Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,165
Sehemu ya 01
Mtunzi: Ally Katalambula
Ndoa ni kama jumba au ngome yenye siri kubwa, waliopo ndani wanataka kutoka nje na walioko nje wanatamani kuingia ndani. Waliotoka kwa makosa ya kujitakia wanatamani kurudi tena ndani na waliopo nje waliokutana na dhahama hawataki tena kuingia ndani. Mimi ni mmoja wa watu waliokutana na dhahama ambayo ilinifanya niichukie na kutoitamani tena.
Kwanza kabisa kabla ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa pumzi na akili timamu za kuweza kuyatoa yaliyonisibu na kuamini nyoka mwenye sumu kali ana afadhali kuliko mwanadamu unayecheka naye mchana lakini usiku anakugeuka. Kupitia mlolongo wangu wa maisha naamini Mungu ni muweza wa yote na malipo ya kila kitu yapo hapahapa duniani, ahera huwa ni hesabu.
Mwanadamu anaweza kukufanya ukaichukia dunia wakati bado unaipenda, lakini nashukuru moyo wa kutokata tamaa na subira ndivyo vilivyonifikisha hapa na kupata ujasiri wa kuutoa ushuhuda huu mbele yenu.
Nina imani mlio ndani ya ndoa mtakubaliana nami haya nitakayoyaeleza inawezekana si yote yakafanana lakini kwa asilimia kubwa yamekukuta. Ndoa nyingi zimevunjika kutokana na kero za wakwe na mawifi. Cha kushangaza kabla hujaolewa unakuwa wa kwanza kuichokonoa ndoa ya kaka yako lakini ukiolewa na wewe yanakukuta na unaishia kulalamika na kusahau kwamba muosha huoshwa.
Najua umebaki na maswali juu ya kauli yangu, kwa nini siitaki tena ndoa na kwa nini siwezi kuwasamehe wala kuwasahau wabaya wangu japo tumefundishwa kuwasamehe watu saba mara sabini! Pia tumeelezwa tusamehe kwanza ndipo tusamehewe lakini kwa hili Mungu atanisamehe.
Naitwa Eliza Elias, umri wangu ni miaka 40 kwa sasa, elimu yangu kidato cha nne, nilikatisha masomo kwa ajili ya ndoa si kwa kulazimishwa bali kwa hiyari yangu mwenyewe. Nilibahatika kuolewa na mwanaume ambaye niliamini ndiye wa maisha yangu.
Alinipenda nami nilimpenda sana tena sana, mpaka tunakubaliana kuwa mke na mume kuna vitu vilinishawishi kuanzia yeye mwenyewe, familia yake akiwemo baba ambaye muda huu ni marehemu na mama pamoja na mawifi.
Mtunzi: Ally Katalambula
Ndoa ni kama jumba au ngome yenye siri kubwa, waliopo ndani wanataka kutoka nje na walioko nje wanatamani kuingia ndani. Waliotoka kwa makosa ya kujitakia wanatamani kurudi tena ndani na waliopo nje waliokutana na dhahama hawataki tena kuingia ndani. Mimi ni mmoja wa watu waliokutana na dhahama ambayo ilinifanya niichukie na kutoitamani tena.
Kwanza kabisa kabla ya yote napenda kumshukuru Mungu kwa kunipa pumzi na akili timamu za kuweza kuyatoa yaliyonisibu na kuamini nyoka mwenye sumu kali ana afadhali kuliko mwanadamu unayecheka naye mchana lakini usiku anakugeuka. Kupitia mlolongo wangu wa maisha naamini Mungu ni muweza wa yote na malipo ya kila kitu yapo hapahapa duniani, ahera huwa ni hesabu.
Mwanadamu anaweza kukufanya ukaichukia dunia wakati bado unaipenda, lakini nashukuru moyo wa kutokata tamaa na subira ndivyo vilivyonifikisha hapa na kupata ujasiri wa kuutoa ushuhuda huu mbele yenu.
Nina imani mlio ndani ya ndoa mtakubaliana nami haya nitakayoyaeleza inawezekana si yote yakafanana lakini kwa asilimia kubwa yamekukuta. Ndoa nyingi zimevunjika kutokana na kero za wakwe na mawifi. Cha kushangaza kabla hujaolewa unakuwa wa kwanza kuichokonoa ndoa ya kaka yako lakini ukiolewa na wewe yanakukuta na unaishia kulalamika na kusahau kwamba muosha huoshwa.
Najua umebaki na maswali juu ya kauli yangu, kwa nini siitaki tena ndoa na kwa nini siwezi kuwasamehe wala kuwasahau wabaya wangu japo tumefundishwa kuwasamehe watu saba mara sabini! Pia tumeelezwa tusamehe kwanza ndipo tusamehewe lakini kwa hili Mungu atanisamehe.
Naitwa Eliza Elias, umri wangu ni miaka 40 kwa sasa, elimu yangu kidato cha nne, nilikatisha masomo kwa ajili ya ndoa si kwa kulazimishwa bali kwa hiyari yangu mwenyewe. Nilibahatika kuolewa na mwanaume ambaye niliamini ndiye wa maisha yangu.
Alinipenda nami nilimpenda sana tena sana, mpaka tunakubaliana kuwa mke na mume kuna vitu vilinishawishi kuanzia yeye mwenyewe, familia yake akiwemo baba ambaye muda huu ni marehemu na mama pamoja na mawifi.