unasema hivyo kwani kuna kitu gani tena kimemtokea mume wangu?”
“Yote iliyopita ilikuwa trela sasa ndiyo picha kamili.”
“He! Nini tena?” nilijikuta nikishtuka na mapigo ya moyo kunienda mbio na kujikuta nimeshindwa kusimama na kukaa kwenye kiti kirefu.
“Una muda gani hujaonana na mzazi mwenzio?”
“Kitambo kidogo!”
“Kama nilivyo kueleza nilikuwa sipo, nimerudi wiki jana, siku ya pili toka nirudi nilimuona mzazi mwenzio baba Jacky, kama una moyo mdogo lazima ulie.”
“Mungu wangu kafanya nini tena?”
“Inasemekana mumeo kaukwaa.”
“Mungu wangu nisaidie mja wako! Una maanisha nini?” nilishika kifua kwa hofu.
“Inasemeka yule mwanamke aliyekutoa ndani alikuwa mwingi wa habari.
Baada ya kuachana na mzazi mwenzio zilipatikana taarifa kuwa ni muathirika, taarifa zile ziliifikia familia ya mumeo.
“Walimweleza kaka yao ambaye wakati huo alikuwa amechanganyikiwa baada ya wewe kumtolea nje.
Alikuwa hajijali alivaa nguo bila kufua wala kuoga, “Mama na wifi zako aliwaona maadui wakubwa walioharibu nyumba yake na maisha yake. Hakutaka kuwaona wala kuzungumza nao kabisa hata kwenye mazishi yake aliwapiga marufuku wasifike.”
Wakati najiandaa kutoka baada ya kumuachia maagizo msichana wangu, moyo ulishtuka kumuona shoga yangu ambaye mara nyingi huja na habari za kushtusha.
Pamoja na kuwa tayari nimeachana na mume wangu kidunia japokuwa kwa Mungu ndoa yetu bado ilikuwa ikitambulika. Lakini sikupenda kusikia habari mbaya za mzazi mwenzangu.
Nilipomuona nilimkaribisha.
“Karibu shoga.”
“Asante.”
“Za siku? Umepotea!”
“Mambo mengi, nilikuwa nalima kijijini, si unajua maisha ya mjini bila mihangaiko unaweza kuwa malaya bure.”
“Lakini kijijini kumekupendeza, umekuja lini?”
“Wiki sasa.”
“Mmhu, una jipya gani? Maana kila nikikuona moyo unapaa.”
“Ni kweli, kuna vitu unaweza kuvikalia kimya lakini vingine huwezi, wacha niitwe mbeya lakini ukweli utabaki palepale.”
Mmh! Kauli ile ilinitisha na kujiuliza kuna kitu gani tena ambacho kimemfanya afunge safari kuja kwangu.
“Kuna nini tena shoga yangu?” moyo uliingia woga.
“Shoga inasikitisha na kuuma, sijui ni laana yako na wanao au ya baba yake?”
“Kwa nini unasema hivyo kwani kuna kitu gani tena kimemtokea mume wangu?”
“Yote iliyopita ilikuwa trela sasa ndiyo picha kamili.”
“He! Nini tena?” nilijikuta nikishtuka na mapigo ya moyo kunienda mbio na kujikuta nimeshindwa kusimama na kukaa kwenye kiti kirefu.
“Una muda gani hujaonana na mzazi mwenzio?”
“Kitambo kidogo!”
“Kama nilivyo kueleza nilikuwa sipo, nimerudi wiki jana, siku ya pili toka nirudi nilimuona mzazi mwenzio baba Jacky, kama una moyo mdogo lazima ulie.”
“Mungu wangu kafanya nini tena?”
“Inasemekana mumeo kaukwaa.”
“Mungu wangu nisaidie mja wako! Una maanisha nini?” nilishika kifua kwa hofu.
“Inasemeka yule mwanamke aliyekutoa ndani alikuwa mwingi wa habari.
Baada ya kuachana na mzazi mwenzio zilipatikana taarifa kuwa ni muathirika, taarifa zile ziliifikia familia ya mumeo.
“Walimweleza kaka yao ambaye wakati huo alikuwa amechanganyikiwa baada ya wewe kumtolea nje.
Alikuwa hajijali alivaa nguo bila kufua wala kuoga, “Mama na wifi zako aliwaona maadui wakubwa walioharibu nyumba yake na maisha yake. Hakutaka kuwaona wala kuzungumza nao kabisa hata kwenye mazishi yake aliwapiga marufuku wasifike.”